Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, November 1, 2017

MKUKI KWA NGURUWE-18


Hatukuweza kuafikiana siku hiyo, hadi siku nyingine tukakutana tena hospitalini, na docta akafufua yale mazungumzo yetu…

‘Unakumbuka nilikuuliza jambo, tukawa hatukuelewana…nahisi hukunielewa dhamira yangu,..nimeliwaza sana hilo nikaona ni lazima tuliongee na tufikie muafaka, sijui unanielewa….?’ akaniuliza na mimi nikawa nimeinama nikiwaza mengi kichwani. Nimekuwa mtu wa mawazo sana kiukweli. Sipati usingizi kabisa, na nahisi itanieletea matatizo, kwahiyo nikaona ni vyema nisikilizane na docta tu..

‘Lakini, mimi sijaona kosa langu, sijaona kuwa nina matatizo kihivyo…, sioni kabisa, kichwa changu kimetaliwa na kazi zangu za kiofisi mambo mengine ni ya kifamilia zaidi, ni mambo ya kawaida tu na nina imani  yataisha tu…,sasa ukiniambia nikuambie kila tatizo la familia yangu unakosea….’nikasema


‘Shemeji, umesema una matatizo ukayataja matatizo kuwa yapo matatozo ndani ya nyumba yako..ambayo uliyaita  ni ya kifamilia, ambayo naona umeshindwa kuyasema ni matatizo gani, kwangu nahisi huenda yakawa ndio chanzo cha yote hayo mengine..sijui lakini nahisi hivyo, maana hujanifafanulia...’akasema na mimi nikawa nimetulia tu.

‘Lakini pia ulisema kuwa kuna matatizo ya huko kazini kwako, hayo ukasema  ni matatizo ya kawaida tu ya kikazi , au sio, siwezi kuingilia mambo ya utawala wako wa kikazi, sawa nimekubali kwa hilo, huko ni kwako na utaalamu wako…?’

‘Yap…ya kawaida..napambana nayo, …’nikasema 

'Hata hivyo nakushauri, hayo mambo ya kikazi, usiyaweke akilini sana, yakawa ndio kipaumbele chako,  kiasi kwamba yanameza maswala ya familia yako, kwani unafany akzi ili iweje, ni kwa masilahi ya familia yako, au sio…sasa ukiumiza kichw ahuko, kazi, ukaupa mgongo, ndo ayako utakuwa umefanya nini…unielewe hapo…’akasema

‘Sawa nimekuelewa docta….’nikasema

‘Lakini kuna hili,…ulisema kuwa kuna matatizo huko kwa rafiki yako,…kuna kitu nataka tuje kukijadili, sio kwa utesi,..sipendi tabia hiyo, bali nataka tujenge na kuondoa tatizo kama lipo…kwa kulianza hili je huko kwa rafiki yako  kuna tatizo gani hasa la kukusumbua kichwa, maana huyo ni rafiki yako, kama nilivyo mimi, au sio…,?’ akaniuliza

‘Huko kwa rafiki yangu ni matatizo ya kawaida pia, wala yasikuumize kichwa, yule ni rafiki yangu namuona kama mdogo wangu , japokuwa tunalingana ki- umri. Kwahiyo mimi kama mzazi lipo ndani ya uwezo wangu....’nikasema na yeye akaendelea kusema;

‘Hata kama ni ya kawaida...kama unavyodai, kitu ambacho sikiamini, kwa vile umeshataja kuwa ni matatizo, ina maana yapo akilini mwako, na yanakusmbua akilini, na yanaweza kukupa matatizo, ukadondoka kwa shinikizo la damu, huwa inatokea, sasa isje kufika huko,…’akasema na nilikuwa sijamueleza kuwa nilipoteza fahamu.

‘Mhh, hata sikuelewi, …kwanini lakini, au kuna kitu unakijua mimi sikijui, kwanini usiniambie tu, kuliko tuzunguke zunguke…’nikasema

‘Kuna kitu nahisi kuwa kipo kati yako wewe na mume wako hujaniambia…, na kuna tatizo kati yako wewe na rafiki yako, nataka kulijua hilo,  kuna kitu ambacho ungeniambia, ningeliweza kuhitimisha hilo ninalolifikiria mimi na tukaangalia njia sahihi ya kulitatua…, lakini kawaida yangu kama unijuavyo,…sipendeleo haya, nimekusihi uniambie wewe kwa vile ni rafiki yangu tu,  la sivyo nisingelihangaika kabisa…’akasema

‘Ndio maana nakushangaa naona kama umebadilika siku hizi…, sio kawaida yako, kwanini uyatake haya ya watu, kuyafahamu,… na mwenyewe mara kwa mara umekuwa ukinikanya kuwa nisiwe na tabia ya kufuatilia mambo ya watu wengine.., na nisiwe mtu wa dhana mbaya kwa watu, au sio wewe…’nikasema

‘Hili sio la dhana mbaya…, ila mimi nataka nikusaidie ili baadae usije kunilauamu, najua kabisa baadae unaweza kunilaumu, kuwa huenda, nahusika, huenda nilijua, nataka nijitoe kabisa, lakini ni muhimu kwangu kulitatua hili kadri inavyowezekana…sasa hebu niambie…huyo rafiki yako, ana kukwanza nini, ni kuhusu ndoa yako…?’ akaniuliza tena

‘Ananikwanza,…!!! Sijasema hivyo… Nani kazungumzia kukwazana kwenye ndoa hapo!!!…nikuambie ukweli, huyo rafiki yangu hahusiani kabisa na lolote katika ndoa yangu,...nakuomba usije ukamuhusisha rafiki yangu na haya maswala yangu,..hahusiki na lolote lile..hilo nakuthibitishia...hayo matatizo niliyosema kuhusu  mimi na yeye, ni matatizo ya kawaida tu kati yangu mimi na yeye, hata mume wangu hajui...’nikasema.

‘Nikuulize kitu, unakubaliana na mimi kuwa mume wako yupo karibu sana na huyo rafiki yako..?’ nikauliza

‘Ndio hilo halina siri..ila kwa vipi sasa …kwa jinsi unavyofikiria wewe unakosea, sivyo hivyo, acha hilo…’nikasema

‘Nisawa nitaliacha, ila…, nataka kuwa na uhakika tu kuwa hilo umeliridhia, kuwa mume wako yupo karibu na rafiki yako, wanakula pamoja, wanatoka wakati mwingine pamoja…na imekuwa sipo karibu sana na yeye kwa vile wanakuwa na huyo rafiki yako,.utasema labda nawaonea wivu, hapa…sasa ,.je hilo halina wivu kwako wewe,  na sio sababu ya matatizo yako na rafiki yako, …wivu labda..?’ akauliza.

‘Karibu sana kwa vipi…ndio, kama umewaona wanaongea, au wanakula chakula pamoja, ni kawaida tu, tumezoea hivyo, wala usiwafikirie vibaya, siwezi kabisa kuona wivu kwa rafiki yangu, kuwa na mume wangu hivyo, na sizani kama inaweza kwenda zaidi ya hivyo, mengine ni dhana zako potofu, na ni wivu wako unakusumbua….’nikasema

‘Kama ni hivyo, sawa, kama umeliridhia hilo, sawa…na sio kwamba nawachimba, au wivu kama unavyodai, hapana,  ndio maana nilitaka uhakika kutoka kwako, nilijua hayo matatizo na rafiki yako huenda ni maswala ya wivu, ok sasa…ili tusaidiane, na mimi nirizike, eeh, ..maana kuna kitu kinanitia mashaka…’akasema

‘Kipi hicho kinachokutia mashaka, kuhusu rafiki yangu na mume wangu au…?’ nikauliza

‘Rafiki yako naona kakimbilia kuzaa kwa kuchelea umri, au sio, ni sawa maana aliwahi kuongea na mimi, kuhusu hilo, na mimi kama dakitari nikamshauri kuwa ni bora aolewe mapema, maana umri umekwenda, akasema yupo mbioni kulitatua hilo, nikajua keshapata mume , sasa naona kazaa, simuoni huyo mume…’akasema

‘Ndio hivyo hakuna shida, au ulitakaje wewe,…?’ nikamuuliza

‘Nilimuambia awe lakini awe makini sana na mawazo hayo…maana yanaweza kumpelekea akataka kuzaa tu, kwasababu ya kukimbizana na umri…lakini hakutaka kuongea na mimi zaidi, ni kweli kuna muda alikuwa karibu sana na mimi, mpaka watu wakatushuku vibaya, hata mke wangu, nikaona aah, tukakosana...’akasema

‘Ndio niliwaona mkiwa sambamba, lakini mimi nilijua mumarafiki tu kama alivyo karibu na mume wangu, japokuwa …alikuja kuniambia ulimtaka kweli si kweli…’nikasema

‘Hahaha, hayo yaache, sasa ni hivi, maana wewe ndiye rafiki yake, kwanini akaamua kuzaa bila kufunga ndoa, ulimshauri wewe hivyo, na je baba wa mtoto wake ni  nani?’ akaniuliza huku akiniangalia kwa macho ya udadisi, na mimi kwanza nikaguna, halafu nikaangalia pembeni na kusema;

‘Hilo hata mimi sijui..labda baba wa mtoto ni wewe,maana mlikuwa marafiki au sio, sasa sijui ,.. au ndio maana unataka kuchunguza kuhakiki kama mtoto ni wako au ni wa matu mwingine…’nikasema.

‘Aaah, sio wangu bwana.. .kama angelikuwa ni wa kwangu angelifanana na mimi, sura yangu haijifichi..na wewe ungelishaniambia , na nafahamu wewe unafahamu mwenzako katembea na nani , kweli si kweli...?' akaniuliza lakini kabla sijamjibu akasema

'Hivi wewe una uhakika kuwa mume wako hajawahi kutongoza wanawake wengine...hata kiutani tu, hayo yanatokea tu,...lakini baadaye unajirudi,... lakini hayo tuyaache maana ilikuwa zilipendwa, sasa niambie ukweli, unamfahamu aliyezaaa na rafiki yako, maana mimi naulizwa na wazazi wake...’akasema.

‘Mimi simfahamu....’nikasema .

‘Ok. Sio shida, nimewaambi ahivyo hivyo, lakini kuna mambo mengi wameniuliza, hasa kuhus urafiki wako na mwenzako…mmh, unajua mambo mengine unaweza ukayaficha, lakini wazee ni wepesi sana kuyagundua…’akasema.

‘Walisemaje…?’ nikauliza.

‘Hebu nikuulize  kwanza, una uhakika kuwa kweli mume wako hakuwa ametokea huko kwa huyo rafiki yako?’ akaniuliza  swali hilo na kunifanya nishtuke kidogo. Akilini nikajiwa na kumbukumbu, kuwa kuna muda niliona gari kama la mume wangu, pili, yule kijana wa kuosha magari, alisema ‘shemeji alikuwepo, huyu naye anasisitiza hilo hilo, na sijui anataka kuthibitisha nini…

 ‘Mimi nilikuwa huko kwa rafiki yangu...kama mume wangu angelikuwa huko si ningelimuona jamani…, labda alipita njia hiyo, sijui akitokea wapi, na sina uhakika na hilo, maana nijuavyo mimi alikuwa kwenye kikao…sasa alitokea wapi akapitia njia hiyo mimi sijui..’nikasema.

‘Kwahiyo mkiwa huko hukumuona mtu, aliyefika kwa rafiki yako, au….?’ Akauliza

‘Labda mdogo wake, nahisi hivyo tu…’nikasema

‘Mdogo wake!!!’ akasema kwa mshangao

‘Nahisi hivyo tu…sina uhakika…’nikasema

‘Kwanini unahisi hivyo…?’ nikaulizwa

‘Nimekuambia sina uhakika, tuliachie hapo tu, maana unanichimba sijui unatafuta nini…’nikasema hivyo maana nilijua hilo linaweza kuendelezwa mpaka nikasema yasiyotakiwa kusemwa.

‘Mbona mdogo wake, nilikuwa naye, alikuja kwangu kuna mambo fulani ya mkewe aliyafuatilia kwangu, ya kiafya..tukawa naye hapa tukiangalia mpira kwenye runinga,na niliachana naye muda mfupi, kabla sijapigiwa hiyo simu ya ajali....sizani kwamba aliweza kuja huko kwa muda huo mfupi,...’akasema

‘Mlikuwa naye nyumbani kwako…?’ nikauliza kwa mshangao

‘Ndio…sasa sizani, kam ni yeye, hata hivyo, yeye aliniomba gari langu kuwa anafuatilia mzigo wake, ndio maana nilishindwa kumchukua mume wako kwa haraka, kwani sikuwa na gari...ndio maana pia tukaamua kuagiza gari la wagonjwa....’akasema.

‘Ina maana gari lako mpaka sasa analo mdogo wa mume wangu?’ nikamuuliza.

‘Ndio maana yake, aliniazima gari langu , kwa vile gari la mumeo alikuwa nalo kikazi, au sio, na anasema alipiga simu kwa mumeo akawa hapatikani, ..haiwezekani akawa ndio yeye, labda yule mdogo wake mwingine, na yule hayupo hapa dar, alisafiri jana kama si kosei kwenda mikoani....’akasema.

‘Basi kama sio yeye, kuna mtu mwingine anafanana na ….huyo….’nikasema

‘Kwanini unasema hivyo…?’ akauliza

‘Hapana, tuyaache tu,  sioni kama kuna lolote baya, nitamgudnua tu kuwa ni nani yangu, ninachotaka kusema, ni kuwa mimi nilihisi kuwa yeye alifika huko kwa rafiki yangu wakati mimi nipo huko, kama sio yeye.basi kuna mtu mwingine anayefafana naye....ni hivyo tu basi...’nikasema nikiwa sina uhakika.

‘Mhh..nisamehe tu..akilini mwangu nahisi kuna tatizo hapo,…’akasema

‘Tatizo gani…?’ nikauliza

‘Hebu niambie ukweli....unasema wakati upo huko, alifika mtu anayefanana na mdogo wa mume wako si ndio hivyo, nyie muda huo mlikuwa ndani, au nje…?’ akauliza

‘Tulikuwa ndani…’nikasema

‘Sasa ulimuonaje kuwa anafanana na shemeji yako…?’ akauliza

‘Mhh..nilihisi tu hivyo, kwa vile mtoto anafanana na shemeji, na huyo aliyekuja alikuwa ….eeh, sasa unataka niongee yale ambayo sikutakiwa niyaongee…’nikasema

‘Nimekuelewa kuwa hisia zako kuwa huyo aliyezaa na rafiki yako, anafanana na mtoto wake, na huyo mtoto anafanana na shemeji yako, … sawa, lakin huna uhakika maana hukutoka ukamuona sawa, na kwahiyo ..eeh, …inawezekana hakuwa huyo shemeji yako, kama unavyofikiria wewe, labda alikuwa ni mtu mwingine au sio, ?’akasema na kuniuliza

‘Ni hivyo lakini rafiki yangu alisema ni shemeji ..akiwa na maana shemeji yangu ndivyo nilivyo muelewa…’nikasema na docta kacheka kiddogo


‘Ah, shemeji..ok…kwa maana nyingine wewe ulifananisha huyo mtu na shemeji yako wewe…, kwa kuhisi tu, kwa kupitia kwa mtoto,….na hakutaka wewe umuone, au sio, kwahiyo yeye…shemeji,…alipogundua kuwa upo hapo,  ...akaondoka kwa haraka…au sio.., hamkuonana naye, uso kwa uso…au sio…?’ akauliza

‘Ndio, kwahiyo unataka kujenga hoja gani hapo…?’ nikamuuliza

‘Nijibu kwanza , …kuna kitu nataka kukipata hapo, ..kwa leo sitaki unielewe vibaya..’akasema

‘Sawa, …ndio, lakini sikuonana na yeye maana alikimbia,..’nikasema

‘Alikimbia!!!..alikimbia,.., kwanini akimbie hapo kuna ulizo, majibu ya haraka ni ili usimuone, labda, kwa vile alitaka iwe siri, lakini anajua kabisa wewe ni rafiki yake au sio..ila wewe ulitaka kuonana naye, ili muweze kuliweka sawa, au sio, kwa nia njema, lakini akakimbia..au sio?’ akaniuliza

‘Mimi nilitaka niongee na yeye, lakini rafiki yangu hakutaka nikutane naye, na hata yeye alimuonya rafiki yake kuwa hataki yeye kujulikana,…nikaona ananiwekea uzito, ndio nikatoka nje , …sikumuona kwa wakati huo, kumbe alikuwa kajificha, sasa wakati nipo ndani ndio nikasikia akikimbia huko nje…’nikasema.

‘Mpaka hapo inaashiria kuwa huyo mtu , ni mtu wako wa karibu hakutaka kabisa umuone, umeona hapo..na hadi kukimbia hivyo, ina maana kubwa, hakutarajia kukuta wewe hapo, ndio maana akakimbia, na huenda alipofika kwenye gari lake, akalichukua na kuendesha kwa kasi sana, sasa wewe huoni ni nani huyo mtu…?’ akauliza

‘Sioni kuwa ni nani….hapana…sijaona kuwa ni nani zaidi ya shemeji yangu, ..lakini sina uhakika , maana sikuonana naye……’nikasema

‘Nje kulikuwa hakuna gari, gari lake alikuwa kaliweka wapi..?’ akaniuliza

‘Sikuliona gari lake hapo nje…na sijui alikuwa kaliacha wapi....’nikasema

‘Je ana gari, rafiki yako hakukuambia hilo?’ akaniuliza

‘Ndio analo, lakini hakuliacha hapo nyumbani,…na rafiki yangu hawezi kujua aliliacha wapi, maana alikuwa hajaingia wakaongea…’nikasema


‘Kwahiyo huyo mtu alipotoka hapo, alipogundua kuwa ni wewe, akaogopa akihisi kuwa atamfuatiliwa, utakuja kumgundua kuwa ni yeye, akatoka akalifuata gari lake akaondoka kwa mwendo kasi, au sio….?’ Akasema

‘Unataka kusema nini hapo mbona unarudia rudia hilo la ‘mwendo kasi’
Najua dhana yako…, kuwa labda anaweza akawa ni mume wangu au si ndio hivyo...?’nikamuuliza.

‘Mimi sijafikia kuhitimisha hivyo, ninachotaka ni kukuweka katika hali ya kuyakubali yote, kwasababu nijuavyo mimi, mume wako hawezi kukuficha kitu, au sio.. na kama kuna kitu kakifanya, atakuwa na wakati mgumu wa kutafuta ni namna gani atakuambia …hiyo ajali yake sio ya kawaida, kuna kitu hapo, ndio maana najaribu kutafuta hilo, ili umsaidie yeye, apone haraka…’akasema

‘Sio mume wangu, kwani kama angelikuwa ni yeye, kwanini alifika kwa haraka, halafu anikimbie, si alikuja kwa nia njema kumsalimia shemeji yake...kuna tatizo gani la kunikimbia mimi…, ndio maana nasema sio yeye, hilo sikubaliani nalo...mume wangu hana tabia kama hiyo...’nikasema nikijaribu kumuwazia huyo mtu aliyefika na kukimbia anaweza kuwa ni nani.

‘Kwani huyo mtu aliyefika, mkiwa huko ndani na rafiki yako alifikafikaje, kuna kitu gani cha tofauti unaweza kusema huyo mtu alikuwa nacho, cha kuweza kumkumbuka,,..?’ akaniuliza.

‘Viatu vyake vilikuwa vikitoa sauti,….’nikasema.

‘Mume wako alikuwa kavaa viatu vya kutoa sauti asubuhi ..?’ akaniuliza

‘Mhh.. ndio alivaa viatu vya kutoa sauti, lakini huo sio ushahidi tosha, au sio…’nikasema

‘Ok…hebu nirejee nyuma kidogo…, samahani lakini, rafiki yako alisema huyo aliyekuja wakati ukiwa kwake ndiye aliyezaa naye, sawa si sawa…?’ akaniuliza

‘Ndio, na alimpigia simu nikiwa pale…’nikasema

‘Una uhakika na hilo…’akasema akiniangalia kwa makini.

‘Uhakika wa nini sasa…, si yeye kaniambia hivyo, nitakuwa na uhakika gani zaidi ya kauli yake, au…’nikasema

‘Na ukiwa ndani, ukasikia akikimbia, lengo ni ili wewe usimuone, ulisikia viatu vyenye sauti…?’ akauliza

‘Itakuwa hivyo, ndio…’akasema

‘Kwahiyo hiyo kwa vyovyote huyo mtu aliyekimbia ni huyo huyo aliyefika awali,…sio kwamba huyo ni mwingine alikuwa kajificha, nataka uwe na uhakika hapo,…na kwa hiyo ndio huyo baba wa huyo mtoto, kutokana na kauli ya rafiki yako, na wewe ulikuwa na hamu sana ya kukutana na yeye au sio….?’ Akauliza

‘Ndio, lakini mimi nilishahisi kuwa ni huyo mdogo wa mume wangu, sasa ukisema mlikuwa naye hapa,…hapo sijui atakuwa ni nani mwingine…’nikasema.


‘Je tusaidiane kumtafuta huyo mtu…, kama ni muhimu sana kwako, na kama itasaidia kuondoka hiyo hali ya wewe na rafiki yako…ili usiwe na wakati mgumu,..?’ akauliza

‘Haina haja, sihitaji msaada wako kwa hilo….’nikasema

‘Sijui lakini…hata hivyo mimi nitaongea na rafiki yangu nitaujua ukweli wote, sio muhimu kwangu sana, lakini sitaki ije kuleta mtafaruku kwenye ndoa yenu,. Hata hivyo mimi…, sitaki sana kuingilia mahusiano yenu, …na usije ukaniona labda nayaongea haya kwa nia ya kukuharibia ndoa yako, ila mimi nataka nikuweke tayari, usije kusema mimi kama rafiki yako sikuwahi kukuambia hili, ukanioana mbaya baadae, nakufahamu sana wewe…’akasema docta

‘Una maana gani kusema hivyo..?’ nikamuuliza

‘Je ikitokea kuwa huyo aliyefika wakati upo hapo kwa rafiki yako ni mume wako utasemaje…’akasema

‘Unasema nini, kwanini unafikiria hivyo, najua wewe unawaza nini, na hata wengine watawaza hivyo hivyo ,lakini wewe hujui mimi na rafiki yangu tulikubaliana nini, na mimi nipo tayari kwa lolote lile..kwasababu ni mimi nilimshauri, ila wewe unataka kuharibu kuwa yeye labda katembea na mume wangu , hawezi kufany ahivyo abadani, atakuwa ni mwehu basi, na mimi sitakubaliana na hilo…?’ nikamuuliza kwa hamaki.

‘Ndio hapo…nawajibika kuingilia kati, ili kuwasaidia wewe na mume wako…najua kwa vyovyote vile mimi ndiye nitakuwa mtu kati…na nakuelewa sana wewe ulivyo….kuliko unavyojielewa wewe mwenyewe….ndio maana nataka kukusaidia hili. Inawezekana ulim-mshauri mwenzako kitu na yeye akakichukulia juu kwa juu, bila kuelewa lengo lako, …na akijua wewe ni rafiki unaweza kumtunzia siri kuliko mtu yoyote yule, kwahiyo …’mimi hapo nikamkatisha na kusema;

‘Mhh, sikiliza, unajua najiuliza kama alikuwa ni mume wangu kama unavyodai wewe, kuwa huenda alikuwa ni mume wangu basi kwanini,  aogope kiasi hicho,mimi namfahamu sana mume wangu..hanificho kitu akikosea, atanipigia magoti kutubu,.., na rafiki yangu alisema huyo ndiye baba wa mtoto wake, …sasa atakuwaje ni mume wangu, hebu na wewe lifikirie hilo, mume wangu ndio aje kutembea na mdogo wangu haiji akilini,…’nikasema.

‘Nimekuuliza tu, …kama ikitokea ndio hivyo, ndio yeye, bado utakubali kuwa ndiye baba wa huyo mtoto, …’akasema

‘Haiwezekani, akawa ndio yeye bwana, sitakubali kabisa,, ...mume wangu hawezi kutembea na rafiki yangu,  na rafiki yangu ambaye nimemchukulia sawa na ndugu yangu, rafiki yangu hawezi kunisaliti, hilo halina maana, na wala tusiliongelee zaidi maana linaweza kujenga dhana mbaya,,...kabisa haiwezekani...kwanini,,,.’ nakasema nikionyesha kukereka.

‘Je ikiwa na kweli, utafanya nini..?’ akaniuliza

‘Haaah, weee, tuliache hilo, sitaki hata kufikiri, ndio maana nasema sio yeye, rafiki yangu pamoja na yote ananifaham nilivyo…labda ahame nchi, ..mungu wangu, sio yeye, sio mume wangu…’nikasema nikiwa na kitu moyoni kinaniwasha.

‘Unajua nilipomuona mtoto,…na yote yanayoendelea hivi sasa nimekuwa nikiliwazia hilo, nakuelewa wewe sana,…je wewe au mume wako, itakuwaje,… na sijui, kwanini nilimshauri rafiki yako ajitahidi kuzaa kwani umri umepitiliza, nahisi alilichukulia ushauri wangu huo kwa pupa …kiukweli mimi nilimshauri hivyo na sitaki kujilaumu maana sikumshauri akatembee na waume za watu…’akasema

‘Mbona hata mimi nilimshauri hivyo…’ nikasema

‘Ndio kama ulishauri hivyo kuwa aolewe, ili azae, ulikuwa ushauri mnzuri, kiukweli, kiumri na …rika lake, alitakiwa aolewe, na mimi nilimshauri mengi tu, na hakutaka kuwa muwazi kwangu, kuwa ana mipango gani,…na labda alishanichukulia vibaya, kwasababu tulishakorofishana…kwahiyo nikajua ni lazima atakuwa kaja kwako,….’akasema

‘Ndio alikuja kwangu, nikamshauri hivyo,… mengine ni siri yangu mimi na yeye…’nikasema

‘Umeona eeh , hapo unanificha, na hapo nahisi kuna siri kubwa, ambayo inaweza kutengua hiki kitendawili…kwahiyo wewe ulimshauri hivyo kuwa ni bora azae kwanza, kwa vipi sasa, maana hilo hakutaka mimi nimuingilie, alisema atalifanyia kazi…’akasema

‘Kwahiyo kumbe wewe unanitega ili ujue niliongea nini na rafiki yangu, kuwa labda nimemshauri akatembee na mume wangu, hivi ukiwazia hivyo, unanifanya mimi ni juha au…’nikasema kwa hamaki

‘Nakuuliza hivi nikiwa na maana,  unielewe sana hapo,…mpaka nakuuliza haya nimeyatafakari sana, nakupenda, na kukujali, nawapenda wewe na mume wako, sitafurahi ndoa yenu ikija kuvunjika, ubaya unaweza kutendwa, kwa bahati mbaya, na hatujui hadi sasa ni kipi kilitendeka,..mimi kuna muda nilikuambia urafiki wako na mwenzako, ni sawa..siukatai…, lakini usifikikie kumuamini sana kihivyo.., ukasema ni kwa vile mimi eti nilimtongaza huiyo rafiki yako akanikataa…’akasema

‘Ndio hivyo..nawafahamu sana nyie wanaume mlivyo…’nikasema

‘Sasa nikuulize tena  ulimshauri vipi maana nijuavyo, yeye hakutaka kuolewa kwa sababu zake za kumtafuta mume ambaye hajazaliwa, kawakataa wanaume wengi tu, mimi mwenyewe niliwahi kumwambia kuna rafiki yangu anataka kumuoa, akamkataa, anasema haendani na yeye, na hilo ndilo lilifanya mim na yeye tukosane dio hivyo mnavyofiria nyie, kuwa nilimtongaza akanikataa,….’akasema

‘Ndio tatizo lake yeye, kuwakataa wanaume,..ndio nikamshauri hivyo, kuwa bora atafute mume azae naye....lakini hayo yameshapita , kazaa basi, haina haja ya kulijadili hilo saana…, nahisi tukilijadili hilo, tutafikia sehemu sisi wenyewe hatutaelewana, na sitaki tufikie huko…’nikasema

‘Una uhakika na hilo kweli, halikuumizi akilini kweli, na baada ya kuyaongea haya nahisi litazidi kukuumiza kichwa, je ..ni kweli kuwa  hutaki kumtambua baba wa huyo mtoto wa rafiki yako,…?’ docta akauliza

‘Nitamfahamu tu,….mimi mwenyewe, au yeye mama wa mtoto ataniambia, maana tulishakubaliana hilo, hawezi kunificha mimi rafiki yake,…’nikasema

‘Hataweza kukuambia, hilo nakumbia ukweli, kwa jinsi ninavyokufahamu wewe ulivyo, lazima atakuwa kaagopa, huenda alivyofikiria yeye awali, sivyo ulivyokuja kukusikia ukilipokea, na kiukweli,…, sasa naomba tusaidiane kwa hili, ili wewe uwe na amani, leo na baadae …’akasema

‘Kwanini unasema hivyo…?’ nikamuuliza

‘Nina uhakika kwa hali hii ilivyo, kama rafiki yako atakuja kukuambia ukweli, kitu ambacho sizani kama atakifanya …kwani nina uhakika kuwa mtakuja  kukosana na yeye kabisa…’akasema docta

‘Docta, docta….docta, najua wewe umeshajenga dhana fulani, na wewe kila mara umekuwa ukinikanya kuhusu hilo, kwanini sasa wataka kuliendekeza hilo, na kumbuka kama ndivyo hivyo, unavyodhania wewe utakuja kukosana na rafiki yako…je kama akisikia hivyo, na nina uhakika sio kweli…itakuwaje…’nikasema

‘Wewe ni rafiki yangu  hatufichani, au sio, na tumekuwa hivyo, nikiwa na tatizo nakuambia wewe hata likimuhusu mke wangu, unanishauri, na mambo yanakuwa sawa…nashukuru sana kwa hilo,…na halikadhalika mimi umekuwa  ukiniuliza maswala mengi haya yanayomuhusu mume wako…nakushauri unayamaliza…’akasema

‘Ndio hivyo nikikwama huwa nakuuliza lakini ukiona sijakuuliza ujue sijakwama, na kwa hili sijakwama..ndio maana ….’nikakatisha

‘Hapana, sema kwa vile ..unahisi wewe ulifanya makosa …sawa, ila nakuuliza tena, je una uhakika hutaki kumfahamu huyo mwanaume aliyezaa na rafiki yako…?’ akaniuliza

‘Nimeshakuambia nitamfahamu mimi mwenyewe…’nikasema

‘Sawa kama hutaki, siwezi kukulazimisha, lakini kama unataka nikusaidie hilo, nipo tayari, ila uniahidi kuwa hutalichukulia vibaya, ...nia ni muhimu umfahamu na ujue ni nini utafanya kwa masilahi ya ndoa yako na maisha yako, basi tulimalize hivyo, mana muda umekwenda…’akasema

‘Nikuulize kitu, wewe una uhakika na unachokidhania…?’ nikamuuliza

Na yeye akaangalia saa halafu akatabasamu, …simu yake ikaita, akaniangalia usoni, halafu akasema

‘Ngoja nipokee hii simu…ni rafiki yako, kanipigia…’akasema

‘Rafiki yangu…!!!’ nikajikuta nasema hivyo kwa hamaki, sijui kwanini naanza kuhamaki, labda ni kwa vile docta kajenga hizo dhana mbaya, au labda..hata sijui, nikasubiria kusikia docta anaongea nini na rafiki yangu..


WAZO LA LEO: Je ukiwa unaufahamu ukweli kuhusu rafiki yako, na unaogopa ukimwambia ukweli huyo rafiki yako inaweza kuleta mtafaruku na mkewe, utafanya nini…?’ ni swali niliulizwa, na jibu langu likawa hivi… ‘ukwel wakati wote ni silaha ya ushindi, lakini hekima yake ni ngao, inatakiwa  tuwe makini sana kwenye baadhi ya mambo, maana ukweli unaweza ukaumiza, japokuwa ni kwa muda mfupi…na uwongo, ni hatari, unaweza ukasaidia kwa muda mfupi lakini ukaja kuumiza kwa kipindi kirefu, na kuharibu kabisa…sasa ni wewe mtoaji ushauri upime mwenyewe.
Ni mimi: emu-three

No comments :