Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, August 26, 2009

MAWAZO YANGU

HAYA NI MAWAZO YANGU, JE WEWE
Wakati napita katikati ya mji, nilimkuta mama mmoja mwenye matatizo ya Akili, mama huyu alikuwa na mtoto wake pembeni. Nilishangaa kidogo,kwani mama huyu ana matatizo haya kwa siku nyingi. Nilijiuliza ilikuwaje akapata huu ujauzito. Kwa hisia za harakaharaka nilikisia kuwa huenda jamaa walimbaka.
Hapa mawazo yangu yalinikumbusha jamaa mmoja aliyekuwa na matatizo kama hayo maeneo ya Kariakoo, huyu alikuwa mwanaume, na akimuona mwanamke aliyempenda hutaka kumshika kwa nguvu, kwahiyo wanawake wanapomuona hukimbia.
Wenzetu hawa wapo dunia ya aina yao, kwani wakati mwingine utawakuta wanaongea, wanaimba, wanacheza na hata kufanya mambo ya ajabu-ajabu ambayo wakiwa na Akili zao wasingediriki kufanya vitendo hivyo. Haya ni matatizo na ni ugonjwa ambao huenda ukapona au usipone kutegemeana na kiini chake.
Kuna wale waliozaliwa na tatizo hilo,au tatizo limetokana na kurithi,lakini kuna wale waliopata matatizo haya kutokana na maisha kwa ujumla. Kuna waliopata kwasababu walidhulumu, wapo waliopata balaa hili kwa kuwatendea wazazi wao isivyotakiwa. Na wapo waliopata matatizo haya kwa kutendewa na binadamu wenzao, na hapa nikajiuliza kwa vipi binadamu aamue kumtesa mwenzake na kumzalilisha kiasi hiki.
Wakati natafakari hivi nikawakumbuka wavuta unga, na waathirika na madawa ya kulevya,ambao hawana tofauti sana na hawa wenye matatizo ya akili,ingawaje hawa wa madawa wanaweza wakajizuia na hubadilika tu pale wanapobwia hayo madawa au kujidunga hayo madawa.
Tarehe ya leo 26-08-2009, nikaona niliweke hili hapa nikijaribu kutafuta mawazo kwa wenzangu kuwa kwanini kizazi chetu kinateketea na madawa haya. Na tufanyeje ili tusipate wagonjwa wa akili wa kujitakia. Huenda tukabuni njia mbadala, mfano kuanzisha kijiji cha vijana ambao wameshaingia katika kundi hili. Kijiji hiki kikawa kama sehemu ya mafunzo, wawepo wataalamu wa kuwahudumia kisaikolojia, wawepo wataalamu wa kazi mbalimbali ili kuvumbua vipaji vyao walivyonavyo. Nafikiri kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeliokoa taifa na kuyaokoa maisha ya hawa ambao wameanza au wameshatumbukia katika balaahili.
Haya ni mawazo yangu tu,kwa leo.
From miram3.com

No comments :