Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, September 20, 2013

MKUKI NI KWA NGURUWE...Utangulizi

           
        
            Utangulizi wa kisa kipya-MKUKI NI KWA NGURUWE...kwa binadamu je?

Wakati tunamalizia kisa chetu cha wema hauozi, nilitarajia kupata maoni mbali mbali kwa wasomaji, lakini haijatokea hivyo, natumai wengi tunasoma kimiya kimiya, na kutafakari ujumbe uliopo ndani yake,ujumbe ambao unaifaa sana  jamii yetu, ambayo sasa hivi inaamini sana mambo ya kishirikina, sio vijijini tu, hata huku mjini. Ni jukumu letu kuupeleka huu ujumbe kwa kila atakayejaliwa , na kwa vile siku hizi simu zinaweza kuwepo  mitandao, basi kazi hii itakuwa rahisi zaidi.

Kwenye mtandao wa kijamii wa facebook, kuna kisa tunakiendeleza cha `mkuki kwa nguruwe...’ kisa hicho tutakifanyia marekebisho na kukiweka hapa kwenye blog, kwani hapa ndipo kwenye maktaba yetu , hapa ndio nyumbani, na kwa siku zijazo, tukijaliwa tunaweza kutumia maktaba hii kwa ajili ya kutunga vitabu. ..hata e-books, kama tutapata wafadhili.

Kisa hicho cha mkuki kwa nguruwe kinaelezea udhaifu wetu wa kibinadamu ambao huangalia zaidi nafsi zetu, bila kujali athari hiyo kwa wengine. Unaweza ukatoa ushauri kwa wengine, ukiwa na nia njema, bila kufikiri zaidi, ukijua kuwa akitenda uliyemshauri,atafanikiwa, na wewe utapata faida fulani, au sifa fulani, lakini ukasahau kuwa huyo atakayetendewa na huyo uliyemshauri, ataumia sawa sawa na wewe, kama ungelitendewa  wewe...wewe hukujali hilo kwa muda huo, kwani ulikuwa mkuki kwa nguruwe.

Yamungu ni mengi, mwenyezimungu anafahamu vyema kuliko sisi, na kila jambo hutokea kwasababu fulani. Kwahiyo huenda ule ushauri ulioutoa kwa mwenzako kuwa akatende jambo, kwa wengine, ili kufanikiwa jambo fulani, huyo uliyemshauri akaja kulitenda hilo kwenye anga zako, na zile athari ambazo ulitegemea hazitakugusa wewe zikaja kwako, zikakugusa wewe, mkuki ukageukia kwako...

Inauma sana ...kusalitiwa, inauma sana mwenzako mumeo au mkeo kuwa na mahusiano nje ya ndoa, sasa inakuwaje wewe umshauri rafiki yako akatende hivyo kwa wenzako, eti ili apate mtoto, kwa vile hajaolewa, na umri umekwenda sana,...na mbaya zaidi unamshauri akatende hata kwa mume wa mtu, ...je kama umemshauri akatembee na mume wa mtu, akija kutembea kwa mume wako utajisikiaje..

Hayo utayapata kwenye kisa hicho cha `mkuki kwa nguruwe,...’ kwasasa kipo kwenye facebook, lakini huko tumekifinya sana, hapa ndipo mahali pa kukiongelea kwa uwazai zaidi. Je ilikuwaje, na ikawaje na itakuwaje...tuwe pamoja kwenye kisa hicho kipya.

Nawashukuru sana wafanyakazi wenzangu walionisaidia kukipata hicho kisa, na nafahamu na wewe unacho kisa chako chenye mafundisho, kwanini usikilete hapa kikasaidia jamii.Kuna baadhi wameanza kuniletea visa vyao, navifanyia kazi, wakati mwingine kisa kimoja kinaweza kumeza visa vingine, ...soma utaona kisa chako kikwa ndani ya kisa kingine, na ujumbe ukawa ni ule ule, ...tunashukuru sana, kwa moyo wenu huo,kwani ukiwa na jambo ukabaki nalo ni hasara, lakini ukilitoa kwa wenzako wakapata fadia ni akiba yako...ni fadia kwako...


Shukurani....na ahsanteni sana.

Ni mimi: emu-three

2 comments :

Yasinta Ngonyani said...

NImesoma utanguliza na nasubiri kwa hamu nyingiiii sanaaaa..Kama hulivyosema ni kweli kama wengi wangekuwa wanasoma hivi visa vingewapa faidi wingi sana nina imani muda si mchache wengi watasoma na kufaidika.

Amina K said...

HIKI KISA KINAELEKEA KITAKUWA KITAMU KAMA WEMA HAUOZI. NI KWELI TUPU HAYO ULOSEMA. HASA SISI WANAWAKE TUNADANGANYANA SANA UMRI UKIWA UMEENDA NA WENGI WAKIONA UMRI UMEENDA ANAMTAFUTA MUME WA MTU KWA UDI NA UVUMBA ILI AZAE NAE. JAMANI HII NI HATARI. RIDHIKA NA ULICHO NACHO.