Kumbukumbu za nyuma ziliuteka ubongo wangu,…nikakumbuka yaliyotokea
huko nyuma, yaliyompata huyu msamaria mwema, tena kwa ajili yangu, akafikia
hadi kufungwa na wazazi wangu, …nikaapa kuwa siku nikikutana naye, nitajitahidi
nifanye lolote kumlipa fadhila zake, sasa nitamlipa nini, …na nilishamsahau,
nikujua hayupo tena duniani…na siku hiyo, ndio nikakutana naye, nikiwa na docta
mtoto wa watu akiwa ni mpenzi wangu…je nilifanya nini, angalia mitihani hii ya
maisha…
***********
Nakurejesha nyuma kipindi
nikiwa binti mdogo, wa miaka kumi na tano,…kipindi hicho ndio nilimuona kijana
mmoja mara kwa mara akiwa anakuja kuonana na mzee mmoja aliyekuwa mlinzi wa
nyumba yetu. Yeye kiumri alikuwa mkubwa kuliko mimi…nikaanza kuzoeana naye tu..
Kuna kipindi baba yake alikuwa akitulimia shamba, basi na yeye
anakwenda kumsaidia baba yake mimi, nikawa nafika shamabi kuchukua matunda,
nawakuta wakiwa wawili, nawapatia chochote, mwanzoni sikuwa naongea naye sana, kutokana na hali
ilivyokuwa wakati huo. Wazazi walikuwa wakali hawakupenda kabisa nizoeane naye,
au kuwa karibu naye,…
Kila huyo mvulana akija, nilimgundua akiniangalia sana, na
ikitokea tukikutanisha macho anayakwepesha kwa haraka na kujifanya kama alikuwa
haniangalii, ikawa kama mchezo fulani wa utu-rika,.. na tukajikuta tunamezoeana
kinamna hiyo, lakini sio ile ya ukaribu ya kukaa pamoja na kuongea.
Ni ikaja muda hata mimi
nikikaa nyumbani, namuwaza yeye, fikiria ni mtoto wa mkulima, mfanyakazi wetu
tunaweza kusema wa ndani…lakini mimi sikulijali hilo, nilimuona sawa na
wavulana wengine. Sio kwamba nilikuwa na tabia mbaya, ya kuwa na mazoea na
wavulana, hapana..ila nilijali sana usawa na utu, hata nikiwa msichna mdogo.
Basi kwa ile hali ya kunyanyapaliwa na wazee, kuwa wakifika
wanakuwa na sehemu yao, hawaruhusiwi kuingia ndani, sikulipenda hilo kabisa,
nikaona lazima nifanye jambo, la kuwasaidia hawa watu wawili…nilimjali sana
huyo baba yake, alikwua na tabia nzuri tu,…huruma na upendo,.
Basi…huyo kijana akifika, ninajua wapi nikae ili aweze kupita na
kuniona, kwa haraka nikakuwa na zawadi yoyote ya kumpa, chakula au matunda,…maji
ya baridi ili wakinda sahamba wapate kuyatumia yeye na baba yake..na
nilijithidi sana wazee wangu wasiweze kuona hayo…
Lakini ikatokea tukio, liloharibu kila kitu, na baada ya tukio
hilo, tukaachana na familia hiyo sisi baadaye tukahama na kuja kuishi Dar,
ambapo baba yangu alihamishia kampuni yake, na huko kijijini tukawa hatufiki
mara moja moja tu. Na sikuweza kuwaona tena. Tukio hilo kwakweli liliniumiza
sana kiasi kwamba niliwaona wazazi wangu kama ni watu wasio na utu-wema.
*************
‘Kwanini hukunitafuta, ulipoachiwa kutoka jela...?’
nikamuuliza, nikikatiza mawazo yangu ya kumbukumbu za huko kijijini….
‘Kwanini nikutafute..ulitaka niendelee kuumia, maana mimi ningelisemaje
kwako, ..hebu nijishushe hapo, baada ya tukio lile, ningelionekana na wewe
tena, si ndio ningepeleka tena jela
nikafie huko.., nakumbuka niliwahi kuandika barua kuja kwako, lakini sikuwahi
kupata majibu...’akasema.
‘Barua,…. hahaha..nani ana mipango ya barua siku hizi, ulindika hiyo
barua kuja kwangu ukampa nani..mbona sijawahi kuona barua yako yoyote,...?’nikamuuliza,
niliona kama ananitania tu.
‘Basi nahisi kuna mtu alikuwa akizipokea na kuzichana, mimi
niliandika, nyie si mna box la barua, na kuna mtu alisema anakuja huko kwenu ,
nikampa barua, lakini nikajua umeshatekwa na familia yako, na huenda hata wewe
hutaki hata kuniona tena, kwa jinsi watu walivonivumishia ubaya....’akasema akitikisa
kichwa kusikitika .
‘Kwanini usingelinipigia, angalau hata simu...?’ nikamuuliza
‘Nikupigie simu!!! Hahaha…, simu hiyo ningeliipata wapi, huko
kijijini, hivi unayafahamu maisha yetu yalivyokuwa...anyway, hayo
yameshapita na wewe una mume wako, ...naona nisikupotezee muda, ...’akasema na
kutaka kuondoka, mimi nikamshika mkono asiondoke.
‘Nimeshakuambia yule sio mume wangu, ni mchumba wangu, hatujaoana
bado…Sikiliza, ..ahadi yangu ipo pale pale…’nikasema na hapo akaniangalia kwa
macho yenye kushangaa.
‘Kwahiyo unataka kusema nini…?’ akaniuliza
‘Ahadi yangu ya kufanya lolote ilimradi niwe nimelipa fadhila
zako, najua inaweza isikidh haja, lakini angalau na mimi niwe nimfanya jambo
kwako la utu wema..sasa mimi nataka tuje tuongee tena nione nitakufanyia nini…’nikasema,
na nikaona kama ananywea, hakuridhika na maneno yangu hayo.
‘Hapana, mimi sihitajii msaada wako, sitaki kuwa mfanyakazi wenu,
au ….kuwategemea nyie tena, hapana…hilo sitaki, …’akasema
‘Najua ni kwanini unasema hivyo, ila mimi natamani zile siku
zirejee tena, kiukweli mimi sijaolewa, na sisemi hivyo kwasababu kuwa nataka
uwe ...mpenzi wangu, hapana mapenzi hayalazimishwi, na…mimi na mchumba wangu hatujafikia
huko, bado kuna mipango mimi, yeye na mimi pia, lakini mimi ninaweza kufany
ajambo la kukusaidia ukafika mahali, usilipuuzie hilo..’nikasema
‘Hilo la kukutana kuongea tena, ni wewe, kama huogopi huyo mpenzi
wako, sitaki kuja kuwaharibia mahusiano yenu, ikawa ndio sababu ya kufichua
yale yaliyopita, sipendi hilo kabisa,…’akasema
‘Kiukweli unanidai sana, mengi umenifanyia, lakini sijaweza kulipa
chochote kwako, kwangu mimi naona ni deni, na nataka uwasamehe wazazi wangu,
hata bila ya wao kufahamu, na hilo naweza kufanya nionavyo mimi, niamini tu,…usijali
kabisa kuhusu hisia za wazazi wangu, nafahamu ni kwanini wanafanya hivyo,....’nikasema
‘Hahaha, hapana , niliapa kuwa sitaajiriwa kwa watu kama
mfanyakazi wa upendeleo, mimi nataka nihangaike kivyangu…sawa nashukuru kwa
kuonana nawewe, mengine tuyaache kama
yalivyo, vipi maisha na mchumba wako, katulia siku hizi..?’ akaniuliza
‘Mchumba wangu hana matatizo, ni mzungu kwakweli, muhimu nimuambie
ukweli tu, hata akiniona tunaongea, yeye atadai nimuambie wewe ni nani, na ni
hivyo, sina shaka naye, ila hayo hayana msingi, wewe sifikiria wako langu la
kukuwezesha, unalionaje hilo…’nikasema
‘Mhh…sivyo nitakavyo, najua hutanielewa, ndio maana nasema
tuyaache tu, yabakie kama yalivyo, kwa maana mimi nilikufanyia nini kikubwa, ni
kawaida tu, na yaliyotokea hadi wazazi wako kufanya hivyo, ni…naweza kusema
hata mzazi mwingine huenda angelifanya hivyo…’akasema
‘Hapana lile tukio lilikuwa kubwa, na kiukweli nakiri wazazi wangu
walikosea, sana,..maana hawajui ulivyofanya, uliweza kuniokoa mikononi mwa
wabakaji, mijitu mikubwa, na wewe ulikuwa sio umbile lako kabisa, ukapigana na
wao kufa na kupona, hawakuliona hilo.
Kiukweli mimi..sitalisahau hilo kamwe, nilikuona kama mtu maalumu
sana kwenye maisha yangu ndio maa niliahidi siku nikikutana nawe, nitafanya
lolote lililondani ya uwezo wangu, ili na wewe uone kuwa nakujali…...’
nikamwambia.
‘Mhh…nilishaipata hiyo zawadi inatosha., wewe wasalimie wazazi
wako na mchumba wako, mungu akipenda tutakuwa tunaonana, lakini nisingelipenda
wafahamu kuwa tumekutana nafahamu watakavyojisikia, huenda ikaja dhahama kubwa
zaidi ya ile…japokuwa sasa nimekuwa mkubwa siogopi, nafahamu haki zangu...’akasema
‘Jamani ina maana hujatusamehe tu…’nikasema
‘Usijali sana ndio ubinadamu ulivyo,..nilishawasamehe mbona…kwa
hivi sasa nimeliona hilo, kuwa yale waliyoyafanya wazazi wako walikuwa na maana
kwao, kwa ajili ya kulinda heshima ya familia yenu, na walitaka kutoa fundisho
kwa jamii, na nasikia familia yenu imekuwa ikiogopewa sana,..ni sahihi,
yamepita yapite.
‘Tatizo wewe hufahamu jinsi gani niliumia...lakini ikafika mahali
nikasema basi tena, mungu ndiye atakupeni yale yote mliyotutendea wewe na baba
yako, na nikatubu sana kwa niaba ya wazazi wangu…kiukweli baba yako nilimuona
kama baba yangu mkubwa...sikupenda kumuita babu, kama walivyozoea kumuita
wengine, mimi ninajua kuzeeka kwake haraka ni kutokana na hali ya maisha, umri
wake haupo mbali na umri wa baba yangu, …mimi nilipenda kumuita baba
mkubwa.....’nikasema.
‘Nashukuru kusikia hivyo, ni wewe tu ulikuwa tofauti na wengine, sijui
kwanini wazazi wako, walikuja kutuchukia hivyo..niliona kabisa hawakupenda,
hata nikukaribie..na nahisi ilipotokea
lile tukio, ndio wakaonyesha hisia zao dhidi yangu. Ni sawa, labda nisiwalaumu
sana, maana huenda hata sisi tungelikuwa kwenye hiyo hali tungelifany ahivyo
hivyo..hata hivyo nawashukuru wazazi wako, kwani pamoja na hilo tukio lakini walitusaidia
sana kimaisha...’akasema.
‘Mimi nilikutafuta sana, lakini sikutaka wazazi wangu walifahamu
hilo, nilitaka kukulipa fadhila zako, niliahidi moyoni kuwa nikija kuonana na
nawewe, nitafanya lolote na nimekkuona
naomba usilipinge ombi langu....’nikamwambia.
‘Mimi sihitaji msaada wenu, ….’akasema
‘Hapana ni lazima nifanye wema wowote, nakumbuka kama isngelikuwa
ni wewe..sijui ingelikuwaje, na….’hapo tena ndio lile tukio likazama kwenye ubongo
wangu nikawa naliona lilivyotokea….
**********
Ilionekana wazo hao vijana watukutu, walikuwa wakinivizia siku
nyingi, na siku hiyo gari la baba lilichelewa kuja kunichukua shuleni, nikaamua
kutembea na wenzangu, na kwa vile shule ilikuwa mbali, wenzangu wakawa
wametawanyika kila mmoja na njia yake, ikafikia mahali nimebakia peke yangu, na
ghafla ndio nikavamiwa na vijana wanne, na kunibeba juu kwa juu.
Walinibeba juu kwa juu, hadi vichakani, na wakaanza kunivua nguo, na
ukumbuke nilikuwa binti mdogo tu, nasoma sekondari..nilikuwa binti, nimeshavunja
ungo, lakini sikuwa na mawazo hayo kabisa, na sikujua ni kitu gani kitakuja
kunitokea,..japokuwa nilifahamu kuwa wanatka kunifanya kitu kibaya.
Nilijitahidi kupigana lakini sikuweza kufurukuta kwa vijana hawa
wenye nguvu zaidi yangu, na kabla hawajafanya lolote mara akatokea mtu,
kijana..machozi yalishatanda usoni sikumuone vyema, akawa anapigana nao, akiwa
na kigongo hivi kama rungu, alipambana nao kiume mpaka anakuja kuwazidi nguvu,
ilikuwa ni kwa msaada wa mungu tu maana wote walikuwa wakibwa zaidi yake…ikafikia
muda, ikabidi wakimbie, baada ya kusikia kelele za watu, wakikaribia eneo
hilo..na yule kijana akapiga ukelele kuomba msaada. Wale vijana wakakimbia huku
wakilaani kuwa watahakikisha wananifanyia hivyo, siku yake...
Sikuweza kuongea nililia hadi nyumbani, nikiwa nimechafuka, nguo
zimechanwa, nnipo kama nudu uchi…na huyo kijana alinsiindikiza hadi nyumbani,
nikawahadithia wazazi wangu, na wao kwa haraka wakaifahamisha polisi na hawo
vijana wakaanza kutafutwa lakini hawakupatikana kwa siku hiyo hata ya pili yake.
Walihama kabisa, kijini hapo.
Cha ajabu wazazi wakaongea na polisi wakaja kumshikilia huyo
kijana kuwa atakuwa anawafahamu hawo watu, na alitakiwa kuwataja, na
aliposhindwa kuwataja, wakamshitakia kuwa ni muhusika wa tukio hilo, ..wanasema
walivyomuhoji, alivyojieleza inaonekana kama analifahamu hilo tukio na yeye
alikuwa mwenza wao, japokuwa alikana kabisa.
Baadae akafunguliwa mashitaka, na yote hayo wakati yanaendelea
mimi nilikuwa sifahamu kinachoendelea kwani ilibidi niondoke hapo kijijini kwa
usalama wangu, kwa vile walitishia kuwa ni lazima watanifanyia tena..ikabidi
baadae wazazi wangu wanihamishe kabisa kwenda kusomea sehemu nyingine.
Nilikuja kusikia kuwa kijana
huyo kafungwa, na nilikuja kufahamu hilo baada ya muda, mtu alishahukumiwa
kufungwa..kwani vijana wale waliofanya hivyo hawakuweza kupatika,ila mmoja wao
alipatikana na alipofika mahakamani, akadai kuwa kijana huo alikuwa mmoja wa
wenzao, walipanga wote, kulifanikisha hilo, nay eye ndiye alitoa maelekezo
jinsi gani wanaweza kumpata huyo bint.
Baba wa huyo kijana akawa anafika mara kwa mara kwa wazazi wangu
kuomba kijana wake asamehewe, lakini haikusaidia kitu, na alichoambulia ni kufukuzwa
kazi...hayo yote nilikuja kuyafahamu baadaye, na nilipolifahamu hilo
nikawaambia wazazi wangu kama hawatamuachia huyo kijana aliyeniokoa basi mimi nitajiua...
Hilo nilidhamiria kweli…
Wazazi wangu awali walifikiri natania, wakaja kunifuma nataka
kunywa sumu, na walipoona hivyo, ndio
baadaye wakaenda kuongea na polisi na baadae mahakama, kuwa kijana huyo
aachiwe, wao wameshamsamehe..ili ifanyike maongezi, wanayojua wao wenyewe na
ndio kijana huyo akaachiwa, hata alipoachiwa sikuweza kuonana naye tena wala
baba yake, kumbe waliamua kuhama kabisa hapo kijijini, na baadae hata wazazi
wangu wakahamia Dar, ndio ikawa mwisho wa kuonana na huyo jamaa hadi hii leo
ndio nakutana naye…
***********.
‘Kwakweli sitaweza kusahau wema wako huo, uliniokoa kwenye janga,
huenda ningelikufa, …’nilimuambia siku tulipokutana naye tena.
‘Ile ni kawaida tu, mtu yoyote muadilifu angelifanya hivyo hivyo,
na haina haja, kulipwa kwa kitendo kama kile, na sizani kama kuna kitu unaweza
kunilipa kikazidi yale ya moyoni kwangu...’akasema na kuinama chini.
‘Una maana gani,ya moyoni mwako, yapi hayo..… ?’ nikamuuliza.
‘Mimi niliahidi siku ile ulipoleta chai na mkate, nilikuambia mimi
nitakuja kukuoa, wewe uliona kama utani, nilimuambia hata baba, alinicheka
sana,..nakumbuka hata wewe ukasema mungu akipenda,..ukimaanisha kuwa umekubali
au sio…’akasema
‘Lakini yale yalikuwa ya ujanani, na niliongea vile kama maongezi
tu, ulitaka mimi niseme nini pale, na ni mambo ya ujanani, hayana maana au sio…’nikasema
‘Hayana maana, ndio unasema hivyo, kwangu yalikuwa na maana sana,
mimi nilikupenda na …samahani, nikisema hivyo, kuwa siku zote nimekuwa
nikikupenda, na kutamani uwe mke wangu, usichukie, ila naelezea hisia zangu,
najua ni ndoto za Alinacha, lakini ndio ukweli kutoka moyoni mwangu…’akasema
‘Aaah, hapana,…sawa nashukuru kwa kusikia hivyo, na…hata sijui
niseme nini, naogopa, nitakuja kuuumiza , naomba unipe muda..’nikasema
‘Hapana nafahamu, huna haja ya kusema lolote, haiwezekani, mtu
kama mimi kukuoa wewe, najua, ila sijui …’akasema
‘Kwanini unasema hivyo…utampata msichana mwingine kwani mimi ni
msichana peke yake hapa duniani..’nikasema
‘Sijaona kama wewe, na wewe ndiye uliyeuteka moyo wangu, kama sio
wewe basi, mimi naomba mungu nisioe tena, na nitaishi hivi hivi maisha yangu
yote…sitaki shida…’akasema sasa akisimama kuondoka. Hapo nilibakia nikiwaza,
sikujua kabisa mwenzangu kadhamiria hilo, na..kiukweli moyoni sikupenda kuja
kumuudhi mtu kama huyu, ambaye naona kama ananidai …
Moyo wa huruma uliniingia,
nikikumbuka yeye ndiye aliniokoa, vinginevyo sijui ingelikuwaje, na zaidi ya
hayo, ananijali sana, kiukweli docta nampenda, na kwa vile pia yupo kwenye
hadhi inayoendana na …tusema hivyo..lakini huyo nimetokea kumjali, na labda
kuna upendo lakini sio kwa vile…sasa nifanyeje..ilinipa wakati mgumu sana,
nikijua kuna wazazi wangu, ambao hawatalisikiliza hilo kabisa
Basi siku hiyo akaondoka, na hatukuweza kukutana kwani nikifika
naambiwa katoka, nikimpigia simu hapokei.
************
Baada kama ya mwezi hivi
tukaja kukutana tena, tukaongea mengine , hakupenda kuliongelea hilo tena,
nikajua keshakubali ukweli, kwahiyo hilo halipo tena, na huku kwa docta, naye
kaanza kunisakama, anataka tuanze michakato ya ndoa..
‘Niambia, lile wazo langu vipi…?’ siku moja akaniuliza sikutarajia
hilo swali.
‘Unajua, wewe unachukulia ndoa kama ni kitu rahisi hivyo, ujue
mimi nina wazazi, na ndoa inakutanisha familia mbili, wakiwemo wazazi, sasa
hebu jiulize, wazazi wangu wataliridhai hili,...je wewe umejiandaaje kuishi na
mke, maana usije ukasema unanioa, kwa vile…’nikasema
‘Mimi nimeshajiandaa kwa hilo, sio kwamba nakuambia kwa vile…ninachumba
na varanda nimepanga, nina kiwanja kijijini, urithi wa baba, nitauza seehmu
nitajenga nyumba,…tutaweza kuishi tu..lakini sikulazimishi, maana kiukweli
hutaweza kuishi maisha y akitajiri kihivyo...’ akasema.
Baada ya maongezi hayo, nikawaza sana, nikajiuliza sana, nifanye
nini…maana sikuwa nimelichukulia kwa maana hiyo tokea awali,…nikaanza kujenga
hisia za kumpenda tu…na huku kwa docta nikawa naharibu, ikawa siivani naye kwa
kila anachokifanya.
‘Vipi kwani kumetokea nini, nakuona umebadilika sana siku hizi,
kama kuna tatizo lolote niambie mimi nitakuelewa tu mpenzi, sitaki kabisa, kukulazimisha
kwa lolote lile, umenielewa, sitaki nikuoe ukiwa hunitaki, unasikia, unieleze
mapema…?’ akaniambia
‘Hakuna tatizo lolote!....’nikawa
namwambia hivyo maana bado nilikuwa sijaamua moja kwa moja, nikijua kuwa wazazi
wangu hawataweza kunikubalia kumuoa huyo
Nikawa sasa najenga ukaribu sana na huyo jamaa hadi docta akaja
kugundua mwenyewe, na aliponiuliza nikamwambia ni rafiki yangu nakutana naye tu
na hawezi kunizuia
‘Nimeshakuambia uwe muwazi kwangu, kama hupo na mimi , sawa,
mapenzi hayalazimishwi, lakini nataka uwe muwazi, unanielewa, sitaki kupoteza
muda wangu na mtu asiye na matarajia na mimi..’akasema
‘Sawa si unataka jibu, sipo na wewe,… nataka kufikiria zaidi, kama
una haraka kuoa katafute mwingine....’nikamwambia hivyo, kiukweli ilimuumiza
sana, na akavumilia kwa kipindi fulani, baadae akalifikisha kwa wazazi kuona
kama wataweza kusaidia
Wazazi wangu waliposikia hivyo, hawakuamini…wakaamua kufanya uchunguzi
ni nani kanighilibu, na baadae wakaja kugundua kuwa ni nani huyo ninayekutana
naye mara kwa mara, na kipindi hicho nimeshamsaidia huyo jamaa hadi akapata
kazi kwenye kampuni kubwa, na akaweza hata kujenga nyumba yake mwenyewe…nilitaka
nifanye hivyo baadae…kama atampata mtu mwingine basi.
Lakini kumbe mwenzangu anajua kuwa nayafanya hayo kwa ajili ya
maisha yetu ya baadae, kukapita kipindi kirefu hapo,…sio jambo la miezi, hapana
ilichukua karibu miaka miwili hadi docta akakata tamaa na mimi....
.
Siku moja wazazi wangu wakanikalisha kikao, walikuwa
wamekasirika kweli kweli..
‘Hivi wewe una akili kweli,..hivi wewe hujaona mwanaume, hadi
umchague huyo mtu,..kama kweli nia yako ni kupata mwanaume mwingine zaidi ya
docta, huyo hakufai, yule ni mlalahoi, mtoto wa mlinzi wetu...bwana shamba,
asiye fanana kabisa na hadhi yako, mbona unataka kutuaibisha....kwanini
unamkataa docta, msomi , familia yao ni ya kiheshima, matajiri.....’akasema
baba.
‘Baba mimi sio mtoto mdogo, na sina lengo la kuwaabisha,
mnakumbuka nilitaka kubakwa nikiwa kule kijijini, niliwaambia ni nani
aliyeniokoa, ....mlifanya nini kwa huyo aliyeniokoa, ..badala yake mlikimbilia
kumshika yeye ati alikuwa anawafahamu hawo watu waliotaka kunibaka, mkamfunga
hata bila ya mimi kujua, kwa vile tu ni mtoto wa masikini..iliniuma sana na
niliahidi kuwa ipo siku nikipata nafasi nitamsadia ili kulipa fadhila zangu
kwake, na kutubu madhambi mliyoyafanya...’nikasema.
‘Kwahiyo malipo yake ndio hayo, kutudhalilisha sisi au sio...sikiliza,
kama sisi ni wazazi wako, tunasema achana na huyo mtu, sisi ni wazazi wako tulijua
ni nini tulichokifanya, wewe hukuona kilichotokea, baada ya kumshika yeye na
kumfunga, kijiji pale tuliogopewa sana…, hakuna hata mtu aliyewahi kuichezea
familia yetu tena....sisi tulifahamu ni nini tulichokifanya, kutoa fundisho kwa
wengine....’akasema baba
‘Mtoe fundisho kwa mtu asiye na hatia,...kunikoa kwake ndio
imekuwa taabu, kama asingelifanya hivyo nikabakwa, huenda ningelifikia kupoteza
maisha au kuambukizwa magonjwa, mngelisemaje, ndio fadhila zeni hizo, wema wao ndio malipo yake hayo,hapana
mlifanyavibaya sana…’ nikasema
‘Je na sisi tusingelifanya hilo, ikatokea tena, maana walidhamiria
kweli kulifanya tena kukukomesha , na wale waliotoroka, walikamatwa wakiwa na
mipango hiyo …walitaka hata kuja kuchoma nyumba na maeneo yetu..hujui kabisa
yaliyokuwa yamepangwa …’akasema
‘Wazazi wangu hamuwezi kujua ubaya huo unaweza ukawageukia nyie
wenyewe siku moja, …au ubaya huo uje utendwe kwa watoto wenu, ili iwe fundisho,
...hamjui kibao kinaweza kuwageukia nyie siku moja kwa tatizo jingine,
hujafa hujaumbika...msijione kuwa nyie ni matajiri hamtaweza kupata shida, mung
anaweza kuibadili hali bila kujua, kisa ni haya mnayoyaona ni madogo tu...’nikasema
kwa sauti ya huzuni na mama akanionea huruma na kuniuliza
‘Kwahiyo ewe ulikuwa unatakaje, tukae kimiya tu, wakati wahuni
walishaanza kuiingilia familia yetu, tulifanya vile kwa ajili ya kuilinda
famila yetu, na tulipofanya hivyo ilisaidia. Na baadaye tulimtoa, na tukampa
pesa za pole,...japokuwa mzazi wake alizikataa lakini baadaye akazichukua hali
ilipozidi kuwa mbaya....ile ni kawaida kwa mzazi yoyote anayetaka kulinda
familia yake...’akasema mama.
‘Mimi sitawaelewa kamwe, na mimi najua nafanya nini, itafikia
mahali, nikiona kampata mtu wake, basi..lakini kwa hivi sasa sitaki kuolewa na
docta…’nikasema,
‘Sasa unataka nini, maana huyo kijana keshasema anataka
kukuoa,..lakini sisi kamwe hatutakubaliana na ndoa hiyo,…’wakasema
‘Baba mimi naona hatutafika popote kwa hili, ila nawaomba, ..kwa
vile mimi ndiye niliyefanyiwa hilo, na namfahamu ni nani aliyenifanyia wema kwa
kuniokoa, mniache tu, najua ni nini ninachokifanya, maana kwangu, alilonifanyia
ni deni kubwa sana,..na.niliahidi kuwa nitamlipa fadhila zake, ....’nikasema.
‘Kwahiyo unataka kumlipa fadhila gani...?’ akauliza mama.
‘Hilo niachieni mwenyewe....sijaja kuwaomba chochote kwenu kwa
ajili yake....’nikasema.
‘Achana na huyo mtu, kama unataka kumuona akiendelea na maisha
yake, achana naye, na kama unataka akaishie jela, endelea naye....hatuwezi
kukuona ukituzalilisha ....atapotea kama alivyopotea baba yake....’akasema
baba.
‘Ina maana mnafahamu kuwa baba yake alifariki,,...?’ nikauliza kwa
mshangao.
‘Tumeshakuambia achana na hiyo familia, vinginevyo utajua kwanini
hukutusikiliza....’akasema baba, na mimi moyoni nikasema
‘Kama ni hivyo basi, nitakubali anioe, ili kuondoa kabisa hiyo
dhana ya madaraja..najua wazazi wangu wamekosea, na hawataki kutubu, basi mimi
nitatubu kwa niaba yao,na njia pekee ni kukubali kuolewa na huyu mtu basi…’nikapanga
hivyo…
NB: Kisa ndani ya kisa….ndivyo kisa hiki kilikuwa …kama nawachosha
mniambie..
WAZO LA LEO: Utofauti
wetu wa hali za kiuchumi usiwe ni tija ya kutokujali utu wa mtu, utu wa mtu
haununuliwi kwa pesa au mali, utajiri wako usiwe tiketi ya kudharau wengine, na
kuwaoana hawana thamani, ukifanya hivyo,hutakuwa na amani katika maisha yako,
kwani kilio cha hawo unaowatendea hivyo kitakuandama.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment