Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, August 17, 2009

Mikataba ya ajira kulikoni

Mkono ukiwa shavuni ukiwa umeshikilia kichwa kilichobeba lukuki la matatizo,na huenda hayo matatizo yangelijazwa kwenye magunia huo mkono ulioshikilia shavu usingelihimili. Hii ilikuwa jumatatu nyingine ya tarehe 17-08-2009, nikikumbuka jamaa yangu nilyemkuta upenuni mwa nyumba anayoishi huku kashikilia shavu.
`Ndugu yangu aheri nimekuona,manake watoto wamefukuzwa shule sijalipa ada sasa mihula mitatu, jana nimepokea barua kuwa mwisho wa mwezi huu mkataba unakwisha na hawana haja ya kunichukua tena. Baba yangu anaumwa na mke wangu ndio huyu hauchihauchi kunakucha sina hela ya kumtibia, je nina thamani gani katika hii dunia, hebu niambie rafiki yangu?' alinielezea huku machozi yakimlengalenga.
Rafiki yangu huyu alimaliza diploma yake vizuri akapata kazi katika kampuni moja ya watu binafsi, aliitumikia kampuni hiyo kwa zaidi ya miaka 15, kwa uaminifu na uchapajikazi bora, kiasi kwamba mwajiri wake alimpenda sana, lakini kwa mdomo, hakuwahi kuongezwa mshahara na walioajiriwa baadaye ambao wangi walikuwa watoto wa wakubwa au wageni toka nchi nyingine walipewa mishahara minono . Alidai haki yake ili naye afikiriwe, na huko kudai kukamtokea nyongo, mwajiri akabadili kibao na mkataba ulipoisha akaambiwa katafute sehemu watakaokulipa mshahara unaotaka, na barua hiyo alipewa jioni wakati muda wa kazi unaishia.
Katika mkataba wake wa ajira alitakiwa alipwe mshahara wa mwezi mmoja tu kama zawadi, na kwa vile alikuwa na madeni hela yote aliyotakiwa kulipwa ilikatwa kufidia sehemu ya deni lake.
Hadithi ni ndefu, na unaweza ukasema yote maisha, lakini dukuduku langu ni huu utaratibu wa nchi, wa kutowalinda raia zake katika sehemu za kazi. Hawa wenye makampuni wanawatega wafanyakazi wao kwa mikataba ambayo hatimayake ni mbaya. Nafikiri kungekuwa na mkataba wa ujumla kuwa kila anayeajiriwa anatakiwa kupata haki hii na alindwe vipi na mikataba hiyo. Makampuni mengi ya watu binafsi hayataki vyama vya wafanyakazi, je serikali inajua hili? Au mimi ndio sijui , naomba tujadiliane hili.
From miram3.com

No comments :