Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, April 30, 2013

WEMA HAUOZI-1



Siku babu aliponialezea ukweli kuhusu maisha yangu, nilijihisi vibaya, nikajikuta najenga hasira moyoni, …sijui kwanini, ….kwanza hata babu alipomaliza kunismulia, mwanzoni nilihisi ni moja ya zile hadithi zake anazopenda kunismulia, lakini…..

‘Hiyo sio hadithi, huo ni ukweli kuhusu maisha yako….’akasema babu.

‘Kwakweli, sikuamini, hadi pale nilipoamua kwenda kwa mama na kumuomba aniambie ukweli ulivyokuwa, na kama nilivyotazamia,…. mama hakutaka kuniambia ukweli, kwani baada ya kumuomba afanye hivyo, alijifanya ana kazi nyingi, akawa anaendelea kufagia wakati alishamaliza kufagia....

‘Mama mimi siwezi kuamini kile alichonisimulia babu,… nataka ukweli kutoka kwako, je hayo aliyoniambia babu ni kweli, au ananivunga na hadithi na visa vyake, na kunifanya nihisi kuwa ni ukweli wa maisha yangu…mimi ni kweli hayo babu aliyonisimuliai?’ nikamuuliza mama.

‘Sijui kakusimulia kitu gani….., lakini vyovyote alivyokusimulia….., kama ni kuhusu maisha yangu, hayo hayakuhusu kabisa…na wala usinichanganye…., wewe bado mtoto mdogo unahitajika kusoma na sio kukimbilia kujua maisha yangu au ya babu au bibi yako, …au…mare-he-..oh, ‘hapo akatulia, na baadaye akasema kabla sijasema kitu;

‘Kwanza ni kwanini babu yako akusimulie mambo yasiyokuhusu….?’mama akanigeukia na kuniangalia huku macho yakiwa yameshatanda ukungu wa machozi.

‘Maisha yako yanayofungamana na babu…kama ni hivyo yananihusu, maana kwa maelezo ya babu wewe ulikuja kuishi naye, wakati nazaliwa, na kumbe…..oh, mama naomba unieleze ukweli, ni kweli hayo babu aliyoniambia…?’ nikasema kwa hasira nikiwa na mimi nimemkazia mama macho, kitu ambacho hakikuwahi kutokea kabla katika kuishi kwangu na mama.

Kwa ujumla mimi mama yangu nampenda sana, na sikutazamia kuwa kunaweza kukatokea jambo ambalo lingeliweza nimuone mama vinginevyo…, na mama alijua hayo, na ilionekana wazi kuwa hata yeye hakupenda kuniumiza kwa lolote lile kwani alinipenda sana,…na huenda ndio maana alikuwa akinificha ukweli wote kuhusu maisha yangu.

‘Mwanangu sikiliza, hayo unayohitajia nikuelezee, hayakufai kwasasa, sio kwamba sitaki kukuelezea, lakini kwanini nikuumize moyo wako mwanangu, wakati huu unahitajika kutuliza kichwa chako kwa ajili ya masomo yako…elimu yako ni muhimu kuliko hayo unayotaka kuyafahamu….na hayo hayatakusaidia kitu zaidi ni kukusononesha moyo wako…’akasema mama.

‘Mama kiukweli , kuanzia leo, kama usiponiambia huo ukweli wa maisha yangu, ulivyokuwa, hadi mimi nikawa sina baba…sina ndugu, tunaishi kwa watu baki, ….akili yangu itakuwa haizingatii masomo tena….’nikasema na mama akaniangalia kwa macho ya kusikitika, lakini nilikuwa nimezamiria hivyo, kuwa nijue chimbuko la maisha yangu.

‘Mama,…sawa umeniambia baba yangu alifariki au sio, hayo ni mapenzi ya mungu,…siwezi kupingana na hilo, lakini siku zote hutaki kuniambai baba yangu alifariki vipi…inaonekana kuna kitu kimejificha kwenye kifo chake….’nikatulia nikimwangalia mama , ambaye alibakia kuniangalia kwa macho ya huzuni.

‘Haya kuna hayo kanisimulia babu, ambayo..oh, yanasikitisha, kuhusu bibi, hayo yana ukweli gani,….hebu niambie ni kweli hayo yalitokea…?’ nikamuuliza mama.

‘Kama nilivyokuambia awali, mimi siwezi kuota nikafahamu hayo uliyoongea na babu yako, na sijui kwanini aliamua kukuambia hayo…ambayo siwezi kujua ni mambo gani hasa kuhusu mimi,au huyo bibi….hebu niambie babu yako kakuambia kitu gani?’ akauliza mama.

‘Tuanzie na hapo…kwanza kwanini unasema ‘huyo bibi….’, ni kweli babu  sio babu yangu wa kuwazaa wazazi wako,…..ni kweli kuwa huyu babu ni babu wa kunilea tu?’ nikamuuliza.

‘Jamani hayo yote yanakuhusu nini, babu ni babu tu, awe asiwe babu wa kumzaa mama au baba yako, yote ni sawa, yeye ni babu yako, kwanini unamsema huyo babu kwani kakusimanga …..?’ akauliza mama.

‘Hajanisamanga lolote,..babu wa watu, siku zote ananipenda sana, na ndio maana hapendi kunificha ukweli wa jambo lolote, na toka jana amekuwa akinisimulia kisa ambacho nimeshangaa kuwa kumbe ni ukweli wa maisha yangu, jinsi yalipoanzia kwa mikosi,…kwa ujumla nampenda sana babu yangu, na sipendi kusikia watu wakisema kuwa huyo sio babu yangu, ila mimi nakushangaa wewe mama yangu ambaye hutaki kuniambi ukweli…kila jambo unanificha, hata lile ninalostahili kulifahamu…kwanini mama….?.’nikasema na kuamaliza kwa kuuliza.

‘Ina maana babu yako huyo kakuambia nini kinachokusumbua hadi ufikie kuniuliza, kama kakusimulia kuhusu maisha yangu, basi inatosha, mimi sipendi kuyaongea hayo yaliyopita,….na kama kakuambia, kuwa wewe sio mjukuu wake halisi, mimi sipendi kusema lolote kwa sasa naomba uyaache maisha yangu kama yalivyo…’akasema na kuinuka.

‘Mama usiponiambia ukweli, mimi sitakula, na wala sitakwenda shule tena…’nikamwambia.

‘Sasa hapo unanitafuta ubaya, hivi, huyo babu yako kakusimulia mambo gani…. mbona babu yako amekiuka makubaliano yetu .. ?’ akasema mama.

‘Makubaliano gani mama ….?’ Nikauliza huku nikiwa na hasira.

‘Mwanangu achana na hayo, nafanya hivyo kwa maslahi yako, ipo siku nitakusimulia mwanzo hadi mwisho, lakini sio kwa muda kama huu,…nielewe mwanangu..’akasema mama.

‘Mama, ninachohitajia kujua kwa sasa ni kuwa je ni kweli hayo babu aliyonisimulia,….maana  ninavyoona wewe una mengi….ambayo huenda hutaki mimi niyajue…sawa, labda ni kwa ajili ya hayo yaliyotokea yanakukwaza….lakini hata mimi nina haki ya kufahamu hayo yote,….’nikasema na kukaa chini, nikisubiri mama aongee.

Mama alitulia, na akageuka huku na kule , kama vile anatafuta upenyo wa kukimbilia, na baadaye alatulia, akajiegemeza kwenye ufagio aliokuwa kaushika, na kuinamisha kichwa akitumia huo ufagio kama kiegemezo, alikaa hivyo kwa muda, na baadaye akasogea na kukaa karibu yangu, akanishika begani akasema;

‘Mwanangu hata sijui nianzie wapi, ….kila siku nikikumuka yaliyotokea, ninajuta sana, nikiwazia hayo yaliyotokea ….’akatulia, na kuangalia pembeni.

‘Mwanangu , mimi na mume wangu tuliishi maisha ya shida sana kabla hatujaweza kujenga nyumba, nyumba ambayo baadaye iligeuka sehemu ya uwanja wa vita….nyumba niliyoitolea jasho, na kuihangaika, nikishirikiana na mume wangu,…lakini baaadaye …oh….’hapo akatulia na kuanza kutoa machozi.

Kwakweli kwa ile hali, nikajikuta tena namuonea huruma mama…sikupenda mama alie, kwani inavyoonyesha maisha yake ni ya huzuni,…na mikasa ya kusikitisha, na ilionyesha kuwa akisimulia, inakuwa kama kutonesha jipu…nikatamani nimuambia asiendelee, lakini nikaona haina haja…ni lazima nijue ukweli ulivyo…

‘Baadaye ilikuwaje mama,…ina maana kumbe ile nyumba hukuiuza, kama mlivyoniambia awali…kumbe ilichukuliwa kwa nguvu, au sio mama, kwanini tusiende mahakamani kama ni hivyo?’ nikauliza nikiwa na hamaki za kutaka kujua zaidi.

‘Mahakamani!….oh, sitaki tena hayo mambo…nilihangaika hadi nikaribie kutolewa roho…hapana, kama wameona ni jasho lao waachie wachukue, lakini mungu atakuja kunilipizia jasho langu lilopotea bure…’akasema mama.

‘Mama kama ni haki ukienda mahakamani utaipata tu….’nikwambia mama, na yeye akaendelea kuonga akisema;

‘Mwanangu mimi na mume wangu tulipooana hatukuwa na lolote, yalikuwa ni maisha ya kubangaiza tu, hakuna mbele wa nyuma, ….na hata kuja kuishi naye ilikuwa kwa bahati tu, kwani alishanifukuza moyoni mwake, toka siku ile nilipomtamkia kuwa nina ujauzito wako…lakini ya mungu mengi…..’akatulia na kuangalia juu. na machozi yakaanza kumtoka, na baadaye akainamisha kichwa chini akiwa kakishikilia....

Alipofika hapo, nikajikuta nakumbuka maelezo ya babu, ambaye ndiye alinifanya nimsakame mama ili anihakikishie kuwa hayo babu aliyoongea ni kweli,..nikawa nayakumbuka maongezi yangu na babu huku mama naye kiongea yale yale aliyonisimulia babu

*******

‘Mama yako alipata shida sana, kwenye uja uzito wako, wazazi wake walimtimua nyumbani wakidai kuwa kaleta mkosi , na aibu nyumbani, kwahiyo aende huko huko kwa aliyempa huo uja uzito huo, ….na alipokwenda kwa huyo mwanaume, naye akamfukuza kwa panga, na kusema hamjui, na wala hataki kusikia lolote kutoka kwake…’babu yake ndivyo alivyomsimulia mjukuu wake.

‘Mimi siitambui hiyo mimba, na niskuone ukifika hapa kwangu tena….’akasema huyo mwanaume

‘Kwahiyo babu ndio kusema kuwa mimi sina baba, au ni kweli kuwa mama alikuwa na baba wengi kiasi kwamba ilikuwa vigumu kumtambua baba yangu ni nani, kwa maana hiyo mama yangu alikuwa akifanya….oh,….?’ Hapo nikatulia kusema lolote, nikimwangalia babu.

‘Hapana, mama yako hakuwa muhuni,..ni ujana tu ulimdanganya, kwani rafiki yake alikuwa huyo huyo, na walianza urafiki wao wakiwa wadogo, wakazoeana, na kwa vile wazazi hawakujaribu kuwaasa au kuwaelekeza ubaya wa kuingia mambo ya kikubwa mapema, basi wakajikuta wametenda kosa, lilomsababishia mama yako kupata shida …..’akasema babu.

‘Baba unaye….kwani katika maisha ya binadamu, hakuna asiye na baba, hata kama baba huyo ilitokea akafariki mapema, bila kumuona, lakini kiukweli baba alikuwepo, ….’akasema babu.

‘Ila ilivyotokea ni kuwa mama yako, alipomfikia huyo mwenzake…alimkana, katu katu akamkana na kujifanya hamjui tena…’akasema babu.

‘Mama yako alipofukuzwa kwao, yeye aliona jambo jema ni kumuendea huyo mwenzake, na kumueelzea ukweli, japokuwa hakuwahi kumwambia mapema kuwa katiak hayo wliyokuwa wakifanya mambo yameharibika….’akatulia babu.

‘Mama yako alifanya kosa, hilo, kuwa ilitakiwa kumwambia mwenzake mapema, kuwa mambo yameharibika, na ili akisakamwa na wazazi wake, aweze kumtaja huyo mwenzake, lakini hakuwahi kufanya hivyo, huenda alikuwa akisubiri wakati muafaka….’akatulia babu.

‘Baada ya kufukuzwa kwao, akamwendea mwenzake, na huku akiwa na matumaini ya kupokewa vyema, kama walivyokuwa wakifanya hivyo siku zote, lakini mwenzake alipomuoana mama yako akija na kanga kichwani, akahisi kuna jambo kubwa

‘Wewe vipi, mbona unakuja kwangu saa hizi, siku zote unanimabia kuwa huwezi kuja kwangu muda kama huu, wazazi waki ni wakali, sas aumefuata nini muda kama huu, usiniletee matatizo, …’akasema huyo mwanaume, wakati huo ni vijana’akasema babu.

‘Nimefukuzwa nyumbani…’akasema mama yako.

‘Eti nini, umefukuzwa nyumbani, …ndio unakimbilia kwangu, kwani hapa ni seehmu ya kuhifadhi wakimbizi, ….hapana nenda kwa ndugu zako, sio hapa, utaniletea matatizo bure….’akasema huyo rafiki yake.

‘Yaani leo hutaki kunipokea kama siku nyingine, kwa vile tu nimekuambai kuwa nimefukuzwa, na wala hutaki kujua kwanini nimefukuzwa?’ akauliza mama.

‘Sihitaji kujua, ….kwanza nijue ili iweje, wewe ondoka hapa kwangu, sitaki matatizo, kwani baba yako alishanichimbia mkwara, …namuogopa sana….’akasema huyo mwanaume.

‘Mimi nimekuja kwako kwasabbu nina uja uzito wako….’akasema mama yako bila kusubiri kuulizwa ni kisa gani kilichomfanya afukuzwe na kukimbilia kwa huyo jamaa.

‘Eti nini, una ujauzito wangu….ooh, ondoka ondoka tena haraka, nenda huko huko kwa hawo waliokupa huo ujauzito, mimi sikujui, na wala sijui huo ujauzito……ondoka…sitaki hata kukuona….umenielewa, nasema ondoka haraka…usinitolee macho hapa kama unataka kukata roho….’akasema huyo mwanaume bila aibu huku mama akitoa macho ya kushangaa,hakuamini kuwa huyu ndiye yule aliyekuwa mpenzi wake, ambaye kila wakikutana ilikuwa ni mpenzi, daling, nakupenda….

‘Yaani leo hii unanikataa,kwasabbu ya huu uja uzito…wakati mwanaume ninayemjua ni wewe peke yako na wewe unatambua hivyo, na karibu watu wengi wanafahamu hivyo, haiwezekani, mimi siondoki humu ndani…’akasema mama huku bado akiwa haamini.

‘Ohooh, hivi unitambui mimi eeeh,….unasema…., huondoki humu ndani kwangu, ngoja nikuonyeshe kazi….’akasema huyo mwanaume na akachepuka kidogo, na aliporudi alikuwa kashikilia  sime, …ikiwa inameremeta, akaja nayo, na kabla hajasema kitu akampiga mama mgongoni na hiyo sime kwa ubapa, na alimpiga kwa pigo la nguvu..’akasema babu.

‘Nakumbia usipoondoka hapa ukiwa hai basi, nitakuondoa mwenyewe ukiwa maiti....’akasema huyo mwanaume, na mama yako alipomwanglia huyo jamaa, akajua kweli mwenzake kazamiria ….kweli ile sura ilikuwa ya kiuaji, sura ambayo aliiona mara moja wakati jamaa huyo alipokuwa akipambana na wabakaji waliotaka kumbaka huyo mama, kipindi cha nyuma.

Siku hiyo mama yako, alikuwa katoka kwa huyo jamaa, na wakati yupo njiani akirudi kwao, mara akakutana na hawo wabakaji, wavuta bangi, wakamshika mama yao na kuanza kumburuza vichakani,…..mama yako akawahi kupiga ukulele, na jamaa , akasikia sauti ya mpenzi wake. Hakusubiri, aakfuatilia hiyo sauti.

Alipofika hapo kichakani, akawakuta jamaa wakiwa wanajiandaa kufanya mambo ya machafu, huyo jamaa mzuka ukampanda, akabadilika na kuwa mnyama, aliwarukia hawo watu na kutoa kipigo ambacho kilikuwa ni cha kuua….

Wale jamaa, walitoka hapo, wakiwa wameumizwa vibaya sana, na ilibidi wajitahidi kukimbia kwa shida, kwani kila hatua, umauti ulikuwa ukiwaita….wakakimbia, na mama yako, alibakia kuduwaa akimwangalia huyo jamaa yake…..hakuamini kuwa ndiye yule yule anayemfahamu.

‘Alibadilika sura, ikawa kama sio yake, macho yake aliyatoa pima, na kubadilika rangi na kuwa mekundu,…alitisha, na hata alipomaliza kuwaadhibu hawo watu, mama yakoa ansema aliogopa kabida kuandamana na huyo jamaa yake.

Sura kama hiyo akaiona siku hiyo….akajua kuwa akiendelea kubakai hapo, atafanywa , kama walivyofanywa hawo jamaa waliotaka kumbaka, …. ikabidi atokea nje na kukimbia….’akasema babu na kutulia, na kuniacha nikiwaza, ina maana baba huyo ni yupi, ni huyo marehemu, au kuna baba mwingine.

‘Babu.... baba ni yupi huyo?’ nikamuuliza.

                                                    *******

NB: Oh, kisa hiki kimeanzia hapo, ngoja nikusanye nguvu, tukijalia tena nitakuja na mambo mapya ya kisa hiki.

WAZO LA LEO: Mnapokuwa marafiki, mke na mume,…(hasa vijana ambao wa shuleni) jaribu sana kuangalia athari za matendo yenu, kwani kosa dogo tu linaweza kuwaharibia mipnagilio ya maisha yenu ya baadaye , …..

Kwanza jiulizeni, je wakati umefika wa kufanya hilo mnalotaka kulifanya, je kweli hayo ndio mapenzi ya ukweli, au ni tamaa za kimwili tu. Subirini, pangeni na kukubalina kabla ya kujiingiza kwenye mahusiano ya ndani.


Ni mimi: emu-three

5 comments :

Anonymous said...

viebrasqueeva xaikalitag Fawtrarse [url=http://usillumaror.com]iziananatt[/url] PrieriRes http://gussannghor.com Kepthughele

Yasinta Ngonyani said...

Kisa cha kujifunza mengi sana...Ila nimekuwa najiuliza mara nyingi sana kwanini wanaume wakimpa mimba msichana wanakataa kabisa na kumfukuza?

Unknown said...

kisa hiki kinafundisha mengi sana

Unknown said...

inatufundisha sn

Anonymous said...

Sikuamini kuwa ningeweza kuungana tena na mpenzi wangu wa zamani, nilipatwa na kiwewe cha kusimama peke yangu bila mwili wa kusimama na kuwa nami, lakini nilipata bahati sana siku moja nilikutana na Dk DAWN, baada ya kumwambia. kuhusu hali yangu alifanya kila liwezekanalo kumuona mpenzi wangu anarudi kwangu, kiukweli baada ya kunifanyia uchawi mpenzi wangu wa zamani alirudi kwangu chini ya masaa 48, mpenzi wangu wa zamani alirudi huku akiniomba kuwa hatoniacha kamwe. tena. Miezi 3 baadaye tulioana na kuoana, ikiwa una hali sawa. Ana nguvu nyingi katika mambo yake;
* upendo
inaelezea * inaelezea kivutio
* kama unataka ex wako nyuma
*acha talaka
* kuvunja obsessions
* huponya viharusi na magonjwa yote
* uchawi wa kinga
*Ugumba na matatizo ya ujauzito
* bahati nasibu
* uchawi wa bahati
Wasiliana na Dk Ediomo kwenye barua pepe yake: dawnacuna314@gmail.com
Whatsapp:+2349046229159