Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha
Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..
Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.
MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.
TUPO PAMOJA DAIMA
Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;
https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:
https://www.facebook.com/diaryyangu/
`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;
Friday, August 28, 2009
MFADHAIKO
Thursday, August 27, 2009
SHIDA YA USAFIRI NA FOLENI DAR
Maoni yangu ni kuwa kuna haja ya wahusika wa usafiri kuruhusu magari ya kutoka maeneo
Ahsanteni na poleni
From miram3.com
Wednesday, August 26, 2009
MAWAZO YANGU
Monday, August 24, 2009
MGENI WETU MTUKUFU
Friday, August 21, 2009
VITENDO NI BORA KULIKO MANENO
Mimi sio mwanasiasa,ila ninaikumbuka hadithi ya babu yangu kuhusu milki moja ya majigambo. Mkuu wa nchi ile alikuwa na washauri wake wawili, hawa walikuwa wakipewa kazi mara kwa mara za kufuatilia mambo ya utendaji na mwisho wa siku huleta taarifa.
Watendaji wake wawili hawa walikuwa wajuzi kila mmoja kwa nafasi yake. Mpole alikuwa akifuatilia na kufanya kazi yake kimya kimya, na mwisho wa siku hupeleka taarifa na kumkabidhi bosi wake,ama kwa kupitia katibu muhtasi wa bosi au wakati mwingine kupitia kwa mwenzake ambaye alikuwa Chakaram kwani Chakaramu anajua kuielezea kazi kama alikuwepo.
Chakaramu alikuwa mjanja, yeye huitumia nafasi ya wengine kufanya kazi yake na kwa uchakaramu wake aliweza kupeleka taarifa nyingi kwa bosi wake kuliko Mpole,kwahiyo bosi wake alikuwa akimtumia sana katika kupata taarifa. Watu kama hawa ndio wamejaa maofisni kibao, maneno mengi, lugha utafikiri kazaliwa huko,lakini…ok ngoja tuendelee.
Likatokea lakutokea,kuna mtu kauliwa, na taarifa zikafika kwa bosi, Chakaram na Mpole wakambiwa wafuatilie, Mpole kama kawaida yake akaifanya ile kazi kwa umakini zaidi akijua ule ni uhai wa mtu na kugundua ukweli,na ukweli huo ulimuumiza sana na akaona ni heri aufiche kwanza ili kwanza awe na uhakika nao. Kwa minajili hiyo akajenga hoja ya kuwa huenda aliyekufa alijiua mwenyewe. Na hii akainasa Chakaramu, akaitenhenezea hoja yenye ushahidi kabambe mwisho wa siku akaipeleka kwa bosi wake.
Bosi wake akaisikiliza,na ushahidi alioletewa, kiasi kwamba aliridhika, na kumsifia sana jamaa, kimoyoni akasema duu jamaa huyu ni mkali, huyu ndiye ananifaauyu ninayemuamini kaniletea ushahidi huu basi sina wasiwasi,jamaa atakuwa kajiua.
Bosi akataka kujua kutoka kwa mshauri wake Mpole. Mople alipofika,kama kawaida yake,akafika kwa katibu muhutasi na kumwambia kuwakesi hiyo ina utata, na anahitaji muda wa kuifanyia kazi. Kitendo hiki kilimuudhi bosi,kwasababu muda ulishatolewa na kwanini mwenzake aweze kuleta matokea yeye ashindwe. Jamaa akafukuzwa kazi.
Licha ya kufukuzwa kazi alifilisiwa na akawa katika maisha magumu. Hatimaye siku ya mwisho aliyoomba apewe kutoa taarifa yake ilifika. Aliomba siku hiyo wawepo wazee wa baraza, na hakimu wa-nchi.
`Ndugu Mheshimiwa, nilisita sana kutoa taarifa yangu kwasababu mdomo kutamka ni rahisi,lakini kile unachokitamka sio rahisi kujielezea,lakini kama utaacha kile ulichokitamka kijielezee ni bora zaidi, hakuna haja hata ya kuinua mdomo. Bosi najua unajua muuaji ni nani, labda tumiite shahidi yangu wa kwanza ambaye ni Mheshimiwa mkeo. …’’ Watu pale wakashangaa,iweje. Na mke wa raisi inasadikiwa kapotea kimijiuza.
Ni kesi ndefu kidogo, nitaielezea kwa undani baadaye. Lakini alichotaka kunieleza babu yangu ni kuwa wakati wote, hakikisha kazi na majukumu yako uliyopewa unayatenda kwa vitendo na ukiyatenda ipasavyo yatajieleza yenyewe, usipende mara kwa mara kutumia mdomo kuielezea kazi yako,iache kazi ijielezee yenyewe, akiwa na maana kuwa vitendo huwakilisha ukweli kuliko maneno. Huu ni ujumbe wangu wa leo tarehe 21-08-2009 Je w ewe mwenzangu wasemaje?
From miram3.com
Thursday, August 20, 2009
MUJIBU WA SHERIA
From miram3.com
Wednesday, August 19, 2009
Dunia ni duara
Leo tarehe 19-08-2009, nilikumbuka tukio moja lilitokea tarehe 25-3-2008, tukio lenyewe lilikuwa hivi:
Dunia hii ni duara, na watu kama tulivyo, kukutana ni wajibu, tofauti na milima. Katika kukutana ndipo tunapojenga urafiki, udugu na hata uchumba, ndio ni kweli hata uadui pia. Lakini tusisahau kuwa kama binadamu tulivyo, kukoseana na hata kujengeana uadui kupo, lakini hili ni nadra, na linapotokea huwa lina sababu, kwani ibilisi huja na visa vyake ili viwe fundisho kwetu.
Diana baada ya kukaa kwenye kampuni moja kwa muda mrefu, alipata bahati ya kuomba sehemu nyingine. Alifanya hivi ili kupata sehemu itakayokidhi mahitaji yake, lakini pia alishachoka kufanya kazi na meneja wake ambaye kila siku waliishia kugombana. Siku alipopewa barua ya ajira sehemu nyingine, ambayo ilimuahidi kipato kikubwa, alitamani dunia yote ijue kuwa yeye sasa hivi, sio yule Diana waliyemjua ni Diana mwingine. Kwa raha aliyokuwa nayo, aliingia ofisisni kwa taksi, na akiwa amechelewa.
Alipofika asubuhi ofisini, aliwasabahi wale waliokuwa karibu naye huku akiwapa mkono wa kwaheri. Alimwendea bosi wake ambaye walikuwa hawaivani, na alipoulizwa kwanini kachelewa alijibu kwa dharau, `tatizo la usafiri,’ Bosi alipotaka kuja juu akaona huo ndio muda muafaka wa kumpa bosi vipande vyake, na kweli alimpa bosi vipande vyake, na kumwambia sasa hivi yeye na kampuni yake basi.Bosi wake Mr. JeuriMbaya ambaye licha ya ukali wake katika kazi, kitu ambacho wengi walimuona ana roho mbaya, alikuwa muungwana pale panapohitajika, alichofanya ni kumtakia kila-laheri, na kumwambia kama katika utendaji wake wakazi walikwazana, basi anaomba msamaha, kwani yeye alikuwa akitimiza wajibu wake tu. Diana alimwangalia kwa jicho la dharau, akageuka na kuelekea kwenye meza yake, huku moyoni akisema, bosi wa namna yako hastahili kufanya kazi na mimi.
Hapo mezani alitumia muda mwingi kuwajulisha marafiki zake kuwa yeye sasa atakuwa katika ofisi za Kampuni kubwa ya Kimarekani, ambapo pia ameahidiwa kupekwa masomoni.Ilipofika jioni, Diana alichukuliwa na taksi, ya mshikaji wake na moja kwa moja walielekea Kaunta. Huko alikunywa kama amesingiziwa. Waliondoka maeneo hayo usiku akiwa hajitambui. Njiani kwa vile walikuwa wamelewa chakari, wakapata ajali mbaya, ajali hiyo ilimvunja Diana mguu na kujikuta anapelekwa Muhimbili.
Kwa vile Kampuni yake mpya ilishaingia mkataba naye, ilimsaidia na kumhakikishia kuwa ajira yake bado ipo ingawaje alikuwa hajaanza kazi. Hii ilimpa faraja sana Diana, na akaendelea na matibabu yake huku akijua hawezi kumrudia meneja JeuriMbaya.. Hapo Muhimbili alikaa miezi miwili. Alipotoka, alipewa mapumziko ya mwezi mzima nyumbani.
Siku ikafika, na hali ya mguu wake ilisharejea vyema, ikabidi aripoti ofisini kwake, kwenye ofisi mpya. Alikariribishwa kwa bashasha na kila mmoja akimpa pole kwa huruma na upendo. Hali hii hakuizoea huko alikotoka. Alifurahi moyoni, na kusema `hapa ndipo nilipokuwa nikapataka…
`Diana tuna bahati kubwa sana, kwani tumepata meneja utawala mpya, ambaye utakuwa katibu muhtasi wake, naye kaajiriwa karibuni, kwahiyo twende ofisini kwake ukatambulishwe’ Aliambiwa na Ofisa utawala.
Akiwa na bashasha ya kumuona meneja wake mpya, ambaye alihisi atakuwa Mzungu, alitabasamu akamtafadhali Ofisa Utawala na kuchepuka kwanza chooni ili aweze kujikwatua. Hii ilikuwa sehemu ya mambo ambayo alifundishwa kuwa anatakiwa apendeze ili kumvutia bosi wake pamoja wageni.
Aliongozana na ofisa utawala, mama wa makamo, mama ambaye aliijua kazi yake vilivyo. Na kwa uzoefu wa siku nyingi, aliona amuelekeze yule binti wake mambo kadhaa kabla hajampeleka kwa bosi wake mpya. Diana alijisikia vibaya, hakupenda kukosolewa, lakini alijikaza akijua kuwa anabembeleza ajira.Kabla ya kuingia kwa meneja huyo ilibidi wapitie kwa meneja wengine mbalimbali, na kila sehemu alipokelewa vizuri na kukaribishwa ofisi mpya.
Mwishowe walifika kwenye ofisi iliyoandikwa `Meneja utawala’ Waligonga mlango wa Meneja Utawala na kukaribishwa ndani.Walipoingia walimkuta meneja Utawala akiwa ameinama na kugeukia upande mwingine, kwahiyo sura yake ilikuwa haionekani vizuri.‘Karibuni tafadhali, natafuta faili moja hapa, la huyu katibu wangu Mhtasi, unasema anaitwa nani vile…’
Aliwakaribisha huku akitaka kulifunua lile faili, bila kuwaangalia.‘Tafadhali bosi hatutaki kuchukua muda wako mwingi, yeye kwa vile mtakuwa naye karibu atajitambulisha kwako vizuri, kama unavyojua alikuwa anaumwa, kabla hata hajaanza kazi hapa….’ Aliongea ofisa utawala.
‘Oooh, karibuni sana,..’ aligeuka akiwa amenyosha mkono.Mshangao alioupata Diana ulimfanya aishiwe na nguvu, na kama asingekuwa ameegemea meza angejikuta kadondoka chini. Hakuamini macho yake…
‘Ahsante, sh-shi-kamoooo bosi’ Alijikuta akitoa salama ambayo hajawahi kumsalimia bosi wake kabla.Aliyekuwa amesimama mbele yake si mwingine ila ni bosi wake wa zamani, ambaye waliachana naye kwa mizengwe, sasa ni bosi wake mpya, Mr.Jeuri Mbaya.JE KAMA WEWE UNGEKUWA NI DIANA UNGEFANYAJE
From miram3.com
Tuesday, August 18, 2009
MWANGALIE ALIYECHINI YAKO
From miram3.com
Monday, August 17, 2009
Mikataba ya ajira kulikoni
`Ndugu yangu aheri nimekuona,manake watoto wamefukuzwa shule sijalipa ada sasa mihula mitatu, jana nimepokea barua kuwa mwisho wa mwezi huu mkataba unakwisha na hawana haja ya kunichukua tena. Baba yangu anaumwa na mke wangu ndio huyu hauchihauchi kunakucha sina hela ya kumtibia, je nina thamani gani katika hii dunia, hebu niambie rafiki yangu?' alinielezea huku machozi yakimlengalenga.
Rafiki yangu huyu alimaliza diploma yake vizuri akapata kazi katika kampuni moja ya watu binafsi, aliitumikia kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka 15, kwa uaminifu na uchapajikazi bora, kiasi kwamba mwajiri wake alimpenda sana, lakini kwa mdomo, hakuwahi kuongezwa mshahara na walioajiriwa baadaye ambao wangi walikuwa watoto wa wakubwa au wageni toka nchi nyingine walipewa mishahara minono . Alidai haki yake ili naye afikiriwe, na huko kudai kukamtokea nyongo, mwajiri akabadili kibao na mkataba ulipoisha akaambiwa katafute sehemu watakaokulipa mshahara unaotaka, na barua hiyo alipewa jioni wakati muda wa kazi unaishia.
Katika mkataba wake wa ajira alitakiwa alipwe mshahara wa mwezi mmoja tu kama zawadi, na kwa vile alikuwa na madeni hela yote aliyotakiwa kulipwa ilikatwa kufidia sehemu ya deni lake.
Hadithi ni ndefu, na unaweza ukasema yote maisha, lakini dukuduku langu ni huu utaratibu wa nchi, wa kutowalinda raia zake katika sehemu za kazi. Hawa wenye makampuni wanawatega wafanyakazi wao kwa mikataba ambayo hatimayake ni mbaya. Nafikiri kungekuwa na mkataba wa ujumla kuwa kila anayeajiriwa anatakiwa kupata haki hii na alindwe vipi na mikataba hiyo. Makampuni mengi ya watu binafsi hayataki vyama vya wafanyakazi, je serikali inajua hili? Au mimi ndio sijui , naomba tujadiliane hili.
From miram3.com
Friday, August 14, 2009
Adha ya Usafiri na diari yangu
Na siku za nyuma niliandika maelezo mazuri kuhusiana na tatizo la Usafikiri njia ya kuelekea Gongolamboto na kuiepeleka kwa michuzi ikiwa na kichwa cha habari kero ya usafiri Gongolamboto.
From miram3.com
Thursday, August 13, 2009
Tusaidie wenye ulemavu
NGO, nyingi zinaanzishwa lakini ni chache zinazopenya vijijini. Ombi langu kwa wenye uwezo wasaidie kuanzishwa shule kama hizi vijijini kwani kati ya hawa wapo wenye vipaji vikubwa, wataalamu na viongozi wa baadaye. Inabidi na wamanchi waelimishwe kuwa kuwa kilema sio mkosi, bali ni sehemu ya maumbile tu ya kibinadamu.
Wednesday, August 12, 2009
Mtoto wa mwenzako ni wako pia
Katika kukuru kakara hiyo mtoto mmoja wa shule ya msingi alidandia, na wakati huo gari linaongeza mwendo na yule konda, au mpiga debe akawa anamsukumia nje. Ilikuwa ni hatari kwasababu kama yule mtoto angeishiwa nguvu na kuachia vile alivyong'ang'ania ule mlango wa gari angedondoka na kuumia. Baadhi ya wazazi mle ndani wakaanza kumshambulia yule konda kwa maneno kuwa amuachie yule mtoto aingie ndani.
Hatimaye yule mtoto alipenya kwa shida akaingia ndani ya daladala. Niliwaza sana ni nikijua kuwa hata mimi watoto wangu watakuwa wanafanyiwa hivyo. Hii ni kujisahau na kutizama yale matamanio yetu ya muda ule. Namshukuru sana mke wa raisi wetu alipotoa kauli kuwa `mtoto wa mwenzio na mtoto wako pia.
Kama usipomjali mtoto wa mwenzio ujue hata wakwako atakuwa hajiliwi pia, ukimtenda ubaya ujue na wakawao atatendewa ubaya pia, hata kama una uwezo ipo siku na wewe au yeye atakumbana na maswahiba hayo.
Ombi langu tusipende kutendea ubaya wenzetu, kwani na sisi yatatukuta kwa namna moja au nyingine, kama sio kwako ni katika uzazi wako, na muumba anatuona kwa hayo tunayo tenda kwani yeye ni mwingi wa hekima.
Tuesday, August 11, 2009
Ubinadamu unatokomea
Je ipo sababu kweli kubwa ya kufanya kitendo hicho?
Kuna wengine walidai, alipopewa mimba aliyempa alimsaliti, lakini je hicho kiumbe kina kosa gani, kwani kusalitiana ni kati yao wawili, na hicho kiumbe hakikuwepo kwenye makubaliano yao. Hii yote ni kujisahau nakujiona tuna maamuzi na utawala wetu binafsi. Tunajisahau kuwa kuna leo na kesho, na yupo muumba mwenye mamlaka na wewe zaidi ya unavyofikiria.
Kwa ushauri wangu binafsi, kila tunalofanya tujaribu kuangalia kulikoni, je ikitokea hivi itakuwaje? Na pili je kama na mimi ningefanyiwa hivi ingekuwaje?
Tushauriane kwa hili