Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, February 26, 2010

Mama wa kambo-3

                                             Na kisa cha Msamaria mwema
Ili uelewe vizuri soma sehemu ya pili kwanza


Kisa cha msamaria mwema kilikuwa bado kinaelea kichwani mwangu, nikitafakari yaliyotokea yasije yakanikuta na mimi, kwahiyo niliona nitumie busara kumshawishi Yule mama, nikamwambia; ‘Mama yangu dunia hii ina mengi, sisi tungependa ulale humu kama ulivyoomba, na kesho uondoke, lakini usiku ni mrefu, na hatujui nini mola kapanga, wema unaweza ukageuka kuwa shubiri mama yangu…’

‘Aaah, jamani, usiku mmoja tu,msiwe na wasiwasi na mimi, nimepita kote nikaona nije hapa kwenu, unafikiri kwanini…hili mlizingatie, ninachoomba nikulala kwasababu huu ni usiku nitaenda wapi, na kama mkikataa, basi mimi nitalala hapa hapa nje, au hata chooni…najua kama ningezaa nisingepata matatizo yote haya…nashangaa hata nyinyi mumejazwa uongo mnakubaliana na huyu mtoto wa mke mwenza, muwongo na ana chuki na mimi tu’ akasema huku anatoa machozi

‘Sio hivyo mama, sheria itatufunga pia, licha ya kukosana na huyo jirani yetu, kuwa tumekulaza bila ridhaa yao. Sasa mama unaonaje kama tukienda kwa mjumbe ili atusaidie kwa hili, huwezi jua ya mungu mengi..’

‘Kwa mumbe, kwani mimi mwizi, na swla la kutoke nini kwani mimi nina kifafa, mimi siumwi siwezi kufa, kama ni wasiwasi wenu au mnaogopa nini, kama hamtaki basi ngoja niondoke, na kama nikikutwa kesho nimekufa barabarani, nyie mtawajibika, nimewaomba msaada wa kujistiri angalau usiku mmoja mumekataa, mnafikiri nyie hayatawakuta kama mimi, au kwa vile sina watoto…haya naondoka lakini… ‘ Yule mama akachukua begi lake akaanza kuondoka. Huruma ikanishika, nikataka kumsimamisha lakini mdomo ukashikwa na kigugumizi. Niliwaza kile kisa cha msamaria mwema, nini kilichomsibu baadaye. Hebu tuendelee nacho:-

Mjumbe alipoitwa pembeni na wasamaria wema akawaambia`Huu sio muda wa kuficha kitu, ila busara inahitajika sana, kwanza ngoja nikaongee naye nje, nyie endeleeni kufungua huo mlango, najua kwenye wengi hapaharibi neno, huenda mgeni wenu huyo kazidiwa na usingizi, lakini kama kuna baya, tutajua nini cha kufanya. Mjumbe akachepuka nje na jamaa wengine wakawa wanaendelea kuufungua ule mlango. Mama msamaria mwema akawa anajenga hisia nyingi, zakujiuliza kama huyu mgeni kazidiwa, huenda alikuwa anaumwa, au baya zaidi kama kafa..hapana hajafa, mungui wangu kama kafa…hapana Mungu atuepushie hilo!

‘Mume wangu kama huyu mama kafa tutafanyeje, si tutaishia jela, ina maana wema utatuponza. Unakumbuka yaliyomsibu yula baba mwenye nyumba tuliokuwa tukiishi zamani. Unakikumbuka kile kisa vizuri, si aliishia jela, kwa kisa kama hikihiki. Mungu wangu, mbona hatukukumbuka pale jana tukampeleka kwa mjumbe kwanza.’ Yule mke mtu akaanza kubwabwaja huku anapigapiga miguu chini. Mume mtu ilibidi afiche hisia zake na kumtoa wasiwasi mkewe, kuwa hakuna kitu kama hicho, wao wametenda wema, na kwa vile walichofanya ni ubinadamu haki itawalinda, hata hivyo kwanini wafikiri kitu ambacho hakipo. Kichwani mume msamaria mwema naye akakikumbuka kisa cha mwenye nyumba wao, na kweli kilikuwa sawa na tukio hili.

Baba mwenye nyumba wao, alijiwa na mke wa mpangaji wake, ilikuwa usiku , mke na mumewe waligombana, na ilikuwa ndio kawaida yao!. Yule mke alipoona kazidiwa akakimbilia kwa baba mwenye nyumba, kwani mumewe alimwambia siku hiyo lazima amuue, na nyumba ya mwenye nyuma ilikuwa pembeni kidogo mwa nyumba ya wapangaji. Bila ajizi baba mwenye nyumba akaamua huyo mama alale kwake hadi asubuhi, kwenye chumba cha wageni. Kumbe kila kipigo kilikuwa kikali, Yule mama akafiriki usiku.

Mume mtu akaamuka asubuhu kwenda kazini, akiwa bado na hasiria. Baadaye akapewa taarifa kuwa mke hajiwezi aje haraka nyumbani. Alipofika akaambiwa aende kwa baba mwenye nyumba, ndipo mkewe alipo!

‘Nini, yupo kwa baba mwenye nyumba, mtaniambia vizuri, kwanza nilishamuhisi mke wangu anatembea na mtu mwingine, nahisi ni huyu baba mwenye nyumba, kwanini akimbilie huko asiende kwao au kwa ndugu zangu…ngoja’ akaingia ndani akachukua panga. Watu wakamsihi, lakini hali ikawa ngumu jamaa, kawa mbogo, hadi kwa baba mweny nyuma. Huko alipofika polisi walishafika, kwani taarifa zilishapelekwa mapema na muda huo walikuwa wakimhoji baba maweny nyumba, jamaa hakujali cha polisi akalirusha panga, badala ya kumpiga baba mwenye nyumba, polisi aliyekuwepo karibu aliliona na kujaribu kumuokoa baba mwenye nyumba, na bahati mbaya likashukia kwake.

Polisi wengine wakaja kusaidia, na kilichosaidia ni pale mmoja aliposema, `wewe badala ya kusikiliza nini kimetokea unapigana, unataka utuletee misiba mingine, mkeo kafa nawe unataka kuua, nini unafanya..’

‘Mke wangu kafa, unasema nini, hata mtanieleza, vizuri, wewe baba mwenye nyuma…aaah, hapana mke wangu kafa..’ ikawa nguvu zimemuishia jamaa, na pingu zikatinga mikononi, yeye na baba mwenye nyumba wakapelekwa polisi. Kesi ikawa ndefu ajabu, baba mwenye nyumba akatiwa hatiani kwa kutokufuata sheri na mume mtu kwa kujeruhi na kusababisha kifo cha mkewe na pia kushambulia kwa silaha na kumjeruhi polisi.

Baba msamaria mwema alipofika mwisho wa kisa hiki cha baba mwenye nyumba wake aliinua mkono juu na kuomba , aliomba yasije yakamkuta makubwa, aliomba akijua kesi kama hii itamgharimu sana, naye yupo katika hali ngumu ya kimaisha, mtoto wao anaumwa anahitaji matibabu, walikuwa wanajadili wapi wakapate msaada saa lizuke kubwa kama hilo itakuwaje. `Ewe mola tuukoe na janga hili’

‘Mke wangu tusubiri mlango ufunguliwe, najua rafiki yetu atatuelewa, kama alimtimua kwake alitegemea akalale wapi, polisi au wapi..’ akasema mume mtu.

From miram3

No comments :