Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, February 3, 2010

Mdharau Mwiba

 Leo siku ya pili kila nikipita kwa jirani yangu namkuta amekaa kiambazani mwa nyumba yake huku kajiinamia, na kujiinamia kule ni kule kukata tama kabisa ya maisha. Nilimuonea huruma nikidhania ni mmoja wa wahanga wa kukosa ajira, lakini leo nikaona ni heri nisimame nimuulize hali, huenda kuna lilomsibu zaidi ya hilo tunalolizania wengi. Hali kama hiyo unawezi ukamkuta mtu kajitundika kamba na kujiua, kumbe ni tatizo ambalo angepata ushirikiano wa karibu lingetatuliwa.


‘Jirani vipi naona umejiinamia, unatunga sheria nini, au mama watoto kakupa mgongo’ nikamuuliza kwa kebehi, nikijua kuwa ni mtani wangu kwahiyo hata ni mtanie vipi siwezi kutupiwa mawe.

‘We mtani acha tu, kama ni mtihani wa maisha, basi mie niliopewa ni wa chuo kikuu wakati nipo chekechea. Hapa nilipo natamani aridhi ipasuke nizame mzimamzima, lakini mmh, maisha bado nayatamani ndio maana natafakari bila majibu’ akisema kwa kuchanganya na lafudhi ya kwao kuonyesha kuwa hali aliyonayo imemkwaza hadi kusahau kile Kiswahili cha visiwani, kwani wengi walizoea kumuiita mkisiwani badala hasa ya kabila lake kutokana na jinsi alivyopenda kuongea lafdhi ya Kiswahili cha watu wa kisiwani.

‘mtihani gani mtani wewe, usije ukawa umefumaniwa na mkeo kaambiwa na sasa …’ nilisema kiutani na hapohapo akanikatiza .

‘Sikiliza mtani, mie sina tabia hizo za kihuni, mimi nilikuaja hapa Dar kutafuta pesa, nikachuma nikajenga na kuwekeza kama unavyonijua, nikarudi kijijini, wazee wakanikazania nioe, sikupenda sana kuoa, niliona pesa ndio mke-wangu. Aaah, lakini nikaona kuna haja ya kuoa, ila sikupenda masharti ya wazee, wao walitaka nioe mke walionichagulia wao.’ Mtani akaanza kunipa kisa na kunionyesha kwa ishara kuwa nikae karibu naye.

‘Basi mtani, mimi kwasababu nina pesa, nina uwezo nikawaambia wazazi nitatafuta mke anayeendana na mimi, awe amesoma na awe mtoto wa mjini na sio wa huko kijijini. Wazee wakaniasa kuwa wao walinitafutia mke ambaye wanajua tabia na mienendo ya koo na sili yao, kwa ajili yangu na kizazi kitakachozaliwa. Mimi nikawaambia hayo ni mambo ya kizamani.

‘Nikamtafuta mke wa kwanza tukafunga hjarusi ya kukata na shoka, wazee wakaja Dar, wakala na kunywa hadi wakasahau kwao, baadaye wakaondoka. Haikupita mwezi mke yule akawa anaumwa ugonjwa wa ajabu. Kila mara anadondoka anatoa mapofu, anapoteza fahamu. Nilihangaika wee, paka nikakata tama, ikabidi mwenyewe asalimi amri arudi kwao, na hutaamini hali ilimwia mbaya hadi akapoteza maisha.

‘Nikaomboleza weee, baadaye nikasema hata lazima nitafute mke mwingine. Mke wa pili alikuwa chuma, lakini bwana we, akawa kila akibeba mimba inaporochoka, hee nikasema sasa inabidi nirejee nyumbani nikatambike manake imekuwa too much. Hutaamimi mimba ikajipanga vizuri inafikia miezi ya katiokati ikachomoka na mwenyewe akapoteza uhai. Je hali kama hii utasema ni nini hasa.

‘Sasa nimakaa nikawaendea wazazi wanieleze kwanini wananifanyia hivyo, kama ni laana, imeshanifunza kwanini wasiniachie maisha yangu. Nikawapa vidonge vyao, nikawaambia bado sijakoma, nitamuoa nimpendaye si wanaompenda wao. Nikatafuta wee, mwishowe nikampata chotara wa kisomali na kibantu, ndio huyo shemeji yako niliye naye sasa, ingawaje jana kaondoka kwenda kwao. Tatizo, likawa kila akizaa ikifikia miaka miwili mtoto anaumwa, damu inakwisha anapoteza maisha, sasa mtoto wa tatu tatizo linajirudia, nimepoteza pesa, kwa matibabu lakini hakuna kilichopatikana. Nikaenda kwa madakitari bingwa wakasema kuna mgongano wa viasilia. Yaani damu yangu na mke wangu haiendani, na ina maana kwa vyovyote kila tukizaa tatizo litakuwa pale pale. Sasa nimechanganyikiwa.

‘Unajua kwanini, wazee nilipoondoka mara ya mwisho niliwaudhi nikaawambia wasitegemee kuwa nitaenda kuwaomba msamaha na kumuoa binti wanaomtaka wao. Na wakasema asiyesikia la mkuu huvunjika guu. Ni wazee wangu wanafikia kusema kuwa mimi siwasikii, nisingewasikia ningewejengea hekalu kule mlimani….hata, sijui ni laana au ni huko kutokusikia, hebu nisaidie mtani.

Nilimshauri mtani wangu kuwa ni kweli tuendapo hakuna cha ukabila, hakuna cha ukoo upi ni bora na hakuna cha kuchambua undani wa nani ni nani kwasababu dunia sasa ni kijiji kimoja, lakini bado upo utaalamu wa kisayansi kuwa kabla hatujaamua kuwa wapenzi wa undani ni vyema tukaangalia afya zetu, na kama tuna uwezo basi kwanini tusiende mbali zaidi ya kuangalia vitu kama damu kama zinaendana. Sio lazima sana lakini ukiona umeumwa na nyoka lazima utashituka kila ukiguswa na unyasi. Basi ni heri ukatahdhari kabla ya hatari, pima vyote mjue afya zenu. Nilimuacha mtani akitafakari, nahisi huenda akarejea kwa wazee wake na hali ilivyo atarejea na binti wa kijijini kwao!

From miram3

No comments :