Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha (diaries), ikiwemo visa , matukio, mijadala na yale yote unayopenda kuwemo humu. Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pina unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu. SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA

Monday, May 20, 2013

WEMA HAUOZI -10



 Niliposikia mlango ukigongwa, na wakati huo yule mwanamke kaanguka chini , na alianza kwanza kupiga piga miguu, na baadaye akatulia, nikajua sasa ni balaa. Nikashika kichwa kuashiria kuchanganyikiwa, na nikageuka kumwangalia babu yako, lakini cha ajabu yeye hakuonekana kujali,…

Mlngo ukazidi kugongwa na sauti iliyosikia sio ya mtu mwingine, bali ilikuwa ni sauti ya mume wa huyu mwanamke rafiki yangu, ..hapo nikageuka kuangalia pale alipolala yule rafiki yangu, na kwa muda huo alikuwa katulia kimiya, kuashiria kuwa huenda kapoteza fahamu au keshafariki,….

‘Oh, kafariki, hapana, hajafariki, atakuwa kazimia tu,….’nikawa najiuliza mwenyewe akilini, …mungu wangu, sikutaka wazao hilo la kufariki liniingie akilini, na liliponijia nikajaribu kuliondoa kwa haraka akili mwangu, lakini athari za hilo wazo, zilishaingia akilini mwangu na kuathiri mwilini wangu maana nilihisi mwili mzima ukisisimuka, na miguu kuishiwa nguvu.

Usiuone huu mwili ukajivunia kuwa mimi nina nguvu, mimi sina matatizo, kitu kidogo tu, hasa mawazo, hasa mshituko, hasira, au kuchanganyikiwa, kinaweza kikaubadili mwili wako na kuwa kitu kingina kabisa, ndio maana unakuta mtu anashikwa na shinikizo mara moja,….na hata kiharusi, wakati alikwua hana tatizo lolote, …..hai hiyo ilikuwa kidogo inipate.

Mawazo ya haraka yakanija, nikachukua khanga yangu na kumfunika yule mwanamke, ili kama mtu akiingia usigundue kwa haraka kuwa kuna mtu kalala, au…, na kwa haraka nikageuka kumwangalia babu yako, kama anaweza kutoa msaada wowote, lakini yeye alikuwa kasimama, kashikilia panga, mwili mzima ukimtetemeka kwa hasira, na nilijua kama huyo mwanamke angeamuka, na kuanza maneno yake, ….angejikuta akicharazwa mapanga.

Kwa haraka bila kumjali babu yako nikakimbilia mlangoni, nia ni kumuwahi huyo aliyepiga hodi asiweze kuingia ndani, kwani kama angeliingia, mengi yangelitokea, ama kutoka kwa babu yako, au vyovyote vile kusingelikalika humu ndani, na lolote lingelitokea, kwahiyo niliona niepushe shari kwa haraka iwezekanavyo

Nikaukabili mlango, huku nikiomba msaada wa mungu, aniepushia balaa hilo, na kunipa busara ya kuongea na huyo mume wa huyo rafiki yangu,nikafungua mlango...na macho kwa macho, nikakutana na mwanaume. Ilionekana alikuwa kasimama hapo mlango kwa muda kidogo, sasa sijui alikuwa kasikia nini, lakini sikujali kwa muda huo.

Kitu nilichogundua kwa haraka, ni kuwa huyo jamaa alikuwa tayari anataka kufungua mlango, na alionekana kama alikuwa akisikiliza ….kwani aliponiona alikuwa kama kashikwa na mshituko, akaniangalia kwa macho yaliyojaa udadisi, na hata bila kusalimia akauliza;

‘Mke wangu nimesikia yupo hapa, nataka kuonana na yeye…’akasema huyo mwanaume huku akikunja uso kwa hasira, na mimi akili ikafanya kazi haraka, hasa kutoka na kauili yake ya kusema `nimesikia yupo hapa, kumba hana uhakika ….’nikamjibu.

‘Mke wako hayupo hapa, aliondoka hapa muda mfupi uliopita, nahisi mumepishana kidogo,..’nikamdanganya, na yule mwanaume akapepesa macho ya kuonyesha mshangao, …akabenua mdomo wa tabasamu la kukebehi, halafu akageuka huku na kule kama anakwepa kuniangalia usoni moja kwa moja akasema;

‘Haiwezekani,….wewe mwanake, unataka kusema nini… nimeambiwa bado yupo humo ndani kwenu,….’akasema na kujaribu kuangalia ndani kupitia kwenye mpenyo wa mlango, lakini haikuwa rahisi kwani nilikuwa nimesimama kati kati ya mlango, huku nimeshikilia mlango, ili usifunguke wote.

‘Na kwanini hunikaribishi ndani, ndio adabu zenu hizo….’akasema.

‘Kwasababu kama unavyoniona,..nipo peke yangu, siwezi kukukaribisha mwanaume ndani , wakati mume wangu hayupo….na..hata hivyo karibu, ….’nikasema huku nikivunga, ial sikusogea pale niliposimama.
Akiwa ameshikwa na kitu kama mshituko wa kushangaa, akukunja uso kuashiria kukasirika,na kama vile haamini kile ninachomwambia, na huenda alijua kuwa namtania, akawa kama anageuka kutaka kuondoka, lakini hakuondoka, akaguna kiume….kama anataka kumeza fundo la hasira, halafu akasema;.

‘Wewe mwanamke, mimi sio mtu wa msihara sihara, mnanijua nilivyo, na unanifahamu jinsi gani nilivyo na uhasama na mume wako, sitaki hili liwe chanzo cha kufumua hasira yangu dhidi yake, sitojali kuwa wewe ni mwanamke,….nitakufumua, niambie huyu mke wangu yupo wapi…. mimi  nina haraka…. , nataka kwenda safari zangu, najua kabisa yumo humo ndani, …kama mumepanga na yeye kuwa useme hayupo, ohoo…..’akasema na sikutaka kumpa mwanya wa kuongea sana, nikasema;

‘Ndio alikuwemo humu kwangu sitakati, ….alifika hapa kusalimia, …., tukaongea kidogo, halafu baadaye,….  akaondoka kwa haraka, akidai anakuja kukuwahi…’nikamdanganya na kauli yangu iliozaa matunda, maana aliniangalai mara ,moja usoni, na akageuka kutaka kuondoka, lakini hakuondoka.

Moyoni nilikuwa niomba dua, ….nikiomba huyu mtu aondoke, maana …..nimeshadanganya na hili litaweza kuleta madhara baaadaye, haya akiondoka,  kwani akijua kuwa kama litatokea lolote akajua kuwa nilimdanganya, moto wake utakuwa mkali sana. Huyu jamaa ni miongoni wa wanakijiji wanaoogopewa kwa kuwa na hasira na haraka haraka.

Alishagombana na mke wake, akampiga karibu ya kumuua, na walipoamuliwa akaingia ndani na kuchunkua panga, hapo kile aliyekuwepo alipata jeraha, na mkewe ambaye kwa muda huo alikuwa hajiwezi, kwa kipigo alichopata, akajaribu tena kumsihi mumewe, na hapo, akawa kajichongea, akajikuta na yeye anakatwa mapanga, na aliponea chupuchupu, kwani hadi leo ana makovu mawili ya usoni, sehemu ambapo alishinwa nyuzi kutokana na kukatwa na mapanga, hajali yeye hasira zikimpanda anaweza hata kuua

Huyu jamaa alishawahi kugombana na mume wangu wakiwa kwenye ulevi wao, na ugomvi wao uliishia kukatana mapanga, na hata walipofikishwa mbele ya mjumbe, jamaa huyu alikuwa hashikiki, hadi pale aliposhikwa na wanaume watano wenye nguvu, na ni baada ya kupambana nao kwa muda mrefu, na aliapa kuwa siku akipata mwanya wa kugombana na mume wangu, atautumia kuhakikisha anamtoa roho yake.

‘Mimi huyu mtu namdai pesa nyingi, kabla hajaiba na kukimbia, sasa karudi anakana kuwa nilikuwa simdai….sasa sikilizeni, hizo pesa zisitaki tena, …nitahakikisha nazipata kwa kumharibu sura yake, na siku yeye au familia, yake wakinikorofisha kidogo, ….hasira zangu zitaishia kubaya….mnanijua mimi …katika familia yetu huruhusiwi kuapa uongo…sasa naapa siku wakinikorofisha yeye au mkewe, ….nitaitoa hii hasira kwao…na mnajua ni nini nitakifanya…..’akasema baada ya kusuluhishwa.

Mume wangu waliposuluhishwa na huyu jamaa alijitahidi sana kutokugombana na huyu jamaa, kwani kweli anamfahamu sana huyo jamaa, maana wamekua pamoja, na historia ya familia yao anafahamu vyema, kuwa wao wakiapa kuwa watafanya jambo fulani, ni lazima walifanye, wana imani kuwa ukiapa uongo, basi wewe sio mwanaume.

Yule jamaa akageuza kiwchwa kwa haraka na kuniangalia, akiwa keshakunja uso , uso wa ugomvi, akakunja ngumi, kama kujizuia hasira zake, halafu akatembea hatua mbili mbele, akasema;

‘Haya, kwa vile nina haraka zangu, sitaki kubishana na wanawake….lakini ….haya sisemi mengi,….ninakuamini shemeji, hujawahi kunidanganya, ila mume wako siwezi kumwamini hata siku moja, …. nilimwambia mke wangu asiwe karibu na familia yenu, maana hatuna mahusiano mazuri, na sitaki mimi nionekane mkotofi kwenu,….haya…mimi nakwenda,…’akasema na kuanza kuondoka lakini ghafla akasimama na bila kugeuka akasema.

‘Huyu mwanamke atakuwa kapitia wapi,…mimi nilimwambia kuwa nina safari, na sikutarajia angelichelewa kiasi hicho, huyu mwanamke kwa umbea…naona kasahau hasira zangu, na kwanini kabadilika kiasi hiki…., yaani kila nyumba anataka apite kumwaga sera zake za kuamini mambo ya kishirikina…..sasa kaenda wapi……' akawa anaongea kwa sauti ya hasira, na akasema;

'Hili nitahakikisha nalimaliza leo hii, na ninaweza kuiharisha hii safari kwa ajili yake, na nikifanya hivyo…..mtasikia….na shemeji hatujamalizana, kama wewe ndiye unayemuharibu mke wangu, leo hakutakalika hapa kijijini....’akawa anachezesha mguu, haku kakunja ngumi, kuashiria kuzuia hasira.

'Sio kweli shemji,...'nikasema, kumbe nisingesema kitu, nilitakiwa nikae, kimiya,wao wanaamini kuwa mwanaume akiongea huruhusiwi kujibu kitu, mpaka upewe idhini ya kuongea, ..hapo nikawa nimeharibu, maana...

Na mara akageuka na kuanza kunijia pale niliposimama, uso ulikuwa umeshambadilika, na aliponifikia tu, akasimama,…nilishaanza kuetetemeka, na hata hoja ndogo ingelitoka, lakini nikajipa moyo na kumuomba mungu, huku nikisema kama angeliinua mkono wake, ningelimuita babu yako,….babu yako ni miongoni mwa wazee waliokuwa wakiheshimiwa sana…

Akasimama mbele yangu huku anatetemeka kwa hasira, akaguna na kwa haraka akgeuka na kuondoka, na mimi nikasema;

‘Shameji huenda mke wako sasa hivi yupo nyumbani anakusubiria….kwanini nikufiche’nikasema na yule jamaa akaondoka akionyesha kukasirika, na nilikuwa na uhakika kuwa akifika huko kwake, halafu amkose,basi anaweza akarudi kwangu kama mbogo aliyejeruhiwa, nikaomba mungu mambo hayo yaishe yasije kuwa makubwa mkononi mwangu.
***************

Nikakumbuka jinsi babu alivyonimabia kuhusiana na huyo mwanamke aliyeanguka ndani kwa mama yangu, na wakati ananismulia haya, alikuwa akikunja uso kuonyesha hasira, ….akasema;

Nilikuwa nimezamiria kupambana na wale wote walioshiriki kumfanya mke wangu azaniwe ni mchawi, kwani nilijua kabisa hizo zilikuwa ni fitina na umbea wa wale wasiompenda kwa sababu zao wenyewe, na nilipoona watu wanaanza kupata madhara, …..nilijua kweli sasa haki itatendeka.

Nilipofika ndio lile vugu vugu la wale vijana, kupatwa na mdhara, lilikuwa limeanza, na sikuwahi kwenda moja kwa moja, kwenye makazi niliyokuwa ninanishi …nyumbanii kwa mama yako, nilifikia eneo langu ambalo kwa muda huo lilikuwa likiendelea na ujunzi, na hapo, nikaweka makazi yangu ya muda, kabla sijajipanga vyema kupambana na hawo waliosababisha kifo cha mke wangu.

Hasira zangu kubwa zilikuwa kwa wale vijana ambao walikuwa wakijifanya walinzi wa kijiji, na kumbe walikuwa nyuma ya huyo wanayemuita `mtaalamu,..’ na habari za kuungua kwa nyumba yake, na yeye mwenyewe kupotea, zilikuwa zimesambaa kwa haraka sana, ……nikajua sasa mambo yameiva, iliyobakia ni kusafisha jina la mke wangu.

Nilifika eneo la nyumba ya yule mtaalamu, kwani kulikuwa na msiba mwingine, kwahiyo nikaona nikajionee mwenyewe ni nini kimetokea, na hapo nikamuona mmoja wa wale vijana akiwa amelala katikati ya sehemu ile iliyokuwa na nyumba ya huyo mtaalamu, sehemu hiyo ilikuwa kama imesakafiwa.

Nikasubiri kidogo kuskiliza watu wanaongea nini, kwani kila mmoja alikuwa akiongea lake, wengine ambao bado walikuwa waumini wazuri wa huyo mtaalamu, walisema hawoo vijana huenda walikosea miiko, ndio maana yamewakuta, hawo na huyo mtaalamu, aliamua kuhama hapo,na hakutaka makazi yake yabaki kama yalivyo, ndio maana akaamua kupaunguza na moto.

Wengine walidai kuwa huenda mizimu imekasirika , wengine walikuwa wakisema ni malipizo ya wale watu waliodhulumiwa nafsi zao…ilimradi kila mmoja alikuwa akiongea lake.

Haraka nikarudi kwenye makazi yangu ya muda, sikutaka kurudi kule nyumbani kwa mama yako, maana nilikuwa na mambo yangu ya kufanya, na nisingelipanda kumuhusisha mama yako. Lakini baadaye wazo likanijia , nikukumbuka kuwa niliondoka bila kuaga, na huenda wazazi wako watakuwa wamehangaiak kunitafuta , nikfika  nyumbani kwa mama yako, kwa nia ya kumwambia nipo, asisumbuke kunitafuta.

Na nilipofika hapo, nyumbani kwa mama yako, ndio, mara nikasikia sauti za watu wakiongea, nikajua ni mama yako anaongea ni mgeni, ….mara nikasikia maneno yaliyoniumiza moyo wangu…

‘Na haya yote ni uchawi wa huyo mwanamama wenu, hamjaushughulia, ….unakumbuka alivyokuambia yule mtaalamu, …wewe ukapuuzia, ….mtoto hajambo sasa, lakini akianza kuumwa na yeye mtatafuatana, sasa hivi ni zamu ya mumeo…..hangaikeni, huyo mwanamama, kaondoka lakini mtaondoka naye,….alikuwa mwanga kiukweli kweli…nawaambia ukweli, huyo atawamaliza wote..’

Mkononi nilikuwa nimeshikilia panga,…nilijikuta nikitetemeka mwili mzima, hasira zikanipanda, na sikutaka kuendelea kusikia zaidi, bila kupiga hodi nikausukuma mlango na kuingia ndani, na jicho langu la kwanza likakutana na huyu mwanamama….

`Ahaa, huyu ndiye mbaya wangu, kwanza nilikuwa namtafuta siku nyingi, ni mchonganishahi, mkubwa, bila kumuondoa hapa kijijini hakutakuwa na amani,..'nikawa nasema kimoyomoyo, huku panga likiwa tayari linaanza kuinuliwa, huku nikisonga mbele, .....

Akaniona, na macho yetu yalipokutana, akahisi hatari,...nilimuona akionyesha kuogopa, na alitaka kuinuka lakini mwili wake ulikuwa kama umekufa ganzi, …na wakati huo mama yako alikuwa kanipa mgongo, kwahiyo hakugundua kuwa ni mimi niliyeingia....

********

Mama akaendea kuongea;

Nilipohakikisha kuwa yule mwanaume, keshaondoka, kwa haraka nikarudi ndani, na nilipofika, nilimkuta babu yako, ndio anamsogolea yule mwanamke, na panga likiwa limeinuliwa juu, na yule mwanamke , rafiki yangu alikuwa kapiga magoti, huku kainua mikono juu, akiomba msamaha..…

NB: Hapa hata mimi naogopa kuendelea...kidogo lakini kikubwa....., dola na muda umekwisha tukijaliwa tutaendelea sehemu hii....

WAZO LA LEO: Tunapokuwa na masahibu yanayoweza kutupandisha hasira, yawe ni mauzi, ugomvi, kuibiwa, kufumaniana …..na hata kufanyiwa mabaya ambayo yanaweza hata kuleta vifo, kwanza inabidi tutulize hasira zetu, kwani shetani hapo hachezi mbali,….

Tukishatulia na kuyakabidhi hayo kwa mola wetu, kinachofuatia ni kututumia hekima, kwa kupambanua ukweli wa hali halisi, kwani huenda hilo tukio lilikuwa na sababu ya kutuashiria jambo jema, lakini kama tutalichukulia kwa hasira za haraka, linaweza likatutia hatiana, na kutupeleka kubaya zaidi. Tukumbuke kuwa hasira mara nyingi huleta hasara.


Ni mimi: emu-three

Friday, May 17, 2013

Kipaji ni rasilimali aliyokujalia muumba wako



Unapopanda mche au mbegu kwenye ardhi, unatarajia mavuno ambayo yatakuwa mbegu kwa mavuno mengine. Lakini mavuno hayo yanatategemeana na jinsi gani ulivyoiboresha hiyo ardhi, na mazingira mazima ya eno hilo.

Kwa utaalamu wa kilimo, mimea mbali mbali, ina stahili yake ya udongo, ndio maana kahawa ya kagera haistawi vyema Kilimanjaro, japokuwa zote ni kahawa. Mahindi na mharage yanahitaji aina fukani ya udongo ili yazae vyema, japokuwa sasa hivi kuna utaalamu wa kuboresha ardhi, lakini kama huo uboreshaji utakosekana, basi ina maana mazao hayo yaliyopandwa kwenye udongo usiostahili hayatastawi vyema.
Wakati nikiwaza hili nikajikuta nikiwazia watoto wetu,….nikaangalia haya matukio yanatokea katika dunia yetu hii, nikakumbuka usia wa babu yangu.

Wajukuu zangu, watoto wa leo, yaani nyie, ndio mtakaokuwa chachu ya amani kesho na kesho kutwa, mjue msipojiweka sawa, kimaadili, mkakazania elimu yenu, mtarajie mavuno mabaya baadaye . Ni sawa na kama vile tunapanda mbegu ya mahindi mahali ambapo, hapana mbolea 

…..Na hata kama pana mbolea, lakini bado tumepanda kwenye udongo usiostahili….leo mlitakiwa msome kwenye shule zilizo na vifaa vya kisasa ili mjue sayansi muwe madakitari, lakini wapi…hata chaki ya kuandikia hakuna….tutafika kweli’

‘Lakini wajukuu zangu msikate tamaa….kama mnajitambua wenyewe, na mnajua nini kipo mbele yenu, msikate tamaa, sisi hatukata tamaa, ndio maana mumezaliwa nyie….cha muhimu sana tambueni vipaji vyenu vya kitaaluma vitawasaidia sana….’

Ni kweli kila mtu amejaliwa kipaji chake, huenda hilo watu wengi hawafahamu, inawezekana vipaji vikalandana, hiyo sio tija, lakini cha muhimu kwanza ni kukitambua kipaji ulichobarikiwa nacho ambacho ukikitambua vyema, utaweza kufanya jambo fulani kwa uwezo mkubwa, kuliko mwingine ambaye hana kipaji hicho. Kuna vipaji vya kujifunza, hilo hatukatai, lakini vipaji vya kujifunza, mtu hawi na wito nacho, kwake yeye ni sehemu ya kukidhi matakwa fulani tu.

Wakati watu wanahangaika kutafuta ni kwanini watoto wetu wanafeli mitihani,…elimu inazidi kudorora, na kujikuta tukilaumiana kuwa kwanini watoto wetu hawafanikiwi kwa kiasi kikubwa, nafikiri pia tungeliliangalia hilo la vipaji kwa watoto wetu, kama sehemu mojawapo yakuwezesha kuboresha elimu za watoto wetu kwa kiasi kinachotakiwa.

Ili kulitambua hili kwa mapana, chukua watoto kadhaa wafundishe hesabu kwa mtizamo sawa, jitahidi sana somo hilo lieleweke kwa kila mmojawapo, utagundua kuwa kati yao kuna watakaoelewa zaidi yaw engine na wengine wanaweza wasielewe kabisa. Sasa je utasema hawa wasioweza kuelewa kabisa au wameelewa kidogo, hawana akili, hapana, kila mtu anakili,…, lakini ni kuwa taaluma hiyo wanaojifunza sio kipaji chao.

Ni kweli ni muhimu, kila mwanafunzi akajifunza karibu kila kitu, (kila somo), maana maisha yetu ni kila kitu, huwezi ukasema nisisome kabisa somo fulani, mfano hesabu kwasababu sio kipaji changu, lakini maisha yetu yanakuhitaji kujua hesabu, ili uweze kwenda na maisha ya kawaida, kuna mambo yatakuhitajia kujua hesabu,kiinhereza, sayansi jiografia nk …., ndio maana kila mmoja anatakiwa angalau ajue kila somo kwa manufaa yake ya baadaye. Lakini kwa muda gani?

Tatizo hapa, ni jinsi gani ya kutambua vipaji vya watoto wetu toka utotoni, na je vipaji hivyo vitawekwa kwa madaraja gani, kwani tukizungumzia vipaji, tunazungumzia kwa lugha pana, yaani kwa ujumla wa maisha yetu….kuna vipaji vya michezo, vipaji vya kitaaluma na vipaji vya kiutendaji, vyote hivi vinatofautiana kati ya mtu na mtu…

Shule za awali zingelikuwa sehemu muhimu ya kutafuta vipaji hivi,…na kumbukumbu za mtoto huyu zianze kuhifadhiwa hapa, ili akifika shule ya msingi, walimu wanakuwa wakimfahamu mtoto huyu mapema, na itakuwa kwake rahisi kumfuatilia kwa karibu, kwa vile atakuwa keshajulishwa umakini wake toka huko awali na yeye ajue vipi atamkazania huyu mtoto zaidi , ili aweza kuendana na mitaala.

Hebu tuulizane vyema, kuna kumbukumbu gani mtoto wa chekechea anakwenda nazo na kukabidhiwa mwalimi wa shule ya msingi, kuwa huyu alikuwa vipi kwenye masomo yake ya awali. Hili halipo,….na halikadhalika kuna kumbukumbu gani za mtoto wa shule ya msingi anakwenda nazo sekondari , ili mwalimu wake ajue ni vipi mtoto huyu alikuwa….sina uhakika kuwa haya yapo. Sisi tunachofanya ni ule usemi wa kiingereza…`try and error’….au kubahatisha.

Zama hizi ni za kitekinolojia zaidi, kumbukumbu za watoto zinaweza kuhifadhiwa kwenye mitandao, siku hizi mitandao ipo wazi, ni swala la kutilia maananitu. Tukaondoa ubinafsi na kuwekeza kwenye elimu, tukatumia rasilimali za madini, kwa ajili ya elimu ya watoto badala ya kununua magari ya kifahari. Hili linawezekana,….

Kama tutaamua kuwa elimi ni muhimu kwa watoto wetu na vizazi vyetu, sio tu kwa familai zetu, bali kwa taiaf zima, na tukawa na mipangilia thabiti ya kuhifadhi haya, kwa ajili ya baadaye tunaweza kabisa. Na hili pia litatusaidia kupata viongozi waadilifu, maana kumbukumbu hazijifichi, ilimradi ziwe zinahifadhiwa kwa umakini na kwa usiri unaostahili kama kumbukumbu binafsi zinavyohifadhiwa, hadi hapo zitakapohitajika. 

Hili nalo tutahitaji wafadhili. Au kwa vile , huenda, hata ukiweka amira halitaweza kuhumuka tukapaat cha juu,…haya tusubiri hadi wenzetu watakapolala, huenda na sisi tutaamuka, na sijui labda ndio itakwua miwsho wa dunia. Twajidanganya tukizania mtoto ni mtoto wangu wa mwingine atajua mzazi wake.

Tunashinda kujua kuwa matatizo yanayoikumba dunia sasa hivi ni kwasababu ya kukwepa majukumu, kuwa kila mzazi ni mzazi wa kila mtoto, ubinafsi umetutawala, na kujiangalia sisi,…na wenyewe ndio sisi….au sio. Moto ukiwaka , wa majanga, matatizo, tujue chanzo ni sisi wenyewe…

WAZO LA LEO: Usikate tamaa katika maisha, kila mtu anacho kipaji chake ambacho akikitumia vyema kinaweza kuwa mtaji wa maisha yake. Tusibweteke kwa kuiga yale yawenzetu kwa vile wao wamefanikiwa zaidi, tukazania huenda na sisi tukifanya hivyo tutafanikiwa kama wao. Inawezekana mkawa sawa na yeye kwenye vipaji,….hilo hatukati, ni sawa kabisa, kama ni hivyo basi,jitahidi uwe kama yeye, au zaidi. Tatizo hap ni je umeshajichunguza na kugundua kipaji chako kipo kwenye Nyanja ipi, anza leo kukitafuta kipaji chako, ukikigundua, utafanikiwa kwa kiasi kikubwa, usikate tamaa.
Hebu msikilize LUCK DUBE HAPA 

Ni mimi: emu-three

Thursday, May 16, 2013

WEMA HAUOZI-8



Siku hiyo niliamua kwenda kuitembelea iliyokuwa nyumba ya huyo mtaalamu, ilikuwa imeteketea yote kwa moto, na hakikubakia hata  kitu kimoja, …yalikuwa ni majivu matupu yaliyokuwa yamebakia. Na kwa vile nyumba za kijijini nyingi zilijengwa kwa miti, zikakandikwa kwa udongo na kuezekwa kwa makuti, moto ukishika, inaungua haraka sana.

Siku zilizofuata kukawa kunanyesha mvua, nilipopita pale siku nyingine niliona yale majivu yote yamegendamana kwenye ardhi kama vile kumpigwa sakafu ya udongo ulaya…na baada ya siku tatu, majani yakaanza kuota kuzunguka lile eneo. Ilikuwa ajabu kabisa, maana pale kati kati, palibakia hivyo hivyo bila kuota majani, huku pembeni yake majani na miti vikiota kwa kasi ya ajabu.

Wiki kadhaa zikapita, na watu walianza kulalamika kuwa wakipita eneo hilo, wanasikia kama sauti za watu wakiongea na kukipiga ukulele, au kunatoka sauti zisizofahamika vyema.

‘Hiyo ni mizmu ya huyo mtalaamu, nini ….?’watu wakawa wanaulizana

‘Kama ni mizumu yake, je haitaweza kutuathiri na sisi?’ mmoja akauliza

‘Inabidi tuwaone wazee wanaojua mambo hayo, maana eneo hili sasa halipitiki…mimi mwenyewe nilipia jioni jioni nikasikia kama watu wanaongea, na vyombo vikigongana, na mara nikasikia kama sauti ya kilio cha mtoto mdogo…’akasema jamaa mmoja, na watu wakamwangalia wakiwa na wasiwasi.

‘Kama ni hivyo, kuna jambo….ni heri tuhangaike, kwanza ni bora tuwaone wazee wa hapa kijijini,….’wengine wakashauri hivyo, na wengine wakapuuzia, na kweli baadhi yao, waliwaendea wazee na kuomba ushauri, na wazee walipoulizwa, walisema bila kuficha;

‘Inaonekana huyu mwenzetu alikuwa na mambo mengine ambayo sio ya kawaida. Tunakubali kuwa alipewa karama ya utibabu, lakini yeye alichanganya hayo na mambo mengine yasiyo ya halali, na hayo mnayoyasikias ni mambo yake mabaya….’akasema mzee mmoja.

‘Na yanahitajika kuondolewa haraka eneo hilo kwani lipo kwenye himaya za makazi yetu, mmiliki wake hayupo, ni nani wa kuyadhibiti hayo madude, hatujui yanakula nini, au yanafanywaje ili yasihangaike kwenye makazi ya watu wengine au kusambaa kwenye njia tunazopita…’akasema mzee mwingine.

‘Na kama ni madude,…., yanaweza yakawakumba watu na kuleta athari…na nahisi huenda kuna jambo linaweza kutokea kama hatutafanya juhudi za haraka..’akasema mzee mwingine

‘Sasa wazee wetu tufanyeje?’ akaulizwa.

‘Inabidi watu wafunge safari kwenda huko milimani na kuwapata watu wanajua mambo hayo….kwa hapa kwetu mtu tuliyekuwa tukimtegemea ndio huyo mtaalamu, sasa keshaondoka. …’akasema mzee.

‘Na ninavyo mimi kaondoka kwa mabaya, tofauti na enzi zetu, kwani mtu kama huyo alitakiwa kuwa muadilifu,… lakini mlimuonaje maisha yake yalivyokuwa,…yeye tamaa ilimzidi akakiuka masharti ya kazi kama hiyo…’akasema mzee mwingine.

‘Mimi niliwahi kumkanya, …lakini aliniona mbaya, tukawa hatusalimiani,…na ilionekana wazi kuwa mambo yake mengine alikuwa akifanya kwa maslahi yake, …sio wote aliokuwa akisema ni wachawi,walikuwa ni wachawi, wengine aliwasingizia pale alipoona wanaingilia maslahi yake….sasa hatuju ni kwanini hili limetokea, lakini nahisi ni mabaya yake ndiyo yaliyomuangamizai…’akasema huyo mzee.

Watu wakaanza kutishika , na kuogopa kabisa kupita eneo hilo, wakijua wanaweza kukumbwa na hayo waliyokuja kujua kuwa ni mashetani ya huyo mzee. Wazee nao wakahangaika hadi kwenda huko milimani, na waliporejea walisema hawakuweza kufanikiwa, kwani inavyoonesha ni kuwa walishachelewa, iliyobakia ni kusubiria tu.

‘Cha muhimu eneo hilo litengwe kabisa….’akashauri huyo mzee, na kweli eneo hilo likawa nje ya mipaka ya wanakijiji, ndio maana hadi leo unaliona hilo eneo likiwa limebakia msitu, na ukiingia ndani ya huo msitu, kuna sehemu ipo pakavu kabisa…..ndio asili ya jina hilo la mzimuni….’babu yake akasema.

********

Niliendelea kukumbuka yale aliyoniahdithia babu, ambayo mengine mama hakuweza kunihadithia a, huenda aliogopa kunisimulia, nisije nikatishika, ….nikakumbuka jinsi babu alivyosema siku ile alipokuwa akinihadithia;

‘Mimi nikarejea nyumbani kwa mama yako nikisubiria nyumba yangu ijengwe, na ndoto zile mbaya za kutisha zikawa zimepotea kabisa,…hata hivyo sikuweza kuwa na amani, bado nilikuwa nikimuwaza mke wangu, na jinsi gani ya kuwapata hawo waliomfanyia hivyo.

Kulianza kutokea maajabu hapo kijijini, kila siku kulizuka jambo la kustaajabisha, na mambo hayo yalionekana kufanana. Vijana walianza kufa ovyo, na vifo vyao, kama nilivyosema awali, vilikuwa vya aina moja…nikajua ubaya umeanza kulipizwa….

‘Hawa inasadikiwa ndio waliokuwa vijana wa mtaalamu, hawa ndio huyo mtalaamu alikuwa akiwatuma kufanya mauaji kwa wale wanaosadakiwa kuwa ni wachawi…na kufuatilia mambo yake.’watu wakawa wanasema.

Hawo vijana, mmoja mmoja akawa anashikwa na kitu kama mshituko, halafu anakuwa kama kachanganyika, au kupandisha mashetani, na kuanza kukimbia ovyo. Alipoanza wa kwanza, watu walizania huenda ni hayo mabangi wanayopenda kutumia vijana, lakini alipofuatia wa pili , watatu , wanne, na wote wanajulikana ni nani, watu wakahisi kuna jambo.

Na cha ajbu zaidi wote walitaabika na hali hiyo ya kuchanganyikiwa, na mwisho wake wanakutwa wamekufa eneo hilo hilo la huyo mtaalamu, mmoja baada ya mwingine. Na siku ya kwanza ya kufariki kwa kijana huyo, ndugu na jamaa wakafika kumtoa pale alipofarikia, na kumpeka nyumbani kwako, lakini ikashindikana, kwani watu walijikuta wakizungukwa na nyuki wengi.

‘Chomeni moto , hawo nyuki wataondoka,…..’mmoja akasema, lakini hakuna aliyeweza kusogea pale, na kila ukiletwa hapo karibu, unazimika.

‘Hili sio la kawaida, inabidi tukawaulize wazee….’mmoja, akasema na wakafuatilia, huko kwa wazee wanajua mambo hayo.

‘Huyo mzikeni eneo hilo hilo,…’akashauri huyo mzee, Na kweli walipoanza kuchimba makaburi, wale nyuki wakawa wanazunguka hewani, hadi walipomaliza kumzika, na nyuki wale wakaanza kuwashambulia, kuashiriwa kuwa waondoke haraka, …

Haikupita siku mbili, hali kama ile ikamtokea kijana mwingine, na yaliyotokea kwa mwenzake ilikuwa hivyo hivyo, na huyo naye wakamzika eneo hilo hilo.

‘Wazee wetu sasa hili ni balaa gani maana vijana wetu wanamalizika…..?’ wakina mama wakauliza.

‘Haya matukio yanaoenekana ni dhuluma ilietendwa na hawo vijana, na inavyoonekana, hawa vijana walikuwa wafuasi wa huyo mtaalamu, kwahiyo waliotendewa hizo dhuluma, walilalamika, na huenda wengine walikwenda kuomboleza kuwa hawow aliofanya hivyo mabaya yawakute….’wakasema hawo wazee.

‘Sasa tufanyeje, maana hali kama hii hatujawahi kukutana nayo?’ wakauliza.

‘Kwanza ni hawo wanahusika kukubali makosa yao, na kwenda kutubu hayo makosa yao kwa hawo waliodhulumiwa, swali kubwa hapa ni je wanajua makosa yao, na hawo waliotendewa hivyo bado wapo hai, kama hawapo hai, ….hatuna la kufanya’wakasema hawo wazee.

‘Oh, sasa tutafanyeje….?’ Wakina mama wenye vijana ambao wanafahamu kuwa vijana wao walikuwa na mafungamano na huyo mtaalamu wakaanza kulalamika na kuhaha huku na kule kutafuta jinsi gani ya kuweza kulikwepa hilo janga.

‘Ubaya unapotendwa, watu wanajionea ni kawaida, na hujiona kama wao ni washindi , lakini unashindwa kufahamu kuwa tunaowatendea huo ubaya ni binadamu kama sisi….wanaumia, na kujiskia uchungu kama sisi, basi dhuluma hiyo haitaisha hivi hivi, mpaka na nyie msikie uchungu kama wao walivyosikia….’akasema huyo mzee.

‘Lakini sisi tulikuwa hatujui,….tulikuwa tukimfuata huyo mtaalamu, kama unavyojua kuwa yeye watu wote walikuwa wakimuamini kwa kila anachoongea….’wakasema hawo watu.

‘Sasa kama mlikuwa mkimwamni kwa kila kitu,….mkasahau kuwa kuna mungu, inabidi mumtafute huyo mtaalamu, …..hakuna la kufanya kwa sasa…’wakasema hawo wazee.

‘Hatuwezii kwenda huko milima kwa watu wema wakatusaidia?’ wakauliza.

‘Wema wao sio wa kudaidia wadhalimu, kwani wakisaidia wadhalimu na wao watakuwa kama wamedhulumu, …hebu fikiria unapomsaidia mwenye makosa, ni nini hukumu yake kisheria,…ni kuwa na wewe unashitakiwa kama msaidizi wa mtenda makosa…’akasema huyo mzee.

‘Wazee tunaomba msaada wenu, nyie ndio wazee wetu, na huenda mambo kama haya yaliwahi kutoeka huko nyuma, je ilipotokea hivi mlifanya nini..?’ wakauliza.

‘Kuna mambo ya kimila yalifanyika, kuna matambiko,….lakini bado kulikuwa na jukumu la kujua kosa na nani waliofanya hivyo, na kwa nani….enzi zetu, watu walikuwa wakweli, kama walitenda kosa, walikiri, na wakatubu makosa hayo kwa waliotendewa…je nyie mnaweza kufanya hivyo?’ akauliza

‘Sisi wazazi tunaweza kufanya hivyo kwa niaba ya watoto wetu..’wakasema hawo wazazi.

‘Hapana, makosa kama hayo yanatakiwa mtu mwenyewe akutubu, …na asichelewe kabla adhabu haijaanza..hivi sasa naona kama mumeshachelewa…..’akasema huyo mzee, na mara sauti ya ukulele unaoashiria masiba, ukasikika kule kule eneo la mzimuni, …

 ‘Je ndio kisasi kimeanza, na ni mbinu gani watatumia, ili kuondokana na janga hilo..?

*****

Mume wangu alianza kuzidiwa, kifua kile hakikutaka kupona, na ikafikia hadi kurudishwa hospitalini na kulazwa, lakini hali yake haikuweza kutengamaa, na ikafikia muda wakashauri arejeshwe nyumbani tu, na hapo tukajua kuwa madakitari wameona uwezekano wake wa kupona haupo tena.

Tukahangaika na tiba mbadala, na ikawa inasaidia kwa muda, lakini baadaye hali yake iliendelea kuwa tete. Na kilichokuwa kikimzidishia zaidi ni kutokana na kutokupenda masharti, Mume wangu alikuwa mbishi sana wa kufuata masharti.

‘Mume wangu huoni kuwa kwa kutokufuata masharti, kama ulivyoelekezwa na dakitari unajiua wewe mwenyewe…’nikawa namwambia mume wangu ambaye kwa muda huo alikuwa kashikilia sigara mkononi.

‘Wangapi wamekufa , hata bila kuumwa,…hata bila kuvuta sigara, hata bila kunywa pombe...kama ni kufa nitakufa tu, … tusisingizie kuwa zifuati masharti, siku yako ukifika uwe umafuta masharti, au hujafuata utakufa tu….kwanza hebu niambie nimekiuka masharti gani ..maana wewe unanifuata futa sana…nikifa una shida gani, nyumba unayo, mtoto unaye…kwanza ndio vizuri umpate mume mwingine asiyeumwa….’akawa anaongea kwa hasira na ilionyesha kabisa kama vile kakata tamaa na kuchanganyikiwa.

‘Umeambiwa usinywe pombe, usivute sigara, lakini wewe hutaki kuviacha hivyo vitu, …huoni hiyo ni sumu ya afya yako…na mume wangu kuumwa ni mitihani ambayo inakufanya umkumbuke mungu wako, ukiumwa, jaribu kutuliza kichwa, achana nay ale yasiyofaa, ili mola wako akusikilize…hayo ya mume mwingine ni mawazo yako, …..’nikamwambia nikiwa namwangalia kwa macho ya huruma.

‘Mimi pombe siachi, sigara nimepunguza kidogooo, japo tatu kwa siku sio mbaya, inanisaidia kuondoa mawazo…..kama nikufa nitakufa tu, kwanza hebu niache….maana walionifunga wameharibu maisha yangu…natafuta mtu wa kuondoka naye, siwezi kukubali kuondoka hivi hivi….yote haya wameyataka hawo wabaya wangu ili nifungwe na hatimaye nipate haya magonjwa mabaya...’akawa analalamika

‘Sasa kwanini wewe uliiba pesa za watu, hujui kuwa wizi ni mbaya, unaweza ukaiba ukaona umeshinda, ukasahau kuwa kwa kumuibia hiyo mtu, umemkwaza sana, huenda pesa hiyo ilitakiwa kumsaidia kwenye matibabu, kula watoto….wewe ukazichukua kulewea….yeye unafikiri atafanya nini, kama anakujua atakufunga tu, na kama hakujui, basi atakushitakia kwa mungu, atakuwa akiomba kwa mola wake,…na hayo ndio malipizo yake…’nikamwambia mume wangu.

‘Wangapi wanaiba bwana, na wanafanikiwa…mimi sio wa kwanza kuiba, sema tu, bahati haikuwa yangu, kwanza ilibidi nifanye hivyo, nimewatumikia miaka mingi, hawanijali, Napata shida, naomba angalau mkopo hawanipi, nikapa ile nafasi, kwanini nisiitumia, sema mjanja mwingine akaniwahi,..huyo mtu ana bahati kweli, maana kapata bila jasho, na matokea yake naumia mimi, sawa…’akashika shavu huku akiiangalai ile sigara ambayo alikuwa hajaiwasha.

‘Mume wangu nakupenda sana, nasikitika kukuona kwenye hiyo hali, kwa kukuonyesha kuwa nakupenda, nyumba nimeandika kwa jina lako kama ulivyotaka….sasa ukifa nyumba itabakia na nani…’nikamsogelea na kumshika begani.

‘Mhh, eti unanipenda, kama ungelikuwa unanipenda tangia mwanzo, usingelipinga na mimi nilipokuambai uandike jina langu, hata hivyo, mimi sitaishi sana, nyumba hiyo itabakia mikononi mwako, lakini nikiwa hai angalau nifaidi heshima yangu….kwasabbau ungeliandika jina lako, ningelizarauliwa….’akasema huku bado akiwa anaiangalia ile sigara.

‘Basi tupa hiyo sigara, maana ukiivuta utaanza kukohoa hapo, hadi utoe vyote ulivyokula….achana na hizo sigara na pombe, ili dawa unazotumia zifanye kazi…’nikamwambia.

‘Umeanza kuniuzi….huku kuumwa, sio mimi wa kwanza, wapo wameumwa kaba yangu, wakapona, na wengine wakafa, sio ajabu mimi nikifa au nikipona,…’akawa anasema huku akianza kukohoa kidogo, na mara akafululiza kukohoa.

‘Tatizo lako wewe ni mbishi sana,…..’nikamwambia mume wangu, ambaye kwa hasira alisimama na kuanza kuondoka. Imekuwa ni kawaida yake, kwani kila ukijaribu kumshauri jambo, mnaishia kwenye malumbano, na akiona umemshinda kwa hoja, anachokimbilia yeye ni kuondoka, kwenda kulewa…ikabidi niwatafute marafiki zake wanakunywa naye wajaribu kumshauri, lakini haikusaidia kitu, akawa ndio anazidi kunywa pombe, kuvita sigara, na mwili ukazidi kuisha,…….

Kuna kipindi kulitokea ubishi wa nyumba tuliyojenga, yeye kwa vile ni mwanaume, alitaka tuandikishe nyumba hiyo kwa jina lake, mimi sikukubali nilijua kuwa nilijenga kwa pesa yangu,..malumbano haya yalileta mgongano mkubwa, mwishowe niliona haina haja ya kulumbana nay eye ndio, nikakubalia nyumba hiyo ikaandikishwa kwa jina lake, nikijua kuwa nyumba hiyo ni yetu wote wawili na mimi nampenda mume wangu.

Baada ya yeye kuondoka, akaja rafikii yangu, tukawa tunaongea hili na lile kubadilishana mawazo, na baadaye akauliza;

‘Nimemuona mume wako akielekea sehemu yake…’ akasema akionyeshea mkono mdomoni kuashiria kuwa mume wangu kaenda sehemu yake anapopenda kwenda kunya pombe.

‘Wala mimi sijui kuwa kaelekea huko….’nikasema nikijifanya kuwa sijui.

‘Lakini kwanini mwanaume huyo hasikii,….ni mbishi sana, namfahamu sana huyu mume wako, kwa ubishi namtolea kofia,….lakini hata hivyo ubishi mwingine hauna maana, haoni kuwa huko kulewa kutamuondoa duniani kabla ya siku zake….’akasema huyo rafiki yangu.

‘Nimesema wee nimechoka…..naona nimuache kama alivyo, maana mwishowe tutagombana, tuihie kushikana, na bahati mbaya nimsukume, iwe ndio kisa cha umauti wake….niambiwe ooh, umemuua mume wako, maana nyie watu hamna dogo…’nikasema kwa utani.

‘Lakini….rafiki twende mbele turudi nyuma,…. hayo aliyo nayo mume wako sio bure…’akasema huku akishika kichwa na kuangalai juu, halafu akaniangalia na kusema;

‘Tatizo lako nikukushauri jambo unachukulia ni mzaha,huyo mwanaume wako usipoangalia utamkosa hivi hivi…na inavyoonyesha huyo aliyemfanyizia, kafanya kazi kweli kweli…maana kakufanya hata na wewe usiwe na akili ya kumgangaikia,….nakuambia ukweli, muda sio mrefu huyo ataondoka….’akasema huku akinikazia macho, sikusema kitu, na alipoona hivyo akasema;

‘Na haya yote ni uchawi wa huyo mwanamama wenu, hamjaushughulia, ….unakumbuka alivyokuambia yule mtaalamu, …wewe ukapuuzia, ….mtoto hajambo sasa, lakini akianza kuumwa na yeye mtatafuatana, sasa hivi ni zamu ya mumeo…..hangaikeni, huyo mwanamama, kaondoka lakini mtaondoka naye,….alikuwa mwanga kiukweli kweli…nawaambia ukweli, huyo atawamaliza wote..’akasema huyo rafiki yangu.

‘Ondoka na mdomo wako mbaya, labda kama wewe ndio mwanga, na unataka kutuondoa, umejuaje yote hayo, kama huhusiki na kumsingizia mama wa watu, ….kwanza wewe bado hujachoka na hayo maneno yako,…umesikia ni kitu gani kinachowapata sasa hivi hawo vijana walioshiriki kuchoma nyumba ya mama huyo na wengine wasio na hatia…?’ nikamuuliza rafiki yangu.

‘Hayo ni maneno ya watu,hawo vijana wamebwia unga wao, na mabangi yamewapanda kichwani, sasa kwa kuwatetea wanasema hivyo, yule mtaalamu mimi namwaminia, hawezi akasema uwongo…mama yako alikuwa mwanga….tena mwanga kweli….’akasema na kukatiza maneno yake, akatulia kama mtu aliyenyamazishwa na jambo la hatari….

Mimi nikamwangalia, na kugundua kuwa alikuwa akiangalia kwa nyuma yangu,…macho yamemtoka na kiwa mdomo upo wazi,… nikageuza kichwa kuangalia ni kitu gani kimemfanya anyamaze vile na kuduwaa kama mtu aliyeona kitu cha kuogofya….na mara macho yangu yakakutana na babu yako;

‘Ba-ba-ba kumbe umerudi, karibu….’nikasema kwa kigugumizi,huku nikiwa nimetahayari, kwani alichosema rafiki yangu ni lazima kakiskia babu yako, na hata mimi sikupenda hiyo kauli yake, lakini sikutaka kuleta migongano kwa watu hawa, nikavunga ili babu yako alainike….lakini

‘Mwambie huyo rafiki yako, mwanga ni yeye mwenyewe,…akome kabisa kumuita mke wangu mwanga..hawa ndio waliopandikiza chuki na fitina….. na leo nataka athibitishe hiyo kauli yake la sivyo nitaufunga huo mdomo wake….’akasema babu na rafiki yangu akainuka kwa haraka akitaka kukimbia, na ghafla akadondoka chini……..na kuanza kujinyonga nyinga, na baadaye akatulia kimiya.

‘Oh, hili sasa ni balaa …..’nikasema, na mara ikasikika hodi , na sauti iliyosikika ilinifanya moyo wangu ulipukwe kwa woga, …..nikageuka kumwamgalia babu yako, aliyekuwa bado kasimama kwa hasira, akiwa hajali ni kilichotokea na wala hakujali huyo aliyepiga hodi ni nani.
Aliyepiga hodi alikuwa ni mume wa huyo rafiki yangu, ambaye alikuwa kalala sakafuni, kimiya, ikiashiria kuwa kapoteza fahamu…

NB: Naona kisa kinasua sua….tatizo jembe hili ninalotumia lina matatizo, mtandao umegoma, sasa inabidi nitafute njia mbadala. Cha kuazima hakisitiri uchi,…

WAZO LA LEO: Tuogopeni sana uzushi, kwani neno moja la uzushi wenye nia mbaya linaweza kuwa baya zaidi ya bomu…uzushi ni sumu ya amani. Watu siku hizi tunaona ni jambo la kawaida kusema uwongo, na kuzua mambo yasiyo na ukweli, eti ili kumzalilisha mpinzani wako, eti ili kumfanya mtu fulani asifanikiwe, eti ili,….. kujiimarisha kwenye masilahi haya ya kidunia yenye muda mfupi tu.

 Jamani, jamani uwongo, uzushi, ufitinishaji, ni mambo mabaya sana katika maisha yetu, lakini sisi tumeona kuwa ni dili, ilimradi tunafanikiwa katika maslahi yetu…huo ni unafiki, tuyaepukeni mambo haya, ili tusiwe wanafiki.




Ni mimi: emu-three

Tuesday, May 14, 2013

WEMA HAUOZI-7



Wakati mama anaendelea kunithibitishia yale aliyonihadithia babu , kila mara akili yangu ilikuwa ikiyakumbuka maelezo ya babu, jinsi alivyokutwa siku hiyo baada ya kupoteza fahamu, akasema;

`Mama yako alinikuta nimepoteza fahamu, na walinihangaikia hadi nikazindukana, na nilipozindukana, nikawa sijiamini, kwani niliyoyaona hadi nikapoteza fahamu, yalikuwa yakiniandama kichwani;

‘Baba kulitokea nini…’akaniuliza mama yako.

‘Hata sijui, ….nahisi ni mauza uza ya kuondoka kwa mke wangu, …’nikamwambai nikiogopa kuongea kile nilichokiona.

‘Baba mbona inaonekana kama ulikuwa ukipigana na mtu , maana vitu humu ndani vimetawanyika, ….?’ Nikamuuliza babu yako na mume akaulia hivyo hivyo.

Nikawa najiuliza mengi, je ina maana ni kweli hayo yaliyonitokea ni kweli sio ndoto, maana kama vitu vimetawanyika, ina maana kweli nilikuwa nikipambana na mtu, nikaanza kukumbuka yaliyotokea ;

********

Babu aliendelea kuelezea na ukumbuke kuwa hizi zilikuwa kumbukumbu nikiwa nipo na mama

Siku hiyo nilipanga kwenda milimani, huko kuna jamaa mmoja ninaye mfahamu, jamaa huyo ana utaalmu wa kupambana na wachawi, na huwa mkimuita kijijini, anawafichua wale wote wenye vitendo hivyo. Nilikuwa nimefikia uamuzi huu baada ya kuona nashikwa na majinamizi ya kila siku.

Basi nilipoamuka asubuhi , nikawa najiandaa, niliamua kuondoka pale tu hawo watoto wakiondoka sikutaka kuwaambia wapi nilipokusudia kwenda, kwani wasingelinikubalia. Nikaweka vitu vyangu tayari, na nikiwa nasubiri, nikajilaza kwenye kitanda change, na mara kausingizi kamang’amu ng’amu kakanijia.

Niliona kitu kama kivuli cha mtu, kikinijia, na huwa kinanitokea mara kwa mara, baada ya kipindi hicho cha kufariki mke wangu. Na nilijua kikinijia kinachofuata ni kukabwa, na nisipojitahidi ninakuwa kama napoteza fahamu kabisa, safari hii sikukubali, nikajitutumua

‘Leo nimekuja rasmi kukumaliza, maana nimekukuanya hunisikii, …’sauti ya kufifia ikasema
Mimi sikumjibu, ikawa kama kwenye ndoto, nikainuka na kujiandaa kwa mapambano. Kile kivuli ambacho sasa kilionekana kam mtu, ambaye sikuweza kumuona sura yake ikacheka kwa dharau;

‘Ndio unataka kufanya nini wewe…’ikasema

‘Nitajilinda na wewe mwanga mkubwa….’nikasema na sauti ya kicheko ya dharau ikasikika, na kilichofuata hapo ni dhoruba, maana hilo lijamaa, lililokuwa na umbao kubwa lilinizoa zoa na kunirusha hewani.

Nilihisi nikidonoka kwenye viti, na maumivu yakajaa mwilini kuonyesha kuwa nimeumia, sikukubali, nikainuka na huku nikikumbuka dua nlizofudishwa za kujilinda na watu hawa. Tatizo ni kuwa japokuwa nilikuwa nazifahamu hizo dua, lakini kila nilipokuwa nikitaka kuzitaja, ilikuwa kama kumbukumbu zimepotea.

‘Nitahakikisha kuwa leo unasalimu amri kwangu….’hilo jitu likasema.

‘Mimi siwezi kukubali kuwa mtumwa wako, kamwe…’nikasema na sikujua kwanini nilisema hivyo, ila inavyoonyesha hilo jitu lilitaka nifanye yale ambayo sikukubaliana nayo.

‘Wewe utakubali tu, wenzako walikuwa wakaidi kama wewe sasa hivi wahaonekani tena, …’likasema hilo dude, na mimi hapo nikakumbuka baadhi ya maneno ya hiyo dua, na kila nilipotamka neno moja lile dua likawa kama linaumia.

‘Oh, ..kumbe ..oh…’likawa linasema huku likionyesha kupepesuka, na kila hatua nikawa naingiwa na kumbukumbu. Nilipoona limeishiwa nguvu, nikainuka, na kuchukua kiti. Huwezi amini, kitu ambacho nilikuwa sikuwezi kukiinua kirahisi, niliweza kukiinua kama chombo kidogo tu, nikambamiza huyo jamaa.

‘Oh, unajifanya kuwa uan nguvu sio…’likasema hilo dubushwa na mimi nikawa nimekumbuka ile dua niliyofundishwa na lile lidubwana likatoweka. Nikayumba na kudondoka chini. Na ndivyo walivyonikuta wazazi wako.

‘Je huyo alikuwa ni nani ananichezea’nikajiuliza pale walipoondoka wazazi wako, na hapo hapo, nikaamua kwenda huko milimani.

*****

Safari ya milimani haikuwa rahisi, maana ilionekana kuwa huyo adui yangu alikuwa akijua kuwa safari hiyo ni ya kumwangamiza, basi akawa ananiandama, kwa kunikabili kwa maajabu ya kila namna, lakini kwa vile nilishazamiria kupambana naye sikuogopa. Na kila aliponitokea nilikumbua hiyo dua, na kila nilipoisoma jitu hilo hutoweka.

Nilifika sehemu yanye mto, na hapo nikataka kunywa maji na wakati naima, nikashitukia nimepigwa na kitu nyuma ya kisogo, kilikuwa kigumu kama chuma, na nikadondokea kwenye maji, na nilipoamuaka nilijikuta nipe kwenye chumba kidogo, huku nikiwa nimefungwa kamba za ngozi ya wanyama mikono na miguu.

Nikiwa nimening’inizwa              hewani na chini kuna mijoka ya kila namna imelala, na mingine ikiwa imeinua vichwa ikiniangalia, kwa uchu, na kila mara kamba ile niliyofungwa ilikuwa ikiisha nguvu, na kuonekana kunisogeza karibu na ile mijoka.

‘Sisi hatuna zaidi ni wewe kukubalina na matakwa yetu..’nikasikia sauti ikisema.

‘Matakwa gani…..hayo. mbona mimi siwaelewi…’nikawauliza.

‘Kwanza achana na huo mpango wako wa kwenda huko milimani kwa huyo muhuni anayeingilia kazi zetu, sio kwamba tunamuogopa sana, …..ila hatutaki kuharibiana katika shughuli zatu, na pili tunakuhitajia uungane na sisi ….’ile sauti ikasema.

‘Na kama nisipokubalina na hayo …?’ nikauliza.

‘Basi hatuna budi, …hawo nyoka wanakuhitaji kwa hamu….na kesho utakutwa ukiwa umeungua kama mishikaki…je umesahau yaliyotokea kwa mkeo, hebu mwangalia kule akiwa katikati ya mto...’ile sauti ikasema na mara nikamuona mke wangu akiwa kati kati ya moto akionekana kupiga kelele ya kuomba msaada.....'hapo moyo wa uwoga, hasira....ukaniingia

Wakati natafakari hayo, akili ikanijia kuwa nikubali kwa kudanganya, lakini mara akili nyngina ikanijia, na nikakumbuka yale maneno ya ile dua, nikaanza kuiomba, na mara nilihisi uvumi mkali ukienea mle ndani ndani, vumbi, na hilo vumbi likawa linazitawanya zile nyoka, na moja moja ikaanza kukimbia.

‘Muueni haraka, msimuachie…’sauti ikasema na mimi sikuacah kuiomba ile dua, huku moyoni nkikumbuka yale mema niliyowahi kuyatenda kwa watu, maana moja ya amsharto ya hiyo dua ni kuwa wakati unaisoma unatakiwa ukumbuke yale mema uliyowahi kuyatenda, na mimi mema yalikuwa mengi hata sikuweza kuyamaliza, na mara nikawa nimesimama peke yangu.

Nikaanza safari ya kupanda milima na ambonde, hadi nikafika nyika, ambayo ndio makazi ya huko ninapokwenda, na hapo, nikahisi nipo kwenye dunia nyingine, maana watu wa huko kwetu wandai kuwa eneo hilo wanaishi watu wasio na dhambi,…ndio maana eneo hilo muda wote lina rutuba, majani yake ni kijani, matunda ya kila namna yalionekana kila kona.

Nilisimama kwa muda nikishangaa eneo hilo, na hapo nikakumbuka zile duwa na nikazisoma na nikaiona ile njia iliyonipeleka hadi kwa huyo mtu niliyemuhitaji, Nikafika kwake, na alioniona alinikaribisha na hata kabla sijamaliza kuongea akasema;

‘Rudi, huko kwenu matatizo yako yamesikilizwa,….ila watu wa kijiji chako wataandamwa na misuko suko, kwa yale waliyoyafanya, wewe utaokoka, kwa maendo yako mema, na kila ukumbuke kuomba na kuyakumbuka matendo yako mema, kwani ndiyo yatakayo kulinda…nenda haraka…

Basi nikareeja huku kwetu, na nilipofika nilisikia taarifa ya moto mkali uliozuka, na kuteketeza nyumba ya yule wanayemuita mtalaamu, na yeye hajulikani wapi alipo, na wengine walidai huenda aliteketea kama alivyokuwa akiwaamrisha watu kuwatekeza wale aliowaita ni wachawi…

*******

Kumbukumbu za babu zikanitoka, na sasa nikawa namsikiliza mama anavyoelezea jinsi ilivyotokea walipokwenda hospitalini

Kilichonishangaza ni jinsi mtoto wetu alivyopona kwa haraka, hata madakitari wenyewe walishikwa na mshangao, kwani tulipofika hapo hospitalini alikuwa na hali mbaya sana, alikuwa amelegea na macho yalishaanza kugeuka meupe kama mtu  asiyekuwa na damu. Alikuwa katapika sana, na joto la homa lilikuwa kali sana.

‘Kwanza inabidi tumpunguze joto la homa….’akasema docta na wakataka kumpiga sindano ya kushusha homa, akatuelekeza kwenda wodini, ambapo matibabu hayo yatafanyika, kwani kwa jinsi walivyomuona waliona ni bora alazwe…wakachukua vipimo vya kwanza lakini cha ajabu hawakuona tatizo lolote, na mtoto akawa amezidiwa, na wakaona ni vyema alazwe kwanza, huku akiendelea na matibabu …

‘Sasa tutafanyaje, …kwani mmoja ni lazima abakie na mtoto,….’nikamwambia mume wangu.

‘Mimi mwenyewe ni mgonjwa, kwahiyo ni vyema nikabakia na mtoto huku nikiendelea kutibiwa…’akapendekeza mume wangu, lakini sikulipenda wazo, kwani matatizo yake yanaweza yakamuambukiza mgonjwa, kwani tulishahisi kuwa huenda ana kifua kikuu.

‘Mgonjwa kweli ataweza kumhudumia mgonjwa….ngoja tuskilizie matibabu yako kuwa watasemaje, ….nikasema na mume wangu akaelekea kwenye matibabu yake. Ni kipindi hicho wakati mume anakwenda chukuliwa vipimo, nikabakia na mttoto, akiwa kalegea, kalala kwenye kitanda cha wodi, na mimi nikajikuta mwili haina nguvu..

Nilishangaa jinsi gani nilivyojisikia vile kwa ghafla, nikawa kama nipo kwenye ulevi wa mdawa, nikawa najitahidi kuizuia ile hali, nikashika macho kuondoa giza lilokuwa liktanda usoni, na hapo nikakumbuka dua aliyonifundisha babu yako, kuwa nikijis vibaya noisome, ….nikaanza kuisoma huku nimeweka vidoke kwenye macho, mtoto akiwa kalala kitandani, nikimsubiria docta aje pale kitandani, kwani alikuwa akiendelea kuhudumia wenzangu na zamu yangu ilikuwa haijafikia.

Ni wakati huo  tunasubiria matibabu ya mume wangu, na nikiwa namsubiria docta afike kwenye kitanda chetu mara nikamuona mtoto akiinuka na kutaka kutoka nje,

‘Unataka kwenda wapi?’ tukamuuliza tukiwa tumeshikwa na mshangao, na wakati huo dakitari wa kumpiga sindano ya kupunguza homa, alikuwa anakaribia kitanda nilipokuwa nimemlaza mtoto. Nikahisi huenda mtoto anaogopa sindano

‘Kwenda cheza….’akawa anaongea kitoto.

Docta akafika na kumshika shavuni, akatugeukia na kutuangalia, na kusema;

‘Mbona hana homa tena..home imeshuka, haina haja, ya kupigwa sindano, ila chukueni vidonge hivi, mumnyweshe, na kama anataka kucheza, tokeni naye nje, halafu baadaye mrejee , ili tumchukue vipimo vingine….’akasema na sisi tukamshika mtoto mkono na kumshusha kitandani, alikuwa amekonda kweli na mwili ulikuwa mdhaifu lakini alijitahidi na kusimama

Basi tukamshusha kutoka kitandani, kwani alishaanza kutembea, na akawa anatoka nje, na sisi tukawa tunamfuatilia kwa nyuma, na alipofika nje,kweli akaanza kucheza, anakimbia huku na kule, na docta alipokuja wodini ambapo tulishapangiwa, akatukuta hatujarudi , akatufuatilia nje, na kutukuta katika hiyo hali.

‘Vipi mgonjwa amepona?’ akauliza huku akimwangalia anavyocheza.

‘Ndio…naona imekuwa hivyo, hata sisi tunashangaa….’tukasema

‘Kuna vipimo nataka kumchukua, mnaonaje tukarudi ndani, huenda dawa alizokunywa zimefanya kazi yake….’akasema docta.

‘Lakini bado, tulikuwa hatujamnywesha hizo dawa….’nikasema na docta akamwangalia yule mtoto kwa mshangao, hata hivyo akasema twende ndani tukachukue vipimo vingine. Na hata vipimo vilivyochukuliwa tena havikuonyesha tatizo lolote.

Docta akatugeukia na kusema;

‘Kama isingelikuwa ni mimi nimempokea awali, ningewaambia kuwa mumemleta mtoto, akiwa hana tatizo lolote, labda kama mlitaka kumchunguza hali yake kwa vile amekonda, lakini mimi mwenyewe ndiye niliyempokea, na niliona hali yake ilivyokuwa mbaya…nashangaa sasa anaonekana mzima kabisa, na hata vipimo vinaonyesha hivyo, je hali kama hii inatoka mara kwa mara?’ akauliza

‘Hapana,…hii ni mara ya kwanza kuonekana kupona, siku zote amekuwa na hali mbaya, joto la homa halishuki, kutapika , hapendi kula kabisa….’nikamwamba docta.

‘Basi huenda ugonjwa umeogopa umekimbia, baada ya mtoto kufika hapa hospitalini…’akasema docta kwa mzaha.

‘Kwahiyo docta, unasema hana tatizo lolote,..na hajapata dawa yoyote…?’ akauliza mume wangu

‘Mimi kwa hali ninayoiona kwasasa kwa mgonjwa, sioni kama kuna haja ya kubakia hapa hospitalini, ….hana tatizo lolote kwa sasa, na kwa jinsi mnavyomuona, …..ondokeni naye, na kama hali itarejea kuwa mbaya, basi mrejesheni….’akasema docta.

‘Sawa docta….’nikasema na docta akamgeukia mume wangu na kusema;

‘Ila kwa baba yake inabidi arudi kesho kuja kuchukua majibu yake…sioni kama kuna haja ya kumlaza, au mnasemaje?.’akasema dakitari kama anauliza.

‘Sisi tunakusikiliza wewe…..’akasema mume wangu ambaye mwili wake ulikuwa umepungua sana, na alikuwa kikohoa mfululizo, na tulijua kabisa, kuwa huenda kaathirika na kifua kikuu.

‘Haina haja ya kumlaza, hali yake sio mbaya sana, ila atakunywa hivi vidonge, ….vitamsaidia huku tukisubiria majibu ya vipimo vyake. Halafu akamgeukia mtoto na kumwangalia kwa makini, alikuwa akionyesha mshangao mkubwa usoni jinsi mtoto alivyobadilika kwa haraka kiasi kile.

Basi mimi na mume wangu tukakubaliana yeye atafute sehemu abakie hapo akisubiria hayo majibu ya vipimo vyake, na mimi na mtoto tukarudi nyumbani.

Niliporudi nyumbani babu yako alikuwa hayupo, na nikawa na wasiwasi sana tukikumbuka kuwa tulimuacha akiwa mgonjwa, kwahiyo huenda kazidiwa kapelekwa hospitali, lakini  hata tulipouliza watu , hakuna hata mmoja aliyefamu kuwa kaenda wapi, tulihangaika huku na kule, lakini hatukupata maelezo yoyote,sisi tukaona tusubiri, kwani hatukuwa na la kufanya.

Ghafla tukasikia mayowe ya watu, na watu wakawa wanakimbilia huko mayowe yalipotokea, na kwa mawazo yangu ya haraka, nikamuwazia babu yako, huenda wamemkuta akiwa kafariki au lolote limetokea ….ikabidi nifuatilie huko mayowe aylipotokea.

Ilikuwa ni maeneo ya yule wanayemuita mtaalamu, nyumba yake ilikuwa inateketea, na moto ulikuwa mkubwa sana….

NB: Je ni nini kilimtokea `mtaalamu..'

WAZO LA LEO : Ni kweli yote yawezekana, wapo walipoona kwa njia hizo, kwa kile tunachoweza kukiita ni miujiza, wapo waliopona kwa imani zao, hata bila kutumia dawa. Na hapo ndipo tunapoamini kuwa mungu yupo na akitaka liwe litakuwa.

 Imani hizi hotofautiana, kutegemeana na dini za watu mbali mbali. Kutofautiana huku kwa imani kusiwe kigezo cha kujenga uhasama uadui na chuki, ….kwani sote ni waja wake muumba, sote ni watoto wa   
Adamu na Hawa, kwanini tusjione hivyo, kuwa sisis ni ndugu wa baba na mama mmoja, kwanini tusipendane, kwanini tusioneane huruma, kwanini tunapenda kutafuta vyanzo vya kufarakana, ambavyo hata havipo kwenye imani za dini, bali ni hisia za uchoyo wetu….vyovyote tutakavyofanya au kujisikia, katu hatubadili hilo, kuwa sote ni wana-wa-Adamu.



Ni mimi: emu-three

Monday, May 13, 2013

Majuto ni mjukuu huja baada ya kitendo



Mtoto mmoja  wa tajiri alijikuta akiokolewa kufa baada ya kunywa sumu, ili apendwe zaidi na wazazi wake akiwa marehemu: Je ilikuwaje,…

Wazazi tuna mtihani mkubwa wa kulea watoto wetu. Unaweza ukalea ukijua unapenda, kumbe unamponda mtoto wako mwenyewe. Tuwe makini sana.

Mzazi mwenzetu huyu, baada ya kuhangaika miaka mingi, baadaye akabahatika kupata mtoto, na furaha iliyoje kwenye familia, wewe fikiria watu walihangaika miaka saba, ili wapate mtoto, ikafikia sehemu wakakata tamaa kabisa. Mungu akasikia kilio chao, na kuwajalia mtoto binti, mrembo kweli kweli.

Hebu fikiria furaha iliyokuwa ndani ya ya hiyo familia, furaha hiyo  ilizidi ile furaha ya mgumba kupata mtoto, au kibogoyo kuota meno…. Wazazi hawa wakawa wanamlea mtoto wao kama malikia. Huduma zote muhimu akawa anapatiwa, hadi akakua akiwa na afya njema furaha na kujiamini kuwa ninapendwa zaidi ya kitu kingine , kwani Kila atakacho anakipata.

Mungu mkubwa, akawajali mtoto mwingine wa kiume. Sasa yule wa kwanza keshakua kidogo, …..ana miaka  minne, kwahiyo mapenzi yakawa sasa yanaeleka kidogo kwa mdogo wake. Hali hii ikawa inamuuma sana dada mtu, yaani kifungua mimba, kwahiyo akawa anajaribu kufanya kile anachoona mdogo wake anakifanya ili na yeye aendelee kupendwa zaidi.

*******

Siku moja mdogo wake alijikata kidole kwa bahati mbaya, wazazi wakawa na pikila pilika za kumsaidia huyo mtoto. Ilimradi mtoto asiendelee kulia, akapakwa dawa, na kununuliwa hiki na kile. Dada mtu akaona hayo matendo, kwani kwa muda huo hakuna aliyekuwa akimjali, hata pake alipoomba kitu, aliona kama wazazi wake hawamsikilizi, wao na mdogo wake tu…kuona hivyo, akaingia ndani kwake, anapolala, akachukua wembe, akajikata mkono.

Tatizo hakujali wapi ajikate, yeye alipochukua wembe kwa hasira akajikata kwenye mkono sehemu ile, yenye mshipa mkubwa, kwahiyo damu ikawa inamtoka kwa wingi sana, na wakati anafanya hilo tukio alikuwa chumbani kwake, na wazazi  wake walikuwa barazani wakihangaika na mdogo wake. Hakuna aliyekuwa na mawazo naye kwa muda huo.

Ilikuja kubainika baadaye kuwa binti hayupo, na walipohangaika kumtafuta ndio wakamkuta yupo chumbani keshapoteza fahamu kutokana na  kupoteza damu nyingi, akakimbizwa hospitalini.
Ilikuwa huzuni kweli siku hiyo kwenye familia hiyo, maana ajali mbili kwa wakati mmoja, na alipoulizwa binti ilikuwaje, yeye akajibu bila aibu kuwa alijaribu kuangalai jinsi mdogo wake alivyojkata ili na yeye asikie maumivu kama mdogo wake, kwa kumuonea huruma, na ili pia nay eye apendwe kama mdogo wake.

‘Hivi huoni ulikuwa unajiua,….?’akaambiwa.

‘Mbona mdogo wangu hakufa, na badala yake mlimpenda kuliko mimi….’akasema.

‘Wewe mjinga kweli kweli…usifanye hivyo tena…..’kauli hiyo aliiweka kichwani, kumbe yeye sasa ni mjinga, hajui, ina maana hapendwi tena….

*********

Hali ile ikaisha, na tabia ile ya kuona mdogo wake anapendwa zaidi ikawa inaendelea kumnyong’onyesha sana. Na siku moja wakati wanapita mitaa ya jirani wakitoka shule ya chekechea, wakakutana na msiba. Pale kwenye msiba, waliwaona wazazi wa mtoto aliyefariki wakilia kwa huzuni kubwa, na yeye akauliza;

‘Kwanini wanalia vile?’ akauliza

‘Kwasababu kipenzi cha hawa wazazi kimefariki, …ndio maana wazazi wa huyo mtoto wanalia hivyo.  Yeye akilini mwake ikamwiingia sana, kumbe mtu akifa anapendwa kiasi hicho, watu wanakuja kwa wingi, wanamlilia, na wazazi wanaonyesha upendo wa hali ya juu.

‘Itabidi na mimi nifanye kitu, ili nife, …lakini nikifa itakuwaje?’ akajiuliza. Hapo akafanya utafiti wa haraka, akaambiwa ukifa unakwenda kuzikwa, na unawekwa  kwenye jeneza nzuri la kifahari….

‘Oh, kumbe….basi nimelewa. ..’akasema na jioni ile akatafuta sumu ya kuulia panya, akaikoroga na kuiweka kabatini.

Muda ukafika, na akijua sasa wazazi wake wote wapo nyumbani, wakiwa na mdogo wake, yeye alikaa pembani, akiwaza alichopanga kichwani, baadaye akaingia chumbani kwake, na kuinywa  ile sumu ….Tumbo likaanza kuuma, maumivi aliyoyasikia hapo, alijuta kwanini alikunywa hivyo…na wazazi wakasikia hilo yowe na kukimblia chumbani kwake.

Yule mtoto alikimbizwa hospitalini, baada ya kupewa maziwa, …aliponea chupuchupu,..na toka siku hiyo hakutaka tena kujidekeza, akajua kuwa kumbe kila jambo lina wakati wake, faida na hasara zake. Na sasa hivi tunaposimulia hiki kisa ni muheshimiwa fulani, akiwa na majukumu ya kulea.

Wanajamii, yaliyotokea kwa watoto hawa, huenda hata sisi tunaojiona ni wazima wazima tunayo kasumba hiyo, kuwa kila wanalofanyiwa wengine , hasa likifanyika huko majuu tunaliona ni bora zaidi, huenda na sisi tukilifanya tunaweza kuwa maarufu na kupendwa na watu. Sio kweli kuwa kila lilofanywa na wengine lina maana kwetu, mengine ni sumu, tunaweza tukajikuta tunajiua wenyewe, na tuombe mungu, itokee bahati, wawepo watu wa karibuni wa kutuokoa.

Tuweni makini sana na maisha yetu, maisha ni kitu chenye thamani kubwa sana, tukichezea maisha yetu, hatari yake ni mara mbili ya hivyo tunavyofikiria, kwani hali zetu ni ngumu, maisha ni magumu, sasa uongezee na hayo matatizo, kweli tutaweza kuji,mudu.

Tujiulize ni nini tunachotaka katika uhai huu mfupi, kumbuka ni  kama jana tu walikuwepo watu mashuhuri, sasa hivi tumeshaanza kuwasahahu, wameshaondoka, na ni nini walichoondoka nacho, hakuna ….sasa tujiulize huo umashuhiri tunaoutaka kwa wanadamu wenzetu , utaweza kutuweka milele,..jibu lake ni kuwa haiwezekani kuishi milele.

Tufanyeni mambo kwa utaratibu wake, tukiwa na malengo chanya, tuache kuiga vitu tusivyokuwa na uhakika navyo, hasa kwenye afya zetu, madawa ya kulevya, kulewa, kuvuta bangi na umalaya, haya yote ni sumu katika maisha yetu. Pia tusikimbilie kuiga mambo ya kisiasa ambayo sio hulika yetu, tuwe makini na ukoloni mambo leo, ni hatari sana kwenye usalama wa nchi zetu, ili mwisho wa siku tuwe na kitu cha kujivunia, sio cha kujijutia.  

Tukumbuke kuwa majuto ni mjukuu huja baada ya kitendo....

NB: Badi nipo kwenye changamoto za hapa na pale, na hili linanipa wakati mgumu kukiendeleza kisa chetu, lakini nitajitahidi tu, tuombeane heri.


Ni mimi: emu-three

Search This Blog

Loading...