Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, September 23, 2019

KILA MCHUMA JANGA...2



KILA MCHUMA JANGA.....

'Mwiziii, mwizi...'ni kelele za asubuh, asubuh....haikupita muda, tukaona moto. Ulikuwa moto mkali na mlio wa kitu kama kinapasuka ukasikika...
Awali tulijua ni ajali...kwa haraka mimi nikajongea japo sio karibu na kwenye tukioa...nikaona watu wakimbeba mama mmoja...

‘Vipi ni ajali ya moto...?’ nikauliza

‘Hapana, ni mwizi...’akasema jamaa mmoja akikimbia mbali na eneo la tukio, sikupenda hili tukio linipite, mwizi..halafu moto, akilini nikahisi vinginevyo, lakini mwizi ..adhabu yake iwe hiyo, akili haikunipa amani, nikazidi kusogea, na watu wakawa wanakimbia ..nikajua huenda ni polisi, nikasimama, na bahati nzuri wakatokea watu wengine walikuwa hawana hawakimbii

‘Vipi moto wa nini ule...?’ nikauliza..


'Ni adhabu ya moto, hao watu dawa yao ni kuwachoma moto tu..'akasema shuhuda mmoja.


'Mumemchoma moto kibaka!' Mzee mmoja akang'aka huyu alikuwa miongoni mwa hao watu, lakini alionekana na huzuni kubwa usono


'Ndio....nyie wazee ndio mnatufugia wezi,...’akasema shuhuda

‘Lakini sio kwa adhabu hiyo, mnaona Yule mama yake alivyopoteza fahamu, mimi namfahamu sana Yule mama, mimi namfahamu sana huyu kijana ..mareh-hemu...’huyu mzee akasema sasa kwa uchungu.

‘Mzee, na bado..hata Yule kijana wako..siku zake zinahesabiwa,....hawa watu wanatusumbua sana , tunafanya kazi, tunaumia huku na kule, hawa, vibaka, watoto wa hawa wazee...wanatuibia, leo zaa arubaini zake zimefika,.hiyo ndio adhabu yao...' akasema mtu mwingine.

‘Sawa...nyie hamjui tu..sisi wazee, tumejichokea, twawategemea nyie...sasa kama mnaiba sisi hatujui tufanyeje...eeh, sikizliza niwaambie..yule mama, ni mama mjane, na Yule mtoto alikuwa mtoto wake pekee...yule mama ana maradhi mabaya sana, dawa zake ni aghali kupundikia,..na mtoto wake alimuahidi mama yake, atamuhudumia ,,mpaka mwisho..’akasema mzee

‘Ndio atuibie...’akasema Yule shuhuda.

‘Sikiliza sasa nikuambie, ulisikia Yule mama kabla ya kupoteza fahamu , baada ya kushuhudia mtoto wake akiteketea na moto alisemaje...’ni kosa langu, ni kosa la maradhi yangu..sasa nitaishije, na mimi nichomeni moto...ndio akapoteza fahamu..mnafahamu fumbo hilo..nawaambia ukweli...kwa hili hamtaishia kwema, ...’akasema huyo mzee

‘Mtatuloga eeh, ndio mnafikiria hivyo, mzee, nakuambia hili na usikie....hamtuwezi mzee, sisi tunalindwa na damu.....’sikusikia alichoendelea kuongea, mimi akili ilishazama kuwazia, kauli ya huyo mzee...

‘...yule mama, ni mama mjane, na Yule mtoto alikuwa mtoto wake pekee...yule mama ana maradhi mabaya sana, dawa zake ni aghali kupundikia,..na mtoto wake alimuahidi mama yake, atamuhudumia ,,mpaka mwisho..’

Nikapanga nije kuongea na huyo mzee, nikisikie kisa kamili cha huyo mama mjane...


Leo asubuhi hii...., eneo la relini, huko Kipunguni... wakati tunapita tukashuhudia moto ukiwaka, kuulizia, tukaambiwa ni mwizi wa bajaji anachomwa moto....!


‘Mhh..mwezi tena, na adhabu yake ni kuchomwa moto ....hivi kweli  mwizi adhabu yake ni kuchomwa moto, nikauliza wenzangu, na mjadala ukazuka.....sitapenda kuuandika  huo mjadala hapa, jadilini na wenzeko uko mlipo,...

 
Ni kweli huyo mwizi anayechomwa moto  akawa ni jambazi kweli na kiukweli..., jambazi ni muuaji, anaiba hata kuua, huyu, kwa vile anaua, ilitakiwa naye auwawe...hata hivyo, jambazi akifikishwa jela...kuna sheria za haki za binadamu, zinawatetea, kuwa muuaji asiuwawe...hapa sasa naona ajabu, kibaka anachomwa moto!


'Jambazi alianiza huko kwenye ukibaka..tunatakiwa tumuwahi mapema, kwa kumchoma moto...’nikakumbuka kauli ya Yule shuhuda.
.
‘ Hii sasa ndio adhabu ya wezi,...’alisema mwingine, swali nikamuuliza, je wewe hujawahi kuiba, ofisini kwako kila siku unamuibia muajiri wako,...nawewe dereva wa bajaji, kila siku mnawadhulumu abiria, ...

‘Lakini sisi tunaiba kiujanga...’wakajitetea

Huko tupaache....


 Tujiulize swali moja, ni kwanini raia wanachukua sheria mikononi mwao..na hili kosa la wezi, wavunja sheria, ni kosa la nani, ni nani alaumiwe...

Raia wanajitetea kuwa wameamua kufanya hivyo kujichukulia sheria mikononi mwao, eti..wezi hao wakikamatwa, wakipelekwa vituoni, kesho yake wapo mitaani,..hata jambazi katetewa na haki za binadamu, karudi mitaani tena ..sasa ni ni jamabazi sugu , mwaliwa wa majambazi... je hili ni Kosa ni la nani...!


Kuna wakati tuliandika habari za majirani kugombana, kisa ni mtoto... !


Mtoto kadokoa kitu cha jirani, mzazi jirani akamuadhibu huyo mtoto mdokozi, mama wa mtoto mdokozi akaja juu, kwanini mwanae kachapwa, ikawa kesi, maana kesi ya mtoto, iliwafanya wazazi wa pande mbili kuingilia kati na kuanza kugombana...hili ni janga..tumelianza wenyewe..sijui mnanielewa hapa...


Tatizo huanzia hapa, tunalichuma janga sis wenyewe na kuliingiza majumbani kwetu...janga hili limeanzia kwenye malezi ya watoto, hakuna elimu ya dini, ilitakiwa shule za watoto wadogo ziwe za kidini, iwe ni sheria, watoto chini ya miaka saba, kwanza wapiti shule za kidini..tutengeze kizazi cha waumini wa kweli..dini mnazipiga vita mnategemea nini...majanga tunayapanga sisi wenyewe.
.
Jukumu la ulezi wa watoto huanzia kwa mzazi, sawa..jirani ni mzazi, sawa, je jirani yupo tayari mtoto wake aadhibiwe na mzazi mwimngine..hilo hatupendi..serikali, nayo vipi,...kwanini mnataka shule za watoto za kufundidhs lugha za kigeni,lakini swala la dini, la kuwajenga watoto kiimani hamlipi kipaumbele..eti mnaogopa imani kali..haya tuone,...kama mtu hamuogopi mungu wake ataogopa kuiba,na kuiba, sio lazima bajaji,..hao walanguzi,wezi wa mali ya umma, wao sio wezi kwanini hawachomwi moto, tusipolitambua hili, tutakuwa tunajenga janga...!


Nawausia enyi wenzangu, yapo mengi tunayapuuzia, vizazi sasa vinaharibika, tuanze sasa kuchukua tahadhari...elimu ya dini inahitajika sana..tena sana, ...elimu sio lugha tu, lakini kuna elimu muhimu ya IMANI..ya kumuogopa Yule muumbaji wetu, ili mtu aaogope kuiba hata akiwa peke yake, tusipolitambua hili, basi tutarajie kuzalisha wezi, mabaradhulu, mashoga..wavuta unga...nk...na amani itakuwa ni msamiati adimu. Wahenga walisemaje, Kila mchuma janga..., itakuwaje vile...



Ni mimi: emu-three

No comments :