Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, October 8, 2018

TUSHUKURU NA WALA TUSIKUFURU


 JE NI ZIPI NEEMA ZA MOLA WETU TWAWEZA KUZIKANUSHA…

Nikiwa kwenye dala dala, niliwaona mabinti wawili, wakiwasiliana…awali kwa fikira za haraka nilhisi ni majigambo,…maana wanaongea kwa vitendo zaidi ya kutumia midomo yao,..au ni katika namna ya  kuhimizana jambo fulani, lakini nilipochunguza  kwa makini nikagundua, …sio kuongea kwa kuhimizana..

Nikasogea karibu, nikijua wanahizana jambo fulani...

Nikagundua kitu,..hawa watu wanaongea kwa ishara, wakitumia vidole na mikono...walikuwa wakiwasaliana hivyo, na walikuwa wakielewana kabisa,..

 Baada ya kuligundua hilo hisia zangu zilinifanya nihisi kama kutoa machozi!!...ni likwenda mbali zaidi kimawazo…hawa wanaweza kuongea wakafurahi, lakini sisi hatuwezi kujua wanaongea nini labda ukisie tu..

Katika hisia hizo, nikakumbuka maneno matakatifu yanayosema ‘…basi ni ipi katika neema za mola wenu mlezi  mnayoikanusha…’ kwa mwenye imani ya kuelewa, ukisikia hayo maneno, utatafakari sana, na unaweza kutamani hata kulia.

Kiukweli, sisi kama wanadamu tuna neema nyingi tu mola katujalia, hata kama utaikosa mojawapo ya hizo neema, una macho, una masikio, una kiwili wili, na unaweza kupumua,..kuacha hayo, kuna mambo mengi ya ajabu, yote ni neema za yule aliyetuumba…! Nilipofikia kuliwaza hilo, nikainua kichwa na kuwaangalia wawili wale.

Niliwaangalia sasa kwa hamasa zaidi, sio mimi peke yangu, wengi, walizamisha mawazo yao na kuyaelekeza kwa mabinti hao wawili wakiwa wanaendelea kuongea kwa furaha kwa kuonyesha ishara ile ya vidole na kiganja cha mkono,,..walikuwa wamevalia vyema kimaadili, na mkononi mmojawapo alikuwa kashikilia simu.

Ilionekana mabinti hawa wawili walikuwa wakienda sehemu , na wakawa wanawasiliana na jamaa zao kwa simu..sasa hapo utajiuliza walikuwa wanawasilianaje na hao jamaa zao huko, na mimi niligunduaje hilo,  kuwa wao walikuwa wakiwasiliana na jamaa zao hao, wakati wanatumia ishara tu...

Mimi nilivutika nao sana, ..nikajitahidi , nikasogea hadi nikafika pale waliposimama, nikajitahidi hadi nikaona ile simu, vidole ndivyo vilikuwa vinafanya kazi, kumbe huyo mmoja alikuwa akiandika ujumbe wa maneno kwa jamaa zao hao..

Swali likawa anaadika nini...?

Kiukweli nilitarajia, atakuwa anaandika kiishara shara kama vile anavyowasiliana na huyo mwingine...hapana, kwenye simu niliona akiandika, kwa lugha sahihi ya Kiswahili na kiingereza.

Ndio sasa nikawa na uhakika , kuwa kumbe ni wenzetu hawa wenye ulemavu wa kuongea, na kusikia, kwa lugha isiyo rasimu, watu wanawaita ‘mabubu na viziwi’.

Wakati huo…watu wengi mle ndani ya gari,wakawa sasa wanawaangalia kwa hamasa, maana mabinti hawa walikuwa wakiwasiliana huku wakicheka, kuashiria wanaongea jambo la furaha na kuelewana vyema kabisa, ni kama mimi na wewe tunavyoweza kuongea kwa mdomo na kwa sauti.

‘Je ni ipi neema ya mola wetu mlezi unayoweza kuikanusha…’ hapo nikawa najiuliza mimi mwenyewe, nikitafakari na jibu likawa  ‘hakuna…’.

Wewe ukijiona huna hiki, au kile, ujue una hiki au kile ambacho mwingine hana, na huenda kina thamani kubwa zaidi ya kile unachoona huna, sema wewe hujui tu…mara nyingi, tunakimbilia kulalamika, na kujisikia vibaya na hata kusema kwanini mimi

Je hawa...je yule mwenye mapungufu hayo asema nini..ni kweli katika maisha yetu ya kawaida, hao,  …tunaokimbilia kuwaita wana mapungufu fulani, tukaona hawawezi kufanya jambo, kumbe kwa kadara za mola, kawajalia mambo ambayo hata wewe na ukalifu wako huwezi kuyafanya…

Nikawaangalia mabinti wale tena, moyoni nikasema kumbe wenzetu hawa wanacho zaidi ya kile tulicho nacho sisi, kwa vipi…!! Utalishangaa hili,…

Sisi twaweza kuongea kwa mdomo kwa lugha tuliyo nayo, lakini je kama huwezi kuongea kiingereza unaweza kuwasiliana na muingereza,  mkaelewana,..au kama unaweza Kiswahili hujui kuongea kichina, unaweza kuwasiliana na mchini mkaelewana, kwa vipi sasa , labda upate mkalimani

Lakini kumbe kuna lugha ya ishara...sasa kwa ukamilifu wetu wa kuweza kuongea na mdomo, na kusikia, lugha hiyo ya mawasiliano hatuiwezil, lakini wenzetu hawa kwa lugha yao hiyo ya ishara ..wanaweza kuwasiliana na mtu yoyote duniani…je hii si neema kwao, je ni ipi neema ya mola wako waweza kuikanusha....

Hapo nikamshukuru mungu, kuwa yeye ni muweza wa kila kitu, yeye, kakadria kila kitu  kwa namna yake, kampa kila mtu kwa namna ainayo yeye ni sahihi kwa huyo mtu au kiumbe hicho..sisi hatuwezi kulifahamu hilo.

Katika dunia hii kila mtu ana matatizo yake, ..kila mtu ukimtafiti ana matatizo yake, mengi tu, sizani kama kila mtu kakipata kila kitu anachokitaka yeye mwenyewe...tunaweza kuhisi kuwa matajiri hawana shida, si wana pesa bwana.

Lakini ndugu yangu, ... tajiri, na utajiri wake wote ana matatizo yake lukuki, sema yeye kutokana na utajiri wake anaweza kuyafukia matatizo yake kwa pazia,..wangapi, wana mali, hawana watoto, wangapi wana mali, lakini hawana raha ya ndoa,..wengine wana maradhi yanawatesa, hata kuitumia mali yake kwa raha hawezi tena wengine wana maradhi ya kisukari, wana presha, hawatakiwi kula vyakula fulani fulani hata kama wanavitamani.

Wapo wengine na utajiri wao huo, walitegemea watoto wao waje kuwasaidia, waishi nao kwa furaha,, lakini watoto hao hao wanageuka kuwa mtihani kwao,..watoto wengine hawasikii, wavuta unga, au wana matatizo haya na yake…lakini mapesa wanayo. Je hizo sio shida kwao...

Ina maana ya kuwa, hata kama una matatizo, au una mapungufu fulani bado kuna neema umepewa na mola wako ambazo, watakiwa ushukuru kwa kuwa nazo...na huenda ukiweza kuzitumia vyema hizo neema, unaweza ukayashinda hayo matatizo uliyonayo, ...

Ndio, unaweza kuishinda hiyo mitihani, hata kama sio kwa kuiondoa, lakini yale matatizo yakazidiwa na hizo neema ulizo nazo, na wewe kwa imani ukaziona, ukujiona una vitu mola wako kakupatia, ukajawa na imani hiyo ya kushukuru, zile shida nyingine zitafifia tu...muhimu kumbuka jambo moja, hizo neema  kakubariki mola wako, bure tu,..je haitoshi wewe kumshukuru kwa hizo neema.

Wakati bado nipo kwenye hiyo safari yangu, nilipita sehemu na kukuta watu wapo kwenye harusi, na pembeni yake mbele kidogo tu, kuna msiba..watu wanalia, ..wamepoteza mwenza wao,..na mtaa wa pili yake karibu na hizo nyumba nikawakuta wakina mama wakipiga vigelele, wamajaliwa mtoto mchanga,..

Je hizo si neema,

Ajabu kabisa..leo kule nimewakuta wati wanalia, mwenza wao safari yake imeshafika, hapa anazaliwa mwingine, mtu mwingine mpya anakaribishwa kwenye hii dunia ya mitihani…na wakati huo huo kule nilipita harusi, wanatayarishwa wengine, kwa maandalizi ya kuleta baraka ya kizazi kipya, ..je hizo zote ni nini, ni neema, na ni nani kazileta , japokuwa nyingine zinaumiza moyoni…

Ni ipi kati ya hizo neema alizotupatia mola wetu twaweza kuzikanusha, hebu niambie wewe

Kweli ukikosa hiki, utalalamika...kwa vile mwenzako anacho au sio..lakini huenda ungelikuwa nacho, huenda ingelikuwa mengine, hayo hatuwezi kuyaelewa kwa utashi wetu mdogo wa ufahamu.

Sasa ni wakati, hicho ulicho nacho, ..shukuru sana, kama una macho, una masikio, umekamilika kwa kila kitu, shukuru sana..na ujue wenzako wasio nacho wanakitamani, japokuwa kwa kutokuwa nacho, mola kawatunuku neema nyingine zaidi ya hivyo ulivyo navyo..tusikimbilie kulalamika, au kuhuzunika tukakufuru.

Hata hivyo kuna wengine ambao mola kawajalia lakini kujaliwa kwao huko, wao badala ya kutumia vyema, wanatumia kwa isirafu,… wapo hao, wanaagiza sahani hotelini, anagusa tu, anaacha, kinaenda kumwagwa...au ndani kwake, kajaza zaidi ya hata ya uwezo wake, huku anamuona jirani yake hana..hataki kumpa, ni bora kiharibike ndani, jamani …wapo wenzetu hata huo mlo mmoja wa siku hawauwezi, na sio kosa lao, ni shida,….inasikitisha....sana

Hii ni nasaha kwangu na kwako pia, ,…tuzishukuru neema za mola wetu mlezi  na wala tusikufuru…


Ni ujumbe wetu sote kwa leo...niwatakie jumatatu njema , jumatatu yangu ya kumbukumbu, ....


Ni mimi: emu-three

No comments :