Hali ya Dalali iliendelea kuwa mbaya, alikuwa kalazwa
chumba cha wagonjwa mahututi na baadae akaingizwa kwenye wodi maalumu, bado
akiwa hajitambui, akiwa anapumulia gesi.
‘Hali ikiendelea hivi itabidi tuondoe tu hii mashine,
haisaidii..’alisema docta, na wanandugu wakabembeleza, ..na madocta wana muda
wao, wakaendelea kumuhudumia hivyo.
Kiukweli…, kwetu sisi tuliomuona hali yake ilipoanzia,
bado tulikuwa tunajiuliza, jinsi gani mtu unavyowezakubadilika ghafla hivyo, na
kuchungulia kaburi. tujuavyo sisi, hali ya Dalali, ilianza kama mchezo tu…
ilianza kwa kwikwi tu,…na kuna muda mimi nilimuona akitoa macho sana, kama
kaona kitu,…na kwa mujibu wa wakili wake, yeye alisema kuna muda alimuona
akishika upande wa moyo kuashiria anahisi mumivu.
Na watu wa nje ambao hawajui kilichotokea wakawa
wanaongea yao mengine, unajua tena.. Dalali ni mtu mashuhuri, habari zake zilishazagaa kila kona,….
‘Je huyo mtu alipatwa na mshituko gani…?’ akauliza
docta anayemshughulikia. Tukaelezea ilivyokuwa kwa kila mtu, jinsi alivyomuona,
na docta akasema;
‘Yaonyesha huyu mtu alipatwa na mshtuko mkubwa…na
hadi kutokea hivi ina maana huo mshtuko umeathiri mishipa ya damu, iri mishipa
ya damu, siwezi kusema zaidi,…mpaka vipimo vitokea, bado tunamchunguza, ila kwa
hivi sasa tusiendelee kujazana hapa na kuongea maneno ambayo yatamzidishia hali
yake kuwa mbaya…’akasema docta.
Na hapo sisi tukatoka nje..na tokea siku ile
hatukuruhusiwa kuingia kumuona zaidi ya mke wake, na ndugu yake mmoja wa
karibu.
Siku ikapita na siku zikapita, wiki sasa, mara mwezi…
Tuendelee na kisa chetu…
*************
Mimi nikawa nawasiliana na mama mjane, na siku hiyo
nilipofika kwake nikamkuta analia,
‘Vipi shemu..kwanini unalia tena, nilishakukataza
kuwa hivyo…?’ nikamuuliza
‘Nashindwa kaka yangu…mengine hayavumiliki..’akasema
na moyoni nikahisi labda ile ajenda ya kuuza hiyo nyumba imerejea
tena,..tulishaomba zoezi hilo lisitishwe mpaka uchunguzi wa kina ufanyike, na
kweli mahakama ikaridhia hilo kwa muda, japokuwa benki waliendelea kushinikiza
tena baada ya kuona mwezi umepita na hakuna kinachoendelea.
‘Yapi hayo kwani kuna taarifa gani mpya..?’
nikamuuliza.
‘Ama kwa taarifa mpya sijaipata ila nasikia tu, benki
wameandika barua ya kulalamika, wakiomba kesi hiyo isikilizwe haraka maana muda
umepita, na hakuna jipya..kwahiyo wanaomba ama kesi irejeshwe mahakamani au
hukumu ya awali ifanye kazi yake..kwasababu wao wana ushahidi wa kutosha, kuwa
deni hilo ni la marehemu..nimesikia nilipokwenda kuonana, na yule
wakili…’akasema.
‘Ok..hilo sawa, ..kesi itasikilizwa, lakini yote
yanategemea watu wa usalama, kwani waliniambia wanalishughulikia wao wenyewe
hilo swala…, na mimi nisiendelea kulishughulikia, nikaona haina haja, ngoja
niwaachie wao, maana wamenithibitishia kuwa wao wana ushahid wa kutosha,
kuhakikisha haki inatendeka…’nikasema.
‘Wenye pesa ndio wenye nguvu..’akasema mama mjane.
‘Hapana , pesa haiwezi kuishinda haki..’nikasema
hivyo.
‘Sawa mimi yote nimemuachia mungu, najua yote
yatatendeka kwa mapenzi yake..’akairejea kauli yake ya mara kwa mara, na mimi nikajua labda hilo
ndilo linamliza, lakini…
‘Kama ni hivyo basi, una imani hiyo thabiti, kwanini unalia, maana naona hata macho
yamevimba kwa kulia…’nikasema na kabla sijaendelea yeye akanikatiza na kusema;
‘Kinachoniliza ni hawa ndugu wa mare-….mume
wangu…’akasema nikaona anasita kuitamka hiyo marehemu, nahisi bado akili yake
haikubali …
‘Wamefanya nini tena..?’ nikauliza
‘Hawataki mimi niende kumuona mgonjwa, je hivi ni
haki hiyo, huyo shemeji ndiye alikuwa msimamizi wa familia, na ndiye aliyekuwa
karibu na mimi,leo hii hajiwezi , mimi nikae tu, bila ya kumuona, japokuwa
mpaka sasa hajaweza kuongea au kumtambua mtu, yupo yupo tu…’akasema
‘Kwanini sasa wanakukatalia…?’ nikauliza
‘Ndio hicho kinaniliza,…na kwanini wani zalilishe hivyo…’akasema na mimi
hapo bado nikawa gizani, na alipoona nasubiria maelezo yake zaidi akasema;
‘Mimi mjane, ..na watoto wangu hawa mayatima, nina
uwezi gani wa kumfanya huyo mtu awe katika hiyo hali…je kweli ni mimi
nilisababisha hayo yote…eti pia ni mimi niliyechangia mume wangu kufariki…leo
hii nimepakaziwa maneno mengi zaidi ya ile ya kwanza..hadi mimi sasa naitwa eti
mimi ni mchawi…’hapo machozi yakaanza kutoka.
‘Shemu, maneno sio njia,..nakuomba tena na tena,
usiyaweke akilini mwako yakakuvunja imani yako, kwenye vita hapakosi mambo kama
hayo, nia yao ni kukuvunja nguvu, huelewi hilo…kumbuka dada, ..hivi ni vita vya
kuitafuta haki yako na watoto wako, kamwe usikate tamaa…’nikasema.
‘Unasema tu hivyo ndugu yangu, maneno mengine
yanaumiza…fikiria nilikwenda hospitalini, na sikuenda kwa hiari yangu, maana
walishanikataza hao ndugu zake kuwa nisifike hapo kumuona huyo mgonjwa,.’akasema.
‘Sasa kwanini ulikwenda..?’ nikamuuliza
‘Docta alinipigia simu akasema. Dalali kuna muda
alipata ufahamu kidogo, akawa analitaja jina langu…kwahiyo akaona labda
nikifika hapo, inaweza kusaidia akaweza kuzindukana, au hata akizundukana,
huenda kuna ujumbe anataka kunipatia..’akasema
‘Mhh, sasa kwanini hukuwaambia hao ndugu zake kuwa
umeitwa na docta, na huenda kuwepo kwako kutasaidia mgonjwa kuzindukana..’nikasema.
‘Nilijaribu kuwaambia hivyo, lakini hakuna aliyetaka kunisikiliza,
walinitoa mle hospitalini kama mwizi, hata docta alipofika,…alikuta
nimeshafukuzwa mbali, na nje nikakutana na watu waliotayarishwa kunizomea,…wakiimba
‘mchawi , mchawi…’…hebu fikiria kama ingelikuwa wewe ungekuwa na ujasiri gani
wa kuyavumilia hayo.
‘Mhh..oh....huenda ikangelisaidia kweli kumzindua,
kama alivyoshauri docta, ina maana hao ndugu hawataki ndugu yao apone …’nikasema.
‘Mimi nilikwenda nikijua hivyo, nikafika na kuongea
na mlinzi kuwa mimi nimeitwa na docta nije nimuone mgonjwa, mlinzi akaniruhusu, ile nataka kuingia tu, mmoja wa
ndugu yao, sijui ndiye aliwekwa kulinda hapo nje,akaniona,.. akaja kunifurusha,,
huku akiwaita wengine, ni kama walijiandaa kunifanyia fujo…’akasema
‘Ina maana muda huo docta hakuwepo…?’ nikauliza
‘Docta aliyenipigia simu kumbe alishatoka, ila alicha
maagizo kuwa mimi nikifika nijitahid kukaa hapo karibu na huyo mgonjwa…tatizo nahisi
huyo docta hakuwaambia wengine,au hata sijui….na kwanini hakuwaambia hao wanandugu
kuwa, mgonjwa alinihitajia mimi…’akasema.
‘Huyo docta unamfahamu na una namba yake siku zote..?’
nikamuuliza.
‘Hapana, ila alijitambulisha hivyo, kuwa yeye ni
docta anayemshughulikia Dalali…’akasema.
‘Oh…nahisi hapo kuna jambo..huenda hata huyo docta aliyekuita
akawa ni docta au sio docta, huenda kuna mtu mwingine alipanga hilo lifanyike,
..lakini najiuliza ili iweje..nahisi hapa kuna kitu…nahisi…ngoja tutakuja kuliona
hilo,...’nikasema hivyo
‘Yaani ni aibu…aibu, …unajua nilivyojisikia…, hebu
lifikiria wewe hivyo, kama ingelikuwa wewe umfanyiwa hivyo..jamani mimi..nimewakosea
nini hao watu..na hadi sasa watu wengine wameshanifikiria hivyo, …ujue Dalali
ni mtu maarufu sana, ana washabiki wengi..yaani ungeliona hilo tukio, aah..,
walinifurusha mimi kama mwizi,…huku wakiananiita mchawi….eti nimefika kumuua
ndugu yao.
‘Duuh…hakuna askari aliyekuwepo karibu, maana Dalali
analindwa na askari, kwasababu yeye ni mtu anayetakiwa na watu wa usalama,
kuhojiwa, hatakiwi kukimbia au kitokee kitu kibaya dhidi yake..?’ nikauliza
‘Sikuwahi kumuona huyo askari..’akasema.
‘Pole sana…’nikasema.
‘Nilijisikia vibaya sana, ..haya mambo nilijua
wanafanyiwa wazee,..kumbe hata sisi wakina mama…oh, sijui nitaishije mimi
jamani,..maana kila nikipita mahali watu wakiniangalia nahisi ni yale yale,
kumbe watu wengine wanauwawa tu bure kwa shutuma za uwongo..hebu fikiria, …..’akasema
kwa uchungu.
‘Pole sana…’nikasema
‘Kinachoniuma zaidi …wamefikia, kuwaita hata watoto,…hawa
watoto wangu eti ni watoto wa mchawi, wameanza kujenga fitina kwa watoto
wengine wadogo, wawe wanavumisha hivyo, jamani hata hawa watoto wana kosa gani…’akainamisha
kichwa chini.
‘Shemu…mmh samahani mimi…, nimezoea kukuita hivyo,
‘nikasema na kabla hajasema neno, nikaendelea kuongea;
‘Hizo ni mbinu za maadui zako za kukuvunja
nguvu,…siri ya ushindi ni kutokuvunjika imani yako uliyo nayo, hivi wakikuambia
wewe hivyo kuwa wewe ni mchawi kweli utakuwa hivyo,…mambo kama hayo yakuongezee
ujasiri, na nina imani mwisho wa siku utasimama shujaa…’nikasema kumpa nguvu.
‘Lakini inauma sana, sijui kama nitaweza kuwa na
ujasiri huo tena…’akasema
‘Nikuulize tu…wakati hayo yanafanyika, hao
watu,..unaweza kumkumbuka yoyote miongoni mwao, je hao ndugu kuacha hao ndugu
za mume wako, hao uliowakuta nje, unaweza kumgundua yoyote mwingine
unayemfahamu,..?’ nikamuuliza
‘Ningeliwezaje , nilichanganyikiwa kwakweli,…halafu
iweje, nikawashitakie au, hapana mimi siwezi kufanya hivyo,..kama ni kuwajua,
haina haja, ni ndugu za mume, ndio chanzo cha hayo yote, lakini siwezi kabisa
kuwashitaki,…’akasema.
‘Unajua kuna kitu nimekiona hapa,…hao watu ni
washabiki wa muhalifu anayetaka kutengeneza uwoga fulani dhidi yako…na hatuwezi
kusema ni washabiki wa Dalali….kuna muhalifu ….kawapanga hao watu wafanye hivyo..sasa
..ngoja…’nikasema na kuchukua simu.
Niliwapigia watu wangu nikawaelekeza jambo, halafu
nikarejea kwa mama mjane, naye akaniuliza;
‘Unataka kufanya nini, wewe si umesema polisi wamekukataza
kuingilia haya mambo…?’ akaniuliza
‘Hii ina maanisha,hizo vurugu zitakuwa zimepangwa na
hao watu tunaowatafuta, kwahiyio mmojawapo, au wote wapo karibu,…na najaribu tu
kubahatisha, huenda miongoni mwa hao watu waliokufanyia vurugu wanaweza
kutusaidia kuwapata hao watu…’nikasema.
‘Kwanini usiwaambie polisi..wao waifanye hiyo kazi…?’
akaniuliza.
‘Polisi hawataki mimi niwafundishe kazi…’nikasema hivyo tu, na kabla huyo mama hajasema neno,
nikaendelea kuongea
‘Unajua wao sasa hivi wanatengeneza propaganda potofu
dhidi yako…wameshaanza kuogopa,…wanatumia ile mbinu ya ukitaka kumuua mbwa
kwanza umuite majina mabaya…’nikasema
‘Ina maana wanataka kuniua mimi…?’ akaniuliza
‘Sio lazima kukuua,..kwa maana ya kuua… ila
kukumaliza nguvu…ila usiogope, nitaongea na wale wapelelezi,.. ubaya wao
utashindwa, maana haki haipo mbali muhimu kwa hivi sasa, kama nilivyokuambia
awali..kuutafuta ukweli wote unaoufahamu ili uje kutusaidia kwenye ushahidi,
ungamgundua kiongozi wa hizo vurugu ingelisaidia sana…’nikasema.
‘Nilimuona mtu mmoja, wakati mwingine huwa anatembea
na Dalali..ni msaidizi wa Dalali,…halafu nimekumbuka, wakati nakimbia,
nilipogeuka nyuma, nilimuona mzee Mtupe..aliponiona, akageuka kama vile
hajaniona…’akasema.
‘Mhh…ok…mzee Mtupe eeh,alikuwa kwenye kundi au ..?’
nikauliza
‘Hapana yeye nilimuona mbali na hilo kundi,
yawezekana ndio alikuwa anakuja hospitalini, akaiona hiyo vurugu, na pale
asingeliweza kufahamu kuwa mimi ndiye nilikuwa nafanyiwa hizo vurugu, labda
walikuja kumuambia baadae, maana mimi nilikuw nakimbia mbali na hapo, baada ya
kuwaponyoka,...’akasema.
‘Lolote lawezekana…mzee mtupe…huyu mzee, huyu
mzee..ok, ngoja nitampitia, ila kila tukio likifanyika hakikisha unakusanya
ushahidi, hujapata kitu chohote cha kusadia huko ndani, popote pale ..?’
nikasema na kumuuliza hivyo.
‘Nitaupatia wapi tena ushahidi mwingine…, mimi..nilijua
zile karatasi zingelisaidia, ..kumbe bado haziwezi kufanya lolote ..’akasema
‘Bado zitasaidia sana, …sema wao hawajanipatia hizo
barua, nikaweza kuzipitia vyema, nahisi kuna jambo ndani yake,…lakini ngoja
nitaona ni nini la kufanya,…ila nataka nionane na huyo mzee…’nikasema
‘Mhh..mimi bado ninaona giza,…nahisi ndoto mbaya
mbaya, na huamini, huyo mzee nimeshawahi kumuota, akiwa kageuka sura ya
kutisha, lakini kwangu ndoto ni ndoto tu…’akasema
‘Uliota hivyo, ulimuota huyo mzee, mmh, labda ni kwa
vile ilitokea hilo tukio, halafu ukamuona,..usijenge hisia hizo mbaya, mimi
nataka kumuhoji, kama anaweza kutusaidia kwenye ushahidi ..’nikasema.
‘Hata sijui, wakati mwingine…nahisi kukabwa..hata
sielewi..na kila ikitokea hivyo anayeniokoa ni mume wangu…na akishaniokoa
ananiambia…usivunje ahadi yako..au, usiniache, au uwe makini,..kitu kama hicho,
sielewi,..kifupi mimi bado..nina mashaka
kweli…’akasema
‘Yah…usivunje ahadi yako, maana yake, nyie mlimuamini
kuwa yeye ni mkweli kwenu, hasemi uwongo,..au sio? ..je leo iweje asingiziwe
hilo deni…natafsiri kihivyo,…na hiyo usiniache, ..ni hii nyumba, hii nyumba kwa
hivi sasa yasimama kama yeye, ukiacha ikichukuliwa umemuacha yeye, na uwe
makini,..ni onyo tu, nahisi hivyo…’nikasema.
Huyu mama akaniangalia kwa makini…halafu akasema;
‘Umesema kweli…lakini tufanyeje sasa.., maana wakili
alivyoniambia, bado sisi hatujaweza kuupata ushahidi wa kutosheleza, hizo barua
hazina uzito wa kuweza kushinikiza hilo deni, na wakili wao kasema hawataweza
kutumia ushahidi walioupata dhidi wa ushahidi wa benki tukashinda…’mama mjane
akasema.
‘Najua sana hilo….kiukweli, mimi niliwaambia hao watu
wa usalama,..cha muhimu ni kuhangaika kuwatafuta hao watu wawili..bila hao watu
wawili , bado tutakuwa hatuna ushahid wa kutosha, maana ushahidi wa kimaandishi
umeshaharibiwa wote..nimeshafika hadi huko benki hakuna …mtandao wao wa zamani
uliharibika, wanatumia mtandao mpya…kumbukumbu za mafaili, hazipo, wanasema
kulitokea moto, kumbukumbu halisi za karatasi zote ziliteketea…’nikasema.
‘Kwahiyo …mimi hapo naona hakuna jipya,…’akasema mama
mjane.
‘Yah….ndio maana mimi nataka hao watu wawili, na
watatu wao ni Dalali, wasimame kizimbani, ..hao wakiulizwa maswali, tutawanasa
tu..’nikasema
‘Je ukikutana nao utawezaje kuwashawishi waongee
ukweli, wewe unawafahamu jinsi walivyo,..ni wajanja , Dalali kasingiziwa…’akasema
‘Ujanja hausaidii….’nikasema.
‘Na hao watu wa usalama, walisemaje, jinsi walivyomuhoji huyo mtaalamu,
hawajakuambia lolote, alichoongea wakati wanamuhoji...?’ akaniuliza.
‘Hawajaniambia lolote, …hata nikiwauliza hawataki
kusema,… wanasema hiyo ni kazi yao kwahivisasa…’nikasema
‘Mimi nilijua watakushirikisha baada ya kugundua kuwa
uliyosema yaweza kuwa ni kweli…’akasema
‘Nawafahamu sana hao watu, kwa namna moja, hawataki
kuonekana hawawezi kazi, kwa namna nyingine wananichukia kwa vile, eti napenda
kuingilia majukumu yao..lakini ngoja tuone…’nikasema
‘Mhh..hata sijui, tufanyeje sasa, mimi naona
tumuechie mungu tu, …’akasema mama mjane.
‘Usikate tamaa, kama tuliweza kumnasa Dalali,
japokuwa hajakubali kabisa.., lakini kwa kupitia kwake, tumeweza kubaini kuwa
kuna udanganyifu kwenye hilo deni,…mpaka polisi wakawa upande wetu, nina imani
kwa kupitia hao watu wengine wawili,.. tukiwapata tu…tutakuja, kubaini ukweli…’nikasema.
‘Hivi wewe ulishawahi kukutana na huyo mtu wa
benki….?’ Akaniuliza.
‘Hapana, …wewe unamfahamuje huyo mtu?’ nikamuuliza
‘Ni mjanja kupindukia, kasomaa…na anapenda kutumia
elimu yake kwa faida.., na anajua jinsi gani ya kujilinda, kujihami hivi....ukiongea
neno la ovyo keshakugundua wapi unaelekea,..ana akili za ajabu-ajabu, kwa jinsi
alivyo, hata watu wanamuogopa, maana kwanini anaweza kugundua unachofikiria
dhidi yake…’akasema na mimi nikasema;
‘Hata mwenye akili sana, kwenye haki atagwaya tu,..naombea
nikutane naye, nimjue vizuri..’nikasema.
Na mara simu yangu ikaanza kuita, ilikuwa namba ngeni
kwenye simu yangu…nikasema;
‘Mhh…hizi namba ngeni kwenye simu yangu sizipendagi,,..mara
nyingi zinakuwa na mitihani fulani, nahisi kuna jambo..’nikasema nikiiweka simu
hewani.
‘Halloh, mtu wa jamii..mimi ni mpelelezi
ninayeshughulikia ile kesi ya mama mjane..nakuhitajia hapa ofisi kwangu haraka
iwezekanavyo…’sauti ikasema
‘Kuna nini mkuu…si nyie mlishasema mimi nisijishughulishe
na chochote au..’nikasema
‘Ndio…hutakiwi, ila kwa hivi sasa tunakuhitajia kwa
haraka kidogo, ..ni katika kutimiza wajibu wetu..’akasema huyo mpelelezi
‘Haya ninakuja afande, kwahiyo niage kabisa, isije
ikawa nakuja kuwekwa ndani…’nikasema na hakujibu kitu, simu ikakatika.
Nikamuangalia mama mjane, naye akaniangalia, akiwa na
shauku ya kujua kitu geni nimeambiwa huko…
‘Ni nani hao…?’ akaniuliza
‘Wananihitajia huko kituoni, polisi…’nikasema na
kumuaga mama mjane,..
‘Kuna la heri huko..?’akasema kwa kuuliza
‘Hata sijui…ngoja nifike nitakufahamisha
kitakachotokea,...’nikasema nikianza kutoka na wakati natoka mara simu ya huyo
mama mjane ikaita..nilikuwa sina muda tena hapo mimi nikatoka nje kwa haraka.
Na wakati natoka nje, nikamuona Mzee mtupe akiwa
anakuja kuelekea kwenye hiyo nyumba,, aliponiona tu akashtuka, ..hakuwa na
ujanja, maana tulishakuwa uso kwa uso .
‘Oh, bahati mzee, nataka kuongea na wewe…’nikasema.
‘Mimi!!!…kuhusu nini, mimi sijui lolote, na..na…nina
haraka, nataka kusafiri…’akasema
‘Lakini nakuona kama unakuja hapa kwa huyu mama mjane
au, unasafiri kwenda wapi…?’ nikauliza.
‘Ndio, ndio..Nataka kumuaga huyo mama, …’akasema huku
anatembea na mimi nikawa najaribu kumfuatilia nyuma.
‘Wapi huko unaposafiri,,..?’ nikamuuliza na hakutaka
kabisa kuongea na mimi
Cha ajabu sasa, badala ya kungia hapo kwa huyo mama
akapitiliza, alionekana ana haraka sana…na mimi nikachukua simu yangu
nikampigia kijana wangu mmoja amfuatilie huyu mzee.
NB: Mhh, mambo yanakuja tu,
WAZO
LA LEO: Hata ukiwa mjanja vipi, hata ukiwa na akili vipi,
huwezi ukafahamu kila kitu..huwezi ukawazidi wote, na hasa pale akili zako, na
ujanja wako unapouelekeza kwenye mabaya badala ya mema.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment