Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, October 30, 2019

CHUMA ULETE-6


 Hata sijui ni kwanini...

Mimi  sikuweza kumuamini huyu mtu wa jamii, kuwa ataweza kunisaidia kwenye hili janga, kwangu mimi, sana sana  niliona yeye anataka kutumia hili tukio, ili aweza kukamilisha utafiti wake tu..na hii kesi inahitajia pesa, inahitajia wakili mwenye ujuzi mkubwa,...mimi sina pesa, rafiki yangu halidhalika, na cha ajabu rafiki yangu kaenda kuniletea mtu ambaye, hana pesa., ...sio wakili kisheria,

‘Huyu mtu atanisaidia nini mimi..’ nilijikuta nawaza na kusema hivyo kwa sauti ndogo.


 Tulibakia wawili , mimi na mtu wa jamii, yeye akaniuliza maswali machache, muda wa kuongea na wageni ulishakwisha, yeye  akaondoka akisema anataka kuonana na mkuu wa hicho kituo, sijui waliongea nini....

Siku hiyo ikapita sikuchukuliwa kwenda Ukonga, niliona ajabu sana...,na hakuna aliyekuja kuniambia ni kwanini..lakini nilijua ni swala la muda, nitachukuliwa tu..

Kisa kinaendelea.....

**************


Kesho yake akaja shemeji, macho yamemuiva, na nilibahatika kuyaona hayo macho yake baada ya yeye kuvua miwani, aliyokuwa amevaa, nahisi aliivaa hiyo miwani kwa makusudi ya kuficha hayo macho yake, ni dhahiri kuwa anavuta bangi, japokuwa yeye, halikubali hilo.


'Shem, kwanini unaniuza..'akaanza kuniambia hivyo, hata bila ya salamu.


'Kwa vipi shem...?'nikamuuliza, nilishamzoea, maana kila tukikutana, mimi na yeye, tunaishia kwenye ugomvi tu, jamaa huyu ananichukia sana, ila kama dada yake yupo, jamaa huyu  anajifanya kuwa ni muungwana kwangu.

'Mimi nimejitolea muhanga kukusaidia wewe, ...unajua ni nini nilichokifanya, imeniuma sana, kukusaidia wewe na haki ya dada yangu ipotee....’akatikisa kichwa.

‘Unaja nikuambie ukweli, tukio hili  ilikuwa ndio wakati mnzuri wa kukumaliza kabisa...ulichokifanya, hakistahiki kusamehewa,..unahitajika kunyongwa,..lakini kwa upumbavu wangu, nikaogopa....niliogopa, nitaambiwa nimechukua sheria mikononi mwangu, na mimi sitaki kuingia kwenye mikono ya polisi...ndio hivyo tu...sasa wewe umeharibu..’akasema

‘Mimi nimeharibu kwa vipi shemu...?’ nikamuuliza

‘Wewe unawatangazia watu kuwa  mimi ndiye niliyekupiga kichwa....kweli si kweli...?’ akaniuliza sasa akinikazia macho, awali nilikuwa nikimuogopa sana huyu jamaa, lakini ikafikia mahali nikaanza kumzoea,..kwahiyo hapo sikujali, nikamkabili, japokuwa siwezi kupambana naye kimabavu.

'Nimemtangaza nani kuhusu hilo, wewe usiwe unasikiliza majungu watu,..ilivyo, hata taarifa ya polisi inasema dada yako ndiye aliniumiza...’nikasema, na jamaa akabenua mdomo kwa dharau.

'Sikiliza, najua wewe na mimi hatuivani kabisa..., na ukiona mimi nimefanya jambo la kukusaidia, ujue kuna gharama, na gharama yake ni kubwa sana...,’akasema na nilikuwa nalisubiria hilo.

'Natakiwa nikulipe shilingi ngapi..hata hivyo ukumbuke mimi ni shemeji yako....’nikasema

'Mjinga mkubwa wewe, wewe moyoni mwangu sio shemeji yangu, kabisa kabisa..., natamka hilo unielewe, na najua unanielewa hivyo...mengine ninafanya kwa heshima ya dada yangu...’akatulia akikunja uso , niliona kama ana sikitika.

‘Mimi  niliapa sitakutambua wewe kama shemeji yangu, kamwe,..nitafanya hivyo tu, pale dada akiwepo, kumridhisha yeye...sasa wewe unataka gharama si ndio hivyo,...haya, je nikikuambia nataka nyumba yako utasemaje..’akasema akitizama miwani yake aliyokuwa kashikilia mkononi.

'Shemeji, huko unapokwendsanaa ni mbali...’nikasema nikihis mwili ukinicheza cheza..nilijua tu, huyu jamaa kalenga jambo.

'Mimi eeh, nimekwenda mbali sio.., najua utakuwa mgumu kwa hilo......sasa kipi bora, nyumba yako ipigwe mnada kwa ajili ya milion chache ulizokopa au...nichukue mimi hiyo nyumba, halafu nipambane na huyo anayekudai,...na dada angelikuwepo, ningewachia muishi,humo, lakini kwa vile...’hapo akatulia.

'Siwezi kufanya ujinga huo, unajua thamani ya ile nyumba,...hahaha, eti ipigwe mnada, kwa deni gani hilo,....hata hivyo, mimi nitamlipa huyo jamaa pesa yake...’nikasema

'Hahaha, wewe mpuuzi, kweli kweli, sitamani hata kukuita shemeji, hebu niambie kwa hali yako, wewe utapatia wapi hizo  pesa, kapuku kama wewe , dada yangu mjinga kweli kweli, sijui alipumbazika na nini kukubali wewe uwe mke wake,..’akakohoa
 Mfululizo, nahisi mate yalimkoholeza.

‘Dada kuolewa na masikini kama wewe ni kosa kubwa sana... wewe hujui tu, ...wakati nyie mumeishiwa kabisa, mimi ndiye nilikuwa nawalisha, sikutaka dada yangu akuambie hilo ila leo nimekuambia ili uelewe kosa ulilolifanya...kiukweli mimi nampenda sana dada yangu, na sikutaka apate shida...’akatulia kidogo

‘Lakini sio kweli, angeliniambia ...’nikajitetea

‘Hivi wewe hukuwa unaona ajabu, ukirudi nyumbani unakuta  chakula kipo, wakati hujaacha hata senti moja, ulifikiri mke angelikula wapi, wakati hukutaka hata aende sokoni, eeh...usitake niseme mengi..’akasema hivyo

Kiukweli, kipindi nimekwamba kabisa, kuna wakati nikrudi nyumbani nikiwa sijaacha chochote, bado nakuta chakula, ...na kila nikitaka kufunua mdomo kumuuliza mke wangu najikuta nashikwa na kigugumizi,ungesema nini tena, huna kitu, nilijua ni jitahada za mke za hapa na pale, ...sikufikia kumdahani mke wangu vibaya...ila  nilishafikia wakati, nilitaka nimuulize...bahati mbaya ndio yakatokea haya ya kutokea.


‘Sasa shemu, nilitumai wewe umewahi kuja hapa jela, kwa nia ya  kunisaidia mimi nitoke hapa, hapa sio sehemu nzuri, na natakiwa kufuatilia maswala ya...ooh, hata sijui kinachoendelea,..sasa wewe kumbe  umekuja kuniongezea maumivu tu, huo ndio ubinadamu gani shemu,?’ nikauliza.

‘Hahaha, mimi nije kukusaidia wewe,...kama ningelipewa nafasi, ya kukufanya chochote,mimi ningekukata kata vipande niwe nameza nyama yako..na kuitema, mimi nakuchukia, unajua kuchukia, we acha tu, lakini siku zinahesabika ..utakuja kuona ..’akasema kwa sauti ya kibabe.

‘Lakini kosa langu ni....’ kabla sijamaliza, akaendelea kusema;

‘Na nikuambie ukweli... kama ingelifaa, mimi ninataka wewe wakufunge ufie huko huko jela,..hapo ndio moyo wangu utatulia, lakini kwanza, kabla hujaenda kuzimu..nataka unilipe..na malipo yangu, kama nilivyokuambia, ...’akatulia.

‘Kuwa ....’nikataka kuongea anakiniashiria kwa mkono ninyamaze kwanza

Nimeshakuambia...nataka nyumba , hilo sikutanii...mimi nitakuja na hati ya makubaliano, ..la sivyo, jamaa mwenye deni atakuja kwako...unamjua alivyo...na ukumbuke yeye anajua mengi kukuhusu wewe...si niliwahi kukugusia,...anakujua fika, kuwa wewe ni muuaji, ..lakini nilikudhamini mimi...’akasema.

‘Sasa kwanini wewe ulinidhamini...?’nikauliza sasa kwa mashaka, maana niliona kweli huyu mtu alinitega.

‘Hahaha, bwege mkubwa wewe..nilishakuambia, mimi siwezi kukufanya jambo kwako lenye manufaaa na wewe..., maana wewe ni nani kwangu, muuaji mkubwa wewe, usitake ni badilike hapa, ..’akanisogelea, nilijua kichwa kinakuja nikakwepa hewa.

‘Hahaha, unakwepa nini sasa, mimi sio mjinga,... hapa siwezi kukufanya hivyo, ila ujue jambo moja, wewe na mimi, ni kama mafuta na maji, eeh, na ,...utajuta kuzaliwa kwa ulichomfanyia dada eeh...sijaanza malipizo yake bado...’akasonya.

‘Lakini ..eeh ili twende sawa, niume na kupiliza...fanya nilivyokuambia,...na unaweza kuona utanivunga, au utasita kukubaliana na mimi...kwanza ukumbuke, mimi ndiye nilitoa kauli ya kukusaidia,..lakini ile ni kauli tata,....bado haina mshiko, kuwa, nilisema hivyo, kuwa dada yangu alikupiga,..hiyo haina mshiko saana, ...’akawa ananichoma choma ni kidole kifuani.

‘Mimi naweza kuitengua hiyo kauli wakati wowote..kumbuka jela kulivyo...eeh, uliponea tundu la sindani, unakumbuka, eeh...sasa kule ni cha mtoto, huko..Ukonga, kule wapo jamaa zangu wengi tu, tunajuana...usijali kwa vipi..., nilishawatipu, ukikanyaga tu pale Ukonga, wewe ni chakula chao, utashindwa hata kutembea..hahaha...’akasimama na kuanza kuondoka.

Nilibakia nimeduwaa...maana nimjuavyo huyu jamaa hana utani, akisema jambo, hatanii....nitafanya nini sasa, dada yake wa kunitetea ndio hivyo hayupo,..jamaa aliponiona nimeduwaa, akarudi na kuanza kunipiga piga begani kwa ngumi kama kunipa moyo, lakini upigaji wake  unahsi  maumivu...nikawa najaribu kuukwepa huo mkono.

‘Sikiliza hii ni dili, hati inakuja,..tena sio kesho leo...na jiulize ni kwanini hadi sasa hujapelekwa Ukonga, eeh...jibu unalo, si ndio hivyo, mimi natoka hapa, nakwenda kwa mwanasheria wangu, keshaikamilisha hiyo hati,..nikirudi tutaelewana, ..’akahema kidogo.

‘Shemu,....’nikataka kusema neon, jamaa akanitolea macho,...halafu akasema;

‘Hata hivyo, wewe una thamani gani..ulitakiwe ufe...nyumba ile ni yangu kwa hivi sasa,..na mimi nitamlipa huyo anayekudai, unasikia, mengine niachie mimi...natumaii umenielewa, mimi sitaki longo longo...unanijua nilivyo..’akaanza kuondoka.

 Kabla hajafika mlangoni, mlangoo ukagongwa, jamaa akavaa miwani yake kwa haraka, mlango ukafunguliwa, mtu wa jamii akaingia, nyuma yake yupo mtu wa dini. Nilifahamu huyo ni mtu wa dini kutokana na mavazi yake, ..moyoni nikasema, huyu mtu wa jamii hana la kunisaidia, yeye kaenda kunileta huyo mtu wa dini  ili aniombee..kuombewa kwa hivi sasa kutasaidia nini kwa hali kama hii.

‘Hapa ninakabiliwa na kesi ya mauaji...na huyu shemu sasa hivi tu, kaniletea janga jingine, anataka nyumba iwe yake kitapeli,..nitafanyaje sasa...nyumba ndio mali yangu pekee ya kujivunia, kiukweli ni nyumba nzuri, na niliijenga kwa gharama kubwa sana...’nikawa nawaza hivyo.

Shemu akasita kuondoka akawa kasimama, na mtu wa jamii, akamsalimia ..lakini shemu hakuitikia hiyo salamu, jamaa akawa kama kashikilia mlango, lakini akawa kasimama tu.

‘Nimekuja, ..kuanza kazi, ..na..huyu ni mtu wa dini, kuna mambo nataka atusaidie,..nikuulize jambo moja,.’akasema mtu wa jamii, kwanza akageuka kumuangalia shemu, shemu akajifanya kama anataka kufungua mlango, lakini hakufanya hivyo kwa haraka.

‘Umeshapata taarifa yoyote, ya kuhusu mkeo, ..je kuna taratibu zozote, maana nijuavyo mimi , nilivyosikia,..mwili wake umehifadhiwa, sehemu ambayo haitakiwi kuonekana...’akasema mtu wa jamii.

‘Mwili wake una maana gani kusema hivyo...?’ nikauliza sasa kwa mashaka, ujue kukweli kuna hisia mbili akilini mwangu, kuna hisia ambayo, bado inatamani kuwa mke wangu bado yupo hai, nyingine inahisi kuwa mimi nimemuua mke wangu.

‘Ina maana huna taarifa hizo, au...?’ akasema mtu wa jamii, sasa na yeye akionyesha wasiwasi Fulani hivi.

Sasa sauti ikatokea mlangoni...

‘Una unakika na unachokisema wewe, ni nani wewe kwanza, wa kumuongelea dada yangu, eeh..mwili, mwili, .....?’ ilkuwa sauti nzito ya shemu, na sasa alikuwa anakuja kukabiliana na mtu wa jamii, sote tukabakia kushangaa,  tukawa tunamuangalia tu..nilitaka kumuambia mtu wa jamii awe makini, maana huyo jamaa kichwa kinamtoka kama mshale..


WAZO LA LEO: Tuweni makini na mikataba tunayoandikishana, hasa ya madeni,na ikiwa ni lazima kuandikishana hivyo, tuhakikishe tumepata ushauri wa mawakili, kabla hatujaweka sahihi zetu,..kwani sio kile anayekuchekea, ana furaha na wewe.
Ni mimi: emu-three

No comments :