Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, August 28, 2009

MFADHAIKO

Katika shida hii ya usafiri, ambayo wakati mweingine hukulazimisha kusimama kwamguu mmoja (mithili ya hadithi za shetani tunazozisikia kuwa anasimama kwa mguu mmoja), unakutana ni vituko vya ajabu ambavyo huwezi kuamini kuwa vipo. Ambavyo vingi unavisoma kwenye magazeti au mitandaoni na kuishia kusema `hizo ni hadithi tu’ lakini lisemwalo lipo, na ukikukutana nalo, ndipo unapoweza kuamini!
Jioni ya siku ile ilikuwa na foleni kubwa ajabu,licha ya foleni watu tulibananishwa kama magunia ya mchanga. Kila kwenye mataa ilibidi tukae zaidi ya saa,kiasi kwamba wale wenye mioyo dhaifu walianza kumuota iziraili. Nami angalau nilikuwa kwenye kiupenyo karibu na dirisha, ingawaje nilisimama na kujifanya nachukua zoezi la kusimama na mguu chamoto nilikiona.
Ukiwa katika hali kama hii mawazo hukurudisha nyuma nakuwaza wenzako watakuwa wapi saa hizi, wengine watakuwa kwenye viti virefu, wengine wanalea na wengine wanaangalia runinga, lakini sio wa Gongo la mbali bado tulikuwa tunaota ndoto za lini nitafika nyumbani.
Katika hali isiyo ya kawaida macho yangu yalimuangalia dada mmoja, kibonge, kweli alikuwa na mvuto, kimaumbile na hata kisura, lakini kilichowavutia wengi ni ile nguo aliyovaa, ilikuwa kama ya hariri na laini,kiasi kwamba maumbile ya ndani ungeweza kuyachora bila kugandamizia.
Mwanadada yule naye kama wengine alikuwa ameminywa katikati ya watu wa aina tofauti, hamna aliyejali kuwa huyu ni dada,mama au kaka, kilammoja alikuwa akiinua kichwa juu kutafuta hewa kama samaki wafanyavyo baharini, au kwenye maji. Haya ndio maisha mazuri kwa kila Mtanzania,kama hupendi nenda kakodi taksi.
Jicho bwana halina pazia na ajabu ya jicho,likiona kitu kibaya, ndio linataka lione zaidi, hivi kweli yaleni `mavi’ ashakumsi matusi lakini ndio mfano wa maana. Jicho langu likaona na moyo ukalipuka kamavile umeshikwana shoti ya Umeme. Sikuamini kile nilichokiona. Lahaula, huyu kweli ni binadamu, lahaula , lahaula.
`Jamani, jamani , umanifanya nini jamani..’kilio cha ajabu kilitanda ndani ya gari,na hapo vichwa vilivyoangalia juu kwa shinda viliinama kutafuta kulikoni. Na mara kishindo cha kusukamana kilijongea upande ule niliopo. Jamaa njema lilikuwa limekwidwa kisawasawa, na sio kukwidwa shingoni,lahasha, lilikuwa limekamatwa sehemu nyeti huko jicho limemtoka kwa machungu na aibu.
`Jamani nini kulikoni..’ watu wengi waliuliza. Mmmh,kile nilichokiona kwa macho kimetoka hadharani, nami ndipo nikaamini kuwanikweli, kwani mwanzoni nilidhani ni ndoto hutaamini hata mimi niliona aibu kama vile nimehusika. Alituabisha jamaa, nilisema na kauli hiyo ilipokewa na wengi. Jamaa ametuaibisha.
`Kwanini umenifanya hivi, kwanini umenichafua, wewe mnyama, mkubwa, nitaikata hii ndude yako..’ alikuwa yule mrembo akilalama huku kamshikilia jamaa, ambaye alihangaika kujitoa kimasomaso’,lakini ilikuwa kazi bure kwasababu ya kule kubanana!
Huu ni mfadhaiko, na jamaa alipobanwa alisema ukweli na kukiri kuwa kutokana na msongamano,na hali ya yule dada alivyovaa, na ulaini wa mwili na akaongezea kusema na vile hajawahi kukutana na mwanamke sasa ni mwaka wa tano uzalendo ulimshinda, akafanya alichokifanya. Alipata raha gani hatujui, lakini ilikuwa zinga la soo!
From miram3.com

1 comment :

Anonymous said...

Huo ni ugonjwa, inakuwaje ufanye huo uchafu hata kama kuna hali kama hiyo, watu kama hao wanatakiwa wachukuliwe hatua