Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, November 8, 2023

HURUMA INAYOUMA-Utangulizi


'Docta, huyu sio mtoto wangu, ….’akasema mdada.

‘Sio mtoto wako…! ' Akasema docta kwa mshangao, na mdada akawa kimia

'Kama sio mtoto wako, wazazi wake wapo wapi…au wewe ni nani kwake?’ docta akauliza, akiangalia saa yake, akikumbuka anahitajika kwenda wodini kuna mgonjwa alihitajia huduma yake.

‘Docta mimi ki-ki ukweli, s-sijui, hutaamini lakini sijui….’kauli iliyomfanya docta aweke peni mezani, akaangalia simu ya mezani, akitarajia kuitwa muda wowote.Lakini  kwa kauli hiyo ya mdada ilimfanya ahisi kuna jambo linakuja.

Docta akaangalia saa yake tena,….halafu akamwangalia yule mdada, hakuweza kuona sura ya huyi mdada vyema kwani kwa muda ule huyo mdada alikuwa kainamisha kichwa chini. Docta akamuangalia mtoto aliyebebwa na huyo mdada, halafu akamuangalai  tena yule mdada. Docta alitafuta jambo kwa wawili hao, huku akichelea muda…!

‘Unajua sikuelewi, kama wewe sio mzazi, wewe ni nani kwa huyo mtoto…?’ akauliza docta

‘Docta , naomba tu unielewe, mimi sijui wazazi wake wapo wapi, mtoto anaumwa, ni huruma ..ni…huruma yangu tu….’akasema sasa huyo mdada kwa sauti ya huzuni.

‘Sawa…lakini kwanza unielewe… ili mtoto atibiwe, eeh, si tunahitaji maelezo, eeh….kwanza kadi yake ya kliniki unayo..?’ akauliza docta

‘Si nimekuambia mimi siwajui wazazi wake, …mimi sina kadi yake… na hata sijui kama ana kadi….’akasema mdada

Docta akahema kama kuchoka hivi….akaangalia saa yake ya mkononi, halafu akataka kama kusimama, akaangalia simu ya mezani…ni kama alitaka kuitumia, au kusubiria kuitwa, akamuangalia mdada…

‘Mdada..!, sijui nikuite hivyo,...sijui kama unanielewa, na sijui kama tutaelewana, huyu ni mtoto mdogo, unasikia sana….umempataje mimi sijui eeh…si wewe umekuja naye, au..?’akasema docta lakini mdada alimkatisha kwa kauli iliyomshfanya docta agwaye kudogo

‘Docta,….naomba msaada wako..!’akasema mdada.

 Msaada….!

Docta kusikia hiyo kauli akilini akasema,…yah…kama nilivyowaza, yale yale….!

Lakini docta hakutaka kulichukulia hilo analoliwaza akilini kwa haraka, kwanza akavuta subira, akawa anamuangalia yule mdada,….mdada alikuwa kimia, bado akiwa kainamisha kichwa chini akimuangalia yule mtoto.

‘Msaada…!, unaomba msaada gani…?’ akauliza docta

Mdada aliendelea kukaa kimia,… halafu baadae yule mdada akainua kichwa na kumtizama docta, mara moja paah…halafu akarudisha macho chini.

Docta aliyaona yale macho, yale macho yalikuwa kama  yanalengwa lengwa na machozi. Hata hivyo, docta hakuweza kumuona vyema,…Hata hivyo,Docta machozi ya wagonjwa ameyazoea!

Docta kwa uzoefu wake, akahisi kuna jambo, na hayo machozi sio kama yale aliyoyazoea, hata hivyo,aliona avute subira, hakuwazia tena huyo mgonjwa mwingine wa wodini,…

Kuna jambo kwa huyo mdada na mtoto….Aliwaza hivyo!

Yule mdada sasa taratibu akainua uso, na sasa akamtizama docta, moja kwa moja, macho ya mdada yakakutana na macho ya docta, hapo sasa ndio docta akaweza kumuangalia vyema huyo mdada, na machoni kulikuwa kukavu,

Mhh...…. Docta aliguna hivyo kimoyo moyoni

‘Docta, ninaomba umtibie tu huyu mtoto tujue ana shida gani….hilo tu docta….’akasema huyo mdada, kabla docta hajahitimisha uchunguzi wake wa kuwalinganisha wawili hao kama kuna uhusiano wowote mdada aliongea hivyo .

Docta, kwa haraka akachukua peni na kuandika kitu kwenye kadi, halafu…

Na mara simu ya mezani ikaanza kulia…


NB. Ni tukio nililokutana nalo hospitalini, na diary yangu ikaona sio vyema lipite bure.....Ni kisa cha mdada na mtoto, Je huruma yake iliishia wapi? Je kuna nini nyuma ya pazia.....

KARIBUNI SANA KWENYE SEHEMU YA INAYOFUATA



i mimi: emu-three

1 comment :

San Manuel said...

Your blog serves as a testament to the impact of passion and dedication in content creation.