Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, September 22, 2023

TUSAIDIE TUPATE BARAKA


Nikiwa nimekaa ndani ya gari la daladala, macho yangu yalivutiwa na abiria wanaogombea kuingia ndani ya dala dala hilo. 

Abiria wanaotaka kuingia walikuwa wengi zaidi ya uwezo wa gari hilo....kwahiyo ilikuwa mshikemshike, na kati ya hao abiria, nilimuona mtoto , nahisi anaweza kuwa kati ya miaka mitano au sita, akiwa na sare zake za chekechea nahisi

Kwa vile abiria walikuwa wengi, na kila mmoja anataka kuwahi kuingia, hakuna aliyemjali huyo mtoto, walimsukumia nje...lakini yule mtoto akawa naye anajitahidi kushindana ili naye awahi kuingia, kwa bahati mbaya akadondoka chini

Hakuna aliyemjali....walioweza kuingia wakaingia, na wengine wakabakia nje, sasa wale waliobaki nje ndio wakamuona huyo mtoto, ...

'Vipi umeumia..?' mmoja wa abiria akamuuliza
 Yule mtoto akawa analia...huku akijifuta futa, na kuokota mkoba wake wa madafutari, na bado akijaribu kuona kama ataweza kuingia

''Endesha gari....' konda wa hilo dala dala akasema, bila kujali kuwa kuna mtoto alianguka, na hakutaka hata kumsaidia angalau aingie

Baadhi ya abiria walioingia ndani wakawa wanamsema konda, asimamishe garii amchukue huyo mtoto

'Wanafunzi wameingia wengi sana, na hata akiingia atakaa wapi...'akasema konda na dala dala likwa limeingia barabara kuu, mtoto akabakia kituoni na abiria wengine.

Hatukifika mbali gari likakamatwa na trafiki kwa makosa ya kupitia njia za mkato...ikawa ndio mwisho wa safari hiyo, kwasababu trafiki alisema hilo gari sio mara ya kwanza, kahiyo linahitajika kituo cha polisi

WAZO LA LEO: Wakati mwingine tunazikataa baraka zetu sisi wenyewe...tuwasaidie wenye shida, kwani kutokana na wao, ndipo baraka zilipo.
Ni mimi: emu-three

No comments :