Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, February 3, 2010

Naomba hamsini...

`Shikamoo’ sauti ya kitoto iliniamukia, na kwa vile nilikuwa na haraka sikuelewa kuwa nilimpita mtoto pale njiani. Nikageuka kumwangalia ni mtoto wa namna gani aliyeniamukia, nikitafakari matukio ya wizi ambayo hufanywa na matepeli wanaojigeuza sauti za kitoto. Unasikia sauti shikamoo, au unasikia sauti mdudu huyu, au unasikia sauti ya umenikanyaga na ole wako ugeuke, utakuta hela uliyoweka mfuko wa shati haipo!


Mtoto wa miaka tisa hivi alikuwa akiniangalia kwa macho ya huruma, alikuwa akisubiri niitikie shikamoo yake, na nilijua nini kitafuata baaada ya hapo. Nilisimama na kumsogelea Yule mtoto, sijui kwanini , ila nahisi kuna jambo lilinivuta ili nisikie nini mtoto yule anataka kusema zaidi ya kunisalimia.

`Marahaba, hujambo mtoto’ nilimuitikia

`Sijambo, naomba hamsini baba, naomba nipate nauli ya kufika mjini’aliatamka yule mtoto akinisogelea. Nahisi alishaambiwa mtu akikuitikia shikamoo yako ni mtumwema wengine watashia kukutukana, wakijua shikamoo yako ina nia ya kuomba.

`Mjini unaenda kufuata nini, nawewe sahizi ulitakiwa uwe shule’ nilimuuliza na moyoni nikajisemea kwanini na mimi asiniulize swali, wewe sahizi unafanya nini hapa wakatui ulitakiwa uwe ofisini au shambani au sehemu yako ya kazi.

‘Ninakwenda mjini kuomba pesa, baba anaumwa hana hela ya matibabu na yakutusaidia kuishi, mama alikufa zamani, sasa kila ninayemsalimia hataki kuitikia kwasababu wanajua nitawaomba pesa. Sio nia yangu kuomba pesa, lakini ninaogopa kuwa na baba naye anaweza akafa, kwasababu anaumwa TB, na hana ndugu wakumsaidia’ alisema yule mtoto huku machozi yakimtoka. Kwa hali kama ile hata kama una roho ngumu namna gani ungeitoa ile senti yako ya mwisho uliyoiweka kwa ajili ya nauli.

‘Wamezoea hao watoto kuombaomba, hawataki kwenda shule wanabakia kuombaomba baadae wanageuka kuwa vibaka’ Jamaa mmoja akapayuka akinipita kwa kasi. Nilimwangalia kwa makini nikajisemea, kama kweli angelisikia masahibu ya huyu mtoto hangelitamka maneno kama yale. Ni kweli wapo watoto ambao hugeuka ombaomba kwa kukaidi kwenda shule, ni sawa na watu wengine wazima wanageuka kuwa ombaomba kwa kujisingizia ugonjwa na kuwafanya wenye haki na wanaostahili msaada kukosa.

Nilimgeukia yule mtoto na kumuuliza kwanini asingeenda shule kwanza, jibu alilonipa ni kuwa hana hela ya sare za shule, hana hela ya madaftari na hata hivyo angewezaje kumuacha baba yake afe ndani na ili hali yeye ndiye anayetegemewa kutafuta pesa, ili wapate angalau pesa kidogo ya kununulia chakula.

‘Baba , wakati baba anafanya kazi tulikuwa tukisoma shule nzuri ya kulipia, lakini mama alivyoanza kuumwa baba akapunguzwa kazi, na hapo baba ilibidi auze baadhi ya vitu ili amtibie mama. Aliuza kila kitu nab ado mama hakupona na hatimaye akafariki. Nilibaki na baba ambaye alikuwa akifanya vijibarua hapa na pale na ghafula naye akaanza kuumwa, alipopimwa akaonekana ana TB. Alianza kukonda na kukosa nguvu ya kufanya vibarua sasa yupo nyumbani sijui kama atapona. Lakini ipo siku nitapata pesa nyingi nitamtibia baba yangu..’ ilikuwa kauli ya huzuni ya yule mtoto.

Nilitoa kilichokuwa mfukoni na kumpa yule mtoto , na alinishukuru hadi kunipigia magoti , na mara gari la mjini likaja akapanda akaondoka. Niliwaza na kuwazua nini dunia inapokwenda, ina maana huruma zimekwisha ndani ya mioyo ya wanadamu? Ina maana hakuna majirani wanaojua tatizo hilo la huyo baba anayeumwa? Ina maana kweli kizazi hiki cha watoto kama hawa kitaishije? Je hata hawo waajiri waliomfukuza au kumpunguza kazi huyu jamaa hawana watoto kama yeye? Labda wao hawatakutana na masihibu kama hayo, kwasababu wao ni matajiti lakini tukumbuke kuwa kuna leo na kesho.

Ombi langu kwa jamii ni kutafuta jinsi gani ya kuwasaidia hawa watoto ombaomba, huenda hadithi kama hii imo kwa wengi. Nina imani kuwa wapo wenye uwezo, na kama tukiamua kwa ukweli, kila tajiri mwenye uwezo akaamua kumsaidia mtoto mmoja mmoja, nina imani tutakuwa tumesadia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo la watoto wa mitaani. Sidhani hamsini, au shilingi mia utakayompa itamsaidia sana zaidi ya kuwasaidia elimu kwa ajili ya maisha yao ya baadaye. Badala ya kuomba hamsini, tuwaambie waombe elimu.

From miram3

1 comment :

Anonymous said...

Hahaha unanikumbusha mbali kweli