Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, February 11, 2010

Miadi ya kumuona bosi

Onapokwenda ofisini kwa watu unakuwa mnyonge, hata kama unayemfuata unamjua sana, ndivyo ilivyonitokea mimi nilipokwenda kumtembelea jamaa tuliyesoma naye kwenye viwangi vya vidato. Niliposikia kuwa ni bosi wa kampuni hii, nilitafuta siku nimwendee angalau hata ushauri ungenisaidia, kuliko kukaa nyumbani na kugombana na watoto.


Nilipofika kwenye hiyo ofisi, nilianza kukwamishwa na walinzi, kuwa nionyeshe kitambulisho na ni nani ninayekwenda kumuona. Nilijaza maelezo yangu kwenye daftari la wageni na kuelekea kwenye jengo la ofisi , sijui kuwa jengo lote hilo ni ofisi moja au kuna ofisi nyingi , nikajisemea moyoni nitajkua hukohuko. Hutaamini Tanzania yetu hii sio ile ya jana, majengo , maofisi yamewekwa kiutalaamu zaidi. Nilitamani name niwe ndani ya jengo hilo nakuitwa mfanyakazi wa kampuni hiyo.

Nilipofika maulizo nilimkuta dada mmoja ambaye kuongea kwake inaonyesha sio Mtanzania, ingawaje baadaye niliambiwa ni Mtanzania ila ni zile mbwembwe za kuongea Kiingreza mara kwa mara ndio maana hata akitamka maneno ya Kiswahili, inakuwa una-jua, you know…eeehe, tell… na vitu kama hivyo.

‘naomba kumuona Mr Mate(sio jina halisi)’ Nilimueleza Yule binti niliyemkuta pale mapokezi. Akaniangalia kwa dharau na baadaye akasema huku anainua simu nikijua kuwa anampigia huyo boso, kumbe anaongea na rafiki yake akimuombe amtoe chakula cha mchana. Alipomaliza akaniuliza nina ahadi naye

‘Kwakweli hapana, ila nilisoma naye na ukimwambia mimi ni nani hatahitaji hiyo miadi’ Nilimwambia

‘Sheria zetu za kazi hapa kama unataka kumuona huyu bosi mpaka uwe na ahadi naye, kwa ushauri andikisha hapa ili siku yako ikifika nitakuarifi kuwa uje umuone lini na saa ngapi, na ningeshauri iwe ni swala la kikazi’ akanisogezea karatasi iliandikwa `appointment to……

Nilitaka nisijaze , niondoke, lakini nikaona huo ni utaratibu, na kila ofisi ina taratibu zake. Lakini kumuona rafiki yangu ambaye tulipokuwa tulikuwa chumba kimoja kwenye sekondari ya bweni, na tulishibana sana. Nikaijaza ile fomu, lakini kabla sijaondoka, nikaamua nimpigie simu ambayo niliipata toka kwa mfanyakzi mmoja ambaye alinielekeza kuwa huyo jamaa siku hizi ni bosi hapo. Simu iliita mapaka ikakata, nikajisemea huenda yupo kwenye mikutano yao, siunajua tena mameneja kila mara ni mikutano.

Nilirejea nyumbani nikijutia nauli yangu niliyoipoteza na kukosa kumuona rafiki yangu huyu ambaye tangu tumalize shule pale , yeye akaenda mlimani mimi nikaelekea Mzumbe, hatukuwahi kuoanana naye tena. Nilikuwa na mengi ya kumuelezea, na huenda akanishika mkono, siunajau tena kazi siku hizi ni mkono kwa mkono, lakini wapi.`Ili umuone bosi lazima uwe na ahadi naye, na uapngiwe saa ngapi na nini cha kuongea..aaah,kweli tumekuwa wadhungu’

Siku ya pili nilimpigia jamaa aliyeniunganisha na huyu `bosi-mate’ akasema yeye alimuendea hado ofisini kwake, akiwa katika kazi zake za kiofisi, na hapo alimdokezea kuhusu mimi, na jibu alilopata hakuamini kuwa alikuwa rafiki yangu, tuliyesoma naye na kuishi chumba kimoja kwenye shule za bweni

`Achana na hawa Waswahili bwana, wakisikia upo ofisi Fulani, basi wao wanaleta ushule hapa. Nimesikia habari zake, sina cha kumsaidia najua kakwama..’ alisema huyo bosi huku anatizama katatasi za miadi, na alipoiona karatasi yangu akaiweka pembeni, ikimainisha haina umuhimu kwake.

Siku ya pili nikasikia gari likisimama nje ya nyumba yangu, nilipotizama dirishani sikuamini aliyekuwa akifungua mlango wa lile gari. Ni Yule Yule rafiki-mate wangu. Alikuwa sio Yule nilyemjua, kachana, suti na kitambi cha haja. Alitembea kwa mitao, huku akiangalia kwa dharau jengo ninaloishi.

Nilimwambia mke wangu huyo jamaa akija amuulize kuwa ana ahadi na mimi, na kama hana aandike kwenye kidaftari ili nitafute muda wa kuonana naye. Mke wangu akacheka na kusema hapa ni nyumbani wageni hawana cha ahadi. Lakini nikamukumbusha hii ni ofisi yangu, na mimi nina haki kama yeye akiwa ofisini kwake.

Nilimkaribisha rafikiyangu na alinitembelea kwasababu kasikia maeneo ninayoishi kuna viwanja vinauzwa kwahiyo anahitaji nimsaidia kuhakiki, asije akauziwa kanyaboya. Nilimkumbusha kuwa nina miadi niliyoiweka ofisni ya kukutana naye. Akacheka, na baadaye akapapasa mfukoni na kutoa elifu kumi. Nilishikwa na mshangao, na kumuuliza kuwa ina maana kila mwenye miadi na yeye anampa shilingi elifu kumi. Akacheka kwa dharau akasema hapana najua hali halisi hii ni kwa ajili ya chai kwa watoto. Nikaikataa,lakini akaipitishia kwa mke wangu, ambaye kiuungwana aliipokea.

Haya ndio maisha halisi, tunajifunza nini hapa. Tujadili hili kama linatugusa.

From miram3

No comments :