Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, February 6, 2018

MKUKI KWA NGURUWE-75



 Baada ya mapumziko mwenyekiti alirudi, na kutuambia tuingie ndani, ili yuendelee na kikao chetu, na wakati huo mume wangu alikuwa keshaondoka na haijulikani kama atarudi tena,au ndio keshakimbia kikao, nikataka kwenda kutoa taarifa kwa mwenyekiti, lakini kabla sijainuka kwenye kiti , mara mume wangu akaingia akiongozana, na jamaa mmoja na moja kwa moja wote wawili wakaenda kuonana na mwenyekiti.

‘Mwenyekiti nimeona nimchukue wakili wangu, ili aweze kunijibia maswali, kwani naona nimelemewa, ...’akamwambia mwenyekiti.

‘Kwani tulikubaliana vipi, na kwanini umtafute wakili, kuna kosa gani kubwa umeliona ambalo linahitajia wakili?’ akamuuliza mwenyekiti.

‘Lakini nyie mna mawakili wenu, ..mbona mimi sijalalamika hilo..’akasema

‘Hawa wapo kwasababu ni watendaji wetu wa kila siku wakili wangu ni mtendaji wangu wa kila siku, huyo wakili wenu, ni mtendaji wenu, anahitajika kutoa ushahidi wa huo mkataba,..haya ni mambo yetu hayahitaji mtu mwingine ambaye sie mtendaji wetu wa kila siku, na kama umeamua kuleta wakili, basi tulipeke hilo swala mahakamani...’akasema mwenyekiti.

‘Hapana nia ya kumleta huyu wakili ni kunisaidia tu, kwa saabbu kuna mambo mengine yanahitajia sheria, na natambua kabisa tukimaliza hapa, watakuja maaskari, kama sio mimi ni kwa ajili ya mdogo wangu, ndio maana nimeamua kumleta huyu wakili...’akasema

‘Ili afanye nini....?’ akauliza mwenyekiti.

‘Ili aone kama kweli ninatendewa haki,..’akasema

************

 Ni katika kipindi kingine baada ya mapumziko, wajumbe wakaingia ukumbini, na mwenyekiti kama kawaida yake alishafika kwenye kiti chake, na walikuwa wakiteta,na mume wangu, baadae mwenyekiti akasema

 'Kuna mjumbe kaongezeka, ...na taarifa hii nimepewa hapa na mjumbe mwenzenu, mume wa mtayarishaji wa hiki kikao; 

'Huyo mnayemuona kakaa karibu na mawakili wengine ni wakili wa kujitegemea, yeye ni wakili anayemuwakilisha mume wa binti yangu...siwezi kulipinga hilo, maana huenda mwenzetu ana dhamira yake...' akasema mwenyekiti

'Lakini ndugu zanguni, je kulikuwa na haja gani ya kumleta wakili mwingine,...kulikuwa na haja gani ya kujihami kiasi hicho, sisi kama kikao, ..na ilivyo mujibu wa vikao kama hivi vya kifamilia, ni kutatua matatizo yale yaliyopo ndani ya kifamilia...'akasema mwenyekiti.

'Sasa ikizidi, au tatizo likivuka mpaka, ndio tunaweza kusema sasa tunakwenda mbele ya sheria, lakini kwa historia ya vikao vyetu haijawahi kutokea hivyo, labda hiki ndio kiwe cha kwanza..'akasema mwenyekiti.

'Karibu sana wakili, na huenda umeshaambiwa ni kitu gani kinachoendelea, sisi hatuna pingamizi, nia na lengo letu ni kuweka haya mambo sawa sawa...'akasema mwenyekiti na kunigeukia mimi

'Nikuulize wewe mume mtu, je upo hiari, na ujio wa wakili huyu , maana siwaelezi, kuwa na mawakili wakili, kila mtu na wake kwa jambo hilo hilo,...'akasema mwenyekiti akiniangalia mimi

‘Kama kaamua hivyo, ni vyema tu, ila nilitaka kumwambia huyo wakili atambue kuwepo kwa mkataba huo halali, na ule aliowahi kuonyeshwa awali autambue kuwa ni batili,..sasa kama yeye kaja na ajenda ya kuusimamia mkataba huo, wa awali ajue kuwa atahitajika kuwasiliana na mahakama au na watu wanaodhamini mikataba hiyo,..’nikasema

Wakili huo akanyosha mkono na mwenyekiti akageuka kutuangalia sisi wajumbe na kusema

'Hili jambo litatupotezea muda, lakini sawa, hebu tuambie muheshimiwa wakili,...'

‘Mimi nimeletwa hapa na huyu mteja wangu, alishanisimulai yote siku nyingi, na nilichukua nafasi ya marehemu, wakili wake wa awali,.., kwahiyo yote nayafahamu, sio mtu mgeni kwa hili linaloendelea hapa...’akasema.

‘Kwahiyo wewe unafahamu undani wa kila jambo la kifamilie, ikiwemo mikataba ya kifamilia, na kikazo..ya kuwa wawili hawa waliamua kutengeneza mkataba, ambao umekuwa ukiongoza familia na taratibu zao za kila siku ikiwemo makampuni yake?’ akaulizwa

‘Nafahamu,..’akajibu

‘Kuna uhakika kuwa mkataba huo wa awali uligushiwa, na mteja wako, akishirikiana na marehemu, kwa matilai  fulani, je unalifahamu hilo?’ akaulizwa

‘Hilo ndilo limanifanya nifike hapa, kwani mteja wangu anashukiwa kufanya jambo ambalo, halitambui,...'akasema

'Kwa vipi asilifahamu maana yeye ndiye muhusika wa kuandaa mikataba yote miwili, wa awali ambo ndio sahihi, na huo mwingine wa kugushiwa...?' akaulizwa

'Kwa maelezo ya mteja wangu, yeye alikuwa akimtegemea wakili wake, na alifanya hivyo ili kupunguza mambo mengi aliyokuwa nayo, kwahiyo akampa na jukumu hilo la mkataba, kwahiyo likitokea jambo la kisheria kuhusiana na mkataba, yeye alikuwa akimuhusisha wakili wake huyo...'akasema wakili

'Ok...endelea...'akasema mwenyekiti.

'Kwahiyo alipopatwa na ajali, mambo yote ya kisheria yalikuwa mkononi kwa wakili wake huyo,na bahati mabaya akafariki,ikabidi sasa achukue ule mkataba aliomkabidhi wakili wake wa zamani awe anausimamia yeye kwa muda, huku akitafuta wakili mwingine ambaye likuja kunipata mimi.

'Kifupi yeye, hadi leo, ambao mumekuja kugundua kuwa mkataba huo una matatizo, alijua kabisa kwua mkataba ni ule ule, na mkumbuke jamani, kuwa mteja wangu alipatwa na ajali na kipindi kingi alikuwa kwenye matibabu, na huo mkataba, kama ulibadilishwa basi ulibadilishwa kipindi hicho akiwa mgonjwa,...’akasema wakili.

‘Una uhakika na hilo muheshimiwa wakili?’ akauliza mwenyekiti

‘Kwa taaifa za kutoka kwa mteja, wangu ndio nina uhakika..muheshimiwa mwenyekiti.’akasema huyo wakili.

Mwenyekiti akachukua simu na kumpigia msajili wa mikataba,na akaweka sauti a kusikika watu wote, na kumuuliza msajili,  

'Samahani muheshimiwa kama nilivyokuomba awali, tutakwua tukikusumbua mara kwa mara, sasa kumetokea tatizo, kidogo, tulitaka kufahamu tu, ni lini tatizo la mapungufu ya kiofisi, lilitokea, nikiwa na maana ni lini iliogundulikana kuwa mkataba wa kifamilia wa hii familia ulibadilishwa

Huyo msajili akataja tarehe , na ikaonekana kuwa tarehe hiyo ni ya kipindi cha nyuma hata kabla mume wangu hajapata ajali,...

‘Umesikia tarehe iliyotajwa hapo, ilikuwa hata kabla mteja wako hajapatwa na hiyo ajali,  mkataba huo uligundulikana kuwa umebadilishwa,je unawezaje kusema hiyo michakato ilifanyika akiwa yeye hajui! Kiukweli yeye alikuwa na ufahamu wake, na alishiriki, na alifahamu ni nini kinechoendelea na ndio maana ugonjwa ukaendelezwa mbele au sio ...’akasema mwenyekiti.

‘Mkataba huo uligundulikana kuwa umebadilishwa, kipindi mteja wangu akiwa hajapata ajali, inawezekana ikawa hivyo, hatukatai, lakini yeye alikuwa hajui kuwa mabadiliko hayo yameshafanyika, hana ufahamu huo kabisa,,...'akasema. na kabla hajatulia akaongezea kusema;

'Na kama waligundua hivyo, hawakumfahamisha mteja wangu,   walimfahamisha wakili wake, ambaye na yeye kipindi hicho pengine, nasemea hivyo pengine, alitingwa na shughli nyingi, na alikuwa akisubiri muda muafaka wa kumfahamisha mteja wake,, na wakati anajiandaa kuja kuonana naye ndipo ikatokea hiyo ajali, ni ajali haina kinga, haina taarifa....’akasema wakili huyo

‘Uwongo una mwisho wake, sisi tunataka kuwaonyesha kuwa hayo yalifanyika kipindi ambacho mume wa familia hii akiwa mzima na fahamu zake na alipanga yeye na wezake hiyo katiba ibadilishwe, si ndio mnataka kila kitu kithibistishwe hii leo, hamtaki kusema ukweli, sasa mimi  namsimamisha wakili wa familia anayetambulikana kisheria,atuelezee ilivyokuwa;…

Wakili wetu wa familia akasimama na kuanza kuelezea mchakatao mzima wa katiba ulivyoanza, hadi kukamilika, na mangapi yemeshafanyika na kumalizwa kikatiba, na mafanikio yake, na alipofika kwenye changamoto zake, akasema,;

‘Pamoja na nia njema ya katiba hiyo, bado kulikuwa na changamoto zake, lakini zaidi ni hizo zilizofanywa kwa makusudi kwa nia ya kuharibu lile lengo jema la kuanzisha hiyo katiba.

‘Kiukweli katiba au makubaliano kama hayo yangelitumika kwenye ndoa zetu, nahisi ndoa nyingi zingaliimarika zaidi, na hakuna ambaye angelidiriki kuvunja ndoa yake kwa matendo yake. Lakini sasa…’hapo akatulia kidogo akifungua makabrasha yake..

'Ilikuwa tarehe mmh,....’akaangalia kwenye mkabrasha yake na kutaja tarehe,’

'Siku hiyo alinijia mume wa familia ofisini kwangu..’akasema

‘Ina maana huyo hapo au sio..?’ akauliza mwenyekiti

‘Ndio mwenyekiti, ndio huyo hapo, ..alinijia ofisini kwangu, akasema amekuja na ombo la kutaka huo mkataba ubadilishwe baadhi ya vipengele  nikamuuliza kwa vipi maana huo mkataba upo kisheria, na ukitaka kubadili chochote kwenye huo mkataba kuna taratibu zake,kwanza inabidi wakae yeye na mke wake wakubaliane, na baada ya hapo, inabidi tuandike barua yenye maelezo  ni kwanini tunataka kufanya hivyo.. ...?’nikamwambia hivyo.

'‘Mimi nafahamu jinsi ya kuubadili, hata bila kupitia hiyo milolongo yrnu isiyo na maana, kwani mkataba ni wa nani, ni wa kwangu mimi na mke wangu, kwanini niwahusishe tena watu wengine, kama nataka kubadili sihitaji kumuomba mtu, wewe sema kama hauwezi nimtafute mtu mwingine atakayefanya hiyo kazi...'’akaniambia hivyo mume wa familia..'

‘Sio swala la kuweza, ni swala la utaratibu, yoyote anayefahamu sheria, ni lazima azifuate taratibu hizo,mimi nakushauri kwanza nenda mkaongee wewe na mke wako, muone kama kuna sehemu za kubadili,mkubaliane,ili tukienda kuomba, tufanye kazi ya kujitosheleza, sio leo hiki kesho kile, hatutakubalika kisheria…’nikwambia hivyo

‘Kama huwezi sema..bwana…’akasema
‘Hapana sijasema siwezi..wewe nenda mkaongee na mke wako kwanza, na kama mtanihitajia mimi niwepo kwenye hicho kikao, mimi nitakuja, ili tufuate utaratibu..’'nikamwambia hivyo'

Yeye akasema hivi....

‘Sikiliza wewe nimeshakuona hutufai, nimeshatafuta wakili mwingine ambaye atashughulikia maswala hayo yote, kwani kama jambo dogo kama hili linakushinda huoni utatukwaza, kuna mambo mengi yanahitajika, na hili dogo ni mojawapo, wewe umeshindwa, mimi kuanzia leo nakufuta awakili wa familia, nimeshapata wakili mwingine....’akasema hivyo kuniambia mimi.

‘Mambo hayaendi hivyo bro, kuna taratibu zake bosi, hata kama mimi mnaona sifai, ujue tumeshaandikishana mkataba , na kama mnataka kuukatisha huo mkataba wangu na nyie pia kuna taratibu zake, huwezi kuamua mara moja kuwa wewe sio wakili tena,....ngoja mimi nitongea na mke wako tukutane, tuone jinsi gani ya kulifanya hili jambo kisheria,...’nikamwambia hivyo

Na yeye akasema hivi....

‘Nimekuambia mimi kama mume wa familia, sijakuambia umwambia mke wangu, mke wangu ana shughuli nyingi za kampuni, hili la uwakili kaniachia mimi, kwahiyo haina haja ya kuongea na mke wangu na hata ukiongea naye haitasaidia kitu,  maana nimeshapata wakili wetu mwingine..anayejua kazi...’akasema.

Mimi niliwasiliana na mke wa familia naye akaonekana kushangaa na taarifa hiyo, akasema nimpe muda kidogo yeye, ataongea na mume wake, na baada ya siku mbili, nikiwa ofisini kwangu nikafikiwa na ugeni..

'Mgeni huyo alikuwa ni marehemu Makabrasha...akiwa na ajenda ile ile kuwa amekuja kuchukua nafasi yangu, kwahiyo nimkabidhi shughuli zote, ...nikamwambia hilo halipo, na ili ahakikishe nikampigia simu mke wa familia, na mke wa familia akaniambia hakuna kitu kama hicho, na nisitoe chchote kwa huyu mtu, yaani Makabrasha...’

Makabrasha akaniambaia kuwa hilo lipo na litafanyika, kwani hayo ni mambo ya kifamilia, mume anaweza kuamau kubadili chochote kwenye mkataba, kama anaona kuna ulazima, kwa masilahi ya familia, ..akaongeza kusema kuwa mambo mengine yanaweza kusimamiwa na mume wa familia bila mkewe kufahamu,...

‘Na kwa jinsi ilivyo, kwa vile kuna mambo kama hayo ya mke kutingwa na kazi nyingi, na mume anatakiwa kuhakikisha kila jambo linatendeka vyema basi kuna haja, ya kurekebisha baadhi ya vipengele kwenye mkataba huo, umeona eeh, hilo halipo wazi kwenye huo mktaba, ndio maana nataka kufanyiwe marekebisho..’akasema.

'Sikiliza nikuambie jambo, ili wewe undelee kuwepo, fanya kama nitakavyo, ni kitu kidogo tu, hata ukirekebisha mke wangu hatafahamu, au sio…lakini kama hutaki sawa, kazi zote hizo itabidi nizifanye mimi, na wewe utakuwa na kazi,gani, eeh..hebu lifikirie hilo...'akaniamba hivyo.

Mimi nikamwambia;-

‘Wewe ni mwanasheria, unafahamu taratibu zilivyo... haiwezekani hayo mambo kufanyika kwa haraka hivyo, kwasabbu huo mkataba umeshasajiliwa, kuna michakato inatakiwa kupitiwa, kwahiyo ni bora hilo swala tukawauliza wahusika wenyewe kwanza na ni vyema tukalifanya wakiwemo wote wawili,  hata hivyo, mke wa familia anasema hakutambui wewe kama wakili wa familia...’nikamwambia.

‘Na mume wa familia hakutambui wewe,a kama wakili wa familia, umenielewa hapo, ni nani mwenye nguvu ya kifamilia, mke au mume....’akaniambia huyo makabrasha.

Sikutaka kubishana na yeye, niliwasiliana na mke wa familia, na mke wa familia akazidi kunisisitiza kuwa huyo mtu hamtambui na kama akizidi kunisumbua,a basi hatua za kisheria zifuatwe,.

Baada ya kikao hicho huyo mtu sikumuona tena kuja kwangu, ila siku moja nilikwenda kwa msajili kwa nia ya kufuatilia mambo aliyonituma mke wa familia, nikiwa pale, nikajiwa na wazo la kupitia mkataba wa familia, nikaenda kuonana na huyo anayesimamia hiyo mikataba,

‘Cha ajabu kabisa huyo jamaa wa masijala ya mikataba akaniambia kwasasa hanitambui mimi,...anamtambua wakili mwingine, aliyeletwa na wahusika, kwahiyo sistahili kuchukua chochote, ikabidi nimpigie simu mke wa familia, na mke wa familia, akaniambia nifuatilie kwa msajili mkuu, na nilipokwenda huko, wenyewe waliona ajabu, wakaniambia niwape muda watalifuatilia hilo swala..

Wakati wao wanalifuatilia huko, mimi nikaona kuwa hilo sasa ni tatizo, hata kama ni ajira,unatafuta kipato, lakini kama kuna sintofahamu ya namna hiyo ni bora uwaachie wenyewe, lakini kwanza nikaona, nionane na wahusika wote wawili. 

Nikaongea na mke wa familia dhumuni langu hilo, yeye alinikatali na kuniomba niachane nalo kwa hivi sasa, yeye ataona ni nini cha kufanya, hata hivyo mimi nikamshauri kuwa ni bora tukae kikao yeye na mume wake, na ikibidi tumkaribishe na huyo Makabrasha tuliongee kwa mapana, ili tupate muafaka, lakini mke wa familia alipinga kabisa kumkaribisha huyo Makabrasha akisema anamfahamu sana huyo mtu yeye hawezi kumruhusu mtu kama  huyo kuingiza kwenye shughuli zake.

‘Basi tukakubaliana kuwa tukae yeye na mume wake, akakubali  na tukakubaliana tufanye hicho kikao mwisho wa wiki hiyo, lakini kabla hicho kikao hakijafanyika ndio hiyo ajali ikatokea...’akasema huyo wakili.

Mwenyekiti akamuangalia wakili wa mume wangu na kumuuliza;

‘Je una swali lolote kwa wakili mwenzako, maana huo ndio ukweli wenyewe,sasa kama ulidanganywa, basi ujue umeingia choo cha kike...’akasema mwenyekiti na watu wakacheka.

‘Mimi hapo sioni tatizo, ..katiba sio msahafu, kuwa hauwezi kubadilishwa, wazo kama hilo la kufanya mrekebisho kumbe lilikuwepo, na alikuwa nalo mteja wangu, kipindi hicho hajapatwa na ajali, na alikuwa katika harakati za kulifuatilia hilo jambo kisheria kwa kupitia kwa huyo marehemu...hilo hatulipingi, ni jambo la kawaida...’akasema huyo wakili na akainama kunong’onezana na mteja wake, halafu akasema;

‘Ni kweli mteja wangu akiwa na nia hiyo alimtumia wakili Makabrasha, ambaye ndiye aliyeanza mchakato wa kufuatilia jinsi gani ya kufanya hayo marekebisho ya hiyo katiba, na wakati anaendelea na mchakato huo, bahati mbaya mteja wangu akapatwa na ajali, ya nyuma yakafutika kwenye ubongo wake, na alipopata nafuu, akaikumbuka katiba yake, na aliyoiona ndio hiyo aliyokuwa akiwaonyesha nyie, hakuwa na kumbkumbu zingine za nyuma, hata mkienda hospitali mtapata taarifa zake...kwahiyo michakato mingine ilifanyika yeye akiwa mgonjwa...’akasema wakili.

‘Nikuulize swali, hayo mabadiliko yaliyofanyika kwenye hiyo katiba mpya ndivyo alivyopendekeza mteja wako kabla hajapatwa na hiyo ajali au kuna mengine yaliongezwa yeye hakuwa hana ufaham nayo?’ akaulizwa

‘Hilo yeye hakumbuki, kwasababu hana kumbukumbu sana za nini kilitakiwa kibadilishwe, na mlipomshinikiza zaidi, ndio kumbukumbu ikaanza kumrejea kuwa hilo jambo lilikuewepo akilini mwake, kipindi cha nyuma, na bahati mbaya akapatwa na hiyo ajali, sasa huenda kweli hayo yaliyopo humo kwenye katiba ndiyo aliyokuwa amependekeza au kuna mengine yaliongezwa kwa ushauri wa wakili wake..yote yawezekana, tatizo lililopo hapa ni Makarasha hayupo, ndiye angeliweza kutupatia majibu ya hayo yote, na mbaya zaidi kazi zake zilikuja kuibiwa zote na watu, sasa sikuweza kujua wapi aliishia...’akasema huyo wakili.

‘Naona tusipoteze muda kwa hio, hapa tumeshaona kuwa kweli, kulikuwa na mbinu za kuibadili hiyo katiba bila ya mke wa familia kuhusishwa, lakini hazikufanikiwa,..vyovyote tutakavyoliweka, litasomeka kuwa kulikuwa na hujuma za hadaa, baada ya kukataliwa na mke wa familia, na wakati mke wa familia anajitahidi waliongee  yeye na mume wake, akitafuta ni kwanini mwenzake anataka kuwe na mabadiliko katika hiyo katiba, mwenzake akawa anajaribu kupoteza muda ili wafanikiwe katika mbinu yao hiyo, na kwa haraka wakakimbilia kufanya hicho walichokifanya...’akasema mwenyekiti.

‘Kwahiyo basi katiba hiyo aliyokuwa nayo mteja wako ni batili, haipo, na haitambulikani kisheria, sisi  tunaendelea kutumia katiba halali, na hiyo ndiyo tunayotaka ifanye kazi yake hii leo,...sawa muheshimiwa wakili?’ akaulizwa, na kabla huyo muheshimiwa wakili hajajibu, mume wangu akamnong’oneza kitu wakili wake, na wakili wake akawa kama anasita kuongea, na kukawa na kama ubishi , na wakili wake, akasikika akisema;

‘Hayo ni mambo ya kisheria huwezi kuyakwepa, acha iwe kama ilivyo, nitajua jinsi gani ya kupambana nao hawaniwezi hawa...’akasema na mume wangu akaonekana kutokurizika na maamuzi ya huyo wakili, na baadaye kidogo baada ya wao kuongea kidogo huyo wakili akamgeukia mwenyekiti na kusema;

‘Samahani kwa kuwapotezea muda, unafahamu mteja wangu anakuwa na wakati mgumu, kwani hiyo katiba inayotambulikana kisheria, yeye, haikumbuki sana, ...sasa inamuwia vigumu kwake kukubali moja kwa moja...naomba hilo mliweke akilini, ila anahisi hadi kufikia hatua ya yeye kuomba kuwe na mabadiliko, marekebisho, anahisi kulikuwa na vipengele vilivokuwa vikimkandamiza na kutokumpa nafasi ya kutumiza wajibu wake kama mume wa familia...’akasema huyo wakili.

‘Kwahiyo..?’ akawa kama anauliza mwenyekiti.

‘Kwahiyo mteja wangu anasema, tukiendelea kuitumia katiba hiyo ya zamani, yeye anaweza akadhulumia na kutendewa isivyo haki, na ndio maana aliamua hiyo katiba ifanyiwe ukarabati,..anaomba itumike katiba hiyo mpya kwa masilahi ya familia, kwani yeye ameipitia na kuiona ina faa sana kwenye familia yake..’akasema wakili.

‘Wewe kama wakili unaifahamu vyema sheria, hilo kweli ni sahihi, maana ukumbuke huo mkataba, ilishatumika huko nyuma, na hakukuwa na matatizo, matatizo yamejitokeza baada ya mteja wako kufanya mambo kinyume na makubaliano,....’akasema mwenyekiti, na kabla wakili hajasema neno mwenyekiti akaendelea kusema;

‘Hoja kama hiyo alitakiwa mteja wako aisema kabla,hajafanya hayo aliyoyafanya, kama tutakuwa tunabadili mkataba kila tukifanya makosa, au tukitaka kukidhia haja zetu, unafikiri huo mkataba utakuwa na maana kweli, je ni mkataba wa masilah binafsi au ni mkataba wa kukidhi haja za wote, na kwanini alipoona hivyo, hakuongea na mke wake kwanza, ..hizo ni njama za makusudi, hayo yanajulikana , hoja yake kwa sasa haina mshiko, hata wewe wakili unaliona hilo, kama unafahamu vyema kazi yako..mimi ninaona tusipoteze muda tuendelee na kikao chetu au sio muheshimiwa wakili,...?’ akauliza mwenyekiti.

'Mwenyekiti akanigeukia mimi, na kuniuliza 

'Au wewe mke wa familia, unasemaje kwa hilo...maana wewe umekuwa mstari wa mbele kumtetea mume wako...haya tukusikilize na wewe...'akasema mwenyekiti.

‘Ndugu mwenyekiti, mimi naomba tuendelee na ajenda nyingine,...katiba yetu ni hiyo hiyo, tumashaona kuwa kulikuwa na njama za kuibadili, kwa vile mume wangu alishaona kuwa kafanya madhambi, tena madhambi makubwa, na akafahamu kuwa kutokana na hiyo katiba, ataingia matatani, akaamua kumshiriksiha makabrasha ,akimfahamu fika kuwa ni mtaalamu wa hadaa, wa kucheza an sheria kibatili, ....’nikasema.

‘Madhambi gani niliyafanya wewe mke, usitie mafuta kwenye moto, ..sisi tunataka kulimaliza hili kwa masilahi a familia, wewe unaleta mambo mengine,mimi ninaangalia mbali kwa ajili ya vizazi vyetu, na sio kwa ajili ya kuwafurahisha watu wengine, wewe hujui kuwa wenzako hapa, nikiwa na maana watu wasioitakia mema ndoa yetu iwepo, wana malengo mengine kabisa, kiuvunja ndoa yetu halali,….akasema mume wangu kwa hasira.

‘Kulimaliza hili kwa vipi ukumbuke hizo ajenda nyingine zinahusiana na huo mkataba, na tumeshindwa kuingia kwenye ajenda hizo kwasababu ya huo mkataba wenu wa bandia..., ‘nikasema na mume wangu akataka kusema kitu na mimi sikumpa nafasi.

‘Ujue fika, …ajenda nyingine, nikuhusu madhambi yako, yale uliyoyafanya ambayo ni kinyume cha katiba hiyo. Tumepoteza muda mwingi kwasababu ya uwongo wako, na sasa uwongo wako umebainika, na madhambi mwenyewe yatakuja kukusuta…’nikasema

‘Madhambi gani wewe…’akasema kwa karaha

‘Ina maana wewe hujafanya madambi, huna makosa…?’ nikauliza

‘Sema ukweli ..kama kwel huna madhambi,...mbona unaogop ahapo kutoa kauli…’nikasema na mume wangu akabakia kimia.

‘Tuendelee na kikao ndugu mwenyekiti…’nikasema, na kabla mwenyekiti hajaanza kuongea mume wangu mara akaanza kuongea kwa kusema;.

‘Sijafanya madhambi yoyote mimi, na wala siogopi, ninachotaka ni kuitetea ndoa yangu ambayo naona wenzako wanataka kuivunja kwa nguvu, kwa kigezo hiki cha kutumia huo mkataba, mkataba ambao uliipendekeza wewe, ukiwa umeshaongea na wazazi wako, mimi hilo nilishalifahamu, lakini kwa muda ule sikuwa na la kufanya...’akasema mume wangu, na mwenyekiti hapo akaingilia kati na kusema;

'Kwahiyo hilo unalikumbuka, kuwa mkataba huo ulipendekezwa na mke wako, wewe hukuhusika, au ...?' akaulizwa

'Sio swala la kukumbuka , ndivyo ilivyo,kila kitu hapa kinajionyesha, mnataka mimi niseme nini zaidi ...'akasema

*************

‘Kwa vile tumeshaona kuwa katiba ya kugushi haina mamlaka tena hapa, sasa tunaingia kwenye sehemu ya nyingine ya ajenda zetu, na ajenda hii, ni kumuacha mke wa familia, aongee ni nini kusudio lake la kuitisha hiki kikao, ...’akasema mwenyekiti. Na pale nikaona mume wangu akiandika kitu kwenye karatasi na kuisogeza hadi kwa wakili …wakili huyo hakuwa amekaa mbali na alipokuwa mume wangu.

Mara wakili wa mume wangu akaonyesha mkono na kusema;

'Mteja wangu anasema hataweza kuingia kwenye ajenda nyingine mpaka swala hili la katiba ya kifamilia litatuliwe, kwani mkataba wao ndio msingi wa mambo mengine yote...'akasema wakili huyo

‘Hatuwezi kupoteza muda zaidi,..tafadhali mkumbuke hapa kuna watu wanataka kusafiri, kuna watu wameacha shughuli zao, kama docta pale, kwa ajili ya hili jambo, kiukweli tutakuwa hatuwatendei haki…’akasema mwenyekiti, na mimi nikaongea hata bila ya kibali.

‘Ndugu muheshimiwa wakili, mteja wako anafahamu fika kuwa kafanya madhambi mengi tu, na aliyafanya hayo akiwa na akili zake timamu, makosa ambayo kikatiba yetu ya kifamilia, ..nikiwa na maana mkataba…madhambi hayo yanatambulikana kama makosa makubwa, ambayo ukiyafanya, kama mkataba unavyojieleza, adhabu yake ni kubwa sana, na haina msamaha..kipengele hicho kwenye katiba ya kugushi kimeondolewa kinamna, ...'nikasema.

'Lakini huwezi kuyaita makosa makubwa , mpaka ibainike wazi kuwa ni makosa au sio na ikiwa na maana ni lazima kuwe  na ushahid wenye mshiko, uliothabiti,  au sio...'akasema wakili

'Na ndio maana tunahitajia tuendelee na ajenda nyingine ili kuyabainisha hayo makosa,...'nikasema

'Lakini mteja wangu hajakubaliana na hiyo katiba iliyojitokeza kwasasa, huwezi kumshikinikiza kwa kitu ambacho hakitambui unielewe hapo maana baada ya kutaja hayo madhambi ni nini kitafuta, si adhabu au, na je adhabu hizi zitatumia kigezo gani...'akasema wakili

'Ndugu muheshimiwa wakili, ukumbuke hii katiba tumeshaitumia zaidi ya miaka tisa, na haikuwahi kuwa a utata, kwahiyo tuna udhoefu nayo, tatizo ni hivi sasa, utajiuliza ni kwanini, ..jibu ni rahisi hapo,ni kwa vile kumetokea matatizo makubwa, matatizo ambayo mteja wako anafahamu fika kuwa ni madhambi makubwa, na hajataka kuyakiri hayo makosa,anajua ni kwanini...'nikasema.

'Sawa,...tumesikia hayo,  lakini huwezi kuyaita madhambi makubwa, kwa mteja wangu, mpaka yathibitishwe, kuwa ni madhambi makubwa, na kwa ushahidi,  ..na ushahidi bayana uwepo, hiyo ushahidi bayana ina maana kubwa sana hapo..’akasema wakili

‘Tutaonyesha hilo, halina shaka…’nikasema

‘Hata hivyo, hatuwezi kukimbilia kuhukumu kwenye katiba ambayo imeshatiliwa mashaka, na pande zote mbili, kwanza haikuwepo, imekuja baada ya hiki kikao, pili mteja wangu haiamini, ndio maana mteja wangu anaona kuwa kuna umuhimu kwanza wa kuhakikisha tatizo la mkataba limekwisha, na kila mmoja akawa karizika,…kwanini tukimbilie kwenye makosa kwanza....''akasema wakili.

‘Nimeshakuelezea hilo, kuwa mkataba huu, na matuzimizi yake haukuanza jana au leo, una miaka mingi, kwanini anaogopa hivi sasa, ni kwa vile kafanya madhambi, ndio maana anajihami…’nikasema

‘Mdhambi gani hayo, na kwenye mkataba yana msimamo gani..?’ akauliza wakili na hapo mume wangu akamuangalia wakili huyo kwa hasira, kama kumuonyesha hapo kuwa katoa swali sio mahali pake. Na mimi kwa haraka nikaamua kuitumia nafsi hiyo kuelezea …

‘Kwenye katiba yetu kuna makosa tuliyaanisha kama makosa makubwa, kama zinaa, uzinzi, kuua, kuiba, ushirikina ....hayo ni baadhi ya makosa makubwa, na humu kwenye katiba tulianisha kuwa, mke au mume akigundulikana kutenda hayo makosa,...hukumu yake..’nikatulia nikijaribu kufungua ule mkataba..

‘Haina haja ya kusoma, ile inasema makosa kama hayo, yanaruhusu talaka moja kwa moja, na mwenye makosa, hatapata haki yoyote, tunatambua kuwa mtoaji talaka ni mume, lakini hata mke anaweza kuiomba hiyo talaka, na hilo limebainishwa hapo, kuwa kama ni mume kafanya hivyo, talaka ipo wazi, sio swala kuomba tena, na mume hana haki y akudai chochote….’nikasema

‘Na maelezo hayo hayakubakia kwa mke au mume peke yake, kila mmoja limagusa,..na hata nini haki mtu anazikosa, zote zimeelezewa kwenye kipengele kinachofuata,..sasa ni kwanini kwa hivi sasa aogope mkataba usifanye kazi yake, ...yeye si anadai hana makosa, ..basi tuache ukweli useme...'nikasema na hapo mwenyekiti akaingilia kati, na kusema

‘Mimi sitaki kuingia undani wa huo mkataba kwani wakili wao yupo hapa, yeye ndiye mtaalamu wa huo mkataba ambo kwao waliuita katiba ya familia, kwani yeye ndiye aliyeikamilisha hiyo kazi kisheria, kama ni muhimu  atasimama na kubainisha au kufafanua kila kipengele, lakini kwa sasa tunataka kuyafahamu hayo madhambi makubwa aliyoyafanya mume wa familia...au sio wakili..?’ akauliza mwenyekiti

‘Sawa ni vyema tukayaona hayo makosa, ili yabainishwe kama kweli mteja wangu kayafanya,…vinginevyo hatuwezi kuyatambua kama makosa..kwa kipengele gani….na...’akasema wakili na kabla hajamaliza, mume wangu akasema.

‘Hilo haliwezekani, huo ni mtego wakili, nimekuambia kuwa, uhakikishe swala la mkataba linamalizika kwanza, mimi siukubali huo mkataba, kwanini unataka uanze kufanye kazi,…wakili fanya kazi yako,…’akasema mume wangu

‘Ndio naifanya hivyo, usiwe na wasiwasi..bosi…’akasema wakili

‘Lazima niwe na wasiwasi, wewe huwajui hao watu, ni wanjana ndio maana nikakuita upambane nao kisheria,, sio ukubaliane na huo utumbo wao na mbinu zao za ujanja ujanja za kunitega, lengo lao ni ili kunichimbia kaburi, kama huwezi kazi sema, nikatafute mtu mwingine....’akasema mume wangu kwa hasira.

‘Ina maana huu tunaoongea hivi sasa hapa ni utumbo, wakili mwambie mteja wako achunge kauli zake…hiyo sio kauli ya mtu muungwana, au sio?’ akauliza mwenyekiti aliposikia mume wa familia akilalamika.

‘Samahani ndugu mwenyekiti, hayo yamemtoka mteja wangu, akionyesha wasiwasi tu, ninamuhakikishia mteja wangu kuwa  hilo la hiyo katiba lisimtie shaka, cha muhimu ni kuangalia hayo madhambi yanatotajwa, ni madhambi gani,  kwani kama yalivyoanza kuelezewa, hayajafafanuliwa na ushahidi ulio dhahiri , kwahiyo hayana msingi, mimi kama wakili nitakutetea kisheria, na haki yako italindwa, una wasiwasi gani, usijali...’akasema huyo wakili kwa kujiamini.

‘Wewe umeharibu kila kitu… huo mkataba ndio msingi wa kila kitu hapa,…haukubaliki, unasikia, haukubaliki…’akasema mume wangu akimtolea macho wakili wake na mwenyekiti akaona asipoteze muda, akaendelea na kikao akisema;

‘Kwanza kabisa kama kawaida ya mambo ya kifamilia huwa tunampa nafasi mtetezi, atoe kauli ya kukiri kosa, kwani jambo hili ni la kifamilia, mtetezi, anaweza akakiri kosa na kuelezea udhaifu wake, na makosa yake, kwanini alifanya hivyo, kwa kupitiwa, au kwa makusudi, na sisi kama familia tutamsikiliza,...mnaonaje jamani tukampa huyu mtu nafasi ya mwisho…'akasema mwenyekiti

'Ujanja huo…swala hapa ni huo mkataba, mimi sina imani nao…'akasema mume wa familia

'Cha muhimu ni  kwako ndugu, mtetezi, ni wewe kuongea ukweli, ukweli ni silaha kubwa kwa mtu yoyote, ukikiri kosa ukatubu, watu wanakusikiliza, kwasababu kila mtu ni mkosaji, sasa tunakupa nafasi hiyo mume wa familia, hapo hatuhitaji wakili wako, tunahitaji kauli yako wewe, kauli yako kwetu ni muhimu sana, ....’akasema mwenyekiti.

‘Mimi sijafanya hayo madhambi makubwa mnayonisingizia, yote ni uwongo na ni mbinu za kuniharibia ndoa yangu...’akasema mume wangu kabla hajaruhusiwa.

‘Je uliposema madhambi makubwa, ina maana unayafahamu hayo madhambi makubwa ni yapi, kikatiba?’ akaulizwa na akakaa kimiya na wakili wake akasema;

‘Mteja wangu anasema kuwa hayo madhambi mnayomshutumu nayo hajawahi kuyafanya, kibinadamu kuna kuteleza, yeye kama aliteleza hakupewa muda wa kujitetea, kama kuna jambo lilitokea akalifanya ni yale ya kibinadamu tu, yoyote anaweza kupitiwa, ndio maana alitaka katiba hiyo ifanyiwe marekebisho, maana inahukumu moja kwa moja bila kujali ubinadamu, bila ya kumpa nafasi mkosaji,...’akasema wakili.

‘Sisi tutatoa ushahidi kuwa hayo aliyoyafanya sio kwa bahati mbaya, kama ni kwa bahati mbaya mbona hataki kuyakiri hayo makosa, kukataa kwake, kuwa hajafanya kunaonyesha usugu, na uthubutu wa mteja wako, na tusipoteze muda, .kama hataki kukiri makosa basi sisi kama wanafamilia tunataka kuyaweka makosa yake hadharani, na wanafamilia watayaangalia, kwa mizania, je alifanya hayo madhambi kwa bahati mbaya au alikusudia,...’akasema mwenyekiti.

‘Kwanini anaogoa kama kweli hajayatenda,hajiamini!  …muulize mteja wako,kwanini anaogopa hata kuyataja hayo madhambi…’nikasema na hapo mume wangu akaniangali na kusema kwa hasira

‘Ni nani anaogopa…siogopi kabisa, ila nawafahamu nyie, mambo yenu mnayapeleka kimtego, mtego…sasa mimi nawaambia hivi,  mimi nitapigania haki yangu mpaka mwisho..ndoa haivunjiki kirahisi hivyo, nimeshalisema hilo, na ndio kauli yangu mpaka mwisho...’akasema na wakili wake, akamwendea na kumnong’oneza jambo, na mume wangu akasema;

‘Sawa fanya unavyoweza wewe, lakini…huo ni mtego, ..kwa hali kama hii, mimi..aah, umeshanikatisha tamaa,...haya endelea, uonavyo wewe...’akasema kwa hasira

Mwenyekiti hakuwasubiria akasema;

‘Mke wa familia uwanja ni wako…na tunataka usiongee maneno mengi, lenga moja kwa moja kwenye makosa, kama ni makosa, na mkataba wenu ndio utakaofanya kazi, kwani tokea mwanzo,mume wako ndiye alisema mkataba wenu ndio kila kitu, basi, sisi hatuna kazi tena, kazi yetu ni kupima uzito wa hayo makosa, kama yapo,..’akasema mwenyekiti, na mimi sasa nikaamua kusimama kabisa, na safari hii, nikiwa sitaki kabisa kumwangalia mume wangu, nikasema;

‘Mume wangu ana makosa makubwa, nikisema makosa makubwa itaeleweka, na hata kwenye mkataba wetu, hayo makosa makubwa yana nafasi yake, na ni mhimu kama tutakubaliana, niweze kuyataja hayo makosa yake kwa kifupi tu, na nitakuja kuyafafanua, au mkataba wenyewe utafafanua…’nikasema

‘Mume wangu kafanya makosa  ya uzinzi, na  zaidu ya hayo yeye ni mnafiki....’nikasema na mume wangu akasimama na kuniangalia kwa hasira

‘Unaleta matusi hapa..mimi ni mzinzi, una ushahid na hilo…’akasema mume wangu kwa hasira na wakili wake akamkalisha chini na kumnong’oneza kitu, na mimi sikumjali nikaendelea na maelezo yangu.

‘Kwanini nasema kuwa mume wangu ni mzinzi na mnafiki, angalia katika katiba yetu, kosa linalotambulikana kama huyo mtu ni mzinzi na au huyo mtu ni mnafiki..'nikasema

'Maneno haya ni kauli yake yeye mwenyewe siku ya kutunga huo mkataba alitaka hayo maneno yawekwe kama yalivyo, kuonyesha madhambi hayo makubwa,  na akataka yawekwe hivyo kama yalivyo,kwahiyo mimi, sijakutukana kama unavyodai wewe, ila umejitukana wewe mwenyewe kwa matendo yako, kauli yangu inashuhudia tu hayo…ila wewwe ulikwisha kuyafanya hayo kwa vitendo vyako mwenyewe, ashakumsi matusi, kuwa wewe ni mzinzi kwa jina jingine wewe ni muhuni na sitasita kukuita malaya....’nikasema na watu wakaniangalia kwa mshangao.

‘Mumesikia wenyewe jamani…’akasema mume wangu akilalamika, lakini wakili wake alikaa kimia.

‘Sitamki haya meneno kwa nia mbaya, hapa wapo wazazi wangu nawaheshimu sana, naomba wakili wetu atusomee kwenye katiba yetu; mzinzi ni mtu gani, au Malaya ni mtu gani:..nikasema na mwenyekiti akatabasamu huku akitikisa kichwa kama kunikubali, na mwenyekiti akanyosha mkono kumruhusu wakili asome maana ya maneno hayo, wakili akasema;

‘Mzinzi ni tabia ya mwandoaa u mtu yoyote ambaye katenda tendo la ndoa kwa asiyekuwa mke wake au mume wake au yoyote akifanya bila kuingia kwenye ndoa..’akasema wakili.

`Na mnafiki ni yule asiyetunza ahadi, mwongo mdanganyifu, mzandiki, aliyeahidi akashindwa kutimiza ahadi yake, aliyeongea uwongo huku akijua anaongea uwongo, aliyeaminiwa akashindwa kutimiza imani yake kwa watu...na ...’akasema wakili. na mwenyekiti akakatisha na kusema

'Endelea na maana ya hilo neno jingine, tusipoteze muda, mtu akitaka kusoma ufafanuzi zaidi mkataba huo sasa upo huru...'akasema mwenyekiti

‘Na Malaya...hebu kidogo hapo..’ akasema mwenyekiti

‘Mwenyekiti mimi naona inatosha....’ nilitaka watu wasikie maana ya hayo maneno mawili ya awali kwanza…’nikasema 

‘Mume wangu nimegundua kuwa wewe ni mzinzi, na tabia hiyo ipo kwenye damu,...na wewe ni mnafiki wa hali ya juu, kwa vile umehini ndoa yetu, umezini na wanawake zaidi ya mmoja, ukijua kabisa kuwa hilo ni kosa, na mungu akatoa ushahidi usiokwepeka, ...’nikasema na yeye akajifanya kutabasamu kwa dharau

‘Mume wangu wewe ni mnafiki, kwa vile umeyakana makubaliano yetu, ukadanganya, ukashindwa kutimiza yale uliyoyaahidi, na ukatafuta njia ya kuhadaa, tena kwa kuwaribuni watu waliopewa dhamana hiyo kwa kuwaonga, hilo ni kosa jingine  kubwa...’nikasema kwa huzuni.

‘Hayo yote ni makosa makubwa, sio kwa mkataba wetu , lakini kifamilia, umejiabisha,… na uliyafanya hayo ukiwa na akili zako timamu na sio mara moja, ingelikuwa mara moja tungelisema,..ooh, ni bahati mbaya, uliteleza, lakini imekuwa ni tabia yako, hadi ukaumbuliwa ....na mungu hakukufichia madhambi yako, ....’mara mume wangu akasimama na kusema;

‘Sio kweli, wewe umeamua kunitukana tu na kunizalilisha tu, hayo unayoyasema yote ni uwongo, wewe nakuona sasa umeungana na wazazi wako, ili mnisaliti, hayo uliyosema nimeyafanya wapi, ni nani shahidi yako, ..nimeshutikia,lengo lenu, nia yenu ni kunizalilisha tu, wakili wangu yanukuu hayo matusi, kwasababu ninaweza kumchukula hatua huyu mwanamke, hanijui tu mimi..’akasema mume wangu.

‘Hujatukanwa, Katiba yenu inaelezea hivyo, ila wewe ulitakiwa umwambia mke wako athibitishe kauli yake, kama ni ya uwngo basi tutayachukulia kama ni matusi na wewe una hiari ya kumuadhibu mkeo, na hata kumshitaki kikatiba,lakini kama ni kweli, wewe una tabia hiyo, basi usikasirike kuitwa kwa sifa hizo..’akasema mwenyekiti.

‘Sio kweli , mimi sina hiyo tabia, yeye ni mtaalamu wa kuongea tu, anaona sifa sana kumharibia mume wake heshima yake, na hajui hilo kindoa ni makosa, unatakiwa ufiche siri za mwanandoa mwenzako, wewe unazianika hadharani, hiyo ni tabia gani, na wazazi wako wanakuunga mkono, siwaelewi kabisa mimi...’akasema mume wangu kwa hasira.

‘Ndugu mwenyekiti, sio kwamba napenda kutaja siri za mume wangu hadharani, lakini kwa hali kama hii alitegemea mimi nifanye nini, inabidi tufanye hivyo, kwasababu hukutaka kukiri makosa yake, na nilimuomba afanye hivyo, tukiwa sisi wawili, hukutaka kusema ukweli,,ni kweli si kweli...?' nikamuuliza mume wangu akasema

'Si kweli...'akasema kwa sauti kama ya kunishushua..na mimi sikujali, niksema;

'Wewe, uliendelea kufanya jinsi ulivyotaka wewe mwenyewe kwa masilahi yako binafsi, na hawo waliokudanganya, hata kwa kile cha makubaliano ya watu wawili...na mbele ya hiki kikao hukutaka kukiri ukweli, japokuwa kusema tu, kweli nilifanya nisameheni, hutukutaka ataje kila kitu, ...kukiri kosa kashindwa, je mtu kama huyu alitaka mimi nifanye nini, mimi nikae tu kimiya huku ukiendelea kuvunja amri za ndoa, hapana, hilo halipo...’nikasema na kutulia

‘Unanisingizia tu, hayo yote ni uzushi, na wewe nashangaa siku hizi unaukubal uzushi, sijui una malengo gani na mimi, lakini kumbuka mimi ni baba wa watoto, watoto wanajua jinsi gani ninavyowajali…’akasema

‘Mimi hayo yote ninayoyasema hapa sijakusingizia,kama  itaonekana ni uwongo, mimi nipo tayari kuwajibika, na kwahiyo, ni bora ukakiri makosa, ili tusipoteze muda hapa,..ongea ukweli,  tuone kikao kitasemaje, je upo tayari kukiri kosa,?’ nikamuuliza na yeye akatikisa kichwa kukataa, na baadae akasema.

‘Usinifanye mimi mjinga, nafahamu malengo yenu ni kunitega, nikiri kosa, ili muanze kuhukumu kwa ….mkataba huo…sasa mimi nasema hivi, wewe si unajifanya unayafahamu makosa yangu na una ushidi,  utoe huo ushahii, na nasema hivi kama huna ushahidi na lengo lako ni kuniharibia, kibao kitakugeukia wewe, ...nitahakikisha naitumia hiyo hiyo katiba kukufunza adabu...’akasema kwa hasira.

'Subirini kwanza, naona mumekwenda haraka kidogo...'akasema mwenyekiti, huku akimgeukia mume wangu, akamtizama kwa makini halafu akageuka kumtizama wakili wake.

'Ndugu muheshimiwa wakili, mtu unayetaka kubeba dhamana yake ndivyo huyo na ndivyo hivyo alivyo,..pamoja na yote, pamoja na kupewa nafasi ya kukiri kosa, bado kabakia na msimamo wake, je ni wewe ulimshauri hivyo...?' akauliza mwenyekiti

'Mwenyekiti..mimi kama wakili wake, kwanza nilipenda kuyasikia hayo makosa, ili niweze kumtetea mteja wangu, je ndio imanipatia hiyo nafasi, ...?' akauliza wakili huyo.

'Hapana nafasi hiyo utaipata tu,..ila kwa vile uwanja ni wa mwenyeji wa kikao hiki nataka yeye mwenyewe ayathibitishe hayo madai yake, maana kama ni uwongo, basi hata mimi nitachukua jukumu hilo la kumuadhibu, maana hayo ni makosa makubwa, ...je msemaji una ushahid gani wa hayo makosa...?' akauliza mwenyekiti.

‘Ushahidi upo mwingi tu…’nikasema

************

‘Nimeongea kwa kifupi ili kutokupoteza muda, na sasa namuomba shahidi wangu wa kwanza kuthibitisha kauli hizo nilizozitoa, sio matusi, bali ndio ukweli halisi. Wapo wengi wakuthibitisha maneno yangu, ila kwa sasa namuomba....’nikageuka kuwaangalia washiriki,nikamwangalia rafiki yake docta…
Docta akainamisha kichwa, nikajua ni kwanini,  nikamwangalia mke wake, mke wake alikuwa kama hayupo, alionekana ana mawazo mengi, na kabla sijatamka neno ...’ mama ambaye muda mwingi alikuwa kimiya akasema;

‘Mimi naomba aje Binti yangu wa kufikia, ..aje yeye kwanza maana anahitajika kwenda kujiandaa kesho anasafiri....’akasema mama na mwenyekiti akauliza

‘Unajuaje kuwa huyo ni shahidi wake, usiharibu utaratibu, au..’akasema mwenyekiti

‘Sawa ila…’nikasema nikiwa sijui lolote kuhusu huyo bint

‘Mimi nina uhakika ni shahidi wake..’akasema mama.

‘Haya, kama muhusika umemkubali kuwa ni mmoja wa shahidi zako, aitwe, au unasemaje mwenyeji wa kikao..?’ mwenyekiti akauliza na mume wangu akawa kabakia kimia, akiwa kashika kichwa.

'Sawa maana shida hapa ni kuthibitisha kauli zangu ambazo mume wangu kasema namkashfu, nimemtukana na sio kweli kuwa ana watoto nje ya ndoa,  ...sasa huyo shahidi atathibitisha hayo niliyoyaongea, ili tusipoteze muda..'nikasema.

‘Hahaha…’akacheka mume wangu akionyesha dharau, kuwa labda nahangaika bure

'Na sio huyo tu, hapa ninao, na wengine hawajafika, ...sio kusudio langu kuyaweka haya hadharani, lakini nitafanya nini,..eeh,..basi aitwe huyo binti, akimaliza nitamsimamisha shahidi wangu mwingine,...'nikasema.

‘Sawa…’akasema hivyo mume wangu, lakini sasa akionyesha wasiwasi kidogo.

'Kama nilivyosema awali kikao hiki nimekirejesha kwa mwenyeji wetu, sitapenda mimi kuingilia, haya sasa akaitwe huyo binti,...'akasema mwenyekiti

Na aliposema hivyo, watu wote wakawa na hamu ya kumfahamu huyo binti ni nani,  ambaye ataweza kutoa huo ushahidi  wa jambo nzito kama hilo, nilimuona hata mume wangu akiwa na hamu ya kumuona huyo binti, hamjui ni bint gani huyo...

Watu wote mle ndani wakakageuza kichwa kuangalia mlangoni, waliposikia mlango ukigongwa, na mara ukafunguliwa, na mwenyekiti akasema;

‘Ingia na njoo huku mbele,...utoe ushahidi wako, tuambie ilikuwaje, na ni nani alikupachika mimba, usiogope, sema kila kitu….’

NB, Ni binti wa kufikia huyo anakuja kutoa ushahidi , je atasema nini



WAZO LA LEO:Kukosa ni kawaida ya binadamu, hakuna anayeweza kujithibitishia kuwa hatendi kosa, yapo ya bahati mbaya na yapo makosa ya kudhamiria, vyovyote iwavyo, unapokosea unastahiki kukiri na kutubu kosa lako, na kumuomba msamaha yule uliyemkosea, unapokosa ukabainika, au hata kama hujabainika, wewe ukalikana lile kosa, unakuwa umetenda kosa jingine. Tujifunze kuwa wa kweli, na tukikosea tujute, tutubu, tuwaombe msamaha tulio wakosea,  na tudhamirie moyoni kuwa hatutarudia tena kutenda hayo makosa. 

Ni mimi: emu-three

No comments :