Nilitembea kwa haraka kama nataka kufanya jambo ...hadi nafika kwa huyo jamaa sikujua nitafanya nini, ili akilini, nilitaka nifanye jambo...nikafika pale aliposimama huyo jamaa,...nilipomkaribia tu,nikasikia mume wangu akiita huku nyuma;
‘Mke wangu unataka kufanya nini…’akasema mume wangu, lakini mimi
sikumjali tena, kwani sasa nilikuwa nimesimama kwa huyo jamaa tunaangaliana uso kwa uso.
Tatizo yeye, alikuwa kavaa hayo mawani, mkwe usinione, nilitamani niitoe, nione anahisi nini, …lakini mkono ukawa mnzito
kufanya hivyo, nilitamani, nifanye jambo, mkono unawasha, lakini mkono ukawa mnzito kuinuka,, lakini kwa haraka mkono wangu ukaenda kwenye mikono ya jamaa, nikamshika mkono na kumvuta
tutoke nje, lakini hakusogea, nilipoona hivyo nikasema;
‘Naomba tutoke nje, kama wewe mwanaume kweli...'nikasema hivyo
'Mhh...' jamaa akaguna tu, na hakusogea
'Sikiliza wewe mtu, mim nataka tukaongelee haya mambo nje, maana hapa sio mahali
pazuri pa kuongea, tutavunja taratibu za hospitali, na pia eeh…tunaweza kuleta
matatizo kwa mume wangu..’ nikamwambia, na yeye kwa haraka ajaibu kwa kusema;
‘Kwa leo mimi siwezi kuongea na wewe chochote, kwa maana mimi nimekuja hapa kwa ajili ya kuongea na
mume wako,...'akasema
'Nafahamu hilo, ...nimeona kuwa umekuja kwa ajili yake, lakini nataka kukuambia jambo la msingi sana....'nikasema
'Hapana, siwezi kufanya hivyo, kabla sijaongea na mume wako,...'akasema
'Unataka nitumie nguvu...'nikasema
'Hapana usifanye hivyo, kwani haitasaidia kitu...mume wako kanipigia simu anataka kuongea na mimi...kiukweli tulishaongea mambo fulani fulani,...sasa nimekuja kuna mambo mawili
matatu ya kumalizana...'akasema
'Ina maana hunielewi, kwani mimi ni nani kwa huyo mgonjwa
'Ni mume wako...'akasema
'Kwahiyo hayo unayotaka kuongea naye mimi hayanihusu...?' nikauliza
'Nitajua nikimalizana kuongea na yeye, natii alichoniomba mteja wangu...'akasema
'Mteja wako...?'! nikauliza
'Ndio....'akasema na muda huo yeye alikuwa akinijibu kwa sauti, kama vile anataka kila mtu asikie wakati mimi nilikuwa nikimuuliza kwa sauti ndogo
‘Mliongea nini na mume wangu, mpaka akuitie huku hospitalini..au ni ule
utapeli wako wa kurubuni watu, …bado unataka kumfanyia tena mume wangu, mimi..nitakuitia
polisi sasa hivi…’nikasema
‘Kwanza nikuambie jambo, mimi sio tapeli..na kuja kwangu hapa sio kwa kujitakia, ni mume wako kaniita..na tuliyoongea mimi na yeye, hayawezi kusemwa mpaka nimalizane na yeye, kama anataka ndio nitakuelezea, kwanini inakuwa vigumu kuelewa….’akasema
‘Kwangu mimi siwezi kukuelewa, japokuwa nakuelewa ulivyo,..na hilo unalotaka kuongea na mume wangu lazima nilichuje kwanza, kwasababu mume wangu ni dhamana yangu, lolote likitokea nitaulizwa...'nikasema, nikimuangalia moja kwa moja usoni
‘Ni kweli,…lakini kwa hivi sasa hata mimi sijajua kikamilifu kaniitia nini, kwasababu kwenye simu
hajaniamba, zaidi ya kusema nifike hapa hospitalini, ni muhimu sana, ..kwahiyo mpaka niongee naye ndio nitakuwa na
uhakika huo,,..'akasema
‘Lakini mlishaongea jambo kabla, wewe na yeye…?’ nikauliza
‘Kifupi, Ndio...'akasema
'Mliongea nini...?' nikauliza
'Mambo mengi, yakiwemo ya afya yake, familia, kazini, na mikataba ...'akasema
'Mikataba gani....?' nikauliza
'Mimi naomba ukamuulize mume wako, maana yeye ndiye kaniita hapa, labda anataka nimfanyie kazi yake..’akasema
‘Kazi gani sasa…?’ nikamuuliza nikitarajia jibu hilo.
‘Oh, mimi nilijua nyie wawili mumeshaongea na kukubaliana, sasa kama
hamjaongea kwanini ameniita,..basi huenda kaniita kwa jambo jingine, ndio maana naomba npate muda wa kuongea naye kwanza ili nijue ni kitu gani, tafadhali...’akasema.
‘Huwezi kuongea naye mpaka nijua ni jambo gani, ili niwe na usalama moyoni, je mkiongea jambo likamkwanza..tafadhali...’ nikasema.
‘Madamu,…siwezi kusema kitu, nitakuambia nini sasa, mimi sijui kaniitia nini, huenda ni maswala mengine,...tafadhali nielewe hapo, tutalumbana hapa bure na sitaweza kukuambia kitu…’akasema
‘Sasa naona unataka na mimi nifanye kazi yangu,… hebu sikiliza,
huyu mume wangu anaumwa, na mara kadhaa amekuwa akipoteza fahamu kwasababu ya
shinikizo la damu..na madocta wakashauri
tusiwe tunamshinikiza kwenye mambo ya kumfikirisha sana,…sasa wewe eeh,…,
hivi nikuulize..kama tukiongea hapa nisipokubaliana na nyie,akashikwa na hasira
akadondoka, ....huoni kuwa utajiweka kubaya...’nikasema.
‘Haiwezi kutokea hivyo madamu..nakuhakikishia hilo…halafu
nikuambie kitu, mimi sijafika hapa kwa ugomvi na wewe kwanini tusielewane...eeh,..na ama kwa huyo mumeo yeye ni rafiki yangu toka siku
nyingi, wewe tu ndiye uliyeingilia urafiki wetu, na kunipiga marufuku nisiwe
naonana na yeye, sawa mimi nilitii...'akatulia
'Sasa umefuata nini tena, nilishakupiga marufuku...'nikasema
'Mumeo anaumwa, na nirafiki yangu, mimi ni binadamu, kuumwa ni kitu kingine, unanisikia sana..sitaweza kuwa na amani, bila kuja kumjuliahali..kwa hapo nilivunja agizo lako samahani sana..’akasema
‘Kwahiyo kumbe ulikuwa unakutana naye mara kwa mara au sio kwa kujifanya wewe ni mwema, au sio…’nikasema
‘Madamu ni wewe tu hunifahamu, mimi ni mtu mwema sana…sina ubaya na watu, mimi ni mtu wa
watu hasa wale wanaotaka huduma zangu…na kwa huyo mume wako, yeye tumeshibana sana,
lakini tunaheshimu tu maagizo yako…kiufupi, wewe usiwe na wasiwasi kabisa na
mimi, ni wewe tu madamu....’akasema.
‘Tatizo ni hivi..kauli yako na nafsi yako ni vitu
viwili tofauti, mimi nakufahamu sana wewe ulivyo, upo tayari kufanya kazi yoyote inayohusiana na taaluma yako kwa ajili y pesa bila kujali kuwa ni kinyume na maadili yako...pesa kwako wewe ni kila kitu....na kwahiyo siwezi kukuamini
kwa lolote lile utakaloongea na mume wangu, la sivyo, liwe halinihusu mimi, unanisikia..’nikasema
‘Hamna shida, ni wewe madamu…’akasema
‘Ila nakuonya, kama utafanya jambo la kumweka mume wangu kubaya,
..kama kuna njama za kumrubuni mume wangu kwa minajili ya kuchuma pesa kwa kutumia mgongo wake..., mimi na wewe tutapambana, kwanza nikitoka hapa
nakwenda kutoa taarifa polisi…’nikasema
‘Mimi hayo siyafahamu…nijuavyo mimi ni kuwa katika kumsaidia mume
wako, nitakuwa nimechangia kwa kiasi kikubwa, kumaliza matatizo yake ya kiafya,
hilo nina imani nalo, kwa kiasi kikubwa nitakuwa nimemaliza jambo linalomsumbua sana mume wako,…je huo nao ni utapeli,..’akasema
‘Wewe ni docta au mganga wa kienyeji...?' nikauliza
'Mimi ni wakili, wakili wa kujitegemea...'akasema
'Hivi wewe hukumbuki kuwa polisi bado wanakuchunguza kwa tabia
yako hiyo ya utapeli,..au unataka kufanya nini tena, unafahamu bado kesi yako
ipo polisi au nikawaite polisi waje wakuchukue?’ nikamuuliza.
‘Hahaha, madamu, tafadhali, ...mimi sio tapeli,....polisi, nilishamalizana nao, hakuna kesi yoyote dhidi
yangu, kawaulize ...., na hilo la kuwaita, usiogope kufanya hivyo, kama unaona ni
njia sahihi ya kumsaidia mume wako haya, karibu, lakini nakuhakikishia mimi nitaweza kumsaidia mume wako kwa kiasi kikubwa sana…’akasema akitikisa kichwa kidogo.
'Sitaki huo msaada wako, siku zote nahangaika naye, leo umeona kapata nafuu, unataka kumpandisha tena shinikio la damu, ngoja nikaongea na docta wakutoe humu ndani...'nikasema
‘Nikuambie kitu madamu, labda kwa taarifa tu, kipindi
uliponishitakia, nilikwenda polisi, nikawaambia waniambie kosa langu ni nini,
na kama nina kosa wanifikishe mahakamani, mbona hawajafanya hivyo hadi leo…,
kwahiyo hili la kusingiziwa utapeli, achana nalo, halina nguvu kabisa, mimi
najiamini, ninafanya kazi zangu kisheria, na wanaobisha twende mahakamani.....’akasema
na kutulia.
‘Sawa safari hii hilo litafanyika, nakuahidi hivyo…’nikasema
'Sawa ...unasema unataka kumuita docta anitoe, sawa, muite tu..usijali madamu, kama itasaidi....'akasema na mimi hapo nikasita kidogo, nikageuka kule walipo mume wangu.
**********
Baada ya kuongea na huyo mtu, nikageuka kumwangalia mume wangu, nilimuona
akituangalia tu, hakuonyesha dalili ya kuingilia maongezi yetu, alikuwa
katulia, huku macho yake yakipepesa pepesa, kama vile anajisikia vibaya, hapo
nikaona nisije nikaleta hali nyingine mbaya, nikageuka kumwangalia huyu mtu na
kusema;
.
‘Mimi nimekuelezea niliyotaka kukuelezea na mimi nimenawa mikono, na naona
hunielewi, sawa, mimi naona ni bora niondoke, ili kuepusha shari, maana mimi
nina uchungu wa mume , wewe hutojali chochote kikitokea…’nikasema
‘Ni wasi wasi wako tu madamu…’akasema
‘Ndio lazima niwe na wasiwasi huo,…ngoja nikuachie huyo mtu uendelee kumdanganya na utapeli wako, lakini kwa masharti, kama kuna lolote litatokea,mume wangu akizidiwa, au
kama kuna lolote baya, kati yako na yeye,....mimi sitasubiria polisi,
wala nani, nitahakikisha nikapasua kichwa chako kwa risasi...hilo
ninakuahidi...’nikasema na yule mtu akabenua mdomo kwa dharau na kusema;
‘Mbona mimi sina neno madamu…, mbona hunielewi, kwanini hayo yote
huongei na mume wako tu kukuthibitishia kuwa mimi sina maana yoyote mbaya, ni
kwa masilahi ya mume wako, sio zaidi ya hilo, umesema unakwenda kumuita docta anitoe, mbona hufanyi hivyo, tunapoteza muda bure, tutafukuzwa hapa na mume wako atakuwa hana amani, unajua ni nini kitatokea, ni nani atalaumiwa kwa hilo, mimi au wewe....’akasema
‘Sawa, nimekuelewa…’nikasema
‘Madam,..usiwe na wasiwasi na mimi, dada yangu, sina nia mbaya
kabisa, mimi nimetii wito kutoka kwa mume wako, kama kuna cha kulaumu, basi
mlaumu mume wako, na...nakuahidi nikitoka hapa mume wako atakuwa salama,
salamini…’akasema
‘Sawa …sasa nimekuelewa, hamna shida…’nikasema.
‘Madamu sikiliza nikuambie
wazi, wewe ndiye unayesababisha mume wako asipone kwa haraka, jaribu
kumsikiliza mume wako ni nini anakitaka, uone kama hatapona, ni ushauri wamgu wa bure
tu, hapo alipo anajikakamua tu, lakini kupona vyema ni wewe tu…shauri lako....’akasema
Aliposema hivyo, nikaona nisiendelee kulumbana naye, maana kwa huyu mtu ni mjanja sana, ukimtaka kwa maneno mtalumbana mpaka kesho;
‘Kwahiyo kwa kifupi, mume wangu anakutakia nini wewe…?’
nikamuuluza
‘Kwa ufupi, anataka mimi niwe wakili wake….’akasema
‘Wakili wake kwa kesi gani…?’ nikamuuliza
‘Sio kesi, ila ananihitajia mimi kuwa wakili wake wa kifamilia na hata mambo ya kazini kwake, ila hatujafikiana muafaka, labda leo ndio kaniita tumalizane, sina uhakika na hilo, madamu....’akasema
‘Lakini mbona tunaye wakili tayari, wa kifamilia na mambo ya kikasi, na unalifahamu hilo…’nikasema
‘Ukamuulize yeye mwenyewe, ila sijajua alichoniitia hapa hii leo, naomba usininakili vibaya...'akasema
'Ni lazima atakuwa kakuambia ni kwanini anahitajia wakili mwingine au sio...?' nikauliza kwa upole
'Ndio kasema wakili huyo hawakilishi matakwa yake, na ana wasiwasi
kupona kwake kunaweza kuwa ni mwanzo wa tatizo jingine,..kwahiyo ameniita mimi kuja
kumsaidia, na zaidi ni kutokana na ushauri wa docta, kuwa ajitahidi kuondoa
yale yote yanayomsumbua akilini...ni hayo tu ninayoweza kukuelezea, siwezi
kueleza zaidi ya hapo...’akasema
‘Wewe uwe wakili wake, ….hahaha, labda niwe maiti…’ nikasema.
‘Madamu, kwanini unasema hivyo, mimi ni wakili au sio…sasa kuna
tatizo gani nikifanya kazi za mumeo, ....cheti changu kinatambulikana kimataifa,
japokuwa fitina zimepita nyingi tu..,’akasema
‘Fitina au ndivyo ulivyo..’nikasema
‘Hao hao watu wanaoleta fitina wakikwama chini kwa chini, wanakuja
kwangu kutaka niwakwamue, na ndivyo ninavyotaka kufanya kwa mume
wako...kumsaidia rafiki yangu…kwenye matatizo yake.’akasema.
‘Mume wangu hana matatizo, kachanganyikiwa tu,na wewe unachukulia
mwanya huo kumghilibu…’nikasema nikigeuka kumwangalia mume wangu, na wakati
huo, alikuwa akiteta jambo na rafiki yake.
‘Docta kanithibitishia kuwa hali yake ipo shwari, na wala
hajachanganyikiwa, na nikimsaidia nitakuwa nimechangia kwa kiasi kikubwa
kumtibia,na nimemuhakikishia docta kuwa mimi nitamsaidia rafiki yangu apone kwa
haraka..kama unabisha, kamuuliza docta wake…’akasema
‘Kwa hili tutapambana..’nikasema
‘Hebu kwanza, maana naona vitisho vyako vinazidi, unaonaje… ,
naomba dakika kumi tu,niongee na mteja wangu, nikimalizana naye mtaongea naye,
na kama atataka kuwaambia lolote,atawaambia yeye, ila baada ya mimi kuongea
naye leo,kama kuna lolote la kumshutumu yeye, naomba mliwasilishe kwangu mimi
kama wakili wake...’akasema.
‘Tapeli mkubwa wewe...sikia nikuambie...’nikasema hivyo na
kugeukia kule alipo mume wangu, walikuwa bado wnaongea rafiki yake, na
walionekana kama wakibishana jambo fulani, na rafiki yake…baadae niliona docta
kama ananyosha mikono juu kusalimi amri,akasogea pembeni kama kukata tamaa.
Mume wangu aligeuka kuniangalia, na mimi nikitabasamu ile ya
kebehi, na yeye alipoona hivyo,akainamisha kichwa chini, na ilionekana hakuwa
na furaha , sijui waliongea nini na rafiki yake,mgeukia huyu mtu na kusema;
‘Nitahakikisha nayafahamu haya yote, na unanifahamu nilivyo...mimi
naondoka, lakini kama kuna lolote baya linaloendelea dhidi ya mume wangu, au
dhidi yangu mimi, tutapambana, ....tutaona mwisho wake, na safari hii,
nitahakikisha hurudii tena...’nikasema huku najifanya natabasamu, na huyo jamaa
akisema.
‘Usijali dada yangu, umeshaniambia hilo mara nyingi tu, usipoteze
pumzi yako, kwa kurudia rudia, kitu kisichotekelezeka,…na sioni kwa nini
usiniamini,...utakuja kunipa mkono wa ahsante, lakini nilijua na wewe unatakiwa
kuwepo ....’akasema na kuangalia saa yake.
‘Siwezi kukaa kusikiliza utapeli wako…’nikasema
Kwa muda ule nikageuka tena
kumwangalia mume wangu, na mara docta akaingia, na sasa akawa anaongea na mume
wangu, na dakitari akawa anaandika kitu kwenye kumbukumbu zake, halafu akageuka
kuniangalia mimi na kusema;
‘Kuna lolote jamani maana muda umekwiisha wa kuwaona wagonjwa,
kama kuna lolote jingine basi niwapa dakika kadhaa..au kama kuna kitu cha
kuulizaniulizeni, vinginevyo dakika zilizobakia ni z huyu mgeni wa mgonjwa, au
sio…’akasema akimuangalia mume wangu
‘Sawa kabisa docta, …na mke wangu,…’akasema
‘Hapana…nahisi ni bora mkaongea na huyu mtu wako hatutaki aina
yoyote ya malumbano, unasikia, bado upo kwenye masharti, vinginevyo, usibiria
mpaka hali iwe sawa, kwa vipimo vyako, bado kidogo…’akasema docta.
Mimi nilimwangalia mume wangu, yeye alibenua mdomo kama
kulazimisha kutabasamu, lakini kwa undani zaidi machoni, niliona kama ana
huzuni, nahisi mume wangu yupo kwenye matatizo makubwa..
‘Huyu mtu ana nini, kwanini amchukue huyu tapeli, sio bure, kuna
tatizo hapa…’nikasema kimoyo moyo
Hapo sikutaka kupoteza muda, au kusikia kile alichosema mume wangu
kuwa na mimi natakiwa niwepo,..., nikageuka, na kuanza kutoka nje,...na kabla
sijafika mbali nikasikia mtu akiniita nyuma yangu, sikutaka kugeuka kwani
sikutaka kuongea naye, lakini huyo mtu hakukata tamaa, alinikimbilia na
kunishika bega.
‘Kwa hali ilivyo , nakushauri, acha wafanye wanavyotaka, ili
kuepusha shari...naona kuna kitu kinaendelea , usipokuwa makini, utaumia, na
unaweza ukampoteza mume wako…’alikuwa na docta rafiki
‘Wacha itokee hivyo, mim sijali tena…’nikasema
‘Lazima ujali huyo ni mume wako…na kwanini hukusubiria ukasikia
wanataka kuongea nini, hasira zako zinakufanya ukose maana…’akasema
‘Acha nikose hadi hapo najua nimesimama na nani, na ni nani adui
yangu, ila kwa mume wangu najua kuna mtego, kategewa na huyo mtu, huyo mtu ni
tapeli, sio bure,..mume wangu anafanya kwa nguvu za….’hapo sikumalizia
‘Hahaha, sio kweli, mume wako anafanya hivyo kujihami, anajua
akipona hapo, utaweza kumshitakia kwa wazazi wako, hiyo ni moja ya sababu lakini pia pia kuna huo mkataba wenu, mimi
sijui unahusu nini, unaweza ukawa ni
sababu nyingine kubwa sana…au..ni ..nakumbuka kuna kipindi ulipokuwa unasomea
sheria ulisema ungelipenda kitu kama hicho…’akatulia akitaka mimi nisema neno,
lakini sikusema kitu
‘Basi kama mlifanya hivyo, mkawa na mkataba kama huo…ndio
unamueweka pabaya, yategemea mumekubalinana nini, maana naona hicho ndicho mume
wako anakihofia sana, hasa akitaja mkataba…’akasema
‘Wala hilo kwangu sio tatizo kubwa, kama kakosea, akiri kosa, na
mimi ni binadamu, tunaweza kuvumiliana kutegemeana na hilo kosa, lakini kwa
jinsi nimjuavyo,…haweze kukiri kosa, atajibaragua na kutafuta uchochoro wa
kujitetea, sasa hilo sitaweza kulivumilia, bora mkataba ufanye kazi yake nijue
moja tu…’nikasema
‘Kutegemeana na kosa,…nakunukuu, je kama kosa ni hilo la kuwa katembea na rafiki yako,
na sasa kazaa naye,utalichukuliaje hilo…’akasema docta
‘Weeeh, mungu wangu, na rafiki yangu, hapana..ingelikuwa na mtu
mwingine baki, hata hivyo, kwenye mkataba hilo ni kosa kubwa, halina msamaha…haaah,
hapana, hawezi akafanya hivyo, maana anafahamu madhara yake…’nikasema
‘Mhh…sasa hilo, nahisi ndilo linamtesa, na huko kuhangaika kwake
yawezekaan ikawa ndio sababu, ..lakini sioni ni kwanini amtafute wakili, hapo
ndio nakuwa na mashaka,…ina maana kweli, huwezi kumsamehe..?’ akauliza
‘Kama mtu akivunja masharti ya ndoa, kama hivyo, akazini nje, ..na
ushahidi ukawepo, basi kakiuka mkataba, na adhabu yake ipo wazi, hatuwezi
kuchezea kiapo, tuliapa na kukubaliana, je kama ingelikuwa ni mimi
angelifanyeje, mkuki usiwe kwa nguruwe, sasa akiri tuone, nita…haaaa…..’hapo
sikumalizia, kwani simu ya docta iliita, na kwa haraka akaipokea, na akawa
anasikiliza kwa muda, na alipomaliza, akaniangalia na kusema
‘Rafiki yako ameshafika,alikuwa akikuulizia, anasema kajaribu
kukupigia kwenye simu yako lakini ulikuwa hupatikani....’akasema na mimi hapo
ilikuwa kama mshtuko mwingine tena kama mtu kanipiga kibao cha kushtukizia usoni..nilishtuka
kweli, na muda huo nilikuwa nimeshikilia mlango wa gari, ukiwa nusu wazi,.. nikajikuta
naufunga huo mlango badala ya kuufungua.
‘Ka…ka…ooh, ….’nikashika kichwa na kutulia kidogo
Kwakweli pale nilihisi moyo ukinienda mbio, kama vile hasira,
au…kutaka kufanya jambo. Nilibakia vile kwa muda, baadae docta akanisogelea
akitaka kunishika, lakini kwa haraka nikaweka mkono kama kinga, asinisogelee,
halafu nikauliza.
‘Yupo nyumbani kwake?’ nikawa nimeinamisha kichwa chini
sikumuangalia docta.
‘Ndio, yupo nyumbani kwake…’akasema
‘Na mtoto wake hajambo…?’ nikauliza
‘Atakuwa hajambo, lakini hakuongelea lolote kuhusu mtoto wake na
mimi sikumuulizia hilo....’akasema.
‘Sawa bosi…’nikasema hivyo
‘Hahaha mpendwa, nimekua
bosi tena, sikiliza ex-wangu,...napenda nikushauri jambo la kutoka moyoni…’akasema
‘Sihitajii ushauri wako…, hivi sasa sitaki kumuamini mtu zaidi ya
wazazi wangu tu, nimeona wazazi wangu …ndio wa kuamini, waliyonishauri nikawapinga
sasa ndio naona matokeo yake, nayaona, lakini sitakubali…’nikasema
‘Sikiliza tu… ninachopenda kukuambia ni kuwa kwa jinsi haya mambo
yanavyokwenda, unanihitajia sana kuwa na mtu wa karibu sana wa kukusaidia, mtu
anayeaminika, kwasababu nakuona upo katikati ya watu ambao unahisi ni marafiki
zako kumbe pembeni wanakutendea visivyo…’akasema
‘Na mmojawapo akiwa ni wewe…’nikasema
‘Sawa kama utaamini hivyo…ila ukweli ndio huo, hao unao-ona ni
marafiki zako, hao hao wanaweza kugeuka kuwa ni maadui zako wakubwa.....hebu
fungua macho na masikio yako unisikilize angalau kidogo....’akasema.
‘Ni kweli unayoyasema, naanza kuamini hivyo,..na hao wanaojifanya
ni marafiki zangu kumbe ni maadui zangu nimeshaanza kuwaona, akiwemo wewe
mwenyewe, siwezi kukuficha hilo,..’nikasema
‘Sio kweli, mimi sitaweza kuwa adui yako hata siku moja,
nilishaapa kuwa nitakusaidia, na itakuwa hivyo mpaka mungu aichukue roho
yangu…’akasema na mimi hapo nikageuka kumuangalia.
‘Hahaha.., usijifanye kuwa wewe haupo kwenye hilo kundi, maana
wewe unauma na kupulizia,...upande mmoja unajifanya rafiki upande mwingine,
unajificha kwenye maadui zangu, nimeshakufahamu kuwa wewe una ajenda ya siri,..’nikasema
‘Sio kweli….’akasema na kabla hajaendelea nikasema
‘Hata hivyo nawaambia hivi… mimi naamini sana watu, lakini nikija
kugeuka, hutaweza kuamini kuwa mimi ndio yule mtu…na kwa hili nitapambana
nanyi, mmoja baada ya mwingine....hilo nawathibitishia...’nikasema nikionyesha
kidole cha kuapa.
‘Mhh, haya bhana, sina la kusema, lakini ipo siku utagundua huo
ukweli niliokuambia,....ila, nakupa angalizo kama mtu anayekujali,
usijidanganye sana na kujiaminisha kuwa utaweza kupambana na hao wtu kirahisi
hivyo, muhimu tafuta muda, tuliza kichwa,… usiyachukulie haya mambo juu kwa
juu, utaumia vibaya sana.....’akasema
‘Hilo sio la kunishauri mimi…, nimeshajua mwenyewe, na hujui
nilivyo, nimekuwa na subira sana, sijachukulia haya mambo kwa pupa, kama
ningelifanya hivyo, sasa hivi tungelikuwa hatuongei…nimeonekana mjinga
nisiyeona au kusikia, unajua ni kwanini…’nikasema kama nauliza na huyo docta
akaongea kama vile hakunisikia
‘Huyo wakili,…sio mtu wa mchezo mchezo kama unavyomfikiria wewe,
ana uzoefu na kazi yake…, na huko polisi anajuana na kila mtu,…hap hapo polisi
wanamtum,ia kwa mambo yao,…huyo jamaa ni mtu hatari sana...usije ukalogwa
kupambana naye peke yako...’akasema na aliposema hivyo mimi nikafungua mlango
wa gari na kuingia ndani ya gari langu, nikashusha kiyoo ili niweze kumuaga
docta.
'Kama ni mtu hatari basi kakutana na mtu hatari zaidi yake, mimi
namfahamu sana, nimeshapambana naye mara mbili na zote kalilia pua...wewe
hunijui tu…subiria uone vumbi langu, kwaheri, nisalimie mkeo…..'nikasema huku
nikikanyaga mafuta.
Niliendesha gari, kwa muda..na nilipofika mbele, nikachukua simu
yangu na kumpigia mtu wangu.
'Sikiliza..kama nilivyokuambia, kuna mtu yupo hospitali na mume
wangu, mfuatilie, hatua kwa hatua, nataka kila kitu anachokifanya..hata ukiweza
kufahamu walichoongea…, na ujue wapi atakapokwenda akitoka hapo hospitalini,
unasikia, hilo ni muhimu sana..kazi njema, ..'nikasema na kukata simu.
NB: Haya hiyo ya moto moto….
WAZO LA LEO: Sio
wote wanaoitwa marafiki ni marafiki wa kweli kwako, sio wote wanakuchekea, wana
nia njema na wewe, cha muhimu, ni kujaribu kutimiza wajibu lakini pia kuwa kuwa
na tahadhari, kwa kutokutoa siri zako, kwa kile unayemuona ni rafiki yako.
Kumbuka adui na rafiki yako ni huyo huyo anayekufahamu sana.
Ni mimi: emu-three
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment