Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, February 3, 2010

Haya sio mapenzi

Nililisogelea lile jumba, geti jeusi na juu kulizungushiwa seng;enge zilizotegeshwa umeme, na tahadhari iliwekwa kuwa nyumba hiyo inalindwa na vifaa vya umeme. Nililisogelea lile geti na bahati nzuri nikakiona kitufe cha kugongea kengele, nikakibonyeza. Nilisubiri dakika mbili, nikakibonyeza tena, kimya. Niliingiwa na wasiwasi, huenda sikumkuta rafiki yangu huyu, ingawaje aliniahidi kuwa siku za Jumapili haondoki nyumbani.


Nikiwa nimekata tama, mara nikasikia mngurumo wa gari ukija kuelekea kwenye lile geti, name nikasogea pembeni. Alieyekuwemo mle ndani alipiga honi mara tatu na mara geti likafunguliwa. Mlinzi akiwa na sare za kimgambo aliharakisha kuliweka geti vizuri na baada ya gari kupita akasogelea ule upande niliposimama, akaniuliza nina shida gani.

`Nilikuja kumuona mwenye nyumba hii, ni rafiki yangu sijui kama yupo?’ niliuliza. Na cha kushngaza yule mlinzi akaniangalia kutoka utosini hadi chini, akarudia mara mbili, halafu akageuka akaondoka kufunga lile geti. Nilishikwa na butwaa, lakini sikukata tama, nikaamua kutumia njia nyingine. Nilikuwa na simu ya huyo rafiki yangu nikampigia, akasema nisubiri anakuja, na mara geti likafunguliwa.

`Mna ulinzi mkali kweli, mnajihami nini hivi?’ nilimuuliza rafiki yangu ambaye aliishia kucheka, na kusema hayo ni mambo ya kawada. Na tulipofika ndani akanitambulisha kwa mkewe amabye alisema aliniona wakati anaingia lakini hakuja kuwa mimi ni rafiki wa mume wake.

‘Samahani sana shemeji , sikujua kuwa aunakuja kwetu, karibu jisikie nyumbani.

‘Mama, nataka maji ya kunywa’ Mtoto wa miaka saba hivi alimwambia mama yake, na mara mama akabonyeza kitufe fulana, akaja dada mmoja akaambiwa ampe mtoto maji. Na mtoto alipokunywa akawa amejimwagia na kuanza kulalamika kuwa nguo zimelowana. Mama yule akafanya kama mwanzo alipokuja yule binti akaambiwa ambadilishe yule mtot nguo. Na mara likatokea hili, na lile kuhusiana na mtoto ikawa kila mara anaitwa mtumishi wa nyumbani. Ilifikia hatua tukawa hatuongei, ni kumsikiliza yule mtoto, mapaka mimi mwenyewe subira ikaniishia.

‘Unajua rafiki yangu, siku moja tulikuwa nyumbani na babu yangu, tulikuwa tunategea kazi tuliyopewa ya kuchota maji. Maji hayo tulikuwa tukiyafuta mbali kidogo. Na kwa nje wakaoneka watoto wakipita na ndoo za maji. Watoto hawa baba yao anauwezo, kwenye kijiji kile alikuwa ni miongoni mwa waliojaliwa kuwa na hali nzuri, nyumba nzuri, umeme, na maji, lakini wakati mwingine maji yanakatika. Cha ajabu ambacho tulimuliza babu ni kwanini pamoja na uwezo wao wote, lakini watoto wa nyumba ile walifanya kazi kama mchwa. Hawakujali utajiri wa baba yao, walifuata majani ya ngombe kama sie, walichota maji wenyewe na wala hawakuwa na mtumishi ndani…’

‘Huo ni ubahili tu, kama wana uwezo kwanini wawatese watoto, inaonyesha hawana upendo kwa watoto’ alinikatiza shemeji yangu.

‘Babu yangu alisema, mtoto ni sawa na maji akiwa bado mtoto, lakini akiwa mkubwa ni sawa na plastiki inayovunjika. Alisema muda wa kumweka mtoto vizuri ni muda akiwa mdogo, na hapo ndipo anaweza kuijenga fikira yake kinamna utakavyomuelekeza. Ukakamavu wa akili, ujasiri heshima na adamu ni wakati mtoto akiwa mdogo. Babu yangu alituasa kuwa ukitaka kumpenda mtoto wako usimdekeze. Kumdekeza mtoto sio upendo, ni kumharibu na huyo mtoto akikua kama atapata matatizo kutokana na kudekezwa huko atakuwa akikulaumu wewe kuwa ndio chanzo. Na kumweka mtoto katika ujasiri wa kufanya kila kazi, hata kama mtoto atalalamika kwa muda ni tunu na ni akiba ya huyo mtoto pindi akiwa mkubwa.

‘Shemeji, ni sawa uongeayo, lakini yote hutegemea wakati, na uwezo, kama mna uwezo kwanini umtese mtoto. Mimi mwanangu sitamtesa kabisa kama bado nina uwezo’ alisema shemeji yangu, lakini rafiki yangu kila nililoongea aliniunga mkono, lakini ilionyesha wazi hana cha kusema mbele ya mkewe.

Baada ya maongezi niliaga, lakini nilimuonea huruma sana yule mtoto. Nilimuonea huruma kwasababu malezi yale hayakustahili hivyo, kwa umri kama ule, alihitajika kujituma baadhi ya kazi, inashangaza hata maji ya kunywa hajui ayapate vipi, chhoni mapaka apelekwe, anawishwe,… jamani wazazi tusihadaike na uwezo, tukawaharibu watoto wetu tukijifanya tunawapenda. Huo sio upendo kabisa, huko ni kumharibu mtoto.

From miram3

1 comment :

Anonymous said...

Huko kunaitwa kudekeza, sio mapenzi kabisa