Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Saturday, July 6, 2019

HUJAFA HUJAUMBIKA...



'Hivi kwanini mimi,...., nimemkosea nini mwenyezimungu...'nilisikia suti hiyo ya huzuni na kunifanya nisimame ghafla, na kunifanya nisite kuendekea na safari yangu, nilihisi mwili ukinisisimuka...'nimemkosea ni mwenyezimungu...' kauli hiyo ilinifanya nigeuze kichwa kuangalia kule nilipohisi sauti hiyo imetokea.

'Oh Mungu, nimekosa nini mimi jamani mpaka nipitie majaribu yote haya, ..mungu wangu naomba unionyeshe tu njia...'maneno ya huzuni yaliendelea wakati huo nimeshageuza kichwa kuangalia sauti hiyo inatokea kwa nani.

Kwa sauti tu,nilihisi ni sauti ya mwanadada, lakini macho yangu yalipotua kwa huyo ninayehisi kuwa ndiye aliyekuwa wakiongea, niligwaya.

Alikuwa binti mdogo sana, tofauti na nilivyodhania.

Kwanza kwa tahadhari nilitembeza macho huku na kule..maana dunia hii imegauka sivyo ndivyo, ya walimwengu ni mengi... kuna mitego mingi ya wahalifu inafanyika hivyo, unajitoa kwa wema unaangukia kwenye mitego ya hao watu, wanakudhuru au kukunyanganya kila na kukuacha uchi. Ila kilichonitia matumaini ni kuwa eneo hilo lina nyumba za watu, na nyumba nyingi ni kubwa zenye ukuta, na wengi wameweka nyaya za ulinzi, kuashiria kuwa wanaoishii humo ni watu wenye uwezo wao.

Niliangalia eneo lile alipokuwa huyo binti..nyumba hiyo kama nyingine ilikuwa na ukuta mkubwa tu na, ..juu yake ilionyesha kuna ulinzi wa kitaalam, ..nikajiuliza huyo binti anafanya nini kwenye eneo hilo, ..hajui kuwa nyumba hiyo ina ulinzi, na wenye nyumba hiyo hawatakubali watu kukaa eneo hilo kiusalama...na kwanini kakaa hapo, na anamlilia nani..

Nilipoona nazidi kutingwa na maswali, ....nikaamua jambo, nikavuta hatua moja, mbili....kabla sijafika pale alipo huyo binti,...na ukumbuke kwa muda huo, bado alikuwa akiongea kwa kulalamika kuhusu masahibu anayokumbana nayo...

Mwili uliendelea kunisisimuka, na hii ni kuashiria kuwa kuna hatari,...mimi nina hisia hizo, mwili ukinisisimuka, ujue kuna jambo la hatari ...lakini nafsi haikunipa uwoga, nafsi ilinipa ujasiri, kuwa nahitajia kujua, nikijua nitajua la kufanya...nikawa sasa navuta hatua, ...

'Ewe mola wangu, nionyeshe kosa langu, hadi nitaabike hivi...nimekuwa mtumwa wa walimwengu, wananichezea kama mpira wa karatasi, naadhirika, na hata wale niliowategemea kuwa watakuwa msaada kwangu wanageuka kunidha....dha...lilisha...'hapo kwikwi ya kilio.

Hapo na mimi nikasita mguu ukawa mnzito kuendelea ...nikatulia kwanza, akilini nikichanganua, je haya ni yangu, ..yasije yakawa maji mazito kwangu, ..aah, nikajipa moyo, ..ngoja nikasikia kwa kulikono,...nikaendelea kutembea...na sikuvuta hatua mbili, mara nikasikia...

'Mimi  ...siwezi tena..bora nife ..bora nijiue.'

Mungu wangu, bora nijiue...

Hapo sikuweza kusubiria, nikahisi nina dhamana, hii ni dhamana maana ni kwanini mola akanifanya niweze kuyasikia hayo, na ni kwanini, niache kiumbe kama huyu ..binti mdogo tu, aje kufanya, hilo alolodhamiria,na ni mashahibu gani yamemkuta hadi kufikia kudhamiria hivyo. Nafsi ikaingiwa na mshawashwa,..ikatamani kujua,...

Nikamsogelea,,,,.

Hata pale niliposegea hadi kumkaribia, bado alikuwa hajafahamu kuwa kuna mtu alikuwa bado hajafahamu kuwa mimi nipo hapo karibu yake, na hata kabla sijaweza kutoa sauti ya kumsalimia huyo binti , nikasikia sauti kali ikitokea ndani mwa hiyo nyumba, ambapo huyo binti kajiegemeza ukutani mwake.

'Huyu mshenzi kaenda wapi....we Taabu, ...we Taabu,...' sauti hiyo ilimfanya yule binti akaurupuke, na kusimama, hapo akaniona, akashika mkono kuziba mdomoni, lakini ...

'Usigope mimi sio mtu mbaya
'Ina maana umesikia nilichokuwa nikiongea
'Hapana...sijui uliongea nini...'nikasema
'Mungu wangu ..'akasema hivyo tu na haraka akakimbilia ndani

Kesho yake nilipita eneo hilo tena, nia ni kukutana na huyo binti, nijue ni nini kinachoendelea kwenye hiyo nyumba, nilipofika hapo nilikuwa watu wamejikusanya
'Kuna nini jamani...?' nikauliza
'Kuna binti kataka kujiua,...'akasema
'Kwanini
'Hata sisi tumebakia kujiuliza tu, na wenye nyumba hawataki kuelezea ukweli, wanasema hata wao hawajui
 Mara nikaona gari la wagonjwa likitoka, ..nikajua watakuwa wamemuwahi, ...
'Akipona ashukuru mungu...'ilikuwa kauli ya askari mmoja aliyetoka kwenye hiyo nyumba
'Kwanini unasema hivyo?'
'Sumu aliyokunywa ni kali sana...na walichelewa kutoa taarifa...'akasema askari

Kiukweli niliumia sana, ni kwanini sikufanya jitihada za ziada kukutana na huyo binti, nikasema na hata hivyo sikukata tamaa, nikafanya utafiti kujua huyo binti kapelekwa hospitalini gani, na wakati nauliza uliza ndio nikakutana na mama mmoja aliyesema anamfahamu huyo binti tokea akiwa mdogo.

'Sasa kwanini kakimbilia kutaka kujiua...?' nikauliza

'Mhh...we acha tu, hujafa hujaumbika, usilolijua ni sawa na kiza cha totoro...yule binti kapitia masahibu mengi, na huwezi amini huyo anayeishi naye ni mama wa kambo, mama yake alishafariki....

NB: Bado tupo kwenye maajribio, ili tuweze kurudi tena.

Ni mimi: emu-three

1 comment :

Anonymous said...

Endeleza basi, twakusubiria kwa hamu