Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, January 31, 2018

MKUKI KWA NGURUWE-71



 Kikao kiliendelea, na mwenyekiti akawa mkali kidogo, kabla ya kusoma dondoo nyingine za kikao, akasema;

‘Ninataka hili niliweke hili wazi, siku nyingine mkiniita kwenye vikao vyenu, sitaki kuona kitu kama hiki, kwanza mumechelewa kufika, mimi kama mwenyekiti natoa onyo, sipendi tabia hiyo itokee tena, mkiniita kwenye kikao chenu mjipange vyema, muda ni mali, sina muda wa kupoteza…’akasema baba

‘Samahani kwa hilo mwenyekiti…’nikasema

‘Sijatoa nafasi ya mtu kuongea…’akasema na mimi nikabakia kimia

‘Pili sitaki mambo kama haya ya watu kujitokeza katikati ya kikao bila mipangilio, na tatu kikao kama hiki mkinichagua mimi kama mwenyekiti wenu, sitaki mtu kujiona yeye yupo juu yangu, mimi ndiye mwenye mamlaka ya kikao hiki, mambo ya familia zenu mnayaweka pembeni...mnanielewa …’akasema.

‘Sawa, lakini mzee, naweza kujitetea kwa hilo…’akasema mume wangu

‘Sijataka mtu kujitetea…’akasema na mume wangu akabakia kimia

‘Naona wewe mjumbe unataka kuongea sana, au nikupishe wewe uje hapa,..siolazima mimi niwe mwenyekiti..na kujitetea, unajitetea nini, kwani mimi nimesema nataka kutoa adhabu leo, ninachotaka kukiweka wazi ndio hicho, unasikia mkwe…na hapa sio mkwe, wewe ni mjumbe wa hiki kikao, au sio…’akasema mwenyekiti

‘Ndio nimekuelewa baba mkwe…, nilitaka tu, nikuelekeze kitu kwenye hiyo katiba…’akasema na mwenyekiti akaiangalia ile katiba halafu akaisogeza pembeni na kusema;

‘Hapa hatuongozwi na hii katiba yako,…maana sisi hatuijui, au nimekosea wajumbe, au niwaulize wajumbe je mnaifahamu hii katiba..?’ akauliza na wajumbe wakakaa kimia, na ndipo akaanza kuuliza mtu mmoja mmoja…

‘Docta na mkewe, mnaiafahamu hii katiba…?’ akauliza mwenyekiti

‘Hatuifahamu ndugu mwenyekiti…’akasema docta, na mkewe akabakia kimia.

‘Na…nimuulize na nani, haya wewe uliyetuingilia kwenye hiki kikao, nikuulize wewe unaifahamu hii katiba…?’ akaulizwa shemeji mtu

‘Mhh..naifahamu kwa mantiki…’akatulia

‘Ongea, usiwe na wasiwasi, nimekuuliza … kwa hivi sasa unaweza kuongea tu…haya kwa mantiki gani..?’akaambiwa na kuulizwa.

‘Naifahamu kwa vile nimemuona kaka akiwa nayo…’akasema

‘Ukajua kuwa ni katiba , au kwa vile imendikwa hapa juu, …Je yaliyoandikwa ndani unayafahamu, yanakuhusu wewe..umeshawahi kuyasoma..?’ akaulizwa

‘Hayanihusu, siku-ya-yasoma kwa sababu hayanihusu…’akasema

‘Kabla ya kaka yako kuionyesha hii katiba hapa, uliwahi kuiona wapi kabla…?’ akaulizwa

‘Mhh…niliwahi kutumwa na kaka, …kuichukua nyumbani na kumpelekea hospitalini…’akasema

‘Kwanini alikutuma wewe…?’ akaulizwa na kukaa kimia

‘Nduguzanguni, ninachotaka kukielezea hapa, ni jinsi gani katiba hii isivyowahusu watu wengine, zaidi ya familia husika,… haya ya kwanini…kukuhusu wewe bwana mdogo yatakuja baadae maana mpaka hapo nimegundua jambo….wewe ndiye unayetumwa kila kitu na kaka yako, au sio…?’ akaulizwa

‘Sio kila kitu mwenyekiti,..ila mara nyingi  ananituma…’akasema

‘Kwahiyo wewe umeifahamu hii katiba kwa kutumwa, na sio kuwa inakuhusu au sio..?’ akaulizwa

‘Ndio mzee, …hainihusu…’akasema

‘Je kwenye kikao hiki inastahiki kutumiwa..kuongoza hiki kikao, ..?’ akaulizwa

‘Hapana mzee, nionavyo mimi, hiyo ni katiba ya wanafamilia, na sisi wengine haituhusu, natumai hilo ni jibu la wote, au sio …’akasema na wajumbe wakatikisa kichwa kukubaliana na hilo

‘Sawa kabisa, kumbe kweli unaifahamu kuwa ni ya wanafamilia, na huenda unaifahamu zaidi ya hilo…mmh, mawakili, nyie kwanza siwaulizi hili, hata mke wangu hapa simuulize maana yeye yupo na mimi, au nikuulize mke wangu,…’akasema akimgeukia mama

‘Hapana endelea tu mwenyekiti, tujali muda…’akasema mama, na baba hapo akanigeukia mimi akitaka kuniuliza lakini akaghairi na kugeukia kikao, akasema;

‘Tujali muda, msaidizi wangu wa nyumbani kaniasa hilo, haya tuliache hilo kwanza, ..nilitaka ndugu mjumbe, mume wa familia kuliweka hili sawa, kuwa kuna mambo ya kurejea katiba yako ni sawa…, na kuna mambo ambayo hayastahiki, na hili la kuongoza hiki kikao, halihitaji katiba yenu, katiba ya hapa ni dondoo za kikao na mimi mwenyekiti ndiye ninayeziongoza hizo, au sio…’akasema mwenyekiti

‘Sawa mwenyekiti nimekuelewa…’akasema mume wangu na alitaka kuongeza neno, lakini mwenyekiti hakumpatia nafasi,…

‘Kingine kuna mambo nataka kuyaweka wazi, ndio mna katiba mna utaratibu wenu wa kimaisha kama familia ni sawa pia…, mimi sikatai, na nimefurahi kama mlifikia hatua hiyo,lakini ninataka niwarejeshe nyuma kidogo, niwakumbushe, nyie wanandoa….’akasema na kumgeukia mume wangu

‘Nilishasema kwenye familia yetu hatutaki mambo ya kashifa, ikiwemo kuvunja sheria za ndoa na za nchi, na kuvunja sheria ni swala pana zaidi, ni pamoja na uwongo, kusalitiana, na kugushi, na mambo kama hayo, ..mambo ambayo yanatuharibia jina letu,achilia mbali kuua, ambalo ni kosa la jinai ....hilo niliwakanya tangu mapema, na nilisema hata kama ni mtoto wangu kafanya hayo, sitasita kumfikisha kunakostahili..

Nilifanya hilo kwa binti yangu, niliposika kakamatwa, sikukimbilia kumtoa, nilifanya uachunguzi wangu ili niupate ukweli, sijamlea binti yangu awe mvunjifu wa sheria,..hilo najisifu…sasa kama akitaka kunisaliti na mimi nitawajibika kwa hilo..hakuua, na ndioa maana nilimsaidia…’akatulia,

‘Sasa kwako wewe mume wa familia,…’akasema

‘Ndio mwenyekiti, nakusikia….’akasema mume wangu

‘Ni kwanini hayo, ni kwanini niliwaasa mapema hilo jambo…’akasema halafu akatoa gezeti, na kulikabidhi kwa mume wangu

‘Hebu soma hicho kichwa cha habari hapo juu…’ akaambiwa mume wangu na akawa anasita kulipokea, halafu akalipokea, na kusoma

‘Mkwe wa familia ya mzeemkongwe wa siasa,(akataja jina) anashukiwa kwa mauaji ya wakili wake…’akaliachia lile gazeti kama kashika kitu kichafu

‘Sio kweli mzee, waongo hawa, watu wa udaku hawa…’akasema

‘Hebu soma na hili…’kampa gezeti jingine

‘Mkwe wa…’akasoma hivyo tu na kuliweka pembeni, akasema

‘Ina maana mzee unaamini haya magazeti, haya hayakufai mzee…;akasema

‘Hebu nikuulize mimi ni baba yako…?’ akauliza mwenyekiti

‘Ni baba mkwe,  mwenyekiti..’akasema

‘Kwanini hao watu wa magazeti hawajaandika, jina lako na baba yako, wakaandika mkwe wa…unaelewa mantiki yake..?’ akauliza

‘Ni magazeti ya udaku hayo tu mzee…’akasema

‘Hujanijibu, hata kama ni ya udaku lakini yanasoma na watu wengi kuliko hayo magazeti mengine,…nimekupati hayo magazeti kama mfano…kukuonyesha ni kwanini, ..nilikuasa mapema kabla hujaoa kwangu..’akatulia

‘Ni kwasababu mimi nipo kwenye ulingo wa kisiasa…silifichi hili, kuwa katika siasa kuna upinzani, na kila mmoja anajaribu kutafuta kashfa za mwenzake..ili afanikiwe kwenye ulingo wa siasa, hilo linakubalika, kisiasa, ndio maana najihami, na wenye lengo jema na mimi watanisaidia kwa hilo, mumenielewa jamani, mimi naongea sana …’akatulia

‘Lakini baba hayo ni maswala yako, na sisi hatuwezi kuyaingilia…au sio jamani..’akasema mume wangu.

‘Ndio maana ulipokuja kuoa kwangu nilikuambia hilo mapema tu, kuwa mimi nipo hivyo, na maisha yenu yawe vipi..na hayo maisha yenu, kuwa vipi sio kwamba nawataka muwe kama mimi, hapana, niliwatahdaharisha kuwa ningelipenda maisha yenu yawe mfani wa mume na mke bora…kweli si kweli…?’ akaulizwa

‘Ni kweli mzee…’akasema

‘Sasa tatizo lipo wapi, nimekosea nini hapo, kuyakemea hayo yanayokwenda kinyume na maadili ya mke na mume bora, nimekosea nin kuyakemea maovu, ..sitaki kashfa, na nilisema kama mtu hataliweza hilo, asioe kwangu, hata binti yangu nilimuwambia kama mume wako ..hana maadili mema, usikubali akuoe, akasema , atahakikisha mume wake yupo kwenye njia sahihi, kweli si kweli…’akasema na kuniuliza mimi, na kabla sijajibu mimi,  mume wangu akasema;

‘Ni kweli mzee, mke wangu kanisaidia sana, na tunaishi vyema tu…mengine ni udhaifu tu wa kibinadamu…’akasema.

‘Sasa mimi nisingelikaa kimia tu, mfanye mtakavyo, na baadae mje kunisema kwanini mimi sikuwahi kuwaambia hilo, je sikukuambia hilo mapema, wakati unakuja kuoa kwangu…?’ akauliza mwenyekiti kumuuliza mume wangu

‘Uliniambia mzee…lakini..’akasema mume wangu

‘Sitaki lakini, huko kujitetea kuwa ni udhaifu wa kibinadamu, sio utetezi, ufanye makusudi halafu usingizie ubinadamu, hakuna hilo..unasikia

‘Sasa…kama kuna kujitetea utakuja kujitetea sana…au kama unataka kujitetea, basi nikuuliza ni kwanini umeyapinga hayo maagizo yangu, Ulidharau sio …kwa vile sasa una mamlaka kama ulivyoanza kunialati ..kuwa mna katiba inayokulinda…?’ akauliza

‘Hatujayapinga maagizo yako mzee, labda ni katika kuwekana sawa tu, au kuwajibika kama limetokea hilo ni kwa bahati mbaya tu mzee, na kashafa gani kubwa tumefanya sisi, kwangu mimi sijaiona, ni mambo ya uzushi tu..’akasema

‘Kufikia hadi kuua, sio kashfa…?’ akaulizwa

‘Mzee nani kaua, hakuna mtu aliyeua hapa,..huo ni uzushi, na polisi wanafanya hivyo kikamata watu katika kuhangaika kumpata muhalifu, lakini sio kweli…’akasema

‘Kutoka nje ya ndoa na kuzaa ovyo sio kashfa…?’ akauliza mzee

‘Aaah, huko mzee umeenda mbali,  ..hapana mzee, ni maneno ya watu  tu, waongo hao…’akasema

‘Una uhakika na hilo jibu lako..?’ akauliza mzee

‘Kwanini mzee unauliza hivyo, mke wangu hajafanya hilo, walimfunga kimakosa, wakimshuku kuwa ameua, na sio kweli, hata wewe mwenyewe umelithibitisha hilo…’akasema

‘Sijamuulize mke wako, nimekuuliza wewe, uliyekuja kuoa kwangu, umesema hujafanya kashafa kubwa, au sio,…na unavyoonekana kuzaa nje kwako sio kashfa, anyway…mimi najaribu kukuweka sawa hapo, au wewe kashafa kwako ni ipi, ya wizi, ya kuhujumu au nini kashafa kwako…?’ akauliza

‘Mzee mimi sijafanya kashafa kubwa kihivyo, ya kukuharibia mambo yako kisiasa ndio utetezi wangu huo…’akasema

‘Haya mume wa familia, ngoja tutakuja kuliona hilo…,’akasema mwenyekiti

‘Sawa mzee nitajitetea kwa shutuma zote, nina imani utakuja kunielewa…’akasema

‘Ngoja tusipoteze muda, twende kwa mujibu wa utaratibu wa kikao, dondoo zinasema sasa ni wakati wa kumkaribisha mwenyeji wa kikao, mtu aliyetuita hapa kwenye kikao, kuelezea duku duku lake, lakini kabla sijamkaribisha, nataka yeye anipe maelezo sahihi, maana yeye amekuwa muda wote akitetea ndoa yake, mume wake nk..sasa nataka haya uyaweke wazi, pamoja na hayo uliyotuitia…’akatulia kwanza akiniangalia mimi, halafu mume wangu

‘Ni kwanini sisi wazazi wenu tusiingilie familia yenu, wakati mumeshaingilia familia kuu, kwa matendo yenu yenye kashfa, ushahidi mmojawapo ni hayo magazeti, ina maana mumefanya mambo ambayo yamekiuka yale makubaliano yetu ya awali…ni kwanini sisi kama wanafamilia kuu tusichukue maamuzi, tuliyoona ni sahihi, kwa masilahi ya familia na vizazi vijavyo,…hili ni muhimu.’akasema mwenyekiti na mume wangu akawa anataka kuongea

‘Tulia…’mwenyekiti akasema na mume wangu akatulia.

‘Ni kwanini nyie watoto mnatengeneza katiba ya kutuzuia sisi wazazi wenu tusiwaingilie hata kama mumeshindwa kutimiza wajibu wenu ndani ya familia zenu, sitaki kusema yapi ni yapi mumeyakiuka, lakini kwa ujumla wake, mumetia doa familia yetu, haijawahi kutokea hivyo kabla, je ni kwanini, na kuna nini...’akasema na kuniangalia mimi, kabla sijasema kitu, mume wangu akanyosha mkono na hata kabla hajaruhusiwa akasema;

‘Mimi kama mume wa familia inayoshutumiwa kwa kukiuka hayo aliyosema baba, nataka kuelezea ni kwanini hayo yalitokea, naomba niongee mimi kwanza kabla hajaanza kuongea mke wangu japokuwa ni yeye aliyeitisha hiki kikao,....’akasema na baba, akataka kumkatiza lakini mimi nikasema;

‘Mwenyekiti, hebu muache kwanza aongee amalize yote…na akimaliza mimi nitaongea tu...’nikasema

‘Kikao ni lazima kiwe na mpangilio, sio kwamba mimi sifahamu hilo, kuwa wewe ni mume wako familia, hata mimi ni mume wa familia, tena ni baba mkwe wako, au wewe ni familia special,..mmh, …’akasema mwenyekiti kwa ukali

‘Hapana mzee…nilitaka kujibu shutuma zako mzee…’akasema

‘Hiki kikao  sio wewe uliyekiitisha, tumeitwa na mke wako, na hii ipo kwenye ajenda ...na kama nilitaka wewe uongee, ningelikupa hiyo nafasi, sipendi kabisa huo utaratibu wako…’akasema mwenyekiti

‘Na nikuambie kitu,.., heshima ni muhimu sana,..sawa kwa vile mke wako kakuruhusu uongee, sijui labda ni heshima au ni kwa mujibu wa katiba yenu kuwa hawezi kuongea mke mpaka wewe umnyoshee njia, …haya ongea kama ulivyotaka wewe, maana kila hatua mnazidi kunionyesha jinsi gani mlivyo....’akasema baba na mume wangu bila kujali akasema;

‘Nakubali kuwa kuna udhaifu ulitokea, na hilo linaweza kutokea kwa yoyote yule, hasa mnapokuwa katika harakati za kutafuta maisha, kuna changamoto za hapa na pale,..huenda katika kuyafanikisha hayo tulijaribu njia ambayo sio stahiki, ...ni katika kujaribu, ndio tukajikuta tumeteleza,..naomba tusamehewe kwa hilo...’akasema.

‘Lakini, pamoja na hayo, mimi nimeshaitoa katiba yetu, ambayo inanilinda mimi jamani, sifanyi haya kwa vile..hapana ni kwa mujibu , ndio maana nikaitoa hiyo katiba hataka kama haiwahusu wote, lakini kikao hiki kinahusu familia husika …samahani kwa hilo mwenyekiti maana mimi nitakuwa narejea mara kwa mara hiyo katiba, kwa mantiki ya kulinda familia yangu…’akasema

‘Endelea…’akasema mwenyekiti

‘Kama kuna kitu kinaitwa makosa,au kashfa imefanyika, ..kama nilifanya mimi, basi ujue nilifanya kwa nia njema tu, na kama nilitenda jambo fulani, kama mume, nina haki zangu, kisheria...na nilifanya mengine kwa minajili ya msilahi ya familia, hatujui kama linakizana na wewe kisiasa, sijui mimi kama hayo ni kashfa..’akatulia

‘Endelea…’mwenyekiti akasema alipoona mjumbe yupo kimia kidogo

‘Na ningelipenda kuliweka hili wazi kwa nia njema tu kuwa, sisi kama familia tuna sheria na taratibu zetu, kwa vile ni familia inayojitegemea, kama mtaona tumekwenda kombo, ni swala la kutushauri tu, na sio kutuingilia kiasi cha kutoa hata adhabu,...’akasema

‘Endelea…’akasema mwenyekiti

‘Mwenyekiti, katiba yetu ipo wazi, inatulinda, inanilinda mimi kama mume wa familia, naomba hilo liwekwe bayana, hakuna familia nyingine yenye mamlaka ya kutuingilia, au kutuadhibu sisi kinyume na hiyo katiba, hakuna…sheria hiyo, hivi mimi kweli naweza kuja kuingilia familia yako mzee, hakuna kitu kama hicho..nachukulia mfano huo sio kwa kukosa adabu naomba nieleweke hivyo...’akasema na kukaa kimia

‘Umemaliza...?’ akauliza mwenyekiti

‘Ndio mwenyekiti, nilitaka kuliweka hilo wazi tu, maana nimeona ukitoa vitisho kwenye utangulizi wako..’akasema

‘Sio vitisho mjumbe…, hayo niliyoongea ni kweli na yatafanyika hivyo…’akasema mwenyekiti

‘Itabidi nimuite wakili wangu kwa hilo…’akasema mume wangu

‘Wa nini..?’ akauliza mwenyekit

‘Unavunja katiba yangu na familia yangu…’akasema

‘Wapi nimevunja katiba yako..?’ akaulizwa

‘Unatoa lugha za vitisho, kuwa nyie kama familia kuu mnaweza kutuwajibisha, ..na vitu kama hivyo, hilo halikubaliki…’akasema

‘Usitupotezee muda, na katiba yako, hii ambayo bado sijaimini, …’akasema

‘Ukisema hivyo mzee utakuwa unatuingilia, na kuvunja kanuni na sheria za nchi, katiba hiyo, inatambulikana maana tumeisajili …au unaniona mimi sifai kuwa mume wa familia…?’ akauliza

‘Sikiliza mume wa familia, ni matendo yako.. , kama ulikubali kuoa kwangu, ujue una wajibu wa kutunza heshima yangu, sio kwamba nakuingilia, ...na sina haja ya kukuingilia, ila kama umevuka mipaka sitasita kukuwajibisha, kama umefanya mambo yenye kuleta kashfa kwenye familia hilo sitalivumilia kamwe, umenisikia, ilibidi mliweke hilo kwenye katiba yenu, maana ndio katiba ya awali wakati unaoa kwangu..’akasema mwenyekiti.

‘Katiba ya familia yangu inanilinda ndugu mwenyekiti samahani sana kwa hilo, mtaniona napoteza muda kwa hilo, lakini ni lazima hilo lieleweke maana nafahamu ni nini kinachofuatia,..mimi sitakubali jambo lolote liende kinyume na katiba yetu ya familia, lije livuruge ndoa yangu, sitakubaliana na hilo..’akasema mume wangu, na mwenyekiti akaichukau ile katiba na kuinua juu na kuuliza

‘Hii ndio Katiba unayosema inakulinda?’ akauliza mwenyekiti

‘Ndio  mwenyekiti, hebu gauze huku, ehee, ndio hiyo hiyo...’akasema mume wangu.

‘Katika katiba yenu halali,…sijui kama ni hii,  mlikubaliana kuwa kila kilichoandikwa kitasimamiwa, kitatekelezwa, na sheria itafuata mkondo wake, si ndio hivyo, kama mmoja akikosea, kutokana na mlivyokubalia atawajibishwa kisheria, hata kama ni kuvunjika kwa ndoa..., au sio?’ akauliza mwenyekiti

‘Ndio…hahaha, kumbe uliwahi kuisoma, …ndio hivyo mwenyekiti…’akasema

‘Sijaisoma hii, maana mimi bado sijaihakiki, kisheria,…nakuuliza tu kama kipengele hicho kipo…’akaambiwa

‘Ndio tumekubaliana hivyo, na kila mmoja analifahamu hilo, ndio maana tukaisajili hiyo katiba, na mimi nipo tayari kuwajibka kwayo, hiyo hapo isome,utaona kila kitu kipo wazi, hakuna nilichokosea hapo,..’akasema ni kunigeukia mimi. Sikusema kitu

‘Lakini unaposema kuvunjika kwa ndoa una maana gani mzee?’ akauliza alipohisi kuna kitu kategwa.

‘Unaniuliza tena mimi, si kipengele hicho kipo kwenye katiba yenu halali au sio, si umakubali kuwa kipengele hicho kipo, au..…’akasema mwenyekiti

‘Nahisi hukusoma sehemu yote kwa ukamilifu wake, ukisoma vyema hiyo katiba utaona kuwa mimi ndiye mwenye usemi wa mwisho kuhusu ndoa, na ndivyo ilivyo hata kwenye dini…au sio,..na mimi kama mume, siwezi kukubali ndoa yangu ivunjike, nitailinda kidini na kikatiba yetu hii ya familia,tuliyokubaliana nayo..’akasema

‘Nauliza tena,  upo tayari kuwajibika kutokana na katiba yenu halali,ambayo inatambulikana na msajili wa katiba,… ?’ akauliza mwenyekiti

‘Ndio nimeshakuambia hilo, yote yapo wazi kwenye hiyo katiba, sioni kwanini uniulize swali hilo, wakati katiba unayo hapo, isome tu mzee, ili kila mjumbe asikie hilo,.. na mimi nimekubali na sahihi yangu ipo na ya mke wangu ipo na ya wakili wa familia pia…wakili ambaye anayetambulikana na mke wangu, au sio mke wangu..?’ akauliza mume wangu.

‘Unajua kuongea sana siku hizi..’akasema mwenyekiti

‘Hapana ni lazima nionyeshe uhalisia, mimi kama mume wa familia, uliniozesha mimi, niwe mume wa binti yako, kwanini nisiongee kutetea ndoa yangu, hata wee utanishangaa nikikaa kimia, au sio..’akasema

‘Huyo wakili aliyesimamia huo mkataba wenu ni nani..?’ akauliza mzee, kabla mimi sijasema neno, na mume wangu kwa haraka akasema;

‘Ni wakili wa familia, yule pale,….akatae kama sio yeye aliyetayarisha hiyo katiba, sahihi yake ipo, hawezi kuikana, au…muulizeni yeye mwenyewe…’akasema

‘Nakumbuka awali ulilalamika kuwa mbona wakili wako hayupo, ina maana wewe una wakili mwingine zaidi ya huyo…?’ akaulizwa

‘Ndio yupo..’akasema

‘Ni kwanini sasa ukatafuta wakili mwingine kama huyu ndiye aliyewawekea sawa hiyo katiba yenu halali, inayosimamia kila kitu kwenye familia yenu mpaka hapa unatulizimisha na sisi tuifuate,…?’ akaulizwa kabla hajajibu mzee akaendelea hapo hapo kwa kusema;

‘Huyo si ndiye wakili wa familia sio, na katiba hiyo halali, ameiweka yeye sawa kisheria, maana nyie ndio mlitayarisha mawazo yenu, mkajadiliana kila mmoja akatoa mawazo yake kipengele kwa kipengele, wakili yeye, alichofanya nikuweka sawa hivyo vipengele kimoja baada ya kingine ili vikae sawa kisheria, kweli si kweli...?’ akaulizwa

‘Ndio mzee,… ni wakili wa familia, lakini kiutendaji, mimi kama mume wa familia niliona kuna haja ya kuwa na wakili mwingine,, ukiangalia kwenye hiyo katiba inanipa mamlaka hayo ya kufanya mambo nikiona ni sahihi kwa masilahi ya familia,…mimi niliona kuna umuhimu wa kuwa na wakili mwingie, sio mbaya wangapi wana wakili zaidi ya mmoja..’akasema

Mwenyekiti akaangalia saa, halafu akaangalia pale walipokaa mawakili, halafu akasema;

‘Kabla sijamuuliza wakili kulithibitisha hilo, nakuuliza maswali haya muhimu napenda uyajibu ukiwa na uhakika nayo …’akasema mwenyekiti

‘Uliza tu mzee, sina wasiwasi kabisa, mimi nipo hapa kwa ajili ya familia yangu ,na ndoa yangu…’akataka kuendelea na mzee akauliza

‘Kwahiyo kwa jinsi ilivyo, nyie maisha yenu , majukumu yenu, na kila kitu, siwezi kusema kila kitu, ila mambo yote muhimu yanategemea huo mkataba halali…?’ akaulizwa

‘Ndio mzee, unatusaidia sana…’akasema

‘Na je mtu akikosea, kuna vipengele vya hukumu,..?’ akaulizwa

‘Ndio vipi, hatukubakiza kitu…’akasema

‘Kwahiyo wewe kama umekosea,au mke wako kakosea, haihitajii kwenda mahakmani, hukumu zipo wazi, na hukumu hizo zinaweza kusimama kama ushahidi unajiotosheleza..?’ akaulizwa

‘Ndio kabisa…’akasema

‘Na wewe hapo ulipo, upo tayari kuhukumiwa kwa mujibu wa katiba yenu halali…?’ akaulizwa na hapo kidogo akasita

‘Kwa mujibu wa katiba yetu ndio…kama inavyosema ..ndio…kila kitu kipo wazi, na nashangaa kwanini mke wangu akaamua kuitisha kikao kama hiki, labda kama anaona yaliyopo kwenye hio katiba, hayafai, tubadilishe, labda, iwe hivyo, vinginevyo, sisi hatukuwa na haja ya vikao kama hivi..’akasema

‘Sasa nakuuliza swali, hili swali ni muhimu sana, nataka ujibu ukiwa na uhakika, maana baada ya hapa, sisi kama kikao, mimi kama mwenyekiti sitarudi nyuma tena, maana sikutaka iwe hivi, ila wewe mwenyewe umenilazimisha nifanye hili, kila mara katiba katiba, haya …ngoja tufuate katiba yenu, pamoja na mengine ambayo ni muhimu kwenye hiki kikao…

Sasa hili nahitajia jibu lako kutoka moyoni, uwe na uhakika nalo..’akasema na mume wangu akasubiria,…

‘Je una uhakika kuwa hii ndio katiba halali mliyokubaliana wewe na mke wako,...?’

Alipoulizwa swali hili akatulia kwanza akionyesha uso wa kushangaa…, halafu akageuka na kuniangalia mimi, mimi nikawa natoa tabasamu tu, lakini sikusema neno, yeye  akasema;

‘Kwanini unaniuliza swali kama hilo mzee, kwani wewe ulikuwepo wakati tunaitengeneza hiyo katiba mpaka utoe kauli hiyo ya shaka,…, kuwa labda unaifahamu katiba nyingine zaidi ya hii…’akasema

Mwenyekiti akamuangalia tu, na yeye akaendelea kuongea kwa kusema

‘Ndugu mwenyekiti, wewe usisikilize maneno aliyonitania mke wangu awali, hakuna katiba mbili, na mimi ndiye ninayeifahamu hiyo katiba kwa vile mimi ndiye mume wa familia yangu, katiba ndio hiyo hakuna katiba nyingine…’akasema

‘Sikutaka maelezo mengi kihivyo, …nataka jibu la uhakika, …nakupa dakika moja ya kulifikiria hilo jibu lako vyema, ni muhimu sana kwangu na kikao hiki kilisikie hilo jibu kama ushahidi…, ‘ akasema

‘Kama ushahidi…!!’ akauliza mume wangu

‘Ndio…nataka kupima uadilifu wako wa ndoa…nataka katiba yako yenyewe ifanye kazi, si wewe umelisisitiza hilo, au unaanza kuogopa…?’ akaulizwa

‘Hapana..siogopi, maana naifahamu vyema katiba yangu, wewe uliza swali lako tu..’akasema

‘Wewe unatamba kuwa wewe ni mume mwema wa familia,,kama kweli wewe ni kiongozi muadilifu wa familia,  nirudia swali langu, kumbuka uwongo, kugushi, wizi..kuua, ni moja ya mambo yanayokiuka sheria, sijui kwenye katiba yenu mumeyawekaje hayo, na kuna mambo ukiyafanya, unavunja ndoa,.., sasa nataka uwe muwazi kwa hilo, kama huna uhakika useme...’akasema mwenyekiti

Mume wangu hapo akakaa kimia kidogo, na mwenyekiti akauliza tena….;

‘Je kweli wewe una uhakika kuwa hii ndio katiba halali, mliyoitengeneza wewe na mke wako, ikasainiwa na wakili wa familia yenu..nasisitiz hapo, tena, je una uhakika nataka unijibu, na nataka uchukue muda kuliwazia hilo jibu lako…’akasema mwenyekiti akiangalia saa yake.

Nilimuona mdogo wake aliyekuwa pembeni, akiinamisha kichwa chini, kama anaomba, halafu akainua mikono na kujishika kichwani, akainua kichwa na kumuangali  kaka yake,…

Rafiki wa mume wangu docta, alikuwa makini kweli akifuatilia hatua kwa hatua, na alipoona mdogo mtu anahangaika, kutaka kuongea, akamuangalia na nahisi alikuwa anataka kumuashiria huyo mdogo mtu atulie…

Sasa nikamuona mdogo mtu kama anataka kunyosha mkono aongee, lakini akarudisha, alipokutanisha macho yake nay a docta, kiukweli hata mimi pale nilipokaa, ..nilitamani huyu shemeji mtu aongee huenda ana jambo muhimu la kumsaida kaka yake, lakini sikuwa na jinsi ya kuingilia hilo

Nikageuka sasa kumuangalia mume wangu, alikuwa akitabasamu tu hana wasiwasi, akasema;

‘Naweza kujibu mwenyekiti, mimi sina wasiwasi…’akasema na mwenyekiti, kabla hajamjibu akaangalia saa yake

NB: Mambo yamenza, ushaidi wa kwanza wa kupima ‘uaminifu kwenye ndoa’.


WAZO LA LEO: Uongozi ni wito, uongozi ni kubeba dhamana za watu, na ukiwa kiongozi mwadilifu, watu wako ni kwanza, na wewe unakuja baadaye, kwahiyo kimasilahi, utahakikisha kuwa watu wako wametosheka kwanza, kabla ya kujali tumbo lako, huo ndio uongozi bora.


 Je kiongozi kama huyo yupo katika hii dunia ya sasa,...
Ni mimi: emu-three

No comments :