Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, September 26, 2018

HATA WENYE AKILI WANA ‘UKICHAA’…




‘Hata wenye akili wana kasoro ya akili,..’ akasema babu yangu

‘Kwa vipi babu…?’ nikamuuliza babu, huku nikijiandaa , maana babu anaanzia mbali.

‘Wengi wanawaona wale walio na mtindio wa ubongo, au ‘vichaa’ au ‘wendawazimu’ kama wanavyopenda kuwaita kuwa wao hawana akili…kumbe kila mwanadamu..pamoja ya huko kujiona ni mkamilifu bado ana kasoro kwenye akili yake, kwahiyo kila mtu, anaweza kuwa..’kichaa’ bila kujijua…’akasema.

‘Mhh, babu…sio kweli…’nikasema

‘Nikuulize, hujawahi kusikia docta bingwa wa maradhi ya kansa, au kifua kikuu, anakufa kwa ugonjwa huo huo, yeye amekuwa mtumiaji wa gongo, anavuta sigara, au anavuta bangi..na matokea yake anakuja kupatwa na maradhi hayo hayo ambayo yeye ni bingwa wa kuyatibu…’akasema kama ananiuliza

‘Haiwezekani babu mtu mpaka awe dakitari, atakuwa na akili sana…’nikasema

‘Haya tuuache mfano huo wa wataalamu…, tuangalia mfano wa maisha yetu ya kila siku ya watu wa kawaida…wewe una safari, umefika kituoni, gari linakuja limejaa kupita kiasi kwa vile una haraka, au hata huna haraka, wewe unaingia tu,…huku unafahamu gari kujaza kupita kiasi ni hatari, wewe unajipenyeza ndani ya hilo gari, au unaning’inia mlangoni kwa shida…huku  unajua ni hatari kwako..

Au mfano mwingine,…wewe ni dereva unaendesha gari kwa mwendo kasi, wakati unajua ni hatari…wewe kweli una akili hapo…, kwanini unafanya hivyo,..kwa vile kuna uwalakini kwenye akili zako, hujataka kufikiria zaidi,…umepungukiwa na kufikiria hatari ya mbele…na unaendesha hivyo unapatwa na ajali,…je wewe ulitumia akili yako vyema, je  wewe sio kichaa…?’ akaniuliza

‘Hahaha babu…huwezi kujiita kichaa hapo…’

‘Kuna mtendo tunatenda, ambayo, hatuoni hatari yake tunapoyatenda,…lakini ni hatari, na tutaiona hatari yake ‘ ni hatari’ pale hatari ikishatokea, na hapo tutaanza kujilaumu…kwanini, kwanini…sio kwanini, akili za kufikiria zaidi hatuna…tuna mapungufu ya akili, tuna nini, upunguani fulani, lakini wenyewe hatujijui..…’akasema

‘Ni wangapi wanafanya mambo ambayo ni ya aibu, kwenye  jamii….siwezi hata kuyataja, mengine hata wanayafanya wanaogopa kuyafanya…lakini wanaonekana wana akili kwenye jamii kwa vile…hatuwaoni hivyo, ….’akasema babu akiniangalia.

‘Lakini  hiyo babu…huo  sio, eeh,  sawa na ukichaa, wa yule anayetembea uchi, akala majalalani uchafu, eeh, sio ndio huyo tunayemuita  kichaa…’nikasema

‘Anayetembea uchi, hamtembei uchii sasa hivi, eeh…hamfanyi mambo hayo, niambie ukweli…’akasema babu, hapo nikabakia kimia, na aliponiona nipo kimia akaniuliza swali;

‘Hebu nikuulize swali, kwani, ‘Ukichaa’ au wendawazimu,  ni nini  mjukuu wangu kwa jinsi unavyoelewa wewe….?’ Akaniuliza akiniangalia machoni.

‘Ni matatizo ya akili, mapungufu ya akili,…yanayokufanya usiwe na akili za kawaida ukawa unatenda matendo yasiyo ya kawaida,…bila kufikiria au kuogopa,..ni yule anyefanya matendo yasiyo ya ki-kawaida, kama mtu utakiwavyo uwe,…’nikasema nikijaribu kuwaza nijuavyo mimi kwa wakati huo.

‘Sawa kabisa mjukuu wangu…’akasema na kuniangalia machoni….

‘Je yule anayefanya  matendo yenye kumuweka hatarini, kiafya, yenye kukufanya uwe kwenye hatari kiusalama, yenye kukufanya ufanye jambo ambalo sio la kawaida kutokana na taaluma yako, au kutokana na utaratibu ulivyo, ukiyafanya hayo, sio umefanya kwa kutokufikiria, na huko kutokufikiria nini, sio ndio umefanya kwa kutokutumia akili yako vyema …na huko kutokufikiria vyema ni nini… sio ndio ukichaa huo au...?’ akauliza na mimi hapo nikacheka.

Sina nia ya kumkashifu mtu, ila nimeliwaza sana hili, kuwa kumbe sisi sote tuna madhaifu hayo…ni mara ngapi tumedandia magari, yakiwa yamejaa kupita kiasi tukijua ni hatari, …na hata kuning’inia milangoni,,… ni mara ngapi tunapanda pikipiki bila kofia za kinga, ni mara ngapi tunaendesha magari kwa mwendo kasi wenye kuhatarisha maisha…au kuendesha sehemu zenye hatari.. ..ni mifano michache tu…

Na ni mara ngapi, tumekula vyakula ambavyo sio salama, ni mara ngapi tumekunywa vinywaji hatari kwa afya zetu, kuvuta sigara, bangi nk..…na ni mara ngapi tumefanya mambo ambayo yanatuweka hatarini,  mfano kugushi, kudanganya, kutokuwajibika kwenye kazi zetu,..kudhulumu nk…je tunapoyafanya haya tumetumia akili zetu vyema, tujiulize tu…

Jeee, kwa kufanya hivyo, kufanya ‘utofauti’ na hali inayotakiwa,..tukaacha kufikiria hatari ya hilo jambo, au  uhalali wa hilo jambo, au usalama wake,…hatujawa na ‘uwalakini’… je hapo tunapofanya hivyo, akili zetu zipo kamili, kweli… eeh,…tusijidanganye, ..kakichaa kadogo kadogo tunako,…kumbe tunako…

Hahahaha kumbee, ahsante babu,


Hata mimi au wewe tuna mapungufu hayo ya akili, ya kutokufikiria hatari ya jambo, kabla ya kulitenda, basi ili tusiwe hivyo, eeh, ndugu zanguni,… kabla ya kufanya jambo lolote…, TUFIKIRIE KWANZA, TUTAFAKARI KWANZA, TUJENGE HOJA, JE NIKIFANYA HIVI NI NINI KITAKUJA KUTOKEA BAADAE,..Tusifanye jambo, kabla ya kutumia akili zetu vyema.

SOMA KISA CHA 'DUNIA YANGU...' utaliona hili....


Ni mimi: emu-three

No comments :