Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, August 24, 2009

MGENI WETU MTUKUFU

Ramadhani mosi (22-08-2009)
Muumini aliwaita wanae kwenye chumba cha siri, na mara nyingi akiwaita kwenye chumba hiki anakuwa na habari muhimu yakuwaeleza,
`Natumai nyote mumeshamuona mgeni wetu mtukufu ambaye tumekuwa tukimsubiri kwahamu, natumai nyote mnafahamu nini cha kumkirimu mgeni wetu huyu,natumai kwa ajili ya aliyotuletea nyote mnahitaji awakilishe makisio mema ya utendaji wetu bora, na kufaulu kwema, kwa kusamehewa kila ovu tulilofanya ,ili kwa fadhila hizo tuweze kurehemewa na kusamehewa mbele ya mola wetu.
`Hivyo basi kwa kukumbushana mgeni wetu hataki kukirimiwa kwa chakula mchana,si chakula tu ila kila kinachoweza kupenya kwenye matundu yetu yanayojulikana, na sio tu kila kinachoweza kupenya kwenye matundu hayo bali pia tunatakiwa tusiseme yale yasiyofaa, tusisengenye mbele yake, tupendane, tusaidiane nk. Na hivyo basi sisi wenyeji wake kama alivyotuusia muumba wetu tunatakiwa tuwe mfano kwake, kama hali nasi hatutakiwi kula,kama hanywi na sie hatutakiwi kunywa na kila ambalo halitaki mgeni wetu kwa muda wamchana basi na nasisi pia tuwe mfano kwake’
Muumini aliwatizama watoto wake ili kujua kuwa wameelewa au la, alipoona kimya kingi akajua kuwa ama wameelewa au hawajui kabisa nini anachowaeleza. Akachukua moja ya boksi aliloleta mgeni. Akalifungua na kutoa zawadi ambayo ilingara kama dhahabu, ikiwa imepambwa na rangi za kila namna juu yake.

Kila mmoja mle ndani aliwaza kivyake, huenda ile zawadi ni alimisi, dhahabu,lulu, pesa au kila kizuri ambacho mwanadamu anachokipenda,angependa akipate . Mhhh, zawadi jamani zawadi, zawadi gani hiyo.

`Hii ndio zawadi aliyotuletea mgeni wetu, zawadi hii inatakiwa tuitumia kila mara, zawadi hii inaelekeza jinsi gani ya kuishi na mageni wetu, leo akiwepo na hata kiondoka, jinsi gani ya kuishi sisi wenyewe na jinsi gani tufanye, kama walivyofanya waliopita, na inatuongoza ili tuifikie ile njia iliyonyooka kwa kutenda mema na kukatazana mabaya, zawadi hii tunayo kila siku,lakini kila muda kama huu huzidi thamani yake. Na muda kama huu ndio wakati wakujipima,kuomba na kutubu na ni-nini ulichofanya na je afanyeje zaidi ili apate kurehemewa, na kupata msamaha wa mola wako’’

Zawadi hii nawakabidhi ili pakipambuzuka mbele ya mgeni wetu tuanze kuifanyia kazi zawadi yetu kwa vitendo.

Pale watoto wakatabasamu na kila mmoja akaipokea ile zawadi akiwa na hamu ya kujua nini kilichomo ndani yake na je ataifanyia nini zawadi hiyo ambayo thamani yake imezidi zawadi zote unazoweza kuzifikiria duniani.
Ni nani asiye mjua huyu mgeni wetu,?

Ni nani asiyejua zawadi aliyotuletea huyu mgeni wetu?, Kama hutujui basi sisi sio watoto wa `muumini’
Na huyu muumini ni nani kwetu?
Tuendelee kutafakari !!!
From miram3.com

No comments :