Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, February 11, 2010

Mtenda akitendewa..(1)

‘Hivi ukifumaniwa na mkeo, ungefanyaje, au ungemshauri nini mkeo?’ Niliulizwa swali lililoniacha mdomo wazi, kwani aliyeniuliza ni mtu ambaye sikutegemea angeniuliza swali kama hili. Nilimwangalia kuhakikisha kuwa kweli alichouliza ana uhakika nacho, na kuhakikisha kuwa anahitaji ushauri wangu akaniuliza tena swali hilo mara ya pili.


‘Kwanini unaniuliza swali kama hili, kwani mimi nalichukulia kama maswali yenye muonekano hasi, yaani swali la kujitabiria ubaya, wakati ni vyema wakati wote tukajitabiria uzuri, mimi..’ nilijaribu kumpa ushauri nasaha lakini akanikatisha.

‘Wewe nijibu kama vile imekutokea kwa vyovyote vile, huenda ikawa bahati mbaya au kutegewa, na hamadi mkeo huyu kakufumania, ungefanyaje?’ aliniuliza huku kanikazia macho

‘Jibu liko wazi, ni kiasi cha kujiuliza, kama wewe umemfumania mkeo ungechukua hatua gani’ nikamuelezea nikijua kuwa kuna jambo zito jamaa anataka kunihadithia.

''Ni sawa, kwa wanaume ni rahisi kwasababu sisi ndio wenye uamuzi mkubwa, na kwa yoyote angesema kuwa talaka ingetoka bila kusubiri usuluhishi, lakini imetokea kinyume, na ujue kuwa mke kama ataamua kama mume, ina maana atakosa haki zake nyingi, nay eye atakuwa kwenye hasara kuliko mume. Naomba utafakari hili swali kwani sio natania, hili ni tatizo kwangu ndio maana nimekuja kwako, umesaidia wengi kwa ushauri, na nahisi utanisaidia kwa hili. Sikiliza kisa kilichonitokea mimi mwenyewe ndio utaweza kunipa jibu la uhakika.

''Ilikuwa siku ya sherehe ya kutimiza nusu karne, na iliandaliwa na mke wangu, sikupenda sherehe hasa zinazohusiana na ulevi ndani yake, lakini kwa vile mke wangu mpenzi ndiye aliyeandaa nikakubali na sikuwa na haja ya kukubali au kukataa kwani ilivyofanyika sikujua nilishanga nimepigiwa simu, nikiwa kazini kuwa kuna tatizo limetokea kwenye ukumbi wa jirani yetu. Jirani yangu ana ukumbi mkubwa wa sherehe na ni mtu ninayemheshimu sana, kwahiyo nilivyosikia kuwa ana tatizo sikuhitaji kuuliza tatizo gani nikaaga ofisini na kwa vile ilikuwa Jumamosi hapakuwa na kikwazo chochote.

''Nilifika kwenye ukumbi huo, na nilikuta mlango umefungwa, na pale ,langoni kumewekwa karatasi kubwa kuwa kuna ajali na watu hawaruhusiwi kuingia. Hutaamini, nilitumia mabavu kuingia, kwani huyo rafiki yangu alivyonipigia simu alisema kuwa mke wangu alikuwepo humo. Simu ilisema, rafiki yangu njoo hapa kwangu kuna tatizo kubwa na mkeo yumo, akakata simu. Sasa nakuta karatsi kuwa kuna ajali usiingie humu, sikukubaliana na hilo kwa muda huo nikawasukuma walinzi na kujitosa ndani mara nikakutana na kelele za `happy birth to you…

''Nilibaki nimeduwaa na mbele yangu alikuja mrembo kuliko wote duniani, alivyojipamba, alivyonivutia, nilitamani nimkumbatie hapohapo, lakini nikashikwa na kigugumizi kwani pembeni yake walikuwepo wazazi wake. Nikatabasamu nakumsogelea, na wote tukaelekea kwenye meza niliyoandaliwa , au tuliyoandaliwa. Nikalitaka kukasirika, lakini sikuweza, nilitaka kusema nina kazi nyingi nimeziacha ofisini lakini ikashindikana, kwani msemaji mkuu alikuwa akitoa burudani ya kila namna iliyonifanya niwe nikitabasamu na kuwaza nini kitafuata baadaye.

''Mara vinywaji vikaletwa, nilitaka kukataa nikijua udhaifu wangu, lakini aliyenisogezea kinywaji kikali ni mke wangu, nikanywa, nikanywa, nikanywa,…kila nikimaliza naongezewa. Mwisho nikamwambia mke wangu basi, naomba twende nyumbani, kwasababu namtamani. Pombe ilishakolewa kichwani. Mke wangu akasema mambo bado subiri.

''Nilitoka kama kwenda kujisaidia, nilipofika njia panda ya kwenda kwa wanawake nikamkukuta binti mmoja, na taswira ikanifananisha na mke wangu. Sijui ilikuwaje nikaanza kumtania, na utani uakazaa mengine nilishangaa tupo kwangu, kwenye kitanda change, na yaliyofuata hapo sitamanai hata kuyakumbuka. Na mara usingizi ukanishika. Niliposhituka ni asubuhi, nilizinduka nikijaribu kukuimbuka yaliyotokea jana, nikafumbua macho taratibu, na mara nikajikuta nimeshika kitu kama maji,…nikashituka na kuamuka haraka, mungu wangu, nilichokiona kilinifanya niamuke kutimua mbio, lakini nikaishia mikononi mwa asikari...''

Hebu fikiria ni nini kilitokea?
From miram3

No comments :