Kumbe `kama zamani ‘ wana maana yao, na walilenga tangazo lililosikika kuhusiana na dawa ya ukimwi ambayo tumesikia kuwa huenda imepatikana kwa asilimia Fulani na italetwa hapa nchini. Sijui kupatikana huko kwa dawa hiyo kupo kwenye majaribio au ndio imeshaathibitishwa kuwa kweli inatibu, na kwanini ikimbiziwe Tanzania, au ndio imeshasambazwa duniani!
http://www.iavi.org/research-development/Pages/is-an-AIDS-vaccine-possible.aspx
Kwa vyovyote itakavyokuwa dawa ni dawa, na kutibu kwake sio lazima iwe mia kwa mia, na inaweza ikatibu mwingine na mwingine isiwezekane. Kwa mfano wa madawa ya malaria, wengine wanapona wengine hawaponi na wengine hawapatani nazo kwasababu ya `sulphur’ iliyomo ndani yake na vitu kama hivyo. Je wewe unajuaje itakufaa?
Cha muhimu ni `kinga’ na kujua nini kinachosababisha ugonjwa huo ili ujihadhari nacho. Kinga ya malaria nii kupambana na mbu na mazalia yake na kuhakikisha unatumia neti. Na kinga ya ukimwi ni kuacha uzinzi na vinavyotokana na ushawishi wake. Uzinzi, au zinaa au umalaya au maambukizi mengine ndiyo yanayokufikisha kuupata huu ugonjwa, kwanini tusiyakwepe tukawa huria, kuliko kusimama katikati ya barabara na kusema ngoja nigongwe nikiumia si dawa zipo nitatibiwa! Hapo ni kukosa hekima na busara.
Kama walivyosema wahenga `kinga ni bora kuliko tiba, basi nasi kama tuna busara ni bora tukajikinga na vinavyochangia kuleta ugonjwa huu, ili hata dawa ikija isije ikatukuta tupo taabani hata kutibiwa kwenyewe kukawa kwa mashaka mashaka na huenda isiwezekane kabisa kwa kuangalia utibabu wa magonjwa mengine unavyosumbua. Na pia inaweza ikaleta usugu au kushindwa kuhimili ukali wa vijidudu hivyo, kwani navyo hujibadilibadili kama kinyonga.
Mimi wenu,
emu-three
3 comments :
Kwani ni mara ya kwanza kusikia kuwa dawa ya ukimwi imepatikana, nyie mnaopenda hiyo starehe hasa ya uzinzi hiki ni onyo kwa muumba, ni vyema tukaacha na kutubia kuliko kufurahia eti dawa sasa ipo tuanze kale ka mchezo ka zamani, tutaangamia sote tusipoangalia
Nimepita nami kusoma Diary hii.
Nimevutiwa nayo, na nitakuwa nikipita mara kwa mara humu kupata changamoto.....ahsante kaka
Karibu sana Shabani jisikie upo kwako, na pia unaweza kuwakaribisha wengine, napia unaweza kujisajili kwenye marafiki, ili tuweze kuliendeelza gurudumu hili la blogs pamoja.
Post a Comment