Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, August 13, 2009

Tusaidie wenye ulemavu

Leo tarehe 13-08-2009, nikiwa ndani ya daladala kulikuwa na watoto wenye ulemavu wa kusikia, walikuwa wkienda shule. Ndani ya gari hilo wengi walikuwa wanawatazama jinsi wanavyoongea kwa ishara kwa kutumia mikono yao. Mimi mawazo yangu yalienda mbali zaidi ya kuwaangalia, nilijaribu kuwafikiria watoto kama hao ambao wapo vijijini, hawana hili wala lile, kwasababu wamezaliwa na upungufu huo wao wanakosa hudumamuhimu kama hii ya kusoma.
NGO, nyingi zinaanzishwa lakini ni chache zinazopenya vijijini. Ombi langu kwa wenye uwezo wasaidie kuanzishwa shule kama hizi vijijini kwani kati ya hawa wapo wenye vipaji vikubwa, wataalamu na viongozi wa baadaye. Inabidi na wamanchi waelimishwe kuwa kuwa kilema sio mkosi, bali ni sehemu ya maumbile tu ya kibinadamu.

No comments :