Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha
Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..
Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.
MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.
TUPO PAMOJA DAIMA
Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;
https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:
https://www.facebook.com/diaryyangu/
`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;
Tuesday, August 30, 2011
IDD MUBARAK
‘Mimi nimenunuliwa nguo ya sikukuu mpya…’ nikamwambia mwenzangu, naye akadai kuwa hata yeye kanunuliwa nguo mpya, ikawa ubishi kuwa ni ipi ni nzuri kuliko ya mwenzake, ubishi huo ukafanya tukubaliane kuwa kila mmoja aende akaivae nguo yake, halafu turudi tukutane ili tuone nani kapendeza zaidi.
Basi kwa kujiiba, kila mmoja akaipata nguo yake toka majumbani kwao, na tulipofika mahali tukavua nguo za kushindia na kuvaa hizo nguo mpya za sikukuu, zilikuwa bado mpya zimepigwa pasi vizuri, kwa ajili ya kwenda nazo kwenye ibada ya Iddi, kama ilivyo ada kuwa siku ya Idd, uvae nguo mpya ikiwezekana na ukaswali nayo, sivyo kama wanavyofanya watu kuwa ile nguo mpya inakuja kuvaliwa baadaye….
‘Unaona nilivyopendeza zaidi yako..’ nikamkoga mwenzangu, naye akadai hivyo hivyo…na baadaye wakaja marafiki zetu wakawa wanatuangalia kwa jicho la husuda na haikuchukua muda kila mmoja akaenda kwao kuchukua nguo walizonunuliwa na wazazi wao kwa ajili ya sikukuu ya Idd, na ikawa kila mmoja ana nguo mpya. Na kama utoto ulivyo, mpira na michezo mingine haikosekani, tukawa tumejisahau kuwa tumeshavaa nguo mpya, mara tukaanza kucheza mpira, na siku mbili tatu kulinyesha mvua, kwahiyo matope na majimaji machafu yalikuwepo .
Baada ya nusu saa tu nguo mpya, hazikuwa nguo mpya tena, kila mmoja alikuwa hatamaniki, tumechafua zile nguo na wenyewe hatutamaniki, huwezi ua kuwa zilikuwa nguo mpya, na kila mmoja akawa anaogopa kurudi nyumbani na wakati huo jioni imeshafika, lakini ikawa haina jinsi, sasa tufanyeje. Utoto ukatutuma tuzifue, hapo tunachojua ni kufua tu, hakuna cha sabuni , na maji tunayofulia ni maji machafu…si tunafua bwana, tukamaliza na haraka haraka tukarejea majumbani mwetu kila mmoja kwao.
‘We Nanihino, mbona nguo zako sizioni sandukuni, nilikuwa nataka kuziangalia kama zipo sawa, maana ujue ibada ya swala ni asubuhi sana…’ akauliza mama. Nikawa najiuma uma, sina la kusema na nilipobanwa sana nikazionyesha na kudai nimezifua kwasababu nguo mpya inatakiwa kufuliwa kwanza..
‘Mamamama hivi wewe una akili kweli, umezifua au ulizitumbukiza kwenye maji machafu…’ wazazi wetu wa zamani kiboko hakichezi mbali ili bidi wanichape kidogo, na hapo ikabidi niseme ukweli ulivyokuwa,…Na baadaye ikabidi wazazi wajitahidi kuzifua tena, lakini madoa na hadhi yake ya nguo mpya ikawa haipo tena, na hata nilipoivaa kesho yake, haikuwa nguo mpya tena, ….
Jamani hiki kisa kimeniijia kichwani kwa kukumbuka utotoni, na visa vya utoto vipo vingi na vyenye mafunzo ndani yake kwani kila jambo hutokea ili iwe sababu ya funzo fulani ukiamua kutafakari kwa mapana. Na hii leo , na wengine kesho ni siku muhimu sana kwa Waislamu, kwa kukamilisha nguzo muhimu sana ya kufungwa SWAUMU, ndani ya mwezi wa Ramadhani, ni ibada muhimu sana yenye mafunzo ndani yake.
Kufunga kulikuwa sio kujizuia kula tu, bali ilikuwa pamoja na kujizua na machafu mengine,na kwa kufanya hivyo, mtu anakuwa karibu na mola wako, na pia moyo wa muumini huyu hutakasika, ikizingatia kuwa kama mwanadamu tunaishi katika mitihani, kutenda madhambi inakuwa haikwepeki, kwahiyo ilikuwa ni muda wa kuutakasa moyo kwa kutubia hayo madhambi. Na katika kufunga huku, tunakufananisha na gari, kuwa kila baada ya muda fulani gari hufanyiwa ukarabati, maana mwaka mzima unakula tu, na wengine wanakula kwa pupa, kwahiyo kunakuwa na akiba isiyo ya lazima ndani ya miili yetu, na akiba nyingine sio njema kiafya, bali ni uchafu tu, na kwa kufunga uchafu huo huyeyuka, hasa mafuta. Hii ni mifano michache tu ya faida ya kufunga.
Lakini kuna kitu kingine, ambacho ni vyema tukakijua kuhusu adui njaa, tunamuita adui kwasababu akiingia mahali madhara yake ni makubwa, kuna watu kama tunavyoona katika vyombo vya habari wanakufa kwa njaa, hawana chakula, hata kile cha mlo mmoja, …hebu fikiria mtu analala anaamuaka anashinda, na sio siku moja tu, ni masiku na miezi mpaka mwili unakunjamana, na hatimaye wengine hufa kwa ajili ya njaa. Kwa waliofunga vyema somo la njaa limepatikana, na hata akimuona mwenzake analia njaa, atingiwa na huruma kwa imani ile aliyoijenga ndani ya mfungo wa Ramadhani. Kwa somo hilo tueleekeze imani zetu kwa wenzetu wanaokufa kwa njaa huko Somalia, …tuwaangalie jirani zetu tunaoishi nao ambao hawana uwezo, wakati sisi tunakula na kusaza, …
Wakati nawaza haya nikakumbuka hicho kisa cha utotoni, kuwa sasa la mgambo limelia, shetani anafunguliwa, ile imani na huruma iliyokuwepo ndani ya mfungo wa Ramdhani itapotea kabisa, ule utulivu ulioonyeshwa ndani ya mwezi wa Ramadhani utapotea, tunasahau kuwa ndani ya mwezi wa Ramadhani tulikuwa tunatayarisha nguo mpya,…kwa kujitakasa, na kuwa kama mtoto aliyezaliwa leo, kama nguo mpya ya sikukuu, nguo ambayo haina madoa doa ya uchafu, lakini baada ya siku moja tu, hutaamini kuwa mtu huyu alikuwa kama nguo mpya, hatamaniki tena, kesharudi kwenye maasi, keshamsahau mola wake, na chuki , uadui na uhasama umeshakita ndani ya mioyo yao…nguo mpya sio nguo mpya tena…
Umri wa binadamu ni mfupi sana, na hebu angalia jinsi gani siku zilivyokwenda haraka, maana na yake ni kuwa na hata umri wa masiha yetu ndivyo yanavyokwisha kwa haraka hivyo-hivyo, juzi tuulikuwa tukiitwa mtoto, jana tu tukawa tunatambua ujana, leo mzee, keshakutwa tutaitwa jina jingine, je una uhakika kuwa utapata muda mwingine wa kuifua nguo yako iliyochafuka, angalau ionekane mpya tena….TUTAFAKARI KWA KINA
Kwa niaba ya blog hii tunachukua nafasi hii kwa kuwatakia wote, IDD NJEMA, kwa kusema IDD MUBARAKA
Ni mimi: emu-three
Monday, August 29, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-21
`Shemeji upo tayari tuondoke, saa za kwenda kuwaona wanyama imefika…..’ Maneno akashituliwa toka katika mawazo yaliyomfanya apitiwe na usingizi na haraka haraka akageuka kuiangalia sura ya Maua, na pale macho yake yalipokutana na macho ya Maua, akahisi vinginevyo, akarudisha haraka macho yake na kutizama chini , halafu kwa kujiiba akamtupia jicho la haraka kumwangalia Maua machoni, lakini cha ajabu hakuona dalili ya chuki, dalili ya….akajipa moyo kuwa huenda shemeji yake ndiye alitaka iwe hivyo, akasimama na kusema, `Shemeji mimi nilishajiandaa muda mrefu nilikuwa nakusubiri wewe tu…’ akasema Maneno
‘Kwanini hukuniita, maana sijielewi shemeji, sijui ilikuwa ni ndoto…sijui ilikuwaje, hutaamini nilikuwa sitaki kabisa kwenda tena huko porini, naogopa kukutana na lile joka …ooh, sijui ni ndoto au ni joka kwali, maana sijielewi…naogoa sana kota ndoto kama ile tena…’ akasema Maua huku akikaa karibu na alipokaa Maneno kama vila anaogoap kitu fulani na kuendelea kuongea kwa kusema, `sijui nilikuwa porini…na naona kama ni kweli tukio hilo …shemeji ngoja twende tu huko kuwaona hawo wanyama, ila natamani nirudi kwetu haraka, naona tukiendelea kukaa hapa, nitajiua….’ Akasema Maua na kumfanya Maneno abakie kinywa wazi, ina maana Maua hajui kabisa nini kilitokea usiku, ina maana yeye ndiye aliyemshinikiza shemeji yake, ina maana …ooh, mungu wangu sifanyi tena kosa hilo, …nitakuwa mgeni wa nani ikigundulika kilichotokea jana….
Safari ya kuangalia wanyama, iliwafanya wasiwe na kumbukumbu ya tukio la jana, kwani ile furaha ya kuwaona wanyama mbalimbali, na vivutio vya kila namna,viliwafanya kila mmoja awe na mawazo tofauti na mwisho wa siku wakawa wanasimuliana hili na lile kuhusina na mnyama fulani na kwanini yupo hivyo, na hapo Maneno akawa anatoa hadithi zake za utotoni kuhusiana na mnyama huyu au yule na watu wakwa wanamsikiliza kwa utaalamu wake wa kutoa hizo hadithi. Ikawa furaha na muda uliisha kama vile hakukuwa na muda hata kidogo na siku ikaisha ikabidi warudi hotelini kwao, kujiandaa kwa safari nyingine …
**************
Waliporejea hotelini, Maua akamwangalia Maneno kwa makini akionyesha kuwa kuna jambo linamkera na alihitaji mazungumzo na Maneno, ha hapo Maneno akawa anaogopa kuwa sasa inawezekana ikawa ndio mwisho wa urafiki, na chuki itachukua mahali pake, lakini akajipa moyo kuwa huenda hata Maua alikuwa yupo tayari kukubali ukweli, na kilictokea jana ni kwa utashi wake, hajamlazimisha, lakinimara akamuona Maua akibubujikwa na machozi…na baadaye akatulia na nakusema;
‘Shemeji kila nikiwaza tukio la jana naona kama ilikuwa kweli, nashindwa kujua ilikuwaje, hivi kweli shemeji niambie ukweli kulitokea nini,…kwasabau nikisema ni ndoto, nashindwa kukubaliana nayo, naona kama kuna ukweli, na sio ndoto na nina uhakika nilala na mtu jana, …nahisi kuna kitu kimetokea kisicho cha kawaida kwani hata wewe nikikuangalia machoni unakuwa kama unanionea aibu, naoma uniambie ukweli kulitokea nini…, ninauhakika kama sio ndoto jana nilikuwa maporini…sijui nilifikaje, na woga huu niende maporini, hapana ile itakuwa ni ndoto tu…’ akasema Maua huku akitizama juu kama anawaza jambo fulani.
‘Unajua shemeji nilipofika huko kwenye kuangalia wanyama, nililiwazika kidogo na kulisahau tukio zima la jana, lakini wakati tunakuja, nikawa nawaza kiundani..na sasa nimeshindwa kuvumilia, najua unajua lolote kuhusu hilo tukio nakumbuka kwa macho yangu mwenyewe nimemuona mtu…yupo wapi huyo mtu?’ akamuuliza shemeji yake.
‘Ulimuona mtu, ulimuona nani,…ina maana shemeji hujui kabisa kilitokea nini jana usiku…’ akauliza Maneno.
‘Ndio najua kuna kitu kimetokea ndio maana nasisistiza uniambie ukweli, hasa huyo mtu niliyekuwa nimelala naye, nakumbuka, kama sio ndoto lazima kuna mtu….najua kabisa na….oh,, huyo mtu ndiye aliyeniokoa, ndiye aliyenileta nyumbani..yupo wapi huyo mtu, shemeji tusipoteze muda, maana mukiendelea kunifanyia hivi, ninaweza nikafanya jambo baya zaidi….mimi muda wote nilikuwa naona kama ndoto,…kwasababu haiwezekani mimi nitoke mwenyewe hadi maporini, naogopa sana wanyama, hasa nyoka…halafu nizungukwe na joka…mungu wangu nyoka…’ alipotamka nyoka, akaruka juu kama vile analiona hilo joka na analiruka.
‘Shameji ina maana hukumbuki nini kilitokea usiku…haiwezekani….?’ Akauliza Maneno akiwa bado anajiuliza mengi kichwani, kama kweli shemeji yake hakumbuki lililotokea mbona itakuwa kashifa kubwa kwake, mbona….
‘Haiwezekani ikawa ni ndoto…nakumbuka kabisa nilikuwa nimezungukwa na joka, kubwa,…lakini mara akaja mtu akaniokoa na kunirudisha hotelini, halafu tukalala naye, halafu, tuka…..ooh, Maneno niambie ukweli kulitokea nini, maana ukinificha lazima ipo siku utaumbuka, maana ninahisi kuna mtu aliniokoa ni nani huyu….na yupo wapi…namuomba nimuone.’ Akaonyesha furaha fulani na kuanza kutoka nje kumtafuta huyo mtu na Maneno haraharaka akamzuia na kumsimamisha, na kuwambia kuwa sio ndoto kuwa kweli alitoka nje, kweli alikuwa kafanya hivyo na kwenda porini, ila yeye kama Maneno hajui jinsi gani ilivyokuwa hadi Maua akafika huko porini.
‘Una uhakika na unachosema Maneno, unajuaje kuwa nilitoka nje na kwenda huko maporini, …’ akauliza Maua huku akimuangalia Maneno kwa macho ya shauku, na baadaye akakunja uso kuonyesha kuwa yupo kwenye kutafakari kuzito akawa akasema `Unasema hujui kabisa nilitokaje usiku na kwenda porini, na hujui kuwa nilikuwa nimezungukwa na joka kubwa?’ akauliza Maua na kumwangalia Maneno usoni, na Maneno akawa anaona aibu kumwangalia Machoni na kugeuka kuangalia dirishani.
‘Unajua mimi sijakuelewa Maua, kwasababu umesema hukumbuki, ina maana kwako ni kama ndoto au sio?
‘Ndio maana nakuuliza, kwasababu hapa nilipo nachanganyikiwa tu, sijui, lakini nilipoangalia lile gauni nililovaa jana nikaliona lina matope, limechafuka lina majani ya porini, lina dalili za udongo, nikakumbuka kuwa hata mimi nilipoamuka asubuhi, nilijihisi sipo kawaida…kuna tendo limefanyika….hapana haiwezekani, ikawa ni ndoto. Alipofikia hapo Maneno akamgeukia Maua na kutaka kujua zaidi kuhusiana na hiyo kauli kuwa ameihisi kuwa hakuwa kawaida…ina maana kuwa….
‘Shemeji mimi naona usijitie kwenye mawazo mazito kama hayo, tulichukulie kuwa ni ndoto na tukubali hivyo iishie hapo, unaonaje?,…ila ni kweli kuwa ulitoka usiku…sasa ulitokaje, mimi sijui labda hizo hisia za kuwepo kwa mtu mwingine, ndio hapo naweza kusema ni ndoto, kwani sijawahi kumuona mtu mwingine humu ndani zaidi yetu wawili …………’ Akasema Maneno huku anamwangalia shemeji yake kwa macho ya aibu, alishindwa kuelezea zaidi, atamuelezeaje kwani hata yeye mambo mengine aliyaona kama miujiza,…hakumbuki nini kilimshinikiza kufanya vile.
‘Shameji unasema ukweli kuwa nilitoka nje hadi maporini,…lakini hukuiniona nikitoka sawa au si sawa? Akauliza Maua halafu alipomuona shemeji yake kanyamaza kimiya akaendeela kusema `mimi nilikuwa naiona kama ni ndoto, ina maana kweli nilikwenda porini, ina maana kweli nilikuwa nimezungukwa na joka,…lakini sasa je ni nani aliyekuja kuniokoa….kwasababu kuna mtu alikuja akaniokoa na hatimaye akanirudisha nyumbani….?’ Akauliza Maua huku akiwa bado anatizama nje kwa hamasa. Na hapo taswira ya usiku ikawa inamjia kichwani na akageuka kumwangalia shemeji yake na macho yao yalipokutana Maneno akainama chini kwa aibu, akijua sasa chuki itaanza. Na hapo Maua akaanza kukumbuka ilivyokuwa hiyo ndoto au ukweli alifnaya hivyo….
***********
Ilikuwa usiku wa manane, wakati Maua aliposhituliwa na sauti ya ajabi kichwani, ni sauti ile ile ambayo ikimjia inakuwa kama ina mamlaka fulani kichwani mwake, inaweza kumuamrisha akafanya jambo ambalo baadaye hajui alilifanyaje, ina kuwa kama mwili unafanya bila utashi wake, na hali hii imeanza baada masiba wa mume wake, hakuwahi kuwa na hali hii kabla. Basii hali hii ilipomtokea, ikawa inamuamrisha atoke pale kwenye hoteli, atoke haraka nje, kwani Mhuja yupo sehemu anamsubiri, bila kuwaza zaidi kuwa huenda ni ndoto tu au ilikuwa sauti ya nini akainuka haraka kitandani, na kutoka nje ya jengo lile la hoteli.
‘Jamani tunawapa tahadhari kuwa mpo eneo ambalo halihitaji mtu kutoka mwenewe na kuingia eneo la mbuga bila mlinzi, au mwongozaji aliyetambulikana, kuna hatari ya wanyama wakali sio wanyama tu , kuna nyoka na wadudu wenye sumu, kwahiyo muwe kwenye hoteli zenu mpaka muda ukifika mtaongozwa na wahusika…’ hayo yalikuwa maneno waliyokuwa wameambiwa walipofika, na kwa hali ya akawaida, lbada uwe jangiri au una nia mbaya, hungeliweza kutoka na kuingia maeneo yenye wanyama wakali, lakini kwa muda ule tahadhari na uwoga huo haukuwepo kwa Maua.
Akatoka nje ya jengo, na alipofika nje ubaridi na upepo wa usiku ukaingia ndani ya mwili wake kupitia kwenye gauni refu la mikono mirefu alilokuwa kalivaa, hakuijali hiyo hali, alichokuwa anakihitaji ni ile sauti inayomuongoza, alichokihitaji ni kufika hapo alipoambiwa kuwa atakutana na Mhuja, akawa anafuata sauti inavyomuamrisha, twende huku pitia hapa…ilikuwa kwa mwendo haraka, hadi akawa kafika mbali kabisa na ile hoteli hadi ndani katikati ya msitu, alipofika hapo , ile sauti ya kumwamrisha ikapotea, akawa kasimama kwa muda akiwa anasubiri maagizo mengine.
Mara akili ikamrejea na kuwa kama kazindukana toka kwenye usingizi , na alipoangalia huku na kule akajikuta katikati ya msitu na kwa mbele aliona kama kitu kinavunja vunja majani , mara kukawa kimiya, woga ukaanza kumuingia,, akawa anajiuliza nipo wapi, ….ooh, nipo msituni, e nimakujaje hapa, akawa anawaza, bila jibu, akaangalia huku na kule lakini hakuona kitu, sauti yam situ mkali…na milio ya wadudu wa usiku…
Mara akasikia sauti kama radi ikitanda hewani, akaziba masikio na mwili ukamzizima kwa woga, akaangalia huku na kule akitaka msaada, lakini inavyoonyesha yupo mbali kabisa na hoteli. Akaanza kutembea kwa kunyata kudogo kidogo, kuelekea asipokujua, lakini kila alipokuwa kitembea alihisi kuwa kuna kitu kinamneyemelea kwa nyuma, akawa anaongeza mwendo na hicho kitu, sijui ni mnyama nacho kikawa kinaongeza mwendo, ….simba…alipogundua hilo akatamani kuanza kukimbia, lakini kuna auti ikamwambia dawa ya huyu mnyama sio kumkimbia unatakiwa urudi kinyumekinyume, mapaka uhakikishe umeondoka maeneo ya umbali wake…
Alifanya hivyo kurudi kinyume kinyume…akawa anarudi kidogokidogo hadi akawa upeo wa mbali wa kile alichogundua kuwa ni simba, halafu akageuka na kuanza kukimbia, alikimbia ,alikimbia hadi miguu ikawahina nguvu tena, na alifika sehemu akawa kakanyaga kitu kama laini lakini ni kama sponji, akasimama na kuangalia chini….ooh…akajikuta mwili umekufa ganzi nyoka…cha ajabu badala ya kukimbia akawa kasimama pale pale…
Alikuwa nyoka mkubwa ambaye hajawahi kumuona katika maisha yake, alikuwa haoni kaanzia wapi, na akawa kama anajiviringa, kumzunguka….akawa hawezi kutikisika,na kukawa na kitu kama sauti ikiwa inamwambia kama wimbo kuwa wakati umefika wa mwana kurudi tumbani, na kusahau machungu yadunia, na sauti nyingine ikawa inamwambia kuwa akimbie, yupo kwenye hatari, lakini miguu ilikuwa imekufa ganzi, haibanduki pale iliposimama na mara sauti ila ya mwanzo ikamwambia tena sasa wakati wa kwenda kumuona Mhuja umefika, subiri hivyo hivyo, sasa huhitai sumu au kamba ya kujinyongea….
Alipotajiwa kamba ya kujinyongea , akaukumbuka kuwa alipotoka nje aliculkua kamba, lakini hakujua ni ya nini, na alipotizama mkononi akajiona ana kamba,…kamba ya kuinyongea, akawa kaishikilia, lakini alipoambiwa kuwa haihitaji tena ile kama akaitupa chini, na huku miguuni, alihis lile joka lijijiviringa miguunii mwake kama mtu anayemfunga migu yote miwili kwa kumzunguka, lakini lilikuw ahalijambana kiasi cha kuweza kuhisi hivyo, cha ajabu kichwa cha lile joka kilikuwa hakionekani…..’
Mara akamuona mtu anakuja,…ooh, keshafika mtu wake aliyeambiwa watakutana naye…hatimaye keshafika, kumbe ni kweli …mpenzi wake, huyo keshafika, watu waongo bwana, eti kafa, sasa huyu ni nani..na wakati anawaza hili, huku akiomba huyu mpenzi wake afike haraka pale alipo ili amuokoe na yule nyoka anayetaka kumviringa,akagundua kuwa nyuma ya yule mtu pia anakuja simba, kwahiyo yule mtu akawa nakuja kama anakimbia, na nyuma yake huyu simba naye anaongeza mwendo…ooh, yule mtu anakimbizwa na Simba, mungu wangu nitamuokoaje mume wangu….na wakati miguu haiinuki, akawa anawaza na wakati anawaza mara yule mtu akamkaribia, na ghafala akamshika na kumvuta, lakini badala ya kuvutika, wakajikuta wanapaa hewani, ina maana yule nyoka aliwarusha akiwa na lengo la kuwabana, lakini cha ajabu kilichotokea ni kuwa yule Simba aliyekuwa akimkimbiza yule mtu alichukua nafasi ile aliyokuwa kasimama Maua, na akawa kazingirwa na yule nyoka, kukawa ni vuramai.
Hapo kumbukumbu ikamtoka hakumbuki zaidi ilikuwaje, ila baadaye alijiona yupo hotelini kwao anapandishwa kitandani…..na baadaye kukawa ni raha ya ajabu..ooh, mpenzi wangu umerudi m nakukabidhi mwili wangu wote ….oooh, ikawa ni raha ….na mara kukapambazuka, hamuoni yule mtu wala hakumbuki ilikuwa ni ndoto au ni kweli….
**********
Shameji nimekumbuka alikuwa ni ‘Mhuja…’akasema Maua. ‘Huyo mtu alikuwa ni mume wangu, ….kama haikuwa ni ndoto, basi ni Mhuja nilikuwa naye jana, kweli sasa nimeamini kuwa yupo hai, nimemuona mwenyewe kwa macho yangu, akiniokoa toka katika lile joka, akanifikisha hapa nyumbani, ….ooh, mungu mkubwa hatimaye sasa, ….lakini yupo wapi Mhuja, hebu muite,…Mhuja, mhuja….mpenzi wangu upo wapi….’ Maua akawa anaita kwa sauti na mara akakurupuka na kukimbilia nje kama mwehu, na kumuacha Maneno akiwa anashangaa tu. Baadaye Maua akarejea akiwa bado ana macho ya kutafakari..
‘Shemeji , nahisi una tatizo kubwa, na hili tatizo inabidi tulifikishe hospitalini haraka iwezeanavyo, na naona hata safari ya Ngorongoro inabidi tuikatize, tutaifanya siku nyingine, kama kweli hukumbuki kilichotokea jana, basi, hilo sasa ni tatizo kubwa, sitaweza kukaa kimiya na kukuacha uteseke, jiandae tuondoke,….’ Akasema Maneno huku akimwangalia shemeji yake kwa macho ya aibu, aliogopa kabisa kama atamwelezea nini kilitokea jana, basi itakuwa balaa,…hasa alivyogundua kuwa kumbe mwenzake alikuwa anajua kuwa aliyemuokao usiku ni Mhuja na…
Hata Maneno alipojaribu kutafuta njia ya kulielezea lile tukio la jana lilivyo, alishindwa kwani hata yeye aliiona kama ndoto, inagwaje yeye anakiri kabisa ilikuwa sio ndoto, lakini angemuelezeaje Maua , kwa kushindwa kulielezea lile tukio na kushindwa kumfichua Mhuja ambaye Maua anadai kuwa yupo kukazua kubishana na hata Maua akawa hataki hata kula, anadai kuwa ana uhakika kuwa Mhuja yupo na Maneno anajua hilo , anachofanya ni kumdanganya,…ikawa hakuna maelwano hata Maneno akataka kusema ukweli, lakini Maua akawa hasikilizi , na Maneno akaona huo sio wakati muafaka wa kuomngea ukweli wote, ni bora asubiri wakati muafaka, kwani Maua alikuwa kama kapandisha jaziba, na hata kumuita shemeji yake mzandiki, mtu anayependa yeye ataseke, ili baadaye amkose kabisa mume ki kabisa kuongea na shemeji yake,…
‘Kama mimi nipo hivyo ili iweje, kama mimi nipo hivyo na huyo Mhuja utamuita nani, kwanini yeye awepo hai na awe anakuja na kujificha kama kweli anakuali na kukupenda,…kama kweli anakupenda kama unavyodai kwanini akuache uteseke hivyo….hiyo ni ndoto tu, ni akili yako inakuadanganya Maua, Mhuja keshakufa…’ akasema Maneno na alijikuta akizabwa kibao kufungwa mdomo. Akashikwa na mshangao kwani kibao hicho kilitokea bila kudhaniwa, na Maua akaonyesha kweli kakasirika, akasema kwa jaziba
‘Usirudie kauli yako hiyo, kauli hiyo nilishaikubali kabla ya tukio la jana, lakini baada ya tukio hilo la jana sikubali tena kuwa Mhuja keshakufa, Mhuja yupo hai, na jana nilillala naye, kama unakubali kuwa jana nilitoka usiku, jana nilizungukwa na joka, na kwanini usikubali kuwa alikuja Mhuja kunikoa, na hata akanifikisha hapa nyumbani tukalala naye na hata…kwasababu yote hayo nayakumbuka…na niliyaona kama ndoto…’ akasema Maua huku anaonyesha uso wa furaha, kuonyesha kuwa kweli ana uhakika kuwa alikutana na Mhuja. Hapo Maneno alibakia kutahayari, kwani kwa hali ile inaonyehsa dhahiri kuwa, Maua anajua kuwa aliyemuokoa ni Mhuja, sio yeye Maua na kama atajua kuwa aliyemuokoa kule ni yeye Maneno, basi , litazuka jambo kubwa sana, na huenda ikajengeka chuki kubwa sana, na itafika kwa shangazi mtu….ooh, nitamuambiaje yule shangazi, kwahiyo lazima kuhakikisha kuwa sehemu hiyo ya mkanda anaikatwa kabisa…….
***********
Safari ya kurudi Dar ikafanyika haraka haraka na walipata bahati ya kuondoka kwa ndege, ilikuwa ni baada ya kukutana na watalii waliozoena nawo wakasema wapo tayari kutoa ufadhili wa ndege, kwani wao walikuwa wakiondoka kwenda Dar, na walitaka kupata wenyeji ambao watawatembeza Dar, na hata Zanzibar, na kwa vile katika kukutana nawo hapo Arusha, walitokea kumpenda sana Maua , kwa vile alikuwa nao karibu akiwafundisha Kiswahili, basi wakamchukulia kama mwalimu wao, na hata baadaye alipokuja Maneno kujiunga katika mazunguzmo ya kuwafundisha Kiswahili, wageni hawo wakaiona wamepata watu waliowataka, kwahiyo wakapewa ufadhili huo wa kuapnda ndege hadi Dar.
Kesho yake Maneno alipokuja kumuona Maua , alimkuta akiwa na uso wa furaha sana, akamuulizia vipi mbona anafuraha sana, Maua akamwambia;
‘Shemeji hawa watalii wamenipa tenda, na tenda hii inanihitaji niende Zanzibar na wao, kwani wanataka mtu kama mimi ambaye nitakuwa nawo bega kwa bega, kwanza wanataka kujifunza Kiswahili, pili wanataka mtu kama mkalimani wao, na mimi wametokea kunipenda name naona itanisaidia kuliko kukaa hapa na kuanza kuchanganyikiwa kwa mawazo …. nimeona niwe nawo kama awalivyoniomba, na animeongea na shangazi kanikubalia, sizani kuwa kitaharibika kitu, kwahiyo kesho tunaondoka na wao kwenda Zanzibar…’ akasema Maua.
‘Lakini shemeji unakumbuka tumekatisha ziara yenu ya kwenda Ngorongoro kwasababu ya afya yako, kwasababu unahitajika kumuoma dakitari bingwa wa magonjwa ya akili…mimi nisingependelea uende hiyo safari yako na hawo wazungu, mimi naweza kuwatafutia mtu mwingine atakayewafaa, nakuomba kesho twende kumuona huyo dakitari bingwa..tafadhali Maua’ akasema Maneno.
‘Shemeji ina maana mimi umeniona ni tahira au sio, kuwa mimi nina ugonjwa wa akili kwasababu ya kukuambia ukweli. Hilo huniambii kitu, wewe mwenyewe kwa kauli yako umenikubali akuwa kweli ilikuwa sio ndoto…umeniambi wewe mwenyewe kuwa kweli nilitoka usiku, ni kweli au sio kweli, ukanimabi kuwa nilizungukwa na joka kubwa ni kweli au sio kweli…lakini hujaniambia ni nani nani aliyeniokoa, ni nani alilala na mimi usiku, kama sio Mhuja…niambia kama sio Mhuja ni nani..kwasababu nimemuona kwa macho yangu mawili…unanifanya mimi tahira sio…ngoja nirudi hii safari …nitamtafuta Mhuja hata kama ni kwa gharama yoyote, najua…yupo hai….’ akasema Maua akiwa na hasira, na mara wakaja wale wegani wao na mazunguzmo yakabadilika…
Na kweli kesho yake Maua wakaondoka na wale watalii, kuelekea Zanzibari, lakini Maneno hakuwa na amani kwa safari hiyo, alitamani aondoke nao, kwa ajili ya usalama wa Maua, alikuwa anajua kabisa huyo mtu bado yupo katika tahadhari na anatakiwa kuwa karibu na mtu anayemfahamu, je akichanganyikiwa huko kama ilivyotokea huko Arusha, nani atajulia, alijaribu kumshauri Maua….lakini Maua alikataa katakata, na kusema yeye sio mgonjwa wa akili kama wanavyomuita ana matatizo ya kiakili…na hata hivyo, hawa wageni wataongezewa gharama ambayo haikuwepo katika mipangilio yao, na alishakubaliana nao kuwa yeye ataongozana nao, bila wasiwasi, yeye anajiona yupo mzima, wasiwe na wasiwasi na yeye…
Maneno akabakia akiwa hajui afanye nini, aliikuta akiwa katika majuto makubwa, kwasababu kwanza alikuwa keshaweka miadi na yule dakitari bingwa mtaalamu wa akili kuwa watakuja na Maua, akaona haitakuwa vyema akibakia kimiya, akamwendea mwenyewe huyo dakitari bingwa kuonana naye, na ikibidi apate ushauri wa kitaalamu. Akamwendea hospitalini kwake na kumuelezea hali halisi ilivyokuwa na yule dakitari bingwa akamshauri kuwa alivyofanya ndio sahihi, lakini lazima waje pamoja na huyo Maua, yeye atajua jinsi gani ya kumuelezea ukweli ulivyokuwa, na ingawaje uwezekano wa kutokea kutokuelewana upo, lakini haitachukua muda kama swala hilo litanyamaziwa hivyo hivyo, kwani huyo muathirika, yeye kajenga hoja kuwa huyo aliyekutana naye ni aliyekuwa mume wake, na hisia hiyo haitamuondoka akilini mwake mpaka apate ukweli wa tukio lenyewe.
Alipotoka hapo kwa huyo dakitari bingwa akarudi nyumbani kwake na kupata taarifa nyingine kuwa shangazi wa Maua alikuja na atarudi baadaye anamazunguzmo na yeye, ya muhimu sana…! Kauli hii ikamtia wasiwasi, mazunguzmo ya muhimu sana, akaanza kuwaza, afanye nini, kwani shangazi yule ndiye mlezi na mzazi wa karibu wa Maua na anakumbuka mazunguzmo yao wakati wanamuaga kwenda kutalii mbuga za wanyama alimwambi mwanzoni kama utani, lakini baadaye akawa anatoa kauli za ukali, za vitisho, alianza kwa kumwambia; `Maneno nakuona ulivyo mwingi,..maneno-maneno, kama jina lako lilivyo, ni sawa inatia moyo kwa kuwa mwanentu anahitaji maliwazo kama hayo, ila nakuomba halahala mti na macho usije ukatumia tatizo la shemeji yako kwa ajili yako..nawajua sana nyie wanaume, huyo ni mwanangu nimemlea mwenyewe, anahitaji muda wa kukaa na kutafakari kabla hajaingia kwenye ndoa tena, najua kweli ni vyema akapata mume kama wewe, mtu anayemjali, lakini …nakuomba tafadhali usije ukaanza ….ukaanza….’ Shangazi hakumalizia yale maneno lakini Maneno aliyaelewa, na kumuahidi kuwa kamwe hatafanya dhambi hiyo
‘Shangazi hivi mimi huniamini, unafikiri kwanini nipokaribu sana na Maua, sio nafanya hivi kwa uchu..hapana, ni kwasababu mimi na Mhuja tulikuwa marafiki wa ukweli na hili nataka jamii ilithibitishe hilo kuwa kwa hivi sasa mke wa rafiki yangu yupo kwenye shida, yupo kwenye dhiki, siyo ya kihali bali ya kihuzuni, ya kimoyoni ambayo inayohitaji mtu wa karibu wa kumliwaza, na mimi ndiye rafiki wa mume wake wakiukweli,….’ Akasema Maneno.
‘Nyie wanaume nawajua sana, hayo Maneno yako yasije yakawa maneno kweli, maana tutakosana kabisa, …hili nakuhakikishia hata ikibidi kukufunga nitakufunga, sina mhezo na mwanagu..’akaongea shangazi akionyesha udhabiti wa kauli yake, halafu akazungumza kihekima kwa kusema ` Ndio ninakushukuru sana kuwa umemjali sana mwenzako na umemuonyesha upendo wa dhati, kuwa hata kama mwenzake hayupo lakini ana mtu anamjali na kumlinda, lakini kila kitu kina muda wake, na muda wa mengine, kama yapo, usubiriwe,… kwasababu mimi sio mtoto mdogo, najua kabisa nini kilichopo moyoni mwako, hata kama hujafikia kuniambia, ila kama ni hivyo nisingependa kamwe yatokee haraka hivyo,…
‘Mimi sio mtoto mdogo, na ukumbuke mwanetu ana heshima zake, sio mwenzake kafa, inakuwa kama vile, kufa kufaana, haipo hiyo, kila jambo kwa muda wake, nielewe kauli yangu, …nakuomba tafadali sana, tafadhali, usinije ukaniona mbaya kwasababu mimi mwenyewe nipo, na nilikuwa tayari kuwa naye kwa lolote lile, lakini wewe mwenye uliniomba kuwa kwasababu Mhuja alikuwa rafiki yako ungelipendelea kuhakikisha kuwa mkewe anaishi maisha mazuri na hata ikifikia muda kampata mwenzake wewe utakwua tayari kuhakikisha kuwa kweli anamfaa, hapo utasimama kama kaka mtu…sasa isije ikatoka kwenye ushemei na kuwa mengine …kwahiyo narudia tena, linda heshima ya mwanangu na linda heshima yangu…’akasema shangazi mtu.
‘Shangazi nakuhakikishia kuwa kama litatokea kama unavyonidhania wewe niweke ndani, na nitamuomba hakimu anifunge maisha, mimi na Mhuja ni zaidi ya ndugu, leo hii nimsaliti kirahisi hivyo…hapana Shangazi hilo halitatokea kamwe, kwanza nitamuanzaje huyo shemeji yangu!..’ akasema Maneno na huku moyoni akiongezea kwa kuwaza akisema kimoyomoyo `Shangazi kiukweli kama binadamu nakubali kuwa hamasa hizo za kumpata mtu kama Maua zipo hilo nalikukubali, na…mmh, shangazi ningelitamani nimapte mtu kama Maua katika maisha yangu, lakini sio kwa kipindi kama hiki, nitauweka wapi uso wangu,’ akamwangalia shangazi yake akatabasamu akasema;
‘Shangazi unaonekana huniamini kabisa, uwe na amanikabisa kwanza huyo shemeji mwenyewe siunamuona alivyo, utamwiingiaje,kwa mambo kama hayo, hapana, namuheshemu sana, na niyailinda heshima yangu…nakuhakikishia hilo shangazi…’akaongea kwa heshima.
‘Sawa Maneno ukumbuke sana kuwa ahadi ni deni,… ila wengi waliahidi kama wewe na mwishowe wakaumbuka, na kwangu utaaumbuka kweli, sina utani…mwanangu kapitia hatua ngumu na sasa kaanza kutulia naomba safari yenu iwe ya heri…’akasema shangazi mtu,
`Je heri yenyewe ndiyo hiyo…?’ akajikuta anajiuliza Maneno kwa sauti, huku akiwaza mengi kichwani, je shangazi yake huyo anamuhitaji kwa lipi, ….huenda Maua kashamwamia nini kilitokea huko Manyara, na shangazi anataka kujua ukweli ulivyo , na kama anataka kujua ukweli ulivyo yeye Maneno atamwamba nini,….?
*************
Maneno alikuwa kama anaota ndoto mbaya, akashituka toka usingizini na kuiona akihema kama vile mtu aliyekimbizwa, akakurupuka kitandani na kusimama, alivaa nguo za baridi kwani alikuwa kalala na nguo nyepesi, kwasababu ya uzoefu wa safari, alijua avae nguo gani na nguo gani ziwe karibu na kitanda kwa ajili ya dharura…alihisi kuwa kuna harati, lakini hakujua ni hatari gani, alichofanya ni kutoka kule chumbani kwake, na alipotoka pale chumba caha mapumziko akakuta mlango wan je upo wazi…tumeingiliwa na mwizi, ilikuwa wazo lake la kwanza..
‘Maua, upo, Maua…’ akaita huku anagonga mlango wa chumba cha Maua, lakini hakusikia sauti yoyote, akataka kuufungua mlango lakini akasita, huenda shemeji yake kalala na huenda kalala vibaya, kuingia bila ruhusa inaweza ikaleta muonekano mbaya..akagonga tena na tena, alipoona kimiya, akaangza kuona wasiwasi na hapo akakumbuka tukio la jana, jinsi alivyomuona shemeji yake akiwa kabadilika alikuwa kasimama mlangoni huku anaangalia kamba, kwanini alikuwa akiingalia ile kamba, na alipomuuliza kulikoni akawa kama kakurupuka toka usingizini na kukimbilia ndani.
Akaona subira imemshinda akafungua mlango na ulikuwa haujafungwa kwa ndani, kinyume na alivyo Maua tangu wafike hapo huwa anafunga mlango kwa ndani, labda kwasababu ya usalama, kitu ambacho Maneno hakukipenda, lakini aliona asimshinikize shemeji na huenda akamzania vibaya kuwa anaomba iwe hivyo ili pate mwanya wa kua kumsumbua, kitu ambacho Maneno hakuwana cho kichwani kabisa..
Alipoingia chumbani alikuta shua lipo chini, ..na kitandani hakuna mtu…akageuka huku na kule , lakini hakuona dalili ya mtu, akaanza kuingiwa na wasiwasi, …akatika haraka mle ndani hadi nje,wazo lake la kwanza ilikuwa kuiangalia ile kamba ambayo shemeji yake alikuwa akiingalia mchana, alisahahuu kuiondoa pale,kwani jinsi sheemji yake alivyokuwa akiingalia alihisi alikuwa na maana yake,….ile kamba haipo, …akaanza kuwaza vibaya, akakumbuka hadithi za watu waliojiua kwa kamba.
‘Haiwezekani, shemeji yangu atakuwa kapatwa na nini..mbani anakuwa kama kachanganyakiwa, kama ningeliua hili mapema ningelimpeleka hospitali akaonane na dakitari bingwa wa mambo ya akili…’ akajikuta akiongea peke yake…
‘Sasa nitamtafuta wapi..naumbuka jinsi walinzi wa hapa walivyotukanay kuhusiana na hali ya hapa kuwa watu wasitoke nje wenyewe, au kuingia msituni…’akaanza kuogoa mwenyewe, maana alisikia mngurumo wa simba…ooh, kama Maua yupo huko…mungu wangu mtoto wa watu keshaliwa na Simba. Maneno ni muongeaji ,lakini kw ahatarii za wanyama, ….hakuweza kuwa na uajsiri huo, akaona akamuulizie mlinzi…lakini kabla hajafika mbali akaona kitu kimedondoka chini…alipokisogelea akaona ni picha ya mtu…akawasha taa ndogo aliyokuwa nayo…picha ya Mhuja..
‘Maua keshaingia msituni na huenda kaeshajinyonga…’ akasema na bila kwenda kumuona mlinzi akaanza kufutaili hisi ake zilivyomtuma, kuwa huyu mtu atakuwa kapitia hapa, akwa anatembea harahaharaka hadi alipofika sehemu fulani, akaona kitu kikitingishika kwa mbali , mara kukapita kitu kama mshale kukatisha barabra…oh, fisi au chui..akasiamama, kurudi nyuma sasa mbali kwenda mbele kunatisha.
Wakati anawaza hili kwa mbele kidogo akaona kitu cheupe…yule sio mtu yule..akaaingiwa na mashaka, isije akawa mwanga..akaanza kumfuatili taratibu, lakini badaye akasikia kitu kama kinakuja nyuma yake, akaingiwa na mashaka, haraharaka akaongeza mwendo kuelekeak kule alipoona hicho kitu cheupe, alifanya hivyo kwasababau ya kuogopa kuwa kunakitu kibaya kipo nyuma yake…akaongeza mwendo kama anakimbia, ilimfanya afikie pale alipoona kile kitu jwa haraka…
‘Maua….ni Maua, mbona kaganda kama kasimamishwa na kitu, akamfikia haraka na kumdaka na mara kitu kwa chini kikajifunga haraka na kuwafanya watupwe huku na kule….bahari yao , maana kilichokuwa kikiwafuata nyuma kilikutana na mzunguko wa jaoka kubwa na kuwafanya wao wanasuke na kuikuta wamelala chini na kwa haraka Maneno akamzoa zoa Maua na kukimburuza mbali …huku akishuhudia vurumai la Simba na nyoka chatu…hakuwa na muda wa kungalia, akambeba Maua begani na kuanza kukimbia naye hadi Hotelini.
Maneno hakuweza kulala kabisa, alipomfikisha Maua hotelini akiwa kachoka, akamwela kitandani kwake na alipomuona yupo salama, na kazindukana ingawaje alikuwa kimiya haongei lolote, lakini alimkagua na kumuon ahana jeraha lolote, aliinuka kuondoka, lakini akashangaa kuona mkono wake umekamatwa...
‘Shemeji tafadhali usiondoke, …naogapa..naogapa kuna kitu kinaniandama kinaniamrisha kujiua…’ akasema kweli akionyesha macho ya uwoga, …Maneno akawaza sana na kumsogeza Maua kitandani halafu akajifanya kama kalala pembeni yake, akiwa na nia kuwa akimuona kapata usingizi anaondoka zake, lakini haikuwa hivyo, kila akipogeuza kichwa kumuangalia alimkuta shemeji yake macho yapo wazi lakini hayapepesuki ni kama yamefunuka tu na hata alipojaribu kupitisha mkono mbele yake kama vile atayapepesa, lakini alikuwa hivyo hivyo tu.
Huyu mtu halali jamani…mbona shida hii.. mbona yupo hivi, kama…ooh, ikifika subuhi cha kwanza kwa dakitari, hili sasa ni balaa….mungu wangu mtoto wa watu , nitasemaje…..’ akajikuta akisema mwenyewe na akajaribu kukaa macho wakati wote, alikuwa anakaa kwenye kiti, na wakti mwingine anasogea kitandani kukaa pembeni, na mwishowe akajikuta kajilaza kitandani pembeni na alipolala shemeji yake na usingizi ukamchukua…
********
Ilianza kitu kama ndoto, akajaribu kujizuia, lakini baadaye akawa anavutika na hamasa ikamshika na kuzifuata hisia zake, na hisia hizo zikambadili akili kabisa na kujiona kama mtu anayeelea kwenye bahari isiyoelezeka, juu ya maji ambapo huibuka na kuzama, lakini kwa mtindo wa aina yake, na jinsi muda ulivyozidi kwenda, na akili nayo ikawa haiona chochote zaidi ya raha isiyomithilikai, na hatimaye uzalendo ulimshinda,…. kilichotokea baadaye ilikuwa kama miujiza na baada ya heka heka ambayo kwake ilikuwa kama ndoto, ndoto ambayo aliiombea siku nyingi itokee hivyo, na muda huo aliombea ndoto hiyo iendelee tu, awe anagolea tu, awe anapiga mbizi nz kuibuka tu, hakutamani kabisa kufika ukingoni, kwani raha yake ni ya ajabu, lakini hatimaye mwisho ukafika, na ulifika kwa kasi ya ajabu na kutua ukingoni…oh kwanini nimefika ukingoni, siwezi kurejea tena nyuma, siwezi kuogelea tena, siwezi kupiga mbizi tena, ….akafungua macho yake..oooh, ina maana ni kweli , …. kilichotoeka baadaye ikawa kutahayari..mungu wangu sasa nimefanya nini, oooh, hili sasa ni balaa..mungu wangu imekuwaje nimeshindwa na udhaifu huu….nimevunja ile ahadi…
‘Ohh shemeji nisamahe sana, sijui imetokeaje kuwa hivyo…’ alijikuta akiongea , kwa wasi wasi ,lakini hakusikia kauli ya shemeji yake…shemeji yake alikuwa akihema kuonyeshga kuwa yupo kwenye usingizi mzito na sasa macho yake yalikuwa yamefumbwa, tofauti na ilivyokuwa usiku usiku…alipohakikisha kuwa kweli shemji yake kalala, akainuka kitandani, …..oh, nipo uchi…nilivua nguo saa nagapi, kabala hajapata jibu, akazitafuta nguo zake ambazo zilikuwa zimekunjamana na shuka zito walilokuwa wamejifunika, na akiogopa kumwamusha shemeji yake, akaziona na kuzivaa nguo hizo haraka, haraka huku akijuta kwa tendo hilo,…lakini hata hivyo hakumbuki kabisa kuwa alifanya vile kwa hiari yake mwenyewe…
‘Nani atakubali hilo,… kuwa kweli sikulifanya hivyo kwa hiari yangu, je kama sio kwa hiari yangu, ina maana shemeji….hapana, sikumbuki kunilazimisha’ akajikuta akiongea peke yake. Huku akitoka mle chumbani haraka haraka, alipofika chumbani kwake akakimbulia bafuni, alipomaliza kuoga, akatamani arudi tena kule chumbani kwa shemeji yake, lakini akaona haifai kufanya hivyo, akatoka na kukaa kwenye chumba cha mapumziko, ili kuhakikisha kuwa shemeji yake atakuwa hayupo katika hali mbaya, ya kuhamaki au ya furaha…kwanini iwe ya furaha, …anamua shemeji yake, singelipenda kabisa tendo kama lile, lakini ….hata mim sikupenda itokee hivyo…ngoa nimsubiri, ilii nimuone sura yake ya kwanza tukionana usoni nitajua hisia zake…akajisemea, huku akizidi kuwaza matukio mazima ya jana, hakuweza kuamini kilichotokea…na utashangaa, tukio la mwanzo la harati, halikuwa lipo kichwani mwa Manenoa tukio lile la hatari ambalo Maua alitoka usiku wa manane na kupotea maporini, yeye alikuwa akiwaza tukio lililotokea baada yake hakuweza kujua lilitokeaje…
Hivi ndivyo ilivyokuwa shangazi, nakuhakikishia kuwa sikutumia nguvu, sijui ilikuwaje, tulijikuta tupo tupo kwenye hali hiyo, nakuapia kwa jina mungu, sikumlazimsiha siku…mbaka….na hata yeye inavyoonekana hajui kabisa nini kilitokea, na hata alipoamuka yeye alijua ni ndoto, ila mimi nikamwambi akuwa kweli alitoka nje, …na alihakiki hilo baada ya kuona nguo zake kuwa ni chafu…, na baya zaidi sijui ni hisia zake au vipi anayemuhisi kuwa alimuokoa, anayemuhisi kuwa alilala laal naye ni Mhuja,…na ana uhakika kabisa na hilo, na hilo lilimfanya achanganyikiwe kabisa kuwa kweli kamuona Mhuja, ndipo nikaona tukiendelea kubakia kule linaweza likazuka zengwe….
‘Unajua Maneno sikuelewei mpaka hapo, kwani inavyoonyesha wewe huoni kuwa umefanya jambo baya sana, na unakumbuka tulichoahidiana siku ile wakati mnaondoka…mimi ni mtu mzima, nilishahisi kuwa una mipango yako kichwani, na ni vigumu sana chui na mbuzi kulala zizi moja, wakati chui ana njaa, na mbuzi ni mgonjwa, hana hata nguvu ya kujitetea…unaona lililotokea….umachukua uzaifu wa mwenzako, kuwa kachanganyikiwa, kuwa....ooh, masikini mwanangu Maua,mbona ana wakati mgumu sana,...sasa, kama nilivyokuambia awali na ukakiri mwenyewe kuwa ahadi ni deni…sasa….
Je shangazi atachukua hatua gani kwani ahadi imeshavunjwa…tuzi kuwemo….
NB: Sehemu hii ni ngumu kidogo, na nilipoiandika nilijikuta najiuliza mwenyewe je inawezekana kweli, lakini ndivyo ilivyokuwa imetokea,....sasa swali kweni wapenzi wangu, je kama ungelikuwa wewe ni Maneno ungelifanyaje, na kama ungelikuwa wewe ni Maua ingelikuwaje kwasababu mpaka hapo anaamini kuwa aliyekutana naye ni Mhuja, na je kama wewe ungelikuwa shangazi mtu, ungelichukua hatua gani...?
Ni mimi: emu-three
Friday, August 26, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-20
Ilikuwa jioni ya saa kumi na mbili wakati Maua na Maneno walipowasili Arusha, Manyara National park, na kwa vile walikuwa wamechoka kwasababu ya safari ya kutoka Dar, kila mmoja alikimbilia chumbani kwake ili kupata maji ya kuoga kwa kuondoa uchomvu wa safari, licha ya baridi iliyokuwepo muda huo, lakini maji ni muhimu ili kuuweka mwili sawa, na ikibidi kujipumzisha kidogo, waliahidiana kukutana baadaye ili kupata chakula cha usiku kabla hawajaanza kujua taratibu nyingine ambazo wenyeji wao waliwapangia.
Maua alipofika chumbani kwake taswira ya siku ile ya kwanza walipofika na Maneno ilimrudia tena, akaanza kuogopa, akaanza kuangali hukuna kule, alikuwa akitafuta kitu…hajui kitu gani, akaanza kukagua begi , lake,…lakini hajui nini anakitafuta…chupa, …mbona hakuna chupa kama hiyo, anatamani kufanya jambo, lakini akili haimtambuzi haraka ni jambo gani, moyo unamwenda kasi…natamani, natamani…..kujiondoa hapa duniani, …lakini hkuna kitu cha kunisaidia kujiondoa, …chupa ya sumu haipo, nitafute kamba nijinyonge…akawa anazunguka huku na kule, kichwa kinamwanga …kichwa kinamuuma…baadaye akagundua kuwa pale nje aliiona kamba, akacheka, akasema nimegundua kitu, kama siku ile nilishindwa kutumia sumu leo nitajaribu njia nyingine, akainuka kutoka nje, na alipofika pale kwenye meza kunapoweka runinga, mara taswira ya safari yao ya kwanza ikamjia kichwani, akasimama kukumbuka lile tukio, ilikuwaje siku ile ya safari ya kwanza..
*********
Siku ya safari yao ya kwanza walikuwa wamefika muda kama huu, muda wa jioni, na wakafikia hiyo hoteli Manyara Hoteli, ambayo walishawasiliana nao kabla, na walipata vyumba vinavyoangaliana, na Maneno alipohakikisha kuwa shemeji yake kaingia kwake yeye akaondoka kwenda kuongea na hawo wanaosimamia taratibu nzima za kwenda kuwaona wanyama. Kwani walipanga kuwa wakitoka hapo wanapitia na Ngororngoro National Park, …Maneno hakuwa na wasiwasi kabisa na shemeji yake, alijua kwa vile shemeji yake kachoka, basi akaifika kitandani ni usingizi kwa kwenda mbele, kwahiyo aliona ampe muda wa kupumzika wakati yeye anongea na hawo jamaa, na yeye akirudi atamtupia jicho mara moja kuangalia usalama , halafu na yeye atahitaji nusu saa tu ya kupumzzika kwake inamtosha kabisa, kwani alishazoea safari za mara kwa mara.
Huku nyuma Maua alijikuta moyo ukimwenda mbio, alikuwa kalifikiria sana jambo lake ambalo alilikusudia kulifanya, akaliendea begi lake na kulifungua, na akakipa kile alichokuwa akikitafuta, …alikitafuta kile alichokuwa akikitaka, kilikuwa chupa ndogo, chupa ambayo ilikuwa na dawa maalumu. Dawa ambayo kwake yeye aliivika jina la `mwisho wa matatizo’, Alipokipata kile kichupa akawaza hatua ya pili aliyoipanga kichwani, akatoka pale chumbani hadi meza varandani ambapo wanachangia na Maneno, kwani kulikuwa na vyumba viwili vinachangia sehemu ya kupumzika na kula, kujisomea nk, akafika hapo mezani, na kusema , hapa akipita shemeji ataiona hii karatasi ambayo alipanga kuandika ujumbe maalumu, akachukua kalamu iliyokuwepo hapo mezani na karatasi akaanza kuandika hivi;
‘Mimi ni Maua ninayeandika ujumbe huu’, akaweka saini yake, halafu aakendelea kwa chini yake
‘Ndugu zanguni, msije mkamshuku huyu shemeji yangu Maneno kwa kitendo hiki, nilichokichukua , kuwa labda ndiye kafanya hivi, hapana yeye hahusiki kabisa, huu ni uamuzi wangu mwenyewe, kwasababu nimechoka kuteseka , nimechoka kuvumilia na pia nimecjoka kuwasumbua, na ili kuondokana na haya ndio nimeamua kuchukua hatua hii….’
Kalamu ikagoma kuandika, alipoiangalia vyema akagundua kuwa wino umekwisha…akakumbuka kuwa katika begi lake kuna kalamu aliiweka na kitabu chake cha kumbukumbu …akaiendea huko chumbani kuichukua , aliitafuta kwenye bagi ikawa haionekani, mpaka akaamua kutoa vitu vyote kwenye begi na baadaye akaigunuda ikiwa imejificha kwenye kona ya begi.
Haraharaka akaichukua huku moyo ukimwenda mbio kwa jambo analotaka kulifanya, akatoka mle chumbani mbio kuelekea pale alipoiacha katarasi yake na ile chupa, alipofika pale akajikuta kashikwa na butwaa, akasimama akiwa kashangaa, kwani alimkuta shemeji yake kainama pale mezani anaisoma ile karatasi.
Maua akashikwa na butwaa, akabakia kasimama pale na kitu alichofanya ni kurudi kinyumenyume hadi karibu na mlangoni ili aweze kujiegemeza, kwanialishaanza kujisikia vibaya, alipojiegemeza kwenye mlango, akahema kwa nguvu, lakini hakuwa na cha kusema. Maneno aliinuka pale alipokuwa kakaka, na kumgeukia Maua, alipokutanisha macho ayke na ya Maua, uso wake ulikuwa sio ule uso wa Maneno anayemjuaa, alikuwa kabadilika, alikuwa siyo uso ulikuwa umekunjamana kwa hasira, na mdomo ulikuwa ukimcheza cheza, akitafuta neno gani alitoe kwanza. Alichofanya ni kuichukua ile chupa na kuyasoma yale maandishi yake, ambayo kuna maneno makubwa ya hatari, kuwa ile ni sumu kali, kwa ajili ya kuulia wadudu wabaya kama nyoka,na wengineo ni hatari kwa maisha ya binadamu, inatakiwa wakati unaitumia ambapo unachanganya na unga au maji, na alzimaa ukifanya hivyo uwe umevaa kinga mikononi….
Maneno alifungua kizibo cha ile chupa bila kujali yale masharti, akamsogelea Maua na kumwanmbia kwa hasira ‘ `Wewe si unataka kujiua, haya chukua kunywa yote, ..kunywa yote, haya kunywa, ufe, …amekufa rafiki yangu mkubwa Mhuja, sembuse wewe, …kwasababu wewe unachofikiria ni kuwa waliokufa wanafaidi saaana, haya kunywa…’ akamsogelea Maua na kumkabidhi mkononi. Maua aliishika ile chupa huku machozi yakimtoka, aliingalia ile chupa, na kuwaza, sasa anywe, au afanyaje….mikono ikaanza kumcheza, akawa kama anaisogeza ile chupa maeneo ya kichwa kama anataka kuinywa ile dawa, ….lakini mara chupa ikamtoka mikononi na kudondoka sakafuni, na mara Maua akayumba huyo akadondoka chini na kupoteza fahamu. Maneno alichofanya harakaharaka akaichukua ile chupa ya sumu na kuificha pembeni ya meza halafu….
‘Sijui ndio nimeua, lakini hakuwahi kunywa kama nilivyomwambia….ooh, kazi hii sasa…’ Akajikuta akihaha na kujiona kachanganyikiwa zaidi akazidi akijuwa kuwa Maua alishakunywa ile dawa kabla, na sumu inaonekana ni kali zaidi, na kwahiyo inabidi Maua awahishe hospitalini, au ni ile hrufu tu ya ile sumu alipoisogeza karibu na uso, hakumbuki vizuri kuwa aliifikisha puani au vipi, akajuta kwa nini alipaniki haraka na kumwambia maneno yale kuwa ainywe, na alifanya hivyo kama kumuonyesha tu kuwa alichofanya sio jambo jema…, akaona sasa kaua, … haraka haraka akakimbilia kule sehemu ya hotelini akanunua maziwa fresh, akarudi nayo kwa haraka, alipofika pale alimpomuacha Maua akamkuta hayupo, akaenda pale alipokuwa kaiweka ile chupa ya sumu, akaikuta haipo…mungu wangu, ina maana huyu mwanadada kaichukua kweli kaenda kujimaliza, …..
Akaingia chumbani hakuna mtu, …ooh, sasa ukisikia kuumbuka ndio huko, akaona heri akaiwafahamishe watu wa ile hoteli ilia pate msaada wa haraka, lakini kabla hajaenda mbali akaona arudi kuhakikisha kuwa kweli hayupo, maana akiwaambia walinzi ina maana kila kitu kitakuwa kimejulikana, na hakutaka kashifa kama ile iwepo na kusambaa, huwezi jua, hata waandishi wa habari wanaweza kuipata na kuiandika na matokea watazidi kumchanganya huyo binti, na alipoingia kwenye eneo la chumba chao akamkuta Maua Maua kakaa kwenye ile meza aliyokuwa kaiweka ile karatasi, na alikuwa kashika kijitabu chake cha kumbukumbu.
‘Sheemeji vipi , upo sawa kweli…?’ akauliza Maneno.
‘Nipo sawa, nilikwenda kuitua ile chupa ya sumu…niliogopa huenda umeenda kuwaita maaskari…nikaona heri niondoe huo ushahidi…’ akasema Maua.
‘Lakini shemeji tulishayaanngea haya maswala na kujua yamekwisha nini tena,….’ Akauliza Maneno kwa huzuni.
‘Hata mimi sijui shemeji kun kitu kinanivuta nifanye kile nisichokusudia, sijielewei kwakweli, na hii inanispa mashaka kuwa kumbe mtu unaweza kujiua bila kupenda…’ akasema Maua akiwa bado kachanganyikiwa.
‘Sasa sikiliza ni bora twende kwenye hospitali ya karibu tuone kama watatusadia kwa hilo..’ akasema Maneno.
‘Hapana sasa nipo kamili, ile hali imeondoka kichwani…nahisi kuna kitu kisicho cha kawaida, sio akili yangu…lakini nitajitahidi kuishinda hiyo hali..’ akasema Maua, lakini Maneno hakuwa nan a raha tena, hata ile hamu yote ya kuja kuona wanyama ilimuishia, lakini akajikaza na kuanza maneno yake ya kuchekesha hadi shemeji yake akatabasamu…
Hawakuongea sana, na baadaye waliitwa kuwa kuwa kuna safari ya usiku kwenda kuwaona baadhi ya wanyama, ikawa ni nafuu kwa Maneno, kwani hakujua jinsi gani atamlinda yule mwanadada, walitoka nje na kuanza kuupata ubaridi wa Arusha, ambao ulichanganyika na upepo mwanana unaotoka kwenye ziwa Manyara! Walitoka pale na kutembea kidogo kama utangulizi ili waone baaadhi ta wanyama, kama, pundamilia, na wengineo hawakutakiwa kwenda mbali zaidi kwani safari yao ilikuwa ni kesho ambapo wangeliweza kuwaona wanyama wengi na mengineyo, na hapo uso wa Maua ukaanza kung’aa.kwa furaha na moyoni akasema safari kama hii tulikuwa tumeipanga na marehemu mume wangu.
‘Kwa makadrio ziwa hili linakadiriwa kuwa kilometa 230 za miraba , ana mbuga yenyewe ina kadiriwa kuwa na kilometa za miraba 330, ikiwa na vivutio vizuri kwa macho ya wanadamu, watalii hufika kwa wingi kuangalia vivutio hivyo, licha ya wanyama kuna ndege wazuri, wadudu watambao, kama nyoka na jamii yake, kuna bustani za kuvutia, wanyama wa kila aina mutawaona, na pia kuna mabonde mazuri yaliyojipanga kwa mvuto wa aina yake!
‘Jina la mbuga hiyo lilitokana na neno la kimasai la `manyara'! Ambalo neno hili lina maana ya aina ya mmea, amboa hutumika kwa kuwalishia wanyama, ni chakula kizuri kwa wanyama , kwa kitaalamu nafikiri mmea huo unaitwa Euphorbia tirucalli! Pia ndani ya mbuga hiyo kuna miti mikubwa, maji yabubujikao na misitu minene, ambayo yote ni kivutio kikubwa sana kwa watalii….’ Akawa anaongea jamaa anayehusika na hifadhi hiyo, ambaye alisema yeye sio mhusika kamili, muhusika kamili watakuwa naye hapo kesho. Maua alifuatlia sana maeelezo hayo kama vile mwanafunzi asiyetaka apitwe na jambo, na kumfanya Maneno aanze kujisikia furaka kuwa angalau sasa shemaji yake kaanza kujirudi, maana alishaanza kutishika kuwa itakuwaje, huyu mtu, huenda ana sumu nyingine kaificha na usiku anaweza akajiuia,...
‘Upande wa kasikazini mwa ziwa hili la Mbuga hizi za Manyara kuna athari za volikano, na kuna maji yanayotiririka kutoka kwenye bonde la ufa! Na kutokana na kuwepo kwa maji maji ya mara kwa mara hali ya hewa ya maenao hayo ni kama mnavyoiona, upepo mwanana wenye ubaridi, na kama mnavyoona majani yanaoenakana ni ya kijani…!’
Baadaye walirejea kwenye hoteli ya Manyara na Maneno alimsindikiza shemeji yake hadi mlangoni mwa chumba chake, alitamani kuingi akukagua humo ndani kuhakikisha kuwa kuna usalama, lakini akasita kufanya hivyo, na Maua alipomuona shemeji yake akiwa na mashaka akaona umuondoe hofu akamwambia…
‘Shemeji usiwe na wasiwasi na mimi tena, unajua nilipowaona hawo wanyama na kuiona hali ya hewa ya hapa ilivyo kwakweli nilifarijika sana, nimegundua kitu kimoja kuwa kweli kufa kupo, lakini pia uhai unahitajika sana, na mtu wa kumtumania ni mungu, aliyeumba kila kitu, mtu utakufa lakini ni kwa siku zako, lakini sio ujiue, na sio umchezee mungu, angalia wanyama hawa wanavyoishi, wamechanganyikana, na wengine hukimbizana kuuana…nawaza sana na kujuta kuwa kwanini nilitaka kuchukua hatua kama ile ina maana nimeguka kuwa mnyama kujiua mwenyewe…najuta sana shemeji naomba unisamhehe na nawaomba msamha wote kwa jinsi gani nilivyowasumbua, na shemeji hili lililotokea hapa naomba liishie hapa hapa…’ akasema Maua huku akionyesha uso wa huruma, mpaka Maneno naye akamuonea huruma, hasa alipomuona machozi yakimtoka usoni, akatoa leso mfukoni, na kumbe leso aliyokuwa nayo niile iliyokuwa na tone la damu la siku ileee..! Amekuwa akitembea nayo kama kitu gani muhimu sana mfukoni mwake, alipogundua kuwa ndiyo ile leso akairudisha haraka mfukoni na kugeuka kutaka kuondoka akasema;
‘Sawa nimekuelewa shemeji, na nashukuru sana mungu kuwa hatimaye umeshaanza kurejea duniani, maana ulikuwa dunia gani sijui, jitahidi sana kuyasahau yote, ..ujue kuwa kuondoka kwa Mhuja sio mwisho wa dunia, wapo wengi wameondoka kabla yao, lakini dunia bado ipo, kwasababu hayo mambo mungu kayaweka ili yawe mitihani kwetu, hapa dunia ni kama mapito tu, kila mmoja yupo safarini, na kuondoka kwa mwingine inatakiwa iwe maandalizi kwa yule anayebakia ….’ Akaongea Maneno, akijarinu kutafuta maeno ya kidini yanaingia akilini.
Na kweli siku hiyo ikaisha salama, na asubuhi sana Maua aliamuka asubuhii na mapema na kujiweka tayari kwa safari na hata alipokutana na shemeji yake alishangaa kumuona anamkudolea macho, maana tangu mumewe Maua aondoke , Maua alikuwa kabadilika kupita kiasi, alikuwa hajipambi tena, alikuwa kaanza kuvaa ovyo ovyo, ..lakini leo akaonekana tofauti, Maua yule anayejulikana alianza kuchanua tena.
‘Leo shemeji umetoka bomba, mwanamke mrembo, na …..mmh, kila mmoja atapinda shingo kwa kukuangalia…’ akasema Maneno.
‘Acha utani wako shemeji, na jinsi nilivyokonda naonekana kama mwanamke wa miaka isiyo yangu…’akasema Maua akishika kwenye mifupa ya shingo
Maua kweli alikuwa mrembo, na leo aliamua kuvaa sweta jekundu na gauni jeupe refu, lenye mikono mirefu, na kichwani akaava kofia pana, utafikiri alikuwa akijifunika jua, sijui mwenyewe alikuwa na maana gani…
‘Unajua shemeji hizi nguo alininunuliwa shemji yako siku moja kabla hajaondoka, alitaka nizivae siku tukisafiri kuja mbuga za wanyama, aliwaona wazungu wakiwa wamevaa hivi ambao walituambia kuwa walikuwa wanakuja huku kwenye hifadhi za mbuga za wanyama, Mhuja alipowaona walivyokuwa wamevaa akapendezewa sana akasema siku hiyo nitakununulia nguo kama hizo, uonekane kama yule dada Muingereza alivyo vaa, akaninunulia kwa msharti kuwa nitazivaa siku ya safari yetu ya kuja huku kwenye mbuga za wanyama…sasa leo nazivaa kwa heshima yake…’ akasema Maua huku machozi ya kimlenga lenga.
Ama kweli Maua ni mrembo, kila kitu chake ni kizuri, hata vile alivyokuwa hajipendi alikuwa mzuri kwa jinsi hiyo, sasa ndio kajiweka kiurembo zaidi, basi hapo Maneno alijikuta mwili mzima ukimsisimuka, alibakia kumwangalia bila kummaliza, mwishowe akasema kimoyomoyo;
‘Ama kweli munguu anajua kuumba viumbe vyake, halafu ndio alitaka ajiue, si hata mimi ningejitundika….mmmh, nijitundike kwangu mimi haiwezekani, maisha yalivyo matamu haya…’ akaikuna kichwa.
‘Shemeji vipi naona macho hayabanduki kwangu, mpaka watu wanakushangaa unavyoniangalia…’ akasema Maua, na kumfanya Maneno ageuka kuwaangalia watu, lakini aligundua kuwa watu walikuwa wakimwangalia Maua kwa uzuri wake, wala sio yeye jinsi anavyo muangalia Maua, akatabasamu na kumsogelea Maua , ilimradi akae karibu naye ili watu wamuone kama yeye ndiye …mmh, mume wake…
‘Ahsane sana shemeji yangu kwa kunijali, isingekuwa wewe sijui ingekuwaje, ilishafikia hatua najiona kama bua, kama mfu , yaani anatembea kama roboti…lakini kwa juhudi zako sasa najiona mzima, nshukuru sana, na wla sijui nikulipe nini, mungu atakuzidishia heri na wema wako huo, najua siku ukimpata mwenzangu atashukuru sana kuwa kapata mume, wewe nakuona una upendo sawa na alivyokuwa mume wangu..’ akasema Maua wakiondoka kuelekea huko mbugani.
Moyoni Maneno alisema, `Sidhani kama nitaweza kumpata mwingine anaye fanana na wewe, namuomba mungu kuwa wewe unikubalie niwe tu uwe wangu…sijui kama utakubali ombi langu hilo…ooh, mungu nisaidie siku ikifika nikimtamkia tu , aseme nimekubali, sijui siku hiyo nitafurahi kiasi gani….`
‘Unikubalie mama weee, tatatatata, .
‘Mawazo yangu uyajue, tatatat…
‘Nisipate taabu kwa ajili yako weweee…’
Akajikuta anaimba wimbo huo kwa sauti, na kwa Maua hakushangaa, maana Maneno anapenda kuimba, halafu akianza kucheza, halafu kuchekesha…yaaani ukikaa naye ni raha kwa kwenda mbele..alkini hata kwa vimbwanga vyake vyote hivyo, Maua alikuwa kapooza,hadi siku za karibuni tu…na wakati wanatembea Maua akawa anamuwaza huyu Maneno kwa wema wake huu, akafikiria zaidi ya kufikiria, akikumbuka siku ile alipomsimulia kuwa yeye ndiye aliyekuwa wa kwanza kumuona kabla ya Mhuja na ndiye aliekuwa wa kwanza kumpenda kabla ya mume wake, ila bahati haikuwa yake…na hapo ile taswira ya siku ile alipomuona alipokuja kumtembelea kuja kumuona shemaji yake, akijua kuwa ni sio Maua anyemjua, lakini…!
***********
Siku ile Maua alikuwa kakaa chumbani, alikuwa anasubiri mume wake amuite waondoke kwenye safari hiyo waliyopanga, na akawa kajiandaa vyema kwa kuvalia nguo maalumu. Mara alisikia Mhuja akiongea na simu na alipomaliza akamuita kwa sauti kuwa kuna mgeni anakuja, kwahiyo watachelewa kidogo kuondoka, basi ikabidi ajilaze kidogo kitandani na wakati anasubiri mara akasikia sauti ya mtu akipiga hodi, na akaskia huyo mgeni akiongea na mume wake.
‘Kwanza nataka nimuone shemeji ..’
‘Kwanza nataka kuiona hiyo zawadi..’ ilikuwa kama mzozo, na akona amuone nani huyo anayezozana na mume wake kiasi kwamba inakuwa kama vurugu, akainuka pale kitandani na kujiweka vyema halafu akachukua hatua ndogo ndogo kutoka chumbani kwenda varandani, alikuwa kama anayemelea kuwaangalia bila wao kujua kuwa anawaangalia.
Alipotokeza kichwa tu, macho yake yakakutana na huyo mgeni, na mara akaona kitu cha ajabu, kwanza aliona aibu kujitokeza kabla hajaitwa, na hakutaraji kuwa ataonekana , lakini zaidi ya yote ni jinsi huyo mgeni alivyomkodolea macho, na alibakia hivyo kwa muda hadi Mhuja alipogeuka kuangalia kule mlangoni, akakuta mkewe akiwa kasimama huku akionyeshwa kukerekwa na jinsi anavyoangaliwa na Maneno, naa kwa vile Mhuja anamfahamu sana rafiki yake kwa vimbwanga vyake, akainuka na kumsogelea mkewe na kuanza utambulisho.
`Maneno huyu ndio shemeji yako , sina lakukuambia zaidi kwasababu macho yako mwenyewe na jinsi ulivyoshangaa imedhihirisha kuwa umemkubali…au sio’ akasema Mhuja akiwa kamshika mkewe kiuona na kutembea naye bega kwa bega..tete-a-tete, kumleta varandani, na Maua akiwa na aibu akawa anafuatana na mumewe had1 karibu na pale aliposimama Maneno akiwa bado kaduwaa, na macho yake yalikuwa hayabanduki kumwangalia.
Baadaye Maneno akajishitukia na kuanza kujibaragua kwa kusema; `Unajua Mhuja, umeniacha hoi, kweli wewe unajua kuchagua ,kweli wewe umenipiga bao, tena la kisigino, ….mmmh, shemeji usione ajabu, mimi na Mhuja ni hivi..’ akaviunganisha vidole huku bado alimwangalia kwa macho yasiyoaamini kuwa hicho anachokiona ni kweli au anaota…
‘Kweli asemavyo Maneno, mimi nay eye tumetoka mbali, toka chekechea hadi shuleni, chuoni hadi kazini..kwahiyo tunajuana na nakuomba ujaribu kumzoea kwani anaongea, unajua kuongea, basi huyu anaongea, hapa tu anaona aibu kwa sababu ni mara ya kwanza kukuonaa, lakini akianza mbwembwe zake utacheka, mpaka mbavu zitauma..’ akasema Mhuja, na Maua akajiuliza kama hapo huyo rafiki yake kaona aibu, je akiwa hana aibu itaakuwaje…maana yeye ahjazoea kukaa na mwanamue akawa akamchangamkia kiasi hicho, hawezzi kumpa nafasi hiyo, kwahiyo hapo alijionea taabu tu…
‘Rafiki yangu huyu anaongea kama kaseti iliyofunguliwa, na ukiwa naye huwezi kuchoka, maana anajua kila kitu…’ akasema Mhuja na kumuelekeza mkewe akae kidogo, na wakawa wanaongea mazungumzo ya kawaida, mpaka wakajisahau kuwa walikuwa na safari….
‘Maua mbona umeduwaa hapo kama….unanitisha au unataka kufanya kama siku ile….Maua akawa kaduwaa tu anaanglia ile kamba…huku anaomba Maneno aondoke, ili aweze kufanya lile linalimvuta kufanya hivyo…
Je ni kitu gani hiki kinamuandama Maua , kachanganyikiwa,...hata mimi sijui kwakweli ngoja tuone toleo lijalo, tuwepo pamoja. Samahanini sana kwa sehemu hii, inawezekana haijakaa vyema kidogo, kwani nimekuwa nikiiandika katika mazingira magumu, nilichelewa kufika ofisini, lakini nimekuwa nikiiandika kidogo kidogo kila ninapopata upenyo hadi hapo nilipofikia…natumai mtaielewa vyema,
******
Ni mimi: emu-three
Thursday, August 25, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-19
`Sweetie wako…., una maana gani kuita jina hilo, Sweetie wako…?’ akauliza Maneno, huku akiwa kasimama mbele ya kochi alilokuwa kakalia Maua. Maua akacheka na kulaza kichwa kwenye kochi huku akiwa kafumba macho kama anawaza kitu kwa mbali, na huku kwa kuwaza hivyo anajiona kama yupo mahali fulani, na neno hilo au jina hilo ndilo linalompa faraja fulani. Aliwaza mbali sana, akiwa analikumbuka hilo jina na chanzo chake.
‘Mume wangu, hivi niwe nakuita nani kama nataka kukuita kwa sauti, ukiwa mbali, nikuite jina lako,Mhuja au nkuite mume wangu, au baba nanihino?’ alikumbuka siku moja alipokuja mgeni, na wakati huo mume wake yupo chumbani, mgeni huyo alikuwa baba mkwe wake alipita kuwasalimia mara moja, sasa akawa anajiuliza amuiteje mumewe kwa sauti. Kwasababu ilikuwa siku za mwanzoni mwanzoni mwa ndoa yao, aliogopa kumuita `mume wangu’ mbele ya mgeni, na kuinuka pale kumuacha mgeni peke yake akaona sio adabu…na bahati nzuri mumewe akatoka nje na kuwakuta baba yake akiongea na mkwewe. Na mgeni alipoondoka, ndipo Maua akamuuliza mumewe, awe anamuita jina gani kwa sauti.
‘Wewe ulitaka jina gani, mimi nitakuita Sweetie na wewe utaniita nani?’ akasema Mumewe
‘Sweetie, ….mmh, mbona jina hilo halifai kuitwa mbele za watu, hilo linafaa kuitana chumbani…” akasema Maua.
‘Chumbani au hadharani kwa mume na mke haina tofauti,mimi na wewe tumeshahalalishwa, hakuna cha kuoneana aibu, kwanza kuniita `mume wangu’ ingelitosha tu kabisa, maana hicho ndio cheo change halali mbele ya mungu na mimi nikikuita `mke wangu’ inakuwa imependeza zaidi, au sio lakini kwa kuonyesha kuwa nakupenda zaidi ya kupenda, na pendo la zati, lenye raha ya ajabu, basi mimi toka leo nitakuwa nakuita `Sweetie’ na wewe utatafuta jina la kuniita…’ akasema Mhuja na kuja kukaa karibu na mkewe, na mkewe akalaza kichwa chake mapajani mwa mumewe.
‘Hata mimi nitakuwa nakuita hivyohivyo…ingawaje jina lenyewe limekaa ki-kike-kike..’ akasema Maua, huku moyoni akimshukuru mungu kwa kumpa mume anayeonyesha kuwa kweli anampenda kizati, hatajaii kuwa kutakuwa na mabadiliko yoyote, akimuomba mungu amsaidie waishi hivyohivyo milele na milele, kwani akiwa karibu na mumewe huyo anajion kama wapo peponi. `Kweli ndoa ina raha yake na hasa mnapokutana wawili mnaopendana na mkajuana nini mwenzako anakitaka!’ akajikuta akiyasema yale maneno kwa sauti ya chini.
`Umenena kweli Sweetie…’ akasema Mhuja huku akichezea nywele za mkewe,
***********
Maua likuwa mbali sana akikumbuka chanz cha ina hilo na ndipo akamwambia Maneno ‘Unaniuliza kwanini nimetamka hilo jina Sweetie, wakati umenipiga marufuku nisiwe nazungumza au kukumbuka mambo yangu yaliyopita, jina hilo ni muhimu sana katika maisha yangu na nikilitamka hilo najisikia faraja sana, na namkumbuka sana mume wangu,…naogopa hata kutanguliza neno `marehemu’ ninapomtamka mume wangu, na sipendi watu wakitanguliza neno hilo, ila nashindwa kuwazuia tu, kwani namuona kama bado yupo hai…siuji kwanini nahisi hivyo…Sweetie ndilo jina lake nililokuwa nikimuita na yeye pia alikuwa akiniita hivyo hivyo….hatukujali kuitana hata mbele za watu, tangu siku ile tulipopeana majina hayo…mpaka watu wengine wakadhani andilo jina langu...’akasema Maua huku akiwa bado kafumba macho.
‘Mhh, Maua, Maua…kwahiyo inavyoonyesha hapo ulipo upo na Sweetie wako kimawazo, ngoja niondoke, maana wewe na Sweetie wako hamuachani, …’ Akasema Maneno nab ado akiwa kasimama mbele ya Maua. Maua akafumbua macho na kumtizama Maneno kwa muda. Maneno alikuwa katizama dirishani na kuendelea kusema `Nimeshakuambia kuwa ili uishinde hiyo dhamira achana na mawazo hayo kwasababu hayo yapo nje ya uwezo wetu wa kibanadamu, tumeambiwa kuwa, mpende umpendaye, lakini ipo siku mtatengana naye, ama yeye au wewe, mmojawapo atatangulia, na penda uyapendayo,iwe mali au umasikini, lakini ipo siku utayaacha…kwahiyo licha ya udhaifu wetu, unyonge wetu wa kujipa moyo na kukubali hayo, lakini ndivyo hali halisi ilivyo…..’ akasema Maneno na kumsogelea Maua akamshika miguu yake miwili kwa mikono yake huku akimwangalia usoni.
‘Maua hata kama Mhuja kaondoka duniani, sio mwisho wa upendo, sio mwisho wa maisha, wapo watu wanakupenda sana kama alivyokuwa akikupenda Sweetie wako.Kwahiyo nakuomba uuachie mlango wa upendo wazi ili aweze kuja mtu mwingine,…’ akasema Maneno huku akimwangalia Maua usoni, na Maua akawa anamwangalia Maneno kwa macho ya kutahayari, kama vile haamini maneno kama hayo yangetoka mdomoni mwa mtu kama huyo. Huyu ndiye rafiki mkuu na alikuwa kama ndugu wa Mhuja, leo yeye anaoenekana kama kamsahau…hapana. Akatamani kuinuka na kukimbilia chumbani, Lakini baadaye akaguna na kukiri moyoni kuwa kuna ukweli ndani yake, hivi ataombeleza mpaka lini, mwaka na kitu sasa, na hata kama ataomboleza hadi mwisho wa maisha yake ndiyo itakuwa nini…akasogeza mikono yake na kuishika mikono ya Maneno kwenye viganja, na kusema;
‘Ahsante sana kwa kunijali shemeji, nimeamini kuwa wewe ni rafiki wa kweli…’ akatabasamu
Hii ilikuwa hatua kubwa sana kwa Maneno kuweza kumsogelea shemeji yake, hata kuweza kumgusa shemeji yake, ilikuwa ni kitu ambacho hakukitarajia kabisa, na siku aliyoweza hata kumkaribia ni baada ya kutoka naye kwenye mbuga za wanyama, aliona kuna mabadiliko makubwa sana na aligundua kuwa Maua anapenda sana wanyama, na akaona hiyo ndiyo itakuwa dawa nzuri ya kumrudisha kimawazo duniani. Alikuwa keshapanga safari nyingine ili kuweza kumsaidia zaidi shemeji yake, safari ya kwenda tena kwenye mbuga za wanyama. Na safari hii alikuwa kaipanga kuigharamia mwenyewe…na wakati.
Unajua Maua mimi na mhuja ni kama mtu na ndugu yake, ingawaje yeye anatokea milimani mimi natokea Pwani, lakini tulikuwa kama wanandugu waliozaliwa tumbo moja, nilimjali sana kama alivyonijali mimi, ndio maana hata akisafiri hana wasiwasi na mimi. Kuondoka kwake ni pigo kwangu pia mimi, kwani mambo yangu mengi yanakwama, alikuwa msaada mkubwa sana kihali na kimawazo, na nilimuahidi kuwa familia yake ni yangu, ingawaje mimi nimechelewa kuoa, lakini tulikuwa tukisema kuwa watoto wake ni wangu…na mke wake…aaaah’ malizia basi shemeji’ akasema Maneno kwa utani
‘Hiyo siwezi kumalizia, kuwa mke wake ni mke wako…haiji hata kama ni ndugu, hata kama ni mrafiki hiyo haiji, mke wake ni shemeji yako…hapo imekaa sawa’ akasema Maua.
‘Hapo imekaa sawa, nakubaliana na hilo, ila tuliahidiana kuwa hata kama ni miradi akiwa hayupo mimi naiendeelza, kwahiyo mimi nachukua jukumu hilo la kuendeleza kila kitu alicho kiacaha, ili uwe na amani, ….hilo nakuahidi shemeji, utaishi kwa amani hadi hapo utakapomupata mwenza utakaye mkubali moyoni mwako..’ akasema Maneno huku moyoni akitamani Maua aseme mwenza wangu ninayemkubali hayupo zaidi ya wewe…
‘Unajua Maua mimi ndiye niliyekujua kabla ya Mhuja, na aliniwahi kibahati –bahati…’ akasema Maneno.
‘Ushaanza visa vyako, ulinijuaje hata mimi nisikujue…’ akauliza Maua
‘Mimi nitakukumbusha ilivyokuwa, unakumbuka siku moja kwenye supermaketi moja ambayo ni ya kwanza kufunguliwa pale Kariakoo, uliwahi kudondosha vitu ulivyonunua na ukavunja chupa ya chai…?’ akauliza Maneno, na kumfanya Maua acheke, kwani ilikuwa kitambo sana, na tukio hilo lilimkaa sana kichwani, akasema `Kwanini nisikumbuke tukio kama hilo…’
‘Ni nani yule aliyekusaidi akuokota vifaa vyako na kuviweka kwenye kapu, na ulipojaribu kuichukua ile chupa ukaikata na kipande cha ile chupa ya chai, na akatoa kitambaa chake kukufuta kidole chako..? akauliza Maneno, na hapo akatoa leso ikiwa na doa dogo la damu, kumuonyesha Maua. Na maua kumbukumbu ikamjia lakini hakumbuki kabisa kuwa alikuwa huyu shemeji yake, na ndipo Maneno akaanza kumhadithia jinsi alivyomjua.
***
‘Maneno mwenetu sasa umeshakua lakini unatupa wasiwasi sana, wadogo zako wote wameshaoa, lakini wewe siui ndio huo usomi wako, hutaki hata kutuletea mwanamke wa kudanganyia, una nini mwanetu..’ akamuulizia mjomba wake.
‘Mjomba mbona leo unanigeuka, ulishatuambia kuwa uhuni ni mbaya, hasa uzinzi, na ulituasa kuwa hutaki katika familia yetu watu wapate watoto bila ndoa, na mimi nafuata masharti yako, nataka nioe kihalali na wewe uwe mhusika mkuu…hilo ndio lengo langu, lakini sijampata nimtakaye…’ akasema Maneno huku akimkumbuka binti mmoja ambaye anamuona mara kwa mara akiwa anatoka kazini, binti huyu anaonekana anasoma, lakini sio shule za sekondari, huenda anasomea kozi fulani.
Akawa anmfuatilia kwa karibu sana, hadi akagundua kuwa ni mtoto mwenye adabu sana, licha uzuri aliojaliwa nao, lakini kiliongezeka kitu kingine kikubwa cha heshima na adabu. Aliahidi kuwa huyo ndiye anayemfaa kuwa mke wake... Akamwambia shangazi yake ajaribu kumsaidia kwa kumchunguza kwa makini, lakini alimuomba sana asije akamwambia kuwa analengo gani, kwani kama watagundua badaye kuwa hafai wasije wakamuumiza kiakili.
Kweli shangazi yake alifanya kazi hiyo, lakini kabla hajaimaliza akapata safari ya kwenda mikoani, kwahiyo hilo zoezi likasimamishwa kwa muda. Lakini yeye mwenyewe hakuchoka kumfuatilia, ila cha ajabu kila mara anapotaka kukutana naye angalau kumsalimia anakutana na kikwazo fulani, moyoni akasema hana haraka sana naye, siku itafika tu kama anamfaa atahakikisha anampata kuwa mkewe…hakupenda kufanya makosa kwa kumpata mtu wa maisha yake.
Shangazi yake akarudi, na akapewa maagizo kuwa sasa anaweza kumuunganishia maana , muda wa Maneno ni mdogo sana, na kila anapopata muda kama huo, anakuwa hafanikiwi, kinazuka kikwazo fulani, kwahiyo akamuomba shangazi yake ahakikishe anakutana naye, na ipangwe siku waonane na Maneno…`shangazi mimi kama nilivyowaahidi nitafuta mila na desturi zenu moja baada ya jingine,sitapeleka mambo kisasa-sasa…’ akamwambia shangazi yake.
Shangazi yake alipofika kwa huyo binti alikuta sura mpya, akauliza hakupata jibu la kumfurahisha, wanasema huyo mtu alikuwa mpangaji, na ameondoka, na hakuna anayejua kahamia wapi…ikabidi arudi kumfahamisha Maneno, na Maneno hakuamini akaenda mwenyewe na kupata jibu hilohilo,akauliza kila mtu anayeishi kwenye nyumba hiyo, lakini hakuna aliyeweza kujua wapi alipohamia, ikawa pigo kwa Maneno. Shangazii yake akamwambia kuwa asijali, inawezekana hakuwa bahati yako,tutapata mwingine bora zaidi yake. Lakini kwa Maneno ikawa haiwezekani, hakuona anayefanana naye, hakuna ambaye atachukua nfasi hiyo.
Na siku moja Maneno akiwa anapita kwenye supermarket moja hapo Kariakoo, akiwa na nia ya kununua baadhi ya vifaa,na akiwa kasimama kwenye fremu moja iliyopangwa vitu , akavutiwa na sura ya amsichana aliyesimama upande wa pili wa hiyo fremu, sio kuvutiwa tu, ila moyo wake ulishikwa na mshituko, oooh, sio yule binti kweli…sio Maua kweli, kwani alikuwa keshamjua hata jina lake. Akaacha kuchagua vitu na kuanza kumfuatilia nyuma huyo binti, ili apate nafasi ya kumuongelesha, na huku akisema kimoyomoyo, kama ndio yeye, basi leo kitaeleweka, lazima aongee naye na ajue wapi walipohamia, ili kila akipata nafasi amtembelee, na aliomba sana awe hana mtu aliyemuwahi. `Lakini binti mzuri kama huyu sidhani kama hajawahiwa…hata kama kawahiwa, ujanja ni kupata sio kuwahi..…
Wakati anamfuatilia mara yule binti kwa bahati mbaya akawa kama kajikwaa akiwa kabeba kapu la vifaa alivyokuwa kanunua, siunajua tena viatu alivyokuwa kavaa huyu binti vilikuwa na visigino virefu vilivyo, ukikosea unaweza ukaaumbuka, basi yule binti akajikuta analiachia lile kapu kujihami, na kumbe kwenye lile kapu kulikua na chupa ya chai, iakw aya kwanza kutoka na ikawa imechomoka kwenye boksi lake ambali lilikuwa hakijafungwa vyema na kudondokea sakafuni,…yule binti kwa kiwewe akaifunua ile chupa harakaharaka kuikagua kuwa ipo nzima na wakati anaitingisha tingiosha vichupa vilivyokuwep ndani vikamwangika, sakafuni, na sijui ni kwasababu ya uwoga,akawa anavizoa kwa mkono ili kuvirudidhia kwenye ile chupa, ingawaje ilikuwa ni ajali tu..
Maneno alishafika karibu yake, yeye akakimbilia kuokota vitu vingine na kuvirudiha kwenye lile kapu, na alipogeuka akamuona Maua kashika kidole kinavuja damu, harakaharaka akatia leso yake na kukifunga kile kidole,ili damu isivuje, na wakti huo wahudumu walishafika kutoa msaada.
‘Vipi umeumia binti, pole sana, ni ajali tu usiwe na wasi wasi tutaangali atutakavyosaidiana , hebu tuone kama umeumia tukakupake dawa…’wakasema wale wahudumu na mara akaja mama mmoja ambaye alionekana ni shangazi wa Maua kujua nini kimetokea na walipojielezea, wakachukuana na kuelekea sehemu ya malipo, na Maneno akawa nafuatilia nyuma, wakati huo kesharudishiwa kitambaa chake, na kila akitafuta upenyo aongee na hiyo huyo binti akawa haipati kwani shangazi yake alikuwa naye sawia.
Na mara Maneno akasikia naitwa kwa nyuma alipgeuka akakuta ni rafiki yake Mhuja, akampungia mkono kuwa anakuja, halafu akageuka kumwangalia ndege wake wa fahari, lakini alijikuta anaangaliana namhudum wa pale sokoni. Akatizama huku na kule hakumuona Maua wala shangazi yake, ikalaani bahati yake hiyo maana haui wapi wanaishi sasa na hakupata hata nafasi ya kuongea naye , kwahiyo ikawa umetoka tena.
‘Duuh, nina bahati mbaya sana ….aah, ndege wangu mrembo kaondoka…’ akajikuta akilaani na rafiki yak akaja na wakaondoka, hakusema lolote, na wala hakumuhadithia rafiki yake Mhuja, kwani hilo swala alitaka liwe siri na aje kumshitukizia rafiki yake huyo.
‘Vipi mbaona upo hivyo, unaonekana huna raha, kuna nini kimetokea?’ akamuuliza Mhuja.
‘Hakuna kitu,kuna ndege nilikuwa namfuatilia, ili ikiwezekana nimweke kwenye kiota changu , lakini karuka….yaani siju nitamata wapi maana msitu ni mnene ajabu…’ akasema Maneno.
‘Wewe na mfumbo yako ya Pwani bwana hata sikuelewi, ndege , au mtu…kama ni ndege mtu wapo wengi, utapata mwingine, ipo siku, na …hili liwe shindano, ni nani atawahi kuoa, ukishinda wewe nitakupa zawadi na nikishinda mimi utanipa zawadi. Sijui tupange zawadi gani..?
‘Zawadi ni zawadi tu, haina haja ya kupanga, mimi naahidi nitakupa bonge la zawadi…’ akasema Maneno akijua kuwa ipo siku atampata huyo binti, na atakuwa kamshinda rafiki yake. Na siku zikaenda hakuwahi kabisa kukutana na huyo binti,alitafuta Dar nzima, kila kona, lakini hakumuoma Maua na wala familia yao, inakuwa kama vile walikuja mara moja na kurudi huko mbali kusikojulikana, na hata pale walipokuwa wamepanga awali walidai kuwa hawajui hawo wapangaji walihamia wapi. Maneno akakata tamaa, na ikawa malengo kumtafuat mtu mwingine, lakini kila aliyempata ikawa analinganisha na mrembo huyo aliyeyeyuka, anakuta hamfai. Masiku na mwaka ukakatika.
Siku moja Maneno akiwa karudi toka safari za mikoani, rafiki yake alimjia na kumpa taarifa kuwa keshapata mtu anayetaka kumtambulisha kama mchumba…! Maneno akaruka kwa furaha na kusherehekea utafikiri mchumba huyo ni wa kwake yeye. Akamuuliza Mhuja `Ni yule yule msichana uliyesema mlikutana naye kituo cha basi, uliyemuokotea kitabu chake cha kumbukumbu…?’
‘Ndiye huyo, tatizo lako kila nikikualika uje tukamuona, unakuwa hukamatiki, lakini nilifanya utafiti wa kina na sina wasiwasi naye, hata wewe mwenyewe ukibahatika kumuona, utanisifia…nakuhakikishia hilo…sasa kwa ujumla nimeshalifikisha kwa wazazi na wao wamelipokea kwa mikono miwili, iliyobakia ni taratibu za kawaida, …’
‘Safi sana rafiki yangu, ina maana sasa umeniwahi, kwahiyo utanidai zawadi, au sio, lakini usihakikishe moja kwa moja, naweza nikampata wangu chapu chapu nikakufunga mabao…huwezi jua’ akasema Maneno.
‘Yote ni heri, kiukweli umri wetu ni wa kuoa, haihitaji kuchelewa zaidi, tatizo linakuwa ni nani anayefaa, kwani wakuoa wapo wengi, lakini swali kubwa ni nani atayekubalika moyoni, ni nani mke mwema, …’ akasema Mhuja.
‘Kama ilivyo kwa wanawake kuiuliza je ni nani mume mwema….ni kazi kubwa hiyo…’ akasema Maneno, na kuongezea kusema `Kwakeli rafiki yangu nimefurahi sana kusikia habari hii..unajua ssiku ile uliponielezea, wakati nina mafikara ya ule mzigo uliopotea, nilikuwa sikuelewi, maana mimi pale nilijua kazi sasa basi, kwahiyo nilikuitikia tu, kumbe mambo yameiva, sawa, tutakuwa pamoja, …hata ikibidi kuomba ruhusa, ingawaje nafasi hii niliyo nayo sitaki kuichezea, siunajua tena safari ndio inatufanya tusihi hapa mjini, mshahara mdogo, lakini ukipata marupurupu ya safari ukayabanabana unafany ajambo la maendeleo..’ akasema Maneno.
‘Ni kweli, mimi na familia yangu tumejipanga vyema, hutaamini kuwa hatukuhitaji hata michango ya watu, hilo swala lilipofika kwa wazee, huyu kaahidi ng’ombe, yule mbuzi, yule mchele, ….yaani mwisho wa siku kila kitu kimekamilika,…tukaona haina haja ya kuitisha vikao, kuwasumbua watu, cha muhimu ni kuwapa kadi za mualiko tu…kwahiyo siku ikifika utapata kadi yako , maana sasa tunachofanya ni zile taratibu za awali, kuna kupeleka barua, …’ akasema Mhuja kwa furaha.
‘Mhuja wewe tumetoka mbali, shule na sasa tupo kazini sehemu moja, na siwezi kukutupa kwa hiko, mimi nitakupa mchango wangu kwa ajili ya maandalizi yako binafsi, na ….usfikiri nimesahau ile ilikuwa ahadi ya kweli, kuwa atakayewahi kuoa,lazima apewe zawadi,…lakini zawadi hiyo nitakupa baada ya ndoa, maana mimi badi nafukuzia, naweza nikakuwahi…’ akasema Maneno akimuwaza yule binti aliyemuona ambaye sasa kayeyuka kama barafu, lakini bado alikuwa na matumaini labda ipo siku atakutana naye tu.
Basi wakaachana na siku moja wakawa wapo pamoja tena, Maneno siku hiyo alikuwa kapumzika nyumbani kwake na kama walivyo kawaida yao, siku Maneno yupo nyumbani hana safari wanajikuta wapo pamoja kama mapacha, wakijadili hili na lile, walishazoeana tangu wakiwa shuleni, wakawa wote chuoni, na sasa wamejaliwa kufanya kazi sehemu moja,…na siku hiyo Mhuja alikuwa na jambo zito la kumwambia mwenzake;
‘Maneno naona leo upo huna safari za kikazi maana tangu nikuambie nimepata mchumba, umekuwa mtu wa safari kiasi kwamba, hata siku moja sijawahi kukutambulisha kwa huyo mchumba wangu, na sijui kama utamjuaje na wewe miguu yako haitulii. Unajua sikutaraji aitakuwa hivyo, wewe ni zaidi ya ndugu yangu, lakini hili swala langu limkuwa la kivyangu na familia yangu, inakuwa kama nimekutenga, sasa leo nataka ushiriki kwenye safari ya kupeleka barua…, leo hata kama ipo safari itaahirishwa tu…’ akasema Mhuja.
‘Kiukweli, Ipo safari, lakini sio mapema sana,…siunakumbuka kipindi hiki mizigo mingi sana,…bishara yetu imekubali, siunaona mwenyewe kwenye mahesabu huko…na safari hii wasiponipa bonsai, tutaelewana vibaya…. Unajua wakati mwingine nawaonea wivu nyie wahasibu, nyie muda mwingi mpo ofisini, na mnasafiri mara moja moja sio kama sisi, lakini najua hivi karibuni utaanza kusafiri, maana wewe utahusika kwenye ufunguzi wa matawi mapya huko Bukoba na Mwanza, kwenda kuwasimika wahasibu wa kanda za ziwa…’ akaongea huku bado akiwaza mengi akilini, lakini kwa vile yeye ni mtu wa maneno mengi, alijifanya hana kitu moyoni, akasema tena ‘Mimi ni mtu wa masoko na mauzo, na unajua masoko na wateja vitu hivyo katika ofisi yetu havipatikani kwa kukaa ofisini kama nyie wahasibu, …lakini tupo pamoja ndugu yangu, usijali sana, hata mimi inaniuma sana, ila leo nitawasindikiza watu wanaopeleka barua,ili angalau nimuone huyo mrembo wetu, ulisema jina lake nani vile..
‘Anaitwa Maua..’ akasema Mhuja
‘Wee,…mamama… unasema anaitwa nani, …?’ akauliza kwa mshangao, halafu akaficha ule mshangao wake akasema kwa utulivu `Umesema anaitwa Maua, ooooh, jina zuri, lakini mbona imetokea sawa na mtu ninayemfahamu…isije ikawa ndio huyo mtu ninayemfahamu, lakini yeye alishahama hili jiji..anaishi wapi sijui, kwani huyo Maua wanaishi wapi na familia yao…?’akauliza Maneno na kabla hajajibiwa wakafika watu wa msafara wa kwenda kwa binti, mchumba wa Mhuja. Hawakupata nafasi ya kuongea tena, maana walikuwepo wageni maalumu na muda ulikuwa mchache, na msafara wa kupeleka barua ukaondoka, bila ya Mhuja.
Wakafikisha ile barua, na waliwakuta wanaume tu, wakauliza vipi mbona hakuna wanawake, wakaambiwa wanawake hawakubahatika kuwepo kwasababu kuna shughuli nyingine ya kifamilia na wao kama wahusika wakuu walitakiwa kuondoka, lakini kwa sababau ya hiyo barua waliona wagawane majukumu, ila wao baada ya hilo tukio wataondoka kueleeka huko kwenye hiyo shughuli. Waliendelea kusema kuwa kwasababu ni barua tu, itapokelewa, na siku nyingine wataikuta familia nzima na watapata nfasi ya kumjua kila mtu muhimu kwenye familia. Na baadaye Maneno akaondoka kuwahi safari ya kikazi hakurudi haraka, na aliporudi safari yake hiyo alikuta mambo mengi yamekamilika, na siku ya harusi imeshafikia, kwani harusi hiyo haikutakiwa kuchelewesha kwa makubaliano ya familia hizo mbili.
Siku ya harusi ikafika na hapo walikuwepo wanafamilia wote, ndugu jamaa, na majirani, akiwemo Maneno, ambaye alikuwa mmoja wa wapambe, hakuwa mpambe mkuu, kutokana na majukumu yake, alikuwa msaidizi wa `mpambe mkuu wa bwana harusi’ kama itakuwa nilazima, lakini muda wote akili ya Maneno ilikuwa ukiwaza mengi kumjua huyo Maua. Alikuwa akijiuliza, ni yuleyule Maua anayemjua yeye au ni majina tu yanafana, na kila mara alijipa moyo kwa kusema kimoyomoyo kuwa sio yeye, mbona hajabahatika kumuona angalau yule shangazi yake anayemfahamu kwa sura akiwemo kwenye hizo pilika pilika. Mbona hakuna hata sura anayoifahamu, aliyowahi kuiona siku alizokuwa akimfuatilia huyo Maua, ina maana kweli chelewachelewa imemkuta mwana sio wa kwake tena…haiwezekani
‘Kama atakuwa yeye sijui nitachukua hatua gani, nashindwa hata kuelezea,…’ Akawaza huku akikuna kuna kichwa, halafu akaendelea kuwaza kwa kusema ’ Kama atakuwa ni yeye kwakweli nitateseka sana, lakini hata hivyo siwezi kumweleza rafiki yangu lolote, maana namjali sana rafiki yangu, nitajifanya sijui lolote…’ akajisemea moyoni. Huku akiwa anawaangalia watu walivyo na shauku ya harusi hiyo, huku akiwazia kuwa anatamani ingelikuwa ni yeye `mtarajiwa’ na hapo anasubiri kukutaa na Maua anayemfahamu…’Lakini kila kitu na wakati wake, najua Maua wangu yupo ananisubiri, atakuwa sio yeye bwana…’ akajipa moyo.
Ikawa ndio kila mtu anajiandaa kueleeka huko kwenye harusi na mara simu ikaja kuwa Maneno anahitajika haraka kwenda ofisini kuna mzigo umefika na yeye anatakiwa kwenda kuukagua,karibu apasuke kwa hasira, lakini hakuwa na jinsi kwani kazi ya watu ni dhamana kubwa,ikabidi amwelezee rafiki yake kuwa imetokea hiyo dharura, na kwa vile rafiki yake anajua , akamwambia asijali aende akawajibika, kama atamaliza haraka asiache kufika, alimwambia hata ukimaliza usiku wewe njoo tu, wakaishia kucheka, na kuagana kwa kupeana kila-laheri kwa shughuli njema. Akaondoka akiwaacha wenzake wakimwaga kwenye magari kuondoka, na bahati mbaya hakuweza kurudi kabisa kuhudhuria hiyo harusi. Na kesho yake akasafiri kwani mzigo uliofika ulikuwa na kasoro, kwahiyo yeye kama mhusika mkuu alitakiwa kwenda kufuatilia kwanini imekuwa hivyo. Alirudi baada ya siku tatu…
Maneno alimpigia simu rafiki yake kumpa hongera na kumuomba amsamehe kwa kutokuwepo kwenye harusi, ingawaje wote walijua kuwa ni sababau ya majukumu ya kikazi kwani wote wanafanya kazi kwenye kampuni moja, na kila mmoja anajua nini kinachoendelea, kwahiyo wasingeliweza kulaumiana, hata siku nyingine Mhuja humuonea sana huruma rafiki yake jinsi gani anavyopigika kwenye kazi, kwani katika nafasi yake ya kazi anakuwa hana ratiba yak wake binafsi, inaweza ikavunjwa wakati wowote, anaweza kuitwa hata usiku wa manane kama kuna mzigo ulioingia usiku huo. Rafiki yake huyo akamwambia anakuja mara moja kumuona shemeji yake…na kimoyomoyo akawa anasema `na kutoa ile zawadi niliyokuahidi.
‘Hata kama mpo fungate, mimi lazima nimuone shemeji yangu…’ akasema Maneno
‘Wewe ndio mimi, usijali, njoo haraka, tunakusubiri, kwani kama kuna mtu nilyemsimulia kuwa kukosekaa kwakwe kwenye harusi yetu ni pengo kubwa sana ni wewe…sijui kwanini imetokea hivyo, lakini yote ni heri, hatuwezi kulazimisha kile kisichowezekana….njoo haraka maana tulikuwa tunatoka mara moja, lakini tutakusubiri…’ na baada ya muda Maneno akawasili. Alipofika alimkuta Mhuja yupo varandani anaangalia runinga, binti harusi alikuwa ndani, na Maneno akawa kasimama mlangoni huku anatabasamu, alikuwa akitabasamu kwani anajua anadaiwa zawadi, na zawadi ilikuwa `surprise’…ya kushutukizia.
‘Kwanza nimuone shemeji….’ Akanong’ona Maneno
‘Kwanza naitaka zawadi uliyoahidi…’ akasema Mhuja kwa sauti ile ya kung’ona...
Oooh, sijui kipi kitatangulia na nini kiliajiri tuwepo karibuni
NB:Samahani kwa kuadimika kwa siku mbili, ni mambo yaliyokuwa nje ya uwezo wangu, lakini tupo pamoja, na nilipata bahati ya kuhojiwa na Blog ya Tanzania Blog awards, kama unataka kunijua vyema, basi tembelea hapo usome; http://www.tanzanianblogawards.com/2011/08/mwanablogger-wa-week-hii-emu-three.html
Ni mimi: emu-three
Wednesday, August 24, 2011
Blog mpya ya IT
YES WE CAN!
www.it4dev.blogspot.com/
Blog itakayoleta mapinduzi ya kitekinolojia na changamoto kubwa ya maendeleo ya taifa.
Wataalamu na wajuzi wa nyanja mbalimbali sasa ndio wakati sahihi kuchangia maendeleo ya jamii yako.
Your knowledge and experience can bring about changes we always believe in. If you think you are one of the smartest people the country and your society is crying for and would like to become one of the authors to post and analyze different topics please send your email and your profile to:
editorit4dev@gmail.com
Our Aim is to become the Center of Excellence for all IT matters.
TOGETHER WE CAN
Ni mimi: emu-three
Monday, August 22, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-18
‘Unauhakika na unalosema Docta, kwasababu shutuma hiyo ni kubwa sana, na kama itafuatiliwa ionekane sio sahihi unaweza ukafikishwa pabaya…’ akasema mganga mkuu wa hospitali ya serikali, na mbele yake walikuwepo madocta wakuu wa vitengo mbalimbali na pia alikuwemo mkuu wa ulinzi
‘Mimi nimewasikia wakiongea na bahati nzuri wakati wanaongea hawakuwa wakiniona, kwahiyo kama ingekuwa uongo, wangeuongopa wakijua kuwa nipo, lakini hawakujua kabisa kuwepo kwangu hapo, na hata walipogundua kuwa nipo na nimewasikia, yule nesi mwingine alikuwa kashika sinia la vyombo, likamponyoka kwa woga….sasa ni kweli au sikweli inatakiwa kuwaulizia wao wenyewe , lakini kama niwajuavyo watakana futi mia, labda muwahusishe polisi wao wanajua jinsi gani ya kuwabana vyema..’akasema Rose.
‘Mimi naona haina haja ya kuwahusisha polisi haraka kihasi hicho, kwanza hili swala bado lipo mikononi mwetu, na kama tutashindwa tutafanya hivyo,…kwanza napendekeza kujichunguza wenyewe, ili tujua kiini cha haya matukio, tukianzia na huyo mgonjwa tuchunguze kuona kapoteaje, maana sio mara ya kwanza kusikia tuhuma kama hizi, na mimi nilitaka kulifuatilia hili kipindi fulani mkanizuia, na nisingependa kitengo change kiwe kinahusishwa mara kwa mara na mimi nisichunguze na kugundua uzaifu huo upo wapi, na hata kama ni mimi siwajibiki nitakuwa tayari kujiuzulu, naona wakati huu ndio wakati muafaka, ili kuondoa hili doa katika hospitali hii….’ Akasema mkuu wa kitengo cha ulinzi.
‘Sawa…mkuu, lakini huko naona umekwenda mbali, sana hatujafikia kunyosheana kidole, na nakubalina na wewe ila nilitaka kumuondoa huyu eeh, Docta…kwani kwa minajili hiyo hili ni swala la ndani, na huyu sio mfanyakazi wetu hastahili kuwepo’ akasema yule mkuu wa ile hospitali na kumgeukia Docta Rose, `Ila Docta Rose nilitaka kuliweka sawa kwako kujua uhakika wa hiyo shutuma…tunakuomba utupishe…’ akawageukiwa wengine na kusema, `Sasa kwahiyo mnakubaliana na Docta Rose, kuwa hilo kweli limetokea na linahitaji kuwajibika sisi wenyewe ndani ya hospitali, maana nilitaka kwanza alithibitishe kwanza Docta Rose, yeye mwenyewe kwa mdomo wake kuwa anauhakika na anachokisema, kabla hatujaingia ndani ya kiini chake chenyewe,…ok’ halafu akamgeukia tena Docta Rose na kusema ‘Sawa Docta Rose, nakuomba hili swala utuachie, na tukikuhitaji tutakuita, samhani sana kwa hilo, …’ akasema yule mganga Mkuu na Rose akainuka kuondoka.
Hata Rose alipofika kazini kwake hakuwa na moyo wa kutulia, alikuwa katoneshwa pabaya, `Ina maana huyu mtu kama kafa kweli basi watakuwa wao hawa hospitali ya serikali kwa namna moja wamehusika kumuondoa duniani, na kwanini wafanye hivyo…?’Akajikuta anaongea mwenyewe kama mtu aliyechanganyikiwa na akafikia hata kuamini kuwa huenda huyo jamaa hajafa….`lakini hata,… bado kuna mashaka,…’ Alipowaza hivyo, haraka akakimbilia ofisini kwa Docta Adamu kutaka kupata mawazo kuhusiana na wazo lake hilo jipya , lakini cha ajabu hata alipomhadathia Docta Adam nini amewaza, mwenzake alifikia kumkatisha tamaa kabisa, kuwa huyo mtu keshakufa, ndio maana wenzake hawakutaka kulifuatilia zaidi,..akamkazania ajiandae kwa safari ya kwenda kusoma, na ikiwezekana wapange maisha ya baadaye pamoja, aliposikia hivyo akaona heri ajiondokee nyumbani ili atafute njia zake mwenyewe za kugundua nini kimetokea kwa huyo mgonjwa.
‘Wewe na mambo yako bosi, safari, safari…imekuwa wimbo, na…hilo la mipango ya baadaye na mimi sahau…moyo wangu upo kwingine kabisa, najisikia sana uchungu na kujiona nimefanya kosa, kumtelekeza yule mgonjwa, na kama kafa kweli, sijui…lakini moyoni nahisi kama bado yupo hai….’ Akasema Rose, huku akitoka nje, na kumuacha Bosi wake kashika shavu akimwangalia kwa makini…na kusema ‘Wewe wangu tu…huyo keshaondoka duniani….’
Siku ya pili yake akawa anatembea ufukweni hakuwa na sababu ya mazoezi, ila alitaka kupunga upepo, na alipofika kwenye mti uliokuwa na kivuli akaona mtu amelala , akiwa kajikunyata sana, inaonekana alikuwa akitetemeka baridi na hakuna mtu aliyemjali. Akamsogelea na kabla hajamgusa mara akasikia yule mtu akiongea maneno kwa sauti ya chini na maneno hayo yaliyomshitua sana Rose, na kusononeka moyo wake.
‘Ohhhh, Sweetie….umeamua kuniacha nife…nilikuomba unilinde, leo nakufa kwa mateso makubwa, …bila hata kosa, hebu niambieni nimekosa nini, nina kosa gani mimi, mnanipiga kama mwizi , mnaniunguza na nyaya za umeme, mnanitesa, eti nikiri kuwa mimi ni gaidi….jamani…halafu hamtaki hata kunitibia…Sweetie upo wapi , sweetie….’ Mara yule mtu akalala na kunyosha miguu, na mara akawa kama anatingishwa, kama vile mtu anayetaka kukata roho. Rose akamsogelea haraka akaanza kutoa huduma ya kwanza, na mwishowe aliamua kutoa koto lake la udakitari na kumvika yule mtu ili apate ujoto.
Baadaye aliomba msaada kwa watu waje wamsaidie, na usafiri ukatafutwa wa haraka, na yule mgonjwa akafikishwa hospitalini kw Docta Adam. Na kwa muda ule alipofikishwa mgonjwa docta Adam hakuwepo, Rose kama msaidizi wake akatoa amri kwa madakitari wengine kumuingiza chumba cha wagonjwa mahututi, na kazi ya uchunguzi na vipimo mbali mbali ikafanyika haraka, …na baadaye docta Adam alifika na kuwakuta Madocta wake wakiwa wanamhudumia huyo mgonjwa, naye bila ajizi , akijua ni mgonjwa mahututi anahitaji huduma zaidi, akaingia kazini, hadi pale mgonjwa alipooekana yupo katika hali ya kuridhisha na kupelekwa kwenye wodi ya wagonjwa wa kawaida.
‘Hebu docta Rose, huyu ni nani, maana mimi nimefika nikakuta mumeshaanza matibabu, nahisi kama niliwahi kuiona hii sura kabla, hebu nipe muhutasari wake kidogo….kiukweli huyu mgonjwa, kama asingewahishwa hapa mapema, ….mmh, kwanini watu hawa wanasubiri mpaka mgonjwa anakuwa mahututi , …..unaona ilivyo ana imonia kali kweli, ana malaria kali , ana….kila gonjwa analo, na nilikuwa na wasiwasi wa TB, lakini naona hilo halipo, kwahiyo ni magonjwa ya kawaida nahisi baada ya sindano hizo kuisha atakuwa na hali njema….poleni sana wataalamu wangu’ Akasem Docta Adam.
‘Ki ukweli labda niseme nahisi kuwa ni nani,maana nilivyomkuta katika ile hali, sikutaka hata kuangalia kuwa ni nani , nilichojali ni kuokoa maisha yake, kwani alikuwa katika hali ya mbaya, kama ya kukata roho ……’ akashindwa hata kumalizia.
‘Huyu sio yule mgonjwa aliyetoroka… , ambaye kwa mara ya mwisho ulisema kuwa umeambiwa kuwa keshakufa….au wanafanana tu..’ akauliza Docta Adam.
‘Hata mimi nahisi hivyo, ila kama ni yeye kapigika kweli, maana kawa mzee, kaisha sana, utazani ana TB, …’ akasema Rose.
‘Lakini sizani kama ni yeye, yule ulishaambiwa keshakufa…lakini huenda ni yeye…sura ni yake, …ila kaisha…kama kweli ni yeye, amepitia hali ngumu sana. Unajua ile jela haifai wka maisha ya mtu, halafu matibabu yenyewe nahisi hakuwahi kupata ya kutosha, lazima atakuwa hivyo….sasa nahisi mzigo, unatujia tena, nashindwa hata kuwalaumu, maana huyu ni binadamu na hali kama hiyo, hata angekuwa nani angejitolea kumsaida, naomba faili lake liwekwe kwenye watu wanaohitaji wahisani wa kujitolea kumsaidia na docta Rose, naomba ujaribu kuwasiliana na wafadhili wetu na kutoa tangazo kutafuta wahisani wa kujitolea, maana hapa nilipo sina ujanja, lazima tuombe msaada…’ akasema Docta Adam.
‘Docta Adam, hata mimi niweke kwenye orodha ya watu wanaojitolea, nipo tayari kukatwa kidogo kidogo kwenye mshahara wangu, …’ akajikuta Rose akitamka hayo maneno na baadaye akashituka na kujiuliza moyoni kwanini katamka vile.
‘Acha mzaha Docta Rose, hayo matibabu yake unajua ni kiasi gani, hapo bila wafadhili hatuwezi …wewe fanya nililokuambia,…na kama inavyoonekana anahitaji bado uchunguzi wa kina, na unakumbuka, kama kweli ni yeye, alihitajika kufanyiwa CT-scan, achunguzwe kichwa, ….huku tunaweza kugundua vyema kuna nini na unajua kipimo hicho kilivyo na gharama. Mimi sikatai kumsaidia na mpaka hapa tumesaidia vya kutosha, vyema tusaidie na sisi tusaidiwe, na kama wapo watu ambao wapo tayari hujitolea, kwanini tusiwaombe hawo, ili kuipunguzia mzigo…’ Akasema Docta Adam
‘Sawa Bosi nitalifuatilia hilo, lakini bado nasisitizia kuwa naomba mimi name niwekwe kwenye watakaojitolea, na…tusitulie kuendelea na matibabu yake mengine kwasababau ya kuogopa gharama, mimi nitamdhamini kwa hapa….’ Akasema Rose na kuondoka kufuatilia hilo aliloagizwa na bosi wake. Bosi wake alibakia akiwa ameduwaa na kumuwaza Rose, halafu akamgeukia yule mgonjwa kumwangalia kwa makini, huku moyoni akisema ina maana kuna kitu fulani kinamgusa Rose kuhusu huyu mgonjwa, sio jamaa yake, hamjui kabisa, lakini kaamua kujitolea kwake kama jamaa yake…mabadliko ya ajabu sana haya,…na namuona kila mara anapokutana na huyo mgonjwa anabadilika kabisa,…mmh, hapa sasa kuna jambo na nina uhakika kuwa ni yule mgonjwa karudi tena, na hii ina maana tatizo lile la mwanzo limerudi tena mezani kwangu, na inavyoonekana Rose hataweza kuambiwa lolote, kuhusiana na huyo mgonjwa mapaka apatiwe kinachohitajika…ok, tutaona hili.
Akaondoka pale wodini akikuna kichwa huku anaongea kimoyomoyo akisema ‘Iliyobakia ni kuhakikisha huyu mgonjwa anapewa huduma zote kama alivyodai Rose, na bili yote itawekwa katika jina lake, na ilivyo, matibabu ya mgonwa kama huyu gharama zake zitakuwa kubwa sana na Rose hataweza kuzilipia…’ akakuna kichwa kuwaza zaidi, akagongesha vidole na kutoa sauti ta taa, kama vile kakumbuka kitu au kagundua wazo la muhimu. Akaondoka hadi ofisi ya mhasibu na kumpa maagizo kuwa bili ya huyo mgonjwa iwekwe kwenye jina la Rose kama mdhamini, na ahakikishe anamsainisha Rose kwani kakubali kumdhamini.
Baadaye aliondoka pale kwa mhasibu na kurudi ofisini kwake huku akiwaza mpango wake huo utakavyofanya kazi, ingawaje…akawa anaingiwa na mashaka na mpango huo akasema kwa sauti `Ninauhakika mwisho wa siku Rose atakuja kwangu kunipigia magoti kuwa gharama hataiweza mwenyewe, labda awe kawapata hawo wafadhili…lakini vyovyote iwavyo, kazi ya kuzikusanya hizo hela za msaada ni kazi nzito inahitaji uzoefu wake, lazima atakua kumomba msaada na hapo nitamweka sawa,….’ Akatabasamu alipofikiria wazo hilo.
Rose alipofika nyumbani kwake akawa kamkuta jirani yake Docta mwenzake, rafiki yake, hajaondoka, akamhadathia nini kinachoendelea kuhusu huyo mgonjwa na kumuomba akifika ajaribu kuwa karibu na huyo mgonjwa ilia pate huduma zote. Mwenzake akamwangalia kwa jicho la kushangaa, na kwa vile hakuwa na muda wa kuongea zaidi yeye akamkubali, lakini mwishowe akaongeza maneno na kusema;
‘Kweli sasa naamini maneno ya watu kuwa apendaye haoni….’ Akacheka kicheko cha kebehi na kundoka, huku Rose akiwaza huo usemi, akijiuliza akilini ina maana kweli analofanya ni kwasababu ya kupenda, ina maana kweli amegubikwa na mapenzi, hapana siwezi kujiingiza tena kwenye mateso, kwanini niteswe na watu, eti kwasababu ya kupenda, ina maana unaweza ukapenda wakati mwenzako hakupendi, sasa ina maana gani, je mapenzi yanaweza kugeuka kutoka kupenda kwenda kwenye chuki, kwanini mapenzi, na chuki….baadaye akatabasamu, akijaribu kuivuta ile sura ya yule mtu ambaye anadhania kuwa anampenda, lakini sasa haikuja ile sura ya kawaida, ya mvuto, ilikuja sura ya mtu aliyekonda, akionekana mdhaifu, mzee kalala kitandani hajiwezi…akakuna kichwa na kusema, ni swala la muda tu atarudia hali yake kwasababu…sura ile ikawa inatawala ubongo wake, sura ya mtu aliyekwisha kabisa na anachosubiri na kusaidiwa tu…..
********
Wakati huo kule hospitalini kwenye moja ya kitanda, alikuwa kasimama Docta Adam, akimchunguza yule mgonjwa , na alipohakikisha mambo yamekwenda vyema mara akaingia yule docta, jirani yake na Rose, akasalimiana na bosi wake, halafu akamchungulia yule mgonjwa, na baadaye akamgeukia Bosi wake ambaye alikuwa kasimama nyuma yake akimtizama kwa makini, na wakawa sasa wanangaliana na Bosi wake, hawakuongea, waliendelea kuangaliana kwa muda na baadaye yule docta akatizama chini, na kujifanya anamtizama yule mgonjwa, na hapo Docta Adam, ageuke kutaka kuondoka.
‘Bosi kwanini umeniangalia sana, na baadaye unaondola bila kusema neno, ina maana sisitahli kuongeleshwa, na wewe ulikuwa ukimpima mgonjwa, hutaki hata kunipa taarifa zake, ndio najua sio kazi yako kunipia hiyo taarifa , lakini nimesikia mwenzangu ana dharura kaondoka mapema…sasa bosi,…mbona …ooh, sijui nisemeje..’ akajikuta akikosa la kuongea.
‘Nakusikiliza wewe, maana ulivyokuja, na ulivyovaa, haiendani na kazi yako, hiyo ndio sare ya kazi, usifikiri nilikuwa nakuangalia tu, nilikuwa nawaza mengi hususani nidhamu ya hapa hospitalini inavyozidi kupungua siku hadi siku, mnashindwa hata kuniheshemu, ….wewe ulivyokuja ulitaka mimi nikupe hiyo taarifa, kwasababu mwenzako hayupo, ndio utaratibu wako uliojiwekea au sio….kwanza tuonane ofisini, na hali ya huyo mgonjwa inahitaji vipimo vya haraka vya TC-Scan, tuangalie huko kichwani kuna nini, lakini tunamuhitaji mdhamini wake…’ akasema huku anaondoka.
‘Nani mdhamini wake Bosi…?’ akauliza akijifanya hajui.
‘Rose…mpigie simu haraka aje’ akajibiwa kwa mkato.
Rose, alipata taarifa kuwa anahitajiwa haraka hospitalini kuhusiana na mgonjwa wake, aliposikia hivyo hakukawia haraka haraka akafika na akaambiwa kuwa anahitajiwa kusaini bili yake ya udhamini , kwani mgonjwa wake anatakiwa kufanyiwa kipimo cha bei mbaya, na haiwezekani kifanyike hivi hivi bila kuwa na uhakika, angalau hata mdhamini au kuwa na njia yoyote ya kufidia hiyo gharama.
‘Sawa lete hiyo bili nitasaini hakuna matatizo..’ akasema Rose, na kuisaini ile bili hata bila ya kuangalia ni gharama kiasi gani. Hata yule mhasibu akashangaa na kumwangalia Rose kwa makini kwa macho ya huruma , na baadaye akamuuliza Rose, imekuwaje akakubali kubeba huo mzigo, na gharama za huyo mgonjwa ni kubwa, zinaongezeka siku hadi siku, ana uhakika gani kuwa huyo mgonjwa atazimudu ukizingatia haijajulikana anatokea wapi au anafanya kazi gani.
‘Usijali, …mmh, hilo litakuwa deni katika mshahara wangu, ..deni halimfungi mtu…’ akasema na kuondoka kuelekea wodini kule alipolazwa mgonjwa wake. Alipofika pale kitandani akakuta kila kitu kipo tayari na mgonjwa alikuwa katayarishwa kwenda kufanyiwa hivyo vipimo, ilivuoonekana mgonjwa alikuwa keshazindukana, kwani alimkuta anaangaza macho huku na huko, akiwa kama anajaribu kujiuliza hapo yupo wapi.
Rose alifika pale kitandani na kumwangalia kwa makini, lakini yule mgonjwa alikuwa akitizama sehemu moja halafu anageuza shingo anatizama sehemu nyingine na baadaye akamtizama Rose, alimtizama kwa muda bila kusema kitu, na Rose akamsogelea na kumuinamia karibu yake.
‘Unajisikiaje mgonjwa…?’ Rose akamuuliza.
‘Unasema, ….?’ Akauliza yule mgonjwa kama vila hasikii nini anachoulizwa, halafu baadaye akasema `Sijui najisikiaje, kwani naumwa nini…sijui nijisikiaje , kwani wewe nani?’ akauliza yule mgonjwa akionyesha uso wa mshangao.
‘Mimi ni Docta Rose, na …’ akasema Rose huku akijaribu kutafakari nini cha kumwambia huyu mgonjwa , na pia alikuwa akiwaza kiundani kutafakari tatizo la huyu mgonjwa litakuwa ni nini, nini kiini cha hilo tatizo, huenda hicho kipimo kikasaidia sana…
‘Unasema unaitwa Docta Rose, lakini hujavaa kidakitari, ndio maana nikakuuliza, nilidhania wewe umekuja kumtizama mgonjwa wako kama wengine…mimi naona sina ndugu wa kunisalimia…sijui ndugu zangu ni nani, nitawauaje wakati hata mimi mwenyewe sijijui ni nani…’ akasema huku anawaangalia watu mbali mbali wakisalimia wagonjwa wao.
‘Mimi mgonjwa wangu ni wewe, na pia ni ndugu yako, ndio maana nimekuja moja kwa moja kitandani kwako kukuangalia, sijaja kama dakitari, kwani leo nipo mapumziko , kwahiyo usijali sana, tupo pamoja, nimekuja kwa ajili yako tu…’ akasema Rose.
‘Nashukuru kama ni hivyo, maana …sijui ilikuwa ni ndoto, au ni kweli ila nahisi nilikuwa nateswa sana, napigwa, nachomwa na umeme…sijui ni akina nani hawo wenye unyama wa aina hiyo, na kwanini wanifanyie mimi hivyo,..nahisi kama ilikuwa ni ndoto, ndio maana nilikuwa naangalia huku na kule, kuhakikisha kuwa kuna usalama, vinginenyo ningetoroka…’ akasema yule mgonjwa.
‘Nakuomba usije ukafanya hivyo…Usijali hayo utayakumbuka polepole, na siui wewe unaitwa nani vile…?’ akauliza Rose kwa kumtega.
‘Mimi sijui naitwa nani, lakini …hapana, sikumbuki jina langu…na sikumbuki kumetokea nini, na kwanini nipo hapa hospitalini…wewe umesema mimi ni mgonjwa wako, ilikuwaje, nilipata ajali, nili…au nilizama majini…’ alipotamka hilo la kuzama majini akawa kama kaguswa na kitu akawa anakodoa macho tu kwa muda mrefu.
‘Kwanini unasema ajali au kuzama majin?’ akauliza Rose.
‘Nahisi kitu kama hicho na nikiwaza kuzama majini, nahisi kama masikio yakiwa yamejaa maji…
masikio yangu nahisi yana maji, au kichwa kina maji…’ akasema na kujaribu kukitikisa kichwa.
‘Sawa, hilo tutaligundua muda sio mrefu…kuna kipimo kinatakiwa kuchukuliwa,…’ akasema Rose.
‘Kwani hapa ni hospitali ya serikali, ….maana siui gharama zitakuwaje, kama sikosei …na naiona hii hospitali kama sio ya serikalini..?’ akawa anasema huku anaangalia huku na kule.
‘Ni kweli hii hospitali siyo ya serikali ni ya mti binafsi, lakini hilo lisikusumbue kichwa, kuna watu wapo tayari kujitolea, kwa watu kama nyie, baadaye tutaangali ukipona, kama utamudu kuzirudisha hizo gharama au la…lakini kwasasa usiwe na wasiwasi na hilo..nitalisimamia mwenyewe..’ akasema Rose.
‘Nashukuru sana, wewe ni mtu mwema sana na inaonyesha una huruma ya ajabu, na sijui nikuite nani…naona nikuite Sweetie..’ akasema yule mgonjwa na kumwangalia Rose kwa macho yaliyoonyesha kuchoka, lakini yakiwa na uhai fulani!
‘Sweetie….!,mmmh, kwanini uniite Sweetie?’ Akauliza Rose huku akionyesha uso wa mshangao na huku anatabasamu.
‘Kwasababu kwanza sijui jina lako,….’ Akawa kama anafikiri halafu akaendelea kuongea kwa kusema `….Na hilo jina limenijia tu kichwani mwangu, nahisi kama niliwahi kulijua kabla au ni kwasababu wewe unavyoonyesha upendo wa kweli…labda niite hivyo, na kama wanadamu wote wangekuwa kama wewe, duinia ingekuwae na raha sana, kama sio kisiwa cha amani! Nakiri kuwa wewe umenionyesha kuwa unanijali hasa kipindi kama hiki ambacho sijijui…na naweza kusema wewe ni rafiki, rafiki wa kweli…nashindwa hata nikuelezeja’ akawa anazungumza haya huku machozi yakimtoka, sijui ni kwasababu gani. Na Rose akatoa leso yake na kumfuta,..na hapo yule mgonjwa akasema ‘Ahsante rafiki wa kweli, Sweetie….’.
‘Sweetie, ndilo jina lako toka sasa, kama hutojali nitakuwa nakuita hivyo, na naahidi kuwa kama nikipona, nitalipa ghrama zote hizi, nitahakikisha naizirejesha, hata kama ni kwa kufanya kibarua, au popote, …nahisi kuwa uwezo huo upo, ingawaje sijui kwa vipi, lakini nahisi nilikuwa na kazi fulani…sina uhakika, maana kumbukumbu hazipo..ila hilo nikuahidi…Sweetie…’ akasema yule mgonjwa na kutoa tabasamu. Tabasamu ambalo liliganda kichwani mwa Rose,…na hapo Rose naye akatoa lile tabasamu lake adimu ambalo lilikuwa limetoweka miaka mingi, na hata kabla hawajapata nafasi ya kuongea zaidi, mgonjwa akachukuliwa kupelekwa chumba cha vipimo, huku Rose akiwa kabakia pale wodini akiwaza hilo jina jipya alilopewa, la Sweetie…..
‘Mhh, Sweetie…’ akasema huku akiwa kaweka shingo upande akiwaza.
NB, Ndugu wapendwa je huyu mgonjwa atapona, na jina Sweetie lina siri gani, ngoja tuingie sura ya tatu ya kisa hiki, kwa kurudi upande mwingine wa tukio hili, kule kwa akina kwa akina Maua na Maneno.
Ni mimi: emu-three