Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, October 2, 2018

YAKUMBUKE MAUTI



TUYAKUMBUKE MAUTI…

'Inalillah wainaillah Rajiuna,..., kwake tumetoka na kwake ndio marejeo yetu..' ndizo lugha tunazisikia kila siku, pale tunaposikia kuwa mwenzatu katangulia mbele ya haki...


 Siku za karibuni tu hapa, nimesikia ustaadhi mmoja kagongwa na gari, kafariki, mcha mungu, kiongozi wa dini, na alifariki akiwa anatimiza wajibu wake wa kiimani,..na kila siku taarifa kama hizi hazikosi kusikika masikioni,..siku zilizopita ajali ya kivuko, wengi wameondoka watoto kwa wakubwa…


Mimi najiuliza tu, je tunapozisikia taarifa hizi au kututokea kwa jamaa zetu, akilini mwetu tunajiuliza nini, je kuna maswali gani twatakiwa kujiuliza..au basi siku yake imefika basi,...sijui ni mimi tu, lakini najaribu kuwaza mbali, licha ya masikitiko kuwa mwenzetu safari yake imeshafika, lakini pia kuna maswali muhimu kwangu mimi na wewe yabidi tujiulize

‘Sisi  ni nani, ni wajanja sana , au ndio tunapendwa sana na mungu,…ndio maana bado tupo hai….?’

-Kama wanaondoka wanazuoni waliojaa imani ya dini, kama wanaondoka viongozi wa dini, tuliokuwa tukiwaendea tukiwa na mataizo watuombee,sisi maamuma, sisi wafuasi tuna nini cha kusema hapo…,


-Kama wanaondoka watoto wadogo, wasio na hata dhambi, je sisi wakubwa ambao tuna madhambi yenye kunuka, tunasema nini hapo….


-Kama wanaondoka vijana, wenye nguvu zao, damu zinachemka kabisa, ambao wangeliweza kupigana na huyo mtoa roho,,…je sisi ambao, umrii umeshakwenda tutasemaje..


-Kama wanaondoka matajiri wenye pesa zao, wenye walinzi wa kila hali, wenye silaha za hali ya juu, na viona mbali, sembuse mimi na wewe ambaye, ulinzi wetu ni wa majaliwa ya mungu, tuna nini cha kusema.Hebu fikiria kwanza hapa…, hawa matajiri si wana walinzi, kwanini hawawatumii hao walinzi wao  kupambana na mtoa roho, lakini wapi….siku ikifika hakuna cha tajiri wala masikini…hakuna mtoto wala mkubwa..sote tutaondoka kila mmoja kwa wakati wake

Sasa ndio najiuliza, …kwanini hatupendani, kwanini hatumtii yule aliyetuumba, kwanini tunatakabari, na kujaa kiburi, kwenye hii nyumba ya kupanga, maana dunia ni nyumba ya kupanga siku yoyote tutaondoka, swali hapa, je siku yangu ikifika nina nini…nitakwenda na nini huko akhera, au kufa ni kufa tu

TUYAKUMBUKE MAUTI…

Tujiulize….siku yangu ikifika nimewekeza nini,nina nini kama akiba yangu ya huko mbeleni, na nini  akina ya huko mbeleni…

Tunaambiwa akiba ya huko mbeleni… ni matendo yetu mema, je hayo matendo mema sisi tunayo,, wakati kila siku kila mtu kwa nafasi yake anafikiria jinsi gani ya KUDHULUMU, sasa hivi ni kamari, kukusanya vijisentI vya watu, walalahoi, viende kwa mtu mmoja tu…, imekuwa ni dili sasa, mpaka hata yule aliyekuwa hana wazo hilo anatamani kufanya,…sababu ya matangazo yake…

Ukienda huko kwa wafanyabiashara, biashara siku hizi ni kudanganyana tu, kuwa hiki ni kizuri, kumbe kimeoza..maofisini mabosi kuwadhulumu watu, nguvu kazi zao, wanapata faida kwa migongo ya wavuja jasho lakini ni nini wanawalipa hawa watu, je kinaendana na jasho lao, hatujali, si kaja mwenyewe....yaani…kila mtu kwa nafsi yake anatafuta njia ya ‘kudhulumu tu..’ hata ndio matendo mema..??

TUYAKUMBUKE MAUTI….


 Haya ….najiusia mimi mwenyewe na kuwausia wenzangu nyie…, tuyakumbuke mauti, tuikumbuke hiyo siku, siku ambayo, haina jina siku isiyojulikana, ..siku hiyo ikifika, utamuacha umpendaye, utakiacha ukipendacho, utayaacha maisha yako ya utajiri, uongozi nk… yaliyokujaza kiburi…cha kusema ‘unanijua mimi nani…’

Ewe mola wetu tunakuomba uwasamehe madhambi yao ndugu,zetu, na  jamaa zetu na marafiki zetu, majirani zetu, waliotangulia mbele ya haki…

Ewe mola wetu, tunakuomba utupe mwisho mwema.


Aamin….

Ni mimi: emu-three

No comments :