Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, August 12, 2009

Mtoto wa mwenzako ni wako pia

Ni asubuhi nyingine ya tarehe 12-08-2009, kama kawaida nilidamka asubuhi nakuwahi kituoni, ilikuwa saa kumi na moja alifajiri. Nilipata basi la kwanza kirahisi, nilipofika Mombasa nilikuta umati wa watu ukisubiri gari, na magari ya kwenda Msasani ni juu kwa juu,yaani hayasimami, na kama hujui kudandia basi utalala hapo kituoni.
Katika kukuru kakara hiyo mtoto mmoja wa shule ya msingi alidandia, na wakati huo gari linaongeza mwendo na yule konda, au mpiga debe akawa anamsukumia nje. Ilikuwa ni hatari kwasababu kama yule mtoto angeishiwa nguvu na kuachia vile alivyong'ang'ania ule mlango wa gari angedondoka na kuumia. Baadhi ya wazazi mle ndani wakaanza kumshambulia yule konda kwa maneno kuwa amuachie yule mtoto aingie ndani.
Hatimaye yule mtoto alipenya kwa shida akaingia ndani ya daladala. Niliwaza sana ni nikijua kuwa hata mimi watoto wangu watakuwa wanafanyiwa hivyo. Hii ni kujisahau na kutizama yale matamanio yetu ya muda ule. Namshukuru sana mke wa raisi wetu alipotoa kauli kuwa `mtoto wa mwenzio na mtoto wako pia.
Kama usipomjali mtoto wa mwenzio ujue hata wakwako atakuwa hajiliwi pia, ukimtenda ubaya ujue na wakawao atatendewa ubaya pia, hata kama una uwezo ipo siku na wewe au yeye atakumbana na maswahiba hayo.
Ombi langu tusipende kutendea ubaya wenzetu, kwani na sisi yatatukuta kwa namna moja au nyingine, kama sio kwako ni katika uzazi wako, na muumba anatuona kwa hayo tunayo tenda kwani yeye ni mwingi wa hekima.

No comments :