Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, March 30, 2012

Hujafa hujaumbika-14




 Ukiwa huna kazi...na ulikuwa umezoea kazi, asubuhi upo ofisini na mwisho wa mwezi unakinga, ni taabu kweli kweli. Ikabidi nijifiche fiche, na wakati mwingine naamua kutembea sana, kwenye maofis hadi jioni, narudi wafanyaakzi wakitoka...lakini nikaanza kuishiwa nauli hakuna, ikabidi kiguu na njia, viatu viakisha soli....ikabidi ninunue ndala....

Mwanzoni tulikubaliana vyema na kimwana, kuwa tuwe tunatoka asubuhi, kila mtu akahangaike kivywake, na jioni tunakutana tuoena tumeppata nini, hakuna kufuatana, ilimradi tunakutane jioni kila mtu anaonyesha kile alichojaliwa nacho, mimi sina kazi, sina biashara nitapata nini....ikawa kila siku anayeleta kitu nyumbani ni mke wangu kimwana....anapatia wapi sijui, ilimradi tunakula...

‘Sasa mimi ni mume, maana nakulisha wewe, huji na lolote, hata angalau tunda, kila ukija unanuka jasho tu...’akaanza kunisamanga.

‘Sasa ndio unanisamanga, nimejitahidi kila ofisi ninayoijua sijapata kazi, na biashara mitaani haitoki, kila mtu ana biashara hata wale wenye kazi wameanzisha biashara, sasa sisi tusio nakazi tutafanya nini...yaani hapa nimechananganyikiwa mke wangu, nahisi dunia imenilemea...sijui ni balaa gani...’nikasema huku nikiwaza mengi.

‘Sikiliza, huwezi kupata kazi kwa mtaji huo, ili upate kazi inabidi ufanye kazi, mimi kama ningelitaka kuajiriwa ningelishaajiriwa muda mrefu tu, lakini sitaki kazi za ofisini tena, siku nilipoachishwa kazi na yule meneja aliyenitaka.... nikamtolea nje, nikasema basi , kama kazi ni lazima ujitoe mwili wako, bora nikaifanyie huko mitaani, huko nje,...sio huku ofisini... nitapata maslahi zaidi lakinii sio kwa yule meneja,..mtu mwenyewe mzee halafu, sura mbaya...’akasema huku anacheka.

‘Eti sura mbaya, hivi hawo wanaojiuza huko mitaani wanaangalia sura....si maslahi tu,.....lakini hata hivyo ukiongea hivyo uanataka kusemaje,....., ujue mimi ni mwanaume, kama lengo lako ndio hilo,....sijakuelewa hapo, maana hata kama pia ni pesa, sina pesa kama ni kuhonga au sijui kujiweka vipi....sasa nifanyeje..?’ nikamuuliza.

‘Dunia hii usipokuwa mjanja utalala na njaa, cha muhumi ...nikupe maarafa...eehe,... nyumba, ukiwa na nyumba, halafu una hati miliki, .... ukatumia akili yako vyema, hulali njaa, hata siku moja...tatizo lako hutakii kutumi akili yako vyema, nikuambie kitu...hii hapa ni nyumba yako, una hati una kila kitu...kwanini huiweki bondiukapata mkopo benki...?’ akaniuliza.

‘Nyumba....ungelijua...’ nikatulia na kuwaza, kwani alikuwa hajajua kuwa nyumba hiyo ipo tayari kupigwa mnada, nilikuwa nimemfica kabisa, nikasema;

‘Lakini hata hivyo mkopo una masharti yake, unaweza ukauchukua ukaishia kunywewa tu sasa mimi sitaki kurejea huko, nakunywa, lakini sitaki niwe mlevi tena....’nikasem ahuku nikiwa sina raha, maana aliponigusia nyumba, nikakumbuka kuwa wale wapiga mnada wa nyumba za wadaiwa sugu wamenipa miezi mitatu tu, niwe nimelipa deni la watu....miezi mitatu tu...nikawaza....na hiyo inaishia.

‘Sasa unasemaje.....?’ akaniuliza kimwana.

‘Miezi mitatu ..nimepewa...’ nikajikuta nikisema.

‘Miezi mitatu tu, yaani uchukue mkopo uurudishe kwa miezi mitatu tu, sio mbaya nenda kachukue mimi nitakuonyesha jinsi gani ya kuuzungusha, nakuambia ukweli, ukiwa na akili,utakuwa tajiri...’akasema huku anaiagalia nyumba kwenye paa, akizungusha kichwa hku na kule .

‘Hivi nikuulize na wewe kule ulipokuwa umepanga niliona vifaa vingi vya thamani, umemuachia nani hivyo vifaa..?’ nikamuuliza, na swali hiloo likamshitua kidogo  na mara ghafla akainuka na kuchukua mkoba wake.

‘Swali zuri sana lakinii sasa nina miadi na bosi mmoja...., huyo najua atatupa hela ya kutusukuma hadi mwisho wa mwezi na akizubaa, ataingia choo cha kike, wewe tulia, ngoja mwanaume nikhangaike, unajua mimi watu wanafikiri ni Malaya, hapana mimi ni mjanja,... mwili huu unakuwa kivutio tu, lakini mwisho wa siku inakuwa akili kichwani mwangu, ni kama kutamani ndizi, ...lakini kuila huili kamwe, wanakula wengine   ndivyo ninavyowafanyia hawa wakubwa...’akasema.

‘Eti nini mbona sikuelewi, wewe umeniambia kuwa una dili zako za kibiashara, hukuwahi kuniambia kuwa unauza mwili...au sikukusikia vyema...huko kwa huyo bosi unakwenda kufanya nini..?’ nikamuuliza kwa hamaki.

‘Nimeshakuambia, akili zitumie vyema, unafikiri hata hawo wanaofanya kazi maofisini pesa zinawatosha, haziwatoshi, lakini utashangaa wanaojenga majumba mazuri  kwa sasa wengi kwasasa ni wanawake....na wengine hawana waume, ni nini wanatumia, nia akili...mwili huu ni kitega uchumi tu...lakini hauuzwi...kama mtu akitaka kuona ndani atakuwa an ujasiri wa hali ya juu sana kama wewe...hakuna mwingine...' akanisogelea na kunikumbatia akilala kifuani kwangu.

'Sasa tutaliongea hilo baadaye, wewe nenda kauchngamkie huo mkopo, chukua hati ya nyumba, kaongee na mameneja kweney benki..mkopo upo nje nje....’akasema huku akijirmba mdomoni.

Maneno ya mke huyu yalianza kunitia wasiwasi, inawezekana kweli ni changudoa,na mimi ananitumia tu, lazimanimchunguze, haiwezekani, kwanza alishaniambia nikimuoa atajituliza na kuwa mke mwema, sasa kila siku anaaga kuondoka, ...lakini hata hivyo asipoondoka, tutakula nini....nikajiuliza bila jibu...wazo likanijia kama mke wangu huyo kule alikuwa na vitu vya thamani na sisi hatuna kazi, kwanini tusiviuze baadhi ili tupate pesa.

Kwangu nilishauza karibu kila kitu na gari ambalo tunalifanya kama taksi bubu, nimeliweka rahani, ina maana ikipita muda wa deni gari, sio langu tena, nyumba sio yangu tena, nitabakiwa na nini...Nilipofika hapo nakatoka na kuingia mitaani. Mkaa bure sio sawa na mtemeba bure, tembea tu hata huna kazi huenda ukaokota,...

*********

Nikafika mitaa ambayo kimwana alikuwa akiishi, nilioana nifike hapo kutizama vifaa vyake, na kujua nani anaishii hapo kwasasa, maana vile vifaa mle ndani vilikuwa vy athamani, sizani kwamba aliviuza vyote kabla ya kuja kwangu, ...

Nilipofika pale, nikakumbuka jinsi nilivyoibiwa gari langu , nikajikagua mfukono, maana hapa pakumbusha mengi, halafu nikagonga mlango...kwa mbali nikasiki kama mtu anaongea, au wanaongea an sauti ya runinga,...nikajua kuna mtu anaisha hapo kwasasa, isije ikawa ni mshikaji wa mke wangu wa siri, leo nitapambana naye...

‘Halloh, mpenzi, karibu, unahitaji huduma....au sio,halafu umependeza kweli, na hapa ukitoka, jasho lote litakuwa limekauka, kuna maji safi ya kuoga, ni mpango wako tu...’sauti nyororo ya kimwana ilifanya masikio yangu yaingiwe kiwi, na jinsi alivyovaa, ni heri tu angeacha kuvaa, gauni ipo karibu kuonyesha chupi...

‘Huduma....namulizia ...mmmh, hapa alikuwa akiishi kimwana,au sio..?’ nikajikuta nikigwaya.

‘Swali kabla ya jibu,nimekuuliza kwanza unahitaji huduma, maana muda nii mali, anaweza akaja mtu mwingine,akazania unahitaji huduma, akaondoka, ukanikosesha bahati...kama unahitaji huduma,karibu ndani, lakini, kila kitu ...’akaonyeshea vidole kwa ishara , ambayo inamaanisha pesa....

Nikabakia bado nimeduwaa, nikaangali mlango kwa juu kuwa huenda kumebadilishwa na kuwa sehemu ya huduma fulani, lakini mimi sikuwahi kupitahapo karibuni, nilipoona hakuna maandishi yoyote nikamtizama yule kimwana, akajirembua....

‘Mhh, wanionaje, .....kwani una ngapi wewe....maana nisje nikaitupa bahati....wewe sema una ngapi, ulicho nacho kinaweza kikakusaidia hata chapu chapu....ongea wewe mwanaume usiwe kama demu bwana, kasema na kunsihika sehemu za siri...nikaruka kwa nyuma..

‘Vipi wewe...unataka kunifanya nini, nimekuja hapa nikiwa na maana ya kuangalia vifaa vya mke wangu, Kimwana, alikuwa akiishi hapa kabla, wewe unaleta mzaha,...unafikiri wanaume wote ni wakutaniwa,mimi nina mke wa maana, sio kama ....kwanza wewe ni nani kwake...’ nikauliza kwa hasira.

‘Mimi ni Kimwana pia,...ukipenda niite Kisura....nani mwingine kimwana zaidi yangu...sikio wewe lofa, kama huna kitu ishia na usije tena hapa kunipotezea muda wangu...mijanaume mingine bwana utafikiri waume kweli, kumbe milofa...haya ishiia usije ukanifukizia kibosile wangu yupo njiani anakuja...hata hivyo umeshanitilia nuksi za mapema,watu kama nyie mkifika hapa wa kwanza mnaharibu siku nzima....aah...’akaubamiza mlango kwa nguvu na mimi nikageuka na kurudi barabarani.

‘Vipi ulikuwa unapata huduma nini..?’ mara nikasikia jamaa akiniuliza nyuma yangu, name bila kugeuka kumwangalia nikasema;

‘Huduma....kuna huduma hapo, ni kuchanganyana tu, kwanza huduma gani hiyo unayozungumzia, maana hata yule binti pale kaniuliza nataka huduma...kwani pale kuna huduma gani?’ nikageuka na kuangaliana na huyo jamaa, alikuwa kabeba nguo za mkononi, ni mmachinga.

‘Wewe unauliza kuwa kuna mate mdomoni...au wewe wakuja nini, ..maana watu kamanyie ndio mnalizwagwa....pale kuna huduma maalumu, huwa wanakuja machangu wenye nazo, wanakodi kwa masaa, wiki na wengine hata kwa mwezi,....kwa ajili ya kutoa huduma....hahaha, ulikuwa hujui wakuja eehe..’akaziweka nguo zake vyema na kuniangalia kwa hamu.

‘Mimi sio wakuja bwana....wewe unafikiri utajua huduma zote hapa Dar, huna kazi nini, iwe kazi ya kujua kila kitu kinachofanyika hapa Dar....’ nikajitetea.

‘Nimeshakujua, hujuii huduma hiyo ni kitu gani, ...ukija mwanaume na vihela vyako, unahudumiwa pale, hakuna longo longo, hakuna eeh, nakupenda sana, hapana, hapeendwi mtu, inapendwa pochi yako...ukizubaa, unachukuliwa jumla jumla, na mwisho wa siku tunakukuta mitaani ukiokota makopo...kuna laana pale....’akasema huyo jamaa akaelekeza macho yake kwenye ile nyumba.

‘Mhh, siamini...kipindi fulani alikuwepo msichana mmoja anaitwa Kimwana, ....sasa kaolewa, alisema kapanga hapo, na...’nikaanza kuongea.

‘Hahaha...sasa kaolewa, maajabu,huyo kampata lofa, ...kaolewa, wanaolewaga hawo ....mmh, visura...sijui labda...maanake huwezi jua ya mungu mengi.....’akaguna na kuziweka nguo zake vyema, na akawa kama anawaza huku akingalia pale kwenye jingo, akasema;

‘Pale majina yao ndio hayo visura,vimwana, mrembo..., ukifika pale wote wanajiita majina hayo, ila leo yupo huyu,kesho yule.....lakini hayo yote ni majina ya bandia,....kweli ni warembo wamejichubua utafikiri wazungu....na wapo wana urembo wa asili, wazuri huwezi amini, ...lakini kama wesamavyo wehenga, sio vyote ving’aavyo ni dhahabu, chunga sana, utalizwa....’akasema jamaa yangu akizichambua nguo zake kama vile ananionyesha ipi bora nichague.

‘Unajua wengi ni mabinti waliotoka hukoooo,makwao, labda wameshindikana, labda,....hatujui, tusema hatujui , ....wakifika hapa bongo....wanachofanyalabda kwa kuelekezwa, au kwa kunaswa na maisha au kwa kupitia mawakala, wanaingia kwenye shule ya huyu mwenye haya majumba, wanafundwa kisawasawa,...unajua kufundwa wewe, hkokwenu mnaitaje, unyago, au...?’ akaniuliza akiniangalia kwa makini.

‘Sijui nini unachoongea....’nikasema huku nikiiangalia ile nyumba, na huku nikimuwaza kimwana wangu, maana siamini,...ina maana hata yule binti mrembo anafanya ....hapana kwanini...siamini...

‘Siamini....’nikajikuta nikisema.

‘Huamini nini hapo.....wale wapo kazini, ...sasa sijui tafsiri sahihi ya kazi ni ipi, maana unaonekana msomi kidogo...hebu niambia wale wanasema wapo kazini, maana mwisho wa siku wanapata mshiko wao, kwa vipi, ....hebu kwanza nikupe jinsi inavyokuwa kwa hawo vimwana, ...kamahuyo kimwana wako, .....’akaweka nguo zake vizuri na kuiangalia machoni.

‘Wakikutana na huyo mwanamama, wenyewe wanamuita Docta....sio Docta wa hivi hivi, ....kaisoema hiyo fani na ana mashahadanamadigrii,sijui na maprofesa....anamjua bindamu, anaijua hisia ya binadamu, anajua tabi na maumbile ya bindamu, kivitendo, kihisia, ...’akasema huku akifikiria neno jingine la kuongezea hapo, na mimi nikaingiwa na hamasa ya kutaka kujua..

‘Kwahiyo ni mwalimu,...akiwapata hawo mabinti, kwanza sifa ya kwanza ili uwe mwanafunzi, ...uwe mrembo, na kamahujakamilika,unatengenezwa....huwezi kumjua akishatengenezwa, hutaamini,...halafu anaanza kufundwa....nyie kule mnaita unyago, lakini tofauti yake, ni kuwa unyagoo huo sio wa amlengo ya kuishi na mume na mke.....unanielewa hapo...’akaniangalia kwa makini, lakini mimi sikumjibu nilikaa kimiya.

‘Anafundishwa  jisni ya gani ya kumpagawisha mwanaume, ...na siri za uzaifu wa wanaume...unafikiri wanaume tuna kitu sisi,....kitu kidogo, eeh, ooh, wewe ni kila kitu, chukua zote, unatoa mihela yako yote...ni kushindwa tu kwa wanawake kutujulia, wangelikuwa wanaijua hiyo siri, mwanamke angekuwa anatamba katika hii dunia....’akaanza kunifunua ubongo huyu jamaa anayeonekana kuijua sana sehemu hiyo.

‘Ina maana....kumbe, wana.....lakini inakuwaje mpaka mwanaume asijijue, ..kwaninii sisi ni wajinga, hapana, lazima kuna dawa wanatumia kumpagawisha mwanaume.....?’ nikauliza.

‘Hakuna dawa kabisa...ni hayo manjonjo tu...ndio maana nakuambia kuwa wanawake wetu wangetujulia, kusingekuwa na hiyo wanayoiita mfumo dume....wana silaha kubwa mungu kawajalia,lakini hawataki kujifunza, wakishaolewa basi, wanajua wamefika,...kazi yao kupika, kufagia..umbea..huku wenzao wanawasoma...na wanaweza wakaja kwako kama rafiki,....nikupe hiyo mapema..’akasemana kuniangalia kwa makini.

‘Akikutana na mkeo,  anamdadisi, na udadisi huo unalenga maswala nyeti....kuanzia ofisini, hadi chumbani...kuna mambo wameshafundishwa, wayajue, wakishayajua,kazi ni ndogo kwao, wanakukokota kama mbwa anavyojipeleka kwa chatu,.....mwisho wa siku unasema dawa, dawa...hakuna daa hapo, ni akili....usicheze na binadamu, nakuambia, binadamu nikiumbe wa ajabu kabisa....’akajionyeshea kwa kidole kichwani mwake.

‘Wenzenu kila kukicha wapo kwenye maabara, sio lazima maabara ya madawa, ya kutafiti ugonjwa, lakini pia kuna maabara ya kumtafiti binadamu, na hidia , hulka na nyendo zake....wanakuchambua juu chini, ...akikuangalia hivi tu, keshakujua udhaifu wako...mwishowe unasema ooh, mazingaumbwe, oooh, wachawi..ooh, dawa, ooh, limbwata..hakuna, ni akili kidogo tu...’akasema na kuchuchumaa .

‘Sasa huyo mama anapaat faida gani....sio kwamba anachumamazambi tu...’nikasema

‘Ndugu yangu wee, matajiri, na utajiri, unanuka zambi...pesa ndio ibilisi wetu mkubwa, pesa imewafanya wengi wakasaliti, na hata vitabu vikubwa vimeandika, ila sitaki kwenda huko....ukisema nikifanya hiki nitapaat zambi, ni wewe na imani yako....mwenzako hamjui wala kuamini hayo....dini yake ya mali, ...mungu wake ni pesa...eti zambi..shauri lako, kaa na imaniyako hivyo hivyo...’akainuka kama anataka kuondoka, lakini hakuondoka.

‘Kuhusu huyo mama anapata faida gani, ....ni mfanyabishara, ala leseni na analipa kodi, kwa kukodisha majengo yake....mengina nini kinafanyika, yeye hajui....akili kichwani mwako, ...kitu anachofanya ili kufanikiwa zaidi ni hivyo kuwa anawafundisha hawo mabinti,kwa nakubaliano ya siri....mwisho wa siku atakata hela yake sijui, au ndio anajua kuwa ataipata kwenye kodi.....’akatulia kama anawaza.

‘Sasa huyo mama mwenye mijumba, kasoma, na kumjulia mwanaume, yeye sasa anatumia huo ujuzi kujiingizia hela, yeye kakaa kwenye kiti chake tu , na hata watu wa kodi wakija, anasema anafnya biashara ya nyumba, kukodi nyumba, ...unaweza ukaita nyumba za wageni, lakini kinaman iliyojificha......kodi zinaingia.....wanalipa hela nyingi sana kukodisha hapo....mama anatajirika,docta anaheshima zake...kwenye ngazi za juu, ana sifa ya mtetezi wa akina nani.....utajaza mwenyewe....’akaniambia huyo jamaaa.

‘Wewe sasa umejuaje hayo...?’ nikamuuliza.

‘Mimi nimejuaje hayo,... kwasababu mimi ni mtoto wa mjini, nimesoma ahdi chuo kikuu, lakini sio cha kukaa darasani,..akili iliyopo hapa ingelikuwa Ulaya au Marekani ningeliitwa docta....naujua kuutumia mdomo, najua mengi, nasikia mengi na nawajua watu...wenzako wanaonijua wananitumia,naitwa mtaalamu wa kujua mengi..mwanzoni nilikuwa wakala wa huyo mama...baadaye nikaona ni ushetani....nikajitoa....’akaniangalia kwa makini halafu akacheka.

‘Unajua nimekungali na kukupima kwa makini..nimegundua kitu, na wewe umelizwa, nina uhakika huo, semausaidiwe...maana unavyodadisi naona kabisa umeshaingia mkenge, na ukinaswa ni kama ulimbo wa kumtegea ndege.. ukinaswa hunasuki, umenaswa....?’akaniuliza akiniangalia usoni kwa mshaka.

‘Hpana, ila huyo dada niliyekutajia, namfahamu sana,....huyo ninayemzungumzia, nilimfahamu kwa jina hilo la kimwana nilifika hapo kwake na akaniambia amepanga hapo siku nyingi,...nilimshangaa maana sizani kama alikuwa na uwezo wakununua vifaa vya tahamani kama vile na kupanga nyumba kubwa ya thamani kama hiyo, tukaongea tukaachana, tulipnaga tukutane humo, sasa hayupo, namkuta msichana mwingine, ana jina hilo hilo...’nikasema

‘Hivyo vifaa ni vya mwenye hizo nyumba sio moja tu,...anazo nyumba nyingi seehmu tofauti....hivyo vifaa kavinunua kwa pesa yake, na anavibadili kila siku , kwahiyo ukifika hapo utakuta mabadiliko ya mara kwa  mara...kutokana na watu wake, na ni moja ya mipango ya kuwavutia wateja,na kuwahadaa mijanaume isiyo na wake, na hata kama ina wake, haitosheki  na hata kama inatosheka, lakini ni limbukeni, wakilegezewa basi, wamelainika....mijitu haina akili ya kufikiri....mimi kama ningelikuwa na uwezo wangu, ningeichapa midume ya namna hiyo viboko....’akasema huyo jamaa.

‘Lakini siumesema ni utaalamu wa shule kidogo uliotumika, ina maana hawo vimwana waliwekwa mahala wakapatiwa shule na nini siri ya kumpagawisha kidume, ina maana wamesomeshwa, na wakamjua mwanaume, na mwanaume hajijui, ...na matokeo yake alipoguswa huko...akajiona kama kafika sehemu ambayo hajawahi kufika,na hakuwahi kufikishwa na mke wake au sio...mimi sioni kuwa ni ujinga....’nikasema kama vila najitetea.

‘Ujinga, huo ni ujinga ...kwanini hukukaa na mkeo mkaongea,na kumwambia  mwenzako vipi unataka iwe,....ni kama chakula, au wali , unaweza ukautengeneza ukaonekana wa ajabu, kutoka hali fulani inayojulikana na kuwa tofauti,  mfano wali hadi pilau, hadi biriani, lakini ni wali ule ule...mkafundishana, ....mtaona ni kitu cha ajabu sana...lakini hamtaki kukaa na kuongea, matokeao yake ndiyo hayo...watu wajanja wamegundua, sasa wanachuma, watu wanaumizwa...sijui mpaka lini, watu wanalia na ndoa zao, hawaelewi sababu ni nini ..’akatikisa kichwa.

‘Nikuambie ukweli, mapaka wakijua tatizo ni nini huyo mama atakuwa tajiri wa kupindukia, na mwisho nasiki anafungua hospitali, au sehemu ya ushauri nasaha wa maisha ya ndoa....sio bure, ni pesa..hayo walikuwa wakifanya mabibibi mashangazi, ....unyagoni, ..siju wapi, lakini tumeyazarau, ....tunawazarau hata hawo mabibi..mashangazi...matokeo ndiyo hayo....’akasema na kukuna kichwa.

‘Tunawazarau kwa vipi...?’.nikauliza

‘Utaoaje, hujui ndoa ni nini,....lini mtu akaendesha gari bila kujifunza...lini mtu akawa docta bila kusoma shule, kwanini hatuisomi hiyo ndoa ni nini....nini cha muhimu na nini kinatakiwa nimfanyie mwenzangu,ili....hapa ujue kuna mambo mengi ya ndoa, lakini kuna jambo kubwa limesahaulika, ambalo ndilo kiini cha ndoa....hata wenyewe wanaita...mmh, la ndoa....’ akaguna na kunionyeshea kwa kichwa kule kwenye hiyo nyumba na tukawa kimia kuangalia nini kianendelea huko.

`Unaona mambo hayo, sio mchezo wewe sikia tu...’akasema huyo jamaa akiangalia kule mlangoni wakati gari la kifahari likisimama mbele ya mlago na jamaa mmoja, aliyevalia suti yake ya kifahari, akatoka harakaharaka na kuingia ndani ya ile nyumba,....mlango ulishafunguliwa mapema, ilionekana alishawasilina na huyo kimwana auache wazi maana gari lilifika, mlango wa gari ukafunguka haraka, na mtu akatoka na kuingia ndani ya nyumba haraka, na lile gari likaondoka haraka, lakini tulimuona alikuwa mtu mzima tu, tena anaonekana ni mheshimiwa...

‘Unaona wanaoingia hapo ni watu wazima,watu wazito, watu wenye wake zao.....sasa jiulize wake zao wanayajua hayo, hawajui, na kwanini inatokea hivyo.....akili ni mali....’akasema na kushika kichwa kwa kidole.

 ‘Ndio maana nika kuambia midume humu hakuna, ....mimi ni mwanaume, lakini nilikuja kugundua hilo...wanawake wanaweza wakatuchezea sana wakitaka..na sisi midume na akili zetu mbovu, tunatamba mitaani maofisni, wapi kuwa mimi sibabaishwi....nyumbani ukifika hakuna kitu....siri ya mtungu aijua kata, ndio maana nasema ni heri tuchapwe viboko....’akasema.

‘Kweli tunastahi kuchapwa viboko....na hata hivyo haina haja ya kuchapwa viboko kama fimbo, dunia yenyewe itatuchapa viboko...’nikasema huku nikiwa nimenywea na kujiona kweli sina akili na kwelii nastahili kuchapwa viboko...

Baadaye jamaa aakondoka akitafuta wateja wa nguo zake, na mimi taratibu nikaondoka pale nikiwa nimenywea kama mtu aliyemwagiwa maji, nilitemeba nikiwa kama sio mimi, ...na baadaye nilijikuta nimeshafika nyumbani hata bila kujijua ,....nilipoikaribia nyumba yangu nikaiangalia vyema huku moyo ukiniuma, ina maana kesho tu wajamaa wa kupiga mnada wanaingia....nyumba hiyo inakwenda, na gari hio linakwenda, sasa nifanyeje, ..akili ikanijia....

Lazima nyumba hii niitafutie mteja chapu chapu, mjini hapa.....na hata gari nitaliuza kinamna...’ nikasemana kushika kitasa cha mlango...nikakuta mlango unafunguka...upo wazi, nikajua mke wangu keshafika, nikajitahidi na hata kupiga mlunzi kama vile baba mwenye nyumba umefika, na unahitaji mke aje akupokee...

Kwanza nilisikia sauti za ajabu ajabu chumbani....na baadaye vicheko vya ....nikashituka, kwanza kwa hasira nikaangalia huku na kule, nikakipata kisu,....mwili uakanichemka,zilehasira zilizokuwa zimejificha zikafumuka, .....nikatamani kuua, .... kwa haraka nikakimbilia mlango wa chumbani...nikausukuma kwa kishindo....

 Je nini kilitokea....tuwepo kwenye sehemu ijayo Ijumaa njema. Nawashukuru sana waliochangia, nilitaraji kisa hiki wangelichangia wengi, hasa wanandoa,....lakini sio mbaya :Tupo pamoja

WAZO LA LEO: Binadamu ni kiumbe wa ajabu sana, huwezi kumdhibiti, huwezi jua nini anakiwaza, na kila siku kuna matendo ya ajabu ajabu yanayotokea duniani na anayeyafanya ni biandamu, nafikiri hata shetani atakuja kuturuka na kusema ‘hayo mimi sikuwahi kumfundisha huyu binadamu,hata mimi nashangaa nijawahi kuwaza hivyo....kwani wahenga walisema `ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Frauni..


Ni mimi: emu-three

Thursday, March 29, 2012

Hujafa hujaumbika-13



 Mke wangu akawa keshaondoka kurudi kwao, na nilibakia na wazazi wangu, ambao hawakutaka kabisa kunielewa, na hawakuamini kile kilichotokea na walitaka kujua kwanini imetokea vile, ...kila sababu niliyowapa haikuwatosheleza, na mwishowe wakanishauri kuwa nifike huko kijijini nikaombe msamaha yaishe, lakini mimi niliwaambia waziwazi, kuwa sihitaji kumuomba msamaha mtu yoyote , kwasababu yeye mwenyewe anajua kosa lake, nikasema bila aibu

‘Yeye ndiye alinisukuma hadi nikafikia huko,....nimejaribu weee....hapana ,sasa nimempata mtu angalau, hata kama hamtakubali hayo, ....basi ndio hivyo na iwe hivyo....’ nikajitetea hivyo.

‘Mwanangu unakumbuka wakati unataka kumuoa huyu binti, nilikuambia wazi,...kwanza hakulelewa katika mazingira mema, kama ulivyokuwa kumuona, anahitaji muda kujifunza kila kitu unachokihitaji, na hatuelewi hizo sababu zako zina msingi gani...hazina mshiko....ni aibu tupu kamawakisikiawazee kule kijijini...kwa ufupo wewe ndiye uliyeshindwa majukumu..’akasema baba.

‘Mwanangu tulikuambia na kujaribu kuzuia ndoa yako, hatukupenda kabisa mtoto wa watu aje kuumia tena...unakumbuka, tulikuambia hakikisha kweli unamuhitaji, kwani yule binti kaumia sana katika maisha yake, hatukupenda kabisa aishie kwenye maisha maisha ya taabu  tena...mimi nilibeba hiyo dhamana toka kwa mrehemu mama yeke, na hapa nilipo nashika nafasi yake kama mama yake...tafadhali mrudie ukamuombe msamaha...’akasema mama..

‘Kwani mimi nilimfukuza, kila kitu anapata, chakula nyumba hiyo hapo , alikuwa anapata,...aje, sijamfukuz amimi, lakini inavyoonekana anajitia kiburi, unaona alivyofanya katimukia huko kwao, sijui kwenu au sijui kaenda wapi, au kwa mwanaume mwingine. Ili alipize kisasi...sijui...yeye mwenyewe atalikoroga,...sina uvumilivu mimi,...kwa mtizamo huo  aspoangalia mimi nitaoa mke mwingine...’nikasema bila kujali..

‘Umechanganyikiwa mwanangu na nani huyo mke mwingine ndiye huyo uliyekuwa ukizini naye...?’ akasema mama kwa hasira.

‘Kwani tofauti ipo wapi mama...mimi huyo naye nampenda,na anajua nini ninachokitaka....mama unajua katika msiah haya ya ndoa nimejifunza mengi,mimi sikuwa natakiwa nikurupuke kuoa, ilitakiwa nifanye uchunguzi wangu mwenyewe,...nifanye majaribio kwanza, mwisho wa siku ningelijua yupi ananifaa...’nikasema bila aibu na mama akaniangalia kwa chuki.

‘Usinichefue wewe mtoto, unafikiri wanawake ni watu wa kufanyiwa majaribio, ina maana huyo binti hafai...hapana, kuna kitu hapo....’akasema mama kwa hasira.

‘Mama sio kwamba huyo mke wangu hafai,lakini tabia zetu zimekwua tofauti, hisa na mapendeleo yangu yawe vipi, ...mama samhani kusema kuwa, yule amekaa kishamba shamba sana, na mimi naishi mjini....unaoana alitakiwa kujifunza hivyo....lakini mengine hataki mimi nifanyeje....’nikasema.

‘Haya kamahutaki kwenda kumuomba mwenzako msammaha, sisi itabidi tukafanye hivyo, maana taratibu na mila zetu, tendo ulilofanya ni baya na faini yake ni kubwa, na inategemea huyo bintii atakusamehe au la...kwasababu ushahidi kila kitu kimeoenekana wazi....’akasema baba.

‘Sikilizeni wazazi wangu, kama mnataka kufanya hivyo, mimi siwakatazi, na mwambieni huyo mke wangu, yupo huru kurudi hapa, mimi sijamfukuza....kama hataki basi, sina jinsi....’nikasema na baadaye wazazi wangu wakaondoka.

                                 *********

Nilibakia ndani na kujiona mpweke, nikawaza mengi, na kun amuda akili inanijia na kujialaumu, lakini sijui kwanini, mawazo tu yalipokwenda kwa huyu kimwana, akili ikaruka na  bila kupoteza muda nikakurupuka mbio mbio nikamwendea huyo kimwana,...

‘Vipi mambo yameendaje, mke yupo nyumbani....maana wanawake wa kijijini wavumilivu hata uwatendeeje, hawabanduki, nakumbuka mama yangu alikuwa akiishii na baba, baba alikuwa mlevi kupindukia, akirudi anafanya maajabu, anampiga mama....lakini mama anakubali tu, na hata kumfulia matapishi,au awakati mwingine kwasababu ya ulevi, anapitiwa na haja...aah, mimi siwezi kabisa..’akasema kimwana.
‘Ina maana na mimi nikiwa hivyo utanikimbia.....?’ nikamuuliza.

‘Ikizidi sana ...., kulewa sio mbaya, hata mimi nakunwa, lakini sio ulewe na mipombe yako iwe kero,...iwe mipombe ya kupigana, .... uje unipige....hapana, tutapigana, mimi hilo ulijue wazi,....siwzi kuw amtumwa, kama nikupendana tupendane,kama tunageuza mapenzi uwanja wa ngumi, tutazichapa...ehe,,haya niambie imekuwaje..?’ akasema huyo kimwana.

Nikamuelezea ilivyokuwa na jinsi nilivyopagawa nikamuelezea kila kitu,....sijui akili yangu muda ule ilikuwaje,sikuwa hivyo kabla....nilikuwa kama mjinga fulani.

‘Sasa unajua mimi name nimetafakari sana kuhus maisha yangu, ....nimejiuiza nitaishi hivi mpaka lini,umri unakwenda, na msiha ndiyo hayo yanabadilika, nahitaji na mimi kutulia na kuwa na watoto wangu, kwa mtaji huo, name nasema hivi...kama unanipedna kweli, tufunge ndoa, na ndo aiwe ya haraka iwezekanavyo...’akasema huyo kimwana.

‘Eti nini...?’ nikashituka.

‘Eti nini..nikuulize unanipenda au hunipendi....?’ akauliza.

‘Hiyo umenishitukizia, nifunge ndoaa na wewe..hapana, sio kwa sasa, unajua ndoa lakini wewe, ukiingia kwenye ndoa, kuna masharti yake, na wewe sizani kama unaweza kutulia kwenye ndoa....tusubiri kwanza kidogo, kwanza sijaachana na mke wangu...mambo hayajakuwa shwari....’nikamwambia.

‘Sikiliza mimi sio Malaya, kama watu wanavyonisema, siwezi kukaa na wewe tu, huku najua mimi sio mke wako, kwahiyo amua moja, tufunge ndoa, au uishie zako...’aaksema kwa nyodo.

‘Sijasema sitaki kufunga ndoa na wewe, lakini ni mapema sana,....huoni hali ilivyo, mke yule tumesigishana, hatujakaa na kuamua kuachana na mara nafunga ndoa na wewe...kwanza yule ni rafiki yako mtaangaliaan vipi...’nikajaribu kujijitetea.

‘Umenisikia, lakini....kama hutaki ndoa, basi ishia,... umenikuta na maisha yangu, ....na kama walivyonikuta wengine na nilipowagusia ndoa wakaukata na wewe unaweza ukaukata vile vile, mimi sio jamvi la wageni na mimi nahitaji mume nitulie...nilee watoto wangu, hayo ndio maamuzi yangu...kwaheri nenda kafikiria ukija hapa uje na jibu,....’akasimamia kwenye msimamo huo na akasoegeela mlango akaufungua na kunionyeshea niondoke.

***********

Mtu mzima niliwaza sana,nikanywa mapaka nikapitiliza, nakumbuka siku hiyo nilijikuta nimelala kibarazani mwanyumba yangu nikiwa bwiii...na kesho yake natakiwa kazini.  Nilifika kazini nikasingizia naumwa, na kwenda kwenye barm huko nakiutwika kisawasawa...

Nilipofika kwa kimwana akanifukuza akiwa na msimamo huo huko wakutaka ndoa,na hakutaka kabisa kunifungulia na alinitishia kuwa nikiendelea kukaa hapo nje ya nyumba yake ataniitia watu kuwa mimi ni mwizi.

Ikawa kila nikienda kwake, ananitolea nje, na siku moja nikakuta mlango umefungwa kabisa, hayupo , hapo moyo ukaanza kuniuma,...wivu ukanijaa moyoni,  ikabidi nihangaike kumtafuta, na nilipompata akasema anajiandaa na safari ya kwenda kijijini kuna jamaa kaahidi kumuona, na yeye anachotaka sasa ni ndoa, ...

‘Muda wa kuolewa umefika, sitaki kuipoteza hii bahati....wewe umeshaoa unajua utamu wa ndoa, mimi je...kwahiyo toka leo tusijuane, mimi ni mchumba wa mtu...’akasema  looh, nikamzaba kibao, na yeye akanirudishia cha nguvu, nikabaki nimeduwaa....

‘Wewe unanipiga kibao mimi,...koma, kama ulivyokoma ziwa la mama..ko... kampige mkeo...toka humu ndani kwangu, sitaki hata kukuona....’akanifukuza kabisa, ikabidi nitoke pale nikiwa nimenywea, nikafika kwangu na kesho yake nilipofika kazini, nikakuta barua ya kusimamishwa kazi....

‘Huu sasa mkosi...’nikasema na kwenda kumuona mkurugenzi ambaye aliniambi waziwazi kuwa wamenivumilia sana, na wamenionya sana, sasa imefikia kikomo;

‘Unasikia ndugu yetu, wewe umeamua kuishi maisha yako unayotaka, ...maisha ambayo hayaendani na maadili ya kazi, unakuja umelewa, kazini hukai, una madeni mengi,uanitia kampuni hasara ....sisi tumechoka kukubeba, kwahiyo hiyo ndio zawadi yako, na ukiangalia hapo, madeni yako ni makubwa hata kuliko mafao yako, lakini kampuni imeamua kukusamehe madeni yaliyozidi, .tutakachofanya ni kukata madeni yetu kutokana na kiwango cha pesa ya mafao yako,...na hutakuwa na chochote kutoka kwetu, zaidi ya .....barua hii....’akasema mkurugenzi.

‘Eti nini, hapo niatawapeleka mahakaamni, sikubali, mnataka mkate kila kitu, nitaishije mimi....’nikalalamika.

‘Sawa wewe nenda huko mahakamani siunadai haki yako bwana, kama ipo tutakulipa, ....kwaheri bwana, tunakutakia maisha mema, kwakweli tumejitahidi vya kutosha, ....nenda kastarehe na kimwana wako...lakini kumbuka kuwa starehe ni gharama......’akasema huyo mkurugenzi na kweli nikafukuzwa na walinzi nikaishia zangu mitaani....

Nilipofika nyumbani kwangu nikamkuta yule kimwana kajaa tele, akanipokea kwa bashasha, utafikiri sio yule aliyenifukuza kwake, na aliponiona nilivyonywea akajua kuan jambo;

‘Vipi mpenzi mbona unakuwa kama umemwagiwa maji....?’ akauliza.

‘Sasa mzee mzima nimeumbuka,kazi sina....’nikasema.

‘Kazi huna, wewe mwanaume bwana, kwani kazi ipo moja hapa duniani, nikuambie ukweli, mimi nilifukuzwa kazi siku nyingi sana, lakini naishi, natesa raha....hapa sin akazi, lakini sijawahi kulala njaa, ni akili kichwani...bongo hapa, wewe tesa maisha, ukiyapatia ....maisha yenyewe mafupi, unataka kuyawahisha kabla ya  siku zake....sikiliza utanioa au hunioi?’akasema bila kujali  matatizo yangu.

‘Sasa wewe umeshasikia kuwa sina kazi....bado unataka tuoane,  tutaishije?’ nikamuuliza.

‘Kwani mimi naishi hivi nina kazi, kwani hawo waliopo mitaani wakihangaika wana kazi zakuajiriwa hebu jiulizei wanaishije...tutajua jinsi ya kuishi wewe usijali kabisa..hayo maisha ya mbeleni niachie mimi, ilimradi usiniingilie,....mimi nitakulipa fadhila zako, ili ujue kweli nakupenda, unafikiri,...hebu jiulize kwanini nisiwang’ang’anie vipoba wanaojigonga kwangu, nakuja kwako, kwasababu nimezimia kwako, ....wewe namimi tunaendana....unasemaje mpenzi...’akasema

‘Sawa kama upo tayari kuishi na mimi hata bila kazi, hapo najua kweli unanipenda....sasa unataka tuoane vipi..harusi au juu kwa juu...maana pesa sina?’ nikauliza.

‘Eti nini, Juu kwa juu, watu watajuaje kuwa na mimi nimeolewa....acha hiyo, ngoja nikuonyeshe njia, tutayarishe kadi, nitawapelekea marafiki zangu na wewe wapelekee rafiki zako, siulishawahi kuwachangia,.... sasa ....sasa ni wakati wao kulipa deni...hilo litafanyika tu....’akasema baadaye tukakubaliaan hilo.

Kweli mambo yalijipanga, baadhi ya marafiki zangu wakanichangia na pesa ikapatikana  yakutosha harusi ikafanyika, bilakujali kuwa nina mke mwingine kijijini, ndoa ikafungwa, ...na kimwana nikawa naishi naye ndani, siku , miezi ikapita,....

                                ************

Siku moja nikapokea ugeni, walikuwa mjomba na mke wangu wa kwanza, na baadaye akaja baba na mama, walikuja kwa mabasi tofauti, na wakanikuta nipo ndani na kimwana, akawakaribisha vizuri tu, ...

‘Huyu ndiye nani ...?’ akauliza mjomba.

‘Ni mke wake...’akajibi kimwana

‘Hujaulizwa wewe binti...’akasema mama.

Mimi nikawaangalia kwa makini halafu nikamwangalia mke wangu wa kwanza, niakasema kwa utaratibu;
‘Hivi ni haki mke kuondoka kwa mumewe ikapita zaidi ya miezi mitatu...aah,ishafika sita?’nikauliza huku nikiangalia kalenda ukutani.

‘Je wewe kwanini ulimruhusu akaondoka, ...na ukumbuek huyu mke, ulimchukua kwa wazazi wake, na ukaahidi kuishi naye ikiwemo ulinzi na usalama wake, je alivyoondoka,ulijitahidi kumtafuta,je ulijuaje anaishi vipi huko alipo....?’ akauliza baba.

‘Najua alikwenda wapi, ndio maana sikumtafuta na mlipoondoka hapa niliwapa maagizo kuwa arudi, hakurudi, ina maana alionyesha kiburi, na....maisha yangu siwezi kuishi bila mke, na ndio maana nikaamua kuoa mke mwingine, kama huyu yupo tayari kuishi nami tena, anakaribishwa, isitoshe, huyu mke wangu mpya walikuwa marafiki sana....mimi sijali...’nikasema.

‘Wewe nani aishi na...’akataka kuongea kimwana wangu, lakini mke wangu wa kwanza akaanza kuongea kwa huzuni. Kwanza aliziba macho yake kwamikono, nafikiri alikuwa akificha machozi, akawa ananiangali kwa jicho moja kupitia kwamkono aliyofunika machoni, na baadaye akaondoa na kuaniangalia moja kwa moja , sikuja ana maana gani.

‘Mama na baba na mjomba, nyie ni wazazi wangu, na ninawaheshimu sana, ..hali ilivyo sizani kwamba kuna ndoa tena hapa, mimi nimekulia maisha ya shida, nimeteseka sana, na nilijua kuolewa ndio mkombozi wangu, lakini naona ni kama kuruka mkojo na kukanyaga kinyesi....’akasemamke wangu wa kwanza kwa huzuni.

‘Wazazi wangu, labda ndivyo mungu alivyonipangia kuwa maisha yangu yawe hivyo...namshukuru sana mungu, ...mwenzangu naye ana hulka na maisha yake ambayo labda nimeshindwa kuyafikia, ...je nikiishi naye hapa yatakuwa yamefikia huko, kwasababu mimi ni yule yule, na tabia zangu ni zile zile...unafikiri itakuwaje ....sio kugeuka mfanyakazi na mtumwa wa nyumba hii...hapana nisingelipenda kuwa hivyo tena.....’akasema mkewangu huku machozi yakimtoka.

‘Mwanangu tulia, huondoki hapa, wewe ni mke halali wa mtoto wetu, tumekuozesha kwa sheria zote,...’ ...akasema mama halafu aaknigeukia na kusema ;

‘Hebu tuambia huyu unayedai kuwa ni mke wako mpya ulimoa kwa sheria gani, nani mzazi wako aliyeshuhudia hiyo ndoa,....huo ni uhuni wenu mumechukuana tu mitaani na kujifanya mumeoana, haipo hiyo...hatuitambui hiyo ndoa kma kweli ipo...’akasema mama.

‘Ndoa zipo za namna nyingi, kuna ya kimlia ya dini na ya bomani,....sasa mama unatakaje,sio lazima nioe kwa seheria za kimlia...mimi na huyu tumeoana bomani, na ndoa inakubalika, na vyeti vyetu vipo, na huyu mke ....maana nashindwa hata kumuita mke, kaondoka kwangu miezi mitatu,...ooh sita sasa....sna inaweza ikawa zaidi kaka huko, nitamuaminije, huenda...alikuwa kwa bwana’ke....’nikasema kwa hasira.

‘Niombe tafdhali....niombe radhi kabisa, mimi sio Malaya kama huyo hawara yako....mimi nimakulia kwenye maadili, siwezi kuuzalilisha mwili wangu kwa wanaume bila ndoa...hilo nakuthibitishia na mungu wangu ni shahidi...kwahiyo kama umeamua kumuoa huyo hawara yako, sawa, mimi naondoka, ila nataka talaka yangu...’akasema mke wangu wa kwanza.

‘Hilo tu, talaka yako ipo tayari nilishaitayarisha, nilikuw anasubiri tu hizi porojo ziishe nikukabidhi, kingine unahitaji nini, sidhani kuwa kuna maliyoyote tulichuma pamoja, sijachuma na wewe hata kitu kimoja....ulikuwa mfanyakazi tu wa ndani...na kuhsu mtoto, mimi nitatoa matunzo yote, atasoma, ukitaka kukaa naye sawa, kama hutaki nitakaa naye mwenyewe hakuna shida...’nikasema.

‘Mtoto wangu nitakaa naye, hawezi kuja kuteseka, kama nilivyoteseka mimi, hilo lisikutie shaka, na kuhusu mali , sihitaji mali yako, unakumbuka uliponitoa, niliweza kuishii maisha magumu kuliko unavyozania, kwahiyo kwangu maisha ni kawaida tu, ninachowatakia ni maisha mema, na nisema kuwa, ....mungu awabariki sana...’akatuli na kuanza kulia.

‘Unalia nini...kama umekubali yaishe basi...’akasema huyo mke mpya.

‘Wew tuli kule, hayakuhsu haya, ...’akasema baba kwa hasira.

‘Yananihusu sana baba, kama hayanihusu, kwanini huyu mwanamke mshamba, alikuwa akinitukana na kuniita hawara, au mliona mimi ni jiti tu, sina mdomo wakuongea...sikilizeni sana wazazi..wa-ngu,mimi nina heshima sana kwa wale wanaotaka heshima yangu, lakini mtu akinikosea,ataikosa heshima yangu, sijali kuwa ni nani, waulizeni wazazi wangu kijijini....’akasema na kutulia kimiya akisikilizia.

‘Kwa hilo tu tunakujau sana, wapo ulipotoka, ndio maana hatutaki uishi na mtoto wetu utatuharibia kizazi, hufai kabisa kuingia kwenye familia yetu, hatukukaribishi kabisa huko...’akasema baba na mjomba ambaye muda mwingi alitulia akasema;

‘Jamani hawa ni watoto wetu, kwa vyovyote iwavyo, na makosa yametokea, na hili ni muhimu tulijue, kuwa kama tutaendeela hivi hatutaweza kulisawazisha hili jambo,...huyu kijana bado anajioa mdogo, na hali niliyoiona hakuna jisni ya kumrudisha nyuma, keshaamua hivyo...labda kuna sababu zake za msingi, lakini hazijafuata utaratibu, na sioni kuwa kuna haja ya kufuata huo utaartibu tena, ...’akatuli amjomba na kuniangalia kwamakini.

‘Kuna usemi usemao, mtoto akililia wembe, mpe, ukimkata atajifunza, sasa wewe umelilia wembe, sawa huo hapo...’akasema na kumwangalia kimwana wangu, sikujlai, ...nikatulia kuskiliza tu, kwakweli akili ilifungwa kabisa, nilimuoa huyo kimwana, ni kila kitu, ...

‘Nakuambia mjomba, mimi maisha niliyapitia, ilifikia mahala niakasema nini natafuta dunia hii, ...starehe zina mwisho wake, na maisha haya yapo, wapo waliishi wafanya makubwa zaidi yetu, wapo wapi....huwezi kufanya lolote likaizidi hii dunia...tunakushauri kama wazazi, kumbuka ulipotoka, kumbuka kuwa maisha ya ndoa sivyo hivyo unavyzania, kuwa natamani hivi , nataka hivi, iwe hivyohivyo mara moja, ....’akasema mjomba name nikampa nafasi maana mjomba namuheshimu hata zaidi ya  baba.

‘Kweli umeonyesha kuwa damu yako inachemka,...na sasa unataka kusihi na wake wawil, hatukukatazi, lakini ujue kuwa maisha ya wake zaidi ya mmoja yana masharti yake....siotu kujiolea...masharti yake ni magumu ndio maana wengi wanashindwa na hata walio-oa, waulize vyema, nini wanachokipata...hukatazwi oa wake upendavyo, laini ukumbuke kuwa na wao ni biandamu,wanstahili zao, uwatendee wema na adilifu, je utaweza hilo...?’ akauliza mjomba.

‘Mzee wangu samahani kwa kuingilia, na huenda tukajadili haya mapaka kesho, wakati swala lipo wazi, kwanza ndio imeshafungwa, mimi ni mke halali, pili kwa kauli ya mume wangu,keshamuacha mke wake wa kwanza,kkwahiyo hapa tuzungumzie ndoa yangu sio ya wake wawili,...'akasema huku akitabasamu kwa dharau.
'Hivi wewe unaongea nini...'akasema mama.


'Ndio mama, huo ndio ukweli, ...ujue kuwa huyo mwenzangu keshaachika, na mimi ndiye mke halali....hukusikia alivyosema mume wangu ...au rudi vyema wasikie...sio nashnikiza iwe hivyo, hapana ila kauli ya mume wangu ndiyo ya msingi...’akasema mke wangu huyo mpya.

‘Nani kakuambia hayo wewe unafikiri ni rahisi hivyo....tulia kwanza wakubwa waongee, na ujifunze kuishi na wakubwa, umeshasema kuwa uheshimiwe na wewe utaheshimu, mbona wewe unakimbilia kuvunja heshima za wakubwa,kweli kwa mtindo huo utasheshimiwa...’akasema mama.

‘Samhani sana mama, nilikuwa naweka wazi, mimi nitafunga mdomow angu mpaka mniruhusu, haya mmmmmh’akasema na kuufumba mdomo wake kwa vidole.

‘Kazi ipo....’akasema baba.

‘Baba msiumie kichwa, mimi haya niachieni mwenyewe kwanza, mimi ni mwanaume, na nawaheshimu na kuwajali sana wazazi wangu, nitakuwa mtomvu wa fadhila kama sitwashukuru kwa yote mliyonifanyia, ...wazazi wangu nyie mumeshatimiza wajibu wenu,nawashukuru sana, ....lakini mimi sio mtoto tena, nimefikia mahala pa mamuzi yangu...’ nikasema huku nwaangali kila mmoja kwa wakati wake.

‘Mimi hapa ni mtu mzima,....namimi kuwa ninachokifanya ni kwa mslahi yangu,....natafuta maisha yangu, na ili nifanikiwe natakiwa nimpate mwenzangu anayekubaliana na matakwa yangu, umerudi kazini, unajihisi , unaburudishwa,hata uchiomvu wote unapotea....si kweli mama, ndivyo wewe unavyomfanyia baba...’nikasema huku namwangali mama kwa aibu kidogo.

‘Sio kwamba binti Yatima alishindwa hayo, kwakweli alijitahidi, ilakuna mambo machache ambayo kwang niliyaona ni muhimu kinaman fulani,..,kweli ana adabu, kweli ana sifa zote za kijijini, kwenu anafaa sana,....lakini niligundua kuwa kwangu itaniwia vigumu,hakubaliani na haendani nitakavyo mimi....hivi wazazi wangu mngelifurahi kuniona natembea mitaani na machangudoa, ...au nivumile tu mpaka nipate vidonda vya tumboni, au .....’nikasema na kucheka halafu nikasema;

‘Kama haiwezekani sawa, lakini kama kuna mbadala, kwanini mtu uumie....kwanini....’kabla sijamaliza kuongea Binti Yatima akanikatiza nami nikatulia kumsikilza nikiwa na hamasa kusikia nini anachotaka kuongea.

‘Wazazi wangu naona kitakachoendelea hapa ni kuzalilishwa tu, kauli hizo sio nzuri, na nisingependa kuingia huko na kulumbana ksuiko na sababu....mimi nimeshakubali, kama alivyosema mwenzangu, kuwa hapa tunaongelea ndoa moja,kuwa yeye keshapata mimi nimeshindwa, ...yote ni heri, karibu sana rafiki yangu na mume huyo wako wote...nawatakia maisha mema,....sina zaidi naomba hiyo talaka yangu,ili kesho na keshakutwa, isije ikawa vinginevyo....na nina... ‘akasema kukatishwa na kilio huku akiziba uso wake kwa mikono miwili, nahisi hakupenda watu wamuone akilia au ndio aibu ya kukaa pamoja na wakwe na kuongea aliyoyaongea..

‘Hivi nani kakuambi umeachika...’akasema baba.

‘Hapana baba mimi sipo kwenye ndoa tena, ndio ni ukweli usiopingika kuwa nilimpenda sana mume wangu, hajui tu, ....nilimpenda tangu siku ile ya mwanzo tuliyokutana naye, nilijua yeye ndiye muokozi wangu na yeye atachukua nafasi ya mama yangu, maana mama yangu alikuwa kipenzi changu,... lakini mungu alimpenda zaidi....lakini kumbe kwa mume huyu nilikuwa kama majaribio ambayo nimeyashindwa na inabidi nikubali ukweli..’akasema huku akifuta machozi.

‘Pole sana....’akasema rafiki yake kwa sauti ya upole, halafu akawa kama kashituka na kuuziba mdomo wake..hakuna aliyemjali kwa muda huo.

‘Hapana hilo kwetu kama wazazi halipo, sisi bado tunakutambua kama mke halali wa mwanetu, kwasababuu taratibu hazijafuatwa,ilitakiwa wewe mtoto wetu, urudi huko kijijini kwa wazee ili tuone tatizo ni nini, na kama inabidi iwe hivyo, basi taratibi zingelifuatwa....’akasema baba.

‘Baba, ukitaka hayo tutaumia wengi...tutaishije hapa...baba , na mama na mjomba kubalini ukweli,najua mnanipenda sana,na nami nawapenda sana,lakini tukubali ukwelil, kuwa kila jambo lina mwisho wake, na ukililazimsiha kuna kuumia hapo , na huenda ukakosa yote, kwani mkamia maji huyanywa...’akasema mke wangu wa kwanza.

‘Hapo umenena mtalaka wangu....na ndio maana nakupenda, ..unajua hali halisi...na nashukuru sana ,na hata hivyo nasikitika, kuwa sikukutendea haki,... lakini hakuna jinsi, inabidi iwe hivyo,...wewe mwenyewe unajua,...tutaishije hivyo...hapana, .... nakuomba uvumilie tu, kwani wapo wengi wanakutafuta kule kijijini, utampata anayekufaa....wewe ni lulu sana kule kijijini...wanakufahamu , wanakupenda na wanaikubali hiyo tabia, hulka, na mienendo yako...sawa eeh..’nikasema huku nakwepa kumwangalia machoni.

‘Nimekusikia na nashukuru kwa kauli yako hiyo, nami nasema hivi, nakushukuru sana, kwa wema wako na mengi uliyetendea,maana ulinitoa kwenye makucha ya simba, isingelikuwa wewe sijui ningelikuwa wapi, ...nakiri moyoni kuwa wewe ulikuwa kila kitu kwangu,lakini kama nilivyosema awali siwezi kulazimisha hali iilivyo,....’akatulia na kuhema kwa nguvu, baadaye akaendelea kusema;

Mimi nimekubali kushindwa, nisamehe kama nilishindwa kutimiza yale uliyoyataka, najua mwenzangu , ambaye alijifanya ni rafiki yangu, ndio kweli tulisoma anye, na namjua vitimbwi vyake na tabia yake, lakini sikujua kuwa ana malengo hayo, haina shida kabisa...kweli mwenzangu anayaweza hayo, ...lakini tukumbuke kuwa binadamu wote hatulingani,....huyu anajua hili na mwingine hajui, lakini lipo analijua kuliko mwenzake, tunazidiana...’akatulia an kumwangalia rafiki yake.

‘Siongei haya kukubembeelza kuwa nataka turudiane,hapana,....moyo umeshachefuka.... na baada ya hayo, naomba hiyo talaka yangu...niondeoke...’akasema huyo binti akigeuka kuondoka na alipofika mlangoni, mama akamrudisha na kwambia arudi ake, naye bila ajizi akafanya hivyo, akarudi na kukaa kwenye sehemu yake.

‘Mimi bado kauli yangu ni ile ile...ndoa bado ipo, sisi huyu binti unayemuita mkeo hatumtambui, na katu hatutamkaribisha kwenye familia yetu kama mke mwana....kwasababu tumajua , tunakijua kizaizi chake,nini unataka kutuletea katika hii familia....hapana, kama umeamua hivyo, basi jua kuwa sisi hatupo pamoja na wewe....’akasema baba na mama akakubali kwa kichwa.

Na mimi sikusubiri nikaingia ndani na kutoka na karatasi ya talaka, nikawa naisoma kwa sauti kubwa huku natembea kuelekea sehemu yangu niliyokuwa nimekaa awali, na kimwana akawa anatabasamu kwa mbali, na binti Yatima machozi yanamtoka, ...sikujali nikaisoma kwa mbwembe:

Mimi mtoto wa Msomali kwahiari yangu mwenyewe, bila kushurutishwa , nimeamua kumuacha mke wangu,kwa talaka zote .....sababu za msingi, kwanza hatuna mahusiano mema kama mke namume, pili kaondoka nyumbani miezi mitatu bila kuaga, na hakuwahi kunipa taarifa yoyote toka huko alipo,...pamoja na mambo mengine nimeamua kumuacha, yeye sio mke wake tena, na yupo huru kuolewa na yoyote yule....hatudaiani...’Nilipofika hapo nikatupa jicho kumtizama binti Yatima, ambaye alikuwa kafunika uso wake na kitambaa akifuta machozi

 ‘Na kuhusu swala la mtoto yupo huru kuishi na mzazi yoyote kati yetu wawili , na hata hivyo nimekubali  kumhudumia kwa mambo yote muhimu, ....nimemaliza,aukunakipengele nimesahau maana mimi mimisioo mtaalamu kwa mambo haya...’nikasema huku namwangalia mjomba, utafikirii ni jambo la heri lililokubalika, nilipowaona wapo kimiya, nikaweka saini yangu chini, na kumkabidhi binti Yatima ile katarasi, ....

‘Hahaha...kweli wewe mtoto umetushinda, yaani umekaa na huyu binti mkapanga muandike hiyo talaka, eti kuwa hii  ndio talaka, huo ndio utaratibu gani,...lini mlikaa baraza la usuluhishi mkayaongea matatizo yenu, hata ikashndikiana, ...hebu niambie, wapi mlikutana na wazazi mkayaongea matatizo yenu, au kwasababu umeguswa mtima nyongo wako na hawo wanaojua wapi ulipo na kuwazuzua wanaume....sikiliza tutakusubiri kijijini uje ufuate taratibu zote, lakini talaka hii haikubaliki.....’baba akaichukua ile talaka na kuichanachana vipande vipande.

‘Hata ukiachana imeshapita hiyo...’nikasema hata bilakufikiria...’na wote wakaniangali huku wananishangaa, hawakuamini kuwa kweli ndiye yule kijana, yule mtoto waliyemtarajia kuwa atashika usukani wa familia kamaalivyo mjomba....wakachoka na hatimaye baba akasimama nakusema;

‘Twendeni zetu....huyu naona kuna lake jambo,...sio bure, .... bila kumkazania huyu tutapoteza mtoto moja kwa moja....’akasema baba na kumgeukia mkewe ambaye alionekana kujawa na huzuni usoni...mama na mtoto bwana,hata awe mkubwa vipi. Na hata mjomba alivyotaka kuongea kitu, akasita na kumfuata baba nyuma, huku kaweka kichwa chini. Mimi mwenyewe kuna muda hisia zilinijia na kutaka kuwaambia wasubiri kidogo, lakini nilipomtizama kimwana, nikayeyuka, nikatabasamu naye akatoa lile tabasamu lake, nikawa hao .....
Mara mlango ukagongwa, tukaangaliana , kwasaabbu ni kwangu nikainuka kufungua mlango, na nje niliona gari ambalo ni la wapiga mnada, nikawaza kuna nini leo hapa, pembeni ya mlango kuna jamaa kashikilia daftari , akaniangali ahalafu akasema;

‘Sisi ni watu wa mnada, hiki hapani kibali toka mahakamani, ...kazi yetu tuliyopewa ni kuwafuatilia wadaiwa sugu, unakumbuka nyumba yako hii ulijenga kwa mkopo...’akawa anaendelea kuongea, lakini sikuweza kumsikia, maana kichwa hapo kilikuwa sio changu,... nilishasahau kuwa hiyo nyumba niliijenga kwa mkopo nadaiwa.....sasa itakuwaje, ...mungu wangu wee....

Je iltakuwaje, na je ilikuwa rahisi hivyo kuwa nimempata kimwana ,ndio kila kitu saafiii...hebu tuone yatakayoajiri...niwaulize kuna yoyote kati yenu aliyewahi kukutwa, au kuwa jamaa yake aliyewahi kukutwa  na majanga kamahaya, je alisaidiwaje?

WAZO LA LEO: Usione watu wapo kimiya, ukazani hawana shida, au matatizo kama yako, ...hapana...kila mtu ana shida au mataizo yake, ila wengine ni rahisi kuyaongea mataizo yao au shida zao na kujiona wao wamezidiwa.

 Ni kweli shida zipo na huenda zikazidiana, na tunatakiwa kusaidiana, na labda wengine wanafikiria kuwa kwa kuongea sana wanaweza kukapata misaada,...inwezekana sikatai, ila isiwe ndio sababu ya kujitangaza kwa kila mtu, kwani kwakufanya hivyo utafukuza baraka, na sio wote wenye nia njema na shida zako. Hili nimejifunza,...sijui wewe,hata hivyo wahenga husema; subira yavuta heri


Ni mimi: emu-three

Wednesday, March 28, 2012

Hujafa hujaumbika-12


‘Mume wangu mbona siku hizi unalewa kupita kiasi na hata unaamua kulala nje, una tatizo gani...ni kazi gani hizo za kulala nje, na ukirudi umelewa chakari, kazi gani utafanya ukiwa umelewa hivyo...?’ akaniuliza mke wangu huku akionyesha uso wa huruma, nilimkwepa kumwangalia, maana ukimwangalia usonii utamuonea huruma.

‘We acha tu, endelea na shughuli zako, maana hata nikikuambia utakimbilia kusema ni mambo ya kizungu....maisha ya ndoa nayaona kwagu ni mitihani, sasa tena watu wananiibia gari langu ...unajua mke wangu sikujua itakuwa hivyo...lakini sio kosa lako, labda nijilaumu mwenyewe...’nikasema huku nikipepesuka

‘Mbona sikuelewi yaani ulevi wako unanilaumu mimi....kulewa ulewe wewe, na lawama zinakuja kwangu..hapana hizo lawama sikubali,...acha ulevi kwanza kama unataka uwe msafi,...mtegemee mungu, kupoteza gari sio kupoteza kila kitu,watu wanapoteza magari, wanapata hasara kubwa sembuse wewe gari moj tu...’akanishauri mke wangu.

 Kwakweli kama kuna kitu kiliniuma katika maisha yangu ni pamoja na kuibiwa hilo gari, sikuamini, maana nililitafuta mpaka mfukoni, ...hata nilipofika kituo cha polis kujieleza, bado nilikuwa najikagua mfukoni, ....
Unajua nilipokuwa nikisoma Ulaya, nilihangaika sana,...kubeba maboksi na kazi za ajabu ajabu, ili kupata pesa za ziada hadi kununua hilo gari, na lilikuwa sehemu yangu ya kujivunia kuwa na mimi nilifika ulaya, sasa nitapata wapi gari kama hilo, maana bei yake kubwa sana, pesa ninayopata haitoshi...

‘Chukua mkopo angalau upate gari la kawaida....’akanishauri mmoja wa marafiki zangu na wazo lake nikalikubali, na kweli haikuchukua muda nikapata mkopo na kununulia gari, ambalo haliwezi hata kufikia nusu ya lile gari langu liloibiwa, lakini angalau niliweza kusema nina gari, na kipindi hicho kampuni yetu ilikuwa ikiyumbayumba kibiashara....

Biashara ilisuka sana, na hatukuweza kupata masoko ya bidhaa zetu kwahiyo mameneja walitakiwa wajitegemee kiusafiri ili kubana matumizi.

Gari likaniweka katika hali yangu ya kawaida,....ukizoea gari inakuwa shida.....basi nilipolipata ratiba yangu ya kurudi usiku wa manane ikaendeelea, na wakati mwingine nalala nyumba za wageni,na kubadilisha wasichana kama nimechanganyikiwa hata ofisini wakaniita kiwembe, binti hakatizi mbele yangu, lazima nitamualika chakula cha usiku....yaani mungu tu kasaidia na kunikweepsha na huu ugonjwa, sijui...

 Mshahara ukawa hautoshi ,kwasabbu starehe zilizidi, kila siku nipo kwenye mahoteli makubwa, kwenye mabar,madanguro....na ukumbuke kuwa nilikuwa nakatwa makato ya madeni, matumizi yangu yalikua hayakadiriwi, na kila siku naomba mshahara kabla ya wakati, ....Nikaanza kuandamwa na barua za maonyo, lakini ilikuwa sikio la kufa halisikii dawa...!

 Siku moja wakati nimerejea nyumbani nikakuta kuna mgeni...sikujali sana, nikapitiliza hadi chumbani, siku hiyo nilitaka kujipumzisha nyumbani,....kwani nilikuwa nimeutwika kisawasawa...na sikutaka kumsumbua mke wangu, ....lakini baadaye nikaona sio vyema nikamuita mke wangu chumbani...Alipofika, nikaanza kumshikashika, ....

 ‘Aaaah, bwana umeanza mambo yako ya kihuni huni, ....,huoni kuna mgeni varandani...na mchana huu umelew hivi...mungu wangu...haya jisaahulishe kidogo....’akasema mke wangu.

 ‘Mgeni gani zaidi ya mke wangu, mimi...ni mume wako, nikikuhitaji hata kama kuna wageni inabidi utafute mbinu waondoke....sikiliza mke wangu, nimevumilia weeee, sasa nachoka, ....niende wapi, nikatembee na machangudoa..mmh, njoo hapa....’nikawa naongea sauti ya kilevi, kweli pale akili yote ilikuwa ikinuka pombe nikamsogelea mke wangu naye akanikwepa na kusema.

 ‘Hebu punguza sauti hujui ni nani yupo varandani...halafu ulvyolewa, mbona leo aibu, hujui huyo ni rafiki yangu mkubwa kaja anataka kukuona shemeji yake...’akasema .

 ‘Haya shemeji shemeji huku mwazima taaa...nakuja maana sikuwezi....lakini ipo siku utajilaumu na hawo shemeji, ....nakuja...ngoja nivae hii bukuta, nani anajali nipo kwangu...’nikasema na kuvaa bukuta yangu, sikujali kuwa ni nani yupo, halafu nikatoka pale varandani....

 Unajua wakati naingia yule mgeni alinipa mgongo, sikuwa nimemuona vyema, ...sasa natoka chumbani nikawa namwangalia moja kwa moja usoni...niliduwaa...nikashikwa na butwaa, lakini baaadaye nikajifanya kujisahaulisha nikasema kwa bashasha..

 ‘Ohh, samahani sikujua kuwa kuna mgeni, mgeni mwenyewe mrembo....shemejii ...mmh, umejaliwa kweli, ....mke wangu umempata wapi huyu mrembo?’ nikauliza.

 ‘Mbona alishawahi kufika hapa nikakutambulisha siku moja,....umesahau, na wewe bwana unazeeka kablasio muda wako.... ulikuwa haujamuoan vyema nini...?’ akasema mke wangu.

 ‘Aaah, labda nilikuwa na mambo mengi kichwani....shemaji jisikie upo huru,mimi nilikuwa na sherehe huko kazini, kwahiyo nimekunywa kidogo...unisamehe, kama nitaongea kauli chafu....unajua tena ukilewa...’nikasema na huyu shemeji akacheka, lile cheko la kumkoma nyani giladi...

 Mazungumzo yalikolea maana mke wangu na huyo rafiki yake, inaoenekana walikuwa wanajuana vyema toka huko kijijini wakiwa shuleni, kwahiyo wakawa wanapeana maisha yao ya shule, na mambo ya kijijini, ikawa ni porojo, utani mwingi na vicheko, na ukinihusisha na mimi kiwembe, huku pombe zinanikoroga kichwani mambo yalinoga kweli.

 Mimi kwa muda huo nilikuwa nimekaa kwenye sofa nikiwa natizamana moja kw amoja na huyo mgeni, mke wangu alikaa pembeni yangu na mara nyingine alikuwa akitoka kufanya mambo ya jikoni, nikawa nabakia na yule binti  na mwanya kwangu kama huo ni kosa . ..

Hata hivyo sijui kama huyu binti, alishanijua uzaifu wangu au vipi, kwani alikuwa hatulizi migu yake na ukizingatia kuwa alivaa nguo fupi,....basi wakati mwingine alikuwa akiinua mguu juu ya mwingine na kuacha sehemu kubwa ya mapaja wazi,...hakujali kuwa mimi nipo mbele yake na namtizama moja kwa moja, pombe ikawa inanichanganya kichwani ...damu ikawa inachemka..!

. ‘Shemu sasa mimi naondoka...’  Baada ya maongezi na kupata chochote mgeni akawa anaaga kuondoka, na mimi sikupenda niiache hiyo bahati hivihivi, akili ikanijia, nikasema ;

 ‘Shemeji ngoja nikupe lifti, unasema unakaa wapi....?’ nikauliza. ‘Hapana shemeji leo unatakiwa upumzike na mkeo,....maana umesema siku zote unarudi usiku huoni kuwa leo ndio siku ya kujirusha na rafiki yangu...’akasema.

 ‘Sawa mpe hiyo lifti tu, hakuna shida,.... kwanza mimi nina kazi nyingi leo, kuna minguo ya kufua, kuna kazi za nyumbani sina hata muda wa kuongea sina, mpeleke lakini urudi mapema, ..'akasema mke wangu na aliponioana nikiinuka na bukta ile niliyovaa inanishitaki, mke wangu akatabasamu na kusema,;

Lakini  kwanza tafadhali kabadili hiyo nguo haina heshima, halafu nina wasiwasi na jinsi ulivyo utaweza kuenedesha gari kweli...?’ akasema mke wangu hata bila wasiwasi au wivu.Moyoni nikasema mambo sio hayo...kichaa kapewa rungu, nakaondoka naye. ....
                           
                   *********
‘Shemu, umenikosha sana,... sijawahi kuoana msichana mrembo kama wewe...na leo sijui nisemeje, ...’niaksema.

 ‘Shemeji bwana, mzuri mkeo,....usinitanie, ...hata hivyo shemeji, naona kama umelewa, na mambo unayoyaanza sasa sio mazuri, unajua mkeo ni rafiki yangu mkubwa, sitapenda kujiingiza katika hayo unayoyawaza, namuheshimu sana.....rafiki yangu....’akasema huyo binti.

 ‘Najua ni rafiki yako, lakini urafiki wa kweli ni kuchangiana...au sio, kwanza, hapa nilipo sijui itakuwaje, ....unaona alivyo rafiki yako, kazi nyingi hazimuishi, ...nipo nyumbani lakini naweza nisimuona chumbani hadi usiku....aah, samahani naongea mambo ambayo siyakuongea...’nikainama chini kwa kujifanya naona aibu kuwa nimeropoka mambo ya ndani.

 ‘Unaoan sasa ni pombe hiyo, inakufanya uongee hata siri za ndoa, lakini kama ana kazi nyingi kwanini usimtafutie mfanyakazi wa nyumbani, ili mpate kuwa naye karibu....’akasema huyo binti

 ‘Hataki....hataki kabisa, anasema yeye hana kazi, ina maana kama nikiltea mfanyaakzii yeye atafanya akzi gani...labda anaona wivu kuwa nitamgeuka, ....’nikasema na kweli moyoni niliwazia hilo hilo, kuwa angekubali kuleta mfanyakzi sijui kama ingeliisha mwezi kabla sijamgeuka....nilijua kabisa uzaifu wangu.

 ‘Shemji mimi hapa ndipo naishi,...’akasema tulipofika maeneo ya kwake.

 Ilikuwa nyumba nzuri tu, na sijui humo alikuwa akiishi na nani. ‘Unaishi peke yako humu ndani....?’
nikamuuliza

 ‘Ndio, kwani vipi, ...mimi sina mume, ningeliishi na nani...lakini ni nyumba ya kupanga, mbona nipo hapa siku nyingi tu...’akasema huku akifungua mlango......ilikuwa nyumba nzuri,kubwa ya viumba vitatu, choo jiko, na kila kitu ndani kwa ndani, lakini haikuzungushiwa ukuta....

 ‘Ohh, kumbe unaishi hapa, tena peke yako hata siamini, ....na rafiki yako ndipo anapokuja mara kwa mara,...keshaniambia kuwa anakuja kwako mara kwa mara,....kweli hapa pazuri,... lakini sizani kama unaishi peke yako, suinidanganye nikaja kuuwawa bure...'nikaanza utani wangu huku najibwaga kwenye sofa hata bila kukaribishwa.

'Amini hivyo...nipo peke yangu....sijaolewa, kama ningeliolewa ningelisema naishi na mtu, ukimuona mtu anakuja kuijiiba tu...'akasema.
'Sawa nimekuamini, akija mwenyewe tutapambana maana hukuniambia ukweli....lakini hata hivyo nikiuwawa sio mbaya maana ,inzi kufia kidondani haijalishi au sio,...' nikasema huku nikimwangali yule binti bila kummaliza.

'Shemeji wewe unapenda sana utani....shauri lako...'akasema na kucheka.

'Unajua kama mke wangu ni rafiki yako kipenzi hata mimi natakiwa niwe rafiki yako kipenzi pia ,au sio...?’nikasema na mazungumzo yakakolea hata sijakaribishwa vyema.

Baadaye akaniuliaza natumia soda gani, huku anaelekea kwenye jokofu lake la vinywaji , maana ndani kulikamilika, kila kitu cha bei mbaya, nikajiuliza huyu mwanamke anafanya akzi gani, maana kuvinunua vitu kama hivyo, labda uwe mkurugenzi wa makampuni mengi

‘Shem, unanitania au unasemma kweli, ....aah, mimi sinywi soda kwani mimi ni mwanafunzi...niletee kinywaji baridiiii....kama pesa huna chukua hii kalete vinywaji vya kiutu uzima..., leo nipo mapumziko...sina shida....au wewe unashida...ukiwa na mimi usijali, pesa ipo mingi tu...’nikasema.

Na yule binti hakujivunga aakchukua pesa niliyompa akatoka kwenda dukani na kurudi na kinywaji, ...mambo yakaanzia hapo. Yule binti kumbe alikuwa na mipango hiyo siku nyingi akilini mwake..mimi bil kujua .nikajiingiza kicwha kichwa, na muonja asali haonji mara moja, tukajenga uhusiano wakaribu kuliko maelezo.

 Nyumbani ikawa nikufika na kuangalia kuwa hakuna tatizo,....aah , kwakweli sikuwa mbahili wa kumjali mke wangu, hanakama nilikuwa na mambo hayo ya kihuni, lakini nilihakikisha kuwa mke wangu ana hela ya kutosha...nikihakikisha hilo mbio naondoka kwa huyo rafiki wa mke wangu, na mke wangu hajui kabisa nini kinachoendelea,....
Mke wangu alinichukulia kuwa ni tabia yangu,au kama aliumia, aliumia kindani ndani...aliogopa kumuuliza mwanaume wapi unakwenda, kwanini unalala nje, kwasababu hata nikilala huko anajionea sawa tu, lakini mwishoowe akakerwa akaamua kusema;

. ‘Mume wangu hivi una nini kinaendelea maana sikuoni kama uko sawa, siku hizi hukai nyumbani, hulali nyumbani, kulewa na wewe, na nasikia wewe na wanawake na pombe ndio maisha yako, una mipango gani ya kimaisha wewe mwanaume...na magonjwa siku hizi ni mengi, huoni kuwa utatuletea wadudu nyumbani’akasema mke wangu.

‘Hahaha..leo hii unalalamika eti wadudu, wewe unajua wadudu wewe, ..hahaha leo hii unauliza mipango gani ya kimaisha, wewe si ndio unataka iwe hivi, hutaki usumbufu, hutaki ....mmmh, sasa ndio hivyo nimenasa kwenye ulimbo....hapo sijui kama nitajinasua maana kile nilichikuwa nikitaka nakipata kwa raha zangu....zaidi ya nijuavyo....mke wangu, sijui niseme, ....nini kwanini lakini....hunielewi, nimekufundisha nimekuelekeza, lakini naona unanifukuza ...haya tuone...’nikawa naongea kilevi levi, bila kuchuja maneno yangu.

 ‘Sawa kama umeamua hivyo ...nitafanyeje, maana mimi nimejitahidi kutimiza yale niliyofundishwa kuwa na adabu njema kwako, na kukufanyia kila kitu....labda hayo kuna mambo mengine siyajui, labda hayo unayotaka ya uzungu-uzungu...mimi hayo siyapendelei,...nashindwa kabisa.... lakini hayo sio kigezo...kwasababu wanaofanya ni wahuni, sio wanandoa, mimi naona tabia hizo kama ni ushetani....sioni umuhimu wake..’akasema mke wangu.

‘Yaani mambo ya mke na mume ni ushetani, hivi wewe upoje....wewe unataka nini, kwani nilikuoa uje kunifanyia kazi tu, kama ningelitaka hivyo, ningeliajiri mfanyaakzi wa nyumbani, lakini wewe nimekuoa kama mke wangu, nikikuhitaji wakati wote unitii, ...leo hayo unayaita ya ushetani...kama ni ushetani, achia mashetani wafaidi...sikusumbui tena....unasikia sikusumbui tena....’nikasema huku napepesuka.

‘Samhani mume wangu kama nimekukosea, sikuwa na maana hiyo...’akajitetea mke wangu.

‘Samahani nikuombe mimi kwa kukusumbua....ninachosema kuanzia sasa, sikusumbui tena, na wewe usiniulize kuhusu maisha yangu ya ushetani...’nikasema na kuondoka, sikujali machozi yaliyokuwa yakimtoka, maana kila nikimfikiria rafiki kimwaan anayejua kumapagawisha mwanaume, nakuwa kama nimepuliziwa dawa, ni mbio mbio kuelekea kwake.

 Siku moja rafiki yangu wakazini akaniuliza , kuhusu mabadiliko niliyokuwa nayo, alianzia mblai kibusara, na mishowe akaamua kunipasulia wazi. Sijui kwanini , kwa muda kama ule, nilikuwa siambiliki, akili yangu iibadilika kabisa, na kama mtu alitaka tukosane aniuliza kuhusu maisha yangu na huyo kimwana;

 ‘Rafiki yangu huko unapokwenda ni kubaya...hebu niambie, una mke mzuri sana nyumbani, kila mmoja anatamani awe na mke kama huyo, mtulivu, mzuri, na tabia njema kabisa, wewe unaruka na viruka njia, kila wikiendi upo Zanzibar, unatesa na huyo kimwana, unamjua huyo kimwana kweli, wenzako pale walishachoka, sasa wewe unachukua makombo....unatafuta kifo muda sio wako...’akaniasa rafiki yangu na hapo akaupalia mkaa.

 ‘Na wewe umeanza kunigeuka,.... yaani mpenzi wangu unamuita kiruka njia, Malaya aliyeshindikana, hivi wewe mkeo wako naye unamuonaje yule, ....hahaha, hukumbuki kuwa mimi nilishachezea nikachoka ndio ukamuoa...au hujui hilo....nakuambia sitaki kunifuata fuata katika misha yangu....na tusijuane..umenielewa, tusijuane....’nikamwambia.

 ‘Sawa wewe ni rafiki yangu na tumetoka mbali, najua huyo mke wangu uliwahii kuwa na urafiki na wewe kama unavyodai kwa kipindi hicho, sio mbaya, lakini kwa sasa nimemuoa katulia, ni kawaida tu ya maisha...hilo halinitii shaka, ila nakupa kama ushauri, kama rafiki yangu...kuwa mambo yako sio mazuri ..na kuna tetesi, huenda ukasimamishwa kazi kwa muda, nakudokezea tu...’akasema rafiki yangu huyo.

 ‘Nani anajali,hayo si majungu yenu, mtaishia hivyo hivyo, tatizo lenu mumejaa wivu, .... kama pesa ninazo.....’nikasema na kuondoka kwenda nyumbani, ili baadaye nielekee kwa kimwana wangu....hapo nilikuwa nimeshachukua mshahara wote , na madeni juu, nilikuwa sina wasiwasi maana kama meneja nilikuwa na nafasi ya kuidhinisha malipo kabla ya mshahara,.... nani ataniuliza, nilikuwa nimejisahau kabisa.

Wakati naondoka hapo, hata kabla ya muda wa kazi mawazo yangu yalikuwa ni kutumia , kwani tulishapanaga kuwa jumamosi , jumapili tutashinda Zanzibar na kimwana wangu...tunatesa, tunatumia, tumia ukiwa nazo, maana maisha ni mafupi...nikawa najiimbia huku nakanyaga gia za gari lifike haraka...

Nilipofika nyumbani sikumkuta mke wangu, nikajua kaenda sokoni, nikabadili nguo kwa haraka na kuchuku `briefcase yenye nguo zangu maalumu, nguo za safri, huyo hadi kwa kimwana wangu, na huko nilimkuta ananisubiri kwa hamu, kuniona tu akanikumbatia na kabla sijakaa sawa akaanza kudai pesa za kodi ya nyumba, nikampa, mara pesa alizokopa kwa ajili ya kutengeneza nywele nikampa....baadaye tukajipumzisha ili kesho tudamkie safari ya Zanzibar.

‘Nani anagonga mlango ...aah,....siulisema hakuna mtu wakutusumbua, vipi tena.....’nikasema huku nikiwa nimelowa jasho chapachapa...na muda huo tulikuwa kwenye masofa, hatukutaka kabisa kuingia chumbani kwasababu ya joto, ....dunia niliiona yangu kwasababau nipo na kimwana anajua raha za kila namna....

'Achana nao unawajali hawo wambea,... labda ni hawa marafiki zangu wanaotuonea wivu....acha wagonge mpaka wachoke, wewe sogea huku, na ulivyolowana...duuh,utafikiri, ulikuwa unakimbiz.....’ na kabla hajamaliza kusema mlango ukafunguliwa,....nilipogeuza kichwa na kuangalia mlangoni, macho yakanitoka pima,....sikuaminii ,kwani aliyeingia mwanzoni ni mke wangu, ...aliyefuatia ni mjomba, na pembeni yupo mama na baba....kila kitu kilinywea.....

Je itakuwaje....kama ingelikuwa wewe ungelifanyeje, maana kila kitu kipo wazi.

WAZO LALEO: Siri moja ya kujenga mahusiano mema ndani ya ndoa ni kujadiliana, ....na hasa pale kunapokea sintofahamu yoyote, kwani ndoa hujengwa na wandoa wenyewe .

Ni mimi: emu-three

Tuesday, March 27, 2012

Hujafa hujaumbika-11



Basi niakaanza maisha ya ndoa,maisha ambayo sikutarajia kuwa yatakuwa hivyo, mwanzoni nilijua ni swala la muda tu,maana kila mmoja anapoingia katika maisha haya anakutana na mitihani mingi, ikizingatia kuwa mumekutana kila mmoja na tabia yake, na pia kila mmoja na,hulka na hata imani tofauti,....lakini iwavyo mwisho wa siku mnakuja kukubaliana na kuwekana sawa, ndivyo nilivyokuwa najua.

Lakini nilikuja kujau kuwa mambo mengine yakijijenga ukiwa mdogo, yanweza yasiondoke kabisa akilini,....kuna watu wanajikuta wamejijenga na hulka na tabia fulani ambayo hawapendi, kuibadili, kutokana na malezi, au maisha uliyokulia, ....ndivyo alivyokuw amke wangu, na huenda ndivyo walivyo wengi, ...maana nilijitahidi kila jambo kuliweka sawa, kufundiha na kuelekeza,lakini kuna mengine nilishindwa kabisa....’akaendelea kuongea rafiki sikutaka kumkatiza, ....

Siku ya fungate iliisha nikiwa ansema huu kwa vileni mwanzo, nitamuelekeza na ayabadilika tu, nikawa namchukulia kidogo kidogo kama mtoto anayeanza kutambaa, hadi kusimama....nikukumbuka maisha aliyokulia ni yale ya kkijijini haswa, ...vitu kama umeme, maisha ya mjini na mazingira yake ni mwazo kukutna nayo....sikujali sana.

‘Sikiliza mke wangu huku ni mjini na vitu vingi ni tofauti sana, huku usitumie kuni,...na kamani lazima tutaumia mkaa, lakini sio lazima kwasababu kuna umeme....’nilimwambia siku moja akiwa kanunua kuni...tulipofika tu...

‘Mimi nimezeoa kutumia kuni...’akajitetea.

‘Hapana nitakueleekza jisni gani ya kutumia umeme,usipate taabu...’nikamwambia, lakini alijaribu kunipinga kumwingilia mambo ya jikoni, akasema mwanaume haruhusiwi kuingia huko.

‘Huku ni mjini...acaha yale mambo na tabia za kijijini,.....lakini hata hivyo usijali, kwa mfano nikuulize je ukiumwa nani atapika..?’ nikamuuliza.

‘Ni hapo nikiumwa, na utamuita ndugu yangu aje akusaidie kupika, lakini mwanaume haruhusiwi kuingia jikoni, au kushika vyombo....au kufagia ndani....sikubali kabisa,...hapo usiniingile...’akasema.

Nikasema kimoyomoyo, hujakutana na majirani, akina mama wenzako watakufundisha na ukijua hayo utabadilika tu, lakini nikumabie ukweli mke wangu huyo hakupenda kabisa kukaa na kuongea na mjirani mpaka wakawa wanalalamika, ....sikuwajali sana kwa hilo, maana ni heri kwa namna moja au nyingine.

‘Mke wangu mbona unaweka chakula cha moto kwenye jokofu....?’ nikamuuliza siku moja, kapika ugali wake vizuri na kuuweka kwenye sahani, lakini mimi nilikuwa sijawa tayari, na akaona ugali ule utapoa, mara nikashangaa unaweka ndani ya jokofu.

‘Si ili kisipoe....’akasema huku akijiamini kabisa.

‘Hapana hiyo ni kwa ajili ya kupoozea vitu, ....huoni humo kunatoka ubaridi....na ukiweka vitu vya moto, unaweza ukaliua kabisa hilo jokofu...’nikamwambia, na haraka akakitoa kile chakula. Nikawa nasema kimoyomoyo huyu atajifunza haraka tu. Lakini ilikuwa unafundisha hiki kesho hiki kimeharibiwa,....mwisho nikasema itakuwaje,maana mimi nitakwua kazini,je nani atamueleekza hiki au kile na vyombo vingi nilivyokuwa navyo ni vya umeme.

Kwa mwezi mmoja, vyombo karibu vyote vya umeme vikawa vimeharibika, na siku moja karibu nyumba nzima iungue na moto, aliwasha `heater’ kwenye ndoo kwa ajili ya maji ya kunywa akaondoka kwenda sokoni, huko akachelewa, maji yakachemka na ndoo ikayeyuka,....fikiria chumba kilikuwaje, kilikuwa kama kuna mvuke umejaa ndani, ...baadhi ya majirani wakaona moshi namvuke ukitokea ndani, ...lakini kwa muda huo mke alikuw hayupo na mlango umefungwa...

‘Sasa tufanyeje maana kunaonekana kuna hitilafu ya umeme humo ndani..na moto ukitokea hapo utatuathiri na sisi nyumba za jirani.’akasema mjumbe.

‘Tuvunje mlango....’akashauri mtu, na bahati nzuri nikatokea, nikaingia ndani..kulikuwa hakuingiliki, lakini nikazima kwenye eneo la kuzima umeme wa nyumba nzima ikawa ndio nimeokoajahazi, ...yalitoke mengi lakini yote nilijua ni kwanini,kwahiyo sikujali sana.
Kitu ambacho kilikuwa kikiniumiza sana ni tabia ambayo hakutaka kabisa kuibadili, tabia ya maisha ya ndani ya mke na mume, yeye alichukulia alivyolelewa kabla ya ndoa ndio hivyo hivyo,...mwili wake ni wake,haruhusiwi mtu kuuona,kuugusa ....vitu kama hivyo, .... nikamshauri na kumeelzsea kuhus maisha ya mke na mume, lakini aliishia kunicheka na kusema hizo ni tabia mbaya za wanaume, hazitaki kuzisikia,

Nilijaribu hata kumletea mikanda ya video ili ajifunze maisha ya ndoa yalivyo, ...alilaani na kulani, kuwa nimemletea ibilisi ndani, ...akawa hataki kabisa hata kuziangalia...

‘Mambo gani hayo ya kishetani....kama unataka kuangalia kaangalie huko huko ..mimi sitaki kuangalia, hizo picha zinazofundisha ubaya...tangu zamani nimekatazwa hayo...kama unataka kuangalia ngalai mwenyewe....’akawa anasema kwahasira.

‘Sikiliza mke wangu, maisha tunayoishi sasa ni ya mke na mume , na hayo ndiyo yanayotakiwa mke na mume wayafanye, sio mambo ya kishetani kati ya mume na mke,....’nikawa namshauri,lakini akawa hataki hata kusikiliza. Nikajiuliza nitumie ukali, labda kazoea kufokewa na kutumia nguvu, ...hapana nikakumbuka maisha aliyowahi kuishi ya kukaripiwa na kutumwa kama punda, ...sikutaka kumrudisha huko.

‘Sikiliza mke wangu, unajua wewe sio mtoto tena, wewe sio yule uliyekuwa ukitumwa kama punda,hapa unatakiwa ujitume mweneywe ujua kuwa hii nyumba na vilivyopo hapa ni vyako, na pia unatakiwa ujifunze jinsi gani ya kuishi na mume wako, mimi sio kaka yako tena, mimi sio mtu baki, mimi ni mume wako ambaye una haki zote, mwili wangu na mwili wako ni halali ya kila mmojawapo iulambiwa kipindi tunafingisha ndoa pale kwenyeule ukumbi....’nikawa natoa darasa.

‘Ule ukumbi wa gerezani kwa watu waliochanganyikiwa, ndio maana walikuwa wakiongea yale mambo yasiyofaa, ...kwasababu wanaokaa huko ni wakosaji siju na sisi tulipelekwa kwa bahati mbaya,....kama ungelifungia hiyo harusi kwenye nyumba za ibada au nyumbani usingelisikia hayo, mimi pale nilitamani kuondoka, maana watu wazima waanongea mambo machafu....’akasema na mimi hapo nikajikuta nikikumbuka siku ile ilivyokuwa....siku ya harusi ya kiaina yake.

*********

‘Jamani sio mara ya kwanza, mjue kuwa hata wafungwa wana haki zao, sio kwasababu umefungwa ndio huruhusiwi kuoa au kuolewa, ila ukioa au kuolewa, bado una majukumu yako, ya kutumikia kifungo chako, utakachobahatisha na kufunga ndoa, na mke au mume wako watakuwa wakija kukutemebelea, na tunajaribu kutafuta njia za kisheria ili mkitemebeleana kuwa na faragha kidogo...’akasema askari mmoja ambaye ni mkuu wa kile kituo, na watu wakashangilia.

Mimi kwa muda ule nilikuwa sijaelewa nini kinachoendelea maana niliamshwa asubuhi, na askari akaniambia nijiandae maana leo ndio siku yangu ya kesi, ....

‘Hapana umekosea fande sio leo...’nikamwambi nikiwa na uhakika kwani tarehe zote za kesi yangu zilikuwa kichwani.

‘Ina maana unanifanya mimi mjinga, unampinga afande, umeanza kuwa na kiburi au umeshazoea kukaa hapa ndio maana unakuwa na kiburi, uliktakwia uwe huko gereza kuu, huko ungekoma ubishi, na ulivyo laini laini, ungegeuzwa chakula cha ...’akasema yule askari huku akiniangalia kwa nyodo.

‘Afande sio kwamba nakukaidi ila nakumbuka kabisa tarehe yangu ya kesi sio leo, na siku mblili zijazo....’nikamwambia.

‘Sasa sikiliza nenda kaoge, ujiandae naenda kukuletea nguo maalumu, kuna nguo maaumu zimeshaletwa hapa, kwa ajili ya kesi yako hiyo, kama itaamuliwa vinginevyo, ujue hufiki huku tena, moja kwa moja gereza kuu..unanisikia, nakupa dakika kumi tu za kuoga,unaoga kama mwanaume, sio kujirembaremba hapa...’akasema huyo askari na kuondoka.

Mimi sikufanya ubishi nakaelekea sehemu yakuoga,na bahati nzuri kipindi hicho kulikua hakuan mahabusu wengi, hakukuwa na foleni,au ile ya kuoga kundi zima pamoja, ...nikamaliza kuoga na kutoka, ..n hat akabla sijafika kwenye chumba cha mahabusu, mara akaja yule askari akiwa kashikilia nguo.

‘Haya vaa hizi , una bahati kuwa wewe unavalishwa suti...unajau unavaa suti ili ukisimama mbele ya hakimu asione kuwa mnanyanyaswa, na hukumu ikitolewa, unabadili suti, unavaa suti maalumu za kifungwa, ndivyo ilivyo.....’akasemana kucheka.

‘Sawa fande nashukuru sana....’nikasema na kuzichukua ziel nguo...’nilishangaa ni inafanana kabisa na moja ya suti zangu nilizonunua huko Ulaya, ni hzi zilikuwa maalumi kwa ajili ya harusi......’niliiangalia ile suti nikasemakimoyomoyo, labda ni kufanana tu, nikavaa.

‘Umependeza kweli mfungwa...hata hivyo utaivaa kwa masaa, ikifika jioni utakuwa na sare maalumu, ...sare na namba yako ...unasikia mfungwa....utakuwa ukiitwa kwa namba...mfungwa namba fulani....’akasema huyo askari, ambaye kila mara anapokuja hapo anaishia kunisimanga utafikiri mimi nina kosa.

‘Sawa afande , lakini ipo siku utagundua kuwa mimi sina kosa kabisa....hayo yote ni maonevu....’nikasema nay eye aliishi akucheka.

‘Kwani mwizi au muuaji anayakubali makosa yake....sheria ndiyo itamuhukumu,lakini katu muuaji hakubali kosa lake,labda awe amechanganyikiwa....haya upo tayari, kaa pale usubiri...’akasema huyo askari na mimi nikatii na kwennda kukaa sehemu ya kusubiria wageni. Nikisubiri nini kitafuta baadaye, maana huku ni mwendo wa kusubiri,kila kitu mpaka uambiwe....

Toka asubuhi nimekaa pale hadi mchan unaingia, ...ilichosha na nikajikuta nasinzia, na mara likaja gari, gari, ni gari la mkuu wa kituo kile, likasimama,na akatoka askari aakmfungulia mkuu wake, na mara akatoka mkuu akiwa na suti yake safi, akanijia na mimi haraka niaksimama.

‘Wewe ndiye Msomali.....?’ akaniuliza.

‘Ndio mimi, mtoto wa Msomali...’nikasema.

‘Kwaini uitwe Msomali , wakati wewe ni Mtanzania...?’akauliz ahuku akinikagua na ile suti niliyovaa, ilishaanza kunipwaya, maana siku nilizokaa mle mahabusu ilikuwa ni adhabu tosha.

‘Hata mimi sijui kwanini, ila najua sisi ni Watanzania...’nikasema.

‘Nyie ndio tunawakaribisha hapa nchini halafu mnakuja kufanay vurugu...dawa yenu inachemka...’akasema kwa sauti ya kiaskari. Mimi sikujibu kitu nilitulia kimiya akamgeukia askari na kusema;

‘Huyu tunaondoka naye, kamanilivyokuambia, kila kitu kipo tayari,...’akasema na kunigeukia mimi;

‘Unasikia wewe Msomali, natakuita Mtanzanai, sitaki hilo jina la Msomali sawa....ni hivi tunakwendaleo kusikiliza kesi yako na hukumu itatolewa huko huko, ukitoka huko ama unakwenda nyumbani kwenu au unelekea gerezani, sitaki kukuoan tena kwenye mahabusu hii, .....’akasema na mara akaingia ndani ya gari.

Yule askari akanisogelea na kunisukumi kwenye gari, akasema; `haya ingia humo ndani ya gari, una bahati sana kupanda gari la mkuu....lakini ni mara ya kwanza na ya mwisho, utakuwa ukipanda lile gari kubwa lililozungushiwa nondo..kwaheri mfungwa...’akasema kufunga mlango.
Tukaondoka pale na gari likiw aan mwendo kasi, na nilishangaa, maana nilijua kwua tuanelekea mahakamani, lakini lakini ule mwendo wakasi uliishia kwenye ukumbi mmoja unaoitwa ukumbii wa magereza...na gari likasimama’

‘Haya shuka tumefika, kwani kesi yako itafanykai humu ukumbuni kwasababu za zarura...’akasema yulemkuu, nikatoka kwenye lile gari na askari mmoja akanishika mkono kuiongoza ndani ya ukumbi....

Nilishikwa na butwaa maana niliona kama naota, kwani kilichonipokea wakati naingia mle ni vigelegele na shangwe....

‘Hii maana yake nini...?’ nikauliza.

‘Kwani ukiona hivi kuna maana gani...?’ akaniuliza yule askari.

‘Kuna maana kuwa kuna harudi, au shughuli fulani....ndio najiuliza harusi ya nani?’nikauliza kwa mshngao.

‘Usijali utayajua mbele kwa mbele, wewe twende huku, maana mimi ndiye nitakuwa mlinzi wako wa karibu na pia nitakuwa mhusika wako wakaribu vile vile, ....’akaniambia yule askari akiniongoza hadi kwenye viti vilivyoopo mbele, huku nikizidi kushangaa, mbona napelekwa sehemu ile maalumu ya wageni mashuhuri, ....

Nilipokaa tu mara vigelegeel vikatanda ukumbini, na mara wakaja wakuu wa dini , wakasogea mbele yangu na mara vigelegele tena kwa shangwe na vifijo, kwani kulikuwa na watu wengine wanaingia, na kwenye kundi hilo nikamuoana binti harusi kavalishwa na kufunikwa mwili mzima...sikuweza kujua kuwa ni nani huyo bibi harusi, na ni nani muoaji...

Mara nikaitwa pale waliposimama wale watu wa dini wa kufungisha ndoa, nikasimama huku nikiwaza mengi, kwanini nihusishwe nah ii ndoa,...lakini kabla sijauliza yule muendeshaji wa shughuli akasimama na kusema;

‘Hii ni harusi ya kipeke sana, maana mtu anasubiri kuhukumiwa, ama aende jela au arusii uraioanai, alkini hukumu yake inakuwa kifungo cha ndoa.....’mara watu wakacheka na kushangailia.

‘Ndugu yetu mpendwa, kwanza tukupe pole sana na mateso ya mahabusu, ndio ukubwa huo, dunia hii kabla hujafa hujaumbika....huwezi jua, leo unaamuka mzima jioni kilema, leo unaamuka tajiri, jioni masikini, ...na pia unaweza ukaaamuka mfungwa na baadaye unakuwa bwana harusi....’watu wakshangailia.

‘Hili limefanywa kinamna, ulitakiwa kuwepo mahakamani asubuhi, lakini kwa dharura, hukuwepo ...tulifanya hivyo makudi, n ahata hivyo haikuwa haja, ...hukumu yako leo ni hapa, wewe kwa mujibu wa utaratibu, unahukumiwa kifungo cha ndoa...kazi kwenu watu wa dini mhukumuni....
Vigelegele na shangwe vikatawala ukumbini,..... na mara akanisogelea mtu wa dini na kuniuliza maswali mengi, lakini sikuwa mvumilivu, nikauliza kwanini yote haya yanafanyika na hata simjui huyo bibi harusi...

‘Humjui bibi harusi, unatucheeksah kweli,....wewe si ulitaka mwenyewe ukapendekeza kuwa unataka umuoe binto Yatima. Ukiwa huko huko mahabusu....au umesahau....’akasem yule mtu wa dini na mara akaja mjomba na ndugu zangu wengine

‘Tumefanikiwa....alikuwa keshapanda basi kuondoka kwennda kijijini....’akasema mjomba

‘Bahati kubwa sana, ingeshindikana leo ingekuwa jambo jingine, mambo yanakwenda shwari maana hata huko mhakamani wamesema hakuna tatizo, inaweza kufanyika maana muuaji keshakamatwa na kukiri kosa.

‘Ni nani huyomuuaji, aliyenifanya niteseke kiasi hiki....’nikauliza kwa hamasa

‘Hayo kwasasa hayakuhus.u la muhimu ni kufunga ndoa yako....haraka mana unahitajiwa mahakamani saa nane, kusikiliza linaloendelea kama utaendelea kushkiliwa aua utaachiwa...’akasema yule askari ambaye alikwua habanduki karibu yangu.
Na hapo moyo ukatulia na harusi ikafungwa...

*******

Nikiwa katika moja ya darasa maalumu la kujaribu kumfundisha mke wangu, na leo ilikuwa maalumu kwa kutoka, ilikuwa kazi kweli kumshauri...hasa ilipofiki sehemu kuwa akaziweke nywele zake tofauti na alivyozoea, yeye anapendelea kusuka tu,..

‘Nywele zangu haziweki hayo mauchafu..kamwe sitaki....’akasema na kukataa kata kata, lakini leo nilizamiria nikasema kwa ukali;

‘Hapana leo lazima ukabidli nywele zako kidogo, ili uone tofauti...’nikamwambia kwa sauti ya ukali kidogo. Akainua uso kuniangalia, hapo sikucheka, kama kawaida yangu, akaona kweli nimezamiria, akasema kwa upole;

‘Haya, kama ni lazima sawa,lakini sipendi kaisa,...’akasemakwa shingo upande.

‘Nikampleka kwenye saluni ya karibu, na kumuacha hapo,baadaye nikampitia kumchukua, kweli alibadilika,na nilitaka awe hivyo kwasababu tulialikwa kwenye sherehe moja, ....huwa hapendi kutoka, na akitoka huwa kajitanda khganga zake, ni nadra sana kumuona katembea kichwa wazi, ...leo nikaona nijaribu kumfanya aonekane tofauti, na kweli huko saluni walimbadili..

Kweli leo alikuwa tofauti, sio yule binti aliyekuwa kakonda, anatia huruma,...mwili wake ulishakuwa msichana mrembo, nilijaribu kumbadili hivi ili nione atakuwaje, mengi aliyakubali,

lakini kuna mengine hakukubali kata kata...na tulivyorudi kwenye hiyo sherehe tukakaa faragha huku nikijaribu kuwa karibu naye, na hata kumkumbatia,.... hakunisukuma kama alivyozoe, nik
amwambia;

‘Mke wangu u mzuri kweli, na leo umekubali ukazitenegneza hizo nywele zako umependeza kweli kweli, ....’nikamsifia.

‘Mimi nimefanya kama ulivyotaka....kwa leo tu, lakini sipendi kutengeneza nywele zangu kuwa hivi ..napenda kusuka tu, na kesho naenda kusuka, sitaki kabisa kuonekana hivi naonekana kama muhuni....’akasema huku akijiangalia kwenye kiyoo nikiwa karibu huku tunajiangalia pamoja kwenye kiyoo, kweli alikuwa tofauti, binti mrembo.

‘Unajua mnapoona mnakuwa kitu kimoja, mke na mume ni mwili mmoja, mwili wako ni wangu na wangu ni wako’nikamwambia na hapo nikawa nimemuuzi akasogea pembeni na kuongea kwa hasira;

‘Mwili wangu ni wangu sio wako,...mimi na heshimu mwili wangu, na sio wa kuitizamwa ovyo, mimi sio muhuni wa kufanya mambo ya kihuni....kama unahitaji wahuni unaweza kwenda kuwatafuta mitaani, lakini sio mimi....’nilishangaa alivyokasirika na kuondoka kufanya kazi zake za ndani.
Unajua mimi ni mvumilivu sana, na ni mwalimu mnzuri, lakini mambo mengine nilishindwa akbisa kumshawishi huyu mke wangu,yapo niliyofanikiwa , lakini sio maisha ya ndani ya mume na mke, ..mke huyu hakukubali kabisa, ....

‘Utabadilika tu ni swala la muda....’nikasemakimoyo moyo.
Muda ulipita na miaka ikapita, hakukubali kubadilika kwa maswala ya ndani, nikasema nifanyeje nitafute mwanamke aje amfunde ndani, au nifanyeje...nikaongee na shangazi yake aje amuelekeze,labda ananiogopa mimi, lakini mimi ni mume wake, nitachekwa kama nikishindwa hilo...nikawa katika mitihani kama hiyo.

Mengine hayafai hata kusema , maana ikifika usiku ilikuwa kama vioja, mwenzangu anahakikisha kuwa taa zimezimwa, kava nguo zake, na hataki umwangalie....na mambo mengine ni mshie mshike....nikajaribu kila mbinu za kumfundisha, lakini haikubadili kitu....lakini hata hivyo tukabahatika kupata mtoto, ...huta baada ya kupta mtoto tabia yake ya ndani ilikuwa hivyo hivyo, ...licha ya kuwa mambo mengine alijfunza kama kutumia umeme na kazi za ndani.

Kazini kulikuwa na sherehe za mara kwa mara, ukumbuke mimi ni meneja katika moja ya vitengo huko kazini,kwahiyo wakati mwingine nahitajika kuhudhuria sherehe na mke wangu, mke wangu hakukubali sherehe kama hizo, nilipompeleka mara moja akaona kulivyo akasema yeye hararudia tena.

‘Mke wako hatumuoni bosi,vipi ni mke wa ndani tu...’akauliza mmoja wa mabinti tuaofanya nao kazi.

‘Ana kazi zake nyingi, sio rahisi kuja kwenye sherehe zetu...’nikajitetea.

‘Basi mimi nitakuwa namuwakilisha kama hutojali...’akasema huyo binti, alikuwa binti mrembo, na kutokana na kazi zetu tukawa tumezoeaan sana, huwa kama hakuna kazi tunaongea sana mambo mengi,.....na kwahiyo tukajikuta tupo karibu sana na yeye haat ikawa tunakwenda kula pamoja na jioni nampitisha nyumbani kwake.

Wakati mwingine nilikuwa najiuliza kwanini binti mnzuri kama huyu hajaolewa, na katika maongezi yetu siku moja nikamuuliza...

‘Mimi sijawa tayari kuishi ndani kama mke, ...kuolewa sio jambo la kukimbilia, hata hivyo, kila jambo lina muda wake...’akaniambia siku moja nilipomuulizia. Na sikutaka kumdadidi sana kuhsu hilo, kwani nilikuwa nikikwepa kujiingiza mweneywe kichwa kichwa...naiheshimu ndoa yangu.

Siku zilivyozidi kwenda nikaanza tabia ya kunywa sana pombe, hii nilianza kama mchezo,ili nikirejeanyumbani, nisiwe na mawazo mengine zaidi ya kulala, sikupenda kumsumbua mke wangu, kwani jioni alionekana kuchoka sana kwasababu ya kazi za nyumbani, na kama nilivyoelezea awali, hakuwa mcheshi sana wa kuliwazana, hayo kwake aliyoaona kama uchafu, ...au uhuni kama alivyopenda kusema.

Sio kwamba nilikata tamaa ya kumfundisha, nilijitahidi lakini ndio hivyo tena, ilionekana kashikili amsioamo wake, basi ikafika mahali nikaona bora niwe naknywa sana, nikirudi simsumbue, ni kuuchapa usingizi, kumbe nilikuwa nikjiharibu bila kujua, ....maana ili ufaidi pombe , unahitajika uwe na wenzako, na vyema zaidi wakawemo marafiki wa jinsia tofauti pembeni, nilianza kama mchezo na baaadaye ikawa mazoea.

Siku moja, kwenye sherehe zetu nilikunywa sana, ...na wakati tunarejea nyumbani ikabidi nimchukue huyo binti nimpitishe nyumbani kwake, kwasababu ilikuw anjia moja, tukafika kwake, na yeye pia alionyesha kulewa , hata wakati akiteremka kweney gari langu, akawa anapepesuka, ikabidi nimsaidia kumshika mkonoo hadi nyumbani kwake anapoishia.

‘Yaani najisikia vibaya hata kupanda kitanda siwezi, naomba tafadhali unifikishe kitandani, halafu ndio uondoke..bosiii, tafadhali....’akaniomba, nikafanya hivyo,.... lakini tulipofika kitandani maombi mengine yakaongezeka.

‘Yaani unaniacha nikiwa na nguo bosi, nisaidie kunivua...viatu, gauni...na....tafadhali bosi usiondoke...siwezi kabisa kukaa peke yangu, najiskia vibaya, ...’nikakamsaidia hili likaja jingine, na hapo ilikuwa kosa,...kilichofuata hapo ni jogoo la asubuhi ndilo lililonifanya nizindukane...

‘Oh, kichwa kinaniuma...’nikalalamika huku nikishika kichwa,kweli kilikuwa kikiuma saana.

‘Pole sana mpenzi inabidi ukazimue...’sauti ya kilevi levi iliongea pembeni yangu, na niliposiki hiyo sauti, nikashituka, maana kauli na sauti kama hiyo sijawahi kuisikia toka kwa mke wangu...nikakumbuka,....nilikurupuka hapo kitandani na kumbe looh, nipo uchi wa kuzaliwa, haraka haraka nikavaa nguo, mbio nikatoka nje, ....nilifika nje gari halipo....

NB:Tuishie hapa kwa leo, lengo ni kukuonyesha jinsi nilivyoanzakubadilika na matokeayake yatakuwaje, tuwepo sehemu ijayo. Kama nilivyosema kisa hiki na mahsusi kwa wale wandoa, watarajiwa na wanaopambana na misuko suko ya ndoa...tusaidieni kwa maoni.

WAZO LA LEO: Kuuliza sio ujinga, kama unataka kweli kujua, ni ukijua fanyia utafiti kua ni kweli au sio kweli. Mara nyingi tunachukulia tetesi au mambo mengine juu kwa juu, kama zilivyo, na matokea yako


Ni mimi: emu-three