Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, February 11, 2010

Nifanyeje jamani...

‘Hodi wenyewe, mama nanihii upo?’ ilikuwa sauti ya mama mmoja alikuja kuchota maji. Mimi nilikauka kimya, siunajua tena siku ya Jumatatu unatakiwa uwe kazini, lakini kwa vile bado nipo kijiweni, sikupenda majirani wajue hili. Mama watoto alikimbilia nje na kumkaribisha huyu mgeni ambaye hakutaka kuingia ndani zaidi ya kuchota maji na kuondoka.


‘Mama nanihii unahitaji mfanyakazi wa ndani?’ Yule mama alimuuliza mama watoto wangu, niliguna moyoni, nikijua nini jibu atakalopata.

‘Kwa hivi sasa sihitaji, inagwaje kweli ni muhimu ningekuwa naye, kwasababu, nashindwa kufanya shughuli nyingine au kutoka, kwa vile sina mtu wa kumkabidhi majukumu’ mama watoto alimijibu.

‘Sawa, lakini huyo ni mtoto mzuri kitabia, ingawaje hawa watoto wa nyumbani unaweza ukawaamini sana lakini wakafanya jambo ambalo hutazamii. Yaani mimi hapa nilipo natamani duniani inimeze kwa tukio lililotokea kwangu, kisa cha mfanyakazi wa nyumbani’ Huyo mama akaamua kukaa kwenye ngazi za nyumba yangu ili aweze kumhadithia mke wangu. Nilikuwa dirishani kwahiyo maongezi yao nilikuwa nkiyasikia vizuri, na kwa vile Yule mama hakujua kuwa nipo aliongea kiundani mambo yake , kama unavyowajua akina mama wakiamua kuongelea swala Fulani kwa mtu anayemwamini.

‘Ndiye unayetaka kuniletea mama nanihii?’ mke wangu aling’aka

‘Hapana sio huyo, huyo wangu namuandaa aende kwao kalikoroga mwenyewe’ Yule mama alisema , na kabla mke wangu hajamuuliza vizuri alianza kuhadithia kisa ambacho kilinifanya nishituke na kuamua kukiweka hapa ili wale wenye nia njema wachangie, na huenda iwe fundisho kwa wenye wafanyakazi wa nyumbani.

Binti huyu niliye naye nilimchukua akiwa mdogo, alipomaliza darasa la saba. Tulikaa naye kama binti yangu, na kwa vile alikuwa na adabu , mchapakazi mzuri niliamua kumsomesha sekondari hadi kidato cha nne. Hakufaulu, lakini tulikuwa na malengo ya kumsomesha zaidi. Lengo hilo lilikwama kwasababu mume wangu kibarua chake kiliota majani, ikawa mimi ndiye mhudumiaji wa familia. Kama unavyojua kipato changu ni kidogo nisingweza kumsomesha na kuilisha familia, kwahiyo tukapanda asubiri hadi mume wangu atakapopata kazi.

Siunajua maeneo ya huku kwetu kama unafanyakazi ili uwahi kazini inabidi uondoke saa kumi na moja alifajiri na kurudi nyumbani ni kuanzia saa mbili za usiku. Hili halikuwa tatizo kwasababu mume wangu alikuwa katika mkumbo huo kabla hawajampunguza kazini kwao. Na pia yupo huyo binti ambaye tulimchukua kama mfanyakazi wa nyumbani nab ado tunaendelea kumlipa, licha ya kujitolea kumsomesha na kumpa huduma zote kama mtoto wetu. Lakini kama walivyosema wahenga, kuku wa kienyeji hafugiki, na kweli kwa hili sidhani kama nitahitaji mfanyakazi wa nyumbani tena.

Mama nanihii, wakati mwingine nawashangaa sana hawa waume zetu, sijui akili zao zipoje. Unajua ninakuhadithia hili sio kwasababu niminga wa kutoa siri za mume wangu nje. Hapana, lakini lilotokea inabidi nimhadithie mtu ninayemuamini ili anipe ushauri. Naujua ushauri, na hasa ushauri nasaha kwani nimeshaupitia, lakini huu sasa ni mkali zaidi.

Wiki kama mbili zilizopita nimepata kalikizo kadogo nikaona nishirikiane na familia kujifanyia miradi midogo midogo, na hapo ndipo nilipogundua kubwa kuliko. Niligundua kuwa mfanyakazi wangu huyu wa nyumbani ni mja mzito. Na nilipombana sana anitajie ni nani aliyempa alikataa katakata, hadi nilipomwambia namrejesha kwao kijijini. Nitamrejesha ingawaje hataki lakini kwa hali ilivyo sitaweza kusihi naye tena.

Unajua tangu aliponitamkia mtu aliyempa ujauzito ule nilishikwa na kitui ambacho hadi sasa siamini na kwa vile hata aliyempa ujazito huo kakataa kabisa nashindwa kuamini kuwa ni kweli, hili linawezekana . Simini, naombeni msaada wenu kwenye janga hili’

‘Ni nani aliyempa uja-uzito huo?’ mama watoto akauliza kwa shauku.

Unajua mama nanihii, kama isingekuwa hili tatizo nililonalo na mume wangu, ningefungasha virago niondoke nimuachie huyu mume nafasi , manake kaniona sifai, lakini tatizo tulilonalo ni kubwa tunahitajiana sana, na hasa kumlea mwanetu ambaye naye pia waligundua kuwa anatatizo kama hilo. Na tuligundua kipindi mtoto wetu anaumwa mara kwa mara. Alipopimwa akaonekana ana virusi vya ukimwi. Ilibidi na sisi tukapime, na wote tukaonekana tunavyo!

Najua wote mnajua hili, sio siri kuwa mimi na mume wangu na mtoto tumeathirika, sasa sikutegemea kuwa mwenzangu anaweza kukosa imani na kudiriki kutembea na mfanyakazi wetu ilihali anajua kuwa anamtataizo haya. Hili mimi siamini kwani mume wangu kakataa katakata, na kusema huyu binti kaumua kumpakazia ili asiondoke hapa nyumbani. Je nifanyeje ili kuupata ukweli na mume wangu namuamini sana, na tangu tuoane naye hajawahi kunisaliti au kunidanganya. Sasa mimi nachanganyikiwa. Nisidieni ushauri, nifanyeje?

‘Fuata sheria mama nanihii, mshitaki na kwnye sheria utapata ukweli’ mke wangu alimshauri kwa harakaharaka hivyo, na ushauri huo ulimfanya Yule mama ainuke na kwa hasira akaaga huku akisema

‘Nini, nimshitaki mume wangu…kwaheri...'
From miram3

No comments :