NGUMI MKONONI-athari
za ulimi.
'Jamani watauana hao watu, mbona mpo watu wazima hapa mnawaachia watu hao, wanapigana na kuumizana hivyo,
waamulieni jamani...'ilikuwa sauti ya mwanamama.
Ni nani atamsikiliza,
watu ndio wanainua simu zao juu kuchukua picha za video, na wengine
wanashangalia…..ni ajabu kabisa dunia ya leo.
Kwa muda ule, mmoja
alishatoa ndutu kichwani, kavimba…na mwingine jicho limevimba, na bado kila
mmoja ana hasira na mwingine….
’nitakuua,
nitakumaliza…’linafuta tusi, ndio lugha iliyosikika kutoka kwa vinywa vya mabondia
hao wasio na kibali, ..ni wakubwa, yawezekana miaka thelathini hivi.
Akatokea askari mmmoja
kupita eneo hilo..ndio ikawa salama, wapiganaji hao, wakaachana utafikiri refa
kawaambia ‘stop’…sasa damu zinawavuja…wamevimba hoi bin taabani..
‘Ehee, endeleeni sasa…’akawatania
mmoja wa wapambe waliokuwa pembeni na simu yake mkononi.
Yule mtu wa usalama
akafika, na kuuliza ni nini kinachoendelea hapo…, watu kimia wengine haoo,
wanaondoka mdogo mdogo, na bahati nzuri yule mtu wa usalama akawaona hao wanandondi wawili wakijaribu kujiweka sawa, lakini mwili haujifichi , ushahidi upo,
utamficha nani hapo;
.
'Haya nyie wawili, tuambieni,
kisa cha nini cha kuumiza dhamana ya
mungu aliyowapa, hamjui huo mwili ni dhamana kwenu, hapa duniani ni dhamana kwa jamuhuri, na huko kwa mungu, mtakuja kuulizwa, kwanini mliuumiza huo mwili uliopewa kama dhamana,...'akasema mtu wa usalama, jamaa kimia.
'Haya mumeumizana mumepata
faida gani, nikawafunge sasa hivi, nina
mamlaka hayo, nifanye kazi yangu eeh, niambieni sasa mnapigania nini....?'
akauliza yule mtu wa usalama ,, wanandondi wale wakawa wanajitetea
'Hivi mwili ni dhamana kwa jamuhuri...'akasema jamaa aliyekuwa nyuma yangu, na mwingine akasema
'Wewe hujui hilo, ...jinyonge upone uone utafanywa nini...'akasema huyo mwingine..huku watu wakianza kutawanyika , kuendelea na shughuli zao. Na wengine
wakiogopa ushahidi…ndio maisha yetu hayo…
Nilisikia wale jamaa wakiendelea kuhojiwa..
.
'Huyu jamaa kazoea
kunitukana, matusi mabaya, leo sikukubali, nimetaka kumfundisha
adabu...'akasema mmojawapo.
'Wewe je..hujanitukana
mimi. ..na pia umezoea kunidokolea bidhaa zangu za sokoni, ndio tabia yako hiyo
mwizi mkubwa wewe…’akasema
‘Wewe umeniona ni
kikuibia, ..wewe ni hisia zako tu…wivu tu, maana kila mara mimi nauza wewe
huuzi,…’akasema mwingine
‘Kakutukana kasema
nini…?’ akaulizwa
‘Yeye, kila kauli
unayotoa ni tusi, tena ananitukania mzazi wangu, mama yangu...'akasema mwingine.
'Mimi sijamtukana mama
yake nimemtukana yeye mwenyewe, kwasababu kazoea kuniibia , yeye ndio tabia
yake hiyo chafu, kazoea,…wizi…’akasema mwingine.
Ilionekana ni jaziba
za ujana, lakini kweli matusi yalitoka, kila mmoja alitumia ulimi wake akatoa
matusi, kauli chafu, na mbaya zaidi matusi yalielekezwa kwa wazazi, wazazi
ambao hata hapo hawapo, wazazi wanatukanwa , wazazi waliwafanya wawepo hapo, leo hii wana minguvu,
wanawatukana wazazi wao...si laana hii .
‘Hivi nyie watu
mnafahamu athari za kutumia ndimi zeni vibaya,..na shetani anapenda sana
kupitia njia hiyo, keshajua madhaifiu yenu yapo huko kwenye ndimi zenu…na
kwanini muwatukane wazazi waliowazaa, wakawalea..?' wakauliza wakabakia kimia
'Haya niambieni, ni….nani mshindi, au bado hamjamalizana,.. tuwaachie mpigane tena, haya piganeni…’akasema huyo mtu wa usalama....jamaa wakawa wamenywea nahisi muda huo ndio wanaanza kuhisi maumivu.
Mimi sikuwa na muda wa
kujua hatima yao, akilini mwangu, nikawa najiuliza tu;
‘Iweje watu
watukanane, na ni nani wanamtukana hapo, kama mtu anamtukana mzazi wa mwenzie
ina maana gani hapo, sio kajitukania mzazi wake pia....haya sasa matusi yamezaa
ugomvi, ugomvi umefikia kupigana, ni nini athari za kupigana, kuumizana,..kuna
faidi gani wameipata hapo, je tusi linaweza kumgeuza mtu akawa hilo tusi..mimi hapo sijui…?’ nikajiuliza tu..
'Kumbe ni ‘ulimi…kumbe
ni mtihani wa ndimi zetu..' nikajikuta nimesema hivyo kwa sauti.
Ulimi umekuwa ni
mtihani kwetu, na kutokana na ulimi, wengi wetu, tutaingia motoni, tusipopata
muda wa kutubia, kabla mlango wa toba haujafungwa…na nikizungumzia ulimi , sio
ulimi tu…ni pamoja utumiaji wa ‘kalamu’
..na kalamu hapa nina maana ya matumizi yote ya kuandika, …hasa huku mtandaoni,
kwenye simu zetu..hapa..tuna kesi kubwa ya kujibu mbele ya mungu.
Enyi mliopewa nafasi
hiyo ya kutumia ulimi, kutumia kalamu,…kwenye mitandao , simu , tv, redio nk…tuweni makini
sana kwa kile tunachokiandika, au kuongea, wengine wanaandika ‘matusi’ kabisa kama
wanavyoyatamka kwenye ndimi zao, wengine imekuwa ni biashara, ukipata wanachama wengi, unapata ingizo, wengine ndio hao wanatunga hadithi
za mambo yanayoathiri hisia za vijana,..
Ni nani anajiuliza
athari za kuhamasisha ‘ngono’…watu wanajiandikia tu…huishii kwa hao wanaosoma
leo, watakuja kusoma wajukuu zako, watoto wako, je hao waliosoma , wakahamasika, kufanya
hayo maasi kutokana na hisia ulizowajengea,..hujui kisa ni wewe, je hujui kuwa wewe ndio umewalogeza 'uasherati'..na yote ni kutokana na
kalamu yako…ndugu yangu unayefanya hivyo, una kesi ya kujibu…
Ukumbuke jambo moja,…..ushahidi
wa kuandika haufutiki, unachoandika leo mtandaoni hakitafutika miele…usijidanganye
kuwa utafuta kwenye simu yako, kwenye komputa yako, nk..hayo hayafutiki kama yameshaenda hewani. Ni halikadhalika, ulichoongea
leo na ulimi wako, ukazua ghadhabu, ugomvi,...nk...hakifutiki, ulimi utakuja kukielezea mbele ya mungu, na kama watu waliumizana, mwili utatoa ushaidi, kisa ni nani,..je uliwahi kuliwazia hilo kwa mapana yake
Ndugu yangu…andika jambo la hekima ili iwe sadaka yako ya baadae, ..
‘Ulimi..’, sasa umekuwa ni tatizo. Hatujui jinsi
gani ya kuuchunga ‘ulimi wetu..’ tukikaa wawili ni kutetana tu,..achilia mbali
hayo matusi,…kusengenya imekuwa ni donda ndugu..unajua kusengenya ni sawa na
kumla mtu nyama yake….sijui kama tunalifahamu hilo...umekula nyama za watu wangapi...
Haya labda ndio huko kutafuta ‘kiki..’, sawa
utapata wafuasi wengi, na wengine ni biashara kwasasa, lakini ukumbuke
ulichoandika atakuja kuulizwa nacho..na wapo waliondika zamani sasa ni
viongozi, wamekuja kuonyeshwa walichoandika kipindi hicho, imekua ni aibu
kwao..sasa hayo ni ya hapa duniani, je huko mbele ahera ambapo kila la siri
litawekwa wazi, kila ulilofanya ukiwa umejifungia chumbani, litabainika,...kila mtu ataliona,..yabidi tulie sana kwenye toba...
Tunaambiwa na watu wa imani, haya ya ulimi, hayaishii hapa hapa duniani,Ulimi
utakuwa ndio shahidi, siku hiyo ya kiama, kila kiungo kitatoa ushahidi wake, kwa
jinsi nafsi yako ilivyokituma,…huna cha kukwepa hapo,..ulimi utasema
ulichoongea kwa kupitia wewe, mkono, macho, na kila kiungo chako…ni siku ngumu
sana jamani,.
Labda kwa wale watakaojiwa na imani wakatubia,
wakapata muda huo wa kutubu madhambi yao, lakini sasa muda huo tunao, na kama
tuliwatukana wazazi wa wenzetu, na ndio tabia yetu, tutawezaje kutubia hilo,
maana toba ya kweli hapo ni uende kwa kila mzazi uliyemtukana umuombe
msamaha..tutaweza hilo.
Yawezekana kabisa
matatizo tuliyo nayo , mitihani tuliyo nayo ya maisha, na mabalaa mengi
yanatokana na ndimi zetu, hulka na tabia zetu, hatujaweza kujichuja , tunachukulia kila jambo kwa jaziba,…kila jambo
tunakimbilia kulalamika tu…kulaumu tu, mwisho tunachukiana, tunanyonyosheana vidole,...tunashikana mashati, tunaumizana…kila
mtu anawaona, je hayo tunayoyafanya kwa siri tukijifanya hatuonekani, usiku tunawanga, hayo yote yatakuja kubainika siku hiyo ya hukumu…tutakuja kusema nini.
Ndugu yangu, toba ya kweli ndio dawa ya maradhi haya ya
ulimi..tutubu na tuache kabisa madhambi hayo…, na toba nyingine ni kukithirisha kutenda
mema, mambo mema hufuta maovu yetu,…
Tumuombe mwenyezimungu
atusaidie maana haya sasa ni zaidi ya uwezo wetu, bila neema yake yule
aliyetuumba, tutaangamia, ulimi, kalamu, mitandao..itatuangamiza,..leo twapigana makonde, kesho yaweza kuwa silaha…wengine
walianza hivyo, hivyo… kikao kidogo ngumi, uchaguzi mdogo ngumi, …kidogo
kidogo, uchaguzi mkubwa je…
Tumuombe mungu
atuepushie hayo na chuki zilizojaa mafundoni mwetu ziyeyuke na kuwa upendo na amani…
Ila kwa wazo la leo, tukumbuke
jambo moja tu…
.
'Maovu, hufutwa kwa
wema, , tutende wema tufute maovu yetu..tutende wema, tuwezeshe wenye maovu,
waone aibu ya kuendelea kutenda maovu yao, ili na wao waje kutenda mema,.., na
tusizidishe maovu kwa kupigana na kuumizana, tutazidi kuifukuza Baraka, na
neema.
Hilo ndilo Wazo la leo, nawatakia ijumaa
njema.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment