Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, February 23, 2010

Mwoga huogapa kivuli chake

Kwa mbali tulisikia mlio wa risasi, au baruti, sote tukakimbilia sehemu yenye kilima. Haya ni mafunzo tuliyopewa, na wakati tunakimbia tulitakiwa tukimbie kwa kupindapinda. Tulupofika kwenye kile kilma tukalala huku kila mmoa akijiuliza ni nini kitafuata baadaye. Niligeuza kichwa kuwatizama wenzangu nikawaona wakiwa katika hali ya uoga. Ndio, uoga kwa binadamu sio ajabu hakuna anayependa kufa!


Ilikuwa zamu yetu ya sungusungu, na kundi letu lilijaa waongeaji, kila mmoja alijifanya anajua hii kazi na ya kuwa aliwahi kupitia jeshini, au mgambo. Wengine walijiita makomandoo, wengine mti mkavu nk. Ilimradi kila aliyepanua mdomo alijitapa kwa namna alivyowea. Hamna aliyebisha kwani wote waliokuwepo kwenye kundi letu walionekana ni wale waliokulia kipindi cha Nyerere. Kama ulimaliza vidato ulistahili kwenda mujibu wa sheria. Na ni wazi kabisa kama ulipitia enzi hizo utasimulia mengi yaliyokukuta na uwongo uliokithiri.

‘Taarifa kutoka kituo kidogo cha polisi inasema kuna majambazi yameoneka yakija kuelekea usawa wetu na polisi wanawafuatilia kwa nyuma, tunachotakiwa wakija tusijaribu kupambana nao kwani wana silaha kali’ alisema kiongozi wa kundi letu. Niliwageukia wenangu hasa yule aliyekuwa akisema sana, nikamuona mdomo upo wazi kwa woga. Nikamwambia ‘muda umefika wa wewe kuonyesha ujasiri wako..’ Akanigeukia na kuniangalia kwa woga akasema; ‘wewe hebu acha utani, hichi sasa ni kifo cha kujitakia, tutapambanaje na majambazi walibeba bunduki, kwanini tusirejee majumbani mwetu tuwaachie polisi..’

Mara gari lilioneka kwa mbali likija kwa kasi, nilichosikia ni mchakato wa miguu, ikipambana na nyasi, na nilipogeuka nyuma sikumuona yule rafiki yangu au wale waliojiita makomandoo wakati wa mujibu wa sheria. Nilishangaa, na kwa mbele nilimuona kiongozi wetu wa sungusungu akihangaika kutafuta mawasailiano na polisi. Nilimsogelea na kumuuliza wenzetu wapo wapi. Aligeuka nyuma nakujikuta anashangaa ‘ina maana hawakunielewa hawa watu, sasa wamekimbia, huko wanakokimbilia kuna usalama, wanaweza wakakutana na hao wamjambazi, watu wengine bwana..’ alisema Yule kiongozi.

Baada ya muda polisi walifika na kuanza kuwafuatilia hao majambazi, na baadaye tulianza kuwatafuta wenzetu walikokimbilia, na wengi wao walishafika majumbani mwao na kujifungia hakuna aliyekubali kuendelea kulinda. Na mmoja aliyetoka nje alisema kuna kundi moja lilikuata na majambazi siku zilizopita na wale majambazi waliawaamrisha sungusungu wote wavue nguo, na kuzalilishwa, ndio maana akakimbia. Ilikuwa hadithi ya uwoga wote tukabakia kumcheka.

Katika maisha yetu yakila siku, wengu tunapenda kuongea sana kuliko vitendo, wapo ambao kwa kuongea wanaweza wakamshinda hata mchezaji wa kombe la dunia, na kwa mdomo anaweza akaishinda timu yoyote, ngoja mtu kama huyu umpeleke uwanjani, utaishia kicheko, kwani badala ya kuupiga mpira vyema utaishia ugokoni! Wapo ambao wanajua kupigana kwa mdomo akikutana na mwenzake atamtambia kuwa yeye ni Tyson, lakini yote ni maneno matupu, kwasababu mdomo ni mwepesi kunena kuliko vitendo.

Tunashuhudia viongozi wetu wanavyotumia midomo yao kutafuta kura zetu, na kipindi chao kinafika. Tujiandae kusikia lugha nzuri za kisiasa, na sisi ambao ni wepesi kudanganyika tutaishia kupokea vijizawadi. Tuweni makini kwa hili, kwani hawa tunaowachagua ndio majemedari wa vita, na zamu yao ya sungusunu ikifika isije ikawa ile hadithi ya mwoga aliyeshia kukimbia kivuli chake mwenyewe na matokeo yake akaanguka kwenye korongo. Isije ikawa wale tuliochaguliwa kulinda sungusungu na majambazi walipokuja tukasingizia hatuna silaha!

From miram3

3 comments :

Anonymous said...

Keep it up , my friend, ona day you will be somebody, i like your stories, and your style.

Anonymous said...

[url=http://www.mocnowgore.com.pl]pozycjonowanie[/url]

Anonymous said...

[url=http://www.page1.pl]pozycjonowanie[/url]