‘Je wewe Dalali,
ulirizika na taarifa ya uchunguzi wa polisi kuwa ajali hiyo
iliyosababisha kifo cha kaka yako ni sahihi,.…?’ akaulizwa Dalali.
Dalali, alibakia kimia kwa muda, na pale wakili wake
alipotaka kuingilia kati, akamuashiria huyo wakili atulie kwanza, na taratibu akaanza kuongea;
‘Ni yale yale kama ilivyokuwa kwenye hilo deni….ni
yale yale wanayonishutumu watu kwa kusema kuwa mimi nashadidia kupigwa mnada nyumba
ya marehemu kaka yangu,…lakini hatusemi kuhusu mahakama ilisemaje…’akatulia
kidogo.
‘Swali linaulizwa, je mimi nilikubaliana na uchunguzi
wa polisi kuhusiana na kifo cha marehemu
kaka yangu, …jamani, hivi mimi ni nani aliyejuu ya ya sheria, je mimi ni nani
aliye juu ya uchunguzi wa polisi..mbona mnataka kunitwika mzigo mnzito ambao
siuwezi kuubeba…’akamuangalia mpelelezi.
‘Mnataka nijibu au sio..sisi kama
wanafamilia…wana-nini, wanafamilia…hatukutaka kupekenyua zaidi, maana mimi
ninawafahamu nyie mlivyo, kama tungeanza kubishana na nyie, ..tungelifika wapi,eeeh,
hebu niambieni,….ina maana kwa kufanya hivyo, tunawakosa kwenye kazi zenu, mimi
sio mtaalamu wa maswala ya ajali za barabarani, ni ningelisema nini
hapo…’akatulia
‘Ila…narua tena ila… kama nyie mlikosea kwenye hiyo
taarifa yenu ya uchunguzi,..mtuambie…’akatulia.
Mpelelezi, akawa anamsubiria Dalali, kama ataendelea
kuongea zaidi, lakini Dalali akabakia kimia, akitikisa kichwa kama kujisifia
kwa kile alichokiongea, lakini kwa upande wa pili wakili wake alionekana kama
kutatizika fulani hivi.
‘Ndugu Dalali,…nilikwisha kuelezea ilivyokuwa, na
kukuarifu kuwa jalada la uchunguzi wa kesi ya kaka yako lilikuwa halijafungwa,
kwasababu kulikuwa na maswali ambayo yalikuwa hayajapatiwa majibu yake..hii ni
kutokana na mimi kupatwa na dharura….sasa ili kuendelea na uchunguzi wetu, na
baadae kuhitimisha kabisa , …kwanza nilitaka kusikia kauli zenu…’akatulia
mpelelezi.
Dalali
akacheka kwa dharau…na kusema;
‘Je kauli zetu zitasaidia nini….kuwa kaka atarejea
tena, kuwa kama mlikosea nyie, eeh, nyie…eeh,…kwenye uchunguzi wenu, tutawashitaki,….eeh,…
je tukiwashitakia, mtafanywa nini…toka lini kesi ya ngedere ukampelekea
tumbili,…sijui mnanielewa…’akawa kama anauliza na mpelelezi akabakia kimia tu.
‘Kiufupi, ni kuwa tutakuwa tunajihangaisha tu…mimi
kama mkuu wa hio familia tuliyokabidhiwa, kwa niaba ya wanandugu wote,..
ninasema hilo kwetu tuliamua kuliacha kama lilivyo,yote yaliyotokea eeh,
tuliyachukulia kuwa ni mapenzi ya mungu....labda nyie sasa, eeh…mtuambie kama
kuna lolote limejitokeza…’akasema Dalali.
‘kwa kusema hivyo ina maana wewe kama mkuu wa hiyo
familia, uliwaarifu wenzako kuhusiana na taarifa hiyo, mkakaa na kuijadili, mkakubaliana
hivyo…au sio, au wewe ulipoisoma kwa niaba ya wenzako ukarizika hivyo, kuwa
kifo kimeshatokea basi,…?’ akaulizwa.
‘Ni hivi….taarifa imeshafika, kuwa kaka alifariki kwa
kifo cha ajali ya barabarani, ..ajali ni ajali, ajali kwani ina kinga, eeh,
ndio kila mtu atakufa kwa sababu maalumu..bro kafariki kwa ajali ya gari, ndio
mwisho wake ulipangwa uwe hivyo… na tuliridhika hivyo baada ya kupokea taarifa
ya uchunguzi kutoka kwenu,..je nyie mlitaka sisi tufanyeje au wewe niambie
hapo..?’ akawa kama anauliza.
‘Je shemeji yako naye alikubaliana na hilo…?’
akaulizwa hilo swali badala ya kujibiwa swali lake.
‘Mhh, yeye kipindi taarifa hiyo inaletwa kiukweli hakuwepo,
kutokana na hali yake ilivyokuwa…, ila sisi wanandugu tulikubaliana na hilo, sisi tulitosha kuwakilisha wanafamilia wote,
tulikubalia na uhalisia, yaishe tu…, unajua tena, mtu akifa, hata
ufanyeje..haisaidii kitu jamani, kwanini haya yazuke tena, ….’akageuka
kumuangalia shemeji yake.
‘Je shemeji yako aliporejea kwenye hali yake uliwahi
kukaa naye mkaliongea hilo, ikizingatiwa kuwa yeye hakuwepo kwenye hicho kikao
cha awali,…na hakuwa na ufahamu kuhusu huo uchunguzi huo wa polisi,..na huyo ni
mke wa marehemu, ni muhimu kwa kulifahamu hilo, je uliwahi kukaa naye mkaliongelea
hilo..?’ akaulizwa.
‘Afande, naona ni maswali ya kujirudia rudia
tu….’akalalamika hivyo.
‘Tunaweza kujirudia mara nyingi, kutokana na utaalamu
wetu ulivyo…’akasema mpelelezi.
‘Haya….shemeji kutokana na hali yake, haikutakiwa
kukaa na kuanza kumuongezea mawazo, sisi tulifuata maagizo ya docta, kuwa tuwe
makini katika swala lolote linaloweza kumrejeshea mawazo mama mjane…na sisi
tukaliona hilo, kwahiyo mimi sikuona kama kuna haja ya kukaa naye na kuanza
kusema ya moyoni, kuwa hatukurizika, au tumerizika…’akasema.
‘Ukisema ya moyoni, kuwa mumerizika au hamkurizika,
inanifanya nikuulize tena hilo swali kama wewe, nataka kufahamu ya kutoka
moyoni mwako kama wewe,..je wewe ulirizika na hiyo taarifa ya uchunguzi wa kifo
cha kaka yako …?’ akaulizwa.
‘Nilishakujibu hilo swali lako afande..’akasema
Dalali….alipoona wakili wake anataka kuingilia kati.
‘Kuwa…?’ akauliza hivyo mpelelezi
‘Kuwa sisi wanafamilia, tuliamua kurizika na hiyo
taarifa kwa vile nyie ndio wataalamu, nyie ndio mliofanya uchunguzi, na
tulikubali kuwa mlivyoona nyie ni sahihi kwetu, tungelifanya nini zaidi ya hapo
eeh…, ila kama..nyie mlifanya makosa, sasa wewe ndio utuambie…’akasema.
‘Uliisoma vizuri hiyo taarifa ya uchunguzi..?’
akaulizwa na hapo akashtuka kidogo, halafu akabenua mdomo kizrau vile.
‘Ndio eeh, ndi- ndio…sijui,…nasita kukujibu hilo
swali kwa maana yangu…’akasema
‘Kwa maana gani, tuambie tu..?’ akaulizwa
‘Kipindi kile kilikuwa kigumu kwetu kama
familia,…ndio niliisoma, eeh mbele ya wanafamilia,..lakini nakumbuka hatukutaka
kuisoma yote kwa ujumla wake, unajua tena, siwezi kusema ni kwanini, lakini kwa
mtu ambaye kapitia hali kama hiyo unaweza kutuelewa tu…muhimu ni yale maelezo
ya mwanzo kuwa ndugu yetu, alifariki kutokana na ajali ya gari…’akasema.
‘Ndio ni kutokana na ajali ya gari,… na hilo gari
lilikuwaje, mpaka likasababisha hiyo ajali, kulikuwa na melezo hayo, kwahiyo
wewe uliyekuwa ukiwasomea wenzako hukutaka kuendelea kuyasoma, ni kwanini
ulifanya hivyo, maana yalikuwa na umuhimu wake kujulikana…?’ akaulizwa.
‘Mhh…unajua…’akataka kujitetea.
‘Je ulisoma, wewe kama wewe, ..na ukaona hakuna
umuhimu kuwasomea wenzako au hata wewe hukusoma kabisa…?’ akaulizwa
‘Nikuambie ukweli, nilipoyapata hayo maelezo,
nilifika kwa wenzangu nilichokifanya ni hivyo, kusoma yale maelezo ya juu,
sikutaka kuingialia undani wake, na nikarejesha hiyo karatasi kwenye bahasha
yake,…basi…sijasumbuka tena…’akasema
‘Hiyo taarifa unayo….?’ Akaulizwa
‘Wala sikumbuki nimeiweka wapi, ni mpaka
niitafute…’akasema
‘Kwahiyo kumbe hukuichukulia maanani, ..au ulifanya
hivyo kwasababu gani,….hiyo sio taarifa muhimu ambayo ulitakiwa kuja
kumuonyesha shemeji yako, ambaye kwa muda huo hakuweza kuiona…?’ akaulizwa
‘Nina mambo mengi afande,…sio kwamba niliitupa,
hapana, ..sijui niliiweka wapi maana niliitafuta baadae sikuweza kuiona tena…’akasema
‘Ni kwasababu haikuwa na umuhimu kwako tena na labda
hukutaka shemeji yako aje kuiona tena, ikaja kumsumbua, si ndio hivyo…au sio…?’akaambiwa
na kuulizwa.
‘Ili iweje , labda nikuulize hivyo, maana ajali imeshatokea, ni kweli ajali yaweza
kutokea kutokana na gari lenyewe, uzembe wa dereva au bahati mbaya,…nakumbuka
ndio..kuna sehemu nilipitia, ..yah ..kuna maelezo kuwa gari lilikuwa na
hitilafu..’akasema
‘Kwahiyo kumbe wewe kama wewe uliisoma, lakini
hukutaka wenzako walielewe hilo…?’ akaulizwa na Dalali akabakia kimia, na kabla
hajafanunua mdomo kuongea mpelelezi, akasem
‘Ok….kabla sijaendelea na wewe…, nataka nirejee kwa mama mjane kwanza…’akasema
mpelelezi.
‘Lakini yeye hajui zaidi ya ninavyofahamu
mimi…’akajitetea Dalali
‘Ni kweli,… ndio maana yeye akalalamika…’akasema
mpelelezi
‘Alilalamika nini sasa…mimi ndiye nafahamu yote kuhus
gari, yeye anafahamu nini, anaongea tu…na kwanini alalamike kwako, na sio
kwangu, ..?’ akauliza akimgeukia mama mjane
‘Utasikia maelezo yake nikimuhoji, wewe tulia kwanza
nitakuja kwako…’akasema mpelelezi.
***********
Mpelelezi
akamgeukia mama mjane, na kumuangalia kwa makini, nahisi alikuwa akitafakari
kuhusu hali ya huyo mama, akasema
‘Shemeji…vipi khali yako kwasasa..?’ akaulizwa mama
mjane.
‘Nzuri tu…nipo sawa..’akasema mama mjane kwa
kuongezea hayo, ‘nipo sawa’ kwa msisitizo.
‘Upo sawa kuelezea ukweli wote, na kwa hili nataka
usifiche kitu, maana ndio hitimisho lake..baada ya hapa, tutafunga hii
kesi…labda kuwe na zaidi…mimi sitaki tena baadae kusikia malalamiko zaidi ….’akasema
huyo mpelelezi, na mama mjane akamkatiza
na kusema;
‘Naelewa, na ndio maana nimekuja hapa, nipo tayari
kwa lolote lile..’akasema huyo mama mjane sasa kwa kujiamini zaidi na Dalali
akamuangalia kwa macho ya mashaka.
‘Je wewe ulirizika na taarifa ya kuhusu ajali
iliyosababisha kifo cha mume wako,…maana shemeji yako anasema taarifa hiyo
waliipata wao, na wao kwa mtizamo wao, kama alivyodai, kutokana ushauri wa
dakitari, wao hawakupendelea kukuonyesha hiyo taarifa , je uliipatia wapi, hiyo
taarifa kuhusiana na ajali ya mume wako…?’ akaulizwa.
‘Kiukweli …kama alivyosema shemeji mimi nilikuwa
naumwa kipindi hicho,na maelezo zaidi ya kifo cha mume wangu nilikuja kuyasikia
zaidi watu wakiongea…na nikawa na hamu ya kujua zaidi,..…’akatulia.
‘Ulisikia nini awali ..na baadae ukasikia nini mpaka
ukavutika kutaka kujua zaidi..?’ akauliza.
‘Kwa mazungumzo ya wanafamilia, nilisikia kuwa mume
wangu alifariki kwa ajali ya gari, ..na ni ajali ya kawaida tu..baadae
nikasikia kwa watu kuwa gari lilikuwa na hitilafu, baadae nikasikia kuwa , mume
wangu hakuwa makini na gari, hakulichunguza vyema, ni kama kumlaumu mume wangu
kuwa hakuwa makini....ni mkanganyika wa maneno ya hapa na pale..’akatulia.
‘Ehe, kwanini ukakanganywa na hayo maelezo…?’
akaulizwa.
‘Kwasababu gari la mume wangu, lilikuwa jipya,…na
maswala ya kuchunguzwa kama gari lina hitilafu, mara nyingi alikuwa akilifanya
shemeji..kwa vile yeye ni mtaalamu wa magari…sasa sijui kwanini mume wangu
alaumiwe kwa hilo…’akasema hivyo na hapo Dalali, akahema kwa nguvu. Na
alipotaka kusema neno, wakili wake akamuashiria atulie.
‘Wewe unafahamu lolote kuhusu gari, kuendesha, …?’
akaulizwa
‘Nafahamu kiasi, wakati napata mafunzo ya kuendesha
gari, nilijifunza kidogo kuhusu gari lilivyo, hata kutengeneza, japo sio saana…’akasema
na Dalali akatikisa kichwa kama kusikitika
‘Kwahiyo ulifanya nini baada ya mkanganyiko huo..?’
akaulizwa
‘Mim sikuweza kuvumilia, nikaamua kwenda polisi ili
nipate maelezo zaidi ili kujirizisha…’akasema.
‘Kwanini ukimbilie polis wakati taarifa alikuwa nayo
shemeji yako, yaani huyu Dalali..?’ akuliza.
‘Kwasababu nilimuomba maelezo, na ikibidi anipatia
hiyo taarifa, akawa ..mara nitakupatia, mara sijui ilipo, mara nahisi
imepotea,..mara subiri mimi nina shughuli nyingi, ilifikia mahali mpaka tukawa
hatuelewani kwa sababu ya hilo…’akasema.
‘Kwanini mkosane..?’ akaulizwa
‘Aliona kama namsumbua, maana tupo kwenye kutafuta
ukweli wa deni, na wakati huo huo natafuta mambo mengine..nilimuelewa kwa
wakati ule… , lakini baadae nikasema kwanini nisifuatilie mimi mwenyewe, ndio
nikaona nije huku kituoni kufuatilia mimi mwenyewe…’akasema.
Hapo Dalali hakuweza kuvumilia
‘Najua tu, kama ulivyofanya kwa deni, ndivyo hivyo
hivyo kwa hilo gari, kunizunguka,..sawa tu…samahani afande, hapo nataka
kujitetea kidogo, mimi sikumwambia shemeji , kwasababu ya kuhofia hali yake..kutokana
na docta alivyosema, kuwa tuwe makini na hali ya shemeji…’akaongea kwa taratibu
‘Ni kweli hata mimi nililiona hilo, kuwa maelezo ya
uchunguzi ya ajali iliyosababisha kifo cha Bro, yalikuwa na upungufu kidogo…,
lakini ingelisaidia nini tena…sasa labda mimi nimuulize shemeji, mimi kwa
kumuonea huruma huko, kuwa nisimpatie mawazo ya kumuumiza zaidi, nilifanya
kosa, …?’ akauliza Dalali.
Mama mjane akamuangalia Dalali, moja kwa moja usoni
na kusema;
‘Shemeji, unakumbuka siku moja tuliliongelea hili
jambo, ukaniambia kama nina shaka nalo kwanini nisiwaulize wale
waliolishughulikia hilo tatizo…, je hao waliolishughulikia ni akina nani, kama sio..hao
polisi,..?’ mama mjane akamuuliza Dalali, na pale Dalali alipotaka kujitetea
shemeji yake akaendelea kuongea;
‘Na kwa vile nimeona kuna utata, …na niseme ukweli,
kilichonisukuma zaidi ni kutokana na
kufuatilia hilo deni la nyumba, hilo deni lilinifungua macho,…maana nilikutana na watu wengi…wakanishauri
hili na lile, na kila nikiwazia zaidi nahisi , nilihisi hivyo, hapa kuna jambo
nyuma ya pazia…akilini,niliwazia hivyo..’akasema mama mjane.
‘Jambo gani hilo, ambalo hukutaka kuniambia mimi shemeji,
…mpaka ukakimbilia polisi, huoni kwa kufanya hivyo, ndio maana hawa watu
wananishuku mimi vibaya, je shemeji huniamini mimi..kuna kitu gani kibaya nimewahi
kukufanyia shemeji…?’ akauliza Dalali, sasa akiwa kakunja uso kwa hasira.
‘Nimeshasema, sikupenda kubakia na duku duku moyoni,
na kilichonisukuma nifanye hivyo ni kutokana na hilo deni, hilo deni sio halali
kwa mume wangu, hata wewe kiundani unalifahamu hilo…’akasema mama mjane na
Dalali akatikisa kichwa kukataa.
‘Utapinga tu…lakini najua, hukubaliani na hilo deni…kuna
siku uliwahi kusema kuwa huenda kuna mtu kafanya mbinu zake, kumbambikia kaka
yako, …hukuwahi kusema hivyo…?’ akauliza mama mjane
‘Ni kabla sijapata huo ushahidi…’akasema Dalali.
‘Sawa…na hili la ajali je…kwanini hukutaka kuniambia
ukweli…kutokuniambia ukweli kwako, ndiko kulinisikuma mimi kufuatilia, je unakubaliana na hilo,
waanlosmea watu kuwa kaka yako, alikuwa mzembe kwenye gari lake,…anaendesha
bila kulichunguza kaam lina hitilafu….mimi sikubaliani na hilo, hata wewe
hukubaliani na hilo..ndio maana nikataka kuujua ukweli…, wewe mwenyewe
unamfahamu kaka yalo alivyokuwa makini kwenye gari lake.. ..’akasema
‘Sasa mimi ningelijuaje hayo..eeh, walioleta taarifa
ni benki, mimi nahusikanaje hapo, na kuhusu ajali, ..taarifa ya uchunguzi
walileta hawa polisi wenyewe, kwa kile walichokigundua, na taarifa ya mwanzo
tu, inasema Bro alifariki kwa ajali ya gari lake, sasa hapo mimi nina kosa gani…?’
akauliza Dalali
‘Haya,…nisubirie na mimi nielezee vyema…’akasema mama
mjane.
‘Tatizo shemu, unavyoelezea, uwe makini,....wewe
hujui tu, unawapa kichwa hawa watu, na kuendelea kunifikiria mimi vibaya…hayo
maelezo yako ni kama yananishitakia mimi…’akasema Dalali, na mama mjane
akatulia, lakini badae kwa kujiamini mama huyo akaendelea kuongea.
‘Mimi nilivyohisi , na sio kuhisi..ni kwa jinsi
nimjuavyo, mume wangu, kama ilivyokuwa deni, na naamini hivyo sio halali yake,
ndivyo nilivyohisi hata kwenye taarifa ya ajali kutokana na maelezo niliyosikia kuhusu ajali
hiyo, moyoni nikahisi pia sio sahihi…’akasema
‘Taarifa hiyo uliiona wapi,…?’ akauliza Dalali
‘Kwanza nilisikia kwa watu…’akasema mama mjane
‘Hahaha, kusikia kwa watu, ndio uamini wayasemayo,
wewe hukuwahi kuisoma hiyo taarifa vyema…labda kama polisi walikupatia
ukaisoma,…lakini kwa kauli yako wewe ulisema, taarifa haikuwepo, …walidai
mapaka aliyehusika areeje, sasa niambie wewe uliipatia wapi hiyo taarifa, acha
kusikiliza maneno ya mitaani…’akasema Dalali.
‘Hata kama ni maneno ya mitaani, lakini kama yana
utata, mimi kama mke wake, ningelitakiwa kufanya nini…ndio nikae kimia tu…hapana
mimi sipendi kuwekeza duku duku moyoni mwangu, nikaamua kufuatilia, na
nilifanya hivyo baada ya kuona wewe hutaki kuniambia ukweli…’akatulia kidogo.
‘Shemeji shemeji…usinilaumu kabisa kuwa mimi sikuweza
kukusaidia, mimi nilikuwa tayari kwa
lolote lile, nimekusaidia mangapi eeh …’akasema Dalali
‘Ndio lakini hilo la kuhusu ajali iliyosababisha kifo
cha mume wangu hukutaka kabisa kunielezea ukweli, kila nikitaka kukuulizia hayo maswali, wewe
ulitoa udhuru fulani, shemu sema ukweli wako, kila nilipokuwa nataka kukuulizia
hayo maswali ulikuwa unasemaje…?’ akamuuliza Dalali.
‘Nimeshakueleza sababu kubwa ni ushauri wa kitaalmu
kutoka kwa docta….sijasema mimi hapo, sijaelezea hilo, usiongeze chumvi…?’
akauliza Dalali.
‘Kwa kiasi kikubwa wewe ulikuwa kama upo pembeni, kwa
hilo , hata kwenye deni kwa asilimia kubwa ulikuwa kama unajiweka pembeni…,
haya umefikia wapi, haya twende, huko mahakamani kama itawezekana, ilikuwa
hivyo, hata hivyo sio kwamba nakulaumu, mimi nakutetea kuwa ni kutokana na
majukumu yako…ndio hukuweza kufuatilia na mimi bega kwa bega, kwa kila kitu
nilivyotaka mimi…’akasema mama mjane.
‘Shemeji hapo ina maana unanilaumu tu, usijitetee, usikwepe
huo ukweli…mpaka mimi sasa naanza kujihis vibaya, nimekufanyia nini kibaya cha
kustahiki hayo unayonifanyia sasa, eeh, niambie ukweli shemeji…?’ Dalali sasa
akawa anauliza maswali mengi kwa mfululizo.
‘Shemeji, mimi nina haki yangu kufuatilia, ..na
sikufanya hivyo bila kufuata utaratibu, ni wewe unasahau tu, kuwa nilikuwa nakuuliza
na kauli zako zilikuwa hivyo,..nenda kauliza benki sio wao wanadai…eeh nenda
kauliza polisi si wao walichunguza…, je hapo mimi ningelifanya nini…?’ akauliza
mama mjane.
‘Sawa…nimekuelewa shemeji yangu,..tenda wema uende
zako, lakini shemeji, ujue hayo uliyoyafanya matokea yake ndio haya, mimi
nashikiliwa kwa makosa ambayo mimi sijawahi kuyafanya, ina maana hadi hapa
ilipofikia, wewe umeshaniweka kwenye kundi la uhalifu, ina maana umenishitakia
mimi , je kwa kosa gani…’akasema Dalali.
‘Mimi sijakushitakia wewe..haya mengine ya kukuhoji
wewe ni kazi zao polisi, na mimi nililalamika kwao hilo…kuwa wasije kukushuku wewe
vibaya, nionavyo mimi wewe huna kosa…sasa kiutendaji wao, mimi nisingeliweza
kuwazuia…’akatulia
‘Khaa….’akasema hivyo Dalali.
‘Ndio ningeliwezaje kuwazuia kuwa wao…, wasikuhoji ,
ila kiukweli mimi niliwaambia kuwa wewe huna kosa, …nakufahamu vyema…wewe ni
msaada wangu mkubwa,..zaidi ya hapo, ni majukumu yao, yaliyowasukuma kufanya
hivyo ..’akasema mama mjane.
Hapo mpelelezi akaingilia kati na kusema;
‘Hebu kwanza Dalali tulia, nimekuacha tu, uingilie
kati,. Ili tukuone hisia zako zipoje, na hata wakili wako amejaribu kukuzia
bila mafanikio..unavyofanya hivyo, unajichora wewe mwenyewe bila kulijua hilo…’akasema
mpelelezi.
‘Mimi sija-jichora hapo…, ni lazima niwajibike, huyu
mama yupo mikononi mwangu, amefanya makosa sana, kuniruka hadi kuja huku
kwenu..huyu .she-shemeji umesahau nilivyokuhangaikia, ndio maana hata Bro,
alikuwa akikulalamikia, kuhusu tabia yako…’akalalamika Dalali
‘Tabia gani!!!…mume wangu hajawahi kulalamika kwa
hilo, hana tabia hiyo ya kuwalalamikia watu wengine kunihusu mimi..na tabia
gani mbaya hapa, kuutafuta ukweli ni kosa…unajishuku wewe mwenyewe tu shemeji,
usinilaumu kabisa kwa hilo…’ akauliza mama mjane na kuelezea hayo kwa sauti ya hasira, na mpelelezi akaingilia
kati.
‘Shemeji…mama mjane, nisikilize kwanza, mamaah…,
tuachane na Dalali, ni kweli yeye mwenyewe anajishuku bure hatujasema yeye ana kosa hapa,
ni katika taratibu zetu tu za kumuhoji yeye kwanza ili kutusaidia kaika kazi zetu, sasa sijui kwanini
anajishuku bure…’akasema mpelelezi
‘Wala! …Mimi sijajishuku kitu, ila ni lazima niongee
pale inapobidi…mimi ninajua ninachokifanya, nina uhakika sina kosa, ndio maana
sina wasiwasi na hilo…’akasema Dalali.
Mpelelezi akanigeukia mimi, alipoona nataka kuongea
na kabla hajanipatia nafasi, au kunizuia, nikawa nimeshaanza kuongea…
‘Mama mjane, je ni kitu gani zaidi kilikusukuma
kisheria,..ni ushauri au ni wewe mwenyewe tu,.. hadi kuamua kufuatilia maswala
ya mumeo..?’ mimi nikauliza hilo swali na mpelelezi, akaniangalia kwa sura ya kukereka,
kuwa nimeingilia kazi yake.
‘Ni kutokana na ushauri wa kitaalamu pia..,..ilibidi
niende kwenye vitengo vya haki za binadamu, ustawi wa jamii, vitengo vya sheria, jinsia na watoto , ..sehemu
nyingi nilipitia kuona jinsi gani nitasaidiwa kwa vile mimi sikuwa na pesa,…za kumtafuta wakili…, ndio wao
wakanishauri, hili swala nilifikishe kwanza polisi,..hasa hili la uchunguzi wa
ajali , iliyosababisha kifo cha mume wangu…’akasema.
‘Kwahiyo wewe ulifanya hivyo kutokana na ushauri wao,
kuwa uende polisi,…au ni duku duku zako
za moyoni ndio zilikusukuma kufanya hivyo?’ akauliza mpelelezi kutaka uhakika
zaidi.
‘Pamoja na duku duku zangu za moyoni,..kutaka
kuwajibika kujua ukweli wote… pia hata ushauri wao,wa kitaalamu, ndio
ulionifanya niwe na moyo zaidi wa kufuatilia…waliniambia ni haki yangu
kufuatilia kisheria,..na nina haki ya
kufungua malalamiko, ili uchunguzi ufanyike
zaidi, nikikaa kimia, itaonekana tumerizika, je kwa kufanya hivyo, si nitakuwa
nimemdhulumu mume wangu…’akasema mama mjane.
‘Baada ya ushauri huo ndio ukaanza kufuatilia, au sio..?’
akaulizwa
‘Ndio nilianza kufanya hivyo..lakini baadae
nikashindwa…’akasema
‘Kwanini ulishindwa…!?’ akaulizwa
‘Kutokana na hali iliyokuwa ikitokea ndani ya familia
yangu..mara ghafla watoto wangu walianza kuumwa, magonjwa ya ajabu ajabu…na
mimi mwenyewe nikaanza kuona vitu vya
ajabu ajabu vya kunitishia amani…’akasema mama mjane.
‘Kutokana na hali hiyo ukakata tamaa kufuatilia ina
maana uliamini hayo mambo, sio mambo ya kishirikina hayo..?’ akaulizwa
‘Kiukweli nilijitahidi sana..na hata kumuomba shemeji
ushauri, na..ndio shemeji akasema hayo maswala sio ya kunyamazia, ni bora
tutafute njia mbadala, maana kama mtoto anaumwa, ukifika hospitalini hakuna
ugonjwa,..sio kitu cha kawaida…’akasema na mara Dalali aakasema;
‘Ni mimi nilikushauri hivyo au ni ndugu yako..?’
akauliza kwa hasira.
‘Ndugu yangu pia alisema hivyo hivyo…’akasema mama
mjane.
‘Aaah, ni nani wa kwanza kukushauri hivyo, ni mimi au
ni ndugu yako…?’ akauliza.
‘Shemeji…kabla ya kile kikao mimi na wewe na ndugu
yako, wewe hukuwahi kunishauri hivyo,..?... kuwa haya mambo yanavyoonekana sio
ya kihospitalini, …ulianza wewe lakini sio kwa siku ile tulipokutana, ilikuwa
siku kabla..’akasema mama mjane
‘Sikumbuki kuongea na wewe kuhusu hilo wazo kabla…sikuwahi…huo
ndio ukweli, sema kwa vile unataka kunishinikiza nionekane mimi ndiye mkosaji,
ni lazima utasema hivyo…’akasema Dalali.
‘Je ni nini zaidi kilikuvuta, hadi kuomba uchunguzi
huo wa polisi kuhusiana na ajali iliyosababisha kifo cha mume wako,..hadi
ukaomba uchunguzi huo ufanyike upya…?’ akaulizwa
‘Muhimu ni hiyo taarifa ya polisi kuhusiana na gari
lenyewe lilivyokuwa,…na mimi mwenyewe nliwahi kufika sehemu gari
linapotengenezewa, kuulizia, wakaniambia nimuulize shemeji , wao kama mafundi hawajui
lolote kuhusiana na gari hilo…’akasema.
‘Hiyo sio kweli shemeji…umeelezea kuhusu taarifa,
sasa umekimbilia kuwalamu hata mafundi…tarifa yenyewe hukuwahi hata kuisoma, na
wewe unahisi ina mapngufu, yapi sasa wakati hata kuiona hukuwahi kuiona.. ,
usichanganye mambo hapa, hizo shutuma ni nzito sana, ‘ akasema Dalali.
‘Oh nilisahau…’akasema mama mjane… akachukua mkoba
wake,..kwanza akavaa kitu kaam soksi mkonononi, halafu taratibu, akatoa bahasha mbili zilizoungua upande…akachukua mojawapo, akaisoma juu,
akamkabidhi mpelelezi
‘Ni nini hii,…?’ mpelelezi akasita kuipokea kwanza
‘Kasema mimi hata hio taarifa ya uchunguzi sikuwahi
kuisoma…natoa ushahidi wangu…na nimejitahidi kutokuzigusa bila ya kinga mkononi...wasije kusema ni mimi niemfanya hivyo...’akasema mama mjane.
‘Hii bahasha mbona imeingua umeipatia wapi…?’
akaulizwa mpelelezi naye akiwa na tahadhari ya kuigusa.
Hapo Dalali, akajiinua ile ya kutaka kuona hicho
alichokitoa mama mjane ni kitu gani, hata wakili wake akafanya hivyo, ..na hapo
hapo wakili wake akawa wa kwanza kusema;
‘Samahani kwa hilo, nilivyoelewa tokea awali, ndio
maana sikutaka kuingilia ni kuwa nyie mnachofanya hapa ni kuchukua maelezo ya kuhojiana…mnamuhoji mteja wangu, anaulizwa maswali ya kuweza kuwasadia,
kumalizia uchunguzi wenu, sasa haya ya kutoa ushahidi, yanakujaje, je mteja
wangu anashukiwa kwa kosa lolote..?’ akauliza wakili
‘Ndio maana nimemuuliza huyu mama mjane,…hizo bahasha
kazipatia wapi,…na majibu yake yatatusaidia kuendelea na maswali yetu,..je
mteja wako ana wasiwasi gani kuhusiana na hiki alichokitoa mama mjane..?’
akauliza mpelelezi.
Dalali…..akabakia kimia…macho yakiwa yanaziangalia
zile bahasha…
NB: Haya niishie kwanza hapa, swali je hiyo ajali
ilikuwa ya kawaida au ina mkono wa mtu,..je mkono huo ni wa nani, na kwanini.
WAZO
LA LEO: Mwenye uwongo wa dhambi, wakati wote huishi kwa
mashaka, hajiamini, na hata akijiamini ni swala la muda mfupi tu…kwani nafsi
yake huhisi labda labda nyingi, kuwa labda keshagundua, labda….maana dhuluma
inamsuta nafsi yake wakati wote..
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment