Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, February 12, 2018

MKUKI KWA NGURUWE-79



Mwenyekiti alituliza kikao baada ya kuona kuna majibishano makali kati ya rafiki yangu na mume wangu, kiasi kwamba kama asingeliingilia kati yangelizungumzwa mengi ambayo hata hayakustili kuzungumzwa kwenye hicho kikao bila mpangilio maalumu..

Tuendelee na kisa chetu…

************.


Rafiki yangu alipewa kibali cha kuongea na mwenyekiti, akawa anatoa maelezo yake, japokuwa mimi akili yangu ilikuwa mbali sana, lakini niliweza kumsikiliza, rafiki yangu alisema;

‘Nitatoa maelezo yangu katika sehemu kuu mbili, ya kwanza ni ukweli kabla sijapata mtoto na sehemu ya pili yenye ushahidi mnzito, ni ukweli baada ya mimi kujifungua, naomba muwe watulivu, ili niweze kuyasema yote niliyoyakusudia kuyaongea leo hii...niliahidi na sasa natimiza’akasema na kuniangalia mimi.

‘Mimi ninaamini kwamba kila jambo huja kwa minajili fulani, na hili la kupata mtoto huenda na kweli limetokea ili iwe fundisho sio kwangu tu, na hata kwa wale wote lililowagusa kwa namna moja au nyingine. Ni changamoto, ambayo sitaweza kuisahau katika maisha yangu, ....’akasema

‘Hii ni changamoto iliyonipa fundisho moja kubwa, kuwa kutaka kupata kitu kwa njia zisizo halali, zina mateso baadae, usijione umepata ukadhani umefanikiwa, mitihani yake ya hicho ulichokipata kwa njia isiyo halali huja baadae, na huko ndipo kwenye majuto…’akatulia

‘Kiukweli mimi nimechelewa kuzaa, na sababu kubwa, naweza kukiri kuwa ni madhaifu yangu ya kupenda kuchagua…nisipoteze muda huko, ni kwanini ilikuwa hivyo, lakini kitu kilichokuja kunigusa baadae ni kuwa, nilikuwa nataka kupata mtoto, sasa swali likaja nimpateje..’akatulia

‘Madhaifi yangu yapo pale pale, nikitaka kitu nakichanganua sana, haya nataka mtoto aweje, na ..afananeje..hilo likawa ni changamoto pia kwangu, kiukweli sio siri, kuna watu niliowapenda, bahati mbaya wengi niliowapenda walikuwa waume za watu, siwezi kulificha hili..hata hivyo sikupenda kuvunja ndoa za watu, nikiwa na maana sikutaka kabisa mahusiano na mume wa mtu.

‘Mimi nilifikia kuhini ahadi yangu ya kuzaa ndani ya ndoa, na pili kwa mume asiye kuwa mume wa mtu, na ilipotokea nilitaka iwe siri kubwa..na pia nikata mtoto huyo asiwe na baba, japokuwa huwezi kuzaa mtoto bila baba, haya nitayaeleze kinamna, kwa jainsi tunavyokwenda..’akasema

Japokuwa nilipanga iwe hivyo, kuwa mtoto ni wangu, na hana baba, lakini mume wa familia alipogundua kuwa nimejifungua, akawa wa kwanza kufika hospitalini, na alipomuona tu huyo mtoto, aligundua kuwa ni wake...haijifichi.

'Kiukweli mume huyu alipagawa hasa pale alipojua kuwa mtoto huyu ni wa kiume maana ndoto yake kubwa ilikuwa kupata mtoto wa kiume,na hapo hapo akasema huyo ni mtoto wake, hakuna ubishi,...

‘Siku ile nilipojifungua nilijaribu kila njia ili huyo mume asijue lolote, lakini ilishindikana, na kama nilivyosema kila kitu huja kwa sababu fulani, nahisi hata kufanana kwa mtoto huyu na huyu mwanaume ni sababu maalumu ya kuliweka hili jambo liwe bayana.

‘Siku ile ile nikajua sasa mambo yatakwenda kinyume na  matarajio yangu, kinyume na makubaliano yangu na mshauri wangu mkuu, kuwa nikizaa, hata kama nimezaa na mume wa mtu , hiyo iwe iri yangu mimi mwenyewe asije kufahamu mtu yoyote.

‘Mimi ninahisi kilichomfanya mume wa familia ang’ang’anie sana ni kwa vile nimepata mtoto wa kiume, na yeye kwa kauli yake mwenyewe, alikuwa akitaka mtoto wa kiume, maana watoto alio nao hadi sasa na mke wake , ni watoto ni wa kike...'akarudia sehemu hiyo.

'Kiukweli mimi sikuyajali hayo kwani mipangilio wangu ulikuwa nizae mtoto, na huyo mtoto awe ni wangu wote hata nikiandikisha jina lake kwenye cheti chake, lisomeke jina lake,na ubini wa baba yake, liwe ni jina langu kwa herufi yangu ya mwanzo, halafu jina la tatu liwe la baba yangu mzazi  ndio nilivyotaka  iwe hivyo...'akatulia

Lakini baadaye tulipokutana mimi na mwanasheria wao na mume wa familia, mume wa familia akasema hilo halikubali, mtoto huyo ni wake, kwani yeye ndiye mume aliyeweka mbegu, naye pia ana haki zake na anawajibika kwa mtoto,na hata kisheria za nchi, inabdii iwe hivyo.

Kwahiyo akanisihi kuwa mtoto huyo aandikwe kwa ubini wa baba yake, nilikataa, na huyo wakili akarudi kwa mume na wakaongea walichoongea, na aliporudi kwangu, akasema mume huyo kasema huyo mtoto ni lazima atambulikane kuwa yeye ni baba yake, na hili atalifaya nipende au nisipende. 

'Sasa hiyo upende au usipende ina maana gani, ndio hapo utaona mbinu walizokuja kutumia baada ya kuona mimi nimekaidi maagizo yao, nitayaeleza hayo kwenye ushahidi wangu wa pili,..ambao una mambo magumu zaidi…

Kabla ya hiki kikao tulikutana mimi na yeye, moja ya ajenda yake ni hiyo ya mtoto kutambulikana kuwa huyo ni mtoto wake kisheria, ...maana mimi nilishakataa...pamoja na mengine mengi aliyoyataka, mimi nikawa kinyume chake...'akatulia

 Kwahiyo yeye akaja huku kwenye kikao, akisema akifika huku kwenye kikao atahakikisha kuwa huyo mtoto anatambulikana, kwa vile anao uwezo wote kikatiba yao ya kifamilia,

'Kwa vipi ...?' akaulizwa

'Alisema mkataba alionao yeye unampa hiyo nafasi, alinionyesha huo mkataba, lakini niliuona una utofauti mkubwa na ule mkataba ambao niliwahi kuusikia kutoka kwa rafiki yangu , sikuwahi kuusoma huo mkataba wao wote kiundani maana ni mambo yao ya kifamilia, lakini kwa kauli ya rafiki yangu, mkataba wao, ulikuwa hauruhusu mume au mke, kujitwalia madaraka bila kumshirikisha mwenzake. Ndivyo nilivyokuwa nafahamu hivyo.

Na nakumbuka rafiki angu huyo aliniambia kuwa kama mmoja akimsaliti mwenzake, na ukapatikana ushahidi bayana, na ushahidi bayana unaweza ukawa wa kuona tendo likitendeka, au ushahidi wa vielelezi kama hivyo mtoto wa nje..basi mtenda kosa kavunja mkataba, na hapo atawajibika, ..kama mkataba wao unavyosema

'Kwahiyo mpaka hapo nilijua kabisa hili jambo likija kugundulikana ndoa hiyo haipo tena,..na ukumbuke kufahamu kuhusu mkataba wa kifamilia nimekuja kulifahamu hilo baada ya mimi kupata mtoto, mkataba wao huo ulikuwa siri yao, wanafamilia haou….mnielewe hapo,….'akatulia

'Na nilikuja kumwambia wazi huyo mume wa ndoa siku kadhaa alipokuwa akizidi kung’ang’ania kuwa huyo mtoto ni wake, ilibidi nimkumbushe hilo, baada ya kugundua kuwa kumbe wana mkataba mkali kama huo...'

‘Wewe unataka huyu mtoto hujui kutambulikana kwake ndio utakuwa ushahid wa kuvunja ndoa yenu? Nilimuuliza hivyo, sasa uone alivyonijibu…’akasema


‘Hilo nimeshalifanyia kazi,  kila kitu kitakwenda sawa, mimi ndiye mumiliki wa kila kitu,na nina madaraka yote, kuna mambo macheche tu hayajakamilika, lakini yapo mbioni kukamilika,..'akasema

'Kwa vipi..?' nikamuuliza

'Wewe utayaona tu, haya yalishapangwa, na yatafanyika tu, usicheze na watu na fani zao, kuna mtu mkali analifanyia kazi, hutaamini..'akasema

'Kwahiyo unataka mimi nifanye nini..?nikamuuliza baada ya kuona ananitishia maisha’

'Wewe ninavyotaka mimi,  hii hatua ya kwanza ikipita, utaona, kuna ujanja ujanja mwingine unatakiwa utumiwe, mke wangu akikubali baadhi ya mambo, na ukapatikana ushahid basi mkataba huo utakuwa umeshafanyiwa kazi,...kila kitu kitakuwa mali yangu, na hapo nitajua jinsi gani ya kukuingiza wewe.

‘Kuniingiza mimi kwa vipi..?’ nikamuuliza

‘Kama mshirika mwenza, wa kila hali, na huenda tukajaliwa kupata watoto wengine zaidi...'akasema

‘Kwanini unataka upate watoto na mimi, kwani mke wako hatoshi..?’ nikamuuliza

‘Hataki, mke wangu hataki,  yeye anasema kazi kwanza, tuej kuzaa kwa malengo, mimi sioni ubaya wa kuzaa, maana mali tunayo, na watoto ndio wa kuzitumia, na sasa hivi tuna mabinti, wataolewa ni nani wa kuendeleza mali zetu…’akaniambia hivyo

Hapo mume wa familia hakuweza kuvumilia akasimama na kusema;

'Mwongo wewe, hivi kwanini unataka kusema huo uwongo, usiseme lolote kuhusu watoto wangu, mimi nawapenda sana watoto wangu, sikiliza tunga uwongo wako wote lakini usiguse watoto wangu, …mke wangu usimsikilize huyu lengo lake ni kuniharibia ndoa yangu…na wewe,..' mume wa familia akaingilia kati kumkatisha mzungumzaji huyu.

'Hahaha, unataka nitoe ushahidi,…?’ akauliza

‘Ndio toa, una ushahidi gani wewe acha uwongo wako..?’ akasema

‘Una uhakika na unachokitaka, unauhakika unataka nitoe ushahidi  au unasema tu kujihami?’ akuliza mzungumzaji na mume wafamilia alitaka kuongea kitu, lakini wakili wake akamzuia. Wakawa wanateta kwa chini chini…

‘Kama unataka niyathibitishe haya kwa ushahidi mimi nipo tayari, ushahidi upo, nikipata kibali kutoka kwa mwenyekiti nitafanya hivyo…’akasema mzungumzaji

‘Ushahidi gani ulio nao wewe…?’ akauliza wakili wa mume wangu

‘Muhimu ni ushahidi, ..siwezi kukuambia kwa hivi nina ushahidi gani, lakini ushahidi upo, nikipata kibali nitauotoa hadharani, ..’akasema akimgeukia mwenyekiti

‘Je naweza kuutoa huo ushahidi…?’ akauliza, na mwenyekiti akageuka kuniangalia mimi, halafu akageuka kumuangalia wakili wake, halafu akasema;

‘Kama kikao, kwa hivi sasa tunahitajia maelezo tu, nia yetu ni kuwaptia nafasi waliokosea wajirudi, wawe wakweli kwetu, tulimalize hili kwa amani, na kama kuna makosa mengine ya kisheria, hayo sio juu yetu,…sasa mpaka tunafikia hatua hii ni kwamba watu hawataki kujisalimisha na kuomba msamaha, lakini sasa wataendelea hivyo haitakuwa na budi, kila kitu kitawekwa hadharani..’akasema mwenyekiti

‘Kwahiyo mwenyekiti unasemaje..?’ akauliza mzungumzaji.

‘Labda utupe maelezo yako tu, kuwa una ushahid wa namna gani, mengine yatafuata baadae…’akasema mwenyekiti.

‘Tulipokuwa na kikao hicho mimi na yeye tulikuwa wawili tu, lakini mimi nilikuwa na kitu cha kurekodi mazungumzo yetu, na kipo tayari hapa kama ushahidi je nitoe hayo mazungumzo yetu yasikike na kila mtu, na tusije kulaumiana baadae..?’ akauliza mzungumzaji

‘Ndio toa…’akasema mume wa familia, baadae wakili wake akawa anamzuia, wakawa wanateta, jambo, mzungumzaji akawa anasubiria wamalize, na alipoona wanaendelea kuongea kupoteza muda, yeye  akasema;

‘Nilishajiandaa kwa haya yote na usahidi kila hatua ni muhimu sana, kama itabidi, nitautoa huo ushahidi na watasikia yote na yale ambayo mume wa familia hatapenda yasikike hapa kikaoni, …’akasema

‘Sawa tumekuelewa…’aliyesema hivyo sasa ni wakili wa mume.

‘Ni kweli maana mume wa mtu alikuwa akinibembeleza, akasahau kuwa ana mke, sasa hayo yakisikika, sio vizuri, au sio, au niyasema hapa ulivyokuwa unanitongoza,..’akasema na watu wakaguna

‘Ni kweli haya ninayoyaongea, ameongea mengi sana na ya aiabu,…wakati mwingine nahisi huyu jamaa yetu hayupo sawa, namuheshimu sana, lakini kavuka mpaka,..na jamani kwa hali kama hii aliyo nayo bado huogopi,.. lakini ndio hivyo, mimi nahisi marehemu alimteka sana akili yake maana yule shemeji ninayemfahamu sio huyu wa sasa,…na pengine, ila mimi sina uhakika na hilo, nasema pengine, hiyo ajali yaweza kuchangia..’akasema.

‘Wakati mnaongea naye, kwa kugusia tu mliongea maswala yapi na yapi, ambayo ni muhimu kama kikao wakayafahamu…?’ akaulizwa

‘Kuna mengi, aliyaongea, mimi kama binadamu siwezi kuyasema au hayafai kusikilizwa hapa mbele za watu, ..maana huenda hakunifahamu kuwa mimi ni nani, wakati namchota akili, na akaingia kwenye anga zangu, akajikuta anaongea kila kitu, hahaha, wewe mtu, uwe makini, hajui kwa hivi sasa kila kauli yake inachukuliwa kwa uzito mkubwa sana, chunga ulimi wako wewe mtu..kwa kuhusu seehmu hii kwa tuliyoyaongea ni hayo, labda kwenye shemu ya pili...'akasema na hapo mume wangu akanywea.

‘Endelea,…kama ushahidi tutauhitajia tutakuambia baadae … ila nina swali..’akasema wakili mtetezi

‘Kuhusu nini…?’ akuliza mzungumzaji
‘Wewe, unaposema kuwa hayo uliyoyafanya uliyafanya kwa kushinikizwa, sio kwamba ulifanya baada ya kuona kuwa mkataba wa familia utakuja kukunufaisha, na sasa unajifanya kujikosha ili uonekane wewe ni mwema..?’ akulizwa na wakili.

‘Kuhusu huo mkataba wao, sikuwa naufahamu kabla, kwani pia unaweza kusema kuwa nilifanya makusudi ili nipate mtoto na huyo mume, ili ndoa yao ivunjike, ili mimi nije kuchukua nafasi ya mke wa mume wa familia, na mali iwe imeshaandikiswha kwa mtoto wangu,..ndio mawazo yak ohayo sio…, au sio..?’ akawa kama anauliza. Na wakili akabakia kimia tu!

‘Hiyo sio kweli, mimi tokea awali nilishawaambia sitaki lolote kuhus mtoto wangu, na pia sina tamaa ya mali, hasa mali hizo za kitapeli, niliwaambia hilo mapema sana wakanishangaa…, na hata kwenye kikao chetu cha hivi karibuni, kama mtataka kuyasikiliza haya mazungumzo utasikia nikilisisitizia hilo, naombeni sana  mniamini kwa hilo. Hapa nazungumzo ukweli kutoka moyoni mwangu...'akasema.

‘Kwani kuwepo kwa huo mkataba wao,  ulifahamu lini…?’ akaulizwa

Mimi huo mkataba wao wa familia, niliufahamu kutoka kwa maelezo y abosi wangu maana alikuw ani rafiki yangu, hakunificha hilo, lakini sio kwa undani wake, na wala hakuwahi kunionyesha …lakini huo mwingine uliokuja kutengenezwa baadae, nilikuja kuelezewa tu , juu, kwa juu, hawakutaka uonekane.

Nilioweza kuuona, ni huo wa kuhamisha hisa..ili nione kuwa hata mimi nipo, na huo niliuona baada ya kuchukuliwa na wao hado ifisini kwao, niliporudi kwa dharura..’akasema

‘Ulirudi kwa dharura, au ulirudi kwa vile umehakikishiwa mafao…usitake kudaganga watu hapa, hilo jambo la kibali ungeliweza kulimalizia huko huko…’akaambiwa

‘Ushahid upo, huko chuoni, na sehemu za vibali za kwenda kusoma nje, nenda kafuatilie, hapa nina ushahidi wa barua niliyoandikiwa, kuwa kuna tatizo la kibali changu natakiwa kurudi nchini kukamilisha baadhi ya taratibu, ‘kurudi nchini’ ipo wazi inasomeka, mimi nisingelipoteza muda wangu wa masomo kwa hayo mambo yao ya kitapeli..’akasema

‘Je wewe unahisi, hiyo kurejeshwa nchini  ni mbinu au ni taratibu za kawaida za vibali…?’ akaulizwa sasa na mwenyekiti.

‘Mpaka sasa kwa uhakika sijalithibitisha hilo, kuwa labda kuna watu wapo nyuma ya hilo tukio,  ila kikao kikitaka mimi naweza kuifanya hiyo kazi na nitaweza kuwatolea maelezo yenye uhakika..’akasema

‘Haya endelea na maelezo yako..’akaambiwa na mwenyekiti, japokuwa wakili mtetezi bado alikuwa na maswali anataka kuuliza.

*************.

 ‘Siku nilipofika uwanja wa ndege nikiwa najiuliza kuna nini kimetokea kuhus kibali changu, kiukweli, moyoni nilikuwa nimemuhisi mdhamini wangu, yaani rafiki yangu kuwa huenda kayafanya hayo kwa makusudi, lakini nimjuavyo yeye, asingelifanya hivyo, angeliniambia moja kwa moja..’akasema

‘Na mpaka nafika uwanja wa ndege bado nilikuwa najiuliza. Na ujuavyo kazi zangu huwa zinanifanya niwe na akili ya ziada, nikawa najiuliza je kama ni kuhusu tatizo la mtoto labda,…ili kumpata baba wa mtoto,basi mtoto wangu anaweza kuwa hatarini.

Nilipojiwa na wazo hilo, kuna mtu nilikuja naye namfahamu na anaifahamu familia yangu, nikaongea naye, ni wazo la haraka lilinijia na bila kusubiria, nikalifanyia kazi..kwahiyo nikamelekeza huyo jamaa yangu , ni nini cha kufanya, tukifika hapo Dar, hakuwa na kipingamizi, akasema atafanya hivyo huyo jamaa yangu.

‘Kama nilivyohisi nilipofika tu, nikavamiwa uwanja wa ndege, walisubiria wakati nimeshaingia kwenye taksii, kumbe hata huyo mtu wa taksi, alikuwa mtu wao, wakasema mimi nipo chini ya ulinzi, nikawauliza kwa kosa gani, wakasema nitaambiwa nikifika kituo cha polis, nikawaomba vitambulisho, wakanionyesha, sikutia shaka

‘Walikuwa ni polisi kweli…?’ akulizwa

‘Mhh…vitambulisho vilikuwa vinaelezea hivyo, sikuwa na muda wa kuhakiki zaidi, na kiukweli sikuwa na muda sana wa kupoteza,…’akasema

‘Sasa wakati tupo njiani, nikasikia wakipigiana simu,, wakaulizwa kuwa mtoto ninaye, wakasema sina mtoto, wakaambiwa waniulize mimi nikawadanganya kuwa sijarudi na mtoto, nimemuacha huko nilipotoka, huyo aliyewapigia akawaambia mimi ni muongo, lakini baadae wakasema;

‘Mkuu kasema, atakuhitajia kuongea na wewe baadae sasa hivi uende nyumbani kwako,  na usiwe na wasiwasi, nia ni kukuonyesha kuwa ujio wako una manufaa makubwa, ila usipoleta ushirikiano, kusoma kwako ndio basi tena, hutasoma tena, na mtoto hutampata…’wakasema na hapo nikawa na mashaka, mtoto sitampata tena, ina maana labda walishamteka mtoto wangu..nikasubiria mpaka waliponiachia, ndio nikampigia simu jamaa yangu

‘Mtoto keshafika hapo kwako…?’ nikamuuliza

‘Ndio, mbona…?’ akataka kuniuliza maswali mengi, nikamkatiza kwa kusema

‘Usijali, gharama zote nitakutumia, hakikisha huyo mtoto anabakia hivyo hivyo, ukimaliza kumuogesha, unamvalisha hivyo hivyo…na usimtoe nje, kuna wabaya wanataka kumchukua mtoto wangu…’nikawaambia na kwa vile huyo ndugu yangu ni jamaa yangu anafahamu mambo  yangu  kidogo, akanielewa.

‘Kwahiyo hadi hapo nikafahamu kuwa mtoto wangu yupo salama, na maelezo mengine kama nilivyotoa kwa rafiki yangu, aliponiuliza kuhusu mtoto wangu, mengi yalikuwa ni namna tu ya kuhakikisha mtoto wangu yupo salama, na kipindi hicho sikuwa nafahamu ni nani wa kumuamini,…nilijitahidi hakuna anayefahamu wapi mtoto wangu yupo, hadi pale niliporudi chuoni…’akasema

‘Hata hivyo, wao hawakujali hilo la mimi kutokuwa na mtoto, hawakulijali sana, walifuatilia wakajua kuwa moto nilikuja naye, sasa kaenda wapi,  hapo hawakuweza kupata jibu, wakaona wasipoteze muda na hilo, walichotaka ni mimi kukubali huo mpango wao,

‘Kwanza alitumwa mtu, akiwa na hiyo mikataba nikatakiwa nisome na nielewe, baadae nikapigiwa simu isiyo na namba ya mpigaji, akaniulize kama nimesoma na kama nimesema nasemaje, nikawaambia, mimi siwezi kuongea mambo hayo kwenye simu, na ndio maana baadae nilikuja kuchukuliwa na hao watu hadi ofisi moja, huko uwanja wa ndege, kwa wakili  marehemu’akasema

‘Hapo ...nikaonyeshwa tena huo mkataba maalumu, nikaambiwa kuwa, kila kitu kipo kisheria, kilichobakia ni sahihi yangu tu, na nikikubaliana nao, basi nitapata mafanikio mengi, na haki za mtoto wangu, ila nikikataa, mtoto atachukuliwa na mimi nitakipata cha moto, kiukweli sikujali hayo, lakini mtu akinigusia mtoto wangu nahisi kuchanganyikiwa.

‘Hapo nikapima vipi nifanye hilo,  kwanza kwa ajili ya usalama wa mtoto wangu, nikaona bora nikubaliane nao tu, halafu mengine yatakuja kufauta baadae,..naona hayo na mengine yaliyofuata baadae nitayaelezea kwenye sehemu ya pili, maana ndani yake kuna mambo ya kisheria, na usalama , kama ni lazima itabidi nitete na mwenyekiti kwanza..’akasema na kutulia kidogo

‘Swali…’ilikuwa sauti ya wakili mtetezi, na hakusubiria kupewa kibali akauliza

‘Wewe umesema uliwahi kusikia mambo kuhusu mkataba wa familia kupitia kwa rafiki yako, na ina maana kuwa wewe ulikuwa unafahamu vipengele vyake, na ulifahamu kuwa ukifanya lolot baya, inakuwa ni tatizo kwa mume wa familia, huoni hapo unatudanganya,..kuwa wewe ulijua hatari yake na bado ukatumia mbinu ili umpate mume wa familia, ukijua masilahi yake…?’ akauliza wakili

‘Kwanza futa maneno yako,..vipengele vipi nilikuwa navifahamu, maana unavyouliza ni kama unafahamu ufahamu wangu wa vipengele ninavyovifahamu kwenye huo mkataba,…lakini pili futa kauli yako kuwa, mimi ndiye nilitumia mbinu kumpata mume wa familia, sio kweli, ngoja nije kuelezea ukweli hasa kwa jinsi gani ilitokea…..’akasema

‘Elezea sasa..mimi siwezi kufuta kauli yangu, wewe ndiye wa kuifuta hiyo kauli kama unaona sio sahihi,..kwa maelezo yako, yenye ushahidi sio unatutungia hadithi hapa…’akasema wakili kukawa na malumbano kidogo na mwenyekiti akaingilia kati na kusema

‘Endelea na maelezo yako, mzungumzaji…’akasema mwenyekiti

NB: Bado kuna muendelezo wa maelezo haya kabla ya sehemu hii ya kwanza, najaribu kupitia pitia, maelezo yake n marefu sana, huenda mengine ni kupoteza muda, kwahiyo ili siku isiende bure, tusome hayo maelezo ..ni muhimu sana, kwani ndio hitimisho ya mambo mengi yaliyotokea kwenye hiki kisa..

WAZO LA LEO: Tusiongee uwongo ili kuhalalisha ubaya wetu, tusisingizie uwongo ili tuonekana sisi ni wema, tusitafute kashfa mbaya kwa wengine ili sisi tuonekane wema, kwa ajili ya masilahi tu ya kidunia. Uwongo, kashfa na fitina kwa wengine kwa ajili ya masilahi kidogo ya hapa duniani, kama kupata cheo, mali, nk.., ni mzigo mkubwa wa madhambi tunayoyabeba mbele ya mola wetu.


Tukumbuke kuwa hayo yote tutakuja kuulizwa siku hiyo ya hukumu. Jiulize swali, je unataka kuyafanya hayo kwa manufaa  ya nani, na je una uhakika gani kuwa utapata muda wa kutubia hayo madhambi, na je huyo uliyemtendea kaumia kiasi gani, na je maumivu yake utaweza kuyafidia vipi kwa huyo uliyemtendea...

Ni mimi: emu-three

No comments :