Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, July 12, 2019

IMANI HUTOKA MOYONI


IMANI YA KWELI HUTOKA MOYONI , NA SIRI HIYO AIJUE NI MOLA PEKEE.

Hiki sio kisa ni ukweli,

Katika maisha yangu… niliwahi kuajiriwa kwenye kampuni moja, nilipofika hapo nikazoeana na msichana mmoja,…nilimzoea kwa vile yeye ndiye alinikaribisha, na kunionyesha mazingira ya hapo kazini, ufanyeje, uende wapi kiutawala na sehemu ya kula, ofsini ipi ni ipo, vitu kama hivyo.

Basi kila nikihitajia kitu namuuliza yeye, na kiukweli hakuwa na hiyana, aliweza kunielekeza vyema tu, na kuna muda watu wakaanza kutuangalia kwa macho ya kujiuliza, huenda tumekuwa marafiki, lakini moyoni mwangu sikuwa na mawazo hayo kabisa.

Siku zikapita, na ule ukaribu wetu na huyo mdada ukapungua, maana sikuwa na cha kumuuliza tena, mimi nipo idara nyingine na yeye yupo idara nyingine, …sasa katika mazungumzo, nikaja kujua kuwa huyo msichana ni wale wenye msimamo mkali…mtakuwa marafiki lakini sio kwenye tendo la ndoa.

‘Huyu dada ni bikira bwana,…’watu wakawa wanamtania.

‘Labda bikira wa sehemu nyingine, mimi sidanganyiki  ‘mmoja akasema.

‘Kwanini, na wewe unamfahamu, tokea tuajiriwe hapa ulishawahi kumuona na mvulana, ..maana hapa hakuna siri, na hata huko nyumbani kwake si unakufahamu, uliwahi kumuona akiwa na mvulana..?’ akaulizwa.

‘Siri ya mtu anaijua yeye mwenyewe..ila mimi siamini kwa umri ule, atakuwa bado bikira, ni lazima atakuwa na mtu wa siri..’akasema huyo jamaa, na wengi hawakumshabikia, waliona ni wale wasiopenda maendeleo yaw engine.

Ikawa ni utani tu, wengi wakawa wanamtania huyo mdada kwa kumuita ‘sister bikira..’ akawa anaitwa hivyo.

Kiukweli mimi sikuweza kumuuliza huyo mdada kama hayo maneno na utani yana ukweli ndani yake,..niliamini kuwa yawezekana,…mtu ukiamua unaweza ukaishii hivyo,, na kwa vile ule ukaribiu wetu wa kumuuliza hiki na kile ulishakwisha, nikawa sikupata muda wa kuwa naye karibu tena, kila mtu kwenye idara yake na maisha yakaendelea.\

 Ila mimi niliamini waliyosema watu kuwa huyo mdada ni mgumu, sivyo kama walivyokuwa wanadada wengine, huyo mdada hakuwahi kuwa na rafiki wa kiume, niliyewahi kumuona au kuambiwa …kama ilitokea kukutana naye hasa kwenye chakula maana tulikuwa na mgawahawa wafanyakazi wote hukutana humo, huyo mdada..alionekana kivyake vyake tu..na ole mvulana ajaribu kumgusa, hata kiutani, ataambulia matusi,…

Hapo kazini karibu kila mmoja alijulikana ni nani na mwenzake wa jinsia tofauti ni nani, na wengine wakatokea hata kuoana kabisa,…lakini kwa miaka kadhaa niliyofanya hapo, sikuweza kumgundua rafiki wa huyo msichana…moyoni nikasema,..basi huyo ni ‘sister bikira kweli’.

Miaka kama miwili ikapita…nikaja kufikiria kama mimi nina tabia yangu kuwa  msichana wangu wa kwanza kukutana naye nikutane naye ndani ya ndoa, sasa kwanini nisifanye urafiki na huyo mdada, ambaye naye anaonekana ana msimamo huo..lilikuwa wazo katika kuhangaika kumpata mwenza wa maisha, ilikuwa wazo, na nikawa na mikakati hiyo, lakini siweza kulifanikisha, maana kiukweli moyoni sikuweza kuvutika na mdada huyo kimapenzi. Nafsi hupenda kile kinachomvutia mtu.

Bahati mbaya, nikahama hiyo kampuni…

Baada ya miaka kadhaa, nikasikia, kuwa yule msichana kafariki,

‘Kafariki!!!... ilikuwaje jamani…?’ nikauliza kwa mshangao na masikitiko.

‘Alianza kuumwa, umwa..akawa anapungua, baadae akazidiwa, anatibiwa, anapona hali inarejea, anaanza kuumwa tena,..baadae..akapelekwa kwao…yaani binadamu hubadilika haraka sana, unamfahamu jinsi alivyokuwa mrembo,...watu waliomuoana kipindi kazidiwa, wanasema ule urembo ulikwisha akawa kama mzee, alikuja kubadilika akawa…mweusi….’akasema jamaa,

‘Mhh...kwasababu ya huko kuumwa au, , kwani alikuwa anaumwa nini…?’ nikauliza moyo sasa ukinienda mbio. 

Unajua kipindi cha nyuma, watu wakiumwa sana, na kukonda, na kubadilika mwili, moja kwa moja unajau ni ugonjwa gani,..kipindi hiho kulikuwa hakuna dawa za kusaidia kuongeza nguvu, kwahiyo watu wengi waliougua ugonjwa huo, waliteseka sana kabla ya umri wao kuisha. Kwa vyovyote iwavayo kila mtu ana umri wake.

‘Unauliza jibu bwana, mdada alipatwa na maambukizi, na ..huwezi amini, ..hata ndugu zake hawakuamini wakasema kalogwa, lakini hakuna siri, aliyemuambukiza aligundulikana, kwani naye kwa kipindi hicho alikuwa akiugua ugonjwa huo huo..na alipoulizwa, yeye alidai huyo mdada ndiye kamuambukiza, lakini uchunguzi zaidi ulionyesha kuwa huyo mvulana alikuwa hajatulia, yeye ndiye alimuambukiza huyo msichana.

‘Mhh..lakini si mlisema huyo mdada ni bikira.

‘Hahaha, tulijua hivyo, kiukweli hata mimi niliamini hivyo…hadi msichana huyo anafikia kuumwa, sote tuliamini hivyo….’akasema.

‘Haiwezekani…japokuwa kila kifo lazima kiwe na sababu..nahis aiumwa maradhi mengine tu..hata hivyo....’nikasema na jamaa akanikatisha kwa kusema.

‘Iliwezekana sasa, na alitembea na cha pombe fulani, wakati yeye alikuwa akituzarau pale kazini kuwa hatuna maana, walevi, eeh..si unakumbuka, alivyokuwa,akitudharau, ...wewe uliondoka, sasa ilifikia mahali hamgusi mtu....anasema yeye ana bwana wake yupo Ulaya...sasa kumbe alikuwa na mvulana cha pombe tu..hakuwa na hadhi kwa yule mdada,…sijui ilikuwaje..masikini mungu amsamahe tu...’akasema huyo jamaa.

‘Kwani hamkujua ilikuwaje..?’ nikauliza.

‘Aaah. ilikuwa kujulikana dunia hii ina siri,na kwa vile alikuwa akiringa, jamaa zake walikuja kuvujisha siri..tukajua kila kitu, ikawa kufuatilia kuhakiki tu....unajua msijifanmye mna imani sana ya dini, aheri muwe kama sisi...unajua imani. ya.kweli ya mtu aijue ni mungu pekee, ujidanganya ipo sisku imani hiyo inataisha kidogo kidogo kama mshumaa unavyokwisha halafu utakuja kuumbuka, ila niliumia sana, yule mdada nilimpenda, nilitamani nimuoe, akanikataa,…’akasema huyo jamaa akionyesha kusikitika.

'Mhh..lakini kweli wewe ukizi  kulewa, nani angekubali umuoe....'nikasema kwa utani.

'A wapi mimi nilikuwa nakunywa kistaarabu, sema, ndio hivyo kila kitu kwa wakati wake, ni kweli kuna muda nilizidisha, nikaumwa karibu ya kufa...kifua ikawa TB,...aisee, nilijua nakufa...nilipopona nikabadilika, ...hapo nikaona umuhimu wa kuoa...sasa huyo mdada alitolea nje kabisa, ..'akasema

'Labda alikuwa na mtu wake kweli...'nikasema

'Ndio yupo jamaa mmoja yupo Ulaya kweli, lakini jamaa huyo akaja kumuoa mzungu, na ndio maana huyo mdada akachanganyikiwa akaanza kulewa...japo hakujionyesha,...nasikia ndio hapo akaja kukumbana na cha pombe..lakini kwa siri kubwa...hayo ni mambo ya ndani, ...'akasema

'Oh, siku zake zilishafika...'nikasema

 Ni kweli kwa taarifa za kifamilia, japo ilikuwa siri, msichana huyo alifariki kwa HIV, kutokana na dalili, na hata vipimo,  kiukweli mimi sikuamini, wengi hawakuamini..japo kwa hivi sasa HIV, unaweza kuipata kwa njia nyingine ila kwa huyo mdada ilikuja kuthibistishwa..aliipata kwa namna gani

Watu katika kuchunguza sana, kumbe, huyo mdada alikuwa akitembea na mvulana kwa siri sana kwa vile alikuwa ni jirani yake..ilikuwa ni kwa siri sana…wanasema alifanya hivyo kwa siri, na hakufanya kwa vile anampenda huyo mvulana, maana kiukweli hawakuwa wanaendana..ila kulikuwa na sababu za kuchanganyikiwa....

Ilivyoonekana, alifanya hivyo, pale anapozidiwa, mawazo na mengine yaliyokuja kusemwa baadae msichana huyo akatokea kuwa mpweke, alikuwa hana rafiki tena, akawa anawachukia wanaume, kila mwanume kwake ni sawa na huyo aliyemuacha solemba, swali likawa ilikuwaje huyo cha pombe amuone sio sawa na wanaume wengine.

Tatizo huyo msichana hakupenbda kuwa muwazi, na .maumbile ya kibinadamu hufikia sehemu utashindwa kuvumilia hasa ukiwa unatumia kilevi..kiukweli yasemakana, siku katika masiku ubinadamu ulimzidi, akakwaana na huyo mvulana, ilikuwa kwa bahati mbaya tu kama alivyokuja kusema..

'Hiyo bahati mbaya, ikaja kuwa mazoea hasa akizidiwa, 'alijitetea.

'Ilikuwa nawaza sana, ..mpaka nataka kujiua,...sasa huyo mvulana akawa ndiye mtu wangu wa karibu wa kuniliwaza,,,akawa anakuja kwangu, usiku wa manane maana nilikuwa naishi naye nyumba moja sema ni chumba tofauti, wote ni wapangaji'

Kiukweli huyo msichana  hakutaka kabisa watu wajue, na kiukweli hakumpenda kabisa huyo mvulana,..na yeye alitaka watu wajue kuwa yupo hivyo, ..bikira. Ila kilichoharibu ni kwa sababu ya huyo mchumba wake kumtelekeza.

Na zaidi ya hapo huyo mdada ndoto zake, zilikuwa  yeye aje kuolewa na watu wenye uwezo kwasababu wapo wengi walimtaka tena kindoa akawakataa.

‘Mimi siwezi kuolewa na mtu kama huyo…hana nyumba wala gari….mmh, mimi siwezi kuolewa na mtu kama huyo hajasoma,..ikawa zake ndio hivyo, siku zikaenda, hadi mauti yanamkuta,
Sasa ilikuwaje aje kutembea na huyo mvulana, ambaye hata kazi ya maana hana,..msikuma mkokoteni, na akipata peza zke ni kulewa tu,..siri ikaja kuvuja,!

**********

Inatokea, kiubinadamu,..tunahitajia umaarufu Fulani, lakini umaarufu huo, uwe wa kweli  , utoke moyoni. Usiwe wa kuwaonyesha wanadamu tu....na hasa umaarufu wa imani. 

Umaarufu wa imani haudanganyiki, utawadanganya wanadamu wenzao, lakini sio muumba wetu,…mola wetu anatufahamu zaidi tunavyojifahamu wenyewe, yeye anajua imani ya mja wake ni ipi ya kweli. Kiukweli  wapo wanajitahidi lakini nafsini mwao, kuna mambo mengi ya tamaa, husuda chuki, nk...na, wapo wanafanya mengi mabaya kwa hisia..nafsi zao zina siri kubwa sana.

Cha muhimu ni kumuomba mole wetu atusaidie tuweze kufikia malengo yetu..yale tunayotamani yawe, yale ya haki, yaweze kuwa hivyo,..na atusaidie kuziondoa tamaa mbaya nafsini mwetu, atujalie tuweze kuwapata wenza wema katika maisha yetu.


Ni mimi: emu-three

1 comment :

Anonymous said...

Wow, this post is pleasant, my sister is analyzing these things, so I am going to inform her.