Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, March 5, 2019

LA KUVUNDA HALINA UBANI...


 Ni wakati nipo msibani macho yangu, yalitua kwa mtoto mmoja aliyekuwa akilia sana, cha ajabu kilichonishangaza mimi,  hakuna hata mtu mmoja aliyemjali, …nilijiuliza ni kwanini, kiukweli hali yake hasa kimavazi haikuonekana njema, nguo zilikuwa chafu, na kuukuu. Hata hali yake ya kiafya yaonekana ni dhoofu…lakini naye ni muombolezaji, naye ana uchungu,….na…
Nahisi huo msiba umemgusa,…na sijui….

Nikageuka huku na kule, nikiwaangalia watu wengine,  watu hapo kwa ujumla  walikuwa kwenye majonzi makubwa,  wengi walikuwa wakilia, wengine wakionyesha nyuso za huzuni,…ilimradi kila mmoja alikuwa kaguzwa na huo, masiba.

Kuna wengine walilia hadi kupoteza fahamu…na watu kama hao, walikuwa na jamaa zao wa akaribu wa kuwaliwaza,..lakini huyu …mtoto, niliyemuona awali, hana…hana hata wa kumkaribia, kila aliyemuona alimtupia jicho moja, na kujifanya hajamuona…, swali akilini mwangu likawa linajiuliza, ni sawa, wengi wameguswa na msiba huo, hata kama sio ndugu wa karibu wa marehemu kivile…na wengi wanalia,…je huyu naye analia kwasababu gani…ni ndugu wa karibu,….au ….

Hamasa ya kufahamu zaidi ikanivuta….

Nikaamua kufanya jambo, …hata hivyo, awali haikuwa rahisi,..maana kulikuwa na watu wengi  mbele yangu na kwa wingi wa watu, nisingeliweza kuwapita  kwa urahisi, nafasi ilikuwa ndogo, ukiondoka sehemu mwingine anakuja kukaa…aah, hata hivyo, hamasa ilizidi…
Niligeuka kumuangalia tena,….bado alikuwa akilia, …tena kwa kwa huzuni kubwa,…hata mimi, pale nilipo, nikavutwa na hisia za kulia,….

Msiba unauma jamani….

Kiukweli msiba unauma…na unauma zaidi kutegemeana na mtu huyo alikuwaje mbele ya jamii, na zaidi kutegemeana na waombolezaji , na je kaacha nini nyuma yake,…watoto, mke au jamaa waliokuwa wakimtegemea, na zaidi ….hata waombolezaji wenyewe, au wana habari, wanaweza kumfanya kila mtu aliyehudhuria msiba huo aweze kulia….

Kwa  jinsi ilivyo, huyu marehemu,  alikuwa mtu aliyegusa watu, kimatendo, kitabia,…ndio maana wengi walifika  kumsindikiza kwenye safari  yake ya mwisho, ambayo ndio safari ya kila mwanadamu, …kwakwe tumetoka, na kwake ndio marejea yetu…

Nilisia mshehereshaji akiongea mambo mazuri ya marehemu…

Kwa vyovyote iwavyo, mtu akifariki, yatubidi tumuongelee kwa mambo mazuri, maana hayo mambo yake mema,  ndiyo taa ya mja huyo huo endapo,…tukiyaongea, taa hii huzi kuwaka,, kamwe tusipende kuongelea mambo yasiyo mema, hata kama aliyafanya, ili tusififishe mwanga wa taa yake..hayo ni maneno mazuri  niliyoyakumbuka kutoka kwa watu wa imani.

Akili yangu ikarejea kwa yule mtoto…ni…kijana, ni kijana wa takiribani, miaka kumi na mbili hivi…….nikaamua kumsogelea, hadi pale alipochuchumaa, pembeni yake kulikuwa na mfuko wa Rambo, na ndani yake kulionekana nguo nguo hivi….kwa muda ule yule kijana, alikuwa kachuchumaa, naona sasa miguu imemuisha nguvu…hawezi kusimama tena, na bado hakuna mtu aliyemjali..

Hakuna hata aliyepoteza muda kumuangalia tena…, wengi walitekwa na matendo yanayoendelea mbele ya jukwaa…watu wanavyoomiongelea  marehemu…na mengineyo.
Mimi nikamsogelea yule mtoto….

‘Pole kijana…pole sana..yote ni kwa mapenzi ya mungu, …’nikasema nikimsogelea na kumshika begani.

Yule mtoto, ..ni kijana akainua uso na kuniangalia, uso ulikuwa umefunikwa na machozi….akatikisa kichwa…kama kusikitika. Akavuta pumzi, haalfu akasema;

‘Ni kweli yote ni kwa mapenzi ya mungu, lakini kwangu, …..kwa-kwa…ngu, ime-ime….kuwa ni….mengine yanauma kaka yangu,sijui nikuite kaka yangu, au baba, hata sikujui…..sijui niseme nini…inaniuma kwa-kwa –kwa -kwe….’akasema. akishindwa kumalizia maneno.

‘Kwa muda huu, hakuna cha kusema iliyobaki ni kumshukuru mungu, kwani yeye ndiye mwenye mamlaka ya haya yote…, kwake tumetoka na kwake ndio marejeo yetu, ndio kauli sahihi,..’nikasema

‘Ni sawa…lakini mwenyewe si umeona..mimi kama mimi nitakuwa mgeni wa nani,…nimetoka mbali nikijua nimeshafika kwa…..lakini sasa,..ooh,.. ‘akaanza kulia.

‘Umetokea wapi…?’ nikamuuliza.

‘Yaani,..nilijua,…nikifika nitamkuta…nitaongea naye, nita…..sasa nakutana na haya….niende wapi mie…’akasema.

‘Oh, ina maana…’nikatakla kuongea kuhusu hisia zangu, lakini yeye akaendelea kuongea.

‘Hebu niangalie…mimi kama mimi nitamuendea nani sasa , hebu niambie kaka yangu…ni nani atakayeniamini, mtoto wa majalalani…niangalia nilivyo, ni nani, ata……kwa hivi sasa sina mama, na sasa sina….ooh…’akaanza kulia,…kiukweli hata mimi nikalia.
Baadae nikamwambia…

‘Oh..usijali yote ni mapenzi ya mungu, yey e ndiye atajua uta…’hapo sikuweza kuendelea yule mtoto, au yule kijana  akalala chini, na kunyooka,…alionekana kupoteza fahamu.
Hapo sasa baadhi ya watu wakafika na kuanza kumsaidia.

‘Huyu ni nani…?’ akauliza mmoja wa jamaa aliyefika pale.

‘Mhh..hata simjui…’akasema mwingine

‘Sio jamaa au mtoto wa marehemu…’nikasema

‘Hapana,….mtoto wa marehemu awe hivi..wewe vipi bwana….’akasema jamaa aliyeonekana kuwa ni mtu au jamaa wa  marehemu.

‘Lakini…..’nikataka kuyarudia yale maneno ya yule mtoto, lakini huyo aliyesema…hapana, akiwa na uhaklika kuwa huyo mtoto sio jamaa ya marehemu akaondoka, .
Kwa muda ule huduma za kwanza za huyo mtoto zilikuwa zikiendelea, baadae akazindukana, na alichosema kwa haraka,,,

‘Najua hawataniamini, ..najua…kwa vile mimi sasa ni yatima, lakini, nasema hivi…haya ni kizalia,, leo kwangu kesho itakuwa kwa mwingine…’aliposema maneno hayo, akapoteza fahamu tena.


WAZO LA LEO: Diary yangu, inatoa pole kwa msiba wa mpendwa wa wengi, …RIP Ruge, ..hatuna cha kuongeza, zaidi ya kukuombea makazi mema peponi, na kuwaombea wazazi na ndugu subira njema, …kwani yote hayo ni kwa mapenzi ya mola.

Ni mimi: emu-three

No comments :