Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, August 27, 2009

SHIDA YA USAFIRI NA FOLENI DAR

Leo tarehe 27-08-2009, niliona niitoe kero yangu katika tovuti ya http://www.wananchi.go.tz/
Tunawashukuru sana kwa kutoa Tovuti hii, na nivyema wananchi tukaitumia vyema kwa kutoa kero zetu, kutoa maoni au pongezi. Nami kwa kuanzia ningependa kutoa dukuduku langu kuhusiana na tatizo la usafiri hasa kwa wakazi wale tunaishi nje ya mji kama vile Majohe,Kipunguni nk, ambapo hakuna magari ya moja kwa moja kuelekea sehemu kama vile Msasani, Kawe, au Kunduchi nk ,na fikiria unatakiwa ufike ofisini saa mbili, bila hivyo kazi huna.

Maoni yangu ni kuwa kuna haja ya wahusika wa usafiri kuruhusu magari ya kutoka maeneo kama hayo ya moja kwa moja kwa kutoa nauli yenye unafuu, kuliko hili la kupanda magari mawili au matatu na mojawapo unalipa nauli ya masafwa marefu(sh 450/-). Na hii ina mana kuwa kwa siku unatakiwa kulipia nauli si chini ya sh 1400/- kama umebahatisha kupanda magari mawili, lakini mara nyingi haiwi hivyo kwasababu inakubidi ulipie nauli ya kugeuza nalo,ili angalau upate kiti au uweze kuingia ndani ya gari bila kudandia (Huwa asubuhi au jioni kama hujui kudandia huwezi kuingia ndani, magari haya hayasimami kituoni kwa kukwepa wanafunzi.) kwahiyo kutumia nauli zaidi ya sh 1900/-kwasiku.
Kero hii inatukwaza sana sisi watu wa maeneo haya kwasababu, sio tu kwa swala la nauli, lakini pia inatubidi tuamuke saa kumi za alifajiri kila siku ya kazi , ili kukwepa foleni ambayo huanzia saa kumi na mbili, na hutaamini kama utakutana nahii foleni unaweza ukatumia zaidi ya masaa matatu kutoka Msasani hadi Gongolamboto bado hujatafuta usafiri wa kwenda Majohe au Kipinguni unapoishi. Kwa minajili hii familia yako unaiacha ikiwa imelalana huenda ukarudi ukaikuta imeshalala pia.
Kwa maoni yangu kuhusiana na tatizo la foleni ndefu, kama inawezekana ni kuanzisha barabara za moja kwa moja, yaani magari yakienda yasirudie njia ileile, nafikiri inawezekana kwasababu zipo njia za mkato kutoka Gongolamboto hadi Ubungo, au Gongolamboto hadi Mbagala, na ndani kwa ndani zipo barabara za mikato ambazo tumeyaona magari ya daladala yakipitia kukwepa foleni, hizi zote zikiwekwa vizuri itapunguza foleni kwa kiasi kikubwa. Na kama inawezekana usafiri wa treni kwa maeneo haya ungefaa pia!
Na pia wakati mataa hayafanyi kazi,matrafiki hutumia muda mrefu kuita sehemu moja tu, sijui hufanya hivi kwasababu gani,kwanini wasitumie `stop-watch’ ili kutowaumiza abiria ambao hujazwa ndani ya daladala kama magunia. Nimeshuhudia abiria wakizimia ndani ya magari haya kwasababu ya kusimama muda mrefu na kukosa hewa!
Natumai wahusika wanalifanyia kazi tatizo hili,lakini ni sie waathirika inabidi tutoe sauti zetu ili mjue kweli tunaumia, kwani tusiposema mtajuaje shida zetu

Ahsanteni na poleni sana kwa majukumu haya mazito.
NB. mfadhaiko nilioushuhudia ndani ya daladala nitautoa kesho Mungu akipenda.

From miram3.com

1 comment :

Anonymous said...

Folni dar kuisha ni majaliwa ya Mungu, hata London kuna foleni sembuse dar
Ubovu wa barabara na mataa ni kikwazo pia