Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha
Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..
Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.
MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.
TUPO PAMOJA DAIMA
![]()
Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;
https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:
https://www.facebook.com/diaryyangu/
`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;
Thursday, December 8, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-60 Hitimisho-4
‘Shangazi sasa mbona tumepoteza muda wetu bure kuja hadi huku nchi za watu, haya huyo mgonjwa mwenyewe yupo wapi, maana hata hilo jina lenyewe ukiwatajia hawa manesi wanaishia kutucheka tu, Sweetie, unajua hilo jina linanikumbusha mbali sana, sijui masikini Mhuja yupo wapi, au ndio ilikuwa ndoto y ajinamizi,..shangazi ilikuwaje siku ile, mbona kila nikikuuliza mswali kuhusu siku ile unanipiga chenga, au ilikuwa ni ndoto …?’akauliza Maua.
‘Tatizo lako una tamaa ya mambo mengi, mimi nahisi ilikuwa ni ndoto, kama sio ndoto, huyo mtu yupo wapi, siku ile tumekwenda sote hadi nyumbani kwao Mhuja, uliambiwa nini…..?’ akauliza shangazi mtu.
‘Waliniambi nisiwaletee uchuro, kwani wao wameshasahau , na nimeamua kuolewa basi, hawanijui tena….lakini yule aliniambia kiutani maana nataniana naye sana…’akasema Maua.
‘Ndio hata kama mnataniana naye sana, iweje wewe umuone wao wasimuone, ina maana aliamua kuja kwako tu, bila kuwajali ndugu zake, hebu jiulize mara mbili,tatu…’akasema shangazi huku akimkwepa kuwamgalia Maua usoni, maana hata yeye mwenyewe aliachwa njia panda, kwamba, huyo mtu alikujaje pale kwenye harusi bila kupitia kwake, na baada ya hapo alikwenda wapi, ..
‘Kama ni jinamizi basi hilo ni la mwaka, huwa namuota , lakini ile nina uahkika sio ndoto, labda alikwua ni yule Tajiri alijibadili na kuja kwa umbo lake ili niteseke, ..hata hivyo, sio mbaya kumuona tena sura yake, natamani aje tena…’akasema Maua.
‘Acha balaa lako, wewe siulisema ulikuwa karibu kuzimia, …unafikiri mchezo wewe, ukutane na mtu ambaye alishakufa, uso kwa uso, utaweza kuhimili vishindo vyake wewe, acha kuinidanganya wewe…hebu tukasubiri pale kwenye kiti.
‘Sasa tunasubiri nini tena, mimi naona turudi nyumbani kwetu, hapa naona hakuna cha mgonjwa wala nani, kwanza mimi nashindwa kujua nitaongea nini na huyo askari.
‘Wewe subiri, Inspekta akija tutajua utaonea nini na pia tutajua huyo mgonjwa kaenda wapi, siunajua hizi hospitali za serikali zilivyo, wanapokea wagonjwa wengi, na inategemea huyo mgonjwa alipokelewa na nani…’akasema Shangazi huki na yeye akiwa na mawazo mazito, kwani kama huyo mgonjwa haonekani kwenye wodi aliyoelekezwa basi kna mawili, kapona karuhusiwa au vinginevyo yupo chumba maalumu..hakutaka kukitaja hicho chumba maalumu ni chumba gani, akaishia kuomba mungu sisije ikawa hivyo.
********
Walipofika uwanja wa ndege. Inspekta yeye alichukuliwa na gari lao la kazini , na shangazi na Maua wakaelekezwa hospitali ilipo, kwani shangazi hakupenda kupelekwa kwenye maeneo ya jeshini ambapo maaskari wana nyumba zao, alipenda kutafuta chumba chake mwenyewe, na likuwa na sehemu yake maalumu anapofikia..
‘Mimi sio mgeni wa hii nchi, nimefanya biashara sana huku, na nina wenyeji wengi, ngoja sisi twende huko hopitalini, utatukuta huko…’akasema shangazi na wakaingia kwenye taksii hadi kwenye hiyo hospitali waliyoelekezwa, walipofika wakaingia hadi sehemu ya mapokezi….
‘Mnasema mgonjwa wenu anaitwa nani.?’ Akaulizwa tena.
‘Nasikia ameandikisha kwa jina la Sweetie..’akasema shangazi.
‘Hilo jina ..mbona geni kwangu, …mwanamke kama sikosei maana …’akasema yule mtu wa mapokezi huku akitafuta katika orodha ya majina.
‘Hakuna jina kama hilo, …’akasema huyo mtu huku akisumbuliwa na watu wengine, na kila alipopata muda alijaribu kutafuta hilo jina bila mafanikio, baadaye akauliza `huyu mgonjwa wenu anasumbuliwa na matatizo gani, na yupoje?’ akaulizwa shangazi na huyo mtu wa mapokezi, na hapo shangazi alishindwa aelezee vipi, licha ya kuwa hisia zake zilikwua zikimtuma kwa mtu fulani. Alikumbuka siku ile ya harusi alivyopata ile taarifa ya juu juu, lakini hakuwa na uhakika nayo sana, ila hisia zake zilimtuma kuwa huenda ndiyo yeye, na angelipenda kujua hatima yake, na kama sio yeye, bado ana mambo mengi ya kufanya , hasa swali analouliziwa na binti yake Maua.
‘Tumesikia kuwa anasumbuliwa na matizo ya kichwa…’akasema shangazi bila ya uhakika.
‘Basi nendeni word namba tisa, kule mnaweza mkasaidiwa zaidi…’akasema huyu mtu wa mapokezi na kuwafanya shangazi na Maua waondoke pale bila mafanikio na wakiwa wamekata tamaa, mara Inspekta akafika;
‘Samahanini sana, kwanza kwa kuwakalisha kwa muda mrefu, lakini hata hivyo, taarifa zilizotujia kule kumbe hazikuwa makini, maana huyo mgonjwa hali yake ilikua mbaya sana, na alipofikishwa hapa, wakawa hawana la kufanya, juhudi zai zikagonga mwamba, …’akasema Inspekta akionyesha uso wa huzuni.
‘Kwani huyo mgonjwa aliandikisha jina gani..?’akauliza Maua.
‘Rose,….’ Inspekta ikamwangalia Maua kwa makini, kuna utata mwingine ambao nataka tuongee kwanza mimi na wewe, maana naona, kuna maelezo nimeyapata, nahisi kuna jambo limekosewa, na wewe ndiwe wa kunipa huo uhakika, …twendeni ofisini kwangu kwasababu hapa hakuna la kufanya tena…’akasema Insepkta.
‘Hakuna kufanya , vipi tena, mbona hujatumalizia kuhusu huyo mgonjwa, amefariki au imekuwaje..?’akauliza shangazi kwa sauti ya huzuni.
‘Alivyochukuliwa hapa, ni kama nusu mfu, hatujui huko alikopelekwa hali yake inaendeleje, watu wetu wanajaribu kuwasiliana na huko, ili kujua hali yake,kwani hata hivyo, hawakuwa na shauku naye sana, hadi , mimi nilipowaomba kufanya hivyo, .. lakini mawasiliano hayapatikani…’akasema Inspekta.
‘Kapelekwa wapi..?’akauliza shangazi
‘Kapelekwa India,..matatizo aliyokuwa nayo ya kichwa, yanahitaji upasuaji wa haraka, na hata hivyo alishacheleweshwa sana..sijui itakuwaje,…’akasema inspekta.
‘Sasa kwanini hawakumuwahisha mapema..?akauliza Maua.
‘Siunajua tena, hali ya kifedha, wakipatikana wagonjwa kama hawo ni mpaka kutokee wafadhili, na hata hivyo kwa kesi yake, haikuwa wazi sana,…na alipokamatwa, kwa vile maaskari hawakujua kuwa ana tatizo la kichwa, wao wakamperekesha, na nahisi ndipo walipotibua tatizo hilo, ..’akasema Inspekta akionyesha kuficha jambo .
‘Kwahiyo kosa ni la hao maaskari na tuseme ni kosa la serikali, kwanini walipogundua hilo wasifanye taratibu za haraka za kumsafirisha huyo mtu, mpaka afikie hali hiyo mbaya..?’akauliza Maua kwa hasira.
‘Huyo mtu kwanza haongei, hajijui,…yaani ilishindikana wapi pa kuanzia, lakini kama isingelikuwa fungu lililoachwa na Adam, na kukaja taarifa kuwa hizo hela zitumike kumsafirishia huyo mgonjwa , yangezungumzwa mengine, kwasababu historia ya huyu mtu haijulikani, na kuna watu wengi wanahitajika kusafirishwa kwenda huko kabla yake,, na kutokana na hali yake ilivyo ya kukatisha tamaa na historia iliyojengwa kuwa huenda ni mmojawapo wa wapiganaji wa msituni, ambaye alikuwa akitumia mbinu kujifanya hana fahamu huku anachukua habari na kwuasiliana na wenzake…basi kesi yake ikawa ya kupigwa danadana, huku wakisubiria kuwa ajifie ijulikane moja…’akasema Inspekta.
‘Jamani watu war oho mbaya, yaani mnasema kabisa ajifie ijulikane moja, ..’akasema Maua.
‘hayo ndio maisha,..nanihii..Rose, nitakuita hivyo hivyo..’akamwangalia Maua kwa makini , halafu akasema `lakini kila mtu na siku yake, keshapelekwa India, na kuna mambo mengi yametokea huku, na vijana wangu hawakuishia hapo , wamegundua mengi zaidi na ndio maana nataka kuongea na wewe,…Rose,..’akasema Inspekta huku akisita kulitaka hilo jina Rose, hata Maua akahisi kuwa huenda keshagundua kuwa yeye sio Rose, na ndilo alilolihitaji sana, hakupenda kuitwa majina ya watu wengine.
Shangazi alipogundua hilo akasema haraharaka, ‘Huwezi kuongea na yeye peke yake, inabidi kama nikuongea uongee nikiwepo, huyu ni mja mzito na namjua mwenyewe hali yake, pili sizani kama unamfahamu kama ulivyodai…kuna mengi yanahitaji uwepo wangu, usije ukamwanga mtama kwenye kuku wengi,…tafadhali sana’akasema Shangazi, na Inspekta akamwangalia Shangazi kwa makini halafu akageuka huku akiwaza jambo.
‘ Sio mbaya nimekuelewa, ndio maana nataka kuongea naye, kwani huenda kuna makosa ya utambuzi …hilo sasa nimeligundua..ok, sawa ni vyema, maana wewe kama mzazi utakuwa unajua zaidi , lakini kumbukumbu zote nimeshazipata toka ofisini, ila ni kwa vipi ilitokea hivyo…kweli utanisaidia wewe kama mzazi,sio mbaya…twendeni ofisini kwangu..’akasema Insepkta.
‘Kabla hatuajenda huko ofisini kwako , kuna mtu nataka kuonana naye, na kupata sehemu ya kukaa, sipendi kukaa maeneo yenu, siyaamini sana ..’akasema Shangazi.
‘Kama huamini sehemu za walinzi wa taifa, utaamini wapi tena, sawa najua unataka kuonana na nani…lakini kwa taarifa yako hayupo …nimeshajua kuwa ni nani..au nimekosea?’akasema Insepkta kwa kuuliza lakini ilionekana hakutaka jibu la hapo hapo, akijua kuwa bado hajawa na uhakika na hilo analoliwazia.
‘Sawa vyovyote iwavyo , lazima nifike hapo nilipokuwa nikifikia, sizani kwamba nitazuiwa, kwasababu yule mlinzi pale najuana naye sana, na tukitoka hapo tutakuja huko ofisini kwako…’akasema shangazi
******
Walipofika kwenye nyumba moja kubwa iliyozungushiwa ukuta, walikwenda moja kwa moja kwenye kibanda cha mlinzi, na huyo mlinzi alionekana kachoka, na usingizi ulishampitia, na walipogusa mlango tu, yule mlinzi akainuka haraka, na kuwakabili kwa,maswali, kuwa wao ni nani na wanahitaji nini. Shangazi akajielezea, na yule mlinzi akawaambia kuwa mwenye nyumba hayupo, waliopo hapo ni wapangaji tu, hana zaidi la kwuasaidia.
‘Naomba namba yake anayotumia sasa hivi, maana ninahitaji kuwasiliana naye…’akasema shangazi huku akimsogelea yule mlinzi, ili amgundue kua ni nani yeye.
‘Siwezi kukupa namba yake , bila kukujua , ..kwani wewe ni nani, ….’akasema yule mlizi na kuwamgalia shangazi sasa kwa makini, na alipogundua macho yakamtoka kwa furaja na kusema kwa sauti `Ooh, nimekukumbuka, samahani sana, siku nyingi kidogo, habari za Tanzania, habari za nyumbani, maana mimi sijfika huko nyumbani muda sasa, siunajau tena kazi zetu hizi…’akasema yule mlinzi kwa furaha.
‘Wewe kama umeama kuukana utaifa wako na kuwa mtu wa huku sio mbaya,… sawa, lakini kwenu ni kwenu tu, ipo siku utarudi tu kwenu, hata ukiwa ndani ya sanduku…’akasema shangazi , na wakati huo Maua alikuwa kajichokea na alikuwa akitafuta sehemu ya kukaa, akasogea mbele kwenye kiti na kukaa huku akishika mgongo,alikuwa kachoka na safari na bado kuna mambo yanayoendelea ambayo hayajui kichwa wala mguu, na mapaka muda huo hakuwa anajua nini kinaendelea, anakokotwa tu kufuata shangazi yake anavyotaka.
Alipokaa pale kwenye kiti, mawazo yake yakawa yanamkumbuka Maneno, na alipokumbuka hivyo , roho ikatibuka karibu atapike,…alimkumbuka pale alipompa taarifa kuwa wanasafari ya kwenda nchi ya jirani, ilibidi amuachie jukumu hilo shangazi yake, maana hata yeye mwenyewe hakuelewa vyema msingi wa hiyo safari, na hata alipoulizwa maswali mengi akashindwa kujieleza.
‘Kuna ndugu zetu wapo huko Uganda na mmojawapo tumesikia hali yake ni mbaya sana, tunahitajika tondoke kesho, na bahati nzuri kuna lifti ya polisi, kwahiyo usijali mambo ya gharama kuhusu hiyo safari..’akasema shangazi mtu.
‘Lakini huyu mke wangu,kusafiri nisingelipendelea, hata wewe shangazi unajua hali yake ilivyo, ya utata utata…’akasema Maneno.
‘Hilo usijali , kama nikiwa naye karibu usitie hofu, wewe huoni, muda wote ananihitaji mimi, sasa nikiamua kuondoka mwenyewe, ukabakia naye hapa, kwanza atabakia na wasiwasi, pili utashindwa hata kufanya hiyo kazi yako,kwa jinsi atakavyokusumbua…na ni vyema nikamtambulishe kwa ndugu zake wengine ambao hawajui wanaoishi huko Uganda, usitie shaka…’akasema Shangazi mtu, na Maneno hakuwa na upingamizi , wakaruhusiwa.
‘Twende ndani Maua, tutakaa hapa hadi hapo tutakapo rejea nyumbani, ‘akasema shangazi na kumkatiza Maua kwenye dimbwi la mawazo yaliyokuwa yameanza kujijenga kichwani.
‘Tutakaa hapa , kwanini tusikae hotelini, kwani hapa ni kwa nani..?’akauliza Maua akiwa kama mtu aliyetoka usingizini.
‘Utajua hilo baadaye, kwanza twende ndani…’akasema shangazi mtu.
Na wakati huo huo yule mlinzi akawa kamsogelea Maua kutaka kumjua kuwa ni nani, na alipomwangalia akaishia kushika mdomo kwa mshangao akasema;
‘Duuh, unajua nilikuwa sijamwangalia vyema, huyu..ooh, Rose, hapana, ….mbona utata…Rose umerudi lini toka Ulaya, haiwezekani, …wewe mtoto, mbona unafanya vibaya, hata vizawadi, halafu unakuja hapa unajikausha, mpaka, mama wa watu anajitambulisha kama mgeni…wewe, wee, halfu umeacha ule uzungu wako…eeeh, umeoelwa nini…?’akasema yule mlinzi akimwangalia Maua kwa makini, lakini shangazi hakumpa muda wa kusema kitu, akamshika Maua mkono na kuingia naye ndani.
‘Shangazi huyo Rose ni nani…maana karibu nimtapike huyo mlinzi, hivi kwanini hawa watu hawaelewi kuwa nina `aleji’ na wanaume..’Maua akauliza kwa ukali.
‘Hiyo mimba ina kazi, …kwahiyo unazania kila mtu atajua kuwa mimba yako haipendi wanaume, …na kuhusu hilo lako na mengine tutayamaliza huku huku, usitie shaka, lakini kila kitu kwa muda wake, usilazimishe, nafanya hivyo kwasababu maalumu, wewe vuta subira.
nb Bado tupo kwenye hitimisho swali kubwa hapa kwanini wanamuita Rose, Maua?
Nani anaweza kukisia?
Ni mimi: emu-three
Wednesday, December 7, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-59 hitimisho-3
‘Mimi sikuja hapa kwa ajili ya ule ugomvi wetu, yale yalikwishapita, na haki yako ulikwisha ipata, na kuja kwangu hapa sikujua kabisa kuwa nitakutana na wewe, kumbe huyu binti ni wa kwako, namfahamu sana, …’akaongea Inspketa akimwangalia Maua.
‘Ulimjulia wapi binti yangu, maana nyie maaskari hamna dogo, huyu ni mke wa mtu na nina hamu sana ya kusikia jambo lililokuafanya uje kwa binti yangu huyu ana kosa gani hadi umtafute, …?’akasema shangazi mtu akimwangalia huyo askari kwa macho ya mashaka.
‘Usiwe na shaka kabisa, binti yako nilionana naye huko nchi ya jirani katika shughuli zangu, nilikuwa huko kwa mkataba maalumu, na katika utendaji wangu ndipo nikakutana naye, ila kila muda unaopita naingiwa na wasiwasi kuhusiana na yeye, maana habari niliyoipta huko kwa mara ya mwisho ni kuwa Rose kaenda Ulaya kusoma, na hata siku za kesi hakuweza kuonekana, na cha ajabu hata mumewe alitoweka kiajabu, kitu ambacho kiliwafanya washukiwe kuwa wana uhusiano wa namna fulani, au kuna jambo ambalo wanalijua na linaweza kusaidia kulimaliza kabisa hilo kundi. Kundi hilo ni hatari hata kuloko wapiganaji wa msituni….’akasema Inspketa.
‘Kundi gani hilo maana sijakuelewa unaongea nini na binti yangu anahusikanaje na kundi hilo…?’akauliza shangazi mtu akiwa na wasiwasi kidogo.
‘Huko nchi ya jirani kuna makundi mengi yanayoipinga serikali, kuna makundi yaliyopo msituni, lakini kuna makundi yaliyokuwa yameandaliwa kitaalamu, kiasi kwamba ilikuwa ni vigumu sana kuyajua,…haya yalijengwa na wataalamu wa Nyanja mbali mbali. Nikisema wataalamu nina maana kuwa ni watu wafanyakazi na nyazifa zao, kwa upande mmoja, lakini kumbe ni watu waliojifunza upiganaji kwa upande wa pili.
‘ Huyu mgunduzi wa makundi haya, ambaye ndiye mfadhili mkubwa alikuwa akiishi nchi za nje, alibuni njia hii mapema kabisa, akatuma wataalamu na silaha, na alichofanya ni kuwakuasanaya wale watu alioona wanafaa akawapika kisawasawa na pia kuwafunza vijana wengine toka vyuo vikuu, ambao walipomaliza masomo yao waliajiriwa na huku wanakujua jukumu lao jingine.
‘Kwa mfano binti yako alikuwa kaajiriwa katika hospitali mojawapo ya watu hawo, anaijua vyema sana, lakini hakujua nini kinachoendeela hapo, sizani hadi hatua ya mwisho kama alijua kuwa kuna watu kama hawo, kwani ilikuwa ni siri kubwa sana, na sisi tulipogundua hilo tukaamua kumfanya yeye kama chambo…’akasema inspekta huku kakunja nne kwenye kiti.
‘Maua alikuwa akitaka kuingilia yale maneno, lakini kila mara alipotaka kutamka kitu shangazi alimwahi na kumuonyesha ishara ya kutulia. Na inspekta bila kujua kuwa anamwaga mama kwenye kuku wengi akaanza kueelezea mambo yalivyotokea huko nchi jirani, akiwa kama mkufunzi na mtaalamu aliyepekwa kusaidia kuleta amani nchi ya jirani.
*******
Mkuu wa ile hoteli alijikuta akiingia kwenye mapigani ndani ya hoteli yake mwenyewe, kinyume na makubaliano na muajiri wake, ambaye alishapata taarifa kuwa bosi wake huyu ambaye ni mumiliki wa hiyo hoteli yupo njiani kuja hapo, aliona ni bora kuliingilia kati hilo tatizo na kuhakikisha kuwa bosi wake akija mambo yamekwishatulia, hakuwa na jinsi....
Akawa anawasiliana na Inspketa akiwa kwenye mitambo yake, kwani kundi hilo liliamua kuleta wapiganaji wake ili kujibu mashambulizi baada ya kusikia kuwa kuna watu wao wamenaswa humo ndani na hawo jamaa wakikamatwa siri kubwa itakuwa imefichuka. Kitu kilichogundulika ni kuwa kundi hilo lilimuhitaji Rose na mwanaume anayesadikiwa kuwa yupo naye,…na kitu ambacho kilihitajika ni kujua kwanini Rose na huyo mume wake walikuwa wakihitajika sana, na hawo watu, ndio maana binti yako anahitajika na mume wake.
Ndani ya hiyo hoteli kundi hilo lilipandikizwa watu wao, ambao kazi yao kubwa ilikuwa kuchunguza chumba baada chumba, kama watawakamata hawo watu wanaowatafuta. Ni wakati huo huo kundi letu la serikali la vijana waaminifu nalo lilishawaingiza wapiganaji, cha jabu vyumba vingi vilishachukuliwa, lakini haikutushinda kitu, licha ya kuwa asilimia kubwa ya vyumba humo ndani vilikwa vimeshikiliwa na wao.
Ndani ya chumba maalumu ambacho kilikuwa kikitafutwa ndipo walipokuwepo Rose na mtu wake, ambaye kwa Inspkta alimtambua kama mume wa Rose, na hapo alishaweka watu wake kwa ajili ya kumsaidia mkuu wa usalama wa hiyo hoteli baada ya kuwasiliana, na baadaye iliwashangaza kwani walipoingia humo chumbani, walimkuta Rose kalala, na mwenzake hayupo.
‘Rose vipi mumeo yupo wapi, maana anatafutwa na hawa majambazi..’akaulizwa Rose na Inspekta.
‘Sijui, nilipitiwa na usingizi baada ya kukesha naye usiku kucha, akiwa kazirai, nilihangaika naye bila matarajio lakini sikuwa na jinsi ya kufanya, kutokana na hali niliyoiona huko nje, …lakini alionyesha dalili njema, ndio maana sikuwa na wasiwasi sana..sijui kenda wapi mungu wangu...…’akasema Rose akiwa na wasiwasi akitaka kutoka nje,lakin wale maaskari walimuia, na msako mkali ukapita bila mafanikio ya kumuona huyo mume wake...
‘Huko nje mapigano yakazuka, kwani hawo jamaa hawakukubali kusalimu amri, na haikujuliakan wapi walipopata silaha kwa mara ya kwanza, na hili liligndulika baadaye kuwa miongoni mwa maaskari tuliowaamini walivujisha siri na alipoingia yule mumilikia wa hoteli baadaye, akawa anawasiliana na watu wa kwetu kinamna ambayo hatukuelewa mwanzoni, lakini hata hivyo ilitusaidia kumnasa mtu mmojawapo mkubwa aliyekuwa ndani ya serikali…hilo siwezi kuwaeelzea zaidi …
‘Jinsi silaha zilivyopenya ilitutatizo kidogo, lakini baadaye tulimnasa kijana wa kwetu ambaye alitumiwa na watu hawo, akapenyesha silaha na kuingia mikononi mwa hawo majangiri, na ilikuwa kazi kubwa sana, ikizingatiwa kuwa hawo jamaa waliiva kwa vita, sio mchezo, lakini tuliwashinda kwasababu walikuwa wachache na walizingirwa ndani ya jengo,na tukawshika mmoja baada ya mwingine, na walikaidi wapambana na mkono wa sheria…’akasema Inspekta.
‘Sasa huyo mume wa Rose alitowekaje, asionekane…?’akauliza shangazi.
‘Mwanzoni tulizania kuwa Rose anajua wapi alipo, lakini tulipofatilia mitambo yam le ndani tuligundua kuwa alizindukana wakati Rose kalala, na alionekana kama kuchanganyikiwa hivi , kwani alipoamuka aliangalia huku na kule na alipomuona Rose kalala karibu naye akamwangalia kwa makini, na bila kumwamsha akatoka mle ndani, …alipofika nje na kusikia milio ya bunduki alirudi na kuvaa koti refu na kofia, na kutoka bila hata mti kumjua…’akasema Inspekta .
‘Hapo sijapaelewa, atoke katika hali kama hiyo bila kujulikana, halafu akaenda wapi?’ akaluiza shangazi akiwa na hamu ya kusikia zaidi, kwani alikuwa kama anahadithiwa cinema fulani anayoipenda.
‘Pale ilikuwa rahisi kwake kutoka, maana mtu kutoka mle walipokuwa wamefichwa ilikuwa ni rahisi, kwasababu hakuna aliyekuwa akijali,mtu anayetoka , ila kuna kauzembe kalifanyika kidogo, walinzi wetu walikuwa wakihakikisha kuwa hakuna mtu anayeweza kuingia, na kwahiyo alipotoka, walihisi kuwa ni mimi, niliingia na kutoka kwa njia hiyo, na alipotoka akatoweka kinamna, na hakuonekana hadi aliporejea wiki liyopita wakati nikiwa huko na wakamkamata, sikuwa na jinsi ya kufanya, kwasababu na mimi nilikuwa nahitajika huku nyumbani,….’akasema Inspekta.
‘Na huyo Rose walimfanyaje, maana hujaniambia vyema kuhusu yeye..’akauliza shangazi na kumwangalia Maua. Na inspekta naye akamwangalia Maua na kutabasamu akasema;
‘Binti yako ni mjanja sana, kwa kipindi kifupi nilichofahamiana naye , niligundua kuwa ni mtu jasiri licha ya fani yake ya udakitari, lakini ni mtu anayeweza kupambana kama askari…unajua hapa nilipo ninashindwa kuamini, kwani hapa kabadilika kuliko maelezo, kiasi kwamba nawaona kama watu wawili tofauti, sijui…’akasema Insepkta huku akimwangalia vyema Maua na kumlinganisha na yule binti aliyekuwa naye akiwa na nywele kama za mzungu.
‘Wewe mwenyewe umekiri kuwa yeye ni jasiri, na uajsiri hasa wa kupambana na watu inabidi ujiabdili kutegemeana na watu, haya nieleze ilikuwaje baada ya hapo?’ akasema shsngazi mtu.
‘Zaidi ya hapo askari wakalivamia lile jengo na kuwakamata wote waliohusika, hutaamini kuwa mumiliki wa hiyo hoteli alikuwa mshirika wa karibu wa huyo mkuu wa hilo kundi, …alipofika uwanja wa ndege vijana wetu walimuona wakawa wanamfuatilia, bila yeye kujua, na hakufika moja kwa moja hotelini kwake, alifikia hoteli nyingine, ambayo kumbwa na mumilikiw ake anahusika pia, humo waliweka kambi ya muda, ilikuja kugunduliak silaha nyingi kwenye hiyo hoteli.
‘Huyo mumiliki alipotoka hapo alikuwa kajibadili sura, na kuingia hotelini kwake kama mtalii tu, na alipofika kwenye chumba alichopewa, akaanza shughuli zake za kuwasilina na wenzake, huku akitoa amri za mapigano, kazi ikaanza, lakini kwa vila tulishajiandaa, haikutupa shida kabisa,na tukaja kumnasa kirahisi, ila alikaidi na kwenye mapigano na kupoteza uhai….’akasema Inspekta huku akiangalia saa.
‘Na kwa Rose ilikuwaje, maana hujaniambia kuhusu yeye..?’akauliza shangazi.
‘Ina maana hajakuambia mwenyewe, nini kilitokea, …?’ akasema inspekta na simu yake ikawa inaita, …akaipokea na kusikiliza kwa makini, halafu akamwangalia Maua.
‘Hali ya mume wako ni mbaya sana, wamemtoa kule jela alipokuwa kaweka na sasa hivi kalazwa hospitali ya serikali, ….’akasema Inspekta, `Na kuna kitu wamekigundua, kuwa huyo mume wako aliwahi kulazwa tena hapo akiwa na tatizo la kichwa, tatizo hilo limeongezewa alipokuwa huko jela, kama ilivyo kawaida ilibidi watumie njia za ziada kupata taarifa walizozitaka, ingawaje haikufanikiwa kwani wakati wanahangaika naye akapoteza fahamu na hakuweza kuzindukana kwa muda wote waliokuwa naye, ikaonenakan haina haja ya kuendelea kukaa na mtu kama huyo, wakati ahwana vifaa zaidi …ndio wameamua kumtoa hospitali ya jeshi na kumpeleka hospitali ya serikali.
‘Mara ya kwanza alipolazwa walijua kuwa alitokea wapi na jina lake mnalijau kuwa ni nani? ‘akauliza shangazi.
‘Hilo ndilo tunataka kuongea na binti yako, najua wanajuana walikutana wapi, kwani uchunguzi uliofanyika haujagundua wapi huyu mtu alitokea, kwani kipindi kingi alichokuwa kalazwa, alikuwa hana kumbukumbu, …na cha ajabu hata Rose hakuwahi kuandikisha jina sahihi la mume wake, alitumia jina la `Sweetie…’ jina moja tu, kitu ambacho madakitari waliompokea sasa hivi wanashindwa kuelewa kwanini wenzao hawakuwa na kumbukumbu za kutosha za huyo mgonjwa, na hivyo basi Rose ni muhimu kuwepo huko kujibu maswali yote hayo, kwasababu hata docta Adam, ametoweka, haijulikanai kaenda wapi..kuna mambo huko…lakini atapatikana tu…’akasema Inspecta.
‘Nini, eti, `Sweetie…’akasema Maua kwa kushangaa huku akingalia juu na baadaye akatabasamu..
‘Sio ndivyo ulivyoandikisha, hayo majina yenu ya kimapenzi mnayatumia hata mahali pasipohusika, kwani huyo mumeo jina lake halisi ni nani..?’akauliza Inspecta na kabla Maua hajajibu kitu, shangzi akaingilia na kati na kusema;
‘Naona hayo tutayaongea baadaye…kwanza tumalizane na moja kabla ya kuingilia maswala mengine ya majina, nilikuwa na wasiwasi na taarifa yako, una uhakika kweli unamfahamu binti yangu vyema…?’ akauliza shangazi mtu.
‘Kwanini unaniuliza swali kama hilo wakati nimekwisha kuambia kuwa nilikutana naye nchi ya jirani, Rose hebu niambie hatukukutana huko nchi ya jirani..?’
‘Nchi ya jirani ipi hiyo…?’ akauliza Maua.
‘Nina maana Uganda, kwani wewe umewahi kufanya hiyo kazi yako nchi ngapi, mimi ninamaanisha nchi tuliyokutana na wewe, hizo nyingine ulizowahi kufanya kazi sina umuhimu nazo, inaoenakana umefanya kazi sehemu nyingi eeeh, lakini kwangu sio muhimu sana…mimi namaanisha Uganda, wakati upo huko na docta Adam, …na…’ akakatizwa na simu , ikabidi atoke tena nje kuongea, aliporudi alisimama na kuwaangalia hawo watu wawili kwa makini, bila kusema neno.
Shangazi naye akamwamgalia Inspekta akiwa na lengo la kutaka kumwambia ukweli, lakini kabla hajasema neno simu ya Inspeta ikaita tena, na Inspekta akatoa tafadhali na kuelekea nje,akijua hiyo simu ni ya kikazi na ni muhimu sana,hakutaka kusikilizia hapo akatoka nje na kuwaacha Maua na shangazi yake wakiangaliana.
‘Shangazi mbona mimi sielewi, au kuna kitu kinaendeela hapa mimi sikijui, huko nchi ya jirani niliwahi kufika lini, na kama tunakwenda huko, mimi inanihusu nini, msinichanganye na mambo yenu, mimi huko siendi kabisa, kwanza nitamuelezaje Maneno,..’ akasema Maua kwa sauti ya chini chini, na alipoona shangazi yake hamjibu kitu akasema `Huyo polisi akija hapa nitamwambia kabisa mimi sio Rose, kama kuna mhalifu anaitwa Rose, anamfananisha na mimi, akamtafute huko huko, mimi na polisi mbali mbali, kwanza hapa natamani kutapika,..’akasema Maua huku akishika mdomo.
‘Na hilo ndilo linalonifanya mimi na wewe twende huko huko, ukamuone huyo Rose anayemfananisha na wewe,…hebu jiulize mpaka polisi anakufananisha na huyo mtu, huoni kuwa..., wewe subiri kwanza, kwani kuna mengi huyajui na ulishaanza kuniuliza maswali mengi kuhusiana na hilo jina Rose, sasa kama unataka kupata jibu la swali lako hilo ni bora twende hiyo safari,…ila nina wasiwasi na huyo mgonjwa, ni nani huyo, nahisi kitu, huyo anayeumwa kama sikosei atakuwa ni …..
Kabla hajasema kitu Inspketa akarudi na kusema,
‘Kesho nahitajika kwenda huko nchi ya jirani, licha ya kuwaomba kuwa mke wangu ni mgonjwa, lakini wamesema hiyo safai ni muhimu sana lazima niwemo, kuna mambo ya kwenda kumalizia, sasa nikaongea na wakuu zangu kuwa kuna watu wawili nawahitaji sana kutoa ushahidi muhimu sana, nia kubwa ni nyie muwepo kwenye hiyo safari, nikawaomba viti viwili kwenye ndege yetu kwa ajili yenu,mnasemaje….?’ Akasema Inspekta akiwa na uhakika kuwa ombi lake litakubaliwa.
‘Kwanini tuwemo, mbona mimi bado sijaelewa…?’Maua akaanza kujitetea, lakini shangazi akamkatiza na kusema `Tutafurahi kuwepo kwenye hiyo safari, kwasababu ni ya dharura na ni muhimu tukamuona huyo mgonjwa ili tuone tutamsaidiaje umesema jina lake anaitwa Sweetie..hahaha, mambo ya mapenzi hayo wanayapeleka hadi kusipofaa, kwanini msiandikisha jina lake..?’ akasema shangazi huku akijifanya kumwangalia Maua,alishaona kuwa ni vyema hali hiyo ikabakia kama ilivyo hadi atakapohakikisha hicho anachohisi kuwa ndicho
‘Shangazi huyo mgonjwa ni…?’akataka kuuliza Maua kwa hasira, na shangazi akamfinya na kumfanya Maua anyamaze kimiya, kwani hiyo ni ishara ya shangzi yake anapomkataza kitu. Na inspekta aliona lile tendo tendo akawaangalia kwa jicho la kujiiba, halafu akageuka kuondoka, na alipofika mlangoni akasema;
‘Basi jiandaeni,na kwa vile hiyo ni safari ya dharura, kinachotakiwa ni kibali cha dharura, na hilo nitalifanyia kazi mwenyewe, nitawapigia simu baadaye mnipe majina na kumbukumbu zenu kamili, ili niweze kuzijaza kwenye hicho kibali cha dharura, nataka ikiwezekana tukayamalize haya mambo kabisa, ili hata binti yako akirudi huko asiwe katika mashaka mashaka, na bado sijaongea naye, kuna mambo nahitaji kutoka kwake, na hayo nahitai kuongea naye peke yake, lakini sio leo, kwasasa hivi nahitajika haraka ofisini, jiandaeni kwa safari, mtachukuliwa kesho, kama mpo tayari lakini…’ akawaangalia kwa makini kwa muda.
‘Sawa tutawasiliana afande…’akasema shangazi mtu akimwangalia binti yake.
‘Na mjue tutasafiri na ndege ya jeshi,…’akaongezea Inspekta, akimwangalia Maua tumboni, moyoni akisema mimba yake bado ndogo haiwezi kusumbua.
‘Hamna shida mimi mwenyewe niliwahi kupitia jeshi kwa mujibu wa sheria, nikapitia mgambo, na huko niliwahi kupewa kazi maalumu, kwahiyo safari kama hizo niliwahi kuwepo…usijali na huyu nitamlinda mwenyewe…’akasema shangazi na Maua akamwangalia shangazi yake kwa uso wa kutahayari.
‘Namba yangu ya simu hii hapa…’akawapa kadi na kuondoka na kabla hajatoka mlangoni gari la Maneno likaingia….
NB. Najua bado kuna sintofahamu nyingi kuhusiana na hiki kisa, lakini hitimisho hili ambalo lina sehemu nyingi, litamaliza mengi kati ya sitofahamu hizo, naombeni tena, kama kuna sehemu tumeruka, hazikueleweka, tuambizane, ili kisa hiki kiishe vyema, nawashukuru sana wale ambao wamenidokeza wapi tumesahau au nini kinatakiwa kiongezwe au kifanyike.., na hilo ndilo lango langu, Tuweni pamoja.
Ni mimi: emu-three
Tuesday, December 6, 2011
akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-58 Hitimisho-2
‘Rose umekuja huku Tanzania na mumeo, au upo peke yako?’ Maua alishituka pale alipoulizwa hilo swali na Inspekta wa polisi, ambaye walikutana naye akiwa maeneo ya hospitalini. Alikuwa kaongozana na mkewe ambaye naye alikuwa mja mzito. Alimsogelea Maua na kusaliamina anye kwa ksuhikana mikono. Maua aliitikia salamu ile bila kuonmyesha hisia zake za kustaajabu kwani hakumbuki kujuana na huyu askari.
‘Huyu ni mke wangu, wakati nikiwa kule Uganda nilikuwa naombea sana mkataba wangu uishe haraka, maana kama unavyomuona alivyo…aliponipa taarifa tu kuwa ana kiumbe tumboni nikasema sasa mambo yameiva, maana mke wangu akiwa mjamzito, namjua mwenyewe… naona hata wewe kama sikosei umeshapandishwa cheo, na wewe ni meneja kama sikosei maana gilo gauni linaeelzea mengi…’akamtizama Maua tumboni, Maua alikuwa hapendi hiyo hali, kwani wengi walishaanza kumsengenya kuwa akolewa akiwa na mimba..
Kwa ujumla hali ya tumbo ilikuwa haijajionyesha vyema, lakini kwa mzoefu angelimgundua ampema sana. Yeye kuja hapo hospitalini, ilikuwa sehemu ya mazoea yake anapijisikia vibaya, …akamtizama yule sakari akijiuliza amewahi kumuona wapi, na kwanini anamuita jina hilo! Na hata hajajua nini amjibu mara akaulizwa swali lililomfanya ashindwe kunyamaza kimiya…
‘Wewe una miezi mingapi vile? ‘akaulizwa swali hilo na Inspecta, huku akimwangalia Maua machoni. Na Maua akaangalia pembeni akitaka kujaribu kulikwepa hilo swali, kwani hakupenda kujitangaza, kihivyo ..
Maua akajivunga hakusema kitu akawa anajibaragua kutaka kuondoka pale alipokuwa kakaa, lakini kabla hajainuka, Inspekta akaja na kukaa naye karibu…
‘Docta Rose una miezi mingapi maana licha ya hilo gauni ulilovaa, lakini hali halisi haijifichi inaonekana umeshakuwa meneja au sio, kama sikosei?’akasema Inspekta kwa utani, na kumufanya Maua acheke bila kupenda, alicjheka kama njia ya kuondoa hali iliyojijenga moyoni mwake, …ilibidi acheke kwa kuitwa jina ambalo sio lake , na pili kuaitwa kuwa yeye ni docta. Toka lini akawa docta, wangelijua kuwa yeye na fani hiyo ni vitu viwili tofauti, licha ya kuwa alipenda kuifanya akzi hiyo wakati anasoma, lakini kutokana na kukosekana na mwalimu wa masomo hayo akajikuta anasomea masomo mengine kabisa.
‘Nina miezi mine, inakimbilia miezi mitano, ..’akasema Maua, huku akionyesha kushangaa, kwani anavyoongea huyu jamaa ni kama vile wanajuana . Maua alitaka kumuulizia huyu askari kuwa wamejuana wapi, lakini aliogopa kumuuliza lolote, kwani hakutaka kuongea na mtu kwa muda mrefu,…hapo alipo tu alikuwa anatafuta mwanya ainuke hapo na kukimbilia chumba cha kunawia akatapike, huwa akiongea na mtu, hasa mwanaume anajisikia vibaya, kichefuchefu…akajitahidi kujizua kwasababu alikuwa kawenye foleni ya kukutana na docta bingwa wa akina mama.
‘Mwenzako ana miezi mitano inakimbilia sita, ndio unamuona hivyo, hatupumui, inabidi niache kazi za ofisini kwa ajili yake, anataka kila mahala tuongozane naye, hata huku klinik, kanilazimisha twende sote, ila tuna miadi na huyu mtaalamu wa akina mama, ni mtu anajua kazi yake vyema, vipi wewe, nilizania kwa vile wewe ni dakitari, ungejitibie mwenyewe nyumbani…’akasema Inspekta kwa utani.
‘Kuhusu hilo swala la kuongozana na mkeo kwenye kiliniki wewe unaonaje hilo, mimi naona ndio vyema,ili kama kuna tataizo au ushauri muusikie pamoja…?’akasema Maua huku akijaribu kujigeuza mbali, lakini hakuweza…akavumilia.
‘Mwambie maana hilo swala limeleta mabishano yasiyo na maana…’akasema mke wa inspekta.
‘Lakini jitahidi ukamuone mume wako, maana nilikwenda mara moja kule, kwa ajili ya ile kesi ya maujai pale hotelini, nilimkta mumeo ana hali mbaya sana, natumai mnawasiliana, aua sio, kwa ujumla hali mumeo sio ya kurizisha..’akasema Inspekta.
‘Mume wangu yupi huyo, mbona sikuelewi wewe askari…’akasema Maua akizidi kushikwa na mshangao.
‘Rose unanishangaza kweli, mumeo yupi, kwani una waume wangapi, …lakini…mmh, name hapa nashikwa na wasiwasi kidogo, ….kule ulikuwa umejifanya mzungu, …tabia yako ya kule ilikuwa tofauti kabisa na ulivyo hapa sasa, nakuona umebadilika kweli au ndio mambo ya nyumbani ni nyumbani na kule ni kazini lazima ufanane na wazungu au sio. Umefikia wapi… , kwasababu nina mazunguzmo na wewe mazito, lazima nije nikutembelee, nina maswali machache ambayo najua ukiwa huku utanijibu vyema, ingawaje lile kundi tumeshalisambaratisha, kabisa, lakini wewe na mumeo mlihitajika mahakamani mkawa hamuonekani, imeleezwa kuwa wewe umeenda kusoma Ulaya na mumeo hajulikani wapi alipo, na alipoonekana tu akashikwa na kuwekwa ndani, walimtoa kwasababu ya afya yake mbaya…kuna mengi yametokea ndio maana nataka tuonane, unaishi wapi…? Akauliza Inspekta.
‘Sasa hivi ninaishi maeneo ya Mbezi, ….’akasema Maua na kumueelekeza huyo askari wapi anaishi, lakini hakupenda kabisa kukutana naye tena, kwani moyoni aliona akizoeana na hawa watu unaweza ukajikuta unaingia mahakamani au jela bila kupenda..
‘Mbezi ….Oooh, mbona mimi nami nina nyumba yangu huko ninahamia huko karibuni, nitafika kwenu,…nina mambo ya kikazi nataka tuongea na wewe kabla hujarudi huko kwenu, unatarajia kuondoka lini, maana kiukweli nenda ukamuone mumeo hali yake sio nzuri, …’akasema huku akimwangalia mke wake ambaye alikuwa kamshika mkono, kama kutaka kumwambia jambo. Maua alibakia kushangaa, na kujiuliza maswali mengi kichwani, ambayo hakuweza kabisa kuyaelewa, na akawa na hamu ya kutaka kumuuliza huyo askari , lakini kwa muda ule alikuwa kamgeukia mkewe kusikiliza nini anachoambiwa, na alipomaliza kuteta na mkewe akamgeukia Maua na kuanza kuongea kabla Maua hajafungua mdomo wake kumuuliza lolote..
‘Kweli Rose umebadilika sana na mabadiliko hayo ni ya haraka kweli, mpaka inanitia wasiwasi kuwa nimekufananisha nini, lakini nina uhakika kua wewe ni Rose, siwezi kukusahau popote pale..na ….;akawa anaongea huyo askari lakini kabla hajaongea zaidi wakasikia jina likiitwa, na kumbe ndio jina la mkewe..
‘Basi Rose nitakuja nyumbani, ….akasema Inspekta akimsaidia mkewe kusimama.
Mkewe akainuka , alionekana ujauito ule ulikuwa umemchosha sana, na kutokana na unene wa mwili tumbo lilionekan kubwa kama vile ana mapacha. Inspekta akainuka naye huku akiomba tafadhali kwa Maua, kuwa wanakwenda kumuona docta, kwahiyo mazungumzo yakakatishwa bila Maua kujua nini kinachoendelea.
Maua akabakia akiwaza mengi, kwanza hilo jina la Rose limetoka wapi, anakumbuka kuitwa jina hilo na Mhuja, wakati wakitaniana …huwa katika maongezi yake alipenda kumuita `Maua , Rose wangu,…’ lakini hajawahi kuitwa na mtu mwingine…oooh, baadaye akakumbuk ipo siku shangazi yake aliwahi kumuita hilo jina na kusema `Maua , Rose, oooh, kwakweli nimejisahau sana…’
‘Kwanini unite Rose, hilo sio jina langu shangazi, mimi sipendi kuitwa majina ambayo siyo yangu..’akalalamika Maua siku hiyo alipoitwa jina hilo na shangazi yake.
‘Ndio maana nikakuambia nimejisahau….samahani maana na wewe huna dogo…’akasema shanagzi yake.na
*****
`Maua umerudi toka kliniki hebu niambie mambo yapo shwari,..’akauliza shangazi huku akimsogelea na kumshika tumbo. Maua akajifanya kama vile hataki kushikwa hivyo, lakini cha ajabu, ni kuwa alikuwa akiona raha kuwa na shangazi yake, lakini sio kuwa na mumewe, wakati mwingine anampigia simu shangazi yake aache shughuli zake aje wakae pamoja.
‘Yapo shwari ila nina mazunguzmo na wewe, ….mazito sana na safari hii sitaki mambo ya kufichana, maana hilo jina ninaloitwa sasa hivi nahisi lina jambo…’akasema Maua.
‘Jina gani tena, …hebu niambie mpenzi, kabla mumeo hajaja, isije ikaleta kisirani, sipendi muwe mnazozana na mume wako, japo kuwa najua huko kuzozaan kwenu kunasababishwa na hiyo mimba, sijui ndio dume linakuja nini, na ningeshauri umuite Mhuja
‘Eti nini shanagzi kwanini unasema hivyo,…?’akauliza Maua kwa kushangaa, kwani kweli akilini mwake alishajiwa na wazo kama hilo kuwa akijifungua mtoto wa kiume atamuita jina la Mhuja, kuonyesha jinsi gani alivyompenda mume wake, na hapo mawazo ya mume wake yakamjia, alimkumbuka sana, licha ya kujitahidi kumuondoa mawazoni.
‘Usipoteze lengo, nina mazunguzmo mengine ya kuhus hilo jina la Rose, maana ulishawahi kuniita hilo jina na sasa leo tena nimeitwa jina kaam hilo na polisi, na tena hakuishia hapo aliniita Docta Rose, toka lini nikawa docta mimi, lazima kuna jambo hapo, na najua wewe unalijua zaidi yangu….’akasema Maua.
‘Wewe mtoto wewee mbona unataka kunileeta balaa, mambo hayo ya zamani yalishaisha, na …hapana unasema nani kakuita hilo jina, polisi gani huyo…
‘Kuna polisi mmoja, nimesikia watu wakimuita Inspekta, mimi nawajulia wapi hawo watu, kwanza mimi na polisi hatuivani, siwapendi hawa watu…’akasema Maua.
‘Unawapenda, sema kwa vile ni mwanaume, na wewe kimimba chako hakitaki wanaume sijui atakuwa dume …atajuwa mhuja huyo..hahahah, hebu niambie anasema anaishi wapi aua nafanya wapi huyo polisi…?’akauliza shangazi
‘Kasema amejenga huku huku na anahamia karibuni…’akasema Maua.
‘Aaah, nimeshamfahamu, huyo ndiye tulizozaan naye kwenye kiwanja chake, kajenga karibu na mimi, akapitisha ukuta wake karibu na eneo langu, halafu analeta mambo yake ya kiaskari, nikamwambia weee, achana na mimi siogopi cha polisi au nani mbele ya haki yangu, alibomoa ukuta wake bila kupenda…’akasema shangazi mtu.
‘Shangazi na wewe, ina maana huogopi polisi, ….tena anaonekana ni mtu ana cheo kikubwa sana…’akasema Maua.
‘Mbele ya haki yako hutakiwii kumuogopa mtu hata kama ni Raisi unapambana naye maana wengine wanataka kutumia vyeo vyao kunyonya wanyonge, lakini sio kwangu, tutapambana hadi mahakamani…haya niambie mliongea nini mpaka akakuita Rose…?’akauliza shangazi.
‘Tulikuwa kwenye foleni ya kumuona dakitari, tumekaa kwenye viti, mara nikamuona huyo polisi akija na kukaa karibu nami, akadai kuwa namba yao ipo mbele yangu, na aliponionyesha hiyo namba ambayo kweli ilikuwa ya mbele yetu, nikawapisha, nikijua kuwa wanatumia ubabe wao wa kipolisi, na baadaye akaja mwanamke mmoja mnene mjamzito na kukaa karibu naye, na kunifanya nirudishwe nyuma tena, kumbe ni mke wake, na amechoka, utafikiri kafika kujifungua, kumbe ndio bado ana miezi mitano tu, je akifikia miezi minane ,au hiyo tisa itakuwaje, jamani sisi wanawake tuna mitihani mikubwa, na kwasababau yupo na mumewe basi anadeka kuliko maelezo, maana mara amuegemee mume wake, mara alale mapajani mwa mume wake, utafikiri yeye pake yake ndiye mwenye mume…’akasema Maua.
‘Sasa kwanini wewe hukwenda na mume wako kliniki ukamdekea kama huyo, siku hizi ni mambo ya kwenda hospitali au kliniki ni lazima uwe pamoja na wanaume zenu, sio sisi , zamani ukienda kliniki unakwenda peke yako,na mwanaume haruhusiwi kufika wodi au sehemu za wanawake, lakini hizi mnaiga wazungu, …siku nyingine mwambie Maneno mwende naye…
‘Eti nini, hapana, sitaki kabisa kuongozana na huyo mwanaume,…’ akasema Maua huku akimuwaza Mhuja, na kilichomshangaza ni kuwa tangu aamuke asubuhi, amekuwa akimuwaza Mhuja, na kujuta kwanini siku ile hakuingiwa na ujasiri wa kumwambia asiondoke, lakini kwa vile hisia zake na wanume zimekuwa hazioani, siku aliomba ile siku iishe haraka, hata kufungishwa harusi kwenyewe alikuona kama mwaka, alizindukana kwenye lindi la mawazo, vigelegele vikitanda hewani, keshakuwa mke wa Maneno, na Mhuja hajulikani alipo. Alikumbuka baadaye alimuita shangazi yake na kumuuliza kuwa Mhuja yupo wapi, …
‘Unasema nini, eti Mhuja, hebu achana naye, kwanza usiseme lolote kuhusu huyo mtu, tmekubaliana hilo…hayupo na hatarudi tena,…wewe sasa mume wako ni Maneno, unafikiri ungelisemaje kama angelikuwepo hapa, hiyo mimba ungembambikia, kila kitu hupangwa na Mungum, huyo sasa msahau….uinasikia…’alisema shangazi yake kwa ukali.
Hapo Maua akakumbuka jisni isiku ile ilivyokuwa, kwani hata kile kisa hakikuweza kuelezewa chote, hakujua nini kilitokea baada ya pale, akakumbuka jinsi Mhuja aliposhikwa na butwaa pale alipomuuliza swali;
‘Maua naona shangazi anafoka huko nje, na kisa hiki sijakimalizia, nikuuulize swali moja, je una uhakika nah ii ndoa, nina maana kuwa je una mpenda kweli Maneno, rafiki yangu awe mmeo badili yangu, na ikizingatiwa kuwa umeniona kuwa nipo hai,,naomba unijibu haraka…?’ akauliza Mhuja, huku akiangalia saa, na nje shangazi alikuwa akiita kwa hasira.
Maua alikuwa akijsikia vibaya, alikuwa akitamani atoke mle ndani na kukimbia, alishangaa, mume aliyempenda kwa moyo wake wote, leo hii yupo mbele yake, lakini hataki hata kumuona, sio yeye tu, hataki sura inayoitwa mwanaume, anaijsikia vibaya kutapika, na alitamani kumwambia Mhuja aondoke haraka mle ndani…
‘Maua muda unakwisha, na kama jibu ndio kuwa umeamua kuolewa na Maneno, nakuomba sana, usije ukamwambia Maneno kuwa uliwahi kuiniona, mpaka siku nitakapotokea tena mwenyewe, kama kweli nitatokea tena, kwasababu yule ni rafiki yangu, hatakubali kukuoa kama atajua nipo, na inaweza ikageuka uadui mkubwa…huyo ni rafiki yangu wa damu, sipendi tukosane…, ninachotaka kwako ni wewe kujisikia huru, mapenzi yangu kwako ni wewe uwe huru, sitaki nikuuzi kwa lolote lile, …’akasema Mhuja kwa sauti ya huzuni.
‘Sikia Maua nipo tayari kuumia kwa ajili yako,…ni kweli nitaumia sana, lakini ni heri niumie mimi kuliko kukuumiza wewe, je unampenda Maneno awe mume wako, sihitaji sababu jibu ni ndio au hapana…’akauliza tena Mhuja, lakini Maua likuwa kimiya, hakuwa anajua anaulizwa nini, kichwa kilishaanza kumzunguka, ilibakia kidogo kudondoka , …ashukuru mnungu kuwa alipojisikia hali mbaya alikimbilia kukaa kwenye sofa, na kwa muda huo kichwa alikuwa kakiegemeza kwenye sofa, na huku kaangalia juu,…na kabla hajasema lolote, mlango ukagongwa na shangazi akaingia na kusema;
‘Wameshakuja waoaji, …’akasema shangazi akiwa keshafungua mlango, na kukawa na kukura kakara, ambazo Maua hakuweza kujua nini kilitokea pale mlangoni, kwani hauwa yeye, akili ilikuwa imesimama, akawa kama mtu aliyepoteza fahamu, kwani alidondokea pale kwenye sofa na kujilaza, na hakuna aliyejua kuwa hali yake imekuwa hivyo, akawa kajilaza pale kwenye sofa kwa muda,alitaka kumwambia shangazi yake ahirishe hiyo harusi maana hali yake sio njema, lakini hakuweza, kauli ilikwisha kabisa, mdomo haufunguki, na alishitukia anaulizwa swali kuwa umemkubali Maneno awe mume wako, na kwa vile hakutaka zaidi akaitikia ndio, ilimradi, watu waondoke na abakie huru,…vikatanda vigelegele, anashitukia keshakuwa mke wa Maneno.
amekuwa sitaki kabisa, bora kama nikwenda na mtu twende pamoja na wewe, lakini sio na Maneno,pale tu alipokuwa akiniongeelsha Yule askari mwanaume nilitamani nimtapikie, sijui kwanini nawachukia wanaume kiasi hicho…sijui kwanini. Sasa shangazi usibadili mada, nilikuuliza swali,…. hebu niambie hilo jina la Rose limetoka wapi?’akauliza Maua
‘Sikiliza Maua, wakati mwingine hutakiwi ujue kila kitu, mengine yanatokana na historia ambayo haitakiwi kujulikana, na mimi siwezi kabisa kujua kwanini huyo askari akuite Rose , inawezekana ni kwasababu yote ni Maua, sikiliza Maua, jambo jema ni wewe kutulia ujifungue salama, sipendi mambo mengine yaingilia kati, hayo hayakuhusu kabisa, na huna haja ya kuyajua, unanisikia vyema…’akasema Shangazi.
‘Hapana usiponiambia kutachimbika, na kutokana na maelezo yako inaonyesha kabisa kuwa hilo jina lina sababu maalumu, kama ulivyosema sitakiwi kuyajua, kwanini sitakiwi kuyajua na wakati mnaniita jina hilo ambalo sio langu, na kama huniambii nitampigia simu baba ajae aniambie, maana sipendi kuitwa majina ambayo siyo yangu na kumbe kuna jambo limejificha, niambie shangazi sasa hivi, kabla sijaanza kutapika…’Kabla Maua hajamaliza kuongea kengele ya mlangoni ikalia,na Maua akashikilia mdomoni, kuonyesha kuwa anasikia kichefu chefu, na kukimbilia chumba cha kunawia…
Shangazi akachungulia nje, kwa kupitia dirishani, wote kwa muda ule, ingawaje sio saa za kawaida, kwa Maneno kurudi nyumbani, lakini walikuwa wakijua hivyo kuwa atakuwa ni Maneno aliyekuja …
‘Huyu sio mume wako, ….wala usijisikie vibaya, nimeona gari tofauti limeimgia getini, na kama sikosei atakuwa. ooh,… mungu wangu…mbona mambo leo…’akasema shangazi mtu huku akionyesha uso wa wasiwasi na kumfanya Maua naye aje kuchungulia dirishani...
NB: Wapendwa nitajitahidi kuwa nanyi kila inapowezekana, hasa kwa kupita internet cafe, ikizingatia kuwa sasa tupo katika hitimisho. Naombeni maoni yenu, ili kama nimesahau kituu niweze kukiweka katika sehemu hii ya hitimisho. Ama kuhusu lile tukio la kule hotelini, linakuja, lipo ...na muhusika atakayetuelezea yupo nchini, ...TUPO PAMOJA.
Ni mimi: emu-three
Monday, December 5, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-57Hitimisho -1
`Maua , nimepewa muda mfupi sana na shangazi, na muda huo natakiwa nikusimulie kisa changu ili uondokane na hisia potofu , ambazo kila mmoja anajua hivyo, kuwa mimi nilishakufa,….mimi sijafa, na kisa hiki kitakuonyesha jinsi gani nilivyookoka na ajali ile. Nakuomba baada ya kisa hiki uwe huru kuamua kwa utashi wako mwenyewe bila shinikizo la hisia ambazo hazipo,au shinikizo la mtu mwingine, utoe uamuazi wako mwenyewe, je upo name au kutokana na hili tukio ulishabadilika, …je kama ungelikuwa wewe ungelichukua hatua hiyo uliyoichukua…siwezi kukulaumu, lakini cha muhimu, najua una haki ya kujua ni nini kilitokea hadi kuwepoleo hii.
‘Maua, mungu ndiye anayejua mwisho wa kila mtu, hata mimi siwezi kuamini kuwa bado nipo hai, nilijua sasa hivi ni meshakuwa nyama za samaki,…lakini mungu hakupenda iwe hivyo, nilishahisi kwa muda wa miaka miwili lolote linaweza kutokea, lakini niliona nije nikuone na nijue nini kinaendelea, …sasa ondoa hisia hizo kuwa mimi labda ni mzuka, au shetani, mimi ndiye yule yule, mume wako ambaye leo unataka kunikana, ..Maua sitaki kukulazimisha, sitaki kukuweka katika njia panda, kwani wahenga wanasema usilolijua ni sawa na usiku wa kiza, huenda yapi makubwa ambayo huyajui, lakini ni bora ukayajua yangu kwanza,,kadrri muda utakavyoruhusu.
‘Maua, kwanza, nimeamini ukweli wa hisia zangu, hisia zangu ziliniashiria toka awali, kuwa safari ile haitakuwa nzuri, unaweza ukasema, ningelijua ningelifuata hizo hisia zangu, nikaahirisha hiyo safari, kwani siku tuliyotakiwa kuondoka, nilikuwa sijiskii vizuri kabisa, nilitamani kabisa nisiondoke, nitakajipanga kuwapigia wenzangu, kuwa sitafika siku hiyo, lakini ikatokea kitu kingine nikajisahau…hata nilipoamuka asubuhi ya safari, nikawa na jivuta vuta kama sio msafiri, na sio kawaida yangu, na hutaamini nilichelewa hata kufika bandarini pale ziwani, lakini kwa vile ilikuwa ni maswala ya kikazi nilikimbilia pale ziwani na kujikuta nimechelewa, hata hivyo nikaruhusiwa kuingia ndani ya meli..
Kwa ujumla walikuwepo watu wengi siku hiyo na wote walitaka kusafiri, na kila waliokuja kuliruhusiwa kuingia kama mimi, kwa mahesabu yangu walikuwa ni zaidi ya mia sita. Nikaingia ndani ya meli na kuitizama, huku nikiwaza, kweli meli hii ni ya muda mrefu, ilionekana kuchoka kweli, lakini akilini nikasema ya kale ni zahabu.Nikiwa ndani ya meli, kila upande nilipokwenda nilikuta watu wamejaa isivyo kawaida, nilitafuta sehemu yangu nikakaa, na huwa mara nyingi sipendi kukaa sehemu moja,…lakini kwa kujisikia vibaya, nilitamani nilale tu, lakini nikasema siwezi kuvunja taratibu zangu, kabla ya kujilaza kwenye kiti changu nilamua kuzunguka zunguka kwanza huku na kule, nilitembea huku na kule, ili mradi kupoteza muda…na baadaye safari ikaanza nikarudi kwenye sehemu yangu na kujilaza.
Pale nilipokuwa nimejilaza nikawa nakuwaza wewe mke wangu, nilitafakari mengi, jinsi mambo ya safari yanavyoweza kuwatenganisha mke na mume, niliwaza, kwanini safari kama hizo tusingekuwa pamoja, lakini baada ya hilo tukio nikasema hapana, aheri nimesafiri peke,yangu maana waliosafiri na familia zao walizisahau wakati kila mtu alipokuwa akihamanika na roho yake. Jamani isikieni ajali tu, huwezi amini kuwa mtu atamshau mwanae, mke wake au mume wake, na kukimbilia kivyake kama hawajuani….
Tulipofika kisiwa cha Kariemo nilihisi kuna kitu kimetokea…, lakini sikuwa na uhakika, hisia zangu ziliniambia kuna tatizo,kwani meli ilikuwa haipo katika msimamo wake wa kawaida. Kwa muda huo nilikuwa najisomea kitabu nilichokuwa nimekinunua, kitabu hicho kiliandikwa juu `Titanic Tragedy’ sijui kwanini nilikichukua hicho kitabu, maana kilichokuwa kinaelezewa hapo kilikuja kufanana na tukio letu,…ingawaje hakukuwa na ile hadithi ya kimapenzi kama ilivyokuwepo kwenye hiyo kitabu, lakini lile tukio la kuzama na mihangaiko yake, ilifanana kabisa na nilichokiona ndani ya kile kitabu.
Wakati naanza kukisoma hicho kitabu, nilikuwa nakisoma kama vitabu vingine vya hadithi tu,…lakini nikikumbuka, kilikuwa kikitabiri ajali yetu,…kwahiyo baadaye sikukichukulia kama historia tu, nakichukulia kama kitu muhumi sana katika tukio letu hilo. Ndani ya hicho kitabu, pamoja na kile kisa cha mapenzi ya wapendwa wawili, lakini hata hivyo niligundua mengi ambayo nilikuwa siyajui kabla, …
.
Wakatu ninaendelea kukisoma, hicho kitabu ,…akili yangu nayo ilikuwa ikitingwa na wasiwasi, nilikuwa nimeanza kuhisi hali isiyo ya kawaida, licha ya kuwa mzoefu wa kusafiri kwenye hii meli, lakini kitu kama kichefuchefu na kutokujisikia vibaya vilisumbua sana,…nikjaribu kutafuta usingizi, na njia pekee niliyoijua ni kusoma kile kitabu kwa bidii. Na kweli kile kitabu kikanipeleka mbali na kuanza kusisimukwa na hilo tukio lililokuwa likieelzewa, na kisa hicho cha wapenzi wawili.
Niligundua kuwa meli hiyo ya Titanic ilikuwa kubwa sana,na kweney safari hiyo watu wengi walijumuika kusafiri, , ilielezewa kuwa , baada ya hiyo meli kupatwa na hiyo ajali, abiria wengi sana walipoteza maisha, watu 1500 hivi walipoteza maisha , na ni watu 705 tu waliookolewa, ilikuwa ni tukio lililotokea mwaka 1912. Hapo nikashikwa na kausingizi kakimang’amung’amu nikalala.
Nje vigelegele vilikuwa vimepamba moto, lakini ndani ya chumba hiki, kulikuwa kumetulia, na ni sauti ndogo ya mtu mmoja iliyokuwa ikiongea tena kwa kuhakikisha kuwa hakuna anayewasikia hicho wanachoongea humo ndani. Hata Maua ambaye mwanzoni hakuwa na shauku ya kusikiliza hicho kisa akijua huyo sio mwanadamu, lakini kila hatua alitamani kusikia zaidi nini kilitokea, akatulia kimiya akiwa muda mwingi kaangalaia chini, lakini akili yake ilikuwa inanasa kila neno.
‘Lakini huyu ni binadamu kweli, mbona kila anachozungumza kinaingia akilini, hapana, Mhuja alishakufa, miaka miwili mtu asikumbuke hata kupiga simu, nikupoteza gani kumbukumbu kwa muda wote huo…aah, ngoja nimsikiliza kwanza, halafu, …..Mawazo ya Maua yalikuwa yakihamanika na ujio huo wa mtu huyu, bado kabisa akili yake ilikuwa akimfikiria kama mzuka, haikuwa bado inamtambua kama miongoni mwa watu waliobahatika kuokoka katika ajali hiyo, ni muda mrafu kwa mtu kuamini hivyo, …Sura, mwili maongezi na kila kitu ni yule yule mpendwa wake, …’akawawa anawaza huku akisikiliza hicho kisa.
‘Maua sijui kama uliwahi kukisikia kisa hicho cha kuza kwa meli ya Titanic, au kuangalia picha yake, ilivyokuwa, ndivyo ilivyokuja kutokea kwetu sisi, nilikisoma hicho kitabu kwasababu ni kisa kizuri cha kihistoroa, lakini ni tukio ambalo kwangu litakuwa kama kumbukumbu ya tukio letu, na nitajitahidi kukitafuta tena hicho kitabu, kama kumbukumbu yangu ya safari yangu hiyo.…’akasema Mhuja, huku akiangalia saa, akijua kuwa muda aliopewa unakwisha na huenda mambo yanakaribia kuiva, lakini hata kama yataiva na Maua atakubali kuachana na hiyo ndoa, basi ndoa itakua haipo, lakini kama atakataa kwasababu zake, ataitimiza ahadi yake aliyoiweka kwa shangazi, na hata kwa Maua kuwa kauli yake ataiheshimu, kwani huwezi kulazimisha pendo, licha ya kuwa anampenda sana mkewe,..ndio anampenda sana mkewe, lakini miaka miwili ni mingi mengi yametokea, huweze jua….
`Wakati nimeshatekwa na usingizi, mara nikazindukana sikujua kuwa ni ndoto ama ni ukweli, lakini baadaye nikajua kuwa sio ndoto, ilikuwa ni ukweli, sauti ile niliyoisikia kama ndoto ikisema `meli inazama, niliisikia tena wakati nimefumbua macho yangu, …kilichokuwa kikiendela kwa wakati ule ilikuwa nikila kona ya meli, vilio , vilio, kelele, na mihamaniko ya kila mtu akitafuta jinsi gani ya kuokoka. Nikiwa ndani ya usingizi, niliota ninaogelea nikiwa nimepiga mbizi, …na naogeela ndani ya maji nikipishana na samaki, huku wale samaki wakisema kwa sauti yajuu `tunazama …’ nikawa najiuliza hawa samaki wanasema hivyo wakati majini ndio kwao, wanazama nini tena.
Nikazindukana na kufungua macho haraka huku nikiangalia huku na kule, kuwaangalia wenzangu …hapo nikaamini kuwa ile ilikuwa sio ndoto, kweli kulikuwa na tatizo, kila mmoja alikuwa akihangaika kivyake na sauti zilikuwa zilia huku na kule,. Sauti za vilio vilitanda hewani na sauti nyingi zilikuwa za ikina mama….
Na mara kweli tukasikia mtetemeko wa meli ukitikisika, na ukiangalia kwa nje, ilionyesha dhahiri kuwa meli ilikuwa imekaa upande, …tukahisi kabisa tukiwa tunapalekwa juu, na abiria wakawa wanajaribu kukimbilia upande wa pili ili kujaribu kuiweka sawa hiyo meli, lakini haikusaidia kitu, tukaanza kuzama kuserereka, kwani meli ilikuwa ikizama upende upande,kwahiyo watu walikuwa wakikusanywa sehemu moja..
‘Meli ikawa inazama…kilichofuatia hapo, ni kila mtu na roho yake…..kwani maji yalishaanza kuonekana ndani ya meli, . Mimi sikupoteza muda tena, …kwa ujumla nilipona hivyo nikajau hapa kinachotakiwa sio kusubiri, nilichofanya ni kuvamia sanduku moja kubwa nikalibeba na kutoka sehemu ili niliyokuwepo hadi upande ambao ulikuwa sehemu ya juu, sikupoteza muda zaidi kuangali nini na kwanini imekuwa hivyo, …mimi na sanduku langu, nikajitupa ndani ya maji,na kuanza kutumia ujuzi wangu wa kuogelea. Nipojitupa kwenye maji kwanza nilizama kwenda chini …na wakati natua kwenye maji kichwa change kiligonga chuma cha meli,…mwanzoni sikuyasiki hayo maumivu, lakini kila dakika iliyokuwa ikienda mbele, ilikuwa kama mtu anapigilia kiti kwenye kichwa changu.
Niliibuka kwenye maji toka na kuweka kichwa juu kuangalia, nyuma yangu, ilikuwa kama ziwa limechafuka kwani watu walikuwa wakijitupa ndani ya maji, makelele ya yakuomba msaada, …na kila kelele niliyosikia ilikuwa inaniongezea maumivu ya kichwa nikaona niogelee mbali zaidi , na huku nalitumia lile sanduku kama msaada, kwani kichwa kilikuwa hakinipi nafasi ya kupiga mikono kama makasia, …kwakweli kama isingelikwua yale maji, kuwa nipo ndani ya maji ningelipoteza fahamu,kichwa kilikuwa kinauma kuliko kawaida,hata nguvu za kuogelea zilianza kuniishia ….
Hutaamini kuwa meli kubwa kama hiyo, kulikuwa hakuna vyombo vya kujiokolea, hasa yale majaketi ya kuweza kuvaa na kuelea, na nilikumbuka wakati tupo humo ndani wengi walikuwa akijadili kuwa meli hiyo imekuwa kuku sana , haikuwa inastahili kuasafirisha abiria wengi, na vifaa vya uokozi vilikuwa vichache saba. Na siku hiyo kila mmoja alikiri kuwa abiria walikuwa wengi kupindukia.
Kwakweli wakati nhangaika ndani ya maji niliwaonea huruma sana wale akina mama na watoto, lakini nani angeliwajali wakati kama huo , kila mtu alikuwa kihangaika kivyake, mama au baba hamjui mtoto, kila mmoja analia mama…sasa sijui mama wa kila mtu ni nani….
‘Maua muda unakwisha, mumemalizana, niingie…’ilikuwa sauti ya shangazi.
‘Bado kidogo shangazi, …’akasema Maua huku akimwangalia Mhuja, …alishaanza kuhisi kuwa huyo kweli ndiye inawezekana akawa ndio yeye …kwanini shangazi aseme mumeshamalizana, na je afanyeje, kwani hali aliyo nayo inamweka katika njia panda,…akaangalia tumbo lake , na kupitisha mkono, na akainua kichwa kumwangalia Mhuja na moyoni akasema `samhani Mhuja…samahani….sijui nifanyeje, kwanini mimi….akajipweteka kwenye sofa na kuchukua mwanasesere ambaye alikuwa kampa jina la Mhuja, akimaanisha kuwa huyo mtoto akimza atampja jina hilo kama ni mwanaume.
'Maua muda unakwisha ....'shangazi akasema kwa nguvu.
NB. Je katika hali kama hiyo kama ingelikuwa wewe ungelichukua uamuazi gani?
Ni mimi: emu-three
Thursday, December 1, 2011
Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-56
Maua alitaka kugeuka kuangalia ni kwanini aliyeingia hajasema kitu tangu muda wote huo, mwanzoni alijua kuwa huyo ni shangazi yake, ambaye alikuwa akiiingia mara kwa mara, ingawaje kuna muda alikaa muda mrefu bila kuingia na hapo ndipo ,Maua akaanza kupatwa na hayo mashaka,mashaka yaliyomtia hasira.
Au atakuwa mpambe wake, ambaye aliondoka muda, na kumuacha mwenza wake kwa muda mrefu Hapo Maua akaona azionyeshe hasira zake kinamna, ajifanye kudeka, kwa kukaa kimya, huku akiwa kalala kifudifudi na kufumba macho, akisubiri wao waanze kuongea, na hapo atajua nini cha kuwaambia…,ikawa kimiya hawasemi kitu na ulalaji ule ulikuwa ukimtesa, na hata kuwaza kama kuna kiumbe tumboni na ulalaji ule, unaweza ukaleta athari, kwahiyo akajigeuza kidogo na kulala kugeukia ukutani.
Maua alijua shangazi yake anavyompenda ataanza kwa kumbembeleza, lakini alijua kuwa akizidisha sana, anaweza akala viboko, …kwahiyo aliifanya ile kwa malengo maalumu na kwa muda fulani tu baada ya hapo atajua nini la kufanya, akasubiri muda aliouweka, lakini kulikuwa kimiya, hakusikia sauti ya shangazi wala mpambe wake. Mwili ukaanza kumsisimuka, akahisi kuna kitu kisicho cha kawaida, …
Alipoona kimiya kimezidi na muda wake alioweka umepita,akahisi kuna kitu kischo cha kawaida, akainua kichwa taratibu na kuangalia muelekea wa mlangoni,…hakuona vyema, …akainua zaidi na kuwa kama anajibinua, huku anaangalia mlangoni,...
Mara Moyo ukashituka,…mwili ukaanza kumsisimuka, akahisi uwoga fulani, ina maana Yule mtu ndiye kaingia,….hapana,...kaingiaje mle ndani asiweze kukutana na shsngazi yake, haiwezekani, ... akaanza kusikia mwili ukimuisha nguvu, lakini safari hii akasema hakubali, kama ni mwanga, basi yeye atakuwa giza nene lisilopitisha mwanga....nitapambana naye, nitapambane naye kama alivyofanya shangazi, na kuitwa mwanamke wa shoka. Mara akajiinua harakaharaka, na cha ajabu safari hii hakuiona ile dalili ya viungo kuisha nguvu, akasema kimoyomoyo , huyu sasa haniwezi.
Hata wakati ule anajitutumua kuinuka, akiwa anamuwaza yule Tajiri, kuwa ndiye aliyeingia, bado aliogopa kumwangalia huyo mtu, hakuwa anaangali mlangoni moja kwa moja, alikuwa kaangalia chini kwenye sofa, na huku akijaribu kuangalia kwa jicho moja huko mlangoni akaona miguu,…
Oh,kweli sio shangazi au mpambe, viatu, sio vya kike..akafuatilia kwa jicho hilo moja, kuelekea juu ooh, mbona kweli kvaa suruali, lakini hata mpambe wake hupendeela kuvaa suruali, na viatu vyake vilikuwa kama vya kiume, alipokuja mara ya kwanza, atakuwa mpambe nini….inawezekana mpambe wake, akasema kwa kujipa moyo, akasema huenda,mpambe wake, aliamua kuvaa suruali kwa ajili ya shughuli zake na baadaye atabadili na kuvaa nguo za kiharusi , akajipa moyo na kutulia kidogo, huku akijaribu kugeuza kichwa taratibu, ….alipoona kimiya kinazidi, akainuka mzima mzima na kuanza kusema;
‘Hivi ndio nini mnanifanyia hivi, kuniacha peke yangu muda wote huu, mnafikirii mimi nina hisia za mnyama au…hamuoni jinamizi la Yule nduli, Yule….jamani, kwanini mnanifanya hivyo….?’ Akaanza kusema kwa hasira, huku kafumba macho, ili asione aibu akiongea na wakubwa zake.
‘Mhhh, Maua…naona ulikuwa mbali sana, umesharizika nah ii hali, kuwa bibi harusi, au sio…?’sauti hiyo, ikamshitua na kumfanya afyumbue macho haraka, ili sisje ikawa ni ndoto,….akayafumbua macho yake haraka, lakini cha ajabu hakutaka kuangalia moja kwa moja, hata hivyo akili yake haikutaka kukubali haraka, haikuwezekana hakusikia vyema nini, mwili ukaanza kumuishia nguvu, safari hii sio kama vile mwanzoni alivyoishiwa nguvu na kushindwa kuinua hata mkono, safari hii ilikuwa kiajabu kabisa, akafunua macho na kuangalia pale sauti ilipotokea, kwa taratibu, na akamuona, …
‘Mzuka, shetani, ….’akajikuta akisema kimoyomoyo. `sio kweli wewe I mzuka au shetani, potea mbali….ushindwe na upotee….mung nilinde na kuniepushia na mashetani hawa wabaya….’akasema Maua kimoyomoyo. Halafu kwa sauti ya amshaka akasema;
‘Wewe ni nani, …tafadhali potea ,nakuomba mungu unilinde na …’akajikuta akianza kumuomba mungu kimoyomoyo , akijua hilo ni shetani limekuja kwa sura hiyo, huyo ni mzuka, kasimama pale mlangoni, na akijikuta macho yakizidi kumtoka zaidi zaidi na zaidi , yalimtoka kwa woga, yalimtoka kwa kutoamini, yalimtoka, akitamani na mdomo utoe sauti, lakini haikuwezekana, akawa katulia na kukodoa macho akiangalia kile kilichopo mlangoni, …
‘Maua tafadhali nakuomba unielewe, kwani muda uliopo hapa n mfupi sana, na nisingependa kuharibu kile kilichokusudia, nakuomba unilewe na utilize akili yako vyema….’akasema huyo mtu, au hicho kitu kilichopo mlangoni.
‘Nakuuliza wewe ni nani…unataak kufanya nini , kwanini hubaki huko kuzimuni,…kwanini unanitesa…..’akajikuta Maua akisema na sasa machozi yakaanza kumtoka, kwa wingi.
‘Maua najua hutaamini , hata kama ingelikuwa mimi labda ningelifanya kama ulivyofanya wewe, lakini yote ni mapenzi ya mungu, inabidi tuyakubali, lakini lazima tuwe na subira asa mitihani kama hii inapotekea, na kabla sijakuelezea kisa cha yaliyonisibu ningpenda nikuulize swali moja, ambalo unatakiwa ulijibu kwa makini, ….’yule mtu akasema huku akiwa bado kasimama pale mlangoni.
‘Maua akajiuliza huyu mtu, kama sio ni mzuka aliingiaje humo ndani, maana ili uingie mle ndani ni lazima upitie hapo walipo akina shangazi na watu wengine, aliwapitaje bila kuwaona, ndipo akaamini kuwa huyo ni mzuka, shangazi asingelikubali mtu kuingia mle hasa huyo, kwani sio binadamu, shangazi yake ni mkali wa vitu kama hivyo, kiimanii kaiva, haiwezekani, huyu ni mzuka katokea hewani, na huenda sio mzuka wa huyo anyemzania ni mzuka wa huyo tajiri, kaamua kujigeuza hivyo ili kumzuga na aingiwe na huruma.
‘Wewe najua ni tajiri Papa unataka kuvuuga kichwa changu, kwasababau ya uchawi wako najigeuza vile upendavyo, tokomoea huko ulipotoka,….tokomoea mbali, tokomoa mbali….’akajikuta Maua akisema, lakini cha ajabu sauti ilikuwa haimtoki vyema, hata pale alipojaribu kuongea kwa sauti ili shangazi yake asikie huko nje….
‘Maua mimi ndiye Yule Yule, na wala sio mzuka kama unavyozania, na swali langu ni muhimu sana kwako, ili dunia na nafsi yako iwe hury, `je una uhakika na unalotaka kulifanya, je unampenda huyo unayetaka kuoana naye, kauli yako ni muhimu sana, kwangu, ili name niwe hutu kwako, najua nitaumia, najua nitateseka, lakini kama moyo wake umesharizika, sina budi kukubaliana na hilo, na naomba ulitamke hilo ukiwa huru kabisa, je una mpenda huyo unayetaka kuoana naye, …?’akauliza Yule mtu.
Maua akabakia kimiya na kuanza kulia, sauti, ni ile ile, mwili ni ule ule….mbona nachanagnyikiwa, kwanini imetokea hivyo, kwanini itokee kwangu, kwanini….mungu wangu sasa nitafanyaje kama ni kweli, …haiwezekani iwe kweli, huu ni mmoja wa mtihani ,….haiwezekani, na hata kama ni kweli nitafanyaje,…’akainamisha kichwa na kuangliana tumboni, na mkono wake ukashika tumboni…
‘Maua kimiya bila kauli ni utata, lakini wahenga walisema ukikaa kimiya ina maana unasiki ahaya kujibu ulicho nacho na mara nyingi ni ishara ya kukubali, nshukuru sana, na huend andoto nilizoziota wakati nipo huko naeseka kwa mengi, zilikuwa kweli, kuwa wewe umeamua kunisaliti, na kulisaliti lile pendo letu tuliloahdiana, …kwa namna nyingine siwezi kukulaumu, maana hutokea hivyo, subira ni ngumu sana,na kuishinda inataka imani…ninachokuomba, usije ukamwambi huyo rafiki tyangu lolote…kabla sijasikia kauli yako, ngoja nikuhadithie kisa changu, nini kilinitokea, …
‘Mimi sijakusaliti…hujui ni mateso gani niliyoyapata hadi kufikia hatua hii,huenda ungelikuta kaburi, kama sio huyo…..anayetaka kunioa…sijakusaliti…oooh. Wewe umekaa niaka zaidi ya miwili, hata kupiga simu kutuarifu kuwa upo hai…siamini kwanza kuwa wewe ndio kweli….siamini, kwasababu ingelikuwa ni kweli, na ukatujali, …hata kama mimi uliamua kutonithamini tena, lakini wazazi wako, jamaa zako, ambao walifikia hata kusoma hitima mara mbili….ulishindwaje kupiga simu,…ooh , hapana sio kweli, wewe ni mzimu, .. kwanini itokee kwangu mimi, sina jinsi , nitafanyaje, maji yameshamwagika, nitafanyaje mimi….mungu wangu nisaidie…’Maua akaanza kulia.
‘Kisa changu kinaanzia mbali sana, nakuomba unisikiliza kwa makini, ili uone jinsi ilivyotokea, kukuonyesha kuwa sikufanya makusudi, ilitokea kwasababu sikuwa mimi , akili , na fahamu zote zilipotea, sikujijua kabisa, ninachoweza kusema ni kuwa akili zote na fahamu zilipotea na mara ziliporejea tu sikupoteza muda, haraka nikaja huku kukuona nikijua unanisubiri, unaitunza ahadi yetu ya ndoa,….sikujua kabisa kuwa nitakutana na mambo haya, …
'Maua nimeongea na shangazi akanielezea kwa ufupi, na nimeahidi kutimiza alichoniomba,ila kwa masharti ya kauli yako…kama bado una mapenzi na mimi, au ndio mapenzi yameshavunjika, sijaelezwa sababu nyingine ya muhimu . Au ipo sababu nyingine ya muhimu, uniambie, nataka kuisikia kauli yako, lakini kabla ya yote ningelipenda usikie kisa changu.
‘Kwasasa sizani kama kauli yangu itakuwa na maana yoyote, kwani mambo yameshaharibika…mambo kwasababu..mambo yameha…har….’Maua nguvu zikamwishia, akataka kudondoka, lakini, taratibu akajilaza kwenye lile sofa, akajikuta akilia, akiwa haamini anachokiona, aliomba iwe I moja ya zile ndoto, za kila siku, lakini hiyo haikuwa ndoto hata hivyo akili yake ilikuwa haijaamini.
‘Sikuelewi ukisema mambo yameharibika, kwasababu, bado mimi ni mume wako halali, …mambo gani hayo yaliyoharibika, ….Maua, miaka miwili ndio imekusinda…kuna nini cha zaidi umepewa mpaka kuivunja ahadi yetu…lakini sitaki kukulazimisha kwa hilo, maana, mpende akupendaye bwana, hata hivyo siwezi kujua rafiki yangu kwa kakupa nini, kakufaa nini wakati wa shida , wakati ukiteseka, ….Je upo tayari kusikiliza kisa changu, au huna haja nacho, nakuahidi kuwa kauli yakoo nitaiheshimu sana, kama kweli umebadilika na kutoamua kutonipenda mimi na kumpenda rafiki yangu, basi , nitafanyaje….labda …’akasema huyo jamaa.
‘Nakuomba sana usiseme hivyo, kwani name yaliyonikuta sio kama unavyozania, sawa anitasikiliza hicho kisa chako, lakini…..’akasema Maua huku akihisi tumbo likimuuma, akalishika, huku akiwazia mbali, je amwambi ukweli kuhusiana na hilo, haamui hivyo kwasabaabu kuwa hampendi, anaamua hivyo kwasababu ya kiumbe kisicho na hatia,….akamwangalia jamaa, ambaye hadi muda huo hakutaka hata kumuita jina lake maana akili yake ilikuwa haijaamini kuwa kweli ni yeye, haiwezekani, …
‘Sikiliza Maua ninachoomba ni wewe usikilize kisa changu ili uone jinsi gani ilivyokuwa, sikumbuki baada ya kuzama meli ilikuwaje, nakumbuka pale ilipozama, na hapo kumbukumbu ziliponijia kwahiyo nitakuhadithia nini kilitokea kwenye meli, hadi nilipozama kwenye dimbwi la kupotewa na fahamu, maana hapo sijui ilikuwaje,nina hamu sana ya kujua kilitokea nini wakati sina fahamu zangu, ……..natamani sana kujua ilikuwaje, lakini sijapata mtu wa kunisimulia, kwani nilipopata fahamu tu, nikaamua kuja huku.
Na hapo mhusika mkuu akaanza kutuhadithia jinsi ilivyokuwa kwenye tukio hilo la kuzama kwa MV Bukoba
Ni mimi: emu-three




