Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha
Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..
Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.
MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.
TUPO PAMOJA DAIMA
Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;
https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:
https://www.facebook.com/diaryyangu/
`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;
Monday, October 31, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-43
Adamu, akiwa katulia nyumbani kwake, alianza kutafakari ni wapi kakosea safari hii, akaona kila kitu kilikuwa kama kilivyotakiwa kiwe, na hakuwahi kufanya makosa, sasa iweje siri za mikakati yake ivuje, haiwezekani, labda kuwe na mtu kavujisha, na ni nani, …akajaribu kuwachuja watu wake, hakuona anayeweza kufanya hivyo, ni watu wanaoaminika sana…sasa tatizo lipo wapi,….akaanza kuchunguza mfulululizo wa matukio mbalimbali hadi kufikia siku ya leo, ili atafute kama kuna kosa limetokea mahali, lakini kila alivyowaza hakuona wapi kwenye kosa. Sasa ina maanisha nini, …ina maana huyu jamaa kaweza kupeleleza na kupenya kwenye himaya yake, ….haiwezekani, kama ni hivyo inamaanisha nini, ina maanisha kuwa mwisho wao umefikia, hapana, bado kabisa,…
Akamuwaza Inspekta, ambaye anaogopwa kama nyoka, huyu wamemjaribu kwa kila njia ili awe kwenye watu wao lakini wameshindwa, walipoona hivyo wakabuini njia ya kummaliza, lakini wakahofia kufanya hivyo, kwani yeye sio raia wa nchi na mtu wa serikali ya nchi jirani, wa ngazi ya juu, kummaliza kunahutaji mikakati ya hali ya juu. Baadaye walikubaliana kuwa wasimmalize kama wanavyowafanyii wengine, wakabuni nia mbadala, na hapo akaumbuka hotuba yam mmoja wa walimu wao alivyosema…, ….
‘Katika kazi zenu zote hakikisheni hamuwagusi watu wa mataifa mengine, majirani , …hatutaki uadui na mataifa mengine au majirani zetu, lengo letu ni kuitengeneza nchi yetu kwa kuwaondoa watu wabaya, lengo letu ni kuondoa mafisadi walioifanya nchi hii ya kwao, ..lengo letu sio kuleta uadui na majirani zetu….’alikumbuka hotuba ya mwalimu wao akiwa kwenye mafunzo mafupi.
‘Mfano mzuri ni Inspekta aliyeletwa toka nchi jirani, huyu ni mbaya sana, lakini kaja kwa mkataba wa muda mfupi, ataondoka, tutaendeela na mambo yetu, kinachotakiwa ni kumbabaisha kwa kesi nyingi, kiasi kwamba atashindwa ashike ipi ache ipi….’ Walielekezwa jinsi ya kufanya, na ndivyo walivyofanya na kweli walifanikiwa, maana kila kukicha kuna tatizo…
Akakumbuka jinsi alivyokutana na Inspekta siku ya leo,kuja kwake imekuwa ni kwa kushitukiza sana, na hakujua kwanini hakupata taarifa toka kwenye vyanzo vyao vya habari, na hili linampa mashaka kuwa watu wao waliopo huko wanazembea, inabidi kutoa taarifa kwa wafuatiliaji, waangale kuna kosa gani. Haiwezekani mtu mkubwa kama huyo kuamua kuja huku bila ya watu wao kujua, haiwezekani… . Alitaka kupiga simu kwa vyanzo vyake vya habari, lakini akaona itakuwa sio vyema,inahitaji muda wa kufanya utafiti.
Kuja kwa Inspekta kwa kushitukizia kumeharibu mipangilio yake yote ya siku, …ilibidi amuwahi Rose kabla hajaondoka, na alimpomkumbuka Rose, mwili mzima ulisisimuka, akaivuta sura yake na kuiweka mbele ya uso wake, akatabasamu, ….`kwanini huyu binti ananipa shida sana, …kwanini nismpate mwingine badili yake, …oh jamanai kupenda kubaya…’ Akainama cini kwa huzuni, akijua kuwa sasa Rose keshamkosa, ….Alipomuona mchana ule kule ofisini, alijua sasa mambo yanaanza kuja vyema, alijua Rose kajileta mwenyewe, ..kwanza kwasababu yule mtu aliyekuwa kikwazo keshaondoka, …huyo ni kazi ya polis kuhangaika kutafuta muuaji ni nani.
Lakini alisngaa kusikia kuwa Rose ana mtu mwingine, na mtu huyo ana sifa za kufuga ndevu, …aliwambia watu wake wamchunguze ni nani,lakini taarifa alizokuwa kazipata zilimtia mashaka kuhusu utendaji wa watu wake, …akawaagiza wafanye lile aliloona ni muhimu kwake, …akatumia ujuzi wake na hatimaye akafanikiwa kwa kuua ndege wawili kwa jiwe moja, …kumuondoa mbaya wake na kumbambikia kesi huyo jamaa ambaye alionekana naye kajificha, kwani tangu aingie humo hotelini hakuwahi kuonekana tena, hiyo sasa ni kazi ya polisi kumtafuta yupo wapi nan i nani, wakimuona watamuandama kama muuaji, siku zinakwenda mambo yanakwenda kama walivyopanga.
Lakini ghafla Inspekta kaibuka ….inaonyesha kuna siri zimevuja mahali, na hii inaashiria balaa, lazima uchunguzi mkali ufanyike. Hata hivyo inavyoonekana kuna tatizo , huenda ni la uongozi au kuna watu wameshaanza kuisahau, inasikitisha kuona kwamba baadhi ya viongozi wameshaanza kum,uingilia katika utendaji wake, nah ii inaweza ikawa sehemu inayochangia kuvujisha mambo, …katika makubaliano yao, haikuwa hivyo…..
Baada ya kuachana na Inspekta, aliangalia saa yake na kukuta muda umekwenda sana, na kwa vyovyote kama Rose alikuwa mtu wa kurudi mjini, atakuwa keshaondoka, kwahiyo hana jinsi, kama kweli bado ana nia naye lazima amfuate mjini, na hilo ni lazima, ..ni lazima amshawishi arudi kazini, nan a kumweleza ndoto yake ya kuanzisha hospitali yao,…alipowaza hilo alimlaani sana Inspekta, hakuwa anataka kabisa kutembelewa na mtu kama huyo, kutembelewa na mtu kama huyo akiwa haumwi, inabashiria hatari…
Akaangalia saa yake tena kuona kama anaweza kwenda kumbahatisha Rose, akasema kimoyomoyo, kwa vile alikuwa hana kazi ya kufanya kwa muda ule ajaribu kumbahatisha, kama hayupo basi atakwenda ufukweni kupoteza muda, akatoka pale nyumbani kwake huku akiwaza mazunguzmo yake na Inspekta, yalivyokuwa, licha ya kumpiga chenga kwa maswali yake, lakini aligundua jambo kuwa keshamhisi kitu, kuna kitu wamgendua, lakini kama wamgeundua kitu mbona hajapata taarifa yoyote, haiwezekani kuwa watu wao waliopo ndani ya polisi hawakuweza kujua lolote linaloendelea huko, …akawaza baazi ya maswali aliyoulizwa na Inspekta kujaribu kuangalia kuwa anaweza kugundua kitu..
‘Sikiliza Docta, wewe ni mtu muhimu sana katika nchi yetu hii, na kwa ujumla tulikuwa
tunawahitaji sana, sio tu katika utaalamu, lakini katika kuhakikisha nchi yetu inasimama vyema, …katika uchunguzi wetu, tumejikuta tunakuhitaji wewe katika kutusaidi maswali machache…’akasema Inspekta.
‘Kama ni maswali yanahusiana na polisi na sheria naomba niwe na wakili wangu, tafadhali…’alisema Docta Adam, akajirabu kumkwepa Inspekta, lakini haikuwa akzi rahisi.
‘Kwanini mnapenda kukimbilia wakili, …kama kweli unajiamini huna hatia, kwanini umuhitaji wakili, sio mbaya ni haki yako,sawa, …kwasababu mna pesa za kuwatumia hao watu, lakini ninachotaka kuongea nawe sasa hivi ni maswali ya kirafiki tu,…nia yangu kubwa ni kutafuta jinsi ya kuleta amani na utengamano, kwa njia ya majadiliano…sipo huko kwenye kutiana hatiani, …’alikumbuka hotuba ya Inspekta.
‘Nawajua sana nyie mapolisi, mnapenda kujifanya kuwa mnaongea kama marafiki, lakini mwisho wa siku kila ulichoongea hapa kinachukuliwa kama ushahidi…hapana, sipo tayari kwa hilo…’aliongea kwa mbinu za kujitetea, lakini alijiona kama anakwepa kupambana na adui yake, kitu ambacho hakukikupenda .
‘Kuna mgonjwa aliwahi kuletwa hapa kwako, mgonjwa huyo alikuwa amechanganyikiwa na huyo mgonjwa alikuwa akifanyakzi kwenye kikosi maalumu cha jeshi cha silaha, na alikuwa mtalaamu sana, alikuja hapa mkamtibia na baadaye akaondoka,unamkumbuka huyo mgonjwa…?’ swali hilo aliliona lina mtego, lakini alishajiandaa kwa swali kama hilo, kwaahiyo halikumpa shida ya kulijibu.
‘Yawezekana, kwasababu wanakuja wagonjwa wengi, na sisi hatuna dhamana ya kuwauliza wagonjwa kila kitu kinachohusu yeye kama hakihitajiki katika matibabu yake,…kwa ujumla sina kumbukumbu ya mtu kama huyo, ikizingatia kuwa mimi sio docta wa kukutana na wagonjwa wote, labda iwe ni kwa tatizo maalumu, hata hivyo, siwezi kukataa kuwa wagonjwa kama hawo hawajawahi kufika hapo hospitlini, wamefika wengi, sasa kujua yupi ni yupi unayemuulizia itakuwa kazi kubwa kuhisi…’alikubuka jinsi alivyomjibu Inspekta.
‘Utakuwa unamjua namzungumzia nani, …unachojaribu ni kukwepa kuniambia ukweli, ila kama unataka nikukumbusha kidogo, ni kuwa huyo jamaa, alikusababishia mpaka ukachukuliwa hadi kikosi cha jeshi,…kwa ujumla huyo mtu ni mtu hatari sana, kwani yeye anautaalamu wa silaha, ndiye anayetengezeza silaha za hatari hapa nchini, pia ana utaalamu wa kila namna, …tunamtafuta sana, …na licha ya hilo huwa akianza kuchanganyikiwa anaua ovyo…inawezekana utaifanya humjui, lakini ni kwa manufaa ya taifa lako, ni kwa manufaa ya kizazi chako, kwasabaabu kizazi chako kitahitaji maendelea, jamaa na ndugu zako wanahitaji amani, na amani haitapatikana kwa namna hii…ubinfasi wa kutaka kupata zaidi wakati wengine wanaumia, huo ni uufisadi..’
‘Kwanini unaniambia haya yote, kwanini unanipa huu muhadhara…sijaelewa Inspekta…’akauliza Adam
‘Najua unaelewa, lakini tatizo ni kuwa hatutaki kuona mbele pale tunapojiona kuwa tumefika, fikiria hali ya jamii, hali ya vizazi vijavyo, fikia maendelea ya watu, …je umemkumbuka huyo jamaa?’ akauliza inspekta.’
‘Mimi ninayemkumbuka ni...jamaa mmoja ambaye baadaye hata hawo wanajeshi walikuja kugundua kuwa sio yeye walimfananisha tu, na wengine walikuwepo, lakini labda warudi tena hapa nianza kuwakumbuka, …’akasema A dam.
‘Kwahiyo unakumbuka kuwa walikosea wakamshika jamaa asiyehusika, unaweza kuniambia kwanini huyo jamaa unamkumbuka vyema…?akauliza Inspekta.
‘Kwasaababu aliendeela kuwa mgonjwa wetu baadaye, na akawa katika mikono ya msaididzi wangu , kwani ilionekana kuwa hajapona vyema, na ata hivyo ametoweka, sijui yupo wapi, kama ndio hilo unalohitaji…’akasema Adam.
‘Ametowekaje, na wakati wewe umesema alikuwa katika mikono na msaidizi wako, huyo msaidizi wake ni nani na yupo wapi? ‘akauliza Inspekta.
‘Msaidizi wangu anaitwa Rose, yupo likizo, zaidi kama unahitaji kuhusu huyo mgonjwa utayapata kwake…..’akabla haja,alaiza simu ya Inspekta ikaita, na inspekta ilisikiliza kwa muda, halafu akaikata na kutulia kimiya kwa muda baadaye akasema;
‘Nitakuacha kwa muda, kama hutojali, nitakuja kukutembelea muda si mrefu, nina mangi ya kuongea na wewe, hasa kuhusiana na kazi nyingine unayofanya zaidi ya huo udakitari, ni vyema tukasaidiana kwani kila jambo lina mwanzo namwisho, na lazima hali kama hii ifike mwisho, tusema basi, sasa turudi nyuma na kuamua kulienga taifa…’akasema Inspekta na kumuacha Docta akiwa kaduwaa….
*******
Inspekta hakuamini, jinsi huyo mtu alivyotoweka kama upepo, hakuamini kabisa, kwani alikuwa na uhakika kuwa yupo nyumbani kwa Rose, na alionekana wakati anaingia, lakini hakuonekana wakati anatoka, ina maana Rose alimficha, haiwezekani, …alitafuta kila kona ya nyumba, lakini hakuona dalili ya mtu huyo, na hali ya hewa ingelibadilika mle ndani, kwani mtu huyo kinachomponza ni harufu inayotoka mwilini mwake, licha ya harufu ya majasho, lakini ana harufu fulani ambayo humtoka hasa akitokwa na jasho.
Hakuiskia hiyo haurufu na wala hakumkuta huyo mtu, na haiwezekani awe amejificha mahali, haiwezekani, …Inspekta akiwa kairudisha bastola yake kwenye koti lake, alimwangalia Rose akiwa kasimama huku akiangalia huku na kule bila kujua nini kinachoendelea..
‘Binti, kuna mtu alikuwepo humu ndani, na hatukumuona akitoka, hebu niambie kaelekea wapi, au umemficha wapi, …huyo jamaa ni hatari, anatafutwa akiwa hai au mfu, tunakuomba kama unajua wapi alipo utuonyeshe, …’akasema Inspecta akiwa anamsogela Rose.
‘Hivi ndio heshima gani, …au ndio tuseme kwasababu nyie ni maaskari mnaweza mkaingia nyumba ya mtu bila hodi na kuanza kupekua pekua kila mahala, …hiyo sheria imetoka wapi, …’Rose akapata ujasiri wa kuongea.
‘Kama ungelikuwa hatarini usingeliweza kusema maneno kama hayo, ninakuhakikishia kuwa huyo mtu uliyekuwa naye muda mchache uliopita ni hatari kuliko unavyowaza wewe…tafadhali binti , usinipotezee muda, naomba uniambie wapi alipoelekea huyo mtu..’akasema Inspekta.
‘Mim sijui unachozungumza, mtu gani, …kama engelikuwepo humu na mumemuona sasa kaenda wapi, …huyo aliyekudanganya nenda kamuulize vyema,. …tafadhali naomba nifunge mlango kwani naondoka..’akasema Rose akionyesha kukasirika.
‘Nchii bwana, kweli mnanishangaza, mnaishi na nyoka, hamuogopi, na wakati watu tunataka kuwaondolea hatri hamtaki kutoa ushirikiano, haya, …kaeni na nyoka zenu, lakini nawaambia kuwa hilo mnalolianya ni jambo la muda mfupi tu, halitawasaidia mbeleni, kizazi kijacho kitakuja kuwalaumu, kwasababu hawo watu ni waharibifu wa mali , ni waharibifu wa kuhamisha maliasili kwenda kusikojulikana, wakiagiza masilaha, yasiyoisaidia serikali, sisi tunajitahidi kuwaondoa ili kuwa na amani, lakini raia mnatuangusha,kwasababu mnaishi na hawa watu, mankula nao, …mnatembea nao, mnawajua, lakini hamtaki kuwataja, ili tuyamalize haya matatizo….’akasema Inspekta.
‘Tatizo mimi sijui nini unachokiongea, ningelijua ningelikusaidia,…’samahani sana, …’akasema Rose, akionyesha kidole kuwa Inspekta atoke nje. Inspekta hakutaka ubishi alitoka nje huku akimwangalia Rose kwa makini, na akilini alikuwa akijisema `huyu binti haiwzekani akawa anshirikiana na hawa maharamia, haiwezekani akawa jambazi,…sikubaliani na hilo…’
‘Sawa binti, ila kama unaijali serikali yako,na unawajali watu wasio hatia, ambao kila siku ya mungu wanauwawa bila makosa, ungelisaidia …na pia nilikuwa na mazungumzo na wewe, nashukuru kuwa nimekukuta kabla haujarudi mjini, …ila kama una haraka, basii tutakutana huko mjini, lakini tukikutana huko mini, nitakuwa mtu mwingine….unasemaje , nakuomba tuongee kwa marafiki wanaotka kuiondoa ncho hii kwenye majanga yasiyofaa…unasemaje..binti…’akasema Inspekta.
‘Kwani wewe ni nani, kwasababu ulipoingia hukujitambulisha, nimekuona kama jambazi fulani…sasa hivi tunshindwa kujua nani mwema na nani mbaya, …’akasema Rose huku akiwaza, kuhus huyu mtu alimuona wapi, sura inaanza kumjia kuwa ni mtu fulani aliyewahi kumuona mahali, lakini hakuweza kukumbuka vyema.
‘Mimi ni mwanausalama, mimi ni askari polisi na lengo langu kubwa lilikuwa kuja kumkamata huyu jambazi mkuu, huyu aliyekuwa humu ndani ni miongoni mwa viongozi wanaoendesha hujuma maporini, sijui kwanini wanafanya hivyo, kama wanataka uongzi kwanini hawajitokezi wakapewa nafasi ya kuomba kisiasa, wao wanatka fujo, umwagaji damu, hatuendi hivyo, na kama wewe utagundulika kuwa unashirikiana na wao basi sheria itachukua mnkondo wake…’akasema Inspecta.
‘Mimi huwezi kunitisha kwa hilo, kama wewe ni polis naomba kitambulisho chako, maana kila mti sasa ni polisi..’akasema Rose.
Inspekta akamwangali kwa makini, halafu akatumbukiza mkono wake kwenye mfuko wa shati, ambali lilikuwa limefunkwa na koti alilovaa, akatoa kitambulisho chake na kumsogela Rose, …Rose akanyosha mkono kukipokea, lakini Inspekta akawa amekishika , huku amekifunua, …ile picha ple kwenye kitambulsisho ilionyesha dhahiri kuwa huyo ni nani, akamkumbuka ….
‘Mungu wangu…samhani sana, …Inspekta, sikukujua kabisa, samhani sana,…’akasema Rose huku akitaka kupiga magoti.
‘Usijali, ni haki yako kufanya kama ulivyofanya ndio maana sikutka kutumia nguvu ya dola, na nakuomba kama una nfasi naomba tuongee, kama huna nafasi basi tukifika mjini nitakuhitaji ofisini tuongee…’akasema Inspekta, hakutka kuyachukuli ahay amaswla kiharaka haraka kama wenzake wanavyofanya, alishaua njia iliyokuwa ikitumika ya ubabe kwasasa haina nafasi, watu wataishia kuuana na kuwekeana visasi bila mafanikio, lazima atumie njia nyingine ambayo ni ya taratibu lakini ana uhakika italeta mafanikio.
‘Kwakeli nina haraka natakiwa kufika leo huko mjini kabla ya saa kumi na mbili kutokana nakibali nilichopewa, sasa naona muda umekwsiha sana, sijui nitafungwa….’akasema Rose.
‘Basi tutaongozana, usiwe na wasiwasi gari langu lipo njiani linakuja kunichukua, na wakati tunalisubiri nilikuwa naomba nikuulize maswali machache kama hutojali, hayahitaji kuwepo wakili wako, ni ya kawaida tu..
Rose liposikia wakili, akaukumbuka onyo la yule mtu anayetafutwa na huyu polisi, kuwa huyo wakili ni miongoni mwa maadui zake, sasa atafanyaje, …akawaza kwa uandani na kuahidi kutokumtegemea tena, na akainua kichwa na kumwangalia huyu askari, …akaumbuka jinsi watu wanavyomuongelea kuwa ni mtu wa msimamo, mchapakazi, na hata moyoni akaingiwa na imani naye, akaona ajaribu kumwamini lakini hakuwa na uhakika, kwani hakuna mtu aliyekuwa akimwamini kama Docta Adam, kumbe sasa…
‘Maswali gani hayo, maana kama nikuhusiana na mauaji ya kule mjini mambo yapo kisheria na sisitahili kuongea kinyume na makubaliano, kwahiyo naomba kama ni mongezi yawe ya kawaida tu…’akajihami Rose.
‘Unajua Rose. Wewe ni msomi...' alisema Inspekta na kumsogelea karibu.., `Na zaidi upo katika idara ya kuhudumia wananchi, ili wasipoteze maisha yao, na hili ndilo hata mimi najaribu kilifanya, watu wanauliwa ovyo, hawana hatia watu wanaishi maisha ya wasiwasi, yote kwasababu ya vikundi vya watu wachache wanaojifanya wanajua kutumia silaha…na ili tuweze kuwashinda hawa watu tunahitajika kuwa na umoja…kati ya sisi maaskari , na nyie raia wema, …’akasema Inspekta.
‘Sawa nakusikiliza, uliza hayo maswali, nitaangalia kama naweza kuyajibu au la…
Mara wakasikia mlango ukigongwa, Inspekta akachomoa bastola na kujibanza pembeni ya mlango na kumuonyeshea ishara Rose afunhue mlango na asiseme lolote kuhusu yeye, …Rose akasoegelea mlango na kwa wasiwasi akaufungua mlango….oh…..
NB:Tuonane sehemu ijayao...Najiuliza mbona maoni yanapungua siku hadi siku, au labda kisa kimekuwa kirafu sana,...nahitaji maoni na ushauri wenu!
Ni mimi: emu-three
Friday, October 28, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-42
‘Natumai unanikumbuka Docta Adam,..’Sauti ya kikamavu iliyosikika ilimshitua Docta Adam , karibu adondoshe ule ufunguo aliokuwa kakamata mkononi, akainua kichwa haraka na kumtizama huyo mtu. Na huyo mtu alimkaribia na kuja kusimama karinbu yake huku akisema `Samahani kwa kukujia muda kama huu, ni tatizo la usafiri, nilikwama kidogo njiani ndio maana unaniona sijaja na gari langu…’Adamu hakuamini macho yake akasimama vyema na kumwangalia, ingawaje alikwu ana hasira za kusumbuliwa, lakini ile hasira iliyeyuka haraka na kubadilika kuwa woga na wasiwasi.
Adam alimtizama tena huyo jamaa, ili kuhakikisha macho yake, halafu akageuka kutizama mlango na kushika kitasa cha mlango na kukitikisa kitasa cha mlango kama vile anahakikisha kuwa kafunga mlango vizuri, kumbe ilikuwa hali ya kuvunga, ili huyo jamaa asimwangalie machoni, moyoni alishashikwa na wasiwasi, hakujua kwanini moyoni alikuwa akihis hivyo, hali ambayo hakuwahi kuihisi…akajipa moyo kama vile yupo vitani akageuka na kumwangalia yule jamaa, halafu akajifanya mnyenyakevu, akijua kuwa huyo aliyepo hapo ni mtu muhimu wa serikali, akatabasamu kiuongo-uongo na kusimama kama vile askari afanyavyo, akasema kwa sauti ya mkwaruzo.
‘Jambo afande, …mkuu, ..Inspecta, habari yako mkuu, sizani kuwa umenijia kwa jambo dogo hasa kwa muda kama huu, ndio nilikuwa nafunga funga, ofisi, na mimi nikapate muda wa kujipumzisha unajua tena hizi kazi zetu muda wowote unaweza kuitwa, hizi kazi zetu hazina tofauti na kazi zenu, …kwahiyo ukipata upenyo wa kujipumzisha unatakiwa uutumie ipasavyo, ndio mkuu nikusaidie nini…?’ akaongea kwa kujiamini, lakini moyoni alishatingwa an mashaka, kwanini huyu mtu amjie , toka mjini hadi huku anafuata nini..!
‘Ndio , sio jambo dogo, ukizingatia kuwa nina majukumu ya kiofisi, lakini …wakati mwingine unatakiwa kuwasaidia vijana, ….kwani mimi siwezi kuumwa docta, huenda nimekuja kutibiwa, ….au ukishafunga, hata akija mgonjwa taabani hihitajiki kutoa huduma….?’akauliza huyo jamaa.
‘Inategemea ugonjwa na mgonjwa, …na ujuavyo, kila ofisi ina utaratibu wake, kama ni mgonjwa wa dharura kaletwa baaada ya muda wa kazi, atakutana na dakitari wa zamu, lakini hawezi kuja kwangu moja kwa moja…labda iwe na mimi nipo zamu, maana hata mimi kuna kipindi nakuwa zamu, ikibidi…’akasema Adam.
‘Basi mimi ni mgonjwa maalumu, ndio maana nimekuja kwako moja kwa moja, …sawa, kwa ujumla nisingetakiwa mimi nikujie mwenyewe moja kwa moja, lakini wakati mwingine inabidi iwe hivyo,…na ili nisikupotezee muda wako, kwasababu sina usafiri, basi tutaongea tukiwa ndani ya gari lako, kama hutojali, au tukifika mahala patulivu tusimame kidogo tuongee, ni maswali machache ya kuhakikia, nina uhakika sitakupotezea muda wako mwingi…nahitaji saan ushirikianao wako…’akasema Inspecta.
Adamu aliposikia hivyo akaanza kujihami, kimoyoni alianza kumuwaza huyu mkuu, alishasikia sifa zake, na huwa anamuona tu juu kwa juu, hakuwahi kukutana naye na kuongea kwa karibu, leo ndio mara ya kwanza kuonana naye kwa karibu na sio karibu tu, ataka kuongea naye, sijui kuhusu maswala gani. Alianza kujipnga kichwani, vipi atamjibu, na kama ikiwa ni maswala magumu , dawa pekee iliyopo ni kusema asubiri ataongea wakili wake akiwepo…
Mkuu huyu wa polisi aliletwa hapa nchini ili kutoa mafunzo katika ile hali ya ujirani mwema, nchi hizi zimelkuwa zikibadilishana wanausalama wao, na hii imekuwa ikitoa changamoto, kwa kujenga ushindani fulani. Huyu mkuu alipoletwa alionekana mchapakazi , na hakuna mtu aliyeweza kumwingilia katika majukumu yake. Wapo waliojaribu kumbadilisha ili ashirikiane nao, lakini haikuwa rahisi, alikuwa mtu wa msimamo, na wahalifu wengi walikuwa wakigwaya pale wanapomuona.
Katika mafunzo yake , Adam, alikuwa kasomeshwa jinsigani ya kupambana na watu kama hawa, kwahiyo haikumtia shaka sana, ila kilichomtia shaka ni kutaka kujua nini kilichomleta, kinahusiana na jambo gani,…akageuka kumwangalia na kumwambia.
‘Sawa mkuu, lakini mimi nikiwa naendesha gari huwa sipendi kuongea, ….na hasa, ikitegemea aina ya mazungumzo,….ungenidokezea ni jambo gani unalotaka kuongea na mimi, ili kama…eeh, naweza kufungua mlango tuakongelea humu ndani, ni jambo gani mkuu?’ akauliza Adam.
‘Aaah, una wasiwasi na jambo lolote, sio jambo la kukutia wasiwasi, ni katika kuwekaan sawa, tu..usiwe na wasi wasi kabisa…wewe twende , na haina haja ya kufungua ofisi wakati ulishaifunga…’akasema Inspketa.
‘Nimekuuliza hivyo kwa lengo langu kubwa kama nilivyokuambia nikiendesha sipendi kuongea, pili ukiongea na polisi ni vyema kujua ni kwa kosa gani, …usije ukanitega kwa maswala yanayogusa sheria, ..' akanyamaza kidogo halafu aakendeela kusema;
'Vinginevyo kama sio maswali ya kisheria, hakuna taabu…naomba mkuu, yasije yakawa maongezi yakuniumiza kichwa…sawa haya twende, nipo tayari….’ Akasema Adamu, huku akiwa an shaka shaka, ya kutaka kujua ni nini kilichomleta huyu mtu toka mjini, …akajipa moyo na kusema kimoyomoyo,kuwa jambo jema ukikutana na tatizo ni kukabiliana na hilo tatizo ni sio kulikimbia, na ni vyema kuondoa shakashaka kwa kufanya utafiti, na utafiti wa shaka shaka kwa mwenzako ni kukubali kuingia katika mazungumzo. Kwahiyo akakubalina na Inspecta na wote wawili wakaingia ndani ya gari na kuondoka.
********
Maua hakuwa na amani, kila dakika iliyopita, aliona kama masaa, alitamani angelipaa na kurudi mjini haraka iwezekanavyo, ….pamoja na mengine kichwani alikuwa haacho kumkumbuka Sweetie, …alikuwa kamkwepa kuingia naye mazunguzo, mpaka wapate nafasi inayostahili, hasa baada ya kuona kuwa keshaanza kurudiwa na kumbukumbu zake. Pia alitaka kujipa nafasi, kujiandaa kwa lolote linalomhusu huyu mtu aliyekwisha iteka nafsi yake.
Moyoni alishajiuliza maswali mengi, kuwa kama huyu mtu kumbukumbu zimemrejea, na atasema anaye mke wake, atachuku ahatu again, wakati keshampenda, je atakubali kurahisrahis hivi hivi tu, …hapana, lazima ajitahidi kulinda penzi lake, lakinikwa njia gani kama itazihirika kuwa huyu ni mume wa mtu?
‘Lakini kama kumbukumbu zimemrejea vyema, mbona bado anasisistiza kuwa mimi ni mke wake, hii bado inanitia wasi wasi,…’akasema kwa sauti.
‘Hlafu anasema nimebadilika, kwa vipi, mke wake alikuwa vipi na mimi nipo vipi, …..ina maana kwenye kumbukumbu zake hajamkumbuka mkewe alikuwa na sura gani, ….hapa nahis ipo namna, labda sehemu ya kumbukumbu bado haijereeja vyema, na kwa sababu hii, bado huyu mtu anahitaji mapumziko ya kina, haihitaji nguvu, …lakini nitajitahidi sana kuhakikisha kuwa nalilinda pendo langu, ….nitafanya juhudi zote, ikibidi…..sijui , ikibidi, sijui…’akawa anaongea huku anajiangali kwenye kiyoo.
Alipofika kwenye nyumba ile waliyopanga, alikuta kupo kimiya, hakuon ajabu ,kwani rafiki yake hayupo, alishaambiwa kuwa kaenda likizo, kwahiyo hakukuwa na mtu wa kuongea naye, na hata hivyo..hakutaka kabisa kulala hapo kwake, alichofanya ni kufika chumbani kufanya usafi, na baadaye akaoga, na kuchukua madini yake yaliyokuuwa yamebakia na kuhakikisha kuwa kila kitu kipo sawa, halafu akatoka nje kidogo kuangali mazingira ya nje, kama kupo salama,
….alipohakikisha kuwa kupo salama, akasogelea mlengo wa rafiki yake kujaribu kuwa umefungwa…akakuta umefungwa….
Baadaye akaamua kurudi kwake, akasogelea mlango wake, …na akahisi nywele zikimsisimuka, akahisi hatari, na hali ambayo humpata mtu, hasa kiwa peke yake, na alikuwa akisi hatari, na kwa vile yupo peke yake, anaweza akzania kuna adui, au kuna kitu cha hatari kipo karibu yake…alihisi kama kuna mtu anamtizama kwa lengo kwa baya, akageuka kuangali barabarani, na huko hakuona kitu cha kutia wasiwasi, kila mtu aliyeonekana, alikuwa akitembea au akiwa katika hamsini zake…
Akafungua mlango wake…na mara pua yake ikahisi harufu ngeni….harufu hiyo alishaisikia kabla, harufu ambayo ilimtia wasi wasi, akatamani kurudishia mlango na kuondoka zake,…lakini viungo vya mwili havikukubali kufanya hivyo akasimama kama mtu aliyepigwa na ganzi, alikuwa kasimama katikakati ya mlango, ambao alishaufungua wote,….akapepesa macho huku na huko kuangali pale varandani kama atamuona mtu, …hakuona mtu, ila alihis harufu…..na mara akasikia sauti.
‘Usiogope Docta, tumekukosa sana, umeondoka kipindi ambacho tulikuwa tunakuhitaji sana, unajua Docta wewe ni mwenzetu ila hujui hilo, wewe ni mwenzetu kwaababu unajali sana maisha ya watu, unajali sana uhai wa watu, …na ndilo sisi tunalolipigania, ila watu hawatuelewi, wanafikiri kuwa sisi kazi yetu ni kuua,…lakini tunaua tu palle inapotulazimu,mfano ukikutana na adui ukamwambia nyosha mkono upo chini ya ulinzi akasalimu amri, hauwezi kumuua, unamkamata na kumfikisha kwenye vyombo vya kisheria akahaukumuiwe…’ Rose aligundua hiyo sauti inatoka wapi, lakini hakuweza kumuona huyo mtu.
‘Sasa tatizo linakuja pale unapompa mtu huyo amri, akawa kaikaidi hiyo amri, na pili hata kama atakukublai hiyo amri yako, ukemuweka chini ya ulizi, aua hataka kama kakaidi, lakini umemdhibiti, unampeleka kwenye vyombo vya sheria, sheria haifanyi kazi yake barabara,….watu wanatakiwa kutekeelza majukumu ya kisheria, hawafanyi kazi yao ipasavyo, mtu huyo anarudi uraiani na kuendeela kufanya maasi kwa kiburi….hapo tunakuwa hatuna jinsi…’ Huyo mtu alikuwa akiongea huku akufunikwa na apzia kubwa lililopo dirishani, alikuwa kasimama kwenye dirisha, na lile dirisha linapazia kubwa, ambali lilikuwa limemfunika.
‘Wewe ni nani na umeingiaje humu ndani..?’Rose akaingiwa na ujasiri wa kuuliza.
‘Tayari umeshanisahau Docta, mimi ni yule yule anayekutembelea mara kwa mara, ila safari hii umetuweza kidogo, maana, umebadili mlango,….umebadili kitasa chako…najua ni kwanini…kazi nzuri docta, lakini nilijua utakuja leo ,…wakati nakusubiri nje hukuniona, , ulipotoka tu nami nikajikaribisha ndani sisi ni wepesi sana,…., usiwe na mashaka, kabisa….’akasema huyo mtu.
‘Haya niambie safari hii nini kimekuleta , maana nina haraka nataka kuondoka …’akasema Rose, na kabla hajamaliza yule mtu akamkatiza na kusema.
‘Najua unataka kuruudi mjini, kwa ajili ya ile kesi ya mauaji au sio, …hahaha..unajua dunia hii ni ya ajabu kabisa, hawo hawo unaowaona ni wa maana kwako ndio hawo hao wanaowazungukeni, unakula nao, unashinda nao na hata unafanya kazi nao, lakini ni maadui zako..pole sana, …ila kesi yenu imekaa vibaya sana , unatakiwa kuwa mwangalifu sana, kwasababu hawo hawo wanaotka kukutetea ndio hawo hawo maadui zako, jaribu sana kuwa mwangalifu,… ndio maana kwa nia njema niliomba sana nikukute na wewe , na bahati nzuri tumekutana nawe…’akasema yule mtu.
‘Silkuelewi nini unachokiongea na hata hivyo ninakimbizana na muda, …’akasema Rose.
‘Hili ninaliotaka kukuambia sasa hivi ni muhimu sana kuliko huko kuwahi kwako, na ni kwa ajili ya manufaa yako na yule jamaa yako wanayemuita tahira, sio tahira yule, ipo siku utagundua hilo, na sio mtu wenu yule, ole wenu auwawe, na wenyewe wajue…nashukuru kuwa umechukua hatua njema ya kumlinda, na ilitakiwa wakushukuru sana kwa hilo…’akasema huyo mtu,na Rose aliona kama anampotezea muda wake tu.
;Wanishukuru kwanini…?’ Rose akazidi kuhamanika kujua zaidi, alitamani hata ake amsikilize yule mtu, lakini akaona bora asimame hivyo hivyo.
‘Kwani uchunguzi wetu, jamaa aliyemuua yule mtu kule hotelini anafanana sawa sawa na huyo jamaa mnayeishi naye, ana ndvu kama za huyo jamaa, yako, tunachojiuliza ni kwa vipi alitoka humo hotelini na kwenda kufanya hayo mauaji na kurudi , wakati ulimuacha mle chumbani…tumejaribu kumtafuta mtu mwingine anayefanana naye hatujabahatika kumgundua….sasa kuna hatari jamaa yako kukamatwa, vinginevyo apatikane mtu mweney sifa kama hiyo…hata sisi hatukubalianai na hilo kuwa ndiyo yeye muuaji , hasa ukichukua ule muda uliotumika, haiwezekani ….’akasema yule mtu na kumuacha hoi Rose.
'Haiwezekani akawa yeye, hilo mumekosea, au ndio nyie mumeafanya hayo mauaji na manataka kumbambikia jamaa wa watu, haiwezekni kabisa….’akasema Rose.
‘Kwetu sisi hatuna shaka, hiyo ndiyo sifa yetu tuliyopewa kwa sisi ni wauaji, …wapiganaji wa msituni, lakini jiulize kwanini tumuue mtu kama huyo, ili iweje, …hatuna shida naye, ila nakuonya kuwa polsi wa kimgundua tu, …oooh, huyo atakamatwa na kufunguliwa mashitaka…wenzenu walicheza vyema,..ina maana kama sio yeye, walishamgundua na kumtafuta mtu anayefanana na yeye, au mtu alijiigiza tu, na kujiweka ndvu, za bandia maana siku hizi utaalamu huo upo….’akasema huyo mtu.
‘Hilo halitatokea, huyo jamaa yangu hawezi kufanya jambo kama hilo, na kwa hali hiyo naomba uondoke nataka kuwahi huko mjini….’akasema Rose
‘ Sawa utaondoka, usiwe na shaka, ila nakupa kama tahadhari usimwamini sana huyo bosi wako, hilo tulitaka tukuambie mapema, lakini hatukuwa na uhakika naye mwanzoni, ….alijivika ngozi ya kondoo…ni hatari sana, …hawa watu wa namana hiyo, watakuja kutuletea matatizo…lakini hata hivyo, lengo lao halipo mbali sana na sisi ina wao wanatumia utaalmu wao kudai haki inayodhulumiwa, kama sisi tunavyofanya kwa njia ya msituni…’akasema yule mtu na kumfanya Rose atulie kusikiliza
‘Mimi siwaelewi, kwanini muingize nchi kwenye vita mkidai kuwa mnadai haki…kwanini msikae kwenye meza moja na serikali mkajidili hilo….?’akauliza Rose
‘Swali zuri sana, kwasababu hawataki kufanya hivyo, wangelikubali hilo, mbona tungeshamalizana, na kwanini hawataki hilo, kwasababu wanajua hawatapata hicho wanachokitaka, kuhujumu mali ya uma, kuhakikisha wao wanashikilia madaraka…na sio kwmba hatukuwahi kuomba hilo, tuliomba tangu tupo makazini, lakini tulionekana mahaini, ndio maana tukajitosa maporini….’akasema yule mtu.
‘Haya sasa niambie umekuja kufanya nini, …na…nashukuru…’akataka kuongea zaidi, lakini yule mtu alitoka haraka pale alipokuwa, na kumpita Rose kama mshale, ilikuwa muda wa sekunde chache, alikuwa keshatoka nje na kuyeyuka, na Rose alibakia ameduwaa….
Rose alitulia kufikiria ni kwanini huyo mtu kaoandoka haraka hivyo, lakini hakuweza kupata jibu la haraka alichofanya ni kutoa chupa yake ya manukato na kupulizia humo ndani kwa haraka, ili angalau ile harufu ya majasho ya huyo mpiganaji wa msituni iondoke, na baadaye kwa haraka haraka akaanza kujiandaa kuondoka, huku akiwaza yale maneno, …
‘Usimwamini sana bosi wako…’akayarudia maneno hayo kwa sauti …halafu kashika shavu huku akiwaza, na kusema kwa sauti; `haijalishi kumwamini au kutokumwamini,…mimi sihitaji kazi kwake tena, …nitatafuta sehemu nyingine, lakini kwanza nijue kuhusu Sweetie…Sweetie wangu,….’ na mara akanyamaza kimiya, kwani alisikia kama mtu anagonga mlango,…kabla hajahakikisha hilo, mlango ukagongwa tena na safari hii kwa fujo….ooh, akajua ndiye huyo jamaa karudi tena nini…lakini…ooh
NB Tukutane sehemu ijayo, nawatakia ijumaa njema,
Ni mimi: emu-three
Monday, October 24, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-41
Adamu alabakia ameduwaa bila kusema kitu . akataka kutamaka neno, lakini mdomo ukawa haufunguki, moyo ukawa unamwenda mbio, katika hisia za ajabu, huku macho kayakodoa kuangalia mlangoni. Alijaribu kukumbuka jinsi gani hali kama hii imeanza kumtokea lini, kwani kwa ujasiri wake aliojijengea hasa baada yay ale mafunzo aliyopewa, angeliweza kujizuia na kupambana na hisa zozote ….lakini sio vile akikutana na huyu …..amegundua kuwa hali kama hii imekuwa ikimtokea mara tu anapokutana naye, na hali hii ilimuandama kipindi kile cha ujanani, na alipokumbuka hivyo, akabenua mdomo na kutabasamu, halafu aaksogea mlangoni na kunyosha mkono wa kukaribisha, hakutaka uwe mkono tu, alitamani angemkumbatia…lakini akajua kuwa sio vyema…huenda ….
‘Vipi docta mbona unakuwa kama mtu aliyeona mzuka fulani,…vipi kwani hukutarajia kuniona lmimi tena, kwanini uwe hivyo, kwanini umeduwaa kiasi hicho…’ akauliza huyo mgeni aliyesimama mlangoni.
‘Sijui nikuambieje,…’akasema huku akitoa tabasamu lake lote. `Hali kama hii ilikuwa inanipata kipindi kile cha ujanani, wakati damu inachemka, kipindi ambacho nilikuwa natafuta ….sasa umri kama huu nateseka kiasi hiki…kwakweli inanipa jakamoyo la aina yake…kwa ujumla moyo wangu umekuwa kama mtu aliyekuwa na kiu mara ghafla maji yakaonekana…lakini maji hayapo mkononi mwangu, natamani niyanywe na kiu ni kali sana, …sijui mtu kama wewe ungelifanyaje…’ akasema Adam huku akiwa bado katabasamu.
‘Mhh, Adamu, kwanini upate shida, mimi kama ningelikuwa wewe, nisingelisumbuka, kwani maji siku hizo yapo mengi madukani, ya kila aina…ningelienda dukani kutafuta maji mengine , nikanywa kiu ingelikwisha….lakini maswala mengine ni ya kujitakia, kwanini ujitese moyo wako na kitu kisichowezekana, na kwa ujumla Docta sina muda mwingi, nimekuja mara moja na natakiwa ni rudi mjini…kama ulivyoshituka kuniona ndivyo ilivyo kuwa sikutakiwa kuonekana leo hii hapa, nilitakiwa niwe huko mjini mpaka kieleweke, mpaka uchunguzi utakapokamilika,…ila, nimeona sio jambo jema kuhini ahadi, ahadi ni deni… kwahiyo nimeruhusiwa kwa masharti ya muda maalumu, …’ akasema huyo mgeni
‘Najua hilo …na inglikuwa mimi ndio wewe, ningelifanya hilo mapema sana…kwa ujumla nimeshangaa sana kukuona hapa leo, kwani nilivyosikia ni kuwa wamekushuku kuwa wewe ulihusika, au unajua chochote na kifo cha yule mtu aliyeuwawa kwenye hiyo hoteli uliyokuwa umepanga, …ni swala la muda tu, lakini hata hivyo swala la mauaji sio la kuchezea, unaweza ukaozea jela ndio maana kwa kukujali nikakutumia wakili…’akasema Adam.
‘Kwa kunijali au kwa kujali maslahi yenu, mimi nisingependa kuwaingilia mipango yenu, lakini mnanisikitisha sana pale mnapowaumiza watu wasio husika kabisa…na hata kuwaua watu wasio na hatia, …nini mnachokitaka katika dunia hii, kuwa mtaishi milele…hakuna atakaye ishi milele, …mwisho wa kuuwa wengine ni kuishia kuuliwa tu…nini kinachotafutwa hapa…sielewi kabisa, ..eti utajiri, ni nani aliyekufa na utajiri wake, hakuna…hata mkilimbikiza mailioni ya mapesa hata mkiwa matajiri wa kupindukia, lakini ipo siku mtaondoka, ipo siku mtakufa kama hawo mliowaua, tumeona wagonjwa wangapi wanakuja kutibiwa matajiri wana kila kitu wanakuja na mapesa yao na kuomba kuwa tuwasaidie wasife, lakini wapi…muda wao unafika wanaondoka, huku tukiwa tumefanya kila aina ya juhudi, pesa zao, utajiri wao haukusaidia kitu…’ akaongea huku machozi yakimtoka.
‘Adamu , inaniuma sana, sikutarajia mtu kama wewe, …sikutarajia kabisa,….kuwa unajihusisha nan a mambo kama haya…inaniuma sana…kwahiyo..nimekuja kuwapa mapesa yenu, ili msiendelee kuniandama, msisendelee kuziandama roho za watu wasio na hatia…manachotaka ni nini , ni pesa, haya pesa zeni hizi hapa…..’akasema yule mgeni akiwa kavaa mawani meusi kuficha macho yaliyokuwa yalkitoa machozi, na Adamu aliyaona yale machozi, yakitiririka hadi chini kidevuni, na yeye hisia za huruma zikamteka, kitu ambacho humjia kwa muda mfupi, lakini akiwa hayupo kwenye uwanja wa mapambano, yeye kwake alijua kuwa yupo uwanja wa mapambano, anapambana na wale wasiotaka wengine wapate maisha bora….akamsogelea mgeni wake na kumshika mkono na kumsindikiza hadi kwenye kiti na yeye hapo hapo akaona hisia za machozi zikimlenga lenga.
Hisia hizo zilipomteka moyo wake, akageuka na kuangalia dirishani na taswira za kimaisha zikapitiliza dirishani na kwenda mbali kabisa…, hali ile ilimtia uchungu sana, na hata yeye alishajiuliza mara nyingi, ni kwanini akajishirikisha na hawa watu, nini lichokuw akikitaka, ni pesa, ni utajiri…hapana ni zaidi ya hayo, ni uchungu wa kile alichokiona, ….uchungu wa jinsi gani watu waliopewa madaraka, wanavyofanya, ….wanavyokula mali ya wanyonge, bila huruma, …nia na lengo lake ni kuhakikisha amewaondoa hawo na ikibidi haki itawale na mali ya wanyonge ibakie mikononi mwao,…aliona kuwa hakuna jinsi nyingine, ….ila hiyo ianayokwenda nayo, ….ilikuwa kama mchezo tu, na hatimaye akawa ndani kabisa ya bahari ambapo alipotoka ni mbali na anapokwenda ni mbali, haoni wapi aelekee, ila alichojali ni upepo unavyomtuma ….sasa je afanyaje, akajitosa na kuanza kuogelea.
*********
Alipoanza ajira alikuwa na ndoto ya kuwa dakitari mkubwa sana, kutokana na akili yake ilivyokuwa kubwa shuleni, tangu alipoanza darasa la kwanza hadi chuo kikuu alikuwa anafanya vizuri katika mitihani yake,na hata walimu wake walimuweka katika kundi la wanafunzi wenye vipaji maalumu. Akafaulu hadi chuo kikuu, katika nyanja ya udakitari, na hata alipomaliza chuo kikuu alijiona hajafikia pale alipopataka, akaomba kwenda kusoma nje, kwani alikuwa na sifa zote…., lakini kwa upendeleo uliokuwepo hakuweza kwenda kusoma nje, nafasi yake ilichukuliwa na watoto wa wakubwa ambao alikuwa akiwazidi sana kimasomo, …alafanya kila juhudi lakini hakufanikiwa hana pesa, hana refa …hana…hapo akaanza kuvunjika moyo, lakini bado ndoto yake yakuwa mmoja wa madakitari bingwa haikumuondoka kichwani.
Alikuja kuajiriwa kwenye hospitali za serikali na kuanza kupambana na maisha, alitumia muda mwingi kujisomesha zaidi ili afikie hatua ya juu, na kweli baada ya muda akarudi chuoni kusoma zaidi na hatimaye akafikia hatua ya udakitari bingwa, lakini kilichomkwaza zaidi ni kuwa kipato alichokuwa akikipata kilikuwa hakilingani kabisa na ujuzi wake, na hasa ukilinganisha na wenzake waliokuwa wamekwenda kusoma nje….akaona atafute mbinu nyingine,….
Katika kuhangaika huku na kule akakutana na wenzake aliosoma nao ambao walibahatika kwenda nje walimshauri atafute hospitali za watu binafsi na kufanya kazi kwa muda wa ziada, wao wapo tayari kumuunganishia kwa hilo, hasa huko wanapofanyia. Basi akawa anafanya hivyo, …anahangaika mchna kutwa katika hospitali za serikali, na ikifika muda wa kuondoka, anakimbilia hospitali za watu binafsi kufanya masaa machache yaliyobakia , hata ikibidi hadi usiku wa manane, na hali hii ilimchosha sana, kwani alikuwa hana muda wa kupumzika.
Siku moja, akakutana na rafiki yake wa siku nyingi , akamshauri kuwa kuna hospitali inafunguliwa na mmoja wa wahusika wakubwa wa hiyo hospitali ni baba yake , na yeye ndiye alitarajiwa kuwa mkuu wa hiyo hospitali, lakini yeye hapendi kabisa kufanya kazi hapa nchini, ndoto yake ilikuwa kwenda kufanya kazi nje ya nchi na keshafanikiwa, …alisema kuwa wazazi wake wamekua juu kwa hasira, kwani wao juhudi zao zilikuwa kwake, walishamuandaa kuchukua nfasi hiyo, sasa amewasaliti…aliwaambia kuwa atawatafutia mtu anayefaa, kwa kazi hiyo, ndio maana amekua kukutna naye, kama yupo tayari, masharti ni kuwa aachana na kazi serikalini ….na kukubalina na msharti machache, na pia kuna mafunzo machache anatakiwa kuyapitia, kama yupo tayari yeye atamuunganishia…!
Adamu alishawaza sana kuachana na kazi za hospitali za serikalini, lakini hakujua aende wapi, kwani kila alipojaribu walikuwa wakimtaka,lakini sio kwa wadhifa kama huu aliopewa na huyu rafiki yake, kuwa anakwenda kuwa dakiari mkuu wa hospitali, …na hospitali yenyewe sio ndogo …Adamu akakubali kwa furaha, na kweli alipokutanishwa na baba wa huyo jamaa, alikubalika, lakini kwanza akubaliane na msharti yao, na mojawapo ni kupelekwa semina maalumu, na pili kupitia mafunzo ya uaskari…hapo akagwaya, lakini akasema potelea mbali, …lazima apambane na maisha.
Kwanza kabisa aliingizwa kwenye semina, semina hiyo ni kumjenga mtu kiakili, alionyeshwa mambo yanayotendeka nchini, akakutana na mambo ambayo hakuamini kuwa yapo nchini kwao…akapikwa ipasavyo….na akaona kweli ipo haja ya kupambana, ipo haja ya kutumia utaalamu wake kuhakikisha naye anakuwa katika hali itakayorejesha yale aliyoyaona kwenye himaya ya wananchi…lakini haikuwa rahisi hivyo…
Siku kabla hajakabidhiwa majukumu akakutana na huyo baba aliyemuunganishia na huyu baba akamkalisha chini,na kumuusia kama mwanae alimwambia;
‘Mwanangu dunia hii haina haki,…utashangaa kwanini haya yapo, ni kwasababu hali ilivyo, kila mtu anavutia kwake, ndio tuseme sera ya ubepari ndivyo ilivyo, kuwa ili ufanikiwe ni lazima utafute njia ya kupata zaidi na ili upate zaidi lazima utumie juhudi za ziada, na kwa nchi yetu hii juhudi za ziada zimebanwa, kinachotakiwa ni kupambana, ….na huwezi kupambana ukiwa umelegea, unatakiwa kujiandaa kwa kila hali, ujijenge kikakamavu….’akatulia yule mzee akimwangalia huyo kijana mbele yake, halafua akaendelea kusema.
‘Mimi ujana wangu niliupotezea katika kulitumikia taifa, nilifanya kazi kama punda, lakini mwisho wa siku unarejea nyumbani, ukiwa na mdeni, huna mbele wala nyuma, ukigeuka unawaona wenzako wanajenga mahekalu…unajiuliza wanapata wapi hizo pesa…mpaka nafikia makamo, sijaweza hata kununua baiskeli, nikasema hapana lazima kuna kitu hakipo sawa, nikafanya utafiti, ndip nikagundua kuwa kuna hujuma, sio kweli nchi yetu kuwa ni masikini kiasi hicho…kama ni masikini mbona hawo wanajenga mahekalu…’akasimama yule mzee na kumsogelea yule kijana mbele yake na kumshika begani.
‘Mwanzoni niliwaza kuwa ile hali ni ya muda mfupo, labda baadaye hali itatengamaa, hasa kipindi kile walipofukuzwa wageni wote hapa nchini na yule jamaa aliyeitwa nduli…lakini badala yake, wajanja wakamiliki zile mali na kuzifanya zao, …mjanja kuwahi…na waliowahi wakaweza kutenegneza maisha yao wao na familia zao, wengine tukabakia kumezea mate, kuwa labda ipo siku hali itakuwa nzuri, …labda, labda, umri unakwisha, …aah, nikasema haiwezekani, tukakutana na wenzangu tuakasema hapana lazima lifanyioke jambao, kwasababu watu wenye nafasi wamezuia kila kitu, kwanini…na kila kinachopatikana kinaishia mikononi mwao kwanini, aaah, tukasema hapana, saa lazima na sisi tujipenyeze tuwe nawo sambamba, tule sahani moja…vinginevyo tutabakia masikini, …’ Yule mzee akamwangali akwa muda yule kijana, kuhakikisha kuwa kweli kaelewa anachomwambia.
‘Kwahiyo sasa ili ijipenyeze kwao, ni lazima uwe nao, uende nao sambamba, lakini hata hivyo kuwa nao sambamba sio kazi rahisi, wengi wao hawapendi kwasababu wameshajenga hulka ya uchoyo wanataka wapate wao wenyewe, ndio maana unaoana kuna makundi makundi, ambayo mengine yameamua kujitenga na hata kuingia msituni, sisi hatutaki kuingia msituni, tuna maujuzi yetu, tutatumia ujuzi wetu kama sehemu ya mapambano, ili tuweze kubanana hapa hapa, sio kwa kwenda msituni, haow wa msituni, wanatumia ujuzi wao wa uaskari, sisi tutatumia uuzi wetu wa kitaaluma, …siri kubwa ni kuwa huku na kule…unauma huku unapulizia, …ndio maana ya ile semina. ..’akasema yule mzee na kuinuka kuondoka akujua kuwa kijana kaiva, na kweli toka siku ile Adamu akaanza kubadilika.
Baadaye akakabidhiwa hospitali hiyo rasmi, akiwa keshakuwa jasirii kama askari mwenye kila kitu, kazi ni kuingia uwanja ni, na kusimama mstari wa mbele wa mapambano…yeye alikuwa na kipaji, yeye alikuwa na taaluma adimu, alikuwa keshamsoma binadamu ndani na nje, na alishajua jinsi gani ya kumbadili binadamu toka alivyo kisura, kihisia na ….na kumtengeneza amtakavyo, na mwisho wa siku anamtumia kama roboti….
Taaluma ikafanya kazi yake na jambo kubwa alilojifunza na usiri katika kazi yao…na akweli aliweza kudumu katika kazi hiyo ya udakitari bila mtu yoyote kumhisi kuwa ana mambo mengine ya ziada, na utaalamu huu ilikuwa siri yake na wanachama walioaminika…akiwa kwenye mafunzo ya uaskari, alionekana kujua vyema matumizi ya silaha na hata kuwa mlenga shabaha mzuri, na kwa ile hamasa aliyokuwa nayo Adamu katika taaluma hiyo, akajikuta anapenda sana kuingia kwenye mapambano, na hata akawa miongoni mwa viongozi wa kificho katika kupambana kisilaha pale inapobidi. Kawaida huonekana dakitari, lakini akiwa uwanja wa mapambano huwezi kuamini kuwa ndiyo yule yule aliyekuwa akaokoa maisha ya watu kwa kutumia mikasi na madawa.
Kwa aijili hiyo wakati mwingine anaitwa mjini kwenda kuingia kwenye mapambano yasiyo rasmi, au kutekeleza jukumo liloshindikana na anapokuwa huko, hafiki kwa sura yke ya kawaida…na kwa mtindo huo hakuna aliyeweza kumjua, kwani alikuwa akijibdilisha sura kama kinyonga….
Siku zilivyoZIDI kwenda ndivyo alivyozidi kuvutiwa na kuhamsaka na kazi hiyo ya ziada, lakini hata hivyo alijikuta akiwa katika maisha ya hatarishi, na hata alipo-oa, hakuweza kuifaidi ndoa yake ipasavyo kwani wakati mwingine alihitajika usiku, na hapo hakuwa na jinsi , ila kudanganya kuwa anakwenda hospitalini kuna dharura, kumbe anakwenda uwanja wa mapambano ,au kwenda kutekeleza ukumu fulani ambalo lilihitaji utaalamu wake. Na baya zaidi akampata mke ambaye hawakuelewana kabisa, na kuishia katika kugombana mara kwa mara,…
Hata alipooa, kwasababu za usalama hakutakiwa kumwelezea mkewe chochote kuhusiana na kazi yake hiyo ya ziada, au kumuonyesja dalili zozote, hata itokee nini…, kwani moja ya masharti ya kazi zao ni kutokumwambia yoyote asiyekuwa mwanachama, hata kama ni familia yako, …kwahiyo alihakikisha mkewe hajui lolote,…baadaye mkewe alianza kumchunguza chunguza, na hili akaambiwa na wanachama kuwa mkewe ni hatari, keshagundua kitu, na amewahi kutumiwa na maadui atafute baadhi ya siri, kwahiyo awe macho naye….
Kabla hajaambiwa hivyo yeye mwenyewe alishachoka na tabia za mkewe, kwani alishagundua kuwa anajihusisha na wanaume kisiri…hili Adamu aliligundua mapema, lakini alitakiwa asichukue hatua yoyote haraka. Baadaye wanachama wakamshauri atafute mbinu aachane na mkewe haraka iwezekanavyo, kwani kuna uchunguzi kuwa anamahusiano na mmoja wa maadui zao, na pale alipomfumania na mshenga wake, ikawa ni nafasi mojawapo ya kumuacha, lakini aikaonekana kwanza wamtumie kama chambo katika kufaniklisha mambo yao…chambo hiyo ilipofanikiwa, huyo mke akaachwa, bila kujua nini kilichokuwa kinaendeela ndani ya nyumba hiyo.
Alimpomuajiri Rose awe msaidizi wake wengi hawakilipendelea hilo, walitaka mtu wanayemjua, waliataka mtu atakayepitia mafunzo yao, na walimuona Rose hafai, bila kutoa sababu maalumu. Adamu aling’ang’ania kuwa yeye alimuhitaji huyo kwasababu kaiva kitaaluma hata akiondoka kuwajibika sehemu nyingine huyo ataweza kufanya kazi yake bila wasiwasi. Wfadhili wale walikubali shingo upande na kutoa agiza kuwa wao watakuwa nyuma yao wakiangalia utendaji wake…
Siku zikapita na Adamu alikuwa anaishi bila mke, wakamshauri atafute mke, …na kipindi hicho Adamu alikuwa anamuwaza Rose awe ndio mke wake, akampendekeza mbele ya wanachama kuwa kama atampata Rose kuwa mkewe atafurahi sana, hapo akakutana na pingamizi kubwa sana, kuwa anataka kugeuza huo mradi sehemu ya mapenzi, ….
‘Kijana unajua tupo kwenye uwanja wa vita,…tumekuona siku nyingi kuwa huyo ulimuajiri kwasababu ya mapenzi, sio kama tulivyotka sisi…sasa umeanza kulidhihirisha hili mapema, tunakuasa tena, …hakikisha unakuwa katika njia tuliyokuagiza, vinginevyo, tutakuwa hatuna jinsi, …na unajua kiapo chetu, ni kiapo cha uaskari, kama unarudi nyuma, …unajua nini kitakachofanyika…sisi hatukukatilii huyo Rose awe mkeo, lakini kwa jinsi ulivyo kwake, tuna wasiwasi unaweza ukatoa siri kwake, …’akaambiwa.
‘Mimi naomba hilo mniachie, nitahakikisha anakuwa katika msitari wangu, ipo siku mtaniunga mkono…’akasema Adam, na kweli wakamuachia ahangaike na Rose wake, wakijua kabisa hataweza kufanikiwa kwa hilo, muda ukapita bila kukubaliwa na Rose awe mkewe, na hata wanachma walikuja kumwambia kuwa Ros hamfai, kwasababu kubwa kuwa akiwa karibu naye ataweza kushindwa baadhi ya majukumu, wanahitaji mtu baki ambaye atakuwa mbali na yeye… hilo hawakumwambia moja kwa moja Adamu, ilikuwa siri ya kundi, na walijua moja kwa moa kuwa Rose hataweza kumkubalia Adam , awe mkewe kwa jinsi walivyomuona, kwahiyo hawakufanya juhudi yoyote ya kumsaidia kwani wangelitaka wangafanya hivyo na Rose asingelikuwa na ubishi, anglikubali tu…
*************
Rose alikuwa alifungua mkoba wake akatoa bulungutu la pesa, na kumkabidhi Docta Adam, Docta Adam akawa kasimama anaziangalia zile pesa, na baadaye akamwangalia Rose usoni, akatabasamu na kugeuka bila kuzishika zile pesa aliangalia nje kwa muda halafu akaelekea kwenye kiti chake na kutoa kitabu cha stakabadhi na kabla hajakifungua mlango ukagongwa, akainuka haraka na kueleeka pale mlangoni, na waliokuwa wamesimama ni yule mkuu wa uadhamini na docta moya aliyeletwa kushika nafasi ya Rose.
‘Ohh, tena mumerudi wakati muafaka, karibu waheshimiwa…’akasema Adam. Na wao awakingia na kujikuta wakishngaa walipomuona Rose, na mbele yake zipo pesa.
‘Ohh, Docta umerudi, ..mbona tulisikia kuwa umeshikiliwa na maskari huko mjini, hebu tuambie ilikuwaje maana tumekusubiri kwenye kikao mara zaidi ya nne huonekani…’akauliza mwenyekiti wa wadhamini.
‘Ina maana uumbe wangu hamkuupata kwa Docta Adam?’ akauliza Rose.
‘Ujumbe haukutakiwa kupitia kwa docta Adam, ina maana hukusoma ile barua tuliyokuandikia maana ilielezea kila kitu, sisi tuliona kabisa umedharau, maana wewe ni msomi, kila kitu kimejieezea kisheria, …hii ilidhihirisha kabisa kuwa nafasi hiyo uliyopewa ilikuwa haikufai, …lakini haina shida tumeshalitatua hilo, nafikiri umeshapata taarifa kwa huyo uliyetka taarifa zako zipitie kwake, na…umeshampa barua yake?’akauliza huyu mkuu wa wadhamini.
‘Hpana ndio mefika na alikuwa akinikabidhi pesa alizokuwa akidaiwa..’akasema Adamu.
‘Haiwezekani, umepata wapi pesa hizo, oooh, safi sana, kama umeweza kuzipata hizo pesa, tutaangalia jinsi gani ya kukuweka katika nafasi nyingine, lakini sio hiyo uliyokuwa nayo mwanzoni, hilo tutaliongea abadaye, kwa sasa tumekuja kwa mambo mengine, sijui mumemalizana, …maana tunahitaji nafasi ya kuongea , na Rose hastahili kuwemo katika maongezi yetu…’akasema yule mkuu wa wadhamini.
‘Mimi naondoka, sina muda mwingi, naomba stakabadhi yangu ya malipo, na ninachotaka kusema nikuwatakia mafanikio mema, maana sidhani kuwa nitarejea hapa kama mfanyakazi wenu, natumai nikija tena nitakuja kwa ajili ya makabidhiano, …nawashukuru sana kwa yote …na kama niliwakosea nawaomba mnisamehe kwasaabbu nilifnay hivyo kwa nia njema kabisa, na huwezi kumuhadithia mtu akakuelewa, …unakutana na mtu kazidiwa hana pesa, na yupo mkononi mwako, utamuacha afe kwasabau hajalipia.., hapo mimi sielewi, ndio maana naona labda nimeingia uwanja usionifaa…nawashukuru sana….’akasema Rose na kuchukua stakabadhi yake na kuondoka,..
‘Lakini Rose nilikuwa na mazunguzmo na wewe, usiondoke kwana naomba unisibiri nje…’akasema Adam.
‘Mazunguzmo na wewe yamekatika ….sina mazunguzmo na wewe natumai umelielewa hili…naomba, na akuomba uwaambie watu wako kuwa, sitaku kufuatwa fuatwa , nimeshamalizana na nyinyi, …kama nyie ni miungu wa hapa duniani, haya endeleeni kinifuatafuta, lakini ipo siku,…’akasema na kundoka, huku mwenyekiti wa kamati ya wadhamini akicheka na kusema;
‘Nilijua kuwa huyu sio mke wa kuoa, Adamu, unatakiwa uwe jasiri, usikubali mapenzi yakulangai, mapenzi ni sumu katika uwanja wa mapambano, hili ulishaambiwa mara kadhaa, muda wa mapenzi ni wakati upon a mkeo nyumbani, lakini kama mpo uwanaj wa mapambano, huruma, haitakiwi, je itakwuaje kama umepewa amri ya kutekeleza jukumu na mkeo yupo karibu yako anakuambia usifanye….?’ Akauiliza yule mwenyekiti.
‘Jamani hilo swala la mimi na Rose nilishasema mniachie mwenyewe, sawa naona tuongee, maana, mumeshanifukuzia ndege wangu, sijui nitafanyaje ili nimpate…sijui …’akasema Adam.
‘Utampata ndege mzuri kuliko huyo, hawo ndege wapo wengi, na kila siku wanazaliwa wazuri zaidi, usikubali kutekwa moyo wako na kufanywa dhaifi kwa kitu mapenzi, huo ni udhaifu usiofaa, ukishindwa tuambie tutakutafutia, wewe tumekulea mwenyewe, hatushindwi kukutafutia mke , tena mke ambay hutaamini, …..ngoja tumalizane na hili, suijali..’akasema yule mkuu wa udhamini, na wakaingia kwenye majadiliano na mabo yao ya kiakzi hata walipomaliza ilikuwa imeshafika jioni.
Ilikuwa wakati Adamu anafunga mlango wa ofisi yake na muda huo pilikapilika zilishapungua,…sehemu iliyoonekana watu ni sehemu ya kulaza wagonjwa. Adamu kichwa kizima kilikuwa kimejaa hasira, akawa anafunga mlango wake, huku akimuwaza kiongozi wa wadhamini kwa kauli zake chafu, ambazo zimemuuashiria kuwa huenda hathaminiki tena na huyo aliyeletwa kushika nafasi ya Rose anandaliwa rasmi kuchukua nafasi yake….eti kafanya makosa mengi ambayo yanaweza kuwafichua na huenda wakaingia kwenye migogoro na serikali, kwahiyo lazima wajiandae, …ili kama atashikwa na kufungwa kuwa na mtu atakayeshika nafasi yake, kwanini ashikwe na kufungwa, kwanini wahisi hivyo……akajipa moyo kuwa hata kama watamundoa kwenye hiyo nafasi yake , bado anahisa, bado anauwezo wa kufungua hospitali yake mwenyewe…labda huko kufungwa, lakini kwa kosa gani….
Na mara wazo jingine likamjia kichwani, akawa sasa anamuwaza Rose, ina maana yeye na Rose ndio basi, hatakubali kwa hilo, akawaza jinsi gani atakuatana naye aili amthibitishie kuwa kweli anampenda na kwa kumuonyesha hilo atamwambia kuwa anaacha kazi na kufungua hospitali yao watakayoiendesha wao wawili, lakini je atakubali, na je bado yupo au keshaondoka mjini, … huenda atakuwa hajaondoka yupo nyumbani kwake, …akazmiria kwenda kwake kukutana na yeye, akafanya haraka haraka kuondoka, na kabla hajafunga mlango vizuri akasikia hatua za viatu zikimkaribia….
‘Ni nani huyu anakua kunisumbua muda kama huu..’akajisema moyoni, huku akihisi nywele zikimsisimuka, kwanza alizania kuwa huenda ni mlinzi,…kama ni mlinzi anakua kufanya nini…akasikilizia huku anafunga mlango, hakuwa na haja ya kugeuka kuangalia ni nani, lakini kitu kilichomshanagza ni hile hali ya mwili kusisimuka kama vile kuna hatari inamkaribia, …akahisi hali isiyo ya kawaida, …huyo sio mlinzi ni nani, atakuwa anakuja nyuma yake, akageuka haraka kuangalia,….na karibu azimie kwa mshituko alioupata…
NB, Unaweza kukisia ni nani huyo aliyemjia muda kama huo na kwanini shitake kiasi cha kutaka kuzimia
Ni mimi: emu-three
Friday, October 21, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-40
Adamu alibakia kwa muda ameshikilia simu mkononi, utafikiri bado anasubiri kuongea na huyo mtu aliyekwisha kuongea naye karibuni, lakini walikuwa wameshamaliza kuongea, ….kilichomfanya aduwae kwa muda ni hzio taarifa alizozipokea kwa huyo aliyempigia simu, …ilikuwa kama mtu kamtonesha kidonda kilichokuwa kimepona…Hakuamini kabisa kuwa Rose kawa na mwanaume mwingine, …haiwezekani,
…ina maana juhudi zote zile za kumuondoa yule mtu aliyekuwa akimzuzua ilikuwa kazi bure,…sasa kapata mtu mwingine, …lakini ni nani,huyo mwanaume . Akakumbuka jisni alivyokuwa akiwasilina na huyo mtu wake;
‘Kwanini mshindwe kumuona huyo mwanaume, ina hatoki nje, ….hata kama hatoki nje ina maana hamuwezi kuingia humo ndani ya hoteli mkamjua ….haiwezekani? ’akauliza Adam kwa hasira.
‘Tunaweza kuingia, lakini hatuna ruhusa ya kukagua kila chumba, ….’akasema jamaa yake huyo.
‘Hamuweze kumshawishi huyo mkuu wa ulinzi kwa namna yoyote ile hata kama ni kwa kutumia nguvu…mumeshindwa hilo?’ akauliza tena Adam kwa hasira
‘Bosi natumai unamfahamu vyema mkuu wa ulinzi wa hiyo hoteli,…sio mtu wa mchezo, ndio tunaweza tukamvamia au kitu kama hicho, lakini baada ya hapo labda awe maiti….. unakumbuka alivyokuwa kazini, polisi kabla hajaachia ngazi, huyo jamaa ni komandoo, unakumbuka jinsi gani tulivyo hangaika naye, juhudi kubwa zilishafanyika ili hatimaye awe kwenye kundi letu, zikashindikana,….’ Akasema huyo mtu wake.
‘Hazikushindikana, ila wakubwa waliona haina haja naye tena, baada ya kuachia ngazi,….au ni yupi huyo unayemuongelea isije ikawa namuongelea mtu baki, ni nani huyo au simkumbuki vyema, lakini hata hivyo , kama mliweza kupenya na kuingia ndani wakati wa kampeni yetu, na kama mliweza kufanya hilo tukio la kummaliza yule mnafiki mtashindwaje kumdhibiti huyo jamaa, au kazi imeanza kuwashinda….kama mumeshindwa nimwambie mkuu…maana hata mimi nachoka sasa kufuatilia kila kitu, hiyo ilikuwa sio kazi yangu, ila kwasababau ya Rose, umesema huyo jamaa ni nani..?’akasema Adam
‘Unamfahamu sana bosi, ni huyo huyo askari aliyestaafu polisi, wakati akiwa nahitajika sana na Serikali, yule aliyekuwa anatuogopesha sana, hashikiki…basi ndiye mkuu wa ulinzi wa hiyo hoteli..’akasema huyo mtu.
‘Una maana Ojong, mnoko yule…ooh, kumbe bado tunaye, kazi ndogo hiyo, nitaongea na mkuu atajua jinsi gani ya kumuweka sawa, sio tatizo hilo, nitawapa ishara ya kuingia humo ndai muda ukiwa muafaka, kama ni huyo msifanya papara, kweli mtaumbuka, ikishindikana nitakuja mwenyewe, najua nikikutana na Rose nitakuwa nimemgundu huyo mtu ni nani. …’akasema Adam na kwa muda huo aliskia mlio wa gari likisimama nje, akajua kuna wageni wamekuja kwake, akawa kaishikilia simu huku akiwaza, na huku askisubiri kukutana na hawo wageni asiokuwa na miadi nao..
Mara mlango ukagongwa na Adam akaishikilia ile simu kwa nguvu mkononi kama vile anamalizi hasira zake, hakutaka kukutana na mtu kwa wakati kama huo, lakini hakuwa na jinsi…mara mlango ukagongwa tena, ….akaiweka ile simu juu ya meza na kuusogela ule mlango, huku akiwaza ni wageni gani hawo, maana hata gari lilikuwa limesimama sehemu ambayo hakuweza kuliona vyema, hakugusa mlango akasogea pembeni na kusema `ingia..’ kwa sauti ambayo aliihis sio yake .
Mlango ulipofunguliwa moyo wa Adam uliyeyuka toka kwenye hasira na kurudi kwenye hali ya kunyenyekea, kumbe wageni hawo ni watu wa heshima kwake, ndio wanaomuweka mjini, walikuwa ni watu watatu, wawili ni viongozi wa udhamini wa hospitali, na mmoja hamjui vyema, …
‘Mbona mumeniingilia bila taarifa…kuna tatizo waheshimwa…?’ akauliza Adam huku akiinama kwa unyenyekevu, hutaamini ni yule mtu aliyekuwa na hasira ya kumvunja mtu shingo.
‘Hakuna tatizo Docta ila ni moja ya utendaji wetu, …na samhani kwa kukujia bila taarifa, lakini kama unavyokumbuka kikao cha mwisho tulitoa hitimisho la uchunguzi wetu na tukafikia muafaka kuwa Rose asipojitokeza katika muda tuliaainisha, basi inabidi hatua za haraka kuchukuliwa...,' akasema yule kiongozi wa wafadhili huku akikaa kwenye kiti , na wenzake wakafanya hivyo hivyo.
‘Ndio lakini nimekwisha waambia kuwa Rose ana matatizo huko mjini, …’akaongea Adamu kwa shauku, akiwa hajui wakuu hawa wamekuja ni jipi jipya, na alipoona wapo kimiya akaendelea kusema
`Nawahakikishia kuwa sio kusudio lake, na nina wahakikishia kuwa keshapata hizo fesa alizokuwa anadaiwa…’ Akaongea akionyesha uso wa furaha kuwa anaongea jambo ambalo litawasuuza mioyo ya hawa waheshimiwa, na alipoona hawajasema kitu tena akaendelea kuongea kwa kusema ;
`Je nini tulikuwa tunataka… ni pesa au sio, na sio lazima tumuone yeye mwenyewe,…lakini hata hivyo kama tunamuhitaji yeye mwenye kujieleza, tusubiri afike ili ajitetee, tusimuhukumu mtu akiwa hayupo tutakuwa tunakiuka haki za binadamu, na pili na ndilo la muhimu ni kuwa tunahitaji pesa, na huyu mtu anazo, kwanini tusumsubiri akalipa kwanza, kama ni mengine yakafuata baadaye, kwasababau tukichukua hatua nyingine, tutampa mwanya wa kukacha kulipa kabisa…’akasema Adam.
‘Tatizo lako Adamu, wewe sasa umegeuka kuwa mwanasiasa, na ujue kazi yetu haihitaji siasa, tunahitaji utekelezaji wa haraka, na kwa muda muafaka, …tupo vitani , tukisema mbele songa, hatuhitaji mjadala, na ukumbuke kazi iliyopo mbele yetu inahitaji muda mfupi sana, ujue nchi yetu inakwenda kwenye mabadiliko, na hujui nini kitatokea huko baadaye…ni bora tukafanya juhudi za makusudi kulinda vitega uchumi vyetu….na kwa hilo basi hatuna muda wa siasa, ngoja nikuambie kile kilichotuleta hapa….’akasema yule mwenyekiti.
‘Sawa nawasikiliza waheshimiwa….’akasema Adam akiwa anawakagua kila mmoja kwa wakati wake.
‘Ndio hivyo Adam,…’akasema yule mdhamini mwingine , halafu akamgeukia kiongozi wa udhamini, kama vile anamuonyesha ishara ya kuendelea kuongea. Na Kiongozi wa wadhamini, akamgeukia yule jamaa mwingine ambaye alikuwa mgeni kabisa kwa Adam, na kumshika begani, huku akisema ‘ Huyu hapa ndiye atachukua nafasi ya Rose, atakuwa msaidizi wako,…’akamgeukia Adam na kumkazia macho, huku akiendelea kuongea kama mtu anayetoa amri.
‘Huyu ana uzoefu wa kazi hii, Rose haoni ndani, na pili tunamjua vyema hana shida nasi, mtashirikiana naye na utaona juhudi zake,…anaitwa Docta Hama,’ akamgeukia Adam na kumkazia macho huku akisema ‘Docta Hama, huyo mbele yako anaitwa Docta Adam, ndiye mkuu wa hii hospitali toka ilipoanzishwa, yeye tunamuita muwanzilishi, …kwahiyo tunakuomba ushirikiane naye kwa hali na mali na mengine utaambiwa baadaye, na yeye atakuonyesha majukumu yako na yeye , na sisi tutawasikiliza nini mumepanga, ….hatuna muda wa kupoteza tena, huyo Rose akija kama ni lazima kuwepo humo hospitlini atakuwa kama docta wa kawadia tu….sawa…?’akasema yule kiongozi wa wazamini na kusimama kutoka kuondoka.
Adamu alitaka kulalamika kuwa taratibu zimekiukwa kwani, alitakiwa kushiriki katika mchakato wa kutafuta msaidizi wake, lakini leo imekuwa kinyume chake. Hii ilionyesha dalili kuwa walishamchoka na huenda hawamuamini tena, …alikuwa keshalitafakari hilo siku nyingi na matendo ya wadhamini hawa yalionyesha dhahiri kuwa hawapo naye sana kama ilivyokuwa awali, na sasa wanamtumia tu kwa manufaa yao kwa vile ni mzoefu na anajua siri na membo mengi ya hiyo hospitlini na miradi mingine.
‘Karibu Docta, nshukuru kukufahamu na tunakukaribisha kwa moyo mmoja, licha ya kutahiniwa na kuingizwa bila mimi kufahamu, lakini wewe isikutie shaka, nitashirikiana na wewe kwa moyo mmoja kwani lengo lengo letu kubwa ni kuhakikisha hii hospitli inakuwa na kuleta maendeleo, …yote hayo najua unayafahamu, …sijui ndio mumeshanikabidhi au ..leo mnanitambulisha tu…’akauliza Docta Adam, akishikana na huyo mgeni mkono.
‘Tumekuja kukutambulisha tu, najua utalalamika kuwa tumekiuka taratibu , lakini kipo kippengele cha kuturuhusu kufanya hivyo pale tunapoona kuwa inabidi…..na ilivyo kama tungelikuachia usingechukua hatua hii mapema, ndio maana tukaamua kuchukua jukumu hili, ila tunakuhakikishai kuwa tupo pamoja nawe, juhudi zako tunaziunga mkono…usiwe na wasiwasi Docta Adam…’akasema yule kiongozi wa wadhamini huku anamshika Docta Adam Mkono na wengine wakafanya hivyo na kutoka nje…
Adamu alibakia akiwa anawaza mengi, alihisi hatima ya ndoto yake haipo tena, na kila hatua anajikuta akikabiliana na mitihani mingi, sasa kama ni hivyo Rose keshamkosa, kwani hatakuwa karibu naye tena, na muda wa kumfuatilia utakuwa haupo, na keshaletewa msaidizi ambaye kila akimwangalia anahisi ndiye atakayechukua nafasi yake, akajaribu kukumbuka alimuona wapi, lakini akili yake haikuweza kumtambua vyema, ila anahisi alishamuona mahali.
Alikumbuka jinsi alivyoingi kwenye mambo hayo, akiwa katolewa kwenye dimbwi la umasikini, na kwa aili ya umasikini huo akawa anafuta kila anachoambiwa, hakuwa na jinsi kwani hawo waliomsaidia hadi kufika hapo ndio hawo hawo waliokuwa wakimpa amri kuwa afnye hiki au kile…na akwa anamfanya ilimradi maisha yake yawe mazuri ingawaje mengii aliyokuwa akiyafanya hakupendezwa nayo.
‘Sasa muda umefika wa kuamua moja, niishi hivii kama mtumwa au niitoe kabisa na hawa watu, naona maisha yangu na malengo yangu hayatakamilika kama nitakuwa na hawa jamaa, kwanza wananifanya niishi kwa mashaka, na pili hawanithamini tena…’akajikuta akiongea huku akitembea mbela na kurudi nyuma, ….
‘Ndio kwakweli wamenisaidia sana, lakini nini hatima yake, niwe mtumwa wao, hapana, lazima nifanye jambo, lazima nijitoe, lakini nikijitoa ina maana ndio basi tena, na huenda wakaniua, hawa watu hawana huruma katu, nawajua, sasa nifanyeje…akawaza, na kabla hajakaa kwenye kiti mlango ukagongwa, akajua labda na hawo jamaa wamerudi kwahiyo akainuka kwa ustaarabu kwenda kuwafungulia.
Alipofungua mlango akageukia ndani , hakuangalia nje kumwangalia aliyegonga, akijua ndio hawo, na hakuwa na hamu ya kuongea nao zaidi alichotka ni kuwasikiliza halafu waondoke zao ili pate muda wa kutafakari mambo yake…alirusi kukaa huku akiwa hajaangalia ni nani anayeingia, na alipokaa na kutulia na kuinua kichwa kuangalia mlangoni, ……
Alibakia mdomo wazi, …alibakia akiwa kaduwaa, akapikicha macho …na kujua sasa mambo yameanza…moyo ukaenda mbio, na shinikizo la damu likapanda….ndiyo yeye….akasema kimoyomoyo…
NB Nilitakiwa kuendelea kwenye sehemu hii, lakini muda ..na wenye mamlaka wanaingia, tukijaliwa na nawatakia Ijumaa njema, tuzidi kuombeana heri.
Ni mimi: emu-three
Thursday, October 20, 2011
Miaka 50 ya Uhuru
Nakumbuka kuna haditho moja alinisimulia babu, na hiyo ilikuwa inaaminika kuwa hivyo, kuwa unapoona kuku wamesimama mlangoni, hata kama sio mlangoni, lakini maeneoya nyumbani na kuku hawo ni wa kwako, ujue atakuja mgeni, sasa katika hadithii hiyo, babu alisema kuwa hawo kuku wanajadiliana kuhusu huyo mgeni kuwa atakuja na neema gani, lakini mmoja wa huyo kuku anamwambie mwenzake kuwa huenda akija siwe ni neema, bali inaweza ikawa ni kilio…
Katika hali halisi anapokuja mgeni mwenyeji anajaribu kuleta mabadiliko, hasa ya usafi na maandalizi ya kumfanya huyo mgeni ajisikie kuwa anathaminiwa. Lakini inaweza ikawa sio mgeni kama mtu, inaweza ikawa tukio muhimu katika jamii, na ili kuleta tofauti watu wanakuwa na maandalizi rasimi, ikiwemo usafi, matayarisho na hata malazi na vyakula, ilimrtadi kuwe na utofauti fulani,…wanasema waswahili kuwa mgeni njoo mwenyeji apone, au sio.
Utotoni mgeni akija tulikuwa tunafurahia kuwa kutakuwa na maankuli ya tofauti na hasa kule kwetu lazima pilau ipikwe na kuku kuchinjwa kama sio mbuzi, …basi mnakuwa hamchezi mbali, maana mgeni anakuja wenyeji tutafurahia, hata kama hatuju ugeni huo ni wa namna gani, huenda ukawa ugeni wa kumuadhibu mmoja wetu kwa utukutu wake, lakini vyovyote iwavyo siku hiyo kutakuwa na furaha.
Mwaka 1961, ndipo tulipata uhuru wetu, na maandalizi ya mwaka huu naona ni tofauti kidogo, kwani mashirika mengi hasa ya kiserikali yamekuwa yakijiandaa kwa mapana zaidi, kwa vile tumeona ikitangazwa , na sio ya mashirika ya kiserikali tu , na hata ya watu binafsi wale walio na uzalendo wa ncho hii wamekuwa wakitumia mwanya huo katiika kutangaza biashara zao.
Kwakweli miaka 50 ni mingi sana, kwa nchi kama hii yetu ni jambo la kujivunia, kwani mengi yamepita, ya heri na ya shari na kila mmoja wetu anastahili kujivunia, na hata kupongezana, na kupongezana kwenyewe ni huko kufanyika kwa sherehe ya kumbukumbu ya uhuru, ambayo hufanyika kila mwaka, na mwaka huu maandalizi yameanza mapema kivitendo, na kila mmoja anakuwa anajua nini kinachokuja mbele yetu, na wengi tunachekelea tukisema mgeni aje mwenyeji apone.
Wenye umri kama wangu ambao hawakubahatika kushuhudi hilo tukio muhimu la kupata uhuru, tunasimuliwa au kusoma na hata kuona kwenye runinga, jinsi tukio hilo lilivyokuwa,na siku ya kilele, tarehe 9 December, macho yetu yanageukia uwanja wa taifa, na hapo ndipo nawaza kwa mbali na kuiuliza hivi mbona kunapokua na sherehe kama hizi tunaishia kuangalia tu, …..hakuna jinsi nyingine ya kufanya hasa katika siku-kuu kama ili kila mtu, ajihisi kuwa naye ameshiriki, maana mgeni aje mwenyeji afurahi, sasa sisi tubakia majumbani tukiwa tumefunga mkanda….
Sio mbaya, kunakuwa na mapumziko ya kutokwenda kazi, …lakini je kweli unaisherehekea hiyo siku? Kwa maoni yangu ni kuwa, ingelifaa, wote kwenye makampuni, wawe na namna ya kuwafanya wafanyakazi wao wahusike, wajisikie, kama tunavyofanya sherehe za kumaliza mwaka na x-mas, mofisini, na hata wafanyabisahara wawe na namna yao…hata kwa kupmba bendera, ingelisaidia tu, kuonyesha kuwa ni siku pekee nay a muhimu.
Nimeona mwisho wa mwaka, kuna kuwa na vijizawadi kwa wale mabosi wanaojali wafanyakazi wao lakini siku-kuu muhimu kama hii, mmmh,, tujaribu kufanya hivyo kwasababu siku hii inamgusa kila mtu bila kujali dini yake, imani yake kabila lake …ni siku-kuu ya kila mtu… au ndio sherehe ya kiserikali tu, tuwaangalie uwanjani wanavyofanya gwaride …tukiwa majumbani kwetu na tuombee mungu kuwepo na umeme, maana umeme ndiye mtawala wa kina-mna yake, vinginevyo tutaishia kusoma magezeti ya kesho yake..kuwa ilikuwaje, tuweni na uzalendo.?
Ni mimi: emu-three
Wednesday, October 19, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-39
‘Sikilza Ojong, nimefuatlia sana taarifa zako, na nimegundua kuwa ulikuwa askari mwema na mchapakazi wa hali ya juu, lakini ghafla ukaacha kazi, na uliacha kazi kipindi ambacho serikali ilikuwa inakuhitaji sana…na sababu ulizotoa hazikuniingia akilini. Baadaye niliona mambo yaliyokuja kuchomekwa chomekwa, haya ni dhahiri kuwa yalipachikwa ulipoocha kazi kuwa ulikuwa sio mwaminifu, na mambo mengi yasiyokuwa na ukweli au ushahidi, ni ilikuwa kulichafua jarida lako kwa taarifa zisizona ushahidi, mimi nilipoletwa hapa nilizifanyia kazi nikagundua kuwa zimepandikizwa kwa makusudi, ili usipate mwanya wa kurejeshwa kazini….’akasema Inspekta Hoko huku akiwa kashikilia kadaftari kadogo alikokuwa akiandika kumbukumbu zake.
Inspekta Hoko, alikuja hapo hotelini kwa nia ya kuonana na Rose, ambaye kwa taarifa za polisi alitakiwa kukamatwa kama mshukiwa namba moja wa mauaji yaliyotokea hapo hotelini. Kwa upande wake alilipinga hilo na akaamua kufanya uchunguzi wa kina yeye mwenyewe…. Na aili fanikiwe hilo aliona ni vyema akakutna na Rose wakaongea uso kwa uso bila kuwepo mtu mwingine pembeni, hakutaka aongee naye akiwemo wakili wake, …hili limekuwa moja ya kikwkatika kazi yake ya kupambana na uhalifu unaotokea hapa nchini,…aliwaza kwanini anakutana na vizingiti kama hivyo, lakini ndio sehemu ya kazi, alijipa moyo kuwa kwa vyovyote hiyo hali itakwisha.
Leo alipanga kuja kuonana na Rose, akijua atamkuta yeye mwenyewe, lakini alipofika akaambiwa Rose kasema ataongea na maaskari tu pale wakili wake atakapokuwepo, ….akajisemea moyoni, kama Rose angelijua nini anachotaka kukifanya angelikubali akutane naye, kwani anachofanya ni kwa ajili yake,…lakini…. Alijua hizo ni mbinu nyingine zimewekwa na hawa mafisadi. Alipogonga ukuta huo akaona atumie mbinu za kiaskari, alichofanya ni kumwachia kazi hiyo msaidizi wake, yeye akarudi ofisni kwake, akabadili nguo na kuvaa kiraia na alipofika jioni akaingia pale hotelini kimiya kimiya.
Kwa uzoefu wake ilimchukua muda mchache kugundua alichokitaka, na kabla hajafanikisha hilo akaona kwanza akutane na mkuu wa uasalam wa hiyo hoteli, ambaye licha ya kuwa wanajuana, lakini imekuwa vigumu kukutana naye kutokana na majukumu yao. Leo akaona ndio muda muafaka, na huenda akafanikiwa makusudio yake.
Wakati anasubiri muda wa kueleekea juu ambapo alishagundua ni wapi ofisi za mkuu huyo, akawa anawaza, kuhusiana na kadhia nzima hii ya kundi haramu ambalo alishagundua kuwa lina mkono wa watu wakubwa wa serikalini. Watu hawo ndio pia kwa namna nyingine wana uhusiano na makundi yanayoongoza mapigano ya msituni. Kundi hilo limeweza kupenya kila nyanja, na kwasababau hiyo huwezi kumwamini mtu yoyote, ….Hata hayo auaji yalipotokea, alijua kabisa kuwa kuna mkono wa hilo kundi, na huyo binti anayezaniwa kuwa ni mshukiwa namba moja, katumiwa kama chambo tu.
Lakini ataonanan vipi na huyo binti, ikawa kikwazao kikubwa , hakutaka kutumia rungu la dola, alitaka kufanya uchunguzi huo kinamna yake, kwani akitumia rungu la dola lazima atakwama tu, ..akaweka dhamira kuwa alzima aonane na Rose kwa namna anayoijua yeye mwenyewe, hata bila kumshirikisha yoyote, lakini kwanza lazima akutane na mkuu wa hiyo hoteli, kwani alishagundua kuwa anajua mengi kuhusiana na hilo kundi, na huenda ndicho kilichomfanya astaafu kazi kabla ya muda wake.
***
Mkuu wa usalama wa ile hoteli alikuwa kashuku kitu, aligundua jambo, lakini hakuwa na uhakika nalo, kuna mtu amemgundua kuwa ni mgeni humo hotelini alimuona akiingia, lakini hakumuona akipitia njia ya kawaida ya kujitambulisha pale maulizo, …..lakini alimpotea katika kamera yake kiajabu ajabu, kitu ambacho hakijawahi kutokea, inaonekana huyo mtu sio wa kawaida, anawezaje kupita pale mapokezi bila hata walinzi kumuona….huyu anaweza kuwa ni jambazi lililokubuhu,..haiwezekani, katika kazi yake hiyo hajawahi kushindwa kiasi kile, …ni nani huyu mtu na kapotelea wapi, akajaribu kurudisha rudisha nyumba komputa yake kutafiti kuwa atamgundua, lakini kila alipokaribia kumuona, alijikuta akikumbana na tukio jingine muhimu la kuangalia….
‘Sasa kazi hii inakuwa nzito, ina maana ninatakiwa kupata msaidizi, kitu ambacho sikihitaji kwa sasa….’akajisema huku akiangalia huku na kule.
Alirudisha tena hadi kwa huyo mtu aliyemuona, akamvuta kwa karibu, lakini picha ya sura yake haikuonekana kabisa, akajaribu kuchunguza mienendo ya mwendo na umbile,…..hakuweza kumuhusisha na mtu yoyote. Huyu mtu alionekana ni mtaalamu sana, na inaoenakana anajua kuwa kuna vyombo vya kunasa matukio ndio maana alichukua tahadhari zote hizo, akaweka chombo chake sawa sawa, na kuanza kufuatilia alipotoka hapo alieleekewa wapi na wakati anafanya hivyo simu ikaita.
‘Kuna mgeni anataka kukuona huku chini….’akaambiwa.
‘Mgeni gani, mwambie kuwa sina muda kwa wakati huu…’akasema na kukata simu, alieleekza chombo chake hadi hapo mapokezi kumtafiti huyo mgeni…ooh, huyu ni kati ya watu asiotaka kuonana nao,…akachukua simu na kumpigia mmoja wa walinzi kuwa ahakikishe huyo jamaa anatoka humo hotelini, na amwambie kama ni kuonana naye wataonana kesho …na kabla hajamaliza kuongea mlango wa ofisini kwake ukagongwa.
‘Ni nani huyu kaja bila taarifa na ofisini kwake hapo anakuja mtu akiwa kafuatana na mlinzi wake anayemuamini…..akakumbuka yule mtu,aliyempotea kimiujiza kwenye kamre yake…harakaharaka akafungua kabati lake na kuchukua bastola.
Akaielekeza kamera yake hadi hapo mlangoni kumwangali huyo jamaa, …lakini hakuonekana mtu…, alikuwa na uhakika kuna mtu kagonga, inakuwaje asionekane mtu.Akawapigia walinzi wake kuwaulizia kuwa kuna mtu yoyote wamemruhusu kuja kwake, wakasema hakuna na wasingeliweza kufanya hivyo hata siku moja….kwani wanajua taratibu za kikazi. Aakona kuna kitu, akaegesha akmera yake iwe inachukua matukio yenyewe, na kufungua mlango, aliangaza huku na kule hakuona mtu. Akajua kuna ujanja unafanyika, akahakikisha kuwa kafunga mlango wake na ufunguo na kuelekea mapokezi.
Kabla hajafikia ngazi za kushuka chini akahisi kuna mtu anamfuatili kwa nyuma, akawa anatembea huku anasubiri muda muafaka wa kugeuka, na alipoifikia ngazi ya kwanza akageuka haraka na bastola ikiwa tayari mkononi.
‘Bado hujasahau mafunzo yako ya uaskari..?’ akakutana uso uso na yule mtu aliyemuona kwenye kamera yake na kwa ujuzi wake akamgundua kuwa ni nani licha ya kuwa kajibadili sura.
‘Siwezi kusahau hilo, kazi hiyo ilikuwa kwenye damu licha ya kunipotezea malengo….niambie kwanini uankiuka sheria,sizani kuwa aunafanya hilo ukiwa hujui sheria….’akasema mkuu wa hiyo hoteli.
‘Najua sana, lakini kwa kazi yetu hii bila kufanya hivyo huwezi kufikia malengo, nakuomba twende mahali tuongee, najua una majukumu makubwa sana, lakini hili ninalotaka kuongea na wewe ni kubwa zaidi ya hayo majukumu yako…’akasema yule mtu….
‘Kwakweli sina muda kabisa, …kama nikuongea tutaongea kesho…’akasema mkuu wa Uslama.
‘Ojong, hili ni pamoja na usalama wako, usalama wa ajira yako….’alikuwa kiondoka lakini aliposikia mambo ya ajira yake yake, akasimama na kugeuka kumwangalia yule mtu…
***********
Kilikuwa kikao cha dharura, kwenye chumba maalumu, baadaye mkuu wa ulinzi wa ile hoteli alikuwa kakaa na kuangaliana na Inspekta wa polisi, ambaye kwa alishavua sura bandia na kuwa kama kawaida, kwani mwanzoni usingelijua kuwa ni yeye, ila ni kwa kipaji cha huyu mkuu wa upelelezi ndicho kilichomgundua, hata kabla hajavua hiyo sura ya bandia…yeye alitulia kimiya na kumsikiliza kwa makini, akijua kuwa kuna jambo kubwa sana, la sivyo inspekta huyu asingelifanya jambo la hatari kama lile, kutokana na wadhifa wake.
Hata hivyo hakujali kuwa anongea na mtu mkubwa kama huyo, kwani alishakutana na watu kama hawo wengi, na moyo wake ulishajenga ujasiri, na katika maisha yake alishajiwekea kuwa hakuna jambo linaweza kutokea bila sababu na hata iweje, kama mungu kapanga iwe hivyo itakuwa hivyo, cha muhimu ni kujiamini …., akamsikiliza kwa makini huyo Inspketa, …anamjua sana mtu huyu kuwa ni mmoja wa watu mashuhuri sana katika kitengo cha upelelezi, na aliletwa toka nchi ya jirani kusaidia kazi hiyo na kutoa mafunzo.
Alimwangalia kwa makini jinsi anavyoshusha siasa za kutaka kumbadili mawazo, lakini alijifanya kama anasikiliza, lakini akili yake haikuwepo humo kabisa. Hakutaka kabisa kuongea lolote litakalomuingiza kwenye kesi za kipolisi, tangu aachane na kazi hiyo amekuwa akiwa mbali nayo kabisa, licha ya serikali kumtumia wayu ,mbalimbali kumshawishi arudi kazini,lakini msimamo wake ulikuwa ule ule, kuwa hataki tena kazi hiyo ya hatari kwa maisha yake na familia yake…. aliapa kabisa kuwa hatarudi tena kwenye kazi hiyo, kutokna na matatizo aliyopata ambayo yaliingizwa hadi kwenye hadi mwishowe aliambiwa achague moja,familia yake au kazi ….
Mwisho wa siku akawa hana jinsi akaamua kuacha kazi, na alipoacha kazi alijikuta katika wakati mgumu, kwani kiasi alichopata kama mafao kisingeliweza kumfikisha katika malengo aliyokuwa ametarajia, kusomesha watoto na hata kuwekeza. Ikabidi afikirie njia nyingine ya kuweza kumsaidia katika maisha, je afanye kazi gani ya kumuingizia kipato, na wakati anawaza hilo ndipo akakutana na rafiki yake mmoja, ambaye walijuana wakati yupo kazini, rafiki yake huyu alibambikiwa kesi ambayo kama asingelikua yeye kumsaidia angeliishia pabaya, lakini kwa juhudi zake akamasaidia na kumuwezesha kushinda hiyo kesi.
‘Nchi yetu imeharibika, kila siku mauaji,…sasa wameingia hadi kwenye anga zangu, licha ya uhdu kubwa niliyoifanya…’akalalamika Ojong.
‘Mambo hayo hayataisha mpaka nchi irudie kwenye utulivu, …mpaka sasa kuna vikundi mbalimbali visivyotii sheria, achilia mbali hawo wapiganaji wa msituni ambao wamapenyeza watu wao kila idara ili kuleta mambo yao haramu, hata ikibidi kuleta fujo au mgongano, ..sasa wao wanachotaka ni kuwa kila kitega uchumi kuwe na watu wao, ili waweze kujitajirisha, ili waweze kununua silaha…..ili waweze kuwa juu ya sheria…’akasema Inspekta.
‘Usemalo ni sawa, lakini ipo siku hali itatengamaa tu….sasa Inspekta niambie ulichonijia maana nipo kazini, na muda kwangu ni muhimu sana kama ilivyo kuwa kwako….ongea naskusikiliza….’akasema mkuu wa ulinzi.
‘Ojongo, kiutaratibu hata kama umeacha kazi serikalini , lakini sifa na wajibu bado unakuwa pale pale, wakati wowote ukihitajika huna budi kutii amri, vinginevyo ….’akatulia akijaribu kutafuta njia za kumuingia huyu jamaa.
‘Nimekuwa katika wakati mgumu katika utendaji wa kazi hii tangu nifike hapa, na baya zaidi nimekosa watu wa kunisaidia, …na hata yule unayemuona kuwa alistahili kukusaidia mwisho wa siku unamkuta ni mmoja wa watu unawaowatili mashaka…..Ikanibidi nijaribu kurafuta wastaafu,…mara nikakutana na jalada lako, nikashangaa, inakwuaje uslistaafu kabla ya muda wako,…. katika kufuatilia utendaji wako, nikagundua ndiwe mtu pekee ninayeweza kumhusiha katika kutimiza lengo langu la kukisambaratisha hiki kikundi haramu, lakini kisheria…kwani sheria sasa imeshaanza kusimama, ingawaje ni kwa shida, lakini tukiwa na ushahidi wa kutosha,…tutaweza kukishinda hiki kikundi, nakuomba unisaidie kwa hili…’akasema Inspekta.
‘Inspekta unanishangaza sana, mimi nimeshaacha kazi hii siku nyingi, na sitaki kabisa kuingia tena huko, au kujihusisha na mambo hayo tena, nikikuhadithia maisha niliyopitia, taabu niliyoipata nikiwa ndani ya uaskari hutaweza kuamini, niliweka maisha yangu rehani, nikaitetea nchi yangu kwa moyo mmoja, ….lakini nini nilikipata, …niliishia kudhalilika, familia yangu kutaabishwa kwa jambo wasilolijua, ….sitaki hata kukumbuka hilo…sitarudi tena huko hata kama ni kwa mtutu wa bunduki…hilo nakuambia,…’akasema Ojong, huku akinuka kutaka kumuacha Inspketa.
‘Sikilia Ojong, sijakuambia urudi kazini, najua hilo, hata mimi familia yangu imewekwa hatarini, ndio maana nikaamua kuirudisha nyumbani, lakini kuna wito, kuna dhamana niliyokabidhiwa na wananchi, dhamana ya kuwalinda wao na mali zao, mimi hilo siwezi kuwahini wananchi, katu siwezi kuwa msaliti,…ninachokuomba wewe ni kuwa msaidizi wangu nje ya pazia. Na huna jinsi, kwani hata ukikaa kimiya wao wameshakuanza, …hili lililotokea hapa ndio mwanzo wao, hilo nakuhakikishia kuwa tukio hilo sio bahati mbaya, huu ni mwanzo tu, …sasa kama mpiganaji hodari unatakiwa kuwawahi kabla hawajakumlaza….’akasema Inspekta na kumuacha Ojong mdomo wazi, kwani katika fikira zake alikuwa hajaligundua hilo.
Akakumbuka mkataba wake na mwenye hoteli, na kwa minajili hiyo moja ya sharti limevunjika, alikumbuka dhahiri walivyokubaliana, kuwa ikitokea mauaji au kesi mbaya ya kuhatarisha usalama, basi utakuwa ndio mwisho wa kuwa mbia,… sasa kumetokea mauaji, ina maana kazi ndio basi, hisa zake ndio basi…haiwezekani,….lazima kifanyike kitu kabla mwenye mali hajarudi, …mwenye mali yupo Ulaya, na sidhani kuwa anaua hilo, kama angelijua angelishatuma ujumbe…anamjua sana mwenye mali, huwa mkikubaliana jambo hageuki nyuma, hajui kuwa ni ndugu au rafiki, kama umevunja mkataba hakusamehi.
‘Ina maana kama anajua hilo ndio …hapana haiwezekani, ngoja nikumbuke ule mkataba vyema, akatafuta kwenye kabati na kuusoma ule mkataba, na kipengeel hicho kilikuwa wazi…wakati anausoma huoo mkataba ndio kumbukumbu za nyuma zikaanza kumrejea, insi gani alikutana na huyo mwekezaji, insi gani alivyomtoa kwenye jua nakumweka kivulini, na sasa inavyoonekana anatakiwa kurudi juani, haiwezekani, na kama haiwezekani afanyeje….oh, hapo ndipo akakumbuka jinsi gani alivyojiunga na mwenye hiyo hoteli kama mbia kivuli….kumbukumbu zikukutana na huyo jamaa tajiri zikamjia akilini..
***********
‘Mkuu , nilikuwa nakuhitaji sana, nilikuhitaji wakati ukiwa kazini, kama mtetezi wa haki, na sasa umeondoka huko kwenye uaskari…’ alikumbuka mazunguzmo yake na mwenye hoteli , siku walipokutana na kufungua ukurasa mpya wa maisha yake. Siku hiyo walikuwa akipata chakula cha mchana huku akili yake ikiwa haipo sawa, kwani alikuwa hana kazi, na likuwa kabuni miradi mingi, lakini yote ilikuwa haifanikiwi.
‘Kuondoka kwako ni pigo sana kwetu…lakini hata hivyo mimi bado sikuachii, bado nakuhitaji, kwani wewe ndiwe mtu pekee ninayemwaminii hasa katika maswala ya usalama, ….nakuomba sana, hata ikibidi nikupe sehemu ya hisa ili kuwa na wewe katika uwekezaji huu niliokwisha uanzisha wa hoteli,…’ akasema huyo jamaa huku akimuonyeshea kwa kidole, hoteli kubwa iliyokuwa katika hatua za mwisho za ujenzi kipindi hicho.
‘Ninachotaka ni kuwa wewe na mimi tuunge ubia, …mali ninayo, lakini mali bila usalama haisaidii kitu, hili nimeliona katika kuhangaika kwangu,…nchi yetu haina usalama kabisa, vita vya chini kwa chini, …makundi ya kiharamia kila mahali,…sasa nikaona ili nifanikiwe, lazima niwe na mtu anayejua usalama,…wazo langu ni mimi na wewe kuingia ubia ..’ akasema yule tajiri na kumuacha hoi yule askari aliyestahafu kabla ya siku zake, ataingiaje ubia na tajiri kama huyu, wakati hela hana….akasikiliza nini anachotaka kuambiwa.
‘Ubia unaweza ukawa wa pesa, lakini pia upo ubia wa ujuzi…ubia wa usalama, mimi nakutaka ujiungena mimi, tuwe pamoja, kwa wewe kutoa ujzui wako wa uslama, mimi nitatoa pesa na mengineyo….ila sitaki ujulikane kihivyo, kwani tutakuwa hatufanikiwi lengo nililokusudia, wewe utakuwa hujulikani kuwa una hisa kwenye hii hoteli, utaonekana kama mlinzi tu, …ninachotaka ni usalama wa hiki kitega uchumi, najua unawajua wahalifu karibu wote, sasa sipendi waingie humu ndani, …’akasema rafiki yake huyo, waliyejuana naye kipindi cha nyuma. Na maneno hayo yalikuwa kama ndoto kwa Ojong, akawa anashukuru kimoyomoyo na kusema kweli mungu hamtupi mja wake
‘Kwahiyo wewe lengo lako ni lipi, unataka kuniajiri au unataka ninunue hisa kwenye uwekezaji wa hoteli unayotaka uainzisha,….?’akauliza Ojong.
‘Mimi nataka uwe na hisa kwenye hoteli hiyo ninayotaka kuianziasha,… lakini wakati huo huo unafanya kazi kama mkuu wa ulinzi, najua sifa zako na kipaji chako, ukiwa humo kama mkuu wa usalama , hakuna mhalifu yoyote atakayeweza kuingia na kuleta mambo yasiyofaa kwenye mradi huo, …..wewe unaonaje?’ akasema rafiki yake huyo.
‘Kwangu sina shaka, ila sijui kiasi gani cha hisa, maana mafao niliyopata si chochoye kitu, kama unavyojua nimebambikiwa kesi nyingi za uwongo, ili tu nitoke bila chochote, na mimi kwa hasira niliamua kuchia kila kitu, ilimradi tu familia yangu iwe huru, bahati nzuri nikapata mwanasheria mmoja ndiye kanipigania , angalau nimepata kiasi kidogo na hicho kiasi kidogo kimemegwa kwenye kupambana na hizo kesi…kwahiyo sizani kama kitafaa lolote kama mwanahisa…’akasema Ojong.
‘Wewe mwenyewe ni hisa tosha, nitaliweka hilo kisheria usiwe na shaka, ninachotaka ni wewe tu kukubali, mengine niachie mimi, ila…naomba sana, usije ukanigeuka, …sitaki kabisa kesi yoyote itokee humo hotelini, kwahiyo kazi yako ni kuhakikisha kuwa unachunga kabisa, mtu yoyote mbya asiingie humo, nimenunua mitambo ya kisasa itakayosadia kuchunguz nyendo zozote za wateja, kwahiyo muda mwingi utakuwa ukitumia chombo hicho, ….mengine tutaongea baadaye, ila halahala, sitaki kesi …hasa za jinai na mauaji, kwenye hoteli yetu…ikitokea bwana tutaachana!
‘Usijali, mimi nawajua wahalifu wote wa nchi hii, na mtu yoyote akiingia humo hotelini nitakuwa nimeshamsoma kwa undani,…kipaji changu kikubwa ni kuwa nikimuona mtu kwa mara moja,nishamweka kichwani kuanzia sura miondoko, siwezi kumsahau tena….kwahiyo hilo halitanipa shida kabisa na ili kufanikiwa hili nitatafuta kumbukumbu zote za wahalifu toka huko kazini, huko nina watu wangu, watanipa habari zote muhimu, ….hilo lisikutie shaka…na sizani kama kutatokea kitu kama hicho, ….nimekubali na tupo pamoja…’wakakubalina na mkataba wa kisheria ukasainishwa, kwa masharti kuwa ikitokea kesi za jinai , mauaji, basi ndipo utakuwa mwisho wa Ojong kuwa mwanahisa na hisa zake zinaweza kuchukuliwa kama itagundulika kuwa amefanya uzembe.
NB Sehemu hii ni ngumu kidogo huenda ikawachanganya, kama tukijaliwa kutunga kitabu itakuwa katika muonekano unaostahili, hapa nimeandika harakaharaka tu lakini najua mtaelewa, ni moja ya sehemu muhimu sana katika tukio hili, tutakuja kuona baadaye.
Ni mimi: emu-three
Monday, October 17, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-38
Rose alipoachiwa ka dhama alikimbilia hotelini kwake, na alipofika tu mapokezi akakutana na mkuu wa ulinzi mle hotelini, alikuwa akiongea na wenzake, na alipomuona Rose anaingia akakatiza mazungumzo na kua kumpkea pale mlangoni. Alimpa pole kwa yote yaliyotokea na kumhakikishai kuwa asiwe na wasi wasi, kwani muuaji atakamatwa tu, na polisi wanamshikilia yeye ki makosa,…
Rose yeye aliona huyo mkuu wa ulinzi anampotezea muda wake , yeye mawazo yake yalikuwa kwenda kukutana na Sweetie, ajue kuwa yupo salama na anaendeleaje, lakini kila alipotaka kutoa hatua yule jamaa mkuu wa ulinzi, alikuwa kama anamzua kwa kumganda na maswali mengi maswali na porojo nyingi mwishowe akaamua kumwambia ukweli;
‘Samhani mkuu, hapa nilip mawazo yangu yapo kwa mwenzangu, kwa ni nilivyomuacha jana lazima atakuwa na wasi wasi sana, ngoja nikamuona kwanza, kwasababu nilimuacaha akiwa anajisikia vibaya, na sijui hali yake ipoje..’akasema Rose.
‘Oooh, mwenzako, usiwe na wasiwasi naye kabisa …nilimuhamisha jana usiku, na kumpeleka sehemu ya usalama zaidi, na kule najua yupo salama, ingawaje sijamtizama tangu nimpeleke kule…lakini nina uhakika atakuwa hajambo na yupo salama….ila anaonekana kama mtu aliyechanganyikiwa kidogo, ana matatizo gani, ….?’ Akauliza yule jamaa, akiendelea kumpotezea muda Rose.
‘Ana matatizo …? ..kwani umemuonaje….?’ Akauliza Rose kwa wasi wasi,…`Ndio anaumwa , lakini sio kwa hali mbaya kiasi cha kuchnganyikiwa….ooh, unanitisha ngoja nikamuone haraka..’akasem Rose akianza kupoandisha ngazi za kwedna juu…...!’ akasema Rose.
‘Ngoja tuongozane maana chumba nilichomuhamishia huwezi kukiona na nilimfungia mlango kwa nje, baada ya kumuona kama kachanganyikiwa hivi , ili asije akatoroka…’akasema yule mlinzi na kumfanya Rose azidi kuwa na wasi wasi, na hatua alizipiga za haraka haraka kuelekea juu, huku yule mkuu wa ulizi akifuatia kwa nyuma, wakaongozana hadi kwenye hicho chumba alichowekwa Sweetie, …..Yule mkuu wa ulinzi akafungua mlango,…na mlango ulipofunguliwa tu macho yao wote wawili yalitua pale akafuni alipolala Sweetie…
‘Vipi Sweetie, …?’Rose akamkimbilia Sweetie pale sakafuni alipolala, na bahati nzuri wakati huo Sweetie ndio alikuwa anazindukana toka katika kupoteza fahamu, aliinua kichwa na kutizama huku na kule halafu akamwangalia Rose machoni, …akajaribu kutabasamu, lakini baadaye akakunja uso na kugeuka kumtizama yule mkuu wa ulinzi…akiwa kama anauliza kumetokea nini….!
‘Mke wako huyo kaachiwa , nilikuambia kuwa ataachiwa, ..na nimepewa amri kuwa msiondoke hapa mpaka upelelezi ukamilike, ….kwahiyo mna siku moja ya ziada, na mimi nitaendelea kuwalinda, lakini kwa masharti mawili, kwanza mfuate yale niliyowaagiza, kuwa msitoke toke nje bila kibali changu, kama ni lazima, itabidi tuongozane, pili nahitaji malipo ya mwanzo tuliyokubaliana, maana haya ya leo na sijuii ya kesho yatakuwa vipi hayo ni hayo ya kesho yatakuwa makubalianao mengine, sawa…?’a akasema Yulemkuu wa ulinzi.
‘Sawa, nitakupa hela yako, haina shida,….’akasema Rose.
‘Pesa umepatia wapi, Sweetie’akauliza Sweetie kwa haraka.
‘Usijali Sweetie, pesa zipo, tutamlipa tu, ninachotaka ni usalama wako,…’akasema Rose
‘Ila nakuomba ukiulizwa na polsi kuwa kwanini mlihama toka mlipokuwa awali na kuja huku, hakikisha mnasema kuwa mlitafuta vyumba vya bei ndogo, ili kubana matumizi, sijaongea na hao polisi kwa mapana, wamenihoji kidogo, lakini najua leo watauliza maswali mengi zaid na huenda hilo linaweza kuwepo, name nitawajibu hivyo hivyo, kuwa amliniomba niwatafutie chumba cha bei ya chini kuliko kile cha mwanzoni,…, ila kwa kujihami,…na kwa uaslama wenu, lazima tuwe pamoja kwa hili tukio la jana, aua sio…’akasema yule mlinzi kabla hajampa Sweetie nafasi ya kuongea kwani kwake yeye alishamuona kama mtu aliyechanganyikiwa….
‘Usalama wangu, kwani nimefanya kosa gani, mbona mnanichanganya, huyu mtu anayejiita mkuu wa hoteli anasema atatulinda, kwanini tulindwe, ..halafu …mnasema kwa usalama wangu, mara kwa uslama wetu, kuna nini kinaendelea hapa…?’kabla hajamaliza simu ya yule mkuu wa ulinzi ikalia, na kwafanya wote kuwa kimiya, …na yule mkuu wa uslama akaipokea… akasikiliza kwa makini , na baadaye akawageukia Rose na Sweetie, akasema .
Polisi wamekuja kwa uchunguzi, zaidi wanataka kuongea na wewe, lakini bahati nzuri wakili wako alifika mapema kawazuia kuongea na wewe bila yay eye kuwepo, lakini polisi hawataki , wanakutafuta, kwahiyo cha muhimu, nikutoe humu hadi kwenye chumba ambacho mtakutana na huyo wakili, ili hawo polisi wakikuona wakuone upon a huyo wakili….au unasemaje?’ akasema yule mlinzi, na kabla hajasema neno akaendeela kuongea.
‘Kwa ujumla hawajui kuwepo kwa huyu mumeo, sijui kwanini, na ni vyema mkaendelea kuwa hivyo, huyu mtu asionekane kwa muda huu, kuna kitu kinawasumbua polisi pia, kuhusiana na huyu mtu wako, kuwa ulipokuja hapa mara ya kwanza ulikuwa na mtu, akachukuliwa hapa kama mgonjwa, ….lakini uliporudi hukurudi naye…lakini hilo halina nguvu sana, …ila kwa polisi wanaweza wakahisi vinginevyo wakitaka kujua huyo mtu yupo wapi…na wanaweza pia wakasema huenda huyo muuajindiye huyo mtu mliyekuja naye,….kwasababu haonekani,…na najua polisi walivyo, watakuulizia tu ,huyo mtu yupo wapi. ….’akasema yule mkuu wa ulinzi.
Rose akashituka aliposikia hivyo, na akawa anawaza ataawaambIa vipi hawo polisi wakimuulizia maswali kama hayo…., ina maana kweli wanaweza wakaenda mbali kiasi hicho, cha kumuhisi Sweetie wake kuwa ndiye muuaji, ndio maana haonekani, na akisema ukweli, ina maana hawo watu wabaya watajua kuwa huyo mtu bado yupo hai…je atamlindaje Sweetie wake asiingizwe kabisa kwenye huo msukosuko…..na hawo watu wabaya wanaomtafuta Sweetie au yeye wana uhusiano gani na Adamu, ….kabla hajawaza zaidi ilibidi akubaliane na msimamo wa huyo mlinzi, kwani hakuwa na jinsi ila kukubali tu, akamgeukia Sweetie na kumwambia asiwe na wasiwasi, kwasababu hana hatia yoyote.
Sweetie akataka kusema kitu, lakini akatulia na kuwangalia wote wawili kwa zamu bila kusema kitu, hakujua hata aseme nini, maana kila kitu anachokiona kwa muda ule ni kigeni kwake, na kila akijaribu kuuliza majibu anayopewa hayaingii akilini, akajipa moyo kuwa muda bado upo,
….akamgeukia Rose, na kumwangalia kwa makini, akashindwa kuamini, ina maana mke wake ndio kabadilika kiasi hicho, …haiwezekani, ina maana akili zake hazijawa sawa au ni kweli….
‘Kabla hujaondoka naomba nikuulize kitu Sweetie…? ‘Sweetie akamnong’oneza Rose sikioni, wakasogea pembeni kidogo.
‘Hebu niambie ukweli, …wewe mbona umebadilika kiasi hicho, na nani ulikuja na wewe toka Dar, umekuja na rafiki yangu au ulikuja peke yako, na huyo aliyekufa ni nani..? ‘akajikuta anauliza maswali mengi kuliko alivyokusudia.
‘Toka Dar….?! ….Sikiliza Sweetie, huu sio muda wa kuyaongelea haya, najua una maswali mengi, ikizingatia kuwa kumbukumbu zako zimeanza kurejea, na hata mimi nina maswali mengi ya kukuuliza, na yote haya yanahitaji muda, na sasa sio muda muafaka, …nakuomba tafadhali tulia kwanza tulimalize hili, …au uansemaje Sweetie?’ akasema Rose huku akimfunga vifungo vya shati ambavyo vilikuwa havijafungwa vyema, na macho yao yakakutana….
Wakiangaliana machoni kwa muda mfupi na baadaye Sweetie aligeuka kumwangalia yule mlinzi aliyekuwa kasimama, kwa kuona aibu kwa kile anachofanyiwa na Rose, lakini yule mlinzi alikuwa kaangalia dirishani, kwani alijua hayo yanayoongewa ni maswala ya mke na mke hayamhusu, na kipindi hicho wakati, Sweetie anamtu jicho yule mlinzi ndio wakati huyo mlinzi keshachoka kuwasubiri, alikuwa amegeuka kuwahimiza wamalizie mazungumzo yao haraka…..
‘Usijali Sweetie nafanya hivi ili kumpa uhakika yule mlnzi kuwa sisi ni mke na mume, usiniangushe…’akasema Rose,
‘Kwani sisi sio mke na mume…?’ Akauliza Sweetie kwa mshangao
‘Usijali utalijua hilo karibuni, hasa akili yako ikiwa imerejea vyema, kwani kama hujanijua kuwa mimi ni nani ina maana bado kumbukumbu zako hazijawa sawa kidogo, lakini usijali ….’akasema Rose.
********
‘Rose polisi watakuja sasa hivi kukuohoji, ninachokuomba ni kutokusema lolote watakalo kuuliza, wewe waambie siwezi kuongea lolote bila idhini ya wakili wangu na utaongea tu pale watakapokubali kuwa mimi ni muwakilishi wako, unanielewa vyema, lakini kabla ya yote nilikuwa napenda kujua ukweli wa tukio zima, ilikuwaje hadi ukafika kwenye hicho chumba?’ akauliza yule wakili.
‘Mimi nilikwenda kuchukua vifaa vyangu kwenye kile chuba ukumbukle kuwa tulikuwa tunaishi mle kbla ahtujahama,lakini baadaye tuliamua kuhama kwenye chumba kingine cha bei ndogo kidogo, ili kubana matumiazi….’akasema Rose
‘Mliamua au mlishauriwa kufanya hivyo….?’akauliza yule wakili na hapo Rose akakaa kimiya.
‘Sasa nakuomba uongee hivyo hivyo bila kuongeza kitu ukiuliza na maaskari, kwani hata mlinzi wa humu amsema hivyi hivyo, na hapo ndipo polisi wanataka kuwatega…ingawaje kuna kitu kingine polis wamegundua na ndio maana wanataka kukuona, najua ndio hivyo….swali kwao muhimu ni kwanini ulikwenda kwenye hicho chumba, na usipojibu kwa uangalifu hapo watakuja kukuingiza kwnye kesi ya mauaji, kwani wamguendu kuwa, kuna mtu alionekana akipanda juu kwenye lile jengo, akiwa kashika kitu kama gitaa, wengi ndivyo walivyozania,…na jamaa jhuyo alipanda hadi juu kabisa ya hilo jengo…’akatulia yule wakili.
‘Utata unaokuja ni kuwa sio mara ya kwanza kwa mtu kama huyo kuoenekana akipanda kueleeka huko juu na kitu kama hicho,…je ni mpango wa siku nyingi, au imetokea tu kuwa hivyo…na kama ni mpango wa siku nyingi, basi utakuwa unaujua….,sasa kinachokunasa wewe kuingia kwenye haya mauaji, ni kwamba, huyo aliyeonekana akipanda kwenda huko juu, huwa anavaa koti refu, kofia na miwani ya kufunika uso, kama ulivyoonekana umevaa wewe jana walipokukamata…
‘Swali jingine, wakati mnatoka hospitalini mlionekana mkiwa na jamaa mwenye ndevu, huyo jamaa tangu uingie humu ndani hajaonekana tena, ni nani na yupo wapi?’ akauliza yule wakili.
'Jamaa mwenye ndevu..." akamaka Rose
NB: tutaonana sehemu nyingine tukijaliwa, wenyewe hawoooo
Ni mimi: emu-three