Ni mimi: emu-three
Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha
Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..
Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.
MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.
TUPO PAMOJA DAIMA
![]()
Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;
https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:
https://www.facebook.com/diaryyangu/
`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;
Friday, March 30, 2012
Hujafa hujaumbika-14
Ni mimi: emu-three
Thursday, March 29, 2012
Hujafa hujaumbika-13
'Hivi wewe unaongea nini...'akasema mama.
'Ndio mama, huo ndio ukweli, ...ujue kuwa huyo mwenzangu keshaachika, na mimi ndiye mke halali....hukusikia alivyosema mume wangu ...au rudi vyema wasikie...sio nashnikiza iwe hivyo, hapana ila kauli ya mume wangu ndiyo ya msingi...’akasema mke wangu huyo mpya.
Ni mimi: emu-three
Wednesday, March 28, 2012
Hujafa hujaumbika-12
‘Mume wangu mbona siku hizi unalewa kupita kiasi na hata unaamua kulala nje, una tatizo gani...ni kazi gani hizo za kulala nje, na ukirudi umelewa chakari, kazi gani utafanya ukiwa umelewa hivyo...?’ akaniuliza mke wangu huku akionyesha uso wa huruma, nilimkwepa kumwangalia, maana ukimwangalia usonii utamuonea huruma.
‘We acha tu, endelea na shughuli zako, maana hata nikikuambia utakimbilia kusema ni mambo ya kizungu....maisha ya ndoa nayaona kwagu ni mitihani, sasa tena watu wananiibia gari langu ...unajua mke wangu sikujua itakuwa hivyo...lakini sio kosa lako, labda nijilaumu mwenyewe...’nikasema huku nikipepesuka
‘Mbona sikuelewi yaani ulevi wako unanilaumu mimi....kulewa ulewe wewe, na lawama zinakuja kwangu..hapana hizo lawama sikubali,...acha ulevi kwanza kama unataka uwe msafi,...mtegemee mungu, kupoteza gari sio kupoteza kila kitu,watu wanapoteza magari, wanapata hasara kubwa sembuse wewe gari moj tu...’akanishauri mke wangu.
Kwakweli kama kuna kitu kiliniuma katika maisha yangu ni pamoja na kuibiwa hilo gari, sikuamini, maana nililitafuta mpaka mfukoni, ...hata nilipofika kituo cha polis kujieleza, bado nilikuwa najikagua mfukoni, ....
Unajua nilipokuwa nikisoma Ulaya, nilihangaika sana,...kubeba maboksi na kazi za ajabu ajabu, ili kupata pesa za ziada hadi kununua hilo gari, na lilikuwa sehemu yangu ya kujivunia kuwa na mimi nilifika ulaya, sasa nitapata wapi gari kama hilo, maana bei yake kubwa sana, pesa ninayopata haitoshi...
‘Chukua mkopo angalau upate gari la kawaida....’akanishauri mmoja wa marafiki zangu na wazo lake nikalikubali, na kweli haikuchukua muda nikapata mkopo na kununulia gari, ambalo haliwezi hata kufikia nusu ya lile gari langu liloibiwa, lakini angalau niliweza kusema nina gari, na kipindi hicho kampuni yetu ilikuwa ikiyumbayumba kibiashara....
Biashara ilisuka sana, na hatukuweza kupata masoko ya bidhaa zetu kwahiyo mameneja walitakiwa wajitegemee kiusafiri ili kubana matumizi.
Gari likaniweka katika hali yangu ya kawaida,....ukizoea gari inakuwa shida.....basi nilipolipata ratiba yangu ya kurudi usiku wa manane ikaendeelea, na wakati mwingine nalala nyumba za wageni,na kubadilisha wasichana kama nimechanganyikiwa hata ofisini wakaniita kiwembe, binti hakatizi mbele yangu, lazima nitamualika chakula cha usiku....yaani mungu tu kasaidia na kunikweepsha na huu ugonjwa, sijui...
Mshahara ukawa hautoshi ,kwasabbu starehe zilizidi, kila siku nipo kwenye mahoteli makubwa, kwenye mabar,madanguro....na ukumbuke kuwa nilikuwa nakatwa makato ya madeni, matumizi yangu yalikua hayakadiriwi, na kila siku naomba mshahara kabla ya wakati, ....Nikaanza kuandamwa na barua za maonyo, lakini ilikuwa sikio la kufa halisikii dawa...!
Siku moja wakati nimerejea nyumbani nikakuta kuna mgeni...sikujali sana, nikapitiliza hadi chumbani, siku hiyo nilitaka kujipumzisha nyumbani,....kwani nilikuwa nimeutwika kisawasawa...na sikutaka kumsumbua mke wangu, ....lakini baadaye nikaona sio vyema nikamuita mke wangu chumbani...Alipofika, nikaanza kumshikashika, ....
‘Aaaah, bwana umeanza mambo yako ya kihuni huni, ....,huoni kuna mgeni varandani...na mchana huu umelew hivi...mungu wangu...haya jisaahulishe kidogo....’akasema mke wangu.
‘Mgeni gani zaidi ya mke wangu, mimi...ni mume wako, nikikuhitaji hata kama kuna wageni inabidi utafute mbinu waondoke....sikiliza mke wangu, nimevumilia weeee, sasa nachoka, ....niende wapi, nikatembee na machangudoa..mmh, njoo hapa....’nikawa naongea sauti ya kilevi, kweli pale akili yote ilikuwa ikinuka pombe nikamsogelea mke wangu naye akanikwepa na kusema.
‘Hebu punguza sauti hujui ni nani yupo varandani...halafu ulvyolewa, mbona leo aibu, hujui huyo ni rafiki yangu mkubwa kaja anataka kukuona shemeji yake...’akasema .
‘Haya shemeji shemeji huku mwazima taaa...nakuja maana sikuwezi....lakini ipo siku utajilaumu na hawo shemeji, ....nakuja...ngoja nivae hii bukuta, nani anajali nipo kwangu...’nikasema na kuvaa bukuta yangu, sikujali kuwa ni nani yupo, halafu nikatoka pale varandani....
Unajua wakati naingia yule mgeni alinipa mgongo, sikuwa nimemuona vyema, ...sasa natoka chumbani nikawa namwangalia moja kwa moja usoni...niliduwaa...nikashikwa na butwaa, lakini baaadaye nikajifanya kujisahaulisha nikasema kwa bashasha..
‘Ohh, samahani sikujua kuwa kuna mgeni, mgeni mwenyewe mrembo....shemejii ...mmh, umejaliwa kweli, ....mke wangu umempata wapi huyu mrembo?’ nikauliza.
‘Mbona alishawahi kufika hapa nikakutambulisha siku moja,....umesahau, na wewe bwana unazeeka kablasio muda wako.... ulikuwa haujamuoan vyema nini...?’ akasema mke wangu.
‘Aaah, labda nilikuwa na mambo mengi kichwani....shemaji jisikie upo huru,mimi nilikuwa na sherehe huko kazini, kwahiyo nimekunywa kidogo...unisamehe, kama nitaongea kauli chafu....unajua tena ukilewa...’nikasema na huyu shemeji akacheka, lile cheko la kumkoma nyani giladi...
Mazungumzo yalikolea maana mke wangu na huyo rafiki yake, inaoenekana walikuwa wanajuana vyema toka huko kijijini wakiwa shuleni, kwahiyo wakawa wanapeana maisha yao ya shule, na mambo ya kijijini, ikawa ni porojo, utani mwingi na vicheko, na ukinihusisha na mimi kiwembe, huku pombe zinanikoroga kichwani mambo yalinoga kweli.
Mimi kwa muda huo nilikuwa nimekaa kwenye sofa nikiwa natizamana moja kw amoja na huyo mgeni, mke wangu alikaa pembeni yangu na mara nyingine alikuwa akitoka kufanya mambo ya jikoni, nikawa nabakia na yule binti na mwanya kwangu kama huo ni kosa . ..
Hata hivyo sijui kama huyu binti, alishanijua uzaifu wangu au vipi, kwani alikuwa hatulizi migu yake na ukizingatia kuwa alivaa nguo fupi,....basi wakati mwingine alikuwa akiinua mguu juu ya mwingine na kuacha sehemu kubwa ya mapaja wazi,...hakujali kuwa mimi nipo mbele yake na namtizama moja kwa moja, pombe ikawa inanichanganya kichwani ...damu ikawa inachemka..!
. ‘Shemu sasa mimi naondoka...’ Baada ya maongezi na kupata chochote mgeni akawa anaaga kuondoka, na mimi sikupenda niiache hiyo bahati hivihivi, akili ikanijia, nikasema ;
‘Shemeji ngoja nikupe lifti, unasema unakaa wapi....?’ nikauliza. ‘Hapana shemeji leo unatakiwa upumzike na mkeo,....maana umesema siku zote unarudi usiku huoni kuwa leo ndio siku ya kujirusha na rafiki yangu...’akasema.
‘Sawa mpe hiyo lifti tu, hakuna shida,.... kwanza mimi nina kazi nyingi leo, kuna minguo ya kufua, kuna kazi za nyumbani sina hata muda wa kuongea sina, mpeleke lakini urudi mapema, ..'akasema mke wangu na aliponioana nikiinuka na bukta ile niliyovaa inanishitaki, mke wangu akatabasamu na kusema,;
Lakini kwanza tafadhali kabadili hiyo nguo haina heshima, halafu nina wasiwasi na jinsi ulivyo utaweza kuenedesha gari kweli...?’ akasema mke wangu hata bila wasiwasi au wivu.Moyoni nikasema mambo sio hayo...kichaa kapewa rungu, nakaondoka naye. ....
*********
‘Shemu, umenikosha sana,... sijawahi kuoana msichana mrembo kama wewe...na leo sijui nisemeje, ...’niaksema.
‘Shemeji bwana, mzuri mkeo,....usinitanie, ...hata hivyo shemeji, naona kama umelewa, na mambo unayoyaanza sasa sio mazuri, unajua mkeo ni rafiki yangu mkubwa, sitapenda kujiingiza katika hayo unayoyawaza, namuheshimu sana.....rafiki yangu....’akasema huyo binti.
‘Najua ni rafiki yako, lakini urafiki wa kweli ni kuchangiana...au sio, kwanza, hapa nilipo sijui itakuwaje, ....unaona alivyo rafiki yako, kazi nyingi hazimuishi, ...nipo nyumbani lakini naweza nisimuona chumbani hadi usiku....aah, samahani naongea mambo ambayo siyakuongea...’nikainama chini kwa kujifanya naona aibu kuwa nimeropoka mambo ya ndani.
‘Unaoan sasa ni pombe hiyo, inakufanya uongee hata siri za ndoa, lakini kama ana kazi nyingi kwanini usimtafutie mfanyakazi wa nyumbani, ili mpate kuwa naye karibu....’akasema huyo binti
‘Hataki....hataki kabisa, anasema yeye hana kazi, ina maana kama nikiltea mfanyaakzii yeye atafanya akzi gani...labda anaona wivu kuwa nitamgeuka, ....’nikasema na kweli moyoni niliwazia hilo hilo, kuwa angekubali kuleta mfanyakzi sijui kama ingeliisha mwezi kabla sijamgeuka....nilijua kabisa uzaifu wangu.
‘Shemji mimi hapa ndipo naishi,...’akasema tulipofika maeneo ya kwake.
Ilikuwa nyumba nzuri tu, na sijui humo alikuwa akiishi na nani. ‘Unaishi peke yako humu ndani....?’
nikamuuliza
‘Ndio, kwani vipi, ...mimi sina mume, ningeliishi na nani...lakini ni nyumba ya kupanga, mbona nipo hapa siku nyingi tu...’akasema huku akifungua mlango......ilikuwa nyumba nzuri,kubwa ya viumba vitatu, choo jiko, na kila kitu ndani kwa ndani, lakini haikuzungushiwa ukuta....
‘Ohh, kumbe unaishi hapa, tena peke yako hata siamini, ....na rafiki yako ndipo anapokuja mara kwa mara,...keshaniambia kuwa anakuja kwako mara kwa mara,....kweli hapa pazuri,... lakini sizani kama unaishi peke yako, suinidanganye nikaja kuuwawa bure...'nikaanza utani wangu huku najibwaga kwenye sofa hata bila kukaribishwa.
'Amini hivyo...nipo peke yangu....sijaolewa, kama ningeliolewa ningelisema naishi na mtu, ukimuona mtu anakuja kuijiiba tu...'akasema.
'Sawa nimekuamini, akija mwenyewe tutapambana maana hukuniambia ukweli....lakini hata hivyo nikiuwawa sio mbaya maana ,inzi kufia kidondani haijalishi au sio,...' nikasema huku nikimwangali yule binti bila kummaliza.
'Shemeji wewe unapenda sana utani....shauri lako...'akasema na kucheka.
'Unajua kama mke wangu ni rafiki yako kipenzi hata mimi natakiwa niwe rafiki yako kipenzi pia ,au sio...?’nikasema na mazungumzo yakakolea hata sijakaribishwa vyema.
Baadaye akaniuliaza natumia soda gani, huku anaelekea kwenye jokofu lake la vinywaji , maana ndani kulikamilika, kila kitu cha bei mbaya, nikajiuliza huyu mwanamke anafanya akzi gani, maana kuvinunua vitu kama hivyo, labda uwe mkurugenzi wa makampuni mengi
‘Shem, unanitania au unasemma kweli, ....aah, mimi sinywi soda kwani mimi ni mwanafunzi...niletee kinywaji baridiiii....kama pesa huna chukua hii kalete vinywaji vya kiutu uzima..., leo nipo mapumziko...sina shida....au wewe unashida...ukiwa na mimi usijali, pesa ipo mingi tu...’nikasema.
Na yule binti hakujivunga aakchukua pesa niliyompa akatoka kwenda dukani na kurudi na kinywaji, ...mambo yakaanzia hapo. Yule binti kumbe alikuwa na mipango hiyo siku nyingi akilini mwake..mimi bil kujua .nikajiingiza kicwha kichwa, na muonja asali haonji mara moja, tukajenga uhusiano wakaribu kuliko maelezo.
Nyumbani ikawa nikufika na kuangalia kuwa hakuna tatizo,....aah , kwakweli sikuwa mbahili wa kumjali mke wangu, hanakama nilikuwa na mambo hayo ya kihuni, lakini nilihakikisha kuwa mke wangu ana hela ya kutosha...nikihakikisha hilo mbio naondoka kwa huyo rafiki wa mke wangu, na mke wangu hajui kabisa nini kinachoendelea,....
Mke wangu alinichukulia kuwa ni tabia yangu,au kama aliumia, aliumia kindani ndani...aliogopa kumuuliza mwanaume wapi unakwenda, kwanini unalala nje, kwasababu hata nikilala huko anajionea sawa tu, lakini mwishoowe akakerwa akaamua kusema;
. ‘Mume wangu hivi una nini kinaendelea maana sikuoni kama uko sawa, siku hizi hukai nyumbani, hulali nyumbani, kulewa na wewe, na nasikia wewe na wanawake na pombe ndio maisha yako, una mipango gani ya kimaisha wewe mwanaume...na magonjwa siku hizi ni mengi, huoni kuwa utatuletea wadudu nyumbani’akasema mke wangu.
‘Hahaha..leo hii unalalamika eti wadudu, wewe unajua wadudu wewe, ..hahaha leo hii unauliza mipango gani ya kimaisha, wewe si ndio unataka iwe hivi, hutaki usumbufu, hutaki ....mmmh, sasa ndio hivyo nimenasa kwenye ulimbo....hapo sijui kama nitajinasua maana kile nilichikuwa nikitaka nakipata kwa raha zangu....zaidi ya nijuavyo....mke wangu, sijui niseme, ....nini kwanini lakini....hunielewi, nimekufundisha nimekuelekeza, lakini naona unanifukuza ...haya tuone...’nikawa naongea kilevi levi, bila kuchuja maneno yangu.
‘Sawa kama umeamua hivyo ...nitafanyeje, maana mimi nimejitahidi kutimiza yale niliyofundishwa kuwa na adabu njema kwako, na kukufanyia kila kitu....labda hayo kuna mambo mengine siyajui, labda hayo unayotaka ya uzungu-uzungu...mimi hayo siyapendelei,...nashindwa kabisa.... lakini hayo sio kigezo...kwasababu wanaofanya ni wahuni, sio wanandoa, mimi naona tabia hizo kama ni ushetani....sioni umuhimu wake..’akasema mke wangu.
‘Yaani mambo ya mke na mume ni ushetani, hivi wewe upoje....wewe unataka nini, kwani nilikuoa uje kunifanyia kazi tu, kama ningelitaka hivyo, ningeliajiri mfanyaakzi wa nyumbani, lakini wewe nimekuoa kama mke wangu, nikikuhitaji wakati wote unitii, ...leo hayo unayaita ya ushetani...kama ni ushetani, achia mashetani wafaidi...sikusumbui tena....unasikia sikusumbui tena....’nikasema huku napepesuka.
‘Samhani mume wangu kama nimekukosea, sikuwa na maana hiyo...’akajitetea mke wangu.
‘Samahani nikuombe mimi kwa kukusumbua....ninachosema kuanzia sasa, sikusumbui tena, na wewe usiniulize kuhusu maisha yangu ya ushetani...’nikasema na kuondoka, sikujali machozi yaliyokuwa yakimtoka, maana kila nikimfikiria rafiki kimwaan anayejua kumapagawisha mwanaume, nakuwa kama nimepuliziwa dawa, ni mbio mbio kuelekea kwake.
Siku moja rafiki yangu wakazini akaniuliza , kuhusu mabadiliko niliyokuwa nayo, alianzia mblai kibusara, na mishowe akaamua kunipasulia wazi. Sijui kwanini , kwa muda kama ule, nilikuwa siambiliki, akili yangu iibadilika kabisa, na kama mtu alitaka tukosane aniuliza kuhusu maisha yangu na huyo kimwana;
‘Rafiki yangu huko unapokwenda ni kubaya...hebu niambie, una mke mzuri sana nyumbani, kila mmoja anatamani awe na mke kama huyo, mtulivu, mzuri, na tabia njema kabisa, wewe unaruka na viruka njia, kila wikiendi upo Zanzibar, unatesa na huyo kimwana, unamjua huyo kimwana kweli, wenzako pale walishachoka, sasa wewe unachukua makombo....unatafuta kifo muda sio wako...’akaniasa rafiki yangu na hapo akaupalia mkaa.
‘Na wewe umeanza kunigeuka,.... yaani mpenzi wangu unamuita kiruka njia, Malaya aliyeshindikana, hivi wewe mkeo wako naye unamuonaje yule, ....hahaha, hukumbuki kuwa mimi nilishachezea nikachoka ndio ukamuoa...au hujui hilo....nakuambia sitaki kunifuata fuata katika misha yangu....na tusijuane..umenielewa, tusijuane....’nikamwambia.
‘Sawa wewe ni rafiki yangu na tumetoka mbali, najua huyo mke wangu uliwahii kuwa na urafiki na wewe kama unavyodai kwa kipindi hicho, sio mbaya, lakini kwa sasa nimemuoa katulia, ni kawaida tu ya maisha...hilo halinitii shaka, ila nakupa kama ushauri, kama rafiki yangu...kuwa mambo yako sio mazuri ..na kuna tetesi, huenda ukasimamishwa kazi kwa muda, nakudokezea tu...’akasema rafiki yangu huyo.
‘Nani anajali,hayo si majungu yenu, mtaishia hivyo hivyo, tatizo lenu mumejaa wivu, .... kama pesa ninazo.....’nikasema na kuondoka kwenda nyumbani, ili baadaye nielekee kwa kimwana wangu....hapo nilikuwa nimeshachukua mshahara wote , na madeni juu, nilikuwa sina wasiwasi maana kama meneja nilikuwa na nafasi ya kuidhinisha malipo kabla ya mshahara,.... nani ataniuliza, nilikuwa nimejisahau kabisa.
Wakati naondoka hapo, hata kabla ya muda wa kazi mawazo yangu yalikuwa ni kutumia , kwani tulishapanaga kuwa jumamosi , jumapili tutashinda Zanzibar na kimwana wangu...tunatesa, tunatumia, tumia ukiwa nazo, maana maisha ni mafupi...nikawa najiimbia huku nakanyaga gia za gari lifike haraka...
Nilipofika nyumbani sikumkuta mke wangu, nikajua kaenda sokoni, nikabadili nguo kwa haraka na kuchuku `briefcase yenye nguo zangu maalumu, nguo za safri, huyo hadi kwa kimwana wangu, na huko nilimkuta ananisubiri kwa hamu, kuniona tu akanikumbatia na kabla sijakaa sawa akaanza kudai pesa za kodi ya nyumba, nikampa, mara pesa alizokopa kwa ajili ya kutengeneza nywele nikampa....baadaye tukajipumzisha ili kesho tudamkie safari ya Zanzibar.
‘Nani anagonga mlango ...aah,....siulisema hakuna mtu wakutusumbua, vipi tena.....’nikasema huku nikiwa nimelowa jasho chapachapa...na muda huo tulikuwa kwenye masofa, hatukutaka kabisa kuingia chumbani kwasababu ya joto, ....dunia niliiona yangu kwasababau nipo na kimwana anajua raha za kila namna....
'Achana nao unawajali hawo wambea,... labda ni hawa marafiki zangu wanaotuonea wivu....acha wagonge mpaka wachoke, wewe sogea huku, na ulivyolowana...duuh,utafikiri, ulikuwa unakimbiz.....’ na kabla hajamaliza kusema mlango ukafunguliwa,....nilipogeuza kichwa na kuangalia mlangoni, macho yakanitoka pima,....sikuaminii ,kwani aliyeingia mwanzoni ni mke wangu, ...aliyefuatia ni mjomba, na pembeni yupo mama na baba....kila kitu kilinywea.....
Je itakuwaje....kama ingelikuwa wewe ungelifanyeje, maana kila kitu kipo wazi.
WAZO LALEO: Siri moja ya kujenga mahusiano mema ndani ya ndoa ni kujadiliana, ....na hasa pale kunapokea sintofahamu yoyote, kwani ndoa hujengwa na wandoa wenyewe .
Ni mimi: emu-three
Tuesday, March 27, 2012
Hujafa hujaumbika-11
Basi niakaanza maisha ya ndoa,maisha ambayo sikutarajia kuwa yatakuwa hivyo, mwanzoni nilijua ni swala la muda tu,maana kila mmoja anapoingia katika maisha haya anakutana na mitihani mingi, ikizingatia kuwa mumekutana kila mmoja na tabia yake, na pia kila mmoja na,hulka na hata imani tofauti,....lakini iwavyo mwisho wa siku mnakuja kukubaliana na kuwekana sawa, ndivyo nilivyokuwa najua.
Lakini nilikuja kujau kuwa mambo mengine yakijijenga ukiwa mdogo, yanweza yasiondoke kabisa akilini,....kuna watu wanajikuta wamejijenga na hulka na tabia fulani ambayo hawapendi, kuibadili, kutokana na malezi, au maisha uliyokulia, ....ndivyo alivyokuw amke wangu, na huenda ndivyo walivyo wengi, ...maana nilijitahidi kila jambo kuliweka sawa, kufundiha na kuelekeza,lakini kuna mengine nilishindwa kabisa....’akaendelea kuongea rafiki sikutaka kumkatiza, ....
Siku ya fungate iliisha nikiwa ansema huu kwa vileni mwanzo, nitamuelekeza na ayabadilika tu, nikawa namchukulia kidogo kidogo kama mtoto anayeanza kutambaa, hadi kusimama....nikukumbuka maisha aliyokulia ni yale ya kkijijini haswa, ...vitu kama umeme, maisha ya mjini na mazingira yake ni mwazo kukutna nayo....sikujali sana.
‘Sikiliza mke wangu huku ni mjini na vitu vingi ni tofauti sana, huku usitumie kuni,...na kamani lazima tutaumia mkaa, lakini sio lazima kwasababu kuna umeme....’nilimwambia siku moja akiwa kanunua kuni...tulipofika tu...
‘Mimi nimezeoa kutumia kuni...’akajitetea.
‘Hapana nitakueleekza jisni gani ya kutumia umeme,usipate taabu...’nikamwambia, lakini alijaribu kunipinga kumwingilia mambo ya jikoni, akasema mwanaume haruhusiwi kuingia huko.
‘Huku ni mjini...acaha yale mambo na tabia za kijijini,.....lakini hata hivyo usijali, kwa mfano nikuulize je ukiumwa nani atapika..?’ nikamuuliza.
‘Ni hapo nikiumwa, na utamuita ndugu yangu aje akusaidie kupika, lakini mwanaume haruhusiwi kuingia jikoni, au kushika vyombo....au kufagia ndani....sikubali kabisa,...hapo usiniingile...’akasema.
Nikasema kimoyomoyo, hujakutana na majirani, akina mama wenzako watakufundisha na ukijua hayo utabadilika tu, lakini nikumabie ukweli mke wangu huyo hakupenda kabisa kukaa na kuongea na mjirani mpaka wakawa wanalalamika, ....sikuwajali sana kwa hilo, maana ni heri kwa namna moja au nyingine.
‘Mke wangu mbona unaweka chakula cha moto kwenye jokofu....?’ nikamuuliza siku moja, kapika ugali wake vizuri na kuuweka kwenye sahani, lakini mimi nilikuwa sijawa tayari, na akaona ugali ule utapoa, mara nikashangaa unaweka ndani ya jokofu.
‘Si ili kisipoe....’akasema huku akijiamini kabisa.
‘Hapana hiyo ni kwa ajili ya kupoozea vitu, ....huoni humo kunatoka ubaridi....na ukiweka vitu vya moto, unaweza ukaliua kabisa hilo jokofu...’nikamwambia, na haraka akakitoa kile chakula. Nikawa nasema kimoyomoyo huyu atajifunza haraka tu. Lakini ilikuwa unafundisha hiki kesho hiki kimeharibiwa,....mwisho nikasema itakuwaje,maana mimi nitakwua kazini,je nani atamueleekza hiki au kile na vyombo vingi nilivyokuwa navyo ni vya umeme.
Kwa mwezi mmoja, vyombo karibu vyote vya umeme vikawa vimeharibika, na siku moja karibu nyumba nzima iungue na moto, aliwasha `heater’ kwenye ndoo kwa ajili ya maji ya kunywa akaondoka kwenda sokoni, huko akachelewa, maji yakachemka na ndoo ikayeyuka,....fikiria chumba kilikuwaje, kilikuwa kama kuna mvuke umejaa ndani, ...baadhi ya majirani wakaona moshi namvuke ukitokea ndani, ...lakini kwa muda huo mke alikuw hayupo na mlango umefungwa...
‘Sasa tufanyeje maana kunaonekana kuna hitilafu ya umeme humo ndani..na moto ukitokea hapo utatuathiri na sisi nyumba za jirani.’akasema mjumbe.
‘Tuvunje mlango....’akashauri mtu, na bahati nzuri nikatokea, nikaingia ndani..kulikuwa hakuingiliki, lakini nikazima kwenye eneo la kuzima umeme wa nyumba nzima ikawa ndio nimeokoajahazi, ...yalitoke mengi lakini yote nilijua ni kwanini,kwahiyo sikujali sana.
Kitu ambacho kilikuwa kikiniumiza sana ni tabia ambayo hakutaka kabisa kuibadili, tabia ya maisha ya ndani ya mke na mume, yeye alichukulia alivyolelewa kabla ya ndoa ndio hivyo hivyo,...mwili wake ni wake,haruhusiwi mtu kuuona,kuugusa ....vitu kama hivyo, .... nikamshauri na kumeelzsea kuhus maisha ya mke na mume, lakini aliishia kunicheka na kusema hizo ni tabia mbaya za wanaume, hazitaki kuzisikia,
Nilijaribu hata kumletea mikanda ya video ili ajifunze maisha ya ndoa yalivyo, ...alilaani na kulani, kuwa nimemletea ibilisi ndani, ...akawa hataki kabisa hata kuziangalia...
‘Mambo gani hayo ya kishetani....kama unataka kuangalia kaangalie huko huko ..mimi sitaki kuangalia, hizo picha zinazofundisha ubaya...tangu zamani nimekatazwa hayo...kama unataka kuangalia ngalai mwenyewe....’akawa anasema kwahasira.
‘Sikiliza mke wangu, maisha tunayoishi sasa ni ya mke na mume , na hayo ndiyo yanayotakiwa mke na mume wayafanye, sio mambo ya kishetani kati ya mume na mke,....’nikawa namshauri,lakini akawa hataki hata kusikiliza. Nikajiuliza nitumie ukali, labda kazoea kufokewa na kutumia nguvu, ...hapana nikakumbuka maisha aliyowahi kuishi ya kukaripiwa na kutumwa kama punda, ...sikutaka kumrudisha huko.
‘Sikiliza mke wangu, unajua wewe sio mtoto tena, wewe sio yule uliyekuwa ukitumwa kama punda,hapa unatakiwa ujitume mweneywe ujua kuwa hii nyumba na vilivyopo hapa ni vyako, na pia unatakiwa ujifunze jinsi gani ya kuishi na mume wako, mimi sio kaka yako tena, mimi sio mtu baki, mimi ni mume wako ambaye una haki zote, mwili wangu na mwili wako ni halali ya kila mmojawapo iulambiwa kipindi tunafingisha ndoa pale kwenyeule ukumbi....’nikawa natoa darasa.
‘Ule ukumbi wa gerezani kwa watu waliochanganyikiwa, ndio maana walikuwa wakiongea yale mambo yasiyofaa, ...kwasababu wanaokaa huko ni wakosaji siju na sisi tulipelekwa kwa bahati mbaya,....kama ungelifungia hiyo harusi kwenye nyumba za ibada au nyumbani usingelisikia hayo, mimi pale nilitamani kuondoka, maana watu wazima waanongea mambo machafu....’akasema na mimi hapo nikajikuta nikikumbuka siku ile ilivyokuwa....siku ya harusi ya kiaina yake.
*********
‘Jamani sio mara ya kwanza, mjue kuwa hata wafungwa wana haki zao, sio kwasababu umefungwa ndio huruhusiwi kuoa au kuolewa, ila ukioa au kuolewa, bado una majukumu yako, ya kutumikia kifungo chako, utakachobahatisha na kufunga ndoa, na mke au mume wako watakuwa wakija kukutemebelea, na tunajaribu kutafuta njia za kisheria ili mkitemebeleana kuwa na faragha kidogo...’akasema askari mmoja ambaye ni mkuu wa kile kituo, na watu wakashangilia.
Mimi kwa muda ule nilikuwa sijaelewa nini kinachoendelea maana niliamshwa asubuhi, na askari akaniambia nijiandae maana leo ndio siku yangu ya kesi, ....
‘Hapana umekosea fande sio leo...’nikamwambi nikiwa na uhakika kwani tarehe zote za kesi yangu zilikuwa kichwani.
‘Ina maana unanifanya mimi mjinga, unampinga afande, umeanza kuwa na kiburi au umeshazoea kukaa hapa ndio maana unakuwa na kiburi, uliktakwia uwe huko gereza kuu, huko ungekoma ubishi, na ulivyo laini laini, ungegeuzwa chakula cha ...’akasema yule askari huku akiniangalia kwa nyodo.
‘Afande sio kwamba nakukaidi ila nakumbuka kabisa tarehe yangu ya kesi sio leo, na siku mblili zijazo....’nikamwambia.
‘Sasa sikiliza nenda kaoge, ujiandae naenda kukuletea nguo maalumu, kuna nguo maaumu zimeshaletwa hapa, kwa ajili ya kesi yako hiyo, kama itaamuliwa vinginevyo, ujue hufiki huku tena, moja kwa moja gereza kuu..unanisikia, nakupa dakika kumi tu za kuoga,unaoga kama mwanaume, sio kujirembaremba hapa...’akasema huyo askari na kuondoka.
Mimi sikufanya ubishi nakaelekea sehemu yakuoga,na bahati nzuri kipindi hicho kulikua hakuan mahabusu wengi, hakukuwa na foleni,au ile ya kuoga kundi zima pamoja, ...nikamaliza kuoga na kutoka, ..n hat akabla sijafika kwenye chumba cha mahabusu, mara akaja yule askari akiwa kashikilia nguo.
‘Haya vaa hizi , una bahati kuwa wewe unavalishwa suti...unajau unavaa suti ili ukisimama mbele ya hakimu asione kuwa mnanyanyaswa, na hukumu ikitolewa, unabadili suti, unavaa suti maalumu za kifungwa, ndivyo ilivyo.....’akasemana kucheka.
‘Sawa fande nashukuru sana....’nikasema na kuzichukua ziel nguo...’nilishangaa ni inafanana kabisa na moja ya suti zangu nilizonunua huko Ulaya, ni hzi zilikuwa maalumi kwa ajili ya harusi......’niliiangalia ile suti nikasemakimoyomoyo, labda ni kufanana tu, nikavaa.
‘Umependeza kweli mfungwa...hata hivyo utaivaa kwa masaa, ikifika jioni utakuwa na sare maalumu, ...sare na namba yako ...unasikia mfungwa....utakuwa ukiitwa kwa namba...mfungwa namba fulani....’akasema huyo askari, ambaye kila mara anapokuja hapo anaishia kunisimanga utafikiri mimi nina kosa.
‘Sawa afande , lakini ipo siku utagundua kuwa mimi sina kosa kabisa....hayo yote ni maonevu....’nikasema nay eye aliishi akucheka.
‘Kwani mwizi au muuaji anayakubali makosa yake....sheria ndiyo itamuhukumu,lakini katu muuaji hakubali kosa lake,labda awe amechanganyikiwa....haya upo tayari, kaa pale usubiri...’akasema huyo askari na mimi nikatii na kwennda kukaa sehemu ya kusubiria wageni. Nikisubiri nini kitafuta baadaye, maana huku ni mwendo wa kusubiri,kila kitu mpaka uambiwe....
Toka asubuhi nimekaa pale hadi mchan unaingia, ...ilichosha na nikajikuta nasinzia, na mara likaja gari, gari, ni gari la mkuu wa kituo kile, likasimama,na akatoka askari aakmfungulia mkuu wake, na mara akatoka mkuu akiwa na suti yake safi, akanijia na mimi haraka niaksimama.
‘Wewe ndiye Msomali.....?’ akaniuliza.
‘Ndio mimi, mtoto wa Msomali...’nikasema.
‘Kwaini uitwe Msomali , wakati wewe ni Mtanzania...?’akauliz ahuku akinikagua na ile suti niliyovaa, ilishaanza kunipwaya, maana siku nilizokaa mle mahabusu ilikuwa ni adhabu tosha.
‘Hata mimi sijui kwanini, ila najua sisi ni Watanzania...’nikasema.
‘Nyie ndio tunawakaribisha hapa nchini halafu mnakuja kufanay vurugu...dawa yenu inachemka...’akasema kwa sauti ya kiaskari. Mimi sikujibu kitu nilitulia kimiya akamgeukia askari na kusema;
‘Huyu tunaondoka naye, kamanilivyokuambia, kila kitu kipo tayari,...’akasema na kunigeukia mimi;
‘Unasikia wewe Msomali, natakuita Mtanzanai, sitaki hilo jina la Msomali sawa....ni hivi tunakwendaleo kusikiliza kesi yako na hukumu itatolewa huko huko, ukitoka huko ama unakwenda nyumbani kwenu au unelekea gerezani, sitaki kukuoan tena kwenye mahabusu hii, .....’akasema na mara akaingia ndani ya gari.
Yule askari akanisogelea na kunisukumi kwenye gari, akasema; `haya ingia humo ndani ya gari, una bahati sana kupanda gari la mkuu....lakini ni mara ya kwanza na ya mwisho, utakuwa ukipanda lile gari kubwa lililozungushiwa nondo..kwaheri mfungwa...’akasema kufunga mlango.
Tukaondoka pale na gari likiw aan mwendo kasi, na nilishangaa, maana nilijua kwua tuanelekea mahakamani, lakini lakini ule mwendo wakasi uliishia kwenye ukumbi mmoja unaoitwa ukumbii wa magereza...na gari likasimama’
‘Haya shuka tumefika, kwani kesi yako itafanykai humu ukumbuni kwasababu za zarura...’akasema yulemkuu, nikatoka kwenye lile gari na askari mmoja akanishika mkono kuiongoza ndani ya ukumbi....
Nilishikwa na butwaa maana niliona kama naota, kwani kilichonipokea wakati naingia mle ni vigelegele na shangwe....
‘Hii maana yake nini...?’ nikauliza.
‘Kwani ukiona hivi kuna maana gani...?’ akaniuliza yule askari.
‘Kuna maana kuwa kuna harudi, au shughuli fulani....ndio najiuliza harusi ya nani?’nikauliza kwa mshngao.
‘Usijali utayajua mbele kwa mbele, wewe twende huku, maana mimi ndiye nitakuwa mlinzi wako wa karibu na pia nitakuwa mhusika wako wakaribu vile vile, ....’akaniambia yule askari akiniongoza hadi kwenye viti vilivyoopo mbele, huku nikizidi kushangaa, mbona napelekwa sehemu ile maalumu ya wageni mashuhuri, ....
Nilipokaa tu mara vigelegeel vikatanda ukumbini, na mara wakaja wakuu wa dini , wakasogea mbele yangu na mara vigelegele tena kwa shangwe na vifijo, kwani kulikuwa na watu wengine wanaingia, na kwenye kundi hilo nikamuoana binti harusi kavalishwa na kufunikwa mwili mzima...sikuweza kujua kuwa ni nani huyo bibi harusi, na ni nani muoaji...
Mara nikaitwa pale waliposimama wale watu wa dini wa kufungisha ndoa, nikasimama huku nikiwaza mengi, kwanini nihusishwe nah ii ndoa,...lakini kabla sijauliza yule muendeshaji wa shughuli akasimama na kusema;
‘Hii ni harusi ya kipeke sana, maana mtu anasubiri kuhukumiwa, ama aende jela au arusii uraioanai, alkini hukumu yake inakuwa kifungo cha ndoa.....’mara watu wakacheka na kushangailia.
‘Ndugu yetu mpendwa, kwanza tukupe pole sana na mateso ya mahabusu, ndio ukubwa huo, dunia hii kabla hujafa hujaumbika....huwezi jua, leo unaamuka mzima jioni kilema, leo unaamuka tajiri, jioni masikini, ...na pia unaweza ukaaamuka mfungwa na baadaye unakuwa bwana harusi....’watu wakshangailia.
‘Hili limefanywa kinamna, ulitakiwa kuwepo mahakamani asubuhi, lakini kwa dharura, hukuwepo ...tulifanya hivyo makudi, n ahata hivyo haikuwa haja, ...hukumu yako leo ni hapa, wewe kwa mujibu wa utaratibu, unahukumiwa kifungo cha ndoa...kazi kwenu watu wa dini mhukumuni....
Vigelegele na shangwe vikatawala ukumbini,..... na mara akanisogelea mtu wa dini na kuniuliza maswali mengi, lakini sikuwa mvumilivu, nikauliza kwanini yote haya yanafanyika na hata simjui huyo bibi harusi...
‘Humjui bibi harusi, unatucheeksah kweli,....wewe si ulitaka mwenyewe ukapendekeza kuwa unataka umuoe binto Yatima. Ukiwa huko huko mahabusu....au umesahau....’akasem yule mtu wa dini na mara akaja mjomba na ndugu zangu wengine
‘Tumefanikiwa....alikuwa keshapanda basi kuondoka kwennda kijijini....’akasema mjomba
‘Bahati kubwa sana, ingeshindikana leo ingekuwa jambo jingine, mambo yanakwenda shwari maana hata huko mhakamani wamesema hakuna tatizo, inaweza kufanyika maana muuaji keshakamatwa na kukiri kosa.
‘Ni nani huyomuuaji, aliyenifanya niteseke kiasi hiki....’nikauliza kwa hamasa
‘Hayo kwasasa hayakuhus.u la muhimu ni kufunga ndoa yako....haraka mana unahitajiwa mahakamani saa nane, kusikiliza linaloendelea kama utaendelea kushkiliwa aua utaachiwa...’akasema yule askari ambaye alikwua habanduki karibu yangu.
Na hapo moyo ukatulia na harusi ikafungwa...
*******
Nikiwa katika moja ya darasa maalumu la kujaribu kumfundisha mke wangu, na leo ilikuwa maalumu kwa kutoka, ilikuwa kazi kweli kumshauri...hasa ilipofiki sehemu kuwa akaziweke nywele zake tofauti na alivyozoea, yeye anapendelea kusuka tu,..
‘Nywele zangu haziweki hayo mauchafu..kamwe sitaki....’akasema na kukataa kata kata, lakini leo nilizamiria nikasema kwa ukali;
‘Hapana leo lazima ukabidli nywele zako kidogo, ili uone tofauti...’nikamwambia kwa sauti ya ukali kidogo. Akainua uso kuniangalia, hapo sikucheka, kama kawaida yangu, akaona kweli nimezamiria, akasema kwa upole;
‘Haya, kama ni lazima sawa,lakini sipendi kaisa,...’akasemakwa shingo upande.
‘Nikampleka kwenye saluni ya karibu, na kumuacha hapo,baadaye nikampitia kumchukua, kweli alibadilika,na nilitaka awe hivyo kwasababu tulialikwa kwenye sherehe moja, ....huwa hapendi kutoka, na akitoka huwa kajitanda khganga zake, ni nadra sana kumuona katembea kichwa wazi, ...leo nikaona nijaribu kumfanya aonekane tofauti, na kweli huko saluni walimbadili..
Kweli leo alikuwa tofauti, sio yule binti aliyekuwa kakonda, anatia huruma,...mwili wake ulishakuwa msichana mrembo, nilijaribu kumbadili hivi ili nione atakuwaje, mengi aliyakubali,
lakini kuna mengine hakukubali kata kata...na tulivyorudi kwenye hiyo sherehe tukakaa faragha huku nikijaribu kuwa karibu naye, na hata kumkumbatia,.... hakunisukuma kama alivyozoe, nik
amwambia;
‘Mke wangu u mzuri kweli, na leo umekubali ukazitenegneza hizo nywele zako umependeza kweli kweli, ....’nikamsifia.
‘Mimi nimefanya kama ulivyotaka....kwa leo tu, lakini sipendi kutengeneza nywele zangu kuwa hivi ..napenda kusuka tu, na kesho naenda kusuka, sitaki kabisa kuonekana hivi naonekana kama muhuni....’akasema huku akijiangalia kwenye kiyoo nikiwa karibu huku tunajiangalia pamoja kwenye kiyoo, kweli alikuwa tofauti, binti mrembo.
‘Unajua mnapoona mnakuwa kitu kimoja, mke na mume ni mwili mmoja, mwili wako ni wangu na wangu ni wako’nikamwambia na hapo nikawa nimemuuzi akasogea pembeni na kuongea kwa hasira;
‘Mwili wangu ni wangu sio wako,...mimi na heshimu mwili wangu, na sio wa kuitizamwa ovyo, mimi sio muhuni wa kufanya mambo ya kihuni....kama unahitaji wahuni unaweza kwenda kuwatafuta mitaani, lakini sio mimi....’nilishangaa alivyokasirika na kuondoka kufanya kazi zake za ndani.
Unajua mimi ni mvumilivu sana, na ni mwalimu mnzuri, lakini mambo mengine nilishindwa akbisa kumshawishi huyu mke wangu,yapo niliyofanikiwa , lakini sio maisha ya ndani ya mume na mke, ..mke huyu hakukubali kabisa, ....
‘Utabadilika tu ni swala la muda....’nikasemakimoyo moyo.
Muda ulipita na miaka ikapita, hakukubali kubadilika kwa maswala ya ndani, nikasema nifanyeje nitafute mwanamke aje amfunde ndani, au nifanyeje...nikaongee na shangazi yake aje amuelekeze,labda ananiogopa mimi, lakini mimi ni mume wake, nitachekwa kama nikishindwa hilo...nikawa katika mitihani kama hiyo.
Mengine hayafai hata kusema , maana ikifika usiku ilikuwa kama vioja, mwenzangu anahakikisha kuwa taa zimezimwa, kava nguo zake, na hataki umwangalie....na mambo mengine ni mshie mshike....nikajaribu kila mbinu za kumfundisha, lakini haikubadili kitu....lakini hata hivyo tukabahatika kupata mtoto, ...huta baada ya kupta mtoto tabia yake ya ndani ilikuwa hivyo hivyo, ...licha ya kuwa mambo mengine alijfunza kama kutumia umeme na kazi za ndani.
Kazini kulikuwa na sherehe za mara kwa mara, ukumbuke mimi ni meneja katika moja ya vitengo huko kazini,kwahiyo wakati mwingine nahitajika kuhudhuria sherehe na mke wangu, mke wangu hakukubali sherehe kama hizo, nilipompeleka mara moja akaona kulivyo akasema yeye hararudia tena.
‘Mke wako hatumuoni bosi,vipi ni mke wa ndani tu...’akauliza mmoja wa mabinti tuaofanya nao kazi.
‘Ana kazi zake nyingi, sio rahisi kuja kwenye sherehe zetu...’nikajitetea.
‘Basi mimi nitakuwa namuwakilisha kama hutojali...’akasema huyo binti, alikuwa binti mrembo, na kutokana na kazi zetu tukawa tumezoeaan sana, huwa kama hakuna kazi tunaongea sana mambo mengi,.....na kwahiyo tukajikuta tupo karibu sana na yeye haat ikawa tunakwenda kula pamoja na jioni nampitisha nyumbani kwake.
Wakati mwingine nilikuwa najiuliza kwanini binti mnzuri kama huyu hajaolewa, na katika maongezi yetu siku moja nikamuuliza...
‘Mimi sijawa tayari kuishi ndani kama mke, ...kuolewa sio jambo la kukimbilia, hata hivyo, kila jambo lina muda wake...’akaniambia siku moja nilipomuulizia. Na sikutaka kumdadidi sana kuhsu hilo, kwani nilikuwa nikikwepa kujiingiza mweneywe kichwa kichwa...naiheshimu ndoa yangu.
Siku zilivyozidi kwenda nikaanza tabia ya kunywa sana pombe, hii nilianza kama mchezo,ili nikirejeanyumbani, nisiwe na mawazo mengine zaidi ya kulala, sikupenda kumsumbua mke wangu, kwani jioni alionekana kuchoka sana kwasababu ya kazi za nyumbani, na kama nilivyoelezea awali, hakuwa mcheshi sana wa kuliwazana, hayo kwake aliyoaona kama uchafu, ...au uhuni kama alivyopenda kusema.
Sio kwamba nilikata tamaa ya kumfundisha, nilijitahidi lakini ndio hivyo tena, ilionekana kashikili amsioamo wake, basi ikafika mahali nikaona bora niwe naknywa sana, nikirudi simsumbue, ni kuuchapa usingizi, kumbe nilikuwa nikjiharibu bila kujua, ....maana ili ufaidi pombe , unahitajika uwe na wenzako, na vyema zaidi wakawemo marafiki wa jinsia tofauti pembeni, nilianza kama mchezo na baaadaye ikawa mazoea.
Siku moja, kwenye sherehe zetu nilikunywa sana, ...na wakati tunarejea nyumbani ikabidi nimchukue huyo binti nimpitishe nyumbani kwake, kwasababu ilikuw anjia moja, tukafika kwake, na yeye pia alionyesha kulewa , hata wakati akiteremka kweney gari langu, akawa anapepesuka, ikabidi nimsaidia kumshika mkonoo hadi nyumbani kwake anapoishia.
‘Yaani najisikia vibaya hata kupanda kitanda siwezi, naomba tafadhali unifikishe kitandani, halafu ndio uondoke..bosiii, tafadhali....’akaniomba, nikafanya hivyo,.... lakini tulipofika kitandani maombi mengine yakaongezeka.
‘Yaani unaniacha nikiwa na nguo bosi, nisaidie kunivua...viatu, gauni...na....tafadhali bosi usiondoke...siwezi kabisa kukaa peke yangu, najiskia vibaya, ...’nikakamsaidia hili likaja jingine, na hapo ilikuwa kosa,...kilichofuata hapo ni jogoo la asubuhi ndilo lililonifanya nizindukane...
‘Oh, kichwa kinaniuma...’nikalalamika huku nikishika kichwa,kweli kilikuwa kikiuma saana.
‘Pole sana mpenzi inabidi ukazimue...’sauti ya kilevi levi iliongea pembeni yangu, na niliposiki hiyo sauti, nikashituka, maana kauli na sauti kama hiyo sijawahi kuisikia toka kwa mke wangu...nikakumbuka,....nilikurupuka hapo kitandani na kumbe looh, nipo uchi wa kuzaliwa, haraka haraka nikavaa nguo, mbio nikatoka nje, ....nilifika nje gari halipo....
NB:Tuishie hapa kwa leo, lengo ni kukuonyesha jinsi nilivyoanzakubadilika na matokeayake yatakuwaje, tuwepo sehemu ijayo. Kama nilivyosema kisa hiki na mahsusi kwa wale wandoa, watarajiwa na wanaopambana na misuko suko ya ndoa...tusaidieni kwa maoni.
WAZO LA LEO: Kuuliza sio ujinga, kama unataka kweli kujua, ni ukijua fanyia utafiti kua ni kweli au sio kweli. Mara nyingi tunachukulia tetesi au mambo mengine juu kwa juu, kama zilivyo, na matokea yako
Ni mimi: emu-three



