Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za maisha (diaries), visa na matukio na yale unayopenda kuchangia na wenzako (mijadala), maneno ya hekima, kusaidiana na pia kutoa dukuduku lako (kilio chako). Soma na uchangie chochote kwa kutoa maoni (comments) yako, au tutumie kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA

TUNAKARIBISHA MATANGAZO YA BIASHARA HAPA

Friday, May 25, 2012

Hujafa hujaumbika-41



Ilikuwa muda wa mchana wakili mwanadada akafika nyumbani kwa wakili mkuu wa kitengo chao nyumbani kwa bosi wake, alikuwa na uhakika kuwa bosi wake huyo hayupo nyumbani muda kama huo, akagonga mlango na kufungulia na mfanyakazi wa nyumbani, na kwa vile walikuwa wakijuana baada ya kusalimiana wakawa wanataniana.

‘Leo mimi ni mgeni wako, nataka unipigie ugali wa nguvu….siunajau tena mimi ndio mume wako mtarajiwa….’akamwambia.

‘Ugali tu, …hapa umefika, nashangaa leo kuja hapa mchana tena muda wa kazi, umekuja kunifumania nini…maana waume nasikia wanafanya hivyo, ….eti mume mtarajiwa, ….’akasema huyo mfanyakazi huku akicheka.

‘Nani kakumabia hayo, ….umeshaanza kunikana, ….unajua lazima nilinde mali yangu, wewe unafikiri huko nilikokutoa nilikutoa kwa mahari ndogo, …mimi ni mumewako..’ Akawa anaigiza suti ya kiume na wote wawili wakawa wanacheka huku wakitaniana, na hili lilimfanya huyo mfanyakazi wa nyumbani amuzoee sana huyo dada wakili.

‘Sasa sikiliza mimi nimekuja hapa, nataka unisadie jambo moja, lakini iwe siri yangu mimi na wewe, …ehe nimekumbuka, kwanza hujanimalizia kile kisa ulichonisimulia,….siku ile hatukuweza kukimaliza, kwanza naomba unisimulie kwa urefu ilivyokuwa halafu kama tutapata muda kuna kitu nataka tukifanye, usijali mimi nipo kwa ajili yako,…’akasema mwanadada.

‘Mimii sipendi kuongea tena kuhusu maisha yangu, maana kila nikiongea nazidi kujiongezea machungu, maana hata mama  huyu mwenye nyumba, naona kafikia kuniona mimi labda ndiye mbaya, anafikiri kuwa mimi ndiye nimefanya mume wake abadilike, na juzi tu alikuwa akitaka kunifukuza nirudi kwetu kijijini, …..’akaanza kulia.

‘Sikiliza mpendwa, mimi nia na lengo langu ni kukusaidia wewe, lakini sitaweza kuchukua hatua yoyote mpaka nijue kiini na ukweli ulivyo, ujue yule ni bosi wangu kazini, na lolote nitakalofanya juu yake natakiwa niwe na uhakika nalo, na ukizingatia kazi yangu ilivyo yeye anaweza akaweka pingamizi ambalo litanifanya hata nisiweze kuanzisha ofisi yangu, kwahiyo nahitajika kuwa muangalifu sana….’akasema wakili.

Kimiya kikatawala, na wakili akasema; Anzia pale huyu mama alipokuja huko kijiji, akakuta ukiwa majalalani, ….’akasema huyo wakili na huyo binti akaanza kuongea;

**********

‘Huyu mama wa hapa alinichukua kijijini,nikiwa mdogo, sijavunja ungo, alinichukua kwasababu mama yangu alikuwa hana mbele wala nyuma, ukumbuke kama nilivyokuambia awali kuwa mama yangu, alipata ujauzito, akafukuzwa kwao na wazazi wake, ….na niliuambia kuwa ili aweze kuishi alianzisha biashara ya pombe,….waanwake wengi kule kijijini wanafnya hiyo biashara ya kuuza pombe,….

‘Huyu mama kukutana naye kwa mara ya kwanza, ni pale alipopita akiwa na wenzake akaniona nikiwa majalalani,akanione huruma, nilivyochafuka kuna baridi lakini nilikuw akifua wazi, na vinguo vilivyochakaa,kwa muda huo, nilikuwa natafuta vyakula vilivyotupwa kwenye hiyo hoteli iliyopo hapo karibu na hilo jalala, angalau siku hiyo ipite, akanionea huruma na kuniuliza mama yangu yupo wapi…

‘Mama anaumwa, kashindwa kwenda kufanya biashara, hatujala toka jana…’nikamwambia, huyo mama hakuniamini, akaniambai nimpeke huko nyumbani akamuona mama yangu, nikamchukua hadi hapo tunapoishi, ni chumba kidogo tu cha uani,akamkuta mama yupo hoi, anatapika na kuharisha. Kwasababu huyu mama ni dakitari akamchuku hadi hospitali ya karibu ….’ Hapo akatulia ilionekana alikuwa akimuwaza mama yake, na wakili akamwambia;.

‘Endela kuongea nataka kusikia kila kitu kutoka kwako, ili nijue wapi pa kuanzia. Ikawaje?’ akauliza.

‘Basi mama akatibiwa kwa msaada wa huyu mama na kweli alipona vizuri, baada ya siku tatu akarudi kwenye kazi yake ya kuuza pombe, na mimi nmara nyingi huwa naachwa nyumbani, ….nilikuwa bado mdogo tu, wakati mwingina mama anakuwa hana kitu, ananiacha bila hata kitu cha kula, naishia kwenda kuomba kwa watu, au kuokota chakula majalalani,.

‘Huyu mama alipoondoka kumbe alishapanga kuja kunichukua,…lakini kwa safari hiyo hakuja yeye, .siku hiyo alikuja mtu anaishi huko huko kijijini , tunamfahamu, akanimbia kuwa yeye katumwa na huyo mama kuwa anichukue niende nikaishii naye, lakini mama yangu kakataa. Mimi niliona kuwa hiyo ndiyo nafasi ya kuondokana na dhiki tuliyokuwa nayo,, licha ya kuwa nilikuwa mdogo,lakini nilishaona haya sio maisha ya kuishi. Nikamwambia huyo mtu nipo tayari kutoroka.

‘Hapana nilivyoagizwa na huyo mama ni kuwa nikuchukue mikononi mwa mama yako, siwezi kukutorosha wale watu wapo serikalini, hawawezi kufanya jambo kama hilo, nandoka, kama huyo mama ana nia ya kweli atakuja yeye mwenyewe. …maana mama yako mimi simuwezi…mwenyewe anauma, hawezi kukuhudumi bado anakung’ang’ania,…eti mwanangi sitaki achukiliwe….’akasema yule mtu na kuondoka.

‘Basi kweli siku hiyo ikashindikana, na baada ya mwezi hivi, yule mama akaja kweli, na kukutana na mama yangu, alichofanya ni kumsaidia mama pesa za msingi za biashara nyingine zaidi ya pombe, mama alipoona pesa, akakubali na kesho yake nikaondoka na huyu mama kuja huku mjini.

Nilipofika huku mjini huyu mama alinifanya kama mtoto wake, na akanifanyia taratibu zote za kusoma, na kuanza darasa la kwanza, nilisoma nikiwa kwakke hadi darasa la saba,na muda owte huo akinilea kama mtoto wake.

‘Tatizo lilianza nilipofika darasa la saba,…mwili wangu ulikuwa haraka, na kuonekana msicha mkubwa, kuliko umri wangu,… baba akaanza kuniangalai kwa jicho la kuniogopesha,…’akasema na kutizama chini.

‘Jicho gani hilola kuogopesha…?’ akauliza wakili.

‘Jicho la …..yaani sijui nisemeje,…anakuwa mara kwa mara anaiangalia hasa nikitembea au nikiwa nimekaa , naona kama ananichunguza chunguza sana, na siku moja nikamwambia mama , mbona baba ananitizam hivyo, akaniambia, niwe mwangalifu,..na kama nitafanya uchafu atanifukuzilia mbali.

‘Uchafu gani huo mama, mimi sina maana yoyote mbaya ni kwa vile naona baba anavyonitizama sio kama ilivyokuwa zamani…anakuwa kama ananichunguza mwili wangu kwa macho….’nikamwambia mama nikiwa sijui lolote, akili yangu ilikuwa haina maana nyingine yoyote.

‘Nitalifuatilia hilo, ila jaribu kutokuwa karibu naye hasa nikiwa sipo,..unanusikia,….’akanionya.
Dada wakili akauliza haraka kabla huyo binti hajaendelea,

‘Kwanza nikuulize baba na mama yako hapa wana maelewano mazuri, nakumuka siku moja uliniambaii huwa wanapigana, bado mambo yao yapo hivyo hivyo…?’ wakili akamuuliza huyo binti.

‘Kwaweli mara nyingi wanazozana, sijawahi kuwaona wakiwa na furaha, naona kila mmoja ana lake, wanaweza hata kupigana kwa jambo dogo tu, na huwa nikisia hivyo nakimbilia nje, sitaki hata kusikia wanavyozoazana, maana mama mkali na baba mkali siuombe, wakianza kuzozana mmoja anaweza akaokota chochote na kimpiga mwenzake…’akasema huyo binti.

‘Je hukuwahi kusikia maswal ya kufumaniana, yaani mama kumsema baba au baba kumsema mama…kuhusu maswala hayo?’akauliza wakili.

‘Na mara nyingi ugomvi wao unahusu hayo maswala, nakumbuka kuna siku mama alimwambia baba kuwa anaushahidi kuwa baba anatembea na machangudoa, na atamkomesha, kwa tabia hiyo….’akasema huyo binti na hapo wakili akatulai kuwaza, halafu akamwambia huyo binti aendelee kuongea.

‘Siku moja mama alisafiri kikazi, akabakia baba na mimi, ujue mama huyu hana mtoto, sijui kwanini, na hil pia limekuwa ni tatizo lao, maana wakija wanandugu hapa wanamsema  sana baba kuwa eti kaoa mke tasa,wanamshauri aoe mke wa pili au amuache huyo mke wake, kwasababu hana maana yoyote, lakini baba hakubali,…nahis huenda baba ndiye mwenye matatizo lakini hataki kukubali ukweli yeye anadai mama ndiye mwenye matatizo…’akasema huyo binti.

‘Kwanini unasema huenda baba ndiye mwenye mtatizo?’ akauliza wakili.

‘Kwasababbu mara kwa mara mama amekuwa akimwambia baba waende wakapime, ili wajue tatizo lipo wapi, lakini baba hakubali, na wakinza kuongelea hayo baba anaondoka kwa hasira na kwenda zake, akirudi amelewa. Hapo hakukaliki, maana ni fujo, nyimbo, kupigana, muda kama huo nijifungia chumbani maana yanayofanyoka hapo hayafai, baba huwa anamshika mama kwa nguvu, hajali hata kama nipo karibu…’akasema.

‘Anamshika kwa nguvu kwanini, yaani kutaka kupigana au anamshika kwa vipi, hebu nifafanulie hapo….?’ Akauliza wakili.

‘Anamshika kwa mambo yao ya kindoa, yaani baba anakuwa kama kachanganyikiwa vile, mama ana taabu kweli kweli, ila huyu mama ni mvumilivu ajabu, anamvumilia sana mume wake,….pamoja na hayo, baba akizidiwa ulevi, anamchukua anampeleka kumalza chumbani kwake…’akasema huyo binti.

‘Ehe endelea ikawaje?’ akasema wakili.

‘Basi huyu baba akarudi kazini jioni, akanikuta napika chakula,…nilikuwa nimetoka bafuni,kuoga,na sikutarajia kuwa baba atarudi mapema hivyo, kwahiyo sikujali, nilijau nipo peke yangu ndani,….baba alipofika akaniangalia kama kawaida yake, akanitizama mwili mzima, huku nikiwa naogopa, …. akaniambia nije anataka kuongea na mimi, nikaacha kupika na kumfuata huku naogopa, nikijua nimefnya kosa nisilolijua ….’akasema.

‘Kakuita umfuate wapi, yaani chumbani kwake au barazani au wapi?’ akauliza.

‘Aliniitia akawa aoanongza chumbani kwangu, na nikajua kuna kitu hakikuwa sahihi huko ndani, na kwa vile najua huwa anakagua kila mahali kuwa kila kitu kipo sawa,  nikajua labda kuna kitu nimeweka vibaya,…’akasema

‘Je ina maana huwa mara kwa  mara anaingia chumbani kwako kukagua?’ akauliza wakili.

‘Ndio, huwa anasema anakagua usafi,…huyo baba mkoloni kweli, akiona vitu vimekaa vibaya hakukaliki, anakagua kuhakiksha kila kitu kipo safi na kimepangwa vizuri…hata mama haoni ndani kwa usafi wa huyo mzee….’akasema.

‘Ehee, ikawaje?’akassemawakili.

‘Yeye alitangulia chumbani kwangu, huku nyuma nawaza sijui kupoje,maana sikuwa nimejua kuwa atarudi mapema,huwa muda wa kurudi nahakikisha kila kitu kipo sahihi,…., nilipofika nikamkuta kakaa kwenyekitanda, nikashangaa sio kawaida yake, kukalia kitanda change, akaniambia nije nikae naye karibu nikaogopa, nikakumbuka alivyoniambia mama, nikakataa katakata, akasimama kwa hasira. Na kusema;

‘Ina maana siku hizi umekuwa na kiburi, mimi nakuita hapa hutaki, ngoja leo nitakiondoa hicho kiburi chako, akanivamia na kunishika kwa nguvu….’akasema huyo binti.

‘Alikushikaje kwa nguvu, kwa vipi, hebu elezea hapo vizuri….?’akaulza wakili.

‘Mimi kwa muda huo kama nilivyokuelezea, nilikuwa nimevaa khangatu, kwasababu nilikuwa nimetoka kuoga, na nilipitia jikono kuangalia kuwa vyakula haviungulii, na nikitoka hapo niende chumbani kwangu kuvaa , sikujua kabisa kuwa huyo baba atarudi muda kama huo, kwahiyo aliposimama pale aliishika ile khanga niliyovaa na kuivuta kwa nguvu, nikabakia uchi, akanivamia na kilichofuata hapo siwezi hata kuelezea….’akaanza kulia.

Yule wakili mwanadada alimpa nafasi huyo binti alie, hakutaka kumsemesha kwa muda, na alipoona katulia 
akamuuliza swali jingine;

‘Mama alikaa huko alipokwenda kwa muda gani….?’akauliza wakili.

‘Mama alirudi kesho yake, na nilijaribu kumkwepa ili asijue ukweli,sikutka kumwambia, ingawaje alihis mabadiliko, maana huyo baba aliniumiza kweli siku ile, hata kutembea ilikuwa natembea kwa shida. Lakini  mama akanigundua na kuniuliza,;

‘Wewe una matatizo gani,ndio kutembea gani huko….?’ Akaniuliza na mimi nikasema ni miguu nilidondoka unaniuma, niliogopa mama akijua atanifukuza na baba alishaniambia kuwa kama nitamwambia mama atahakikisha kuwa naondoka hapo nyumbani….’akasema huyo binti.

‘Je mambo kama hayo yaliwahi kutokea teana, na kamailitokea ilikuwaje..?’akauliza wakili.

‘Ilitokea tena....siku hiyo mama alikuwa kasafiri na siku hiyo nilipiga makelele mpaka majirani wakaja, na hata walipofika huko nje, huyo baba hakufungua mlango mpaka alipomaliza shida yake …yaani ungemuona siku hiyo,huwezi kuamini kuwa ni mtu na heshima zake, alikuwa kama kichaa, …nilipigana lakini yeye ana minguvu 
akanishinda,…yaani siku hiyo nililia sana,…unajua hakujali kuwa watu wapo nje, kwani  alipotoka nje kuonana na hawo majirani aliwadanganya kuwa, eti alikuwa akiniadhibu kwasababu nimeharibu vitu, na kweli hawo majirani walimuamini, ....’akasema.

‘Mama alivyokuja hukumwambia , uliendelea kukaa kimiya?’akauliza wakili.

‘Mama alikuja kupata taarifa toka kwa majirani, na hapo akanijia juu na kuniambia kuwa nisiposema ukwelii ataniridisha kwetu, ikabidi nimwambie ukweli...’akasema na kutulia.

‘Huyo mama alisemaje,….?’ Akauliza wakili.

‘Alichanganyikiwa, alisikia hayo aliinuka akachukua gilasi ya maji aliyokuwa kashika na kutupa ukutani, nafikiri kama baba angekuwepo hapo angempiga nayo,…na baba aliporudi nilijua leo kuna mambo, huenda ikawa siku yangu ya mwishoo kuishi hapo.

Siku hiyo hakukalika, mama na baba walipigana vyombo vikavunjika, vitu  vikadondoshwa huku na kule, hakuna jirani aliyejali, kwani walishawazoea, wakaumizana kweli damu zinawatok, hawajli,…., baba akavimba jicho hakuweza kwenda kazini kesho yake,,…hata mama hakwenda kzini siku hiyo, na baba alipopata mwanya akasema atahakikisha ananifukuza hapo nyumbani…., na kumbe  mama alisikia akaja na kusema haondoki mtuu hapo nyumbani na atahakikisha kuwa huyo baba hanifanyo lolote tena.

‘Hawa watu wanatoka wapi,….mkoa gani…?’ akauliza wakili na kabla huyo binti hajajibu akamuuliza swali 

jingine kkwa haraka;

‘Ina maana baada ya yote hayo huyo mama hakuchukua hatua yoyote?’ akauliza wakili.

‘Nakuambia huyo mama ni mvumilivu sana, alimsamehe mume wake, lakin kwa masharti kuw akirudia tena 

analipeleka hilo swala kazini kwa baba, na unajua likifikishwa huko kazini kwa baba itakuwa vibaya…baba akaomba msamaha ’akasema huyo binti.

‘Huo msamaha ulifanywaje, mlikaa kikao, au waliongea wenyewe ukasikia…?’ akauliza wakili.

‘Tulikaa kikao, baba aliniita mimi na akamuita mkewe, akaanza kuongea, kuwa anajua yeye ndiye mkosaji, na ibilisii alimpitia kwasabbu ya pombe,….huwa anapenda kujitetea kwa njia hiyo kwa kusingizia kuwa anafanya yote hayo kwasababu ya pombe, na mama anamwambia kama ni pombe achane nayo, lakini baba anasema yeye hawezi kuacha pombe…kwasababu anakunywa kumuondolea mawazo....’akatulia kuongea huyo binti.

'Mawazo gani hayo, ya kuja kuharibu .....'akasema mama kwa ahsira.

'Wewe mwanamke, huwezi kujua mawazo aliyo nayo mwanaume, tuna mambo mengi ya kufikiri....pombe ndiyo inasaidia kunituliza akili, kunipa maarifa, ....hujui wewe....'binti akawa akawa anaongea kuigiza sauti ya kilevi ya baba yake, na wakili atakatabasamu na kusema;

‘Nikuulize swali moja, unijibu kwa moyo wako ukiwa huru hebu niambie ukweli, je hayo aliyokufanyia huyo baba uliyachukuliaje?’ akauliza.

‘Kiukweli huyo baba namuona kama baba yangu mzazi ingawaje simjui baba yangu yupoje,  yeye nilimuona ndiye baba yangu….kwamba nieyachukuliaje,…sijui niseme nini…’akatulia kwa muda halafu akasema;

‘Mimi,nimeyachukulia kuwa kanifanyia hivyo kwasababu hanijali ananiona kama mtumwa fulani, au changudoa tu, mtu nisiye na thamani kwake, kuwa anaweza kunifanya atakavyo kwasababu nakula kwake, ananilisha yeye, nasema hivyo kwasababu, siku hiyo aliponibaka kwa mara ya kwanza aliniambia ni nini atapata kutoka kwangu baada ya fadhila zote alizonifanyia mimi, akaniambia kuwa mimi ni damu ya Malaya muuza pombe, changudoa….alitamka hilo akimaanisha kuwa mama yangu ni Malaya, muuza pombe na anajiuza…kwahiyo hata mimi nipo kama yeye,…iliniuma sana….’akasema na kuanza kulia.

‘Kwahiyo hujafurahia hilo tendo,…nina maana kuwa, kuna baadhi ya wasichana niliowahoji, baada ya kufanyiwa hivyo, walisema kuwa wanatamani wawe wake wa hawo wanume waliowafanyia hivyo na wengine kudiriki kuzivunja ndoa za hawo wenye nyumba, kwa kudai kuwa kama baba mwenye nyumba kampenda, kwanini ajivunge,…’wakili mwanadada akautulia na kumwangalii huyo binti na alipoona yupo kimiya akasema.

‘Unajua kwanini nakuuliza hivyo, au hujanielewa,…..kwasababu gani nasema hivyo, kwanini hukutafuta mpango wa kuondoka hapa, maana naona hakuna amani…au ungelichukua hatua nyingine za juu, hata kuwaambia majirani wakusaidie, lakini wewe ulikaa kimiya, je una hisia zozote na huyo mzee?’akasema wakili.

‘Nitaenda wapi mimi,…. mama yangu huko kijijini anaumwa sana, anahitaji pesa, na mimi lengo langu nikukusanya pesa nikamtibie,….ingawaje huyo mama anajitahidi,alijaribu kumtibia lakini naye ana majukumu yake huko kwao, anasomesha wadogo zake, na pesa hazimtoshi na mume wake, tangu walipogombana kuhusu mimi, alisema yeye hatatoa pesa yoyote kunisaidia mimi tena….’akasema huyo binti huku akilia.

‘Kwahiyo ina maana hata akiamua kukufanyia hivyo na kukuahidi pesa utavumilia tu, ili upate pesa za kumsaidia mama yako?’ akauliza wakili.

‘Baada ya kile kikao,mimi nilimuamini kuwa hataweza kunifanyia hivyo tena ndio maana nikawa na amani, ili nilijiahidi kumkwepa , sikuwa karibu naye tena…’akasema huyo binti.

‘Hakuwahi kukufanyia  hivyo tena…?’akauliza wakili.

‘Mama alijitahidi kuhakikisha kuwa mume wake akiwa nyumbani na yeye yupo, ana watu wake kawaweka majirani, wakisikia baba kaja nyumbanai na yeye huja haraka, kwahiyo baba amekuwa hapati mwanya huo tena, ila namuona kila mara anatafuta mbinu nyingine …naskia mama akisema huyo baba kaamua kutembea na machangudoa ili kumzalilishiai yeye , eti hamtoshelezi…’akasema huyo binti kwa aibu.

Yule wakili alitaka kumuuliza swali jingine lakini akasita, na kuangalia saa yake. Halafu akasema huku akiinuka kwenye kiti na kujinyosha,ilikuuwa kama vile anataka kuondoka, akasema;

‘Nina mengi ya kuongea na wewe, …lakini nikuulize tena, haijawahi kutokea tena kukufanyia hivyo, nauliza hilo swali mara nyingine nikiwa na maana yangu, niambie kiukweli….?’ Akauliza huyo wakili alipoona kuwa huyo binti anaficha baadhi yaukweli.

‘Kuna mara nyingi anakuja usiku chumbani kwangu, lakini mama anamuwahi kabla hajafanya lolote…na hajaweza kufanikiwa kwa hilo….nashukuru kwa hilo….’akasema huku akiwa na wasiwasi.

‘Kwa mfano, nikuulize swali kwa namna nyingine, kama huyo baba akisema anataka akuoe wewe,…upo tayari?’akajikuta akimuuliza hilo swali kimtego, lakini  baada ya kufikiri sana, huku akimwangalia machoni huyo binti, yule binti aligeuka pembeni akawa hamuangalii moja kwa moja huyo wakili , kwanza alitulia na baadaye machozi yakaanza kumtoka na kusema;.

‘Huyu baba kwangu namuona kama baba yangu, ….siwezi kabisa kuolewa na yeye , nitakaaje naye, hata kufikiria hivyo sifikirii, kitendo alichonifanyia sitaweza kukisahau maishani kwangu….naona kama ni hivyo ,kama ndivyo mateso yalivyo ….machungu niliyoyapata, naona ni heri nsiolewe, sitaweza kuvumilia tena …..’akatulia huku akiangalia chini.

‘Una maana gani kusema hivyo…?’ akauliza wakili.

‘Natumai hapo umenielewa dada, ni maumivu unayoyapata, sijui nikuambieje, ….kama kuna watu wanasema hivyoo kuwa wanatamani kuolewa na baba zao, sio mimi…sitaki hata huko kuolewa kwenyewe, kuna raha gani kama ni hayao mateso….’akasema na na wakili akamuelewa na kutabasamu.

‘Siku itafika utaolewa na mume anayekupenda utayasahau hayo yote….’akasema wakili mwanadada na yule binti akasema kwa uchungu.

‘Mimi hapa nipo kwa vile sina pa kwenda,sina kazi sina mbele walal nyuma,…nitafanyaje mimi,mimi mtoto wa masikini, mimi naitwa mtoto wa Malaya muuza pombe,…matatizo ya mama, na mimi nabebeshwa huo mzigo, labda kama wanavyosema mtoto wa nyoka ni nyoka, lakini mimi sifikirii kuwa kama mama, na mama alifanya hivyo ili kujisaidia katika maisha, sizani kama alipenda hayo maisha,….mmh, mimi sijui la kufanya kama huyo baba ataendelea kunifanyia tena tendo kama hilo, naona kama nikunizalilisha tu…’akawa analia.

‘Nimekuuliza hivi kama atasema anakupenda wewe, uwe mke wake, …nijibu tu unavyofikiria moyoni, ungalimjibu vipi kama kakujia na hoja kama hiyo, na mke wake akakubali, kwasababu labda ya kutaka kupata watoto au tu huyo baa kakupenda, natoa kama mfano,?’ akauliza huyo wakili.

‘Nikuambie ukweli dada, mimi hapa natamani dunia ipasuke nizame, na kila nikimuona huyo baba, natamani sijui nifanye nini, simpendi kabisa, lakini, mimi kama nani,… maana imefikia mahali sioni raha ya kuishi hapa duniani, siku moja nilishaamua kunywa sumu, ….lakini bahati huyu mama akanifuma, na aligombeza sana akajaribu kunipa ushaurii nasaha, nikamuelewa,…. ndio maama bado nipo tu, lakini kama huyo baba ataendelea tena kunifanyia hivyo, kwakweli, sijui nitachukua hatua gani….’akasema huku akionyesha chuki ya wazi usoni.

‘Sikiliza katu usije ukafanya ujinga huo,…nina maana ujinga wa kutaka kujiua, ili iweje,…. maana wewe utajiumiza mara mbili,….umezalilishwa wewe na bado ukimbilie kujiua, umemkomoa nani kama sio kujikomoa mwenyewe,  huko ni sawa na kujiumiza mara mbili, na je ukijiua huko kwa mungu utasemaje,….!’akasema na kumwangalia machoni.

‘Lakini mungu anaona nini ninachofanyiwa, ….hebu jiweke katika nafasi yangu, uone, machungu yake, mtu anakubaka, tena sawa na baba yangu,….hajali , anakubaka huku anakusimanga, kuwa wewe ni Malaya tu kama mama yako kama nini sijui….mimi nimeujuaje huo umalaya, wakati yeye ndiye mtu wa kwanza kuniharibu, kunifanyia huo uchafu….hebu niambie dada yangu….mungu anayaona yote haya, sio kwamba nimepnda, anaiona nafsi yangu,….’, akasema huku akiwa analia kwa uchungu.

‘Sikiliza ushauri wangu ni hivi,mababa kama hawa wanatakiwa kuchukuliwa hatua za kisheria, ili iwe ni fundisho,…ndio maana mimi nataka tushirikiane na wewe kwa hilo,…sasa leo nataka tuanze kwa kufanya jambo moja muhimu, naona muda umekwenda …’akatulia huku akiangalia saa yake, halafu akasema;

‘Najua leo mama harudi mapema na mzee mwenyewe nimemuacha kwenye kesi, kwahiyo tuna muda kidogo umebakia naweza kufanya jambo ambalo litatusaidia, ili tuweze kukusanya ushahidi….nitapambana na huyo baba….na utakuwa huru, …lakini sitaweza kufanikiwa hili kama utakuwa unanificha jambo….’akasema na kumwangali yule binti.

‘Unataka tufanye nini maana ninavyomuogopa yule mzee, sijui kwanini….sikujakuficha kitu, ndivyo ilivyokuwa hivyo….’akasema.

‘Kuanzia sasa usimuogope, wewe mpe heshima yake tu kama baba yako, na kama atataka kukufanyia hivyo hakikisha unapigana naye, piga ukulele, nitakupa simu  uifiche kabisa, akitokea kukufanyia hivyo,  nipigie haraka, hata hivyo kuna kitu nataka nikifanye humu ndani ingawaje ni hatari kidogo…..lakini sina jinsi,…’akasema huku akiwa kashikilia kitufe kidogo mkononi.

‘Ni nini hiyo….?’ Akauliza huyo binti.

‘Wewe usitake kujue mengi, yatakutia wasiwasi bure, hayo niachie mimi, wewe nifungulie huo mlango wa chumba cha makitaba cha mzee, najua bado una ufunguo wake,au sio….?’ Akauliza.

‘Ndio upo kule juu ya kabati, huwa nautumia tu anapokuwepo, ngoja nikauangalie….’akasema na kuingia ndani kwenye chumba kikubwa cha weney nyumba. Baadaye akaja na kusema tayari.

‘Sasa wewe kakae nje mlangoni, hakikisha kuwa  ukiona dalili yam zee au mama kuja nipe ishara….’akasema.

‘Lakini mimi naogopa dada…’akaanza kulalamika

‘Ukiwa na mimi usiogope, wewe fanya nilivyokuambia sawa…hili nalifanya kwa jaili yako, ….mengine tutajua mbele kwa mbele, sasa hivi nabeba dhamana hiyo usijali….’akasema wakili mwanadada, na kuingia huko ndani.

*******
Sehemu inayofuata itakuwa hivi.....

Huko kwenye mahakama alipo wakili mkuu wa kitengo cha sheria kesi aliyokuwa akiisimamia ikaahirishwa, na wakili mkuu wa kitengo cha sheria, akakumbuka kitu, alikumbuka kuwa alipoondoka nyumbani hakufunga kabati lake ambapo huweka vitu vyake vya siri, na anavyojua yule binti wao wa kazi  anaweza akingia kufanya usafi, licha ya kuwa alishamwambia kuwa awe anaingia humo akiwepo tu, lakini moyo ulikuwa ukishauri arudi nyumbani akalifunge hilo kabati kwanza....

‘Kwanza najua mke wango hayupo ana semina mapaka usiku, ngoja nifike nyumbani,kabla sijafika huko nipate chupa moja tu ya kunichangamsha,..’akasema na kupitia sehemu akapata chupa moja, na ikawa sio moja tena, mbili, tatu, na baadaye akajiona yupo tayarai kuondoka.

'Sasa nipo tayari, ...nikifika nyumbani nitajua nini cha kufanya,....aah, mimi mwanaume bwana,naogopa nini,eti, atanishitaki kazini,.....na ashitaki.nikifukuzwa kazii na yeye atapata nini....tutaona huko mbele kwambele...…na kabla wazo hilo halijajiweka sawa kichwani; mara simu yake ikaita.

Aliipokea ile simu huku akikunja uso alipoona ni moja ya watu wake waliopo huko hospitalini, na aliyempigia ni nesi rafiki yake, akasikiliza kwa makini na kumwambia;

‘Kwahiyo keshazindukana,..na anaweza kuongea?’ akauliza na alipojibiwa akaongeza gari mwendo na kumwambia huyo nesi

‘Hakikisha haongee na mtu yoyote kabla yangu…nafika nyumbani mara moja, nitakuja huko..’akasema kwa hasira.

NB: Mambo yanaanza kujikoroga, hapa hata mimi nachanganyikiwa nilimuangalia huyu msimuliaji na kutaka kumuuliza mbona hicho ni kisa kingine kipya,…na yeye akahisi hivyo nakusema, ‘

‘Hicho sio kisa kingine ila ni mnyumbulIko ambao utakuja kufichua siri kubwa katika mfululizo wa matatizo yaliyomkuta’

Haya ….tuzidi kuwepo, kama mumechoka semeni, tuanze kisa kingine kipya, au mambo mengine …

WAZO LA LEO: Ukiwa na uwezo hebu jaribu kuwakumbuka hawa watoto wanaoitwa watoto wa mitaani, najiuliza,  hivi  kweli hakuna matajiri wenye uwezo wa kuwasaidia hawa watoto, …najua wapo lakini hatujali hilo, kinachonishangaza ni kuwa wapo hawo matajiri wanafika hata kwenye yumba za ibada na kusikia wakiambiwa wawasaidie mayatima, masikini…lakini akitoka hapo keshasahau. 

Jamani kusaidia mayatima, au  msikini, au wale wasiojiweza ni amri ya mungu, kwasababu wao hawakupenda iwe hivyo.....tukumbuke kuwa ... HUJAFA HUJAUMBIKA.


Ni mimi: emu-three

Thursday, May 24, 2012

Hujafa hujaumbika-40



‘Msomali, unahitajika kuna mgeni wako…’ nikasikia nikiitwa, nikainuka haraka, nikijua kuwa mwadada wakili kesharudi, lakini cha ajabu nilikutana na mtu mwingine tofauti,..mtu ambaye sikutegemea kabisa kuwa nitakutana naye, .

‘Tangu ufarakane na familia kwa ajili ya mwanamke wako, nimekuwa sipati uzingizi, hata safari ya kuja huku sikuitarajia, na hata sikuwaambia wazazi wako kuwa nakuja kwako, nimeagana kuwa nafuatilia mambo yangu ya kibiashara, najua kama ningewaambia kuwa nakuja kwako, wangelipinga kwa nguvu zao zote,….’akasema .

Niliposikia hivyo moyo wangu uliniuma sana, sikutaka iwe hivyo, kwani kwa ujumla nawapenda sana wazazi wangu, na sikutajia kuwa itafika muda, niwe mbali nao, nikaimana chini huku moyoni nikitubu na kuomba kwa mola anijalia nitoke pale nakiwaone. Nikasema;

‘Na mimi sikutaka kuwasumbua kuhusiana na maswali yangu, ambayo najua hamsitahili kuhusishwa, haya nimejitakia mwenyewe, naona nipambane nayo mwenyewe…hadi mwisho wake, sioni kuwa itashindikana, lakini , nataka nionane na wazazi wangu, …’nikasema.

‘Unalosema linaweza kuwa sawa, lakini ukumbuke kuwa kuna wazazi wako wanasononeka, na wazazi kwa mtoto haifutiki kama wangali hai, kila siku inayopita bilakusikia lolote kutoka kwako, ndivyo uanvyozidi kuwaumiza,..ujue, kila unalopambana nalo wanalihisi mwili, mwao, ukiwa na matatizo kuna hisia zinawajia wanaju tu sasa mwanetu yupo pabaya….na hili nimeliona kwa dada yangu, hana raha kabisa…’

Hapo akawa kaniuliza kweli, nilijaribu kumuwaza mama yangu, najua jinsi gani anavyonipenda,na nilitaka nifike kwake nikiwa na zawadi ya aina yake, nakumbuka siku moja aliniambi kuwa, zawadi kubwa ninayotaka kutoka kwako ni mjukuu…sasa mjukuu nitampataje kwa halai kama hii,….nakasema kwa sauti ya huzuni….

‘Nimkuelewa sana mjomba, ndio maana sitaki kabisa wajue haya yanayonisibu, mategemeo yangu ni kuwa nikishajiweka sawa nitakuja nikiwa na hali nzuri ili niwape faraja, lakini kwa sasa nikija nitazidi kuwaumiza, hebu fikiria wamenisomesha hadi nje, nini nimewapatia zaidi ya haya matatizo….ndio maana nashindwa kwenda kuonana nao uso kwa uso nikiwa katika halai kama hii…’nikasema huku nikitamani kulia.

‘Sikiliza mjomba, haya ni maisha ya kawaida, na ukizaliwa duniani lazima ujue kuna shida na raha, lakini vyovyote iwavyo, hustahili kuikwepa jamii yako, ….umekosea ..inabidi ukubali hilo, na ukiwakosea wazazi wako, kinachotakiwa ni kwenda kuwaomba msahamaha, wao hawana tatizo na wewe. Ni wewe tu ufike usema wazazi wangu samhanini, …ukipata Baraka zao, hutaamini, kila kitu kitakunyookea…..’akasema mjomba.

‘Ndivyo nilivyopanga, …lakini sio katika hali kama hii, nikuambie mjomba, ilibakia kidogo tu nije huku,lakini huwezi amini, kila nikijipanaga, linatokea tatizo kubwa la kunizuia, kama unavyoona sasa, mimi sina kosa, nimejitolea tu kwa tatizo ambalo nikikusimulia utasema natunga uwongo, lakini mungu ndiye anajua …..’nikasema na mjomba akatabasamu na kusema;

‘Unajua mimi sio mtoto mdogo, najua mengi, na mengi nimeyapitia, ila mimi sikuwahi kufungwa jela, wewe umevuka mpaka, najua nini kinakusumbua, na hapo ulipofikia nasjua kabisa umeshajifunza, cha muhimu ni kutafuta mke mwema, ukatulai naye, …..’akasema mjomba.

‘Mke mwema,mmh, sasa hivi sipapatiki tena, na itachukau muda mpaka niamua kuwa sasa mke wangu ni huyu, …..kwasababu nimeshaumwa na nyoka…’nikasema na mjomba akanikatisha an kuniuliza.

‘Kwani mkeo imekuwaje…?’ akaniuliza.

‘Kwani huna taarifa, mbona keshafariki dunia…..’nikasema na mjomba akaniangalia usoni kwa mshangao.

‘Lini, …mbona hilo kwangu ni geni, kwanini kijijini hawajui maana familia yao nilikutana nayo, na sikusikia wakiliongela hilo, maajabu kabisa na wewe ukakaa kimiya hukutaka hata kutuambia, nyie watoto mbona mnapotea , sio vyema namna hiyo….’akalalamika mjomba.

‘Mjomba, yeye nasikia aliwaambia marafiki zake kuwa akifa, hatakai kabisa apelekwe huuko kijijini na hata huyo ambaye aliyempokea aliaambiwa kabisa, kama akifa hata taarifa zake zisipelekwe huko kijijini,….’nikamwambia mjomba.

‘Kwani kafa lini?’ akauliza mjomba.

‘Mbona miezi mitatu imeshapita…..’nikasema na mjomba akaniangalia kwa muda halafu aksema;


‘Sio kweli….’akasema na kuangalia juu.

‘Kwanini unasema sio kweli….?’nikamuuliza.

‘Ingelikuwa ni wiki moja iliyopita ningekubaliana na hilo, lakini miezi, ….hapana ,lakini ngoja nisiseme mengi, maana dunia hii ina mambo, hayo uliyoniambia yananishngaza kabisa, ….hapana, haiwezekani, na kwanini iwe hivyo….’akasema mjomba na mimi sikumuellewa kabisa.

‘Mjomba unataka kusema nini, uliwahi kukutana na huyo mwanamke karibuni, maana hapo unanichanganya.

‘Sikiliza mjomba, inaonekana wewe umetumbukizwa katika mambo ya viini macho,maana sizani kuwa ni msukule, au ni jinamizi, …ila kwa vile na mimi sina uhakika na hilo, ngoja nikirudi kijijini nitakwenda kuoanana na wazazi waa huyo mkeo, nijue zaidi, lakini nikuambai kitu, msiba ukitokea kwa mtu yoyote wa aple kijijini, wte tutajua,….hilo la mke, nalisikia toka kwako leo hii…lakini sina ushahidi zaidi….’akasema mjomba. Na mara akaja askari kumwambia mjomba kuwa muda umekwsiha.

‘Mjomba, ….umeniweka njia panda, naomba lolote utakalolipata huko nijulisha mapema, maana hujanielewesha ….ama kwa hili langu litakwisha, ni jambo dogo tu,….usije ukawaambia wazazi wangu, …’nikasemana na mjomba alionekana kuchanganyikiwa  na taarifa niliyompa, akaniangali tu kwa macho  yaliyojaa huzuni, akageuka na kuondoka.

Ni siku iliyokuwa ngumu sana kwangu, kuja kwa mjomba kuliniongezea simanzi, na maongezi yetu yalinifanya nisiwe na amani, sijua mjomba ana maana gani, ….lakini nikaona hilo alilosema mjomba haliwezekani, maana mimi mwenyewe nilishuhudia mwili wa Kimwana ukizikwa, ingwaje ni kwa siri,….

‘Hapo mjomba kachemka, na huenda wazazi wake hawajui kabisa,…..’nikajikuta nikisema.

Moyoni nikaahidi kuwa nikitoka hapo ni moja kwa moja kwenda kuwaona wazazi wangu, nilijiona mkosaji na licha ya kujua nimekosa bado nimekuwa mkaidi….na kuja kwa mjomba kulikuwa kama nuru fulani imeniingia akilini,….

Nikawaza kuhusu tatizo lililopo mbele yangu na kumkumbuka wakili mwanadada, kwakweli huyo dada nilishamuweka kama mmoja wa ndugu zangu, amekuwa karibu sana na mimi na amejaribu kunisoma na kunijua,kwakweli siku mbili hizi alizoondoka bila kuwa karibu naye nimekuwa kama mkiwa,…

‘Natamani arudi haraka, ili nijue nini kinaendelea huko ,maana bila yeye nashindwa kujua hili tatizo limefika wapi, na lini dhamana yangu itakubaliwa, na je huyo mgonjwa anaendeleaje, na nitapata wapi nafasi ya kumuoana…’nikajikuta nikiongea mwenyewe kama punguani.

*******

Mkuu alikuwa kasimama ofisini kwake na mara akaingia wakili mkuu wa  kitengo cha sheria, mkuu alipomuona akashikwa an mshangao, na haraka akasimama na ule mshangao ukaabdilika na kuwa furaha, haraka akamwendea ,wakashikana mkono, akamwangalia kwa makini na halafu akamuuliza hali yake.

‘Kwakweli najisikia nafuu kidogo,…na nimeona ili nipone kabisa, nahitjika kuchapa kazi, nikikalala tu, nitaumia,…nilichogundua ni kuwa kila nikipta shinikizo litakalo nipa wasiwasi, ndipo nahisi maumivu, na hili linaniogopesha kwani kazi zetu hizi hazikosi misuko suko,..nashindwa hata nifanye nini….lakini kwa sasa nasema mbele kwa mbele...’akasema wakili.

‘Afya ni bota kuliko chochote, kazi ipo, na ukiwepo au usipokuwepo itafanyika tu, wewe angalai afya yako kwanza, cha muhimu ni kuhakikisha kumwa umepona kabisa, ili ukija ofisini uwe na afya ya kufanaya kazi….’akasema mkuu.

‘Ndio najua hilo, lakini …kinga ni bora kuliko tiba, nimeshajijua wapi niliteleza, na ndio maana najaribu kufukia mashimo, lakini kila ukifukia, ukigeuka unakuta limefukuliwa…..nimefika ofisini nimekutana na mambo mengi hayajafanyiwa kazi, na sasa kesi mbili zimekuja, bado hazijawekwa sawa, haya mimi siyataki, …..halafi nikuulize…kwani huyo mwanadada  aliyepigwa risasi anaendeleaje?’ akauliza.

‘Kwakweli bado hajawa na kauli,walimfanyia upasuaji na kutoa ile risasi, na wanasema kuna athari zilitokea kutokana na hiyo risasi, na mengi yanategemea majaliwa  ya mungu….’aksema mkuu.

‘Kwahiyo mpaka sasa hatuwezi kuiita kesi ya mauaji,….na huyu mshukiwa naona bado yupo rumande, na kiutaratibu anatakiwa kupelekwa gerezani, haiwezekaani akabakia hapo mahabusu kwa muda wote huu, hili mumelifikiriaje?’ akasema wakili.

‘Ndivyo ilivyo, lakini kila ukiangalia ushahidi ulivyo, tunashinndwa kuamua….ndio vipengele vingi vinamuweka matatani, lakini ukiangaia kwa namna nyingine ni janga limetokea na kwa vile hakuna mshukiwa mwingine yeye anonekana kama ndiye mkosaji….’akasema mkuu.

‘Mimi nimesoma kesi nzima, na kila kitu kipo wazi, ….inabidi uchunguzi wa kina ufanyike na kama yeye anahusika awe ni fundisho maana hili ni tatizo, na kwa vile mimi nimeliona kwa vitendo, nataka tupambane nalo na kuhakikisha wote wanahukumiwa….nataka iwe fundisho kwa hawa watu, ndio maana nimejikongoja leo kukuamabia kuwa sasa nipo tayari kuingia mahakamani kupambana  na hawa watu…’akasema wakili.

‘Sawa, lakini cha muhimu ni afya yako ….’akasema mkuu.

‘Na dada wakili yupo wapi, sijamuona siku mbili hizi maaan alikuwa mara kwa mara akinitembelea, lakini skuku mbili kawa kimiya, nimepga simu yake haipatikani, yupo wapi….?’ Akauliza.

‘Hivi sijakuambia, amekwenda Kenya,….’akasema mkuu.

‘Amekwenda Kenya kufanya nini….?’ Akauliza kwa mshangao, na kabla mkuu hajajibu kitu akasema kwa hasira.

‘Huyu mwanammke vipi….anaacha kesi muhimu anakwenda kustarehe,haya ndio matatizo ya hawa wanawake, ukiondoka kidogo tu, ukirudi mambo yanakwenda shanghala baghala…sasa kaondoka sina hata taarifa….hizi ni taratibu za kazi kweli ’akasema kwa hasira.

‘Ukiondoka ofisini, wapo watu wanaendelea nayo, ….hajaenda kustarehe kama unavyodai ni moja ya kufutilia maswala ya hii kesi,…ina maana kila hatua ya kila aianchokifanya natakiwa akuambie, ujue wewe ulikuwa likizo ya ugonjwa na tuliona sio vyema kukushiriksha kwenye hizi kesi, ili upambane na afya yako kwanza.’akasema mkuu.

‘Mimi ninachojiuliza, kesi hii inahusianaje na huko Kenya, kama ni kuhusu yule mama Docta, tulishaona kuwa hana hatia, na hahusiki tena, na mambo yanayotokea hapa kwa sasa hayamuhusu,..kwasababu unaona hayupo , lakini mambo kama hayo yanatendeka…vifo hivi ni majanga haya ni ya watu wa humu humu….’akasema wakili akiangalia saa yake.

‘Alichopanga yeye ni kuwa antaka kuona chimbuko la haya matatizo, maana kila ukifuatilia unagundua kuwa mambo mengi yameanzia kwa huyo mama Docta, wahusika wengi walikuwa wafanyakazi wake,….sasa kaona kuwa kuna haja ya kukutana naye aone kwanini imetokea hivyo…’akasema mkuu.

‘Hainiingii akilini, haiji kabisa,…..labda kama ana mambo yake mengine, sio mbaya, hata hivyo nilishamuona kuwa anataka kujitoa serikalini awe wakili wakujitegemea, ndio maana anakusanya marupurupu apate msingi….au kaenda kutafuta wafadhili,…unafikiri mchezo kuwa na ofisi yako mwenyewe,…..’akasema huyu wakili.

‘Lakini mimi sikupenda wazo lake la kujitoa serikalini ni wakili mnzuri sana, hasa inapofikia maswala ya kesi za kifamilia …ana hekima ya kuzishughulikia, mara nyingi yeye anaangalia kwa undani na matokeo yake tunakuja kugundua tatizo ambalo usingeligundu akirahisi…’akasema mkuu.

‘Sawa aende huko, mimi nitabakia serikalini na nitapambana na uhalifu kwa nguvu zangu zote ,mimi ni mwanaume bwana,….na kama ikibidi nitapambana naye kwenye ulingo wa mahakama …maana akiwa wakili wa kujitegemea itafika muda tutakutana mahakamani….’akasema huku akijiandaa kuondoka.

‘Sikutarajia kusikia kauli hiyo toka kwako, maana nilitaka nyie muwe pamoja,badala ya kutofautiana na kujenga ushindani,…kesi hizi zilizofuatana zinahitaji mshikamano, ukumbuke kuna mauaji bado hatujayatatua , sasa limezuka hili jingine, hatujui kama itaishaje, tunaomba huyo mgonjwa apone, akipona atatusaidia sana, na asipopona tutajikuta kwenye kesi nyingine ya mauaji,…kesi zinapandana..’akasema mkuu..

`Yote sawa tutayamaliza tu,….nitahakikisha yanakwisha yote ndani ya ulingo wa mahakama, na wote wanaohusika watapambana na mkono wa sheria,….wamejitakia wenyewe….na huyu dada wakili akirudi, kama atapitia hapa kwako naomba umwambie aje ofisini haraka, ….’akasema na kuondoka.

*****

Wakili mwanadada altua uwanja wa ndege wa Dar-es-salaam, huku akiwa hajui afanyeje ili aeleweke, kwani alishafikia uamuazi wa kuwa wakili wa kujitegemea, na taratibu za kuanzisha ofisi yake zimeshakamilika, lakini ofisini hawataki kumruhusu. Akiwa anatafakari hayo na mengi aliyoyagundua huko alipokwenda, aliona jambo jema ni kuhakikisha hizo kesi zilizopo mbele yake zimekwisha.

Kichwani alikuwa kabeba mengi ambayo anahisi wengi hawataamini,na ili waamini inahitajika kuwa na ushahidi wa kutosha , mapaka muda huo hakuwa na ushahidi wa kimahakama, na ili uweze kuishawishi mahakama inabidi kutafuta vielelezo, na mashahidi ,ambao bado hajakubaliana nao, ili waje kuthibitisha hayo,…mwenyewe alijikuta akiwa kwenye mshangao, akasema kimoyomoyo, siku itafika na ukweli utadhihiri.

Alipofika nyumbani kwake aliwasha simu yake ya mezani ambayo aliitegesha kwa ajili ya kupokea ujumbe wa sauti, na mara akakutna na mfulululizo wa ujumbe ukitoka kwa wakili mkuu wa kitengo chao cha sheria, na kwa ujumla alikuwa akitaka wakutane haraka iwezekanavyo.

‘Kumbe huyu mtu keshapona, …na huu ndio muda wangu wa kujiandaa kuachana na kitengo chao….’akasema huku akijipumzisha, lakini kila alipjaribu kutafuta angalau usingizi, akajiukuta akili haitulii, akainuka pale kitandani na kwenda kuchukua mazoezi kidogo..

Wazo likamjia kuwa kwanza akaonane na mkuu wa kituo cha polisi, alitaka apate muda aongee naye, , huyi ndiye mtu pekee aliyekuwa akimwamini kwa muda huo, na alimuhitaji ili aweze kufuatilia baadhi ya mambo, na wazo hilo lilipomjia akilini, akajiandaa kuondoka . Alisoma baadhi ya ujumbe kwenye hiyo simu yake, na mara akaona ujumbe usio na jina,…ulisema;

‘Unakumbuka nilikutumia vitu,ili uvifanyie kazi,je umefikia wapi…?’  akajiuliza ni vitu gani hivyo,….na mstari wa mwisho ulisema, `naomba ukishavifanyia kazi unirudishie mwenyewe, na kama umeshindwa naomba unijulishe maana huyu mtu haeleweki….’ Akakumbuka ni vitu gani, na hapo akasema kimoyo moyo,

‘Sijashindwa bado, natafuta muda muafaka…’

Alipoona hakuna zaidi akatoka hapo nyumbani kwake na kuelekea kwa mkuu wa kituo chao cha usalama, wao wanamtambua kwa jina la Mkuu, na alipofika akamkuta akiwa kwenye vikao na vijana wake, akasubiri. 
Na mkuu alipomuona akawaondoa vijana wake na kumwita wakili huyu mwanadada aingie ofisini kwake, na kuanza kumuhoji kwa kusema;

Wakili mwanadada akiwa kavaa miwani yake, akakaa kwenye kiti, na mkono akaupeleka kidevuni, kidole kimoja kikawa kimeshika shavuni, na kuwangalia moja kwa moja usoni Mkuu ambaye alionekana mwenye hraka, Mkuu akasema,

‘Vipi umesharuditoka huko Kenya, kuna habari gani huko, maana mwenzako anakusubiri kwa hamu sana, na alitoa maagizo kuwa ukija tu, kwanza umuone yeye…na swali kubwa ni kwanini uliondoka bila kumpa taarifa, na kuna kitu gani muhimu kilichokupeleka huko kama sio starehe…..’akasema mkuu.

‘Kwa mpangilio wangu kwanza nataka nikuone wewe, kwasababu kuna mambo yanahitaji ufuatiliaji wako, naomba tuongee kwanza kuhusu hilo kama una nafasi,kama huna tupange siku nyingine…’akasema mwanadada.

‘Haya nipe kwanza taarifa zile zilizokupeleka huko....kwa haraka, kwa ujumla kwasasa hivi sina  nafasi ya maongezi marefu, ratiba hainiruhusu kabisa,  je ulifanikiwa…?’akasema mkuu.

‘Kama huna huo muda ni bora tusubiri baadaye,…kwani maongezi haya hayahitaji uharaka, ila ynahitaji umakini wa kutafakari, ….mmh,  ila jambo ambalo nataka kukutonya ni kuwa nataka kuanza mikakati ya kuachana na kazi hizi za serikalini,  nilishakuambia hilo, lakini  muda kamili wa kuachana na hiyo ofisi nilikuwa sijakuambi, nataka wiki hii nimalizane na nyie, ili nipate muda wa kujiandaa kwa ofisi yangu kama wakili wa kujitegemea….’akasema.

‘Kwanini umeamua kufanya haraka hivi,….?’ Akauliza.

‘Kwasababu nikiwa ndani ya hicho kitengo sitaweza kufanya kazi yangu vyema, naona kuna siasa nyingi na kulindani kwingi, na ubinafsi mwingi, hili linanikwaza mimi kutimiza malengo yangu ya kupambana na watu wanaotumia madaraka yao vibaya, na nia yangu kubwa sio huko, ….sio kisiasa, nikisema madaraka vibaya usije ukazania nataka kujiunga na mambo y akisiasa, hapana, …..mimi lengo langu nataka nitimize ndoto yangu ya kuwa wakili wa kujitegemea wa kuwasaidia akina mama…’akasema wakili mwanadada.

‘Kwani huko Kenya ndipo kwenye wafadhili wako, maana hilo wazo limefumuka baaada ya kurudi hiyo safari yako, ….?’ Akauliza.

‘Hapana sina wafadhili….naanzisha kwa nguvu zangu mwenyewe, nilichojifunza huko, ni kuona wenzangu wameweza, na wapombali sana,  na nilipoongea nao nikagundua kuwa inawezekana , na haihitaji mtaji mkubwa, ….

‘Mimi naona utakuwa unakimbia vita, na kama vile mtu anakimbilia nchi ya jirani, kwa vilencho yake ina vita, na wakati huo yeye ni askari,….nakushauri kwanza hakikisha umemaliza hizo kesi kabla hujaondoka,ili uilinde hadhi na heshima yako,….na hilo la kuacha kazi serikalini na kuwa wakili wa kujitegemea, hakuna anayekukatza, ila ni vyema ukuafuata utaratibu….’akasema mkuu.

‘Utaratibu upi tena mkuu, mimi nilishamalzia mkataba wangu  wa ajira, na niliombwa nisaidie tu baadhi ya kazi kwa vile huyo mwenzangu alikuwa anaumwa,na sasa keshapona, au bado anaumwa….?’ Akauliza mwanadada.

‘Kasema keshapona na ana motomoto wa kuhakikisha hizo kesi zimekwisha haraka iwezekanavyo, nakwa ujumla amekuwa mbogo,ofisini kwake watu wanachapakazi sio mchezi, kwakweli ni mtendaji mzuri….’akasema mkuu.

‘Mimi silipingi hilo kuwa huyo jamaa ni mtendaji mzuri, lakini kuna mambo mimi nay eye hatuivani, na Ili kumaliza haya matatizo nahitajika niwe huru, na nilishajifunza kuwa nikifanya kazi na huyu mwenzangu, nakwazika,huwa mara nyingi ana tabia ya kunizarau kama mwanamke,..ana tabia ya mfumo dume hata kweney kazi, mimi sipendi huo mtindo, kazi ni kazi, na mambo ya milana desturo kuwa mke hawezi hili, asiwe msemaji mkuu, sijui…..hapana hayo hayana nafasi kwangu, na ili niweze kumuonyesha kuwa sivyo hivyo anafofikiria ngoja..….

Mara simu ikalia na mkuu akaipokea na kuiskiliza,….

‘Unajua nilishasahu,natakiwa kwenda kuonana na mwenzako kwa ajili ya kukamilisha maandalizi ya hii kesi mpya, ndio huyo kanipigia simu, nakuambia amekuja na moto mkali, ….hata mimi nimefurahia kuwa kazi zinakwenda mbio mbio,sipendi kuwa na mlolongo wa kesi nyingi katika kituo chetu, kaniambia kuwa yeye yupo tayari, ….kwahiyo tunaweza tukafuatana, au unahitaji kupumzika kidogo….?’akasema mkuu.

‘Sawa tunaweza kufuatana, lakini msimamo wangu ndio huo…nafikiri umenielewa  na kesho nahitaji tuwe pamoja, …..’akasema.

‘Tutaongea huko,….lakini kuna nini kikubwa umegundua huko, hujaniambia bado..? akauliza mkuu.

‘Nimegundua mengi sana, ambayo kama nitafanikiwa kupata huo ushahidi ,basi hali itabadikilka kabisa, na kwakweli nihitaji nguvu za ziada, ndio maana nimesema nikiwa humo ndani ya kitengo chetu sitaweza kufanikiwa,….kinachonikwaza ni hiz kesi mbili ambazo zipo mhakamani, na nipo uapnde ambapo sitaweza kupambana vyema …..nataka kama ikiwezekana nijitoe upande huo niwe uapnde wa kujitetea…’akasema wakili mwanadada.

‘Hapo mimi sijakuelewa, inabidi unipe muda, tuongeee vyema, maana huko ni kukimbia kupambana na wahalifu na kutaka kukaa upende wao, hainiingii akilini…’akasema mkuu.

‘Vipi kuhusu hali ya yule mgonjwa….?’ Akauliza wakili mwanadada.

‘Hali yake bado haijawa njema…na jana alizindukana akaendeela kumtaja Msomali…

‘Sasa kwanini hamkumkutanisha na huyo Msomali?’ akauliza wakili dada.

‘Wakili wetu aliweka pingamizi kuwa asiruhusiwe kumuona mpaka na yeye awepo, na mudahuo alipozindukana huyo wakili alikuwa mahakamani kwenye kesi nyingine, na tusingelwieza kumtoa, ikabidi tuahirishe hilo zoezi…’akasema .

‘Kwahiyo huyo mgonjwa sasa keshazindukana….?’ Akauliza wakili

‘Alizindukana hiyo mara moja, na alikaa kwa muda, na baadaye akapoteza fahamu tena….’akasema mkuu.

‘Kwa mtizamo huo natamani ikiwezekaan hata leo, niwe wakili wa kujitegemea, ili niweze kuifanyia kazi hii haraka, …..maana sio mantiki, ya kumzuia huyo jamaa asionane na huyo mgonjwa, wakili wetu,ni mchapakazi mahiri, lakini huwa akiang’ang’ania kitu chake huwezi kumbadili mawazo,..mimi naomba ufanya kilaiwezekanavyo Msomali akutane na huyo mwanadada, na mimi nitajitahidi niwepo,….’akasema wakili mwanadada.
‘Sawa tuombe kesho huyo mgonjwa awe nahali nzuri…’akasema mkuu


NB: Kila hatua ni kwenda mbele, sikutarajia hiki kisa kitafikia huku, lakini kisa kama kisa hakikosi mkasa, naombe tuwe pamoja, tu....tusichoke,....


WAZO LALEO: Kuna mtu mwema mmoja aliniambia kuwa kama ingeliwezekana, ilitakiwa kila ukipata chochote, katika riziki yako, ulitakiwa umkabidhi mzazi wako yeye ndiye akugaie matumizi yako. Lengo lake  hapa ililikuwa kunionyesha umuhimu wa wazazi. 
 Tuwakumbukeni wazazi ,tuwajali na tusikae mwezi,miezi bila kuwajulia hali na kila riziki unayopata hata kama kidogo namna gani, ukumbuke kwa ndani yake kuna sehemu ya mzazi wako, tuwajali wazazi wetu kwa kila hali, kwani ni nani kama wazazi wetu. 
Ni mimi: emu-three

Wednesday, May 23, 2012

Hujafa hujaumbika-39



 Nilikuwa nimekaa kwenye kona ya kile chumba cha mahabusu, huku nimejikunja kama mkiwa. Kwakweli ilikuwa imeniuma na moyoni nilikuwa nimekasirika sana,...hapo nilikuwa mahabusu tu, kichwani mwangi nilikuwa nimepanga kuwa nitagoma kabisa kupelekwa huko Segerea au Ukonga, sikubali kupelekwa tena huko.

 Kwa ujumla sikuamini kuwa nimefikishwa mahala kama hapa tena, hata baada ya kuwa mwangalifu na maswala ya kuvunja sheria, lakini hujafa hujaumbika, ....nikiwa nimekunjata nikawa namumimba mungu, nisije nikapelekwa huko jela,…iliniuma sana kuona kuwa dunia hii haina wema,yaani kujitolea kwangu huko,kuwafahamisha polisi kuhusu hilo tukio ndio ninashikiliwa eti kwa kuisadia polisi.

‘Usijali hizi ni taratibu za kawaida, utatolewa, na wamekushikilia kwa sababu ya maelezo yako uliyowapa, ilinakuweka mahali ambapo yoyote angeliweza kukuhisi kuwa uanahusika. Na linapotokea jambo kama hili la kesi za jinai, kama hii, ukatiliwa mashaka ni lazima wakushikilie kwa ajili ya kuisaidia polisi.

‘Kwa vipi wanahisi ni mimi na maelezo gani niliyotoa yanayoniweka kwenye mashaka..?’ nikamuuliza.

‘Ukumbuke kuwa huyo mtu kauliwa kwa silaha na muuaji anajua kulenga shabaha, wewe alipokuuliza mkuu kuwa unaweza kutumia silaha ulisemaje?’ akamuuliza dada wakili.

‘Nilimuambia ukweli,…nilimwambia ndio najua kutumia silaha,maana niliwahi kupitia mujibu wa sheria, kule tunafundishwa yote, nakumbuka tulipopelekwa uchaka, huko tulifundishwa mbinu zote za kivita na kwenye shabaha nilikuwa mtu wa kwanza, sikukosa hata moja…..niliizoea silaha utafikiri nilizaliwa nayo….’nikasema kwa majisifu.

‘Sasa hayo maelezo yako yanakuweka pabaya, sio kwamba ni vibaya kusema ukweli, lakini kwa fikira zao, na tetesi walizo nazo polisi na hata kwa mtizamo wa mtu yoyote kwa haraka haraka, muuaji alikuwa anajua vyema kulenga shabaha….na wewe unajua kulenga vyema shabaha. Na je alipokuuliza swali, kuwa ulipoingia humu ndani ulifanyeje, ulimjibu vipi…?’ akaniuliza dada wakili.

‘Unajua kuna mambo mengine unajifunza kutokana na uzoefu, mimi kwa ajili ya kujindaa kuja kufanya kazi kwenye ofisi yako mpya mwakani,nimekuwa nikihudhuria mafunzo ya sheria na upelelezi, na huko nimejifunza mambo mengi ya kujihami na kujilinda,….kuna sehemu tumefundishwa kuwa unapofika kwenye tukio unalolitilia mashaka….’nikatulia kidogo pale nilipomuona dada wakili akionyesha uso wa furaha.

‘Endela kuongea, mbona unakatisha ameno,…nimetabasamu kwasababu ya kusikia hivyo, kujiandaa kwa ajili ya ofisi yangu,…., safi kabisa,nashukuru kusikia hivyo, haya niambie umejifunza nini huko ambacho umekitumia kwenye hili tukio?’ akaniuliza.

‘Unapofika sehemu yenye mashaka, ni vyema ukachunga kuacha alama za vidole, sasa mimi nilipofika hapo kweny hiyo nyumba,…niliingiwa na wasiwasi, hasa pale nilipogonga mlango na kuona kupo kimiya, nilichofanya ni kuvaa soksi,…unajua nilichofanya ni kuvua soksi zangu za miguuni, na kuzivaa mkononi, kuogopa kuacha alama za vidole….’nikasema bila wasi wasi.

‘Hapo unafikiri polisi wataamini kuwa ulifanya hivyo kwa ajili ya kujihami,…. swali kubwa kwao, ni je ulijuaje kuwa kuna tatizo, mpaka uvae hizo soksi,….lazima hapo watakutilia mashaka. Na je walipokuuliza kuwa ulipoingia ndani ulifanya nini ulisemaje?’ akaniuliza swali jingine.

‘Niliwaambia kuwa nilipoingia ndani,cha kwanzakuona ni tundu kwenye kiyoo, na kuvunjika na pale chini kuonekana vipande vya kiyoo, …na baadaye nikagundua kuwa kuna mtu yupo sakafuni,….kama nilivyowaelezea mwanzoni, na pia huyu mtu alikuwa akanionyesha kwa kidole kule kwenye kabati la vitabu,….sikuona kitu,….ila wakati nasubiri polisi waje, nikaanza kupekua huko kwenye kabati aliponionyeshea, …na hapo nikagundua kibksi, chenye jina langu, labda ndicho alichokuwa akinionyeshea, na kilikuwa kimeandikwa  jina langu,….’nikasema.

‘Hapo pia wamekutiliwa mashaka, maana inaonyesha kulikuwa na kitu wewe unakitafuta, hasa hilo boksi, ulipomuona yupo kwenye hali mbaya, au ….lengo lako lilikuwa ni hilo boksi, kwahiyo ukamtishia kuwa akuonyeshe hilo boksi au umulizie….kwa ujumla wao wanahisi kuwa kunajambo, hapo kati kati, kati yako na huyu mwanadada na hilo boksi, na wanahisi kuwa kwenye hicho kiboksi kuna kitu muhimu sana kwako,bado wanalichunguza….’akasema wakili mwanadada.

‘Lakini ngoja nikuulize swali, kama ungelikuwa wewe seehmu yangu ungelifanyaje, maana tuzungumze katika hali halisi, wewe mtu kakuita uende kwake, na umefika umeikuta hali kama hiyo na zaidi kakuonyeshea hivyo kwa kidole, utasema hapana ngoja mpaka polsi waje…, hata hivyo niligundua vitu ambavyo sikutaka polisi wavione…nikavificha….’nikasema na hapo wakili akashituka.

‘Eti nini….ulificha kitu gani, ..na ole wako polisi wakigundua hilo….’akasema wakili kwa mashaka.

‘Aaah, naogopa hata kusikia kauli hiyo, yaani ningekuambia usiniambie jambo hilo,lakini kwa ajili ya utafiti wangu,inabidi nilijue, lakini….ooh,…..hapana kama inawezekana nipe hivyo vitu nikawakabidhi wenyewe…’akasema wakili mwanadada.

‘Una uhakika kuwa nikikupa utawakabidhi wenyewe, una uhakika kweli na hilo…na nani utampa ambaye unamwamini…ndio huyo wakili wenu, ambaye keshaumwa na nyoka,….na huenda bado yupo mikononi mwa hawo watu kwa kashifa iliyomkuta, …wewe huoni hilo, ….ndio maana anachelea kusimamisa kwenye hizo kesi, bado wanamtishia kuwa ukisimama tutakuumbua, wewe huoni hilo …?’ nikamwambia huku nikimwangalia kwa wasiwasi.

‘Unajua yeye anajua sheria, usimuone hivyo, na wakati mwingine, unaogoap usije ukashindwa kusimamaia haki kwa jambo fulani, inabidi kidogo ukae pembeni, mfano ni kesi ya mkeo, na wewe ni wakili ,hutaweza kuisimamia vyema,…hapo inabidi umpe mtu mwingine aisimamie,….na mambo mengine juu yake ni tuhuma tu,….’akasema na kutulia kama vile anawaza jambo,halafu akasema;

‘Kiutaratibu yeye ndiye anayestahili kupewa hivyo vitu, ujue kwa sasa ndiye  mkuu wetu wa kitengo cha sheria, ….’akasema huku akikunja uso.

‘Siwezi kumpa mtu kama yule,hata huyo mkuu wenu….siwezi siwezi,…., nimekuambia wewe tu kwasababu ni mtu ninayekuamini, vinginevyo ningelikaa kimiya….’nikasema kwa msisitizo.

`Ujue hivyo vitu ulivyochukua ni sehemu ya vitu vya ushahidi,…..sheria hapo itakubana sana,….hutakiwi kuficha kitu chochote kwenye tukio la kesikama hizi , unavuruga ushahidi na utachukuliwa kama mshukiwa muhimu wa hiyo kesi…..’akasema wakili mwanadada.

‘Nalijua hilo, lakini….unakumbuka siku ile Kimwana alipouliwa…..wewe hukuchukua vitu fulani kutoka kwake, hukuchukua simu na saa yake,….mbona hukuikabidhi kama viti muhimu kwenye hiyo kesi…hujakiuka sheria hapo..?’nikamuliza na yeye akaniangalia kwa uso wa wasiwasi,…..

‘Mimi najua kwanini nilifanay hivyo, kisheria….na ningejitetea kisheria, je Wewe?,…. hebu achana na hilo….hata hivyo vilitoweka kiajabu vile vitu, nilichukua nikitaka nimkabidhi mtu ninayemuaminii, sikuwa na uhakika na wale watu waliofika pale na nilishaanza kuwashuku watu kwenye kitengo chetu, kuna watu nilishaanza kuwatilia mashaka,…lakini cha ajabu nilikuta vyote havipo….na hili linaniweka katika hali ngumu, kuwa kuna mtu ndani ya kitengo chetu, anatumiwa,aua anahusika….’akasema wakili mwanadada.

‘Unajua niliviona kwenye hilo boski …..sasa na hiyo simu, halafu vimewekwa kwenye kimfuko cha plastiki kimeandikwa juu Kimwana, ….’akasema.

‘Niliandika mimi hivyo….siku nilipovichukua,….’akasema wakili mwanadada.

‘Oooh,sasa vimefikaje kwa huyu mwanadada, mbona mambo ya ajabu…?’nikauliza kwa mshangao.

‘Ndio maana nsemakuna mtu ndani ya kitengo chetu cha sheria anatumiwa, ….na nimejaribu kila njia nimeshindwa kumgundua, maana vitu kama hivi hutakiwi kukisia tu, unahitajiak uwe na ushahidi uliokamilika,…na mtu kama huyo amejiandaa vya kutosha….’akasema mwanadada na akaniuliz akuna viti gani vingine nilivyovichukua, nikasema;

‘Kuna nakala ya ile picha yangu ya utotoni….na picha kama ile niliyomkuta yule dada aliyeidondosha kule siku ile ,…yule aliyekuwa akinikimbia….na vyote hivyo nimevificha…, pia nilikuta mkanda wa CD’s…ulikuwa na jina langu,…nahisi una mambo yangu,…..mmh, ambayo nahisi ni yale waliyokuwa wakinituma akina Kimwana na mama Docta, nikayafanye kwa manufaa yao,….’nikatulia hapo kidogo nikiwaza jambo.

‘Nikuambie ukweli sikupenda yale mambo yaje kujulikana katika familia yangu, maana wao ndio walionilazimisha, kufanya hayo yaliyopo humo, nikataka kuuharibu pale pale, lakini muda ulikuwa hautoshi,…na cha ajabu nilikuta baadhi ya barua zangu za ujanani, nilizokuwa nikiandikiana na yule msichana wa kijijini…’nikatulia nilipoona wakili mwanadada akiniangalia kwa mshangao.

‘Eti nini, barua za ujanani, ulizokuwa ukimwandikia nani, ….oh, na umeviweka wapi hivyo vitu, kweli nilitakiwa nivione kabala hawajavchukua hawa watu?’ akaniuliza.

‘Hizo barua ni zile nilizokuwa nikimwandikia yule binti wa kijijini, yule niliyejuana naye tukiwa watoto,..na kwasasa tafadhali, …. usitake kujua wapi nimeviweka, sitaki kabisa kumpa mtu hivyo vitu, ….maana kuna vitu vynagu muhimu sana,….vile nilivyokuwa navyo vimeshapotea, sasa nimevipata hivyo, itakuwa kumbukumbu yangu,….’nikasema.

‘Navihitaji haraka,….hiyo ni kwa usalama wako, …. inabidi unielekeze wapi vilipo,….na hakuna vitu vingine?’ akauliza huku akionyesha uso wa mashaka..

‘Nilivyochukua ni hivyo kwa haraka, unajua lile boksi lilikuwa na vitu vingi sasa, na jinsi ilivyokuwa sikuweza kuamua kwa haraka, kipi cha kuchukua na kipi cha kuacha muda ulikuwa hautoshi,….maana baadaye polisi waliingia, na mimi nikalirudisha lile boksi pale pale….’nikasema kwa harakaharaka.

‘Kwa ujumla hivyo vitu vyote unatakiwa uvikabidhi kwa polisi, na kama wataona vinahitajika kuhifadhiwa kwa minajili ya kulinda hadhi ya kibindamu, watafanya hivyo, lakini kwa kibali maalum,. Hatujajua hatimaya huyo mtu, maana hali yake ni tete sana, nilipokwenda kumuona, ….oh,mungu mwenywe ndiye ajuaye, dada wa watu yupo kwenye hali mbaya sana…’akasema wakili mwanadada kwa sauto ya huruma.

‘Oh, nilitaka niende nikamuone,lakini hawa jamaa hawaniruhusu….na mmoja ananidhihaki na kusema kuwa nataka kwenda kummalizia….’nikasema huku nikiwa nimekunja uso kwa hasira.

 ‘Unajua kinachowashangaza ni kuwa,kila anapopata fahamu anakutaja wewe, hili ni mojawapo ya jambo linalowafanya polisi wakushikilie, ….kwanini, awe anakutaja wewe, anaweza akawa anakutaja wewe kama kukushitakia kuwa wewe ndiye uliyemfanyia hivyo, au anakutaja wewe kwa nia njema, labda ana ujumbe anataka kukufiksihia wewe,hatuji,….’aliposema hivyo akanitia simazi, nikawa nawaza mengi, na nilishindwa hata cha kuongea, nikabakia kimiya.

‘Na huenda nikasafiri….’akasema.

‘Ukasafiri…!’ nikasema kwa mshangao ,halafu nikaongezea kusme;

‘Sasa ukisafiri mimi itakuwaje hapa,ina maana mimi nitakaa  huku rumande mpaka lini…je huwezi ukawaambia waniachie kwa dhamana?’nikalalamika.

‘Itakuwa safari ya siku mbili, sizani kuwa nitakaa siku nyingi…nia na lengo ni mamaDocta, na maeongezi yangu hayahitaji ufuatiliaji wa jambo jingine,…na kuhusa dhamana yako, utapata tu,…kwa hali ilivyo siwezi kuwaingilia kwa sasa,i kuna mambo ya kisheria yanayohitajiwa kuwekwa sawa…lazimakuwa na hatua fulani ya uchunguzi kabla hawajaamua kukuachia kwa dhamana, hata mimi siwezi kuyaingilia hayo kwa sasa’akasema huyo mwanadada.

‘Kwahiyo unasema unasafiri, unakwenda wapi?’ nikamuuliza

‘Nakwenda,hapo jirani tu, …Kenya…..nia na lengo langu ni kukutana na huyo anayejiita Docta mama, uzuri ni kuwa nimebahatisha kuongea naye kwenye simu, …na kwa kweli huwezi amini kuwa ni yule alikuwa hapa, anangea vyema kabisa na akakubali nimtembelee, maana kwa muda huo nikiwa naongea naye alikuwa kwenye mikutano yake, akasema kama namuhitaji kwa maongezi ni vyema nikutane naye….’akasema.

‘Unasema Docta Mama…..?’ nikasema kwa kuhamaki, halafu baadaye nikatuliza hamaki zangu na kusema taratibu;

‘Mimi huyo mama sitaki hata kumsikia, yaani hapana,hata sikuelewi, wa nini huyo,….unajua ndiye aliyesababisha yote haya…unamtakia nini..?’ nikauliza kwa hasira.

‘Kama ndiye aliyesababisha yote haya,basi ni muhimu nikakutana naye, najua nitapata mengi sana, hasa kuhusu Kimwana, na hawo wanawake wengine watatu, ambao wamekuwa kama miujiza, maana hawa wengine wawili wametoweka kiajabu,tumebakiwa na huyu ambaye naye ni mahututi…’akasema wakili mwanadada.

‘Na kweli hivi wale wakina dada wengine wapo wapi maana wote wana tabia moja, ya kuwa na manywele mengi,….lakini sura zao tofauti….ila nimegundu kitu fulani,kuwa tembea yao, inafanana, na hata ukichunguza viwiliwili vyao havitofautiani sana, labda mavazi yao na..na..usoni, kuna tofautia nikimaanisha sura zao, hasa usoni naona kuna utofauti,….lakini macho….unajau kuna kitu nilitaka kukuambia, mbona macho yao kama yanafanana….’nikasema nikiwaza.

‘Mhh, hilo sikuligundua maana sikuweza kuwaona hawo wengine kwa karibu sana..zaidi ya huyo  mahututi ambaye nimekuwa nikikutana naye mara kwa mara, hawo wengine, zaidi nimesikia kutoka kwako…’akasema wakili.

‘Kwahiyo huko Kenya unakwenda  kikazi au ndio huo utafiti wako…?’ nikamuuliza.

‘Yote mawili, ….lakini zaidi ni kutokana an utafiti wangu, kwanini akatoweka, na najua atakuwa anawafahamu sana Kimwana na huyu mwanadada tuliye naye hospitali, nitawaomba wakuruhusu ukamuone huyo mgonjwa, nilitaka niwepo ukimuona, lakini kama atazindukana na kuwa katika hali njema nimewaomba uende ukamuone, ili tujue ni kwanini anakutaja wewe.

‘Oh, isije nikawa ni mtu wake wa mwisho kuniona, naogopa sana hilo, maana watu wakiwa katika hiyo hali na unasikia wanamuhitaji mtu fulani aje, …..inakuwa kama vile huyo mtu nayehitajiwa ndiye  mtu wa kukamilisha idadi ya watu anaotakiwa kuwaona kabla hajafa...naomba sana isiwe hivyo maana itanitesa sana katika maisha yangu,….’nikasema na kujaribu kuikumbuka sura ya huyo mwanadada. Lakini ilikuwa haiji akilini, naona sura tatu tofauti, nikasema;

‘Kwahiyo huyo Docta mama hukuwahi kumuulizia lolote kuhusu haya yaliyotokea hapa?’ nikauliza

‘Nilimuulizia akawa kama anashangaa, na kudai kuwa hajui lolote ninaloongea, na ndio akasema angehitaji kukutana na mimi ,kwani namuuliza mambo mageni kwake,…..’akasema wakili dada.

‘Lazima atasema hivyo,mjanja sana yule mama, elimu yake, anaittumia sivyo ndivyo…unatakiwa ujiandae sana, maana unakwenda kukutana na mjanja,nasikia anajua sana hula tabia za watu, yeye kayasoema hayo kiundani,….’nikasema.

‘Tutaona, hata mimi nimeyasomea hay ohayo, na zaidi ya hayo naijua sheria….nilitka kabla ya kuondoak nikaonane na huyo mwanadada huko hospiatalini,…’akasema huku akiangalia saa yake.

‘Hata mimi natamani nimuone, sijui kwanini natamani sana nimuone, niongee naye, nijue aliniitia nini, na zaidi ya vile vitu vilivyokuwa kwenye hilo boksi, kuna taarifa gani kuhusiana navyo,…angala hata kama hajazindukana natamanini tu, niwe naye karibu, nimjue vyema , niione sura yake vyema….moyo wangu unamuwaza sana yeye kwa hivi sasa….’nikasema.

‘Kwa kifupi umempendahuyo mwanadada,hata kama humjui…au?.’akasema wakili na kucheka.

‘Sijui kama ni hivyo….szani kuwa ni kuhusu kupenda,….sijui, …’nikasema na dada wakili akainuka pale alipokuwa amekaa, huku akiwa kajawa na tabasamu mdomoni, na huku akitingisha kichwa na kusema;

‘Wanaume bwana. ..katu, hamueleweki.'.

NB. Jamani ndio hivyo tena, wanasema cha mwenzako `mavi'.....samahani kwa kutumia neno hilo, ila ni namna ya kutaka kukufikishia ujumbe.

 WAZO LA LEO: Siku zote haziwi sawa, maisha kama ilivyo safari kuna kushuka na kupenda,...kuna mabonde na mito,yote yachukulie kama changamoto za kimaisha. 
 Kwa wanandoa msikate tamaa pale mnaposigishana , mjue kuwa kama kwenu kunafuka moshi kwa wengine kunawaka moto, kama sio kuteketea kabisa, ...lakini yote ni maisha, ongeeni, jadilianeni na tafuteni tatizo lipo wapi, mtayashinda majaribu...


Ni mimi: emu-three

Friday, May 18, 2012

Hujafa hujaumbika-38



Mwanadada wakili alikuwa wa kwanza kufika eneo la tukio, na moja kwa moja aliingia ndani, na kukuta watu wa huduma ya kwanza wakifanya kazi yao, hakupewa nafasi kabisa, akaona haina, akasogea pembeni kuwapa nafasi, …na haikuchukua muda mara ule mwili ukainuliwa kwenye machela tayari kwa kukimbizwa hospitalini,….

Hakuana na jinsi, alitaka kumuona kuwa ni nani, lakini haikuwa rahisi hivyo, askari hawakumpa nafasi hiyo, walisema kazi yao ni kujaribu kuokoa maisha ya huyo mtu hawawezi kumchelewesha hapo zaidi, ikabidi atulie na akawa anaangaza macho huku na kule mara mara akamuona, jamaa kakaa pembeni, huku kainamisha kichwa chini,akamsogelea na kumgusa kwenye bega kwa nyuma.

‘Vipi …ooh, ni wewe, umefikaje huku….?’ Akamuuliza kwa kushangaa alipogundua kuwa ni mtu anayemjua.

‘Oh,…afadhali umefika, hapa nilitaka nikupigie simu,  kumbe na wewe umekuja, afadhali maana hawa polisi hawana dogo, Mimi ndiye niliyewapigia simu polisi,lakini nawajua wanaweza wakanigeuka , wema wangu uanweza ukaniponza….’akasema.

‘Imekuwaje wewe uwapigie simu, ulifikaje huku, Ina maana hapa unapajua….hebu niambia kwa ufupi na kwa hara…’akasema wakili mwanadada, na kabla hajaongea kitu, mkuu na kundi lake wakaingia na walipoona watu wakimalizia kazi mbali mbali mle ndani, akawaona wapenafasi kwanza,ili awaulize kila mmoja kwa wakati wake.

‘Imebidi awahishwe hospitaliu haraka,…huenda tukaokoa maisha yake,….’akasema askari kumwambia mkuu.

Mkuu akamsogeza huyo askari pembeni, karibu na tuliposimama, huyo askari ndiye aliyefika hapo mapema na kundi lake baada ya kupigiwa simu, akamuuliza swali la kwanza;

`Hebu niambie,ulifikaje hapa..?’ akauliza swali la utata.

‘Tulipigiwa simu na jamaa mmoja,…..mmh, yule pale,…’akanyosha kidole kunielekeza mimi.

‘Huyu jamaa kwenye simu alituambia kuwa amefika hapo baada ya kupigiwa simu na …..huyo aliyefikwa na hayo maafa,….mapaak sasa hatujamjua ni nani, huyo mwanadada, alisema kuwaanamuhitaji huyo jamaa kwa haraka , hayo ni kwamaeelzo yake ya haraka, sijamuhoji vyema, nimemuweka pembeni kwanza ili tumalize hayo ya muhimu…’akasema huku wote wawili wakiniangalia mimi

‘Tutamuhoji baadaye, wewe elezea kuhusu kazi yako,nini ulikiona uligundua nini…’akasema mkuu.

‘Nilipofika hapa, nilifika na kikosi kamili, maana nashukuru huyo jamaa alitupa maelezo safi kabisa, kwahiyo tulkuja tukiwa tumejiandaa, niliuagiza docta na kundi lake wafike hapo haraka, pia tulikuja na wataalamu wa alama za vidoela na wachukua picha, na wachunguzi wote niliwapata kwa haraka, kwahiyo tulipofika hapa kila kitu kilifanyika kwa haraka, hakuna kilichokosewa, tumewaachia sasa madocta wamalizie kazi yao ili watupe taarifa….kwasasa wamesha mchukua huyo ….eeh ,tuseme majeruhi hadi hospitalini’akasema huyo askari.

‘Kwahiyo unaweza kusema nini kuhusu hili tukio…?’ akauliza mkuu.

‘Ni tukio la kutaka kuua, kwa kutumia bunduki, …kwasasa tunaweza kusema ni majambazi, lakini hatuja wan a uhakika nalo,….siwezi kusema ni mauaji maana hatujapata taarifa ya docta, lakini huyo muathirika kapigwa risasi,…na ngoja tumsubiri docta atuambie wapi na athari yake, lakini mimi na wenzangu tuiimkuta akiwa bado hajapoteza fahamu….

‘Naona pale dirishani, kumemeguka, ina maana ile ni sehemu risasi ilipopitia kutoka kwa nje, ….’mkuu akaangalia pale dirishani na kiyoo kilikuwa kimevunjika kidogo,….na alipokichunguza vyema akagundua kuwa kile kiyoo kilikuwa na matundu, na risasi ilipenye kwenye moja ya tundu, ilikosea kidogo ndio maana kiyoo kimemeguka…na kile kipende kilichomeguka kikaanguka chini na kusambaratika.

‘Ndio mkuu, pale ndipo risasi ilipopitia, wataalamu wamepapima, na huyo muuaji alikuwa kwa nje, akalenga shabaha kupitia kwenye moja ya matundu ya hicho kiyoo, akiwa anmuona huyo mwanadada kwa ndani tundu…’akasema huyo askari.

‘Kwahiyo huyo muuaji alikuwa kasimama kwa nje, au sio….?’akauliza mkuu.

‘Hapana kutokana na mtaalamu wetu wa silaha anasema mlengaji alikuwa mbali kidogo, na ukiangalia kule, kuna jengo ambalo lipo juu kidogo, ina maana mtu akiwa kule anaona huku kwa ndani, na kwa vile taa hapa zilikuwa zinawaka, kama unavyoziona, licha ya kuwa ni jioni jioni,….tulizikuta hivi hivi,….’akasema na kuangali juu, kweli taa zilikuwa zinawaka.

‘Ukiwa kwenye lile jengo unaweza kuona huku, ukitumia silaha yenye darubini unaweza ukaona vyema tumejaribu hilo kwa haraka….’akasema huyo askari.

‘Sijawaelewa , ina maana huyo aliyekusidia kuua alikuwa kwenye lile jengo, akatumia silaha yenye darubini kumlenga huyo …..mmh,muathirika,je alijuaje kuwa kuna tundu kwenye hili dirisha…na kweli unaweza kuona ndani ukiwa pale, mbana naona kama haiwezekani,kama ni usiku sawa,lakini jioni hii?’ akauliza.

‘Tumechunguza hilo, unaweza ukaona,taa hizi nikali sana, na viyoo vya nyumba hii vinaonyesha vyema,hata ukiwa pale unayaona haya matundu vyema..na hasa ukitumia silaha yenye darubini….’akasema huyo askari.

‘Hata hivyo ni kazi kweli kupenyesha risasi kwenye haya matundu, aliwezaje kufaya hivyo?’akauliza mkuu.

‘Yapo matundu mengi, labda alibahatisha tu, na bahati risasi ikapenya kwenye hilo tundu, licha ya kuwa ilikosea kidogo, ….sizani kuwa ni labda ni shabaha ya huyo mtu, kuwa alikusudia hiyo risasi ipenye kwenye tundu…kama itakuwa hivyo basi atakuwa mlenga shabaha mahiri…’akasema huyo askari.

‘Ehe, kwahiyo mumeshajua ni aina gani ya silaha iliyotumika…au mpaka risasi itokewe…?’ akauliza mkuu.

‘Kwa makisio ya mtaalamu wetu, baada ya kuchunguza jereja amesema ni risasi ya silaha kubwa,…na ni hizi zinazoweza kulenga toka mbali,….lakini pale kwenye jengo sio mbali sana..’akasema huyo askari, na kutlia kidogo, halafu akasema tena;

‘Naona ingekuwa ni bora tukasubiri hiyo risasi ikatolewa kwanza ndipo tukaweza kutoa maelezo yaliyo sahihi….kwasababu mengine yote yamekamlika imebania kazi ya madocta…’akasema huyo askari

‘Hiyo ni sahihi kabisa na je mumeshaongea na huyo aliyewapigia simu…?’akauliza mkuu na yule Askari  akageuka na kuangali huku tulikosimama na dada wakili, na kabla mkuu hajapata jibu alilolitaka akatusogelea pale tulipo na kuniangalia kwa mshangao, na baadaye akamwangalia dada wakili akatabasamu na kusema,…

‘Usiseme kuwa wewe ni wakili wake, hatajibu maswali mpaka umruhusu…’akasema kwa utani huku akitabasamu.

‘Na ndivyo ilivyo, mimi ni wakili wake toka siku nyingi, ila kwa wewe na kwa leo nakuruhusu umuhoji maswali yote unayotaka..’akasema wakili mwanadada.
Mkuu aliniangalia kwa makini, halafu akasema;

‘Naona tunakutana mara kwa mara, na kukutana kwetu inakuwa katika hali isiyo rasmi, vipi unataka kujiunga na polisi nini, maana kila ninapokwenda na kukuta upo, na kuwepo kwako kunakuwa  sio kwa heri, haya hebu nieleze ilikuwaje?’ akauliza mkuu.

‘Mimi nilikuwa nyumbani kwangu ninapokaa, na nikapokea simu , ….nilipoiangalia hiyo namba ilikuwa ngeni kwangu,….nilizarau kuipokea, lakini ilipoita mara ya pili  nikaipokea na mara nikasikia sauti ya kike, ilikuwa ikiongea kwa taratibu, labda ili watu wasisikie au ni kutokana na hali ya kiafya, sikujua ni kwanini, ila sauti ilikuwa ya kama kunong’ona….’nikasema.

‘Ilisemaje hiyo sauti….?’akauliza.

‘Ilisema, kuwa …niende nyumba na 512, mtaa huu  hapa Sinza, ….na nifike haraka, kwanza sikupaelewa, licha ya kuwa alinieleza , akanifafanulia nifikie wapi, na ni vyema nichukue boda boda ii nifike haraka, na akasisitiza kuwa ni muhimu, nikichelewa nitakuja kujuitia katika maisha yangu yote…nikamuuliza kwanini na yeye ni nani?’nikatulia kidogo.

‘Ehe elezea tu, tunataka kupata maelezo ya haraka haraka, ikawaje…?’ akauliza mkuu.

‘Alisema nitajua nikifika huko,…halafu nikasikia kama sauti ya kiyoo kikivunjika, au kama hicho, mara na na sauti ya `aaaaah’ na ikawa kimiya, lakin nilihisi hiyo simu bado ipo hewani’nikasema nikujaribu kukumbuka ilivyo kuwa…

*******

Siku hiyo nilikuwa nimepigika kweli, watu siku hizi husema nilikuwa nimefulia, na kila nilipojaribu kutafuta chochote sikuweza kupata, nikaenda kwa mama mmoja niliyomzoea, akanipa ukoko, na nikamsaidia kusafisha vyombo, basi tumbo lilipojaa, nikaaona nikajipumzishe chumbani kwangu,kwanza nilioga nikuwa nimenyoa jana , kwahiyo sikujusumbua kuangalia ndevu,kwani huko ninapokwenda kufanya kazi hotelini usiku wanahitaji uwe mtanashaji. Kuna mtu mmoja aliniwahi kunishauri nijiunge na wanamitindo.,....eti ninafaa sikupenda hilo wazo, 

Nikaona nijipumzishe tu, kwani unaweza ukatoka kutembea ukakutana na mabalaa, na mimi najaribu kuyakwepa,....sizitkai mbichi hizi,sina pesa, nitafanya nini, nikaamua nipige mbavu,maana nilikuwa na sehemu ya kufanya kazi, ni bora nikusanye nguvu.

Nikiwa ndani ya usingizi,nikaota ndoto kuwa nipo kijijini kwetu, lakini ndoto hiyo ilinirudisha siku nyingi nyuma, nikiwa natoka shuleni, nikakutana na msichana mmoja, sikuwa na mjua,msichana huyo akaniambai kuwa mimi ni mtu mbaya sana,

‘Kwanini unasema hivyo?’ nikamuuliza.

‘Kwasababuu wewe unaharibu watoto wa watu halafu unawaacha njia panda….akaniambia nimewaharibu hata kwenda shule hawawezi,….na wazazi wao wamewafukuza…’akasema huyo msichana mgeni kwangu.

‘Mbona mimi sijafanya hivyo, wapo wapi hawo watoto?’nikamuuliza

‘Wale pale….’akanionyesha kwa vidole,na kweli pale niliona watoto wamelazwa, lakini cha ajabu chini ni watoto, lakini kwenye vichwa vyaoo ni watu wazima,na mmojawapo niliyemuona ni Kimwana, yeye alikuwa kilia na machozi yake yalikuwa nii ya damu, na sura nyingine ambayo najaribu kuiwaza ,lakini siikumbuki vyema,… ilikuwa yenyewe inaniangalia kwa kushangaa,…

Nikamuuliza huyo msicahana mbona ni wana sura za namna hiyo, kichwani watu wazima lakini kiwili wili cha kitoto,akacheka na kusema, wewe hujioni, kichwani mnaonekana watu wazima, lakini mtendo yenu ya kimwili ni ya kitoto, aheri hata ya mtoto, utasema anafanya hayo kwasababu ni mtoto, hebu jiangalie wewe…’akasema na mimi nilipojiangalia, nikajikuta mwili wangu ni wa kitoto…

Nilishituka kwa hofu toka usingizini, na sikuweza kulala tena,nikiwazi hiyo ndoto, mara nyingi nikiota ndoto, huwa ina maana fulani, au inanieleekza jambo fulani, lakini ndoto hiyo haikuwezakunipa maana halisii ni nini, nikaamua kuipotezea na nikajinyosha kidogo na kabla sijamaliza kujinyosha simu ikalia.

Nilipotizama ile namba, nikaiona ni ngeni kabisa machoni mwangu, nikaidharau na kuinuka kitandani,simu ileiliita mapaka ikakatika, nikasema hapigi tena, lakini mara akaanzakupiga tena, nikasema moyoni ni bora kusikiliza huenda ni simu ya pesa, nikaipokea;

‘Fika haraka hapa Sinza, ukifika hapa Kwaremi, ingia barabara inyofuata hadi nyumba namba SN X500, nipo ,fungua mlango utanikuta..’ikasema sauto ya kunong’ona. Nikamwambia kuwa huko sipajui na sina nafasi kwa sasa.

‘Ni muhimu sana,..usipokuja utajijutia masiha yako yote, nahitaji kukuona kwa jambo muhimu sana kwa ajili ya maisha yako ya baadaye….chukua boda boda, wengi wanapajua hapa mahali…nitamlipa huyo mwenye boda boda…’akasema kwa sauti hiyo hiyo ya kunong’ona.

‘Kwani wewe ni nani ….na umenijuaje….?’ Nikamuuliza.

‘Usiulize maswali mengi,unapoteza muda,weweukifikahapa utajua kila kitu na hata kie ambacho ulikuwa hukijui utakijua…njoo haraka…’mara nikasikia sauto ya kama `’kaaah’ naweza kusema ni sauti ya gilasi au kiyoo kilichovunjika, nasema hivyo baada ay kuona hivyo viyoo vilivyovunjika hapo, lakini kwa muda ule sikuweza kutambua ni sauti ya nini.

‘Ila nilichosikia cha wazi ni hiyo sauti ya `aaaah’na kutulia,nikabaki kusema `halooh, haloooh’ lakini sikusikia sauti nyingine sehemu ya pili, nikainuka kitandani haraka, na kutoka nje, ukumbuke sina pesa na ni nani angekubali akuchukue bure, ..bahati nilipotoka nje tu, nikamuona rafiki yangu mmoja,

‘Vipi broo, huna abairia leo…?’ nikamuuliza.

‘Kuna abiria mmoja kaniita nikamchukue huko Sinza, sasa najaribu kuliangali pikipiki langu maana huyo ni mtu wapesa…’akasema huyo rafiki yangu na moyoni nikasema mambo si hayo.

‘Hata mimi nafika huko, lakini sina pesa, kuna jamaa kaniambia nikifika huko atanipatia chochote, naomba lifti…’nikasema.

‘Wewe kila siku huna pesa….hujui nikikupakiza wewenitakosa abiria njiani,lakini twende tu, utanilipa tukifika…’akanimbia na mimi nikapanda kwenye hiyo pikipiki na haraka tukafika Sinza, na nilipomuulizia mitaa ya hapo, akasema Sinza anaijua sana kwani ndipo alipokulia na hata hiyo nyumba anaifahamu, ni nyumba nzuri, iliyojengwa kwa haraka sana…

Basi akanifikisha na kuniambia kuwa pesa nitampa huko nyumbani, name nikashukuru na kueleka kwenye hiyo nyumba. Kwakweli ilikuwa ni nyumba nzuri, imezungushwa geti la nguvu, nikafika kwenye geti na kukutata hakuna mlinzi, nikafungua mlango wa geti na kuingia ndani….nje kulikuwa na bsutani nzuri,nikaitamani ile nyumba.

Nikaharakisha kwenda kugonga mlango wa hiyo nyumba, lakini kulikuwa kimiya, nikafungua mlango na kuona upo wazi, nikaingia ndani. Macho yangu yalitua kwenye dirisha moja kwa moja, nikaona pale palivyomegeka, na kipande cha kiyoo kimedondoka chini na kuvunjika, nikaona ajabu,….sikuwa na mawazo ya kuangalia skafauni.

Mara nikasikia sauti ya mtu akiguna kuonyesha maumivu,…haraka nikageuza kichwa kuangalia kule sauti ilipotokea, ooh, nikashikwa na mshituko, damu, zilikuwa zinavuja toka kwa huyo mtu aliyelala sakafuni, zilikuwa zikitoka eneo la bega,…karibu na kifua…mawazo yangu yalikuwa labda kapigwa kisu,lakini kulikuwa hakuna kisu,…nikamsogelea alikuwa mwanadada akiwa na nguo za kulalia, niakogopa hata kumgusa, nikujua sasa hilo ni balaa

‘Msoma…..mso….mali…naku….naku……’akawa anataka kusema kitu, lakini sauti ilikuwa hatoki vyema na wala hakuweza kumalizia hilo neno, alilotka kusema,  sikujua anataka kusema nini, na mara akaonyosha kidole nakunionyeshea kwenye kabati,…nikaangali sikuona kitu zaidi ya kabati la vitabu….nikamgeukia na kutaka kumuinua.

Lakini nikaona nitakuwa mjinga mtu kaumia badala ya kutoa msaada naanza mengine,nikapiga simu polisi na kuwapa maelekezo, na bahati nzuri,walisema kuwa wapo karibu na wanapajua hapo ninapowaelekeza, nikawapa hali halisi ilivyo.

Haikuchukua muda wakafika,…ndivyo ilivyokuwa mkuu,...'nikamaliza kujieleza.

Nb, leo najisikia hali sio shwari,....tuonane sehemu ijayo mungu akipenda.

WAZO LA LEO: Unaweza ukajikuta ukiandamwa na matatizo lukuki,hata kuwaza yasiyokuwepo, ooh, labda mkono wa mtu, ooh,kwanini mimi....cha muhimu ni kuvumilia na kujikabdihi kwa mungu, maana yote yameumbwa kwa ajili yetu wanadamu, yawe mazuri au mabaya. Jua kuwa mvumilivu hula mbivu.


Ni mimi: emu-three

Thursday, May 17, 2012

Hujafa hujaumbika-37



Kesi ya Jangiri kama muuaji ilikuwa ya aina yake, maana kama ilivyotarajiwa huyu jamaa alikataa makosa yote ni kudai kuwa alitamka kuwa ndiye aliyemuua Kimwana kwasababu ya mateso na shinikizo la polisi, alifikia hadi kuonyesha alama za vidondoa eti vilivyotokana na mateso hayo, sijui aliteswa saa ngapi,…

Mara kwa mara wakili mwanadada alifika kwenye hiyo kesi na wakati mwingine alimuachia msaidizi wake,huku akiwa katika uchunguzi wake binafsi, alikuwa na mambo mengi ya kufuatilia, kiasi kwamba aliona muda haumtoshi, na leo akiwa ndani ya hii kesi, akapokea simu toka kwa mmoja wa wafanyakazi wake

‘Nipo mahakamani unasemaje?’ akauliza.

‘Kuna mtu kaleta barua hapa, na anasema hiyo barua ni ya muhimu sana, anataka wewe mwenyewe uipokee…ndani yake kuna mkanda wa CD’s,umeandikwa `confidential…’ na huyo mletaji anasema anahitaji jibu la harakakutoka kwako…’akasema.

‘Usiufungue huo mzigo, au huo mkanda ,inawezekana ikawa ni bomu, …nakuja…’akamsogelea msaidizi wake kwenye hiyo kesi na kkumnong’oneza jambo, rafiki yake akakunja uso, hakupenda abakie peke yake, lakini aliona hilo jambo alilokuja nalo rafiki yake ni la muhimu ….akakubali aondoke, nakesi ikaendelea,

Alipofika ofisini kwake,akaichukua ile barua na kuiangali kwa makini, akaichukua ile CD’s , na kuiweka kwenye mashine ya kuikagua na kugundua kuwa haina hatari, akaichukua na kuingia ndani ya chumba chake cha siri, na kuiangalia…halafu akamwambia huyo aliyeileta kuwa anaifanyia kazi,...

*****
Mkuu mimi nataka nionane na huyo mshitakiwa, faragha, bila ya kuwepo wakili wake, ….’akasema wakili mwanadada.

‘Kwanini, siunajau sheri zilivyo….’akasema mkuu.

‘Najua lakini wakati mwingine inabidi ufanye hivyo, ili kuweza kufanikisha sheria inayotaka kukiukwa…’akasema.

‘Kwani kuna nini umegundua…?’ akauliza mkuu.

‘Hayo ni maswala ya kimahakama, na mbinu za kisheria, kuna kitu nataka kuhakiki…nikifanikiwa nitakuja kukuambia, wewe jitahidi nionane na huyo mtu kwa faragha…’akasema na kuondoka.
Ilikuwa usiku na wakili mwanadada akaweza kukutansihwa na Jangiri, akamwangali kwa makini kabla hajamuuliza swali, nia ni kutaka kumjua hulka yake, kila mtu na hulka yake, ukiijulia unaweza ukamsoma na hata kumgundua kuwa anasema ukweli au uwongo,…

‘Mimi naamini kuwa kweli wewe sio uliyemuua Kimwana…’akasema na kumfanya Jangiri ashikwe na mshangao,akasema;

‘Wewe dada mjanja sana, ndani ya mahakama umekuwa ukinishinikiza mimi kuwa ndiye muuaji naua wanawake wasio na hatia…sasa unakuja na mbinu yako hii….hunipati ng’ooo, sawa mimi sio muujaji nimeshasema huko mahakamani sasa unataka nini kwangu…’akasema.

‘Ndio maana nataka ushirikiano wako, kama wewe sio muujai ni nanii aliyemuua Kimwana…nilikipaya fununu kutoka kwako, tutaweza kumshika huyo muuaji, nikuulize swali, wewe na kimwana mlijuana toka lini, ..’akauliza.

‘Hayakuhusu hayo , kama uantaak nijibu lolote, kwanza namuhitaji wakili wangu,….’akasema na kumwangali huyo wakili kwa mashaka.

‘Sikiliza nikuambia, …mimi napenda sana kuwa mkweli , na mtu mkweli kwangu ni rafiki mwema, na nikikuahidi kuwa nitakusadia, ujue kweli nitafanya hivyo…nataka nikusaidie, lakini pia nataka haki ikitendeke, ili tumjue aliyemuua Kimwana,….kwa uchunguzi wangu, ile risasi ilitoka kwenya bastola yako sio hiyo iliyomuua Kimwana….lakini kuna ujanja umetumika na huo ukweli umefutika,lakini kwa kupata maeezo kutoka kwako naweza kuufichua…’akasema wakili.

‘Una uhakika na hilo…..?’ akauliza Jangiri.

‘Nina uhakika ndio maana nikatafuta njia za kuongea na wewe, ili nipate maelezoo yatakayoniwezesha kulinda hoja ayangu….ukishirikiana na mimi, kesi ya mauaji juu yako itafutika,…siwezi kukuahidi makosa mengine, lakini hilo la mauaji ninaweza kukuahdi,ikiwa utaniambai ukweli….’akasema wakili.

‘Ukweli upi unaotaka kutoka kwangu…?’ akauliza.

‘Kwanza niambia jinsi gani ulivyomjua Kimwana….kama kweli ulivyodai kuwa ulikuwa ukipenda na isingelikwua rahis kwako kumuua…?’ akauliza, na yule jamaa alikaaa kwa muda kifikiria,akasema baadaye.

‘Ina maana kesi ya mauaji ianweza ikafutwa, na huenda kama nikufungwa sitafungwa kwa kesi ya mauaji na kweli sio mimi niliyemuua Kimwana…ni nani basi kafanya hivyo…inawezekanakabisa,nakumbuka vyema….’akatulia.

‘Hebu kumbuka vyema,….lakini kwanza niambia ulivyomjua Kimwana…?’akasema wakili.

‘Kimwana ni bosi wangu, lakini kabla ya kuwa bosi wangu, ….alikuwa rafiki yangu..’akatulia na kuwa kama anakumbuka jambo,…na baadaye ndio akaanza kuhadthia maisha yake na Kimwana…

*******

`Kimwana alikuwa rafiki yangu toka zamani sana, naweza kukiri mimi ndiye mwanaume wa kwanza kumjua, …na huenda naweza kukiri kuwa mimi ndiye niliyemuharibu. Nasema hivyo kwasababu, nyingi tu, achilia mbali kumuingiza mjini.

`Kipindi narudi nyumbani nikiwa na pesa za kumwanga kutoka na madili yetu ya hapa na pale, nilikutana na huyo msichana akiwa antokea shule, nikampla lifti , kipindi hicho nilikuwa na gari, maana pesa ilikuwa hainichezi mbali, nikamtamani huyu binti, licha ya kuwa alionekana mdogo,lakini alishakuwa msichana aliyevunja ungo.

`Nikaanza kumtongoza, na unavyojua wasichana wa kijijini, wanajifanay hawapendi kumbe wanapenda, na kumba huyo binti alishakuwa na hisi hizo zakimapenzi, labda kutokana na makundi rika au aliwahi kusimuliwa au kufundwa, kwahiyo hata nilipokuwa nikiongea naye, alionekana kujihami kikubwa….’akasema Jangiri.

‘Hata hivyo kumbe sifa zangu zilikuwa mdomoni mwa kila msichana, siku ya pili yake nilipomtamkia kuwa nampenda na nipo tayari kumpa chochote anchotaka ,akaniambai kwua na yeye ananipenda, ila yeye anachotaka ni mimi nimchkuea tukaishii naye mjini,kwani masiha ya kijijini hayataki…nikaona mambo sio ndiyo hayo.

Tukasuka mpango,nikamtorosha huyo binti na kuja naye mjini,…kipindi hicho niliwahi hata kuwekwa ndani kwa ajili yake, maana wazazii wake walikuja kugundua kuwa mimi ndiye nilimyemtorosha wakanitumia maaskari, nikakamatwa na kuwekwa ndani.

Nilikaa siku tatu, na aliyewezesha mimi kutoka na huyo huyo binti,aliwaendea polisi na kuwaambia kuwa mimi ni mchumba wake, na hakunitosroha yeey, ila yeey ndiye alitoroka an kuja kwangu, kwahiyo kam ni kumshika wamshike yeye,…

Wazazi walikuja juu kweli, lakini Kimwana alikuwa kazimia kwangu, akawa hawajali wazazi wake, na kuwaambia kuwa hataniacha mimi kamwe kwasababu keshanipenda na huko kijijini harudi. Basiwazazi wangefanya nini, ikabidi wakubali shingo upande.

Nikawa naishi na huyu binti, lakini taarifa zangu zilifika hukoo kijijini kuwa mimii nafanya shughuli za kijamabzi, kwahiyo binti yao atapotea, na wakaja kunifuata kuwa wanamtaka binti yao kwasababu mimi ni jamabzi, nikawahamaki,nilihamaki kweli na Kimwana naye akinisadia na hata akawafukuza wazazi wake na kuwambai kuwa wasimfuate fuate kuhusu maisha yake….na ikawa mwishoo wa wazazi wake kumfuatilia.

Maisha yana kkupnda na kushuka, ikafikia mahli sina pesa, na dili hazipatikani, nikaona sas nitaumbuka na Kimwana ni mtu wa amtumizi, alikuwa mrembo, kama ulivyomuona na kila mwanaume alikuwa akimtaka, kwahiyo ilibidi niwe natumia ikiukweli,…sasa nikawa sina kazi ya maana nikawa sina pesa na kimwana akaniambai moja kwa moja kuwa yeye alinipednea kwasabbu yapesa, sina pesa, kwahiyo …

‘Ina maana alikuwa hakupendi ,alikuwa akipedna pesa zako tu….?’ Wakili akimuuliza.

‘Ndivyo ilivyokuwa,na kiukweli Kimwana hana habari na mapenzi haya ya kupenda eti, nakupenda kimoyoni, yeye anapenda matumizi, labda  niseme mpenzi wake ni pesa, kama huna pesa huna matumizii huna nfasi kwa huyo binti…’akaseam jangiri.

Basi nikaona nitamkosa, lakini nikabuni mbinu,, nikaoan kwa ajili ya urembo wake. Lazima nimtumie,nikamawambi nipo tayari kumuachie ajirushe na wanauem wengine,ilimradi tuapete pesa, lakini tufanye mbinu za kuishi, nikamsuka mapaka akakubali, tukaanza kazi ya kurubuni wanaume wa watu wenye pesa,…’

‘Kwa vipi….?’akauliza wakili.

‘Yeye kwasaabbu ya urembo wake, wapo matajiri waliokuwa wakimtaka, na hawo matajiri walikuwa na ndoa zao,tulichokuwa tukifanya ni yeye kukubali kwenda nao nyumba za wageni, na mimi nakuja baadaye nikiwa na cheti cha ndoa kuonyesha kuwa huyo ni mke wangu, na tunamshikilia huyo tajiri kuwa asipotupa kiasi fulani cha pesa tuankwenda kutoa taarifa polis na kwamkewake,….wengi walikuwa wakitoa pesanyingi tu, wengine walikuwa wakigoma…

Siku moja nikakutana na mama mmoja ,alikuwa akiendesha gari lakifahari, nikavutiwa nalo, mwanzoni nilitaka nifanye mpango na washikaji tuliibe, lakini siku ya pili yake nikakutana na huyo mwanamke akaniita na kuniambai kutokana na mwili wangu anaona nitafaa kuwa mlinzi wake, lakini kwanza anatka anaifundishe jinsi gani ya kuwa mlinzi….nikakubali na kwelii nikapitia chuo cha mafunzo ya ulizni ,kutumi asilaha,nilikuwa najua kutumia silaha kabla,lakini hapo nilifundishwa kutumiasilaha ya aian yoyote, silaha jisni ilivyo, na uliznii wa hali ya juu.

‘Basi nikatulia an huyu tajiri mwanamke, na kumwambia Kimwana kuwa sasa nimepta kazi, atulie nyumbani, haat hivyo pesa niliyokuwa nikipta ilikuwa haitoshi, ikawa tunafananya dili zetu hizo hizo na siku moja huyu tajiri yangu akaniuliza Kimana ni nani wangu,..

‘Yule ni mpenzi wangu, kani vipi?’nikasema.

‘Nahitaji kufungua chuo cha warembo, na yeye namuona ni mrembo kweli, unaweza kumshawishi ajae kwenye hicho chuo,….’akaniamabii na mimi nikamwambai ahkuna shida, nikamwambia Kimana licha ya kwa mwanzoni aliktaa, lakini baadaye akakubali na ikawa mwanzo wa yeye kujuana na mama Docta.

Akiwa na mama Docta akapanda chati,nakuanza kunsiahau mimi,lakini sikujali, maana kazi ninayo, na kama ni wanawake nikiataka Napata,lakini kiukweli Kimwana nilipenda sana, na hata nikaja kumtamkia kuwa nataka nimuoe, alicheka sana sikuu hiyo….

‘Lakini mbona nasikia alikuwa lkiolewa na wanuem wengi, au ndio hiyo kazi aliyokuwa kapewa na huyu mama Docta.?’ Akauliza wakili.

‘Kimwana sio mke wa kuweka ndani, mtu amabye angeliweza kuishi naye na kuelewana naye, ni mimi peke yake, maaan namjua toka utotoni, najua nini anachokitaka, na tabia zetu zinaendena wengina wote waliomuoan zilikuwa ndoa  za kibiashara tu…hilo ninauhakika nalo…ila alipokuja kuolewa na huyo mwanaume,…nani huyu Msomali, pale niliona mabadiliko, inaonekana alimpenda kiukweli…lakini hata hivyo hata kama alimpenda kiukweli, badi alikuwa na kasoro, hakuna na pesa, na kiwamanamapenzi kwake ni pesa…’akasema.

‘Sasa ilikuwaje Kimwana akawa ndio bosi wako?’ akauliza.

‘Kutokana na utendaji wa kikazi, mimi nilikuwa mkali wa ulinzi na kutumia silaha, tulikuja kugudnu akwua Kiwamana ana maadui wengi sana, basi tukakubaliana kuwa kila anapokwenda niwe nayemimi,na kwa viletulikua tukijua kabla haikuw ashida kwangu,….

‘Haya sasa niambia ilikuwaje siku ile y atukio.

‘Siku ile ya tukio. …nilipata taarifa kuwa wewe unatakiwa uondoek duniani…kwa pesa nyingi tu’ akasema.

‘Ni nani alikupa hiyo taarifa au ni nani aliataka mimi niondoke dunianai?’ akauliza wakili.

‘Haina haja ya kumtaja mpaka hapo unaweza kujua ni nani, licha ya kuwa sikutaka kukuambia yote hayo,lakini kwa vile umenihakikishai kuwa mimi sio muuaji wa Kimwana nitakuambia kila kitu….

********

Baada ya kumaliza mazoezi ya kulenga shabaha, Wakili mwanadada alimwangalia mkuu kwa muda bila kusema kitu, hata mkuu akajikuta akijiuliza kwanini huyu mwanadada kila mara ananiangali sana , na ameligundua hilo mara nyingi, hakutaka kumuuliza, akasubiri, akijua kuwa subira huvuta heri , huenda kuna kitu anatka kuniambia;

‘Mkuu unajua sana kulenga shabaha,…’akasema wakili mwanadada.

‘Unanitania, katika walenga shabaha, mimi nipo mbali  sana, ….huoni hata wewe leo umenishinda kwa mbali sana, kwa ujumla mimi siwezi kujisfu kuwa nina shabaha, katika kundi letu sisi mwenye shabaha sana ni wakili wetu mkuu kwenye kitengo chetu cha sheria, kila tukifika hapa hakosi hata  mara moja, ana kipaji sana cha shabaha….

‘Mimi sijawahi kuja naye, nikamuona anavyplenga  shabaha,natamani nimuone,ili nijue siri ya uwezo wake huo…nasikia hali yake ni tete, huu ugonjwa wa shinikizo la damu, unawasumbua watu wengi sana siku hizii…’akasema wakili huku akijaribu kuwaza jambo.

‘Kwakweli yule ni mkali wa shabaha,…na ni mtu mwenye afya sana, nashindwa kuelewa hili shinikizo limemshindaje,…lakini ndio hivyo, mwili wa binadamu ni mwili tu, unawezwa ukalazwa kitandani kwa kuchomwa na sindani kwenye kidole,…unajua kama isingelikuwa haya matatizo yaliyomkumba, tungekuwa naye hapa, lakini natumai atayashinda yote,… …’akasema mkuu.

‘Kwani ana matatizo mengine, nilisikia ana matatizo ya kifamilia, …ilikuwaje….?’ Akauliza wakili mwanadada.

‘Ina maana wewe hujui hayo au unaniuliza kiubembe, hujui kuwa alikuwa na tuhuma nzito, iliyosukwa na hawa wahuni,…, na picha mbaya zikatolewa , …akaja kudaiwa pesa nyingi tu na hawo wahuni,  alihangaika na baadaye akaamua kulitoa hili jambo kwetu kisiri, tukasuka mpango ili kuwakamata hawo watu,lakini hatukufanikiwa,…hata hivyo lilikwisha, ila hapo ndipo afya yake ilipooanza kutetereka…’akasema mkuu.

‘Ina maana ndio maana hakutaka kushiriki kwenye hii kesi?’ akauliza wakili.

‘Haiwezi ikawa ndio sababu ya moja moja,….kwasababu tulishayamaliza mataizo yake , waliomfanyia hivyo ni vibaka wa kawaida tu,…Siku walipomletea hizo picha,alipatwa na mshituko mkubwa, na tangu siku hiyo anasema kuwa amekuwa akipata maumivu makali upande wa kushoto,…na limekuwa ni tatizo ambalo linamfanya ashindwe kutimiza wajibu wake, anahitaji mataibabu ya hali ya juu…’akasema mkuu.

‘Unajua hili tatizo halina asili kwa jamii zetu, na mtu anaweza akafumaniwa isiwe na tatizo, lakini jinsi uchumi unavyokuwa, na watu kuingia katika maswala ya kisheria katika kurithi mali, …na vitu kama hivyo, tatizo hilo linakuwa moja ya janga, maana unakuta labda utajiri upo kwenye familia ya mke, na mume kwao ndio hohe hahe, …..’akasema mwanadada na kutulia kwanza.

‘Kuna kesi moja iligubikwa na mambo hayo,…katika makubaliano ya ndoa ,mume aliambiwa kama atakutwa na tatizo,lakashifa hasa hiyo ya kuvunja sheria za ndoa, ya kufumaniana,au madawa ay kulevya, ….basi ndoa itakuwa imevunjika…sasa mke akampata mshikaji mwingine ,akaona njie pekee ya kuachana na mumewe, na kumtumbukiza kwenye kashfa, na alichofanya nii kumtegea mwanamke….’akatulia kwanza.

 Akasuka huo mpango ukiwashirikisha mke wa mtu na mshikaji wake, wakamtegea huyo mume wa huyo mke, …wakamtafuta msichana, hawa wanawake wanaojua hizo kazi, wanachohitaji wao ni pesa tu,…na wanaume mlivyo wazaifu, akategeka na tendo likafanyika na picha zikachukuliwa,….hutaamini hilo lakini lilitokea….

‘Sasa hapo tamaa ikatawala, huyo mshikaji alichokuwa akimpendeahuyo mke ni pesa, mengine yanakuja tu, kwasababu ya pesa, na tamaa ya huyo mshikaji ikamtuma afanye jambo jingine, kwasababu ule mpango wa kumkamatisha huyo mume wa huyo mke, huyo mshikaji, alikuwa  akiujua kiundani na ushahidii uliotakiwa ni picha ya tukio, yeye akaona kuwa kumbe anaweza kuzitumia hizo picha kuchuma pesa kirahisi,….’Yule wakili mwanadada akatulia na kumwangalia mkuu wake kama kweli anamsikiliza na kumuelwa akaendelea kusimulia hiyo kesi kwa kusema.

‘Baada ya lile tukio ushahidi ambayo ni picha akawa kabakia nazo huyo mshikaji, na wakapanga nini kitakachofuata…kwahiyo sasa ilibakia vitendo,…mke aanzishe chokochoko kuwa mume wake anatembea nje ya ndoa keshavunja mkataba,….kuna kitu kilitakiwa huyo mshikaji akifanye kwanza, lakini jamaa akawa hatimizi hiyo ahadi ili yule mke anze kashikashi, ingwaje kwa ndani ya familia, alishaanza kwa kumshutumu huyo mume kuwa anatembea nje ya ndoa,na mume akawa mkali na kukataa kata kata, na kudai ushahidi,….

‘Nia ya huyo mke ilikuwa ni hivyo,kuwa aachane na huyo mume ili aje baadaye aolewe na mshikaji wake, sababu ni kuwa mume wake ni mvivu katika maswala ya ndoa,…alimpenda kwa muonekano wa nje, kumbe mambo mengina hayatimiziki kihivyo, na siku alipokutana na huyo mshikaji kisiri akagundua kuwa kumbe kuna mambo ambyo hayapati kwa mumewe, yapo kwa waume wengine, kwa tamaa hizo  akaona kuwa huyo mshikaji ndiye anayefaa kuwa mume wake…’akatulia huyo mwanadada na kutizama chini.

‘Haya mambo yapo jamani, yanatesa jamii, usione watu wanatoka nakusema mume wangu ,au mke wangu, kuna watu hawana raha inapofikia katika hayo maswala, lakini yanapelekwa kimiya kimiya, watu wanaumia kimiya kimiya, kwa kuogopa kashifa, kwa kuogopa, kuwa atatoa siri ya ndoa,…ndoa zinalege lega, na wengine wanaachana kwa kisngizio kumbe chanzo ndio hicho  kisichoelezeka.

Sasa kumbe hata huyu mshikaji, hakuwa na upendo wa dhati na huyo mke wa mtu, ni kwasababu ya kutaka pesa na mali,..wapo wanaume wa namna hiyo wengi tu, kama walivyo wanawake wengi tu,..’akasema huyo mwanadada na mkuu akatikisa kichwa kukubali, akawa huku akiwa anasikiliza hicho kisa cha hiyo kesi anayoielezea wakili mwanadada.

‘Basi huyo mshikaji akawa anachukua nakala moja ya picha na kumpelekea yule mume wa mtu kwa siri, na kumwambia kuwa asipomlipa pesa nyingi atalifikisha hio swala kwa mkewe….hebu fikiri hapo jamaa alipoziona picha picha alikuwaje, alichanganyikiwa, …. akahaha, na kweli akampa hizo pesa, kwani pesa alikuwa nazo, kwa kupitia kwenye miradi ya familai ya mke, lakini muonja asali haonji mara moja, huyo mshikaji akafanya ndio sehemu ya kupatia kipato, ikawa ni kamchezo….’yule wakili mwanadada akacheka na kusema.

‘Unajua nimegundua jambo, ibilisi akishaingia akilini, anakuchezea kama mtoto mdogo, huyu mke,akawa anazitaka zile picha, lakini huyo mshikaji anamzungusha, na bila hizo picha ndoa haiwezi kuvunjika na yeye keshampenda huyo mshijaki, na mume kambana hapati mwanya wakwenda kuyapata yale ambayo hayapati toka kwa mume wake…akaona anawekewa kiwingu, akaamua kumtegea sumu mumewe….’akatabasamu tena huyo wakili na mkuu akasisimuka na hicho kisa, akasikiliza.

‘Sasa siku hiyo kaweka kinywaji chenye sumu, akitarajia kuwa mume wake akija atakinywa, yeye akwa akwa aktoka kwenda kazini, ….mume ana kawaida ya kurudi mchana kupata chochote, nay eye ndiye mwenye ufunguo wa nyumba, akasahau kuwa alishawahi kumpamshikaji wake ufunguo, ili wakija asipate shida ya kuingia ndani.

Sasa huyo mshikaji anajua kuwa huyo mume muda kama huo anakuwa nyumbani, na alihitaji pesa, akachukua nakala nyingine na kwenda huko kwa huyo mume wa mtu, alipofika kwa kujiamini,akafungua mlango na kuingia ndani….

 Alipoingia ndani akakuta mezani kuna  maandalizi,….yeye hakujali sana, akacukua kinywaji na kujimiminia, akajisaidia na chakula, hana wasi wasi, huku akisubiri, akaweka gilasi mojayakinywaji akanywa, akawa anakunywa taratibu, huku akisubiri, lakini jamaa siku hiyo akakutwa an foleni y magari akawa kachelewa kufika….mshikaji , akaongeza gilasi ya pili,….tumbo likaanza kuuma.

‘Mume anakuja anakuta mtu yupo chini mapofu yanamtoka mdomoni…hajiwezi kabisa, haraka akaita polisi na jamaa akakimbizwa hospitalini,…akafia njiani,  na yule mume akashikwa kuwa yeye ndiye kampa sumu huyo jamaa….sasa angali kesi kama hiyoilivyo,…inaumiza kichwa sana, unataiwa uwe makini, ukichukulia juu juu, utasema kweli, huyo mume ndiye kampa sumu huyo jamaa kwasababu ya hiyo tabia ya kumdai pesa kwa kutumia picha chafu…..’akatulia na kumwangaliwa mkuu .

‘Hapo ndipo uchunguzi ,akili na hekima inatakiwa kutumiwa, ukichukuliwa juu, juu ,….utafunga watu wasio na hatia,….ndio maana naogopa sana hizi kesi zinazofungamana na jamii na,…mahusiano,…usipokuwa makini utaumiza watu wengi wasio na hatia badala ya kuponya….’akasema wakili mwanadada.

‘Nikuulize hicho kisa kina maana gani kuhusiana na hii kesi yetu….?’akauliza mkuu.

‘Nilikuwa nataka kukuonyesha jinsi gani haya mambo ya kutishiwa kuwa usiponilipa pesa nitatoa siri yako jinsi sasa yanavyokuwa sumu kwa watu, ni kama uuaji wa namna fulani,inabidi jambo hili lifanyiwe kazi ya haraka na jamii ielimishwe,…’akasema huyo wakili mwanadada na alipoona mkuu katulia akamuuliza swali,

‘Na je tuhuma kwa huyu mama docta kuwa ana michezo kama hiyo imefikia wapi,?’ akauliza wakili.

‘Tatizo kubwa mambo kama haya hayana ushahidi, wale wanaotishiwa hawataki kuyaleta hayo mashitaka kwenye usalama, wakiogopa kuwa siri zao zitajulikana, na matokeo yake tunawapa nguvu sana hawa watu, nafikiri ndio silaha yao kubwa, kuwa wanafanya namna ambayo mtu waliyemlenga hataweza kutoa hiyo taarifa polisi

‘Huyu mama docta kaondoka muda sasa…..nafikiri karudi kwao Kenya….’akasema mkuu
Wakili akatulia kwa muda bila kusema neno, huku mara kwa mara akimwangalia mkuu huyo, alijua kabisa hisia zake zinaweza zikapingwa na mkuu, lakini kila mara alipowaza hilo jambo aliona inawezekana, kinachotakiwa ni kuhakikisha anakusanaya ushahidi, na ikiwezekana amshirikishe huyo mkuu kwa kila hatua, akageuka na kumwambia mkuu;

‘Samahani sana mkuu, usione kwanini nimetulia kimiya hivi bila kusema kitu, nilikuwa nikijaribu kujiuliza mwenyewe , na kutafakari kile ninachotaka kukuambia, najua unaweza usiniamini, lakini nahisi inaweza ikawa ndivyo hivyo, licha ya kuwa sijaweza kupata uhakika wa moja kwa moja…..’akasema wakili mwanadada na kutulia kwa muda.

‘Wewe ongea na kusikiliza…’akasema mkuu.

‘Mimi nina uhakika kuwa Jangiri siyo yeye aliyemuua Kimwana,…’akasema wakili.

‘Unasema nini,…mbona ushahidi upo, na yeye mwenyewe alikiri mbele yangu kuwa  yeye alikuwa na nia ya kukua wewe, lakini bahati mbaya risasi ikampiga Kimwana,amekuja kukana baada ya kumpata huyo wakili wao,….kama umjuavyo yule wakili anajua kucheza na sheria….’akasema mkuu.

‘Risasi iliyomuua Kimwana haikutoka katika bastola aliyokuwa nayo Jangiri,taarifa hii imebadilishwa kinamna, na ukweli kufichwa, kitu ambacho kinaonyesha kuwa kuna mtu ndani ya wanausalama anahusika na hiki kifo, au kafanya hivyo kwa shinikizo fulani, lakini hilo la kufanya kwa shinikizo halina nguvu, ….naoana kafanya hivyo makusudi ili kuhakikisha kuwa ukweli haujulikani,…’akasema wakili mwanadada.

‘Haiwezekani…’akasema mkuu na kumwangali wakili mwanadada.

‘Nakuomba leo twende kule Mbezi nikakuonyeshe ushahidi ambao huenda ukakufungua macho, lakini usiseme lolote kwanza kwa mtu yoyote, hili ni kati yangu mimi na wewe tu…kwasababu ikijulina nina uhakika kutakuwa janga kubwa…’akasema wakili mwanadada, na kumfanya Mkuu kumwangali huyu mwanadada kwamacho ya wasiwasi.

‘Usishangae mkuu, mambo hayo yapo, na usione kuwa labda u kiongozi, unafuatilia kitu, kuna mengine yanatokea nje ya uwezo wako, leo unayemuamini na yeye akajitahidi kuaminika kesho anaweza akahini huo uaminifu, huenda kajitihadi kikomo cha uwezo wake, akasema basi ngoje iwe hivi, akijua haitajulikana…hujafa hujaumbika, na ukistaajabu ya Musa ….’akasema huyo mwanadada na kabala hajamalizia huo usemi simu ikapigwa…..

NB: Sehemu hii nimeiandika kwa shida sana, sijui kama ipo sawa, tuzidi kuwepo kwenye sehemu ijayo..

WAZO LA LEO: Katika maisha haya usichukulie kila jambo kuwa ni sawa au si sawa, cha muhimu ni kuwa na uhakika nacho,maana ukiwa na pupa na hamasa ya kila jambo unalolisikia utaumia bila faida yoyote; Pupa huua,  na mwenye pupa hadiriki kula tamu.


Ni mimi: emu-three

Search This Blog

Loading...