Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, February 12, 2010

Mtenda akitendewa (2)

 Tuendelee na sehmu nyingine ya Mtenda akitendewa. Rafiki yangu aliendelea kunielezea:-

''Mimi na mke wangu tunapendana sana na nikuhakikishie kuwa sijawahi kutoka nje au kushawishika na mwanamke yoyote Yule na kutenda tendo la kuvunja ndoa yangu. Hili lilivyotokea ninahisi kuna mpango ulipangwa si bure. Lakini kama upo mpango basi umeniumiza vibaya sana, na sidhani kama nisipopata utatuzi wa mke wangu , sidhani kama nitaweza kuishi tena kwa raha.


''Hivi ninavyoongea mke wangu yupo jela kwa kosa la kutaka kuua bila kukusudia. Na baya zaidi alikiri mbele ya mahakama kuwa alifanya alichokifanya, kwahiyo mahakama iamue yenyewe. Nakumbuka alivyosema, au kuwauliza wazee mahakama. Aliwauliza hivi

‘Kama mume akimfumania mke wake anampa talaka na kama haitatoka talaka kitatoka kipigo na kudhalilishwa, je kama imetokea kinyume chake mke afanyeje, ikizingatiwa kuwa mali na watoto ilikuwa jasho la wote wawili , hakuna mali ya urithi au ndugui wa pande nyingine?’

 Wazee wale walimwangalia kama mke aliyepagawa, na hakimu alichukua rungu lake la dola na kusema Pamoja na kuwa kosa limefanyika, haijalishi kuwa ni ni nani, sheria ndio ingetakiwa ifuate mkondo wake na sio kujichukulia sheria mkononi, kwahiyo mahakama inatoa adhanu kali iwe kama fundisho kwa wengine. Hutamini, mke wangu alinigeukia na kutabasamu, akisema ''haki imetendeka, ukitaka mfuate huyo kimada wako au nisubiri nikitoka nitahakikisha kuwa haki yangu ninaipata''. Na baadaye alianza kulia na sikuweza kuvumilia na mimi nikajikuta ninalia''. Alipofika hapa kweli alianza kulia, ikabidi nifanye kazi ya kumliwaza.

''Ushahidi ulionyesha dhahiri kuwa mke wangu aliporudi toka kwenye ile shughuli alinikuta nikiwa uchi na huyo mwanamke ambaye simjui na ilikuwa mara yangu ya kwanza kukutana naye. Niliambiwa baadaye kuwa alikuwa rafiki mkubwa wa mke wangu.

''Alipofika hakuamini macho yake alitoka mbio hadi jikoni na huko alikuwa panga. Aliporudi akamkuta Yule mwanamke akitaka kukimbia akamsukumizia kitandani na hapo likafuata pigo la panga, moja baada ya jingine. Kumbuka na muda huo mke wangu alikuwa kalewa. Mahakama yote hayo ilifikiria lakini ikatoa hiyo hukumu na nimemuona wakilimmoja ili anisaidie ili nimkomboe mke wangu. Na kama itashindikana ni heri na mimi niende jela , na ninahakikisha nitaenda jela kwa kmtafuta huyu mwanamke aliyenitega kiasi hiki, nasikia hakupata majeraha mengi...''

Nilibaki mimeduwaa nikitafuta ushauri mwema kwa jamaa yangu huyu ambaye ninamjua kuwa ni miongoni mwa waadilifu, na kama limetokea lililotokea ni ushawishi wa pombe. Pombe ni kishawishi kikubwa cha kutenda usiyoyategemea, ni vyema tukawa waangalifu na hili. Sasa nimshauri nini huyu ndugu yangu, ili kwanza amuokoe mke wake atoke jela, na je ipo sheria ya kumuokoa mtu kama huyu aliyekiri mbele ya mahakama kuwa ametenda alilotenda. Na pili ni jinsi ya kumuokoa rafiki yangu huyu ambaye nia yake ianweza ikampeleka pabaya, anayofikiria ni mabaya zaidi.

Hebu tuchangie kabla sijasema nilichomshauri !

From miram3

No comments :