Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, June 10, 2025

NDANI YA DIARY YANGU-KWA MTORO


Ni mara nyingine leo siku ya Idd nimekuja kuswalia kwa Mtoro , Nimewahi sana ili angalau niswali ndani, na sehemu ambayo nitanuona imamu.
Msikiti huu unajaa sana, sijajua ni sababu ya kihistoria au kuna mengine ya ziada.
Kwangu mimi msikiti huu una historia nyingi kwangu kiimani.
Nakumbuka enzi hizo za harakati za Uislamu, watu wanakamatwa kamatwa, enzi za Mwembe chai nk

Nakumbuka sana enzi hizi sikosi kufika , hata siku za kawaida, hapa msikitini pamoja na yote nilikuwa nakuja kununua kanda za mawaidha mbalimbali. Mojawapo nyingi ya hizo kanda zilikuwa za mawaidha ya sheikh Bachu.

Misikiti sasa imeboreka, ukiwemo huu, sasa hivi msikiti huu ni wa ghorofa, na umezungukwa na majengo ya magorofa,.,
Nilianganza huku na kule, wale wauzaji wa kanda za mawaidha hawapo tena, sasa hivi kuna wauza nguo, kanzu, madawa,...

Sasa hivi hapa kuna hata tv ...tv mtoro

Ni mimi: emu-three

No comments :