Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, February 9, 2018

MKUKI KWA NGURUWE-78




‘Hebu mleteni huyo mtoto...’akasema mwenyekiti, na mama yangu akatoka nje, na aliporudi akawa kambeba mtoto, kila mmoja akawa na shauku ya kumwangalia huyo mtoto.

Kila mtu alitaka kumuona huyo mtoto kwa sura, na huku wakijiuliza ni kwanini mume wa familia akang’ang’ania mtoto aletwe…

Tuendelee na kisa chetu

********

Mtoto akaletwa na mama hadi kwenye kiti kilichowekwa maalumu kwa mtoa ushahidi, na mama akakaa naye hapo, huku akiwa kambeba yule mtoto, hakutaka kumpa yule binti, mama wa huyo mtoto, sasa akawa anamfunua ili kila mtu amuone kwa uwazi mkubwa, na wa kwanza kusema alikuwa rafiki yake mume wangu, yani docta akasema;

‘Bro, wewe kweli damu yako ni kali,  huwezi kukataa hapo, utafikiri ni pacha mwenzako...’akasema docta.

Mume wa familia, alikuwa katulia kimiya, hakuinuka, wala kusema neno, aliyeinuka alikuwa ni wakili wake, ambaye alikwenda hadi pale alipokaa mama, na kumwangalia yule mtu, akatabasamu, na kugeuka, akarudi pale alipokaa, mteja wake, akamnong’oneza kitu.

Mume wangu akamwangalia kwa macho ya kuonyesha mshangao, lakini hakusema kitu, akabakia kimiya, na mwenyekiti alipohakikisha kila mtu kafika kumuona yule mtoto, na ambaye hakuweza kufika alikuwa mume wangu, mume wangu hakuinuka, alibakia pale pale akiwa kainamisha kichwa chini, na mwenyekiti akasema;

‘Mume wa familia ni zamu yako kumuona mtoto, usikatae, maana hilo tumelifanya kutokana na ombi lako, ulifahamu kuwa una mtoto, lakini ukajifanya hujui, ukifikiria kuwa huyo binti kaja peke yake, hana ushahidi, sasa mtoto ndiye huyo hapo, nenda kamuona, je ni mtoto wako, je ni damu yako, sasa uikane damu yako mwenyewe,...’akasema mwenyekiti.

Hata hivyo mume wa familia hakuinuka, mimi nikainuka na kwenda kumchukua yule mtoto kutoka kwa mama, nikaenda naye hadi alipokaa mume wangu nikamuonyesha mume wangu.

‘Huyu hapa, muone anavyofanana na watoto wangu, utafikiri mapacha, muone anavyokuangalia, katambua kabisa kuwa wewe ni baba yake..humdanganyi mtu hapa, sura yake haijifichi, anafanana kabisa na wewe...kwa kila kitu, haya niambie, ..’nikamwambia

Mume wangu badala ya kumwangalia mtoto akawa ananiangalia mimi usoni, na macho ya kutahayari, nilipoona hamuangalii mtoto, ananiangalai mimi tu, nikamuweka yule mtoto mapajani kwake, hakusogeza mikono yake, wala kusem a neno, moyoni nikasema ;ujumbe umefika. Nikamchukua na kumrudisha kwa mama, ambaye alimwangalia mwenyekiti kujua ni nini kinachofuata

‘Haya naona zoezi hilo limekamilika,...’akasema mwenyekiti na mama akamchukua yule mtoto na kwenda kukaa sehemu yake, pale alipokuwa amekaa awali.

‘Bado mwenyekiti, mimi nataka mume wa familia akubali kuwa huyu ni mtoto wake au sio mtoto wake, na kauli yake, ichukuliwe hapa  rasmi ndani ya kikao hiki, kama akimkana, basi kwa vile wapo wanasheria hapa, wataandika, mkataba rasmi wa huyo mtoto kuchukuliwa na mtu mwingine, maana hatakuwa hana baba...’mimi nikasema.

‘Sawa, ni wazo zuri, na sisi tupo tayari kumchukua huyo mtoto kama baba yake atamkana kuwa sio mtoto wake,..’akasema mwenyekiti.

Wakili wa mume wangu akawa anaongea na mume wangu, na niliona mume wangu akisita kusema neno, na baadaye akasema neno kwa wakili, na wakili akasema;

‘Mteja wangu  kasema hilo ni jambo lake binafsi, asingelipenda mtu kumuingilia, kwasababu kila kitu kipo wazi, anaona hilo la mtoto liachwe kama lilivyo, ataongea na mimi na ni jinsi gani ya kufanya..’akasema wakili wake.

‘Swali lwetu lipo pale pale, je huyo ni mtoto wake, au sio mtoto wake, kikao kinataka majibu?’ akaulizwa

‘Ni mtoto wake kwa mtizamo wa haraka, lakini kuna maswala ya kuthibisha kitaalamu, maana kufanana sio tija….yeye anafanana na wadogo zake, je haiwezekani akawa mtoto wa wadogo zake, kwahiyo mteja wangu kaomba apewe muda,…tuhakiki hakiki hilo kitaalamu zaidi...’akasema wakili na watu wakaguna, maana hapo hakuna cha kuhakiki, kila kitu kipo wazi.

‘Pamoja na hayo kuna swali la ziada, namuuliza mume wa familia, je anakubali sasa kuwa alimbaka mfanyakazi wa ndani…?’ akauliza mwenyekiti

‘Ndugu mwenyekiti, kama mteja wangu alivyosema awali, hawezi kuwa na uhakika na matukio hayo ya nyuma, kuna mengine mpaka sasa hayakumbuki, kwahiyo kwa hivi sasa hana jibu la swali hilo mpaka kupatikane vipimo vya kitaalamu.

‘Je vipimo vya kitaalamu vikisema huyo sio mtoto wake atafanya nini..?’ akaulizwa

‘Basi yawezekana akawa mtoto wa ndugu zake wengine..’akasema wakili

‘Na je ikithibitishwa kuwa ni mtoto wake, yeye ana kauli gani , rejea mkataba wao ulivyokuwa unasema..?’ akaulizwa

‘Mpaka sasa hatuwezi kusema lolote kwa hilo ..kwanza tupate uhakika, mfahamu alivyo mteja wangu yeye anathamini sana ushahidi, maana mambo mengine ya nyuma ameyasahau, na ikitokea ni kweli, basi hapo atakuja kutoa tamko lake..’akasema wakili wake.

************

'Huo ushahidi umakamilika, iliyobakia ni je katiba inasema nini,. Asileta ujanja ujanja wa kusahau hapa…tumekuwa tukienda na yeye kiuungwana ili tuone na yeye ni muungwa na kiasi gani..hana hiyo hulka…’akasema mweneykiti

‘Sasa tuspoteze muda, tuone kosa kaam hilo mkataba wao unasema nini,  na je ni nini mkataba wao, unasema kwa watoto wa nje au hilo halipo, maana hata kama baba yake kakubali kwa shingo upande,lakini sisi kama familia ni lazima tujue hatima ya huyu mtoto kifamilia, kwani kazaliwa ndani ya familia,na hatuwezi kuliachia hivi hivi, zaidi alifanyiwa kitendo hicho kwa nguvu...’akasema mwenyekiti.

Mwenyekiti akakaa kimia akisubiria mawazo ya watu, na docta akasema;

‘Hatuwezi kukimbilia kwenye hukumu kwanza maana bado sheria, haijabaini kuwa mlengwa ni mkosaji, sisi bado tupo kwenye ushahidi au sio, mimi naona ukianza kuangalia katiba inasema nini utakuwa umeshahitimisha kila kitu..’akasema docta

‘Nafahamu hilo, kama nilivyosema awali, binti anastahiki kuondoka kwenye kikao hiki mapema ili akaweze kujiandaa, kwani yeye ana safari, kwahiyo tunahitajia aondoke hapa akiwa na ufahamu kamili ni nini hatima ya mtoto wake…’akasema mwenyekiti

‘Kwa hali kama hii, mimi ningelishauri huyo binti asisafiri, aahirishe hiyo safari yake, ili muafaka ufikiwe kwanza, ni muhimu sana aondoke akiwa na uhakika, kuliko kusubiria au kutumia njia zisizo faa…tunafahamu baba wa mtoto wake anastahiki kuwajibika kwa hilo, lakini je ni kweli, huyo baba wa mtoto ni nani..ni huyu au yupo mwingine..’akasema docta

‘Mimi sijawahi kutembea na mwanaume yoyote mwingine zaidi ya yeye, yeye ndiye alinibaka, na sikuwa hiyari kwa hilo tendo, aliniumiza, alishika kwa nguvu kama nilivyokwisha kusema awali…’akasema binti.

‘Bado nahitajia mawazo, …maana ni lazima huyo mtoto ahakikishiwe anapewa haki zake zote ikiwemo mama yake,..na kwa ushahidi wake imedhihirisha hali halisi, ni ipi tabia ya mume wa familia, na inavyoonekana ni kama vile bado ana watoto wengine nje, hilo nalo litakuja kutolewa ushahidi, sina shaka, …’akasema mwenyekiti na mume wa familia akainua uso kumuangalia mwenyekiti.

‘Kama nasema uwongo, nataka mume wa familia anikane…nina ushahidi wa hilo..’akasema mwenyekiti. na mume wa familia akawa anateta na wakili wake.

‘Haya mimi namuachia mke wa familia atoe kauli yake kwanza, maana tumempa muda wa kutosha wa kutuliza akili yake , haya mambo yasikieni kwa wengine, yanagusa mioyo ya watu…’akasema mwenyekiti

‘Lakini kabla sijalirejesha hilo jukumu kwa mke wa familia hii, nataka nisisitize wazo langu, kuwa kwa huyu mtoto, kwa vile imeshathibitika hivyo, tunataka kikao hiki, leo hii , kitoe tamko rasmi, tena kisheria, ili mtoto huyu atambulike rasmi kuwa ni mtoto wa nani, je ni mume wa familia, au ni wa nani,...'akasema mwenyekiti akimuangalia mume wa familia

'Ushahidi upo kuwa huyo mtoto ni wa mume wa familia,..huo utaalamu anaouhitajia yeye, upo, hautahitajia, kusubiria yeye, kuwa eti anahitajia utaalamu wa zaidi , hiyo ni namna ya kupoteza muda,..au sio jamani, lakini huko tutafika kama bado atazidi kuwa mkaidi, au sio jamani...?' akauliza mwenyekiti, na kabla watu hawajajibu mimi nikasema;

'Kama wao wanahitaji kuthibitisha kitaalamu, kivyao.. sisi hatulipingi hilo,  lakini akumbuke kuwa kuna matendo kayafanya na huyo binti, na iwe isiwe kuwa huyo mtoto ni wake, au si wake, bado yeye ana madhambi, ya kavunja sheria za ndoa yake yeye mwenyewe, na pili kavunja sheria na haki za huyo binti,..huo ushahidi upo dhahiri...labda aulizwe hata ushahidi huo wa kumzalilisha huyo binti, anahitajia vipimovya kitaalamu…?’ akauliza mama

‘Wakili unasemaje..?’ mwenyekiti akauliza, na wakili akawa anateta na mteja wake

‘Mteja wangu anasema hayo ya ushahid ni kuzalilishana, hayana umuhimu kuonyeshwa, lakini hilo la mtoto lina umuhimu wake, maana baada ya hapo, ndio ataweza kutoakauli yake..mengine kama alivyosema hakumbuki..’akasema wakili.

‘Akionyeshwa huo ushahidi alivyokuwa akizalilisha mtoto wa wezake atakumbuka tu…’akasema mama

‘Mimi naona ushahidi dhahiri upo hapa hapa,..kama alivyosema mke wangu, na ushahidi huo unaonyesha dhamira ya kweli ya mtendaji, ..aisje kusingizia ulevi, maana humo humo kuna sehemu kabisa hajalewa…’akasema mwenyekiti

‘Kiukweli nimeuangali huo ushahidi wote, ilibidi nifanye hivyo ili kujirizisha, sio kwamba nilifurahia kuuona uchafu huo, kiukweli inakera, na ukiangalia hiyo video, unaweza ukafanya jambo baya sana,..mliona kipindi fulani nilikuwa na hasira sana na huyu mtu..ni sababu hiyo..’akasema mwenyekiti.

‘Sasa kwangu mimi, nataka sheria ichukue mkondo wake, sio haki kulifumbia macho hilo, sisemi hivi kwa vile namchukia huyo mkwe wangu, hapana, ila namuangalia huyu binti, …alichotendewa sio halali, na kama mtasema liachwa hivyo hivyo, jiulize ni ni haki ya huyu binti..hilo mimi nitawaachia wana kikao hili muamue wenyewe..’akasema mwenyekiti,na kuniangalia mimi, na mimi nikasema;

‘Huo ulikuwa ushahidi mmoja katika madhambi yake mengi, kuna mtoto mwingine ambaye hajajulikana, naona sasa ni zamu ya mume wangu kuongea mwenyewe, kwasababu anafahamu hilo, na anafahamu huyo mwingine kazaa na nani, mimi naona ni muda wa yeye kujirudi, ili tusipoteze muda....’nikasema

‘Haya mume wa familia, unasikia sasa wewe mwenyewe unaitwa kama shahidi, usema ukweli wako, na ninafasi nyingine ya kutoa lako la moyoni, hatuwezi kukulazimisha kutubu, lakini unatakiwa sasa useme neno, ..maana kumbe wewe ni dume la mbegu..’akasema mwenyekiti na watu wakacheka

Na hapo wakili tena akawa akiteta na mteja wake, na wakawa kama wanasigishana, na baadaye wakili akasema;

‘Mteja wangu anasema hayo ni mambo yake binafsi hataki kuyaongea hapa,..na hata hivyo, yeye hana mtoto yoyote mwingine kama mnavyo dai nyie, hayo yote yanayoletwa kwa hivi sasa ni shinikizo, na inabidi akubali tu,...lakini huo sio utaratibu mzuri, ....kwahiyo kwa swala la watoto, analiomba lisitishwe, tuongee mengine, yeye anahitaji muda wa kulifanyia kazi...’akasema wakili.

‘Kikao hiki kinatoa madhambi ya mume wa familia, ambayo yeye aliyakana tokea awali, kama yeye angekubali kuwa kuna madhambi kayafanya, akayasema japo kwa uchache, sisi kama waungwana tungemuelewa, tukatafuta jinsi ya kumsafisha, lakini kwa ujeuri wake, akaona sisi hatujui lolote..yeye ni mjanja, aliju yeye anaweza kutuvunga akafanya apendavyo, sasa hatutayaacha madhambi yake yapite hivi hivi, yatatajwa yote, ...’mimi nikasema.

Na hapo mume wa familia akafunua mdomo na kusema;

‘Hivi wewe unaposema nina madhambi, wewe ni mungu, unafahamuje kuwa nina madhambi, huwezi kunihukumu kihivyo, hayo ni makosa tu, yoyote anaweza kuyafanya, na kwanini unasema kuwa na mtoto ni dhambi..huyo mtoto alipangwa patkane hivyo, sio kusudio langu..?.’akasema mume wangu kama ananiuliza huku kakunja uso kwa hasira.

‘Swala hapo ni je huyo mtoto umempataje,mtoto hana kosa..ndio.., ila taratibu za kumpata huyo mtoto ni zipi,....hebu tuambie, huyo aliyeletwa hapo umempata kwa njia gani, sio kwa njia ya kumbaka, hiyo sio dhambi, .?’ akauliza mama sasa kwa ukali.

‘Nimesema hilo sikumbuki mimi…’akasema mume wa familia

‘Aaah, unaulizwa kubaka sio dhambi, au wewe dhambi unaielewaje, kutembea nje ya ndoa sio dhambi au ulikuwa umefunga ndoa ya muda na huyo binti..?’ aakulizwa

‘Mnielewe jamani…sikumbuki hayo madhambi kama kweli mimi nilifanya, sikumbuki…’akasema

‘Je na huyo mtoto mwingine, hatujui umempataje huenda ni kwa kubaka hivyo hivyo, huenda hiyo ndio tabia yako ya kubaka, na ujue, uliyafanya hayo ukiwa wewe ni mume wa mtu, ukaikana ndoa yako kivitendo, ukaisaliti ndoa yako, je hiyo sio zambi?’ akaulizwa na mama.

‘Kwahiyo nyie mnataka mimi nisema nini, kama mumeamua kama familia, baba, mama mke mniandamu mimi sawa, semeni mnavyopenda, ..mimi kwa sasa nasubiria maamuzi yenu, ila nasema hivi, ndoa yangu haitavunjiki, na haki zangu zipo pale pale...kama mumelipanga hili liwe hivyo, na nyie ni waungu wa kuhuku kuwa mimi nina dhambi…sawa, lakini mkumbuke kuna mimi nina nafsi, hamjui nilivyomlilia mola wangu...’akasema kwa sauti ya kukerwa.

‘Hayo yatafuata baadaye kama unavyodai kuwa ndoa haivunjiki, na haki zako zipo pale pale. Ni sawa tutaliona hilo, hapa tumekamilika, sheria itasema, na hatutako hapa mpaka kieleweke, ...sawa si sawa…?’ akauliza mwenyekiti akimuangalia docta

‘Tupo pamoja…hata mimi ningelipenda haya matatizo yafikie muafaka, lakini pia, nisingelipenda kuwe na maamuzi ya haraka kihivyo, kama ni hukumu au maamuzi inafaa tupate muda, muhimu leo tujadilianeni tu..’akasema docta.

‘Leo kila kitu kitabainika, na maamuzi hayatasubiria,… sisi tulitaka tushirikiane na yeye kama ndugu, tukamuomba na kum-bembeleza, ili hili tatizo tulimalize kindugu, lakini yeye amasaidia vipi kulitatua hili, na umesikia kauli zake za sasa hivi, kwahiyo wakili wake ana kazi kubwa ya kufanya, kama ana ubavu huo wa kugeuza hayo makubaliano yao kimkataba, lakini pia makubaliano yetu kama ndugu,.....’akasema mwenyekiti.

‘Makubaliano gani mnayoyasema, ya huo mkataba wenu, hapana  mimi hayo makubaliano siyatambui, nilishasema toka awali kuwa ninachokitambua mimi ni huo mkataba niliokuwa nao mimi, huo mwingine sijui umetoka wapi...mnanichangany tu, mara huu mara ule, kwanini iwe mikataba miwili mimi sijui…’akasema kwa hasira

‘Naona wewe hujui sheria, kwa kukusaidia tu, wewe kaa uongee na wakili wako vizuri, atakushauri vyema kuhusu sheria, maana hapo unavyoongea, unaongea kama mtu asiyesoma, mkwe, usiniangushe...’akasema mwenyekiti, na kumfanya mume wangu amuangalie mkwe wake kwa macho yaliyojaa hasira.

**********

‘Tunaendelea na jingine, mke wa familia ulisema dhambi alizokufanyia mume wako ni nyingi, na tunaona kuwa yeye sio mtu wa kukubali na kukiri kosa, sasa ili tusipoteze muda, labda tukuulize, kuna dhambi gani nyingine, ambazo, amekiuka, na anahitajika kuwajiba nazo, au tumuulize tena mwenyewe muhusika, kuwa yupo tayari kukiri makosa yaliyobakia, ili tusipoteze muda?’ akauliza mwenyekiti.

‘Mimi sipendi kuyaongelea machafu yake,lakini yeye ananilazimisha nifanye hivyo, kama nilivyosema awali mume wangu ni mzinzi, ana tabia chafu, ambayo haivumiliki, inasadikiwa kuwa ana mtoto mwingine nje ya ndoa zaidi ya huyo aliyempata kwa kubaka…’nikasema

‘Ndio maana ningelipenda akiri yeye mwenyewe hilo, ili nimuone kuwa kweli sasa kawa ni muungwana, na yupo tayari kuwa raia mwema, kwa jamii, kwani yote tuliyomshukutumu nayo yamethibitika kuwa ni kweli,  je na hili la kuwa na mtoto mwingine nje, atalikataa...nataka nisikie kauli yake yeye mwenyewe?’ nikauliza, na mwenyekiti akamwangalia mume wangu.

Mume wangu alipoona watu wapo kimya wanamuangalia yeye, kwanza akamuangalia wakili wake, na wakali wake akamuonyesha ishara kuwa aongee, na hapo mume wangu kwa hasira akasema;

‘Sina mtoto mwingine, kama unavyodai wewe, mimi nimeona lengo lenu ni  kunizalilisha, sasa mimi nasema sina mtoto mwingine, kam yupo huyo mtoto mwingine mleteni nimuone, ili nijaribu kuvuta kumbukumbu zangu kama ni kweli….’akasema mume wangu kwa hasira

‘Una uhakika na hilo, maana sasa tukianza kutoa ushahidi mwingine, hakuna kurudi nyuma sisi tutachukulia kuwa wewe ni jeuri, hututhamini, na kwahiyo kama wanafamilia, tutahukumu, bila msamaha...’akasema mwenyekiti.

‘Nimeshawaaambia kuwa sina mtoto mwingine, kama yupo Malaya anayedai hivyo aje kama livyofanya huyo,wote kwangu hao ni wahuni tu walaghai, walifanya hivyo ili labda kunitega, ili wapate pesa, hakuna kingine ...’akasema na kila mtu akawa kimiya kwa kauli yake hiyo chafu.

‘Kwanini unazungumza hivyo, huoni kuwa hiyo ni lugha chafu kwa walengwa, na wakati wewe uliwabaka…?’ mwenyekiti akamuuliza

‘Nimechukia sana, kwani kinachoendelea hapa ni kunizalilisha na mimi, hilo hamlioni au mimi sio binadamu,..nia yenu ni kunichafua , ili nionekane mbaya, na mwisho wa siku mfanye mnavyotaka, mimi nimechoka, na labda niseme hivyo, maana hamtaki ombi langu, nyie fanyeni maamuzi yenu muonavyo ni sahihi…’akasema

Na watu wakabakia kimia, hawaamini anachokiongea huyo mume wa familia.

‘Na narudia hivi,  kauli yangu ni ile ile, mimi sikubali kuvunja ndoa yangu,na wala sikubali kuachia chochote kilicho changu,  kwa ajili ya hawo wajanja wajanja, hao ni wahuni tu ,…na sitasita kuwaita Malaya,..’akasema na wakili wake akamzuia kuongea hivyo.

‘Ni Malaya tu,..kama wameamua kutumia ujanja wa mwili wao kupata pesa kutoka kwangu, na kudai eti watoto wangu, kama yupo malaya mwingine kama huyu aje athibitishe hayo, kuwa ana mtoto wangu, mimi sina mtoto na Malaya yoyote zaidi ya mke wangu huyu hapa...’akasema na kauli yake ilikatishwa, kwani kuna mtu aligonga mlangoni, na sote tukageuka kuangalia mlangoni.

Haikupita muda, huyo mtu akagonga tena , na kufungua mlango, ….

Kiukweli pale nilipokuwa nimekaa nilijikuta nikishikwa na mshangao, .na niliona hali hiyo pia ilitokea kwa wengine…!

Hakuna aliyetegemea…..

Rafiki yangu alikuwa kasimama kati kati ya mlango, akiwa na mtoto wake mkononi..

‘Hiyo kauli chafu imenikera, ...unafikiaje kutuita sisi Malaya, wewe ambaye uliyetembea na wanawake wengi tutakuitaje, au unataka tuseme kila kitu, sasa mimi nimefika, nasema hivi huyu hapa ni mtoto wako niliyezaa nawewewe,....’akasema rafiki yangu, ...’

Watu wote walijikuta wakishikwa na mshangao, hakuna aliyesema neno kwa muda huo hata mwenyekiti alikuwa kimia, akimuangalia huyo aliyeingia, na mimi hapo nikapata nafasi ya kugeuka na kumuangalia mume wangu,  alikuwa kwenye mshangao wa aina yake..ni kama haamini.

Mwenyekiti alipoona hiyo hali, akasema;

‘Hebu kidogo,..naona haya mambo yanajirudia , nilichokikataa kinajirudia tena, hii maana yake ni nini…huyu mtu alistahiki kuwepo kwenye hiki kikao.., na ni ustaraabu gani huu…’akasema mwenyekiti.

‘Samahani mwenyekiti, nilipewa taarifa ya kuwepo kwenye hiki kikao, lakini kutokana na yaliyotokea, sikupenda kufika kabisa…hata hivyo, ikafika muda, nikaona ni kwanini nisiwepo, ni kwanini isiwe nafasi ya kuja kuusema ukweli..’akasema.

‘Na kwa bahati, …ila sikutarajia hili, ..nilikuwepo hapo nje muda mrefu tu, nikisita kuingia ndani, na kauli hizo chafu za kutuzalilisha sisi wanawake ndizo zimenifanya niingie, nije ..nipambane na huyu mtu anayetuzalilisha wanawake..’akasema

‘Lakini sio ustaarabu ulioufanya..’akasema mwenyekiti

‘Samahani sana,…ila mwenyekiti, mimi naona mnapoteza muda wenu na huyu mtu , hatutaweza kukaa kimiya tukisubiri huyu mtu aseme ukweli, ambao hataweza kuusema, huyu mtu ni mwongo,mzalilishaji mbakali na pia anahusika na uuwaji,..’akasema

Mume wangu akataka kusema ..lakini wakili wake akamzuia..

‘Kama mtu huyo ana tabia hizo, unategemea nini, nawaambia ukweli, mnapoteza muda wenu bure, je hamna mambo yenu mengien ya kufanya, mpaka mumbembeleze mtu kama huyu,, imeniuma sana, …anafikia kutuita sisi malaya...’akasema rafiki yangu kwa sauti .

‘Mimi nataka anijibu swali langu kuwa ni nani Malaya, yeye aliyetembea na wanawake wengi huku ana ndoa yake halali au sisi ambao kwa hadaa zake alituzalilisha, ..ni nani Malaya?’ akauliza rafiki ynagu kwa hasira.

‘Kwani nilikuja nikakushika kwa nguvu,....wewe ulijileta mwenyewe kwangu, ukidai unataka mtoto, au umesahau, usitake nikakuumbua bure hapa...’akasema mume wangu kwa hasira.

‘Wewe mwanaume, mimi nilikuja kwako nikakuambia nataka mtoto,..?’ akauliza kwa mshangao.

‘Umesahau eeh…’akasema na kutulia, baada ya kuhis wakili wake akimzuia.

‘Sio kwamba mipombe yako ilikutuma na kunitilia dawa ya kulevya kwenye kinywaji kwa siri, nikazidiwa, ukanifanya ulichonifanya huko sio kubaka, wewe ni mbakaji, na sio mara moja, kama wewe ni mwanaume kweli kwanini utumie mbinu hiyo,…’akasema

‘Sema sasa kama wewe ni mwanaume kweli kwanini ulishindwa kuongea.....na ole wako, chunga sana kauli yako, na ninakuambia hivi yale yote uliyoyaandikisha kwa ajili ya huyo mtoto ninayataka yote, nimeshayawakilisha hayo maombi kwa wakili wangu, sikutaka kufanya hivyo lakini sasa utawajibika,…unasikia utawajibika...’akasema rafiki yangu kwa hasira.

‘Kama una wakili wako na mimi nina wakili wangu, usinibabaishe, ...hukutaka kukubali matakwa yangu toka awali, sasa unakuja kwa nyodo, hupati kitu hapa, nimeshakuambia,..wewe si umekataa na mtoto wako, haya kaa naye sasa, umtafute baba yake, sio mimi...’akasema na wakili wake akamkatisha na kumtuliza.

‘Jamani hebu kwanza…’akasema mwenyekiti, lakini mama akamzuia, amueche huyo mdada aendelee kuongea;

‘Ndugu mwenyekiti samahani sana, sikutaka kuyasema haya yote kama hivi, ilitakiwa niyasema ili kuondoa hii sintofahamu lakini sio kwa utaratibu huu, ila hatua iliyofikia inabidi niseme kila kitu, ili mumuone huyu mtu jinsi alivyo, nakiri kuwa kweli nilimkosea rafiki yangu, lakini ni lazima mwisho wa siku tumtambue mbaya wetu ni nani...’akasema rafiki yangu.

‘Mimi nimekuwa hapo nje nikisiliza yote , awali nilikuja na ajenda nyingine kabisa ya kutaka kumsaidia huyu mtu, kumbe ni mtu mbaya sana , sikumuelewa kabisa,..sasa wakati umefika wa kusema ukweli wote, na nasema ukweli wote sitaficha kitu ili haki itendeke, hata kama mimi ni mkosaji, basi niwajibike kwa madhambi yangu…’akasema rafiki yangu

‘Najua rafiki yangu hatanielewa kwa hivi sasa…, lakini univumilie kwa hili..na yale uliyokuwa ukiniuliza leo utayapata majibu yake hapa hapa, kuwa huyo mume wako sio mtu mnzuri, ni Malaya, mbakaji, muongo, mwizi, ..na sifa zote mbaya, anazo, hakustahili kabisa kuwa mume wako…’akasema akimnyoshea kidogole mume wa familia

‘Usininyoshee kidole wewe mwanamke, ..usitake kikao hiki kikaharibika,.kama umekuja na yako, fanya yaliyokuleta, si unataka upate mali, haya,…endelea na tabia hiyo kama utazipata…ndio zenu.’akasema mume wa familia na wakili waka akawa anamsihi.

‘Nitakunyoshea sana maana, muda wa kukueshimu umepita, nilikuheshimu sana kipindi cha nyuma, lakini sio sasa, umejivunjia heshima yako wewe mwenyewe, umajitoa kwenye ubaba, ulezi, ..ushemeji na kujitwika yasiyostahiki…na ..’akajizuia kulia

‘Ongea tu, hiyo ndio shukurani yako…na toka humu ndani maana hujaalikuwa, umekuja na mihasira zako, ulitaka nikumbembeleze, sasa sikiliza hupati kitu , Malaya mkubwa wewe..’akasema mume wangu na wakili wake akamzuia.

‘Shukurani gani wewe upewe, ..utufanyie unyanyasaji, utuzalilishe, ututukane , halafu utegemee shukurani, ..nakuambia hivi mimi sikuogopi, usinione hivi, mimi ninaweza zaidi ya hili, mimi sio mwanamke kama wanawake wengine, kama ni kupigana nipo tayari, na wewe wala hunishindi, nitakuzalilisha mbele ya watu hawa, umeniuzi sana mimi…’akasema.

‘Kwahiyo unataka nikuonyeshe mimi ni nani, sio…ukweli umekuuma eeh..’akasema mume wangu.

‘Ukweli gani, ..sasa, ulikuwa hujaniafahamu mimi upande wa pili wangu,s asa utanifahamu…umemtoa nyoka pangoni, sasa atakuuma, mimi nitawaambia watu wote hawa kila kitu ...bila kuficha, nilishaahidi kuwa nitasema kila kitu siku ikifika, naona sasa muda umefika...’akasema rafiki yangu sasa akimsogelea mume wangu.

‘Aah, usimsogelee, kaa pale kwenye kiti kile cha ushahidi…’akasema mwenyekiti wake..

‘Ndugu mwenyekiti, huyu mtu hajaalikwa hapa, mnamkaribisha, huyu kaja na yake kwa vile kakosa alichokitaka, huyu mtu ni muongo mkubwa, hana jipya hiyo ndio tabia yake,…amekuwa akimtimua mke wangu, kujinufaisha, na baadae kaja kumsaliti rafiki yake mwenyewe, ..hapa, sasa a jifanya kujikosha..nakuambia hivi, wewe mwanamke kwa sasa hupati kitu kwangu na kwa rafiki yako umeharibu,umalaya wako umekuponza ....’akasema  mume wa familia, bila kujali

Na hapo mwenyekiti akaingilia kati na kusema;

‘Hebu tutulizane kwanza, na nawaombe nyie wajumbe wawili mrekebishe hizo kauli zenu, tusija kukifanya hiki kikao cha watu wasio wastaarabu, .na kwa hizo kauli  tutahitaji uhalali wake, huwezi kutamka tusi,au nen la kashifa kwenye kikao kama hiki lipite bure, utastahiki kulitolea ushahidi, vinginevyo, wewe mtamkaji utashitakwia kwa kutoa maneno machafu mbele ya kikao halali..’akasema mwenyekiti

‘Mimi nitathibitisha kauli yangu mwenyekiti, hayo maneno niliyotamka dhidi ya huyu mtu ni kweli na nina ushahid nayo…’akasema rafiki yangu

‘Hata mimi nitathibitisha  hayo ya kwango dhidi yako, ya kuwa wewe umekuja hapa kwa nia ya kujikosha tu, na ni kutokana umekosa ulichokitaka kutoka kwangu, mimi sio mtu wa kuchezewa...’akasema mume wangu.

‘Subirini tutakwenda hatua kwa hatua,.., tutakuhitaji nyote kuyathibitisha hayo maneno yenu la sivyo kikao kitawajibika kuwachukulia hatua…. kwanza nataka tutulie, maana naona mambo yanajileta yenyewe, tunakuomba ndugu uliyeingia, utulie kwanza, ili tufuate utaratibu wetum huwezi kutuingilia na kuharibu ajenda zetu...’akasema mwenyekiti.

‘Ndugu mwenyekiti, naomba mnipe hii nafasi , niongee, nafahamu mna utaratibu wenu, lakini naona kuna mengi yalitokea, na imefikia mimi  kuonekana mbaya, hata kwa rafiki yangu, na ubaya zaidi ukaka kupandikizwa juu yangu,…’akasema

‘Ubaya huo ni wa mauaji ya Makabrasha, nakuja kushangaa, naambiwa mimi nilihusika, wakati huyo mnayemuita mume wa familai siku hiyo alikuwepo, wakati marehemu anauliwa, yeye anafahamu kila kitu,.. hebu muulizeni vizuri siku hiyo kule kwa Makabrasha alifuata nini, na wakati alistahiki kuwa hospitalini,…je aliwezaje kufika huko..huyu ndiye muuaji, anafahamu kila kitu...’akasema na watu wakawa wametulia kimiya.

‘Hayo ni yako…mimi sijui kutumia silaha, wewe ni mtaalamu wa silaha, je sio wewe uliyefanya hayo mauaji, ili kunibambikia mimi, unejileta mwenyewe…’akasema mume wangu

Mwenyekiti hapo akatulia kwa makusudi…

‘Unataka nielezee siku ile ilivyotokea au sio, maana wewe huamini kitu mpaka uambiwe ukweli, wakati ni kweli ulikifanya, ndio tabia yako, sio…sasa ‘akatulia akimgeukia mwenyekiti.

‘Naomba kibali chako, ndugu mwenyekiti ili nisema kila kitu kwa ukweli wake na ushahidi, sitako niongee kama yeye, umeniuma sana, maana nimefika kutoka masomoni na kukamatishwa watoto wa kihuni wanifanyie unyama,…mimi, wakati mbaya mwenyewe yupo, kwanini yeye asifanyiwe hivyo,  leo ni lazima niseme…’akasema

‘Sawa utasema lakini ngoja tufuate utaratibu..’akasema mwenyekiti

‘Samahani mwenyekiti ninaona kabla huu mukari haujashuka, uniache mimi niendelee kwanza, sitaweza kuvumilia, mkizunguka zunguka, wakati muhalfu yupo nanyi, na ninavyomfahamu hatakubali ukweli, mtazungushana naye tu, tafadhali mwenyekiti, mimi nafahamu kila kitu mnachokihitajia…’akasema

Mwenyekiti akageuka kuniangalia mimi, halafu wakili wa mume wangu, kabla hajasema neno, rafiki yangu huyo akasema;

‘Mimi sijawahi kutukanwa hivyo, eti mimi ni malaya… eti kwa vile nimetembea na mume wa mtu, yeye huyo mume wa mtu ataitwa nani, mbakaji mkubwa huyo, yeye ndio Malaya, tena wa hali ya juu, mbakaji ana sifa gani..ni nani mwenye dhambi kubwa, kati ya mtu mwenye ndoa na asiye na ndoa, kwenye maswala ya uzinzi, aniambie yeye,..’akasema na alipoona mwenyekiti anamuangalia yeye, akasema

‘Samahani sana mwenyekiti,..naomba nikae hapo kwenye hiki kiti maalumu, ili niweze kuwaelezea kila kitu kiushahidi na mwisho wake, tutaona ukweli upo wapi, kuwa mimi ni Malaya au ni yeye...’akasema na kwenda kukaa kwenye kiti cha mashahidi.

**********

‘Mke wa familia unasemaje, tuendee naye au una shahidi mwingine?’ akaniuliza mimi na wakati huo nilikuwa nimeshikwa na hasira, sijui kwanini nikimuona huyo rafiki yangu, ninakuwa hivyo, nilitamani wale wahuni waje, wamfanyie ubaya mbele ya watu wote hawo, nikamwangalia huyo rafiki yangu kwa macho ya hasira, maana nilishampatia dhabu yake na haikuwahi kufanyika,…hapo nikamwambia mwenyekiti.

‘Nataka huyu mtu asema ukweli wote, na haki itendeke, kwani wote lao ni moja,  mume wangu, na huyo rafiki yangu, alikuwa rafiki yangu, kwasasa hivi sio rafiki yangu tena, nawaona wote lao ni moja, kwangu mimi ni wasaliti, sina msamaha na hawa watu wawili, ....’nikasema

‘Mke wangu…’akataka kuingilia mume wangu na mwenyekiti akamzuia kwa ishara ya mkono, na rafiki yangu akachukua nafsi hiyo kwa kusema;

‘Hata wewe usijitetee, na kujiona msafi sana nakuheshimu sana, na nitaendelea kufanya hivyo…ila na wewe una mapungufu yako.., kwani isingelikuwa wewe kunishauri haya, unafikiri mimi ningeliyafanya …nisingeliingia kwanye ubaya na mume wako,..’akasema

‘Lakini hayo kwangu nimeyasahau, ..najua hata nifanye nini, ubaya wangu hauwezi kuzidi haya niliyokufanyia, lakini…kuna mbaya wetu zaidi, ambaye anastahiki kuzibeba lawama zote hizo,..huyo mume wako,…, uneyemuita mume wako, nataka leo akitoka hapa, anaelekea jela, kwani hastahili kuishi kwenye maeneo ya raia wema, nina ushahidi wa kutosha, kwa hilo wa kumweka, ndani...’akasema rafiki yangu.

Mume wangu akajifanya kucheka na kutikisa kichwa, huku akimuangalia wakili wake, na wakili wake akamuashiria atulie kwanza..lakini mume wangu hakuweza kutulia akasema;

‘Usinitishe wewe, ....toa huo ushaidi wako, na mimi nitakuja kutoa ushahidi wangu kuwa wewe ni Malaya, pili mlaghai, na tatu, msaliti, na pia wewe unahusika na mauaji ya Makabrsha,..utasema ukweli ulikuwa wapi siku ile…nilikuja kuyafahamu hayo, wewe siku ile tokea muda mrefu ulikuwa na marehemu, ukajifanya kujificha uwanja wa ndege…’akasema mume wangu

‘Haya sawa, ngoja tuone mimi na wewe ni nani zaidi, si ndio hivyo, kikao kitatusikiliza, kila mtu atoe ushahidi wake, na uwe wa ukweli, na hapo ndio tutaona ni nani malaya, ni mimi au wewe, ninani ana sifa hizo mbaya, usaliti, wizi, ubakaji, umalaya na uuaji, tuanza kazi mwenyeki....’akauliza akimgeukia mwenyekiti, na mwenyekiti akageuka kuniangalia mimi.

Na mimi nikaguka kumuangalia wakili wangu…

NB: Haya mambo yamekwenda haraka kihivyo, tumerahisishiwa kazi…, lakini ndivyo ilivyotokea, tuwepo kwenye sehemu ijayo,


WAZO LA LEO: Tuchunge sana kauli zetu tunapoongea, kuna maneno yakitamkwa mbele za watu, yanakuwa na picha mbaya, lakini kuna watu ni wepesi  kuyamtamka hayo maneno kama vile ni maneno ya kawaida, kwa lugha sahihi, yanaitwa ‘lugha za matusi’ .


 Kuna baadhi ya watu wanayatuma haya maneno bila kujali anayamtaka wapi, na kwa nani, na anamlenga nani, baya zaidi, wengi wanaozalilishwa kwa maneno hayo ni akina mama, ...iweje ugombane na mtu mwingine baki, wewe unakimbilia tusi linalomlenga mama, mzazi wa mwenzako, unamtusi yule mtu mwenyezi aliyekuzaa, je  huyo mama kakukosea nini, ...tuchunge sana ndimi zetu, kwani tunajilaani sisi  wenyewe kwa kauli zetu chafu.

Ni mimi: emu-three

No comments :