Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, October 3, 2018

YOTE NI KWA MAPENZII YA MUNGU-53



‘Huyo muhasibu yupo hai…’sauti ikasema

‘Wewe ni nani hebu pita huku mbele…’akasema hakimu

Watu sasa wakawa wanampisha huyo mtu…safari hii ni  tofauti na ilivyokuwa awali, huyo mtu alipishwa kwa nidhamu, hadi akafika sehemu ya kuonekana, maana licha ya kuzuiwa watu kujaa, bado wengi waliweza kuingia,

Jamaa sasa akawa keshafika mbele, kwa upeo wa kuonekana na kila mtu,..akawa anatembea taratibu kama vile anataka kila mtu amuone, ..hadi akafika sehemu karibu na shahidi aliyekuwa akihojiwa.

‘Wewe ni kwanini na kwanini hufuati taratibu za mahakama…?’ kaulizwa

‘Muheshimiwa hakimu, kama ningeamua kusubiria utaratibu huenda nisingelipata nafasi ya kufika hapa hii leo…kuna mengi hamjayafahamu bado..’akasema , na hakimu akawa anamuangalia kwa makini, na jamaa alipoona hakimu anamuangalia sana akasema

‘Najua labda …sina uhakika lakini, hakimu unaweza kunikumbuka…mimi nakukumbuka sana, wengi wa leo, wakiniona hapa, wasio kuwa na moyo wa uvumilivu wanaweza kukimbia, au kuzimia…’akasema

Hakimu akawa anateta na wenzake, halafu baadae akasema

‘Kwa upendeleo wa dharura, shahidi uliyekuwa ukiongea, usubiria kwanza, ili tuweze kumsikia huyu mtu, nataka kufahamu zaidi kuhusu yeye, na kwanini anatoa kauli kama hiyo ambayo, inasigishana na kauli yako, …’akasema hakimu.

Hakimu akamuangalia wakili, kama vile anataka kumuarisha afanye jambo, na wakili akawa kimia tu.

Mimi pale nilipo nikamtupia jicho Dalali, Dalali alikuwa vile vile kama kagandishwa akimuangalia huyo mtu aliyeingia, mpaka nikaingiwa na wasiwasi, na kwa haraka nikageuka kumtafuta mama mjane kwa macho, sikumuona ile sehemu yake aliyokuwa amekaa awali, sijui kama alitoka kidogo, au kaenda wapi, sikuwa na muda wa kumfuatilia, mawazo yangu yakaelekea kwa huyo mtu aliyeingia sasa hivi, nikijiuliza je ni nani huyu mtu, na kwanini uwepo wake umeweza kumdatisha Dalali.

Mimi nikamsogelea wakili , na kumnong’oneza jambo, na kwa haraka akamtupia jicho Dalali, halafu akatikisa kichwa kama kusikitika

‘Unahisi yupo sawa…?’ nikamuuliza

‘Atakuwa sawa, sema labda hakutarajia kumuona huyo mtu,…’akasema

‘Kwanini…?’ nikamuuliza wakili

‘Wewe subiria tu,….’akasema wakili na kunifanya na mimi niwe gizani, sikuipenda hiyo hali, …

 Dalali sasa akawa kama kalegea hivyo, kaegemea upande mmoja, kama anataka kudondoka,…na docta aliyekuwa mbali akanyosha mkono, huku akiashria kwa hakimu amuangalia Dalali, na hakimu akamuona..akatambua docta ana maana gani.

‘Vipi wewe Dalali una nini…?’ akauliza hakimu sasa akimshangaa Dalali ambaye alikuwa kalegea kabisa,…na Hakim kuona hivyo, akasema

‘Docta hebu muangalia huyo mgonjwa wako, kama ana tatizo lolote…’akasema hakimu na docta akasogea pale alipokuwa Dalali na kuanza kumpima pima, baada Dalali, akawa kama kazindukana, na kwa haraka akawa kama anataka kusimama, lakini akawa anashindwa..baadae sauti ikatoka kwa Dalali ikisema;.

‘Haiwezekani, huu ni mzuka….’akasema Dalali akiendelea kumtolea macho huyo jamaa aliyeingia.

Yule jamaa sasa akawa kamkaribia Dalali….Dalali…akajaribu kuinua miguu, lakini hakuweza, huyo akaporomoka chini…watu wakawa wanasukumana ili kuona kinachoendelea huko mbele..

‘Watu wa usalama …’akasema hakimi na watu wa usalama wengine wakawa wanawatuliza watu wengine wakimsaidia Dalali kuweza kukaa kwenye kiti chake tena.

‘Vipi wewe unaogopa nini…?’ akauliza

‘Huyu siamini kama …ni binadamu…’akasema

‘Kwanini…?’ akalizwa

‘Nijuavyo mimi alikufa na kuzikwa hata mkienda makaburini mtaliona kaburi lake…’akasema

Huyo mtu hakujali hicho anachoongea Dalali, yeye akajisogeza hadi mbele, na kusimama, …..

‘Haya hebu tuambie wewe ni nani, na kwanini unaingilia Mahakam , si unajua tarataibu za mahakama, kwanini unapayuka huko nyuma…?’ akaulizwa

‘Imebidi nifanye hivyo, kwa maana kama ningelikwenda moja kwa moja kwa watu wangu nikajitambulisha, nina imani wengine wangelikimbia…kama unavyoona huyu hapa…ananifahamu vyema, na anafahamu kuwa mimi ni marehemu…’akasema

‘Ina maana wewe ndio huyo….’kabla hajamaliza kuulizwa, yeye mwenyewe akasema;

‘Mimi nilikuwa muhasibu wa benki kabla sijafukuzwa, na kutambuliwa kuwa nimeshafariki,…ndivyo inavyojulikana hadi hii leo…huko benkia nilifukuzwa kwasababu ya njama za bosi wangu,..’akasema


‘Bosi wako ndio yupi..?’ akulizwa


‘Majaliwa…’akasema


‘Tuambie ilikuwaje…?’ akaulizwa


‘Ukweli wa hili jambo naufahamu sana mimi kuliko yoyote hapa..,..na ndio maana ilisaidikiwa kuwa mimi nimekufa..lakini sikuwa nimekufa, nililipwa pesa nyingi, nitoweke, na ni baada ya kuonekana hivyo, kuwa mimi nimeshafariki,..lakini kuna kitu kilinifanya nirudi tena…’akasema


‘Kitu gani…?’ akaulizwa


‘Marehemu mtaalamu ni baba yangu wa kufikia, …yeye alizaa na mama yangu, na kupatikana kwa mimba hiyo ni kutokana na michezo yake mibaya, nilikuja kuambiwa na bibi, mama yake mama yangu..


Bibi aliniambia, kuwa …baada ya kuzaliwa mimi, mama alinitambulisha kwa huyo baba, …kiukweli huyo baba hakunikataa kama unavyoona tunafanana naye sana,..alipokubali hilo, akafanya mambo yake na mama yangu akawa anaumwa sana, ulimi ukawa unavimba, akawa hawezi tena kuongea, hadi anafariki…’akasema.


‘Kwanini mama yako aliumwa hivyo, ni ugonjwa wa namna gani.?’ Akaulizwa


‘Marehemu ..alikuwa na tabia hiyo, kuwachezea wanawake, baadae akiwachoka anawateketeza kwa mbinu hizo, lengo lake ni kutaka wasije kusema lolote kumuhusu yeye..na niliposikia hii kesi nikaona wakati umefika wa kuyabainisha haya…


Yaliyotokea kwa mama yake Majaliwa ni hayohayo yaliyotokea kwa mama yangu, na Dalali, alihadaiwa afanye hayo,… kama kinga, hakulijua hilo…mimi nimehangaika sana kumtafuta…Majaliwa, ili niongee naye sikufanikiwa, nikaona nije hapa, lolote liwalo na liwe…Huyu Dalali, yawezekana siku ile yeye alitumiwa hivyo, ambake huyo binti, kuuficha ukweli wa marehemu…na huenda hiyo mimba ni ..ya marehemu…’akasema


‘Niliposikia habari ikiongelewa, kuhusu yaliyotokea kwa mama wa…Majaliwa,.. imeniuma sana… nikakumbuka kilichotokea kwa mama yangu na wengine wengi walioafanyiwa hivyo, nimeshindwa kuvumilia, nipo tayari kuhatarisha maisha yangu, kwa ajili ya hili….’akasema


‘Ehe, haya…tuambie sasa hayo ya bank…?’ akaulizwa


‘Bila shaka….mimi …, nitawaambia kila kitu…ninatambua baadhi ya njama za hayo madeni maana nilikuwepo yakifanyika, …na baadhi ya mbinu za kulifanikisha hilo ilitokana na marehemu,..’akatulia

‘Kuna watu hawajui, kuwa mtaalamu,…aliwahi kufanya kazi benki…akaacha, na kujiingiza kwenye mambo ya kiganga, anasema aliacha kwa kutii wito wa mizimu, kwahiyo mambo ya benk anayafahamu…yeye ndiye alifanya mipango nikajaariwa benki…na kila mara alikuwa akinitembelea kazini, hasa akiwa na shida ya pesa, na… siku moja aliniambia, amegundua jambo, nikamuuliza jambo gani, akasema;


‘Unajua kuna sahihi za watu wawili zinafanana, na hao watu ni maadui zangu, ila hawajui kuwa wao ni maadui zangu, nataka kuwamaliza, na kuna mtu naye …tutamtumia lakini hatakiwi kulifahamu hilo, hata yeye ni adui za hao watu…’akasema hivyo.


‘Wawili hao ni akina nani…na mimi nahusikanaje na hilo…?’ nikamuuliza


‘Wawili hao ni Dalali na kaka yake, je wewe si mahasimu wa hao watu?’ akaniuliza

‘Ni kweli lakini mimi sina haja ya kuwafanya lolote, nilishawasamehe tu…’nikamwambia


‘Sikiliza bwana mdogo, mimi…nimegundua jambo, hata kama umewasamehe..lakini kwa kupitia wao, tunaweza kufaidi,..wewe wataka kuishi masikini mpaka ufe…’akasema. Kiukweli hiyo familia ni watu wasio na uhusiani mnzuri na familia yetu…kuna migogoro ya maeneo unajua tena..’akasema


Basi nikamuuliza mtaalamu,kwahiyo…unataka iweje?’ nikamuuliza


‘Usiwe mjinga bwana…mimi najuana na huyo meneja wa benki, alikuja kwangu, akitaka nimfanyie mambo fulani, fulani…unajua mambo mengine hujileta tu,..Dalali, aliwahi kuniambia sahihi yake inafanana na ya kaka yake…sikumoja alipokuja huyo meneja, anakuja kwa kunizoea, pamoja na mambo yake mengine,nikaongea naye kuhusu kufanana kwa sahihi, …huyo meneja ni mjanja sana, …akanielewa, ila hakuwa anawafahamu watu vizuri, ni nani wa kushirikiana naye..’akasema


‘Una maana huyo meneja bosi wangu, aje kwako kwa mambo kam hayo, kwa umasikini gani alio nao,…haiwezekani…?’ nikamuuliza


‘Hayo mengine huhitajiki kuyafahamu, wewe si unataka kuwa tajiri, sasa wakati umefika, nimeshaongea na huyo mkuu kasema hayo nimuachie,…ila yeye anahitajia mambo fulani kutoka kwa mtu wa nje…ndio maana alipofika kwangu, kwa shida zake akaniamini..’akasema.



‘Mhh,…mimi sikuelewi, sasa wewe unataka mimi nifanye nini…?’ nikamuuliza.


‘Nimekuambia…mengine hayakuhusu..kuna mambo nitakuwa nakuambia uyafanye, usiulize kwanini niyafanye…ila wewe utalipwa vizuri sana, unasikia,..umasikini bye bye..kama utafanya nitakavyokuagizia, utakuja kunishukuru, mimi niliacha kazi benki lakini bado nina ndoto za kupata utajiri kwa wazo langu hilo, na wazo hilo kumbe kuna mwenzangu naye alikuwa nalo…’akaniambia.


‘Kiukweli nililipinga sana hilo…lakini kukatokea hali ya mchafuko hapo banki,..mageuzi, mbali mbali, nikajikuta na mimi ni miongoni mwa watu wanaotakiwa kupunguzwa hapo kazini..lakini kwa haraka nikahisi ni mbaya wangu, bosi Majaliwa…’akasema.


‘Kabla ya kufikia hatua hiyo ya kupunguzwa kazi,  ndio mtaalamu akanijia , na kuniambia, sasa umeonaeeh…usijali kwa haya yaliyotokea, kuwa wewe unapunguzwa kazi, hiyo ni sehem ya mikakati ya kukufanya wewe uwe tajiri, lakini kabla ya kuondoka,  kuna mambo yanatakiwa wewe uyayafanye kwa haraka…’akasema


‘Umefahamuje kuwa kuna zoezi kama hilo…haya ni mambo ya ndani ya benki…?’ nikamuuliza


‘Usiulize sana…wewe utapunguzwa kazi, ni katika kufanikisha mambo ya utajiri, unielewe hapo, na usipofanya hayo, unajua ni nini kitatokea kwako, kwanza utakosa nini, eeh, wewe waenda kijijini utaishije, au unafikiri utapata kazi haraka, kazi hapa nilikufanyia mpango mimi…’akasema.


‘Kiukweli nilishajua kuwa kazi sitakuwa nayo tena, ..nikakubaliana nao, nilichotakiwa kukifanya ni kusimamia mikopo, kuwasainisha watu, wanaohusika…sasa mojawapo  ya vocha hizo ni ya huyo marehemu, na kwa vile sahihi yake marehemu inafanana na y a Dalali, mimi sikuwa na tatizo, nikampigia simu Dalali, akaja…


‘Nilimuelezea kuwa hapo benki kuna mabadiliko, na ni ya haraka, yeye anatakiwa kwanza akalete Dole gumba la kaka yake, na sahihi yake…lakini muhimu ni dole gumba la kaka yake, sahihi hata yeye anaweza kuiweka…’akasema


‘Dalali, alikubali,…hakutaka hata kuuliza zaidi..kesho yake nikapata nilichokitaka na yeye akaweka sahihi…kwa kila nilichomuambia aweke sahihi…, hakufahamu kuwa anapitisha deni la kaka yake…kiukweli sikupenda hilo, lakini ningelifanya nini…watu hawamfahamu mtaalamu, ni mchawi wa kutupwa….’akasema.


‘Kwa vipi, na tutaaminije hayo unayotuambia, unaongea kuhusu marehemu nay eye hayupo hapa kujitetea..?’ nikamuuliza.


‘Kuamini haya mtafuteni huyo meneja wa hiyo benki ya zamani, mtajua kila kitu…na chunguzeni kufukuzwa kwangu kama sio kwa njama…ulizeni kufariki kwangu kulikuwaje, je watu wanaonifahamu wanajuaje kuhusu mimi, …’akasema


‘Mimi baada ya kupokea barua ya kuachishwa kazi , ilitakiwa nionekane nimejiua, kutokana na kuonea, halafu maisha magumu, iliandaliwa hivyo, walioshuhudia kifo changu waliona huo ujumbe niliouwacha....na kuna dawa nilipewa na mtaalamu, nilipomaliza kuzinywa, nilipoteza fahamu, hata mtu akinipima anaona nimekufa kabisa,…’akasema.




‘Una uhakina na unachokiongea, na kwanini hukukataaa aukutoa taarifa polisi, na kama ulikufa hukuzikwa, au hapo ilikuwaje..?’ akaulizwa.

‘Sikuzikwa mimi, ulizikwa mgomba, mimi baadae nilisafirishwa usiku hadi mikoani, huko nikapewa dawa ya kunirejesha fahamu…na pesa nyingi za kutumia, na onyo, kuwa mimi kuanzia muda huo sipo duniani,..na ikitokea nikarejea  Dar, basi ndio itakuwa mwisho wangu wa kiukweli…wataniua…kwahiyo, eeh…ikatambulikana hivyo kuwa mimi nimeshakufa, na hata familia yangu ilijua hivyo, huko nilikaa na kuoa mke mwingine..’akasema.

‘Ulioa..!!  na mke wako na watoto wako walikwenda wapi…?’ akaulizwa


‘Hiyo pia ni moja ya mipango yao ya kunifanya niisahau familia yangu,..awali nilijua ndio hivyo …hata hivyo…kabla mambo hayajawekwa hivyo, mimi kufa na kutoweka, nilipewa nichague moja, niachane na familia yangu, iwe hai, huru na tajiri, au nisaliti huo mpango, familia yangu iteketee, tena kwa moto…’akatulia

‘Unajua watu hawa wanapenda sana kutumia moto kuangamiza jambo….wakitaka jambo lipotee kabisa, wanatumia moto…sasa kwa vile nilishawahi kuona matendo hayo kwa watu wengine waliofanyiwa hivyo, sikupenda kabisa hilo lije kutokea kwenye familia yangu, nikaamua kufuata watakavyo wao…nikimuomba mungu kuwa ipo siku haki itatenda…mungu yupo…

‘Kwahiyo mimi nilifanya hayo baada ya kutishiwa maisha yangu, mimi na familia yangu, kuna mambo makubwa yalitokea kwenye familia yangu, kabla ya ..kufikia huko, familia yangu iliteseka sana…nisingelipenda kuyaelezea hayo, wenyewe mkiwauliza watawaambia, huo ni ushahidi kwenu, sitaki kuuingilia…’akatulia

‘Ndugu zanguni…haya sio utani, utaamini hayo ninayoyasema siku yakija kukukuta, watu hao waliamini kwenye mali, na adui wao ni yule anayeingilia mipango yao..na ukiwa adui yao, …tiketi yako ni kifo…tiketi yako, ni kukatwa ulimi…kama watataka uendelee kuishi kidogo, lakini lazima watakumaliza…na wanaweza kukupatia sumu, ikakutesa, na ikaonekana ni kansa…utakufa tu…’akatulia

‘Sasa swali mtaniuliza kama hayo yapo na yanafanyika, ..je kwanini sasa nimeamua kurudi, siogopi tena,  kiukweli kilichonipa nguvu yakurudi huku ni kwa vile nimesikia Mtaalamu hayupo tena duniani, huyu kwa hapa nchini ndiye walimtegemea kwa kuangamiza, kimiya kimia au kwa nguvu za giza, ..pia ni kwa vile…mfadhili wao, kakimbia hapa nchini, hayupo tena, hawana pesa tena…’akasema.

Hapo hakimu akawa anaongea na watu wake, baadae akamgeukia huyo mzungumzaji mpya, na huyo mzungumzaji akasema;


‘Na ndugu zanguni …hili jambo lilikuwa sio mpango wa  mtu mdogo kama Majaliwa,  kama…eeh…hata huyo marehemu, sawa yeye alipewa hiyo kazi tu kwa vile ni mjuvi wa mambo ya giza na kwa vile ni wao walimfundisha hizo nguvu za giza, walimuona ana kipaji hicho cha kurisi…lakini wanaofadika na wengine analipwa nini , kidogo tu.


‘Haya ...huyo Majaliwa, sizani, kama alikuwa akifahamu mpango huo kiundani, labda…mimi sijui zaidi, maana sikuambiwa, haya ninayowambia nimeambiwa….jinsi mipango ilivyopangwa, huyo Majaliwa, …yeye kaingizwa kama kiini macho tu, kwa vile ana visasi vyake, basi ikaelekezwa huko, ionekane hivyo…labda mimi sijui zaidi…lakini nina imani yeye hajui zaidi ya hivyo nijuavyo mimi...’akatulia kidogo.

‘Hata mimi….kuyafahamu hayo…ni baada ya kuwasiliana na mtaalamu, wakati anakaribia kukata roho, nilifika kwa siri kumuona aliponiona alinisikitikia sana, kwanini nimerudi, na nilipofanya ukazidi wa kurudi huko nilipotoka ndio akaniambia…


‘Kijana mimi nakufa, sitaishi tena, sasa kama huamini haya shauri lako, kwa vile sitaishi sana, nitakusimulia, ila nataka uwe na ushahdi unaoweza kuja kukusaidia, chukua video, ili iwe ushahidi, nahisi hili litanipunguzia dhambi zangu..na kwako wewe hata sijui nikusaidieje,…ila nataka uje kuwasaidia baadhi ya watu wanaotumika bila kujijua, wajue kuwa wapo hatarini…mzee mtupe anaweza kukusaidia,…haya ni mikakati ya kundi haramu…wao wakikuchoka, wanakumaliza…’akasema

‘Kundi gani hilo mtaalamu…?’ nikamuuliza

‘Hapo ndio…yeye  akanisimulia kila kitu..na ushahidi ninao hapa, kanda ya video, niliyorekodi, yeye akiongea, akiwa taabani, akikaribia kukata roho..kama mnataka kusikiliza ushahidi huo, huu hapa…’akasema akitoa kanda ya videoa

‘Sasa …, mimi sijui zaidi ya hicho nilichokisikia kutoka kwa huyo mtaalamu mwenyewe, na wengi wa wahanga …wametumiwa tu, kupitia kwenye visasi vyao,…’akasema.


‘Kuna jingine..hili sikutaka kulisema, lakini..kwa hivi sasa inabidi,…kumbe hata mke niliyemuoa, alikuwa ni mtu wao,..yaani ilifanyika hivyo, nimuoe, ili ahakikishe mimi sifungui mdomo, na ninakuja kufariki kimia kimia…’akatulia

‘Hamuelewi haya..yapo ndugu zanguni, msipende kujiunga kwenye makundi ambayo yanajifanya yana utajiri, au yanaweza kukufanya wewe uwe tajiri….., kumbe huyo mke ni muathirika wa HIV…, anajijua na anatumiwa kuambukiza wahanga wanaotakiwa waambukizwe, na mbaya zaidi, ukishaupata huo ugonjwa, kuna dawa utapewa, za kukumaliz haraka,…na ukipimwa itaonekana umefariki kwa kupitoa ugonjwa huo, wao sasa hivi wanatumia ugonjwa huo, na ugonjwa wa kansa, kuwamaliza maadui zao…ukifa ukipimwa inaonekana ulikufa kwa ugonjwa, unaojulikana unaua…’akatulia kidogo.

‘Haya nisingeliyefahamu bila kupitia kwa mtaalamu, na niliporejea nyumbani sikumkuta tena huyo mke, alishaondoka, na alicha ujumbe kuwa nisimtafute, kwani sitampata, tutaona kuzimu..…kazi aliyopewa ilitakiwa iwe imekamilika, lakini sijui ni kwa kudra ya mungu, au ni kwa …huruma ya huyo mke, lakini mimi najua yote ni kwa mapenzii ya mungu, ndiye aliyefanya hilo liwezekane….siku zote nilizoishi na huyo mke,..huyo mke, alinisihi nitumie kinga…na nashukuru kwa hilo, kwani nimeshapima, sina maambukizi..

Alitulia kidogo, na alipoona haulizwi maswali, akaendelea kuongea…


‘Hilo deni na mengine ni mpango kabambe ya huyo meneja, mtafuteni, kama bado yupo hai, ataambia kila kitu, na hata hiyo benki hamjui tu, ni moja ya miradi ya hilo kundi…’akageuka kumuangalia wakili

‘Mimi  ….sijui zaidi ya maelezo ya mtaalamu, mtasikia wenyewe akielezea japo kwa sauti ya shida,…ilitakiwa baada ya kumaliza kazi yao waliyopanga, hiyo benki iwabambikie marehemu madeni mengi sana, halafi ipambana na kukusanya pesa kupitoa huko, kupiga minada mali za marehemu, ndio hivyo wanavyowekeza

‘Sasa ni..nini watapata…hebu fikiria wameshapiga minada nyumba ngapi, majumba ya watu yenye thamani kubwa tu…ujanja ujanja wa kupitia kwa watu, waliowasoma wakaona kwa kupitia kwao inawezekana…’akasema


Hakim alionekana kufuatili hayo maelezo, kwa uso wa kushanga , ni kama haamini hayo kuwa kweli yapo..na sasa aliyeuliza swali alikuwa ni wakili ….


‘Ina maana gani hapo, kiukweli hayo maelezo yako yapo kama mikakati pia ya kuuficha ukweli halisi, ni kama njama za kuwatetea hao watu Majaliwa, Dalali na kundi lake,,… kwa vile yaonekana labda una damu damu nao…sasa utuambie ukweli, ni nani kakuambia uje kuyasema haya, maana hapa ni mahakamani..uwongo wako utakufanya uozee jela.?’ Akaulizwa.

‘Ushahidi nimesema ninao hapa, na…nilishawaambia watu wenu, wafuatilie hayo…, wachunguze, mbona ukweli upo bayana….kiukweli mimi siogopi kufa tena, nimeshajitolea muhanga, najua kama hilo kundi halitakamatwa, basi, maisha yangu yapo hatarini, lakini bora nife kihivyo kuliko kufa kidhambi, najua wengi hamtaam,ini haya, lakini, kama watu wenu watafanya kazi vyema, nina imani…….’


Kabla hajamaliza, mara akaingia mpelelezi , akiwa na bahasha kubwa mkononi, akamsogelea wakili na akawa anamnong’oneza kitu, wakawa wanateta kwa sauti ndogo…’

Nilimuangalia yule shahidi aliyekuwa akiongea, ..yaonekana alikuwa na mashaka sana, nikageuka kumuangalia Dalali…alikuwa kama hayupo, docta alikuwa karibu yake akihakikisha mambo yanakwenda sawa, ila kiukweli hali ya Dalali, ilionekana ipo mashakani.

‘Samahani muheshimiwa hakimu ule ushahidi tuliokuwa tukiusubira , umeshafika,..huu ni zaidi ya …tulivyofikiria, …naomba nitete na mpelelezi wetu…’ akasema, akionyesha ishara ya heshima…na hakimu akageuka kuongea na wasaidizi wake.

Mimi nikawa nawasikiliza wawili hawa wakiongea, pale nilipo niliweza kuwasikia vyema, na walipomaliza kuongea, wakili akanigeukia na kusema;

‘Tumemaliza kazi …’akasema akiniangalia mimi, na mimi nikabakia kimia, wakati ule nilikuwa najiuliza mama mjane kaenda wapi, maana hayupo kabisa mle ndani,.nimejaribu kutizima pande zote hayupo.

Hakimu akawa anasubiria tu, naona sasa aliona akae kimia, aone ni nini kaleta huyo mpelelezi, maana hii kesi sasa sio kesi ya madeni tu, imekwenda zaidi ya hapo.


‘Safi kabisa …, ‘wakili akawa anakubali, akionyesha ushahidi na maelezo ya huyo mpelelezi,…

‘Sasa kazi imekwisha….’akasema na sasa akasogea mbele na kumuangalia muheshimiwa hakimu, akasema;

‘Muheshimiwa hakimu,  tulikugusia kuwa kuna ushahidi mkubwa unakuja kwa ajili ya kulimaliza hilo kundi haramu,..’akasema

‘Ni kundi haramu lililojifanya ni wajanja wa kugeuza geuza mambo,….sasa mpelelezi wetu ameshafika, je ni kweli Majaliwa, Dalali na kundi lao hawahusiki ..au ni njama zao, je ni nini ukweli wa hayo madeni, tunao ushahidi wote, na …tunataka tuliweke hili wazi, haki iweze kutendeka kwa kupitia kwako muheshimiwa hakimu.

Hakimu akaangalia saa…halafu akageuka kuongea na wasaidizi wake


NB: KESI IMEKWISHAJE..


WAZO LA LEO: Usiwe mwepesi wa kuamini kila jambo unaloambiwa, au kusambaza kila ujumbe unaotumiwa. Au kuwa mwepezi kusambaza taarifa usizokuwa na uhakika nazo….Kuna watu kazi yao ni kusoma mazingira na watu, kutafuta fursa kwa kupitia kwenye tabia na hulka za watu, na wanatumia mitandao kufanikisha malengo yao…Nia kubwa ni kupata washabiki wengi, na wingi wa washabiki, ndio wingi wa kuingiza kipato kwao. Tuweni makini kwa hilo, tunageuzwa chambo cha biashara kwa wengine.

Ni mimi: emu-three

No comments :