Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, May 10, 2023

NIMLILIE NANI....

                                                  NIMLILIE NANI....


Nilishika shavu, nikiwa nimeinamisha kichwa chini, kichwa kikiwa karibu ya magoti...nilikuwa hivyo kwa muda, baadae nikainua kichwa kujaribu kuangalia mbele, macho hayakuweza kuona,...macho bado yalikuwa yakilengwa lengwa na machozi, Lakini machozi hayakuweza kutoka tena...moyoni nilishaapa sitalia tena.....

'Sitalia......inatosha....basi...'

Nilijaribu kugeuza kichwa kushoto na kulia...japo ni kwa shida maana shingo ilikuwa kama imekakamaa...kiukweli sikuweza kuona kitu, zaidi ya ukungu, sio ukungu wa hali ya hewa, nahisi ni ukungu wa macho yangu...

Nilihisi mwili kuishiwa nguvu....moyo kwenda kasi, na kichwa kikazidi kuuma, sasa kikiuma kwa kasi zaidi,....ghafla...giza likanijia, na hatimaye ....

'Vipi kaamuka...?
Ilikuwa sauti ya kwanza kuisikia baada ya kupoteza fahamu, nahisi nilipoteza fahamu, au,...sina uhakika!

'Nahisi hivyo, japo hajafumbua macho...'sauti nyingine ikasema

'Usimsumbue kwanza, ngoja nikamuite docta..,usiondoke hapo,....'sauti nyingine ikasema

Hapo nikajitahidi kufumbua macho....

Ni mimi: emu-three

No comments :