Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, October 4, 2018

MUDA HAUMSUBIRII MTU

        
               
       MUDA HAUSUBIRI MTU..

 Leo nilikuwa na miadi ya kwenda,kulipa ada za watoto benki, nikadamuka kama kawaida yangu,  alfajir na mapema nikijua nitakuwa wa kwanza nimalize shughuli zangu niwahi kibaruani…ni Kariakoo tu hapo..nafika benki, maandishi,…kazi kuanzia saa mbili na nusu…nilishasahau tena, nikijua sasa ni mwendo wa viwanda, kazi masaa 24…

‘Utaratibu mzee, uje saa mbili na nusu….’akasema mlinzi, nikaangalia saa saa kumi na mbili na nusu…nikageuka kuondoka, hakuna jinsi..

Ni kweli kwa utaratibu wa benki ao maofis mengi ya serikalini au hata makampuni ya watu binafsi, ukitaka huduma ni kuanzia saa mbili…tena saa mbili na nusu ndio wanafungua na kupata huduma labda kuanzia saa tatu…kwa wale wenzangu na mimi.

Nilijutia kupoteza  muda wangu, labda ningelipitia kazini kwangu kwanza,…lakini nisingeliweza kufika kazini na kutoka, kutokana na utaratibu wa kazi zangu,..na hata ukipanga ratiba kuwa ufike kazini, uombe saa moja la kutoka haitawezekana, kwa shida za usafir, wa Dar, na foleni hasa asubuhi…kwa ujumla kwa jiji letu hili,, huwezi kupanga ratiba ya wapi utakuwa kwa muda gani.

 'Sasa nifanye nini,..?’ nikajiuliza, sasa nikiona muda unakwenda taratibu, tofauti na nilivyokuwa kwenye daladala, niliona gari linanichelewesha…kumbe nilikuwa nawahi buree.

Basi, kuliko kukaa bure, nikaona nifurahishe macho, nikatembelea sehemu nilizokuwa nikipendelea kufika, ya kwanza, nikaona nipitie  msikiti mmoja unaitwa ‘Kwa mtoro’ kama ulifika enzi hizo ukawa mgeni wa Dar, ukirudi sasa hivi unaweza kupotea…, sasa msikiti huu umezungukwa na magorofa, marefu kuliko msikiti wenyewe …watu wanataka kufika mbinguni kwa majengo, sio kwa imani…maendeleo haya.

Akilini nikakumbuka miaka ya elifu mbili mbili hivi… haikuwa hivi. Nikakumbuka enzi hizo nafika kununua cassette za dini, nikiwa na redio yangu unayoweza kucheza hizo cassette…nilipenda sana kununua caste na alimuruhumu Nassoro Bachu.

Kiukweli kwa Dar.., kuna mabadiliko makubwa ya kimajengo, na nilijaribu kuwatafuta wafanyabiashara niliokuwa nikiwafahamu, wengine walishahama,..hawapo tena, na niliowakuta niliwatambua kwa sura, lakini kichwani bati jeupe limeshaezekwa, sura zile za ujana hazipo tena….umri haumsubiri mtu.

Maisha na umri havimngoji mtu hata siku moja… Nashangaa sisi bado mambo mengi ni ya kusubiria, ukiwa na shughuli za kibenki au serikalini kwenye ofisi zao,..hata makapuni ya watu binafsi, usubirie saa mbili na kuendelea…ndio taratibu zetu..KUSUBIRI.

Kwa maana hiyo hata kama mimi ninashida, au ni msafiri, basi, siwezi kuipata huduma hiyo kama nilitarajia kuipata siku hiyo, na ukiwa mtu wa ofisini,..uwe umeshaomba ruhusu jana yake la sivyo, kwa wenzetu, wasio na simile, siku imekatwa…na usemi juu, mshika mawili, moja hufanya nini vile...

Je kwa hali hii, tutaweza kukimbizana na muda kweli,…kama wanavyofanya wenzetu. Wenzetu sasa hivi, hata ule muda wa dakika moja ya kusalimiana hawana. Mkikutana mkiwa huko makwao, ni mwendo wa Hai,hai…kila mtu mbio-mbio, anawahi kazini au kwenye majukumu fulani, kila kitu kimeshakadiriwa muda wake…wanaweza kwasababu hata usafiri wao sio wa huku kwetu…wa KUSUBIRIA…wa FOLENI.

Hata hivyo sisi wenyewe swala la muda bado sio ajenda muhimu kwetu, tunaweza kupoteza siku nzima kwa ajili ya kikao cha harusi..mnasubiriana na hata kikao kikianza, porojo nyingi, nje ya ajenda kuu na wakati mwingine kikao kinaweza kuchukua mambo mengine ambayo sio ajenda kuu, na muda huo hauna hauna marejesho…

‘Ni upendo wa kifamilia,ndivyo tunavyoona hivyo…. Ndio maana tunaweza  kusalimiana nusu saa nzima ukikutana na rafiki yako zilipendwa, ni nini mnaongea, utesi, na yaliyopita, ambayo hayarudi tena, na ole wako ujifanye una haraka, utaambiwa  unaringa…lakini cha ajabu mtu huyu mwambia aingie nyumba ya ibada nusu saa tu ataiona nyingi…ataondoka na kusema yupo bize,…yupo bize kwa maswala ya kumshukuru yule  aliyempa dhamana hiyo ya muda..,

Haya… achilia mbali masaa kadhaa tunayoyapoteza vijiweni, ushabiki wa mpira na,mambo ya kisiasa, ndio hapo mtu hakumbuki muda, muda haumtoshi,…. Leo waitwa kijana, kesho baba, au kwa msemo wao dingi, au dadi, usishangae ukitwa babu...babu wakiwa na maana umeshapitwa na wakati, haupo kwenye wakati wa ujana, kwenye  kuvaa, kimuonekano, na sura…


 Mbona hatujiuliza hili, hivi umri umekwenda wapi, je umekwenda na nini, kwa faida au hasara,..tukumbuke jambo moja, umri huu, nijuavyo mimi ni dhamana kwetu, aliyetupatia huo umri, atakuja kutuulizia, tuliufanyia nini, tuulifanya nini,… achilia mbali tu,…huko kuja kuwajibika uzeeni, wakati tukitwa babuuu….


Haya ngoja nisubiria hiyo saa mbili na nusu, wenye mamlaka ya ajira, wenye nafasi za kuamua, ni muda gani tuanze kazi, ..ndio maisha huenda hata mimi ningelikuwepo hapo ningalifanya hivyo,


Ni wazo tu la leo…ndani ya diary yangu.

Ni mimi: emu-three

No comments :