Yule askari, yaonekana alitaka kuhakikisha kuwa wahusika
wote wanaohitajika kwa kikao hicho wameshafika, kwani baadae aligeuka na
kuondoka, huku akifunga mlango bila kusema neno
Wakili, aliyeingia, pamoja na kushikana mikono na
mwenzake, ya kusalimiana, cha ajabu wakili huyo hakuongea neno, akawa
ananiangalia tu , baadae akasema;
‘Huyu ni nani….?’ Akauliza akiniangalia mimi
‘Ni yule Peku peku niliyekuambia…’akasema Dalali,
akimsogezea huyo wakili kiti ili aweze kukaa,…huyo wakili akakaa lakini bado
akiendelea kuniangalia mimi, na mimi nikawa kimia tu…
‘Nilishaonna naye mahali fulani, najaribu kumkumbuka
nyema, anyway, its ok…haya niambie….’akasema sasa akimgeukia Dalali.
‘Kama nilivyokuelezea awali kwenye ujumbe wa maneno,
japokuwa simu yangu waliishikilia kwa muda, hili nalo ni jambo la kuwalalamikia
hawa watu, kwanini wachukue simu yangu…’akalalamika Dalali
‘Wameshakurejeshea…?’ akaulizwa
‘Ndio, lakini najua wamechunguza kila kitu, hata
hivyo mimi sijali, sina makosa na kwa vile wewe umeshafika,…nitakuelezea
unachotakiwa kukifanya..’akasema Dalali, na hapo wakili akanigeukia mimi
‘Unaweza kutupisha mara moja…?’ akasema huyo wakili
akiniangalia mimi
‘Muheshimiwa, hapana, muache tu awepo,…kwa kifupi, hakuna muda wa kuongea, mimi na wewe hapa,
nilichokuitia wewe ni ili uweze kusikilizia maongezi yangu na polisi, wakinihoji,….’akasema
Dalali
‘Kuhusu nini, kosa gani wanakuhoji nalo…?’ akauliza
wakili
‘Hutaamini hadi sasa hawajaweza kuniambia kosa langu
ni lipi..lakini mimi sijali, maana mimi sina kosa lolote kama nilivyowahi
kukuambia awali,..na,..na utakuta maswali yao mengi ni ya kunitega tu, ili mimi niingie kwenye kosa ambali
sijalifanya, na mimi ni mjanja, hawaniwezi…’akasema akigeuka kuniangalia mimi.
‘Sasa ni hivi, kwa vile wao ndio wamelianza hili
nataka wanifahamu kuwa mimi ni nani….sijataka haya, na …kiukweli mimi muda
mwingi,…nipo na familia yangu, nimekuwa nikijitahidi kujenga maisha yangu kwa
jasho langu…lakini wivu wa watu ndio umechangia haya…’akasema
‘Una maana gani kusema hivyo..?’ nikajikuta nimeuliza
hilo swali.
‘Kwanini ukaniuliza maswala ya nyumba…unajua
nilivyohangaika kuzijenga hizo nyumba, hata Bro, alifikia hatua ya
kunipongeza…ni juhudi zangu mimi mwenyewe, sikupata hata senti moja ya bro au
ya mtuto yoyote…nimezijenga kwa jasho langu mimi mwenyewe….’akasema
‘Nilikuuliza nikitaka ukweli…na lengo langu halikuwa
wivu kama unavyofikiria wewe, lengo langu ni ukweli wa uhalali wa hilo deni,
…’nikasema
‘Kwahiyo unafikiria mimi nilijenga hizo nyumba kwa
hilo deni au , hayo ni mawazo ya kijinga, samahani kwa hiyo kauli, lakini
nitasemaje hapo…?’ akasema hivyo.
‘Yawezekana yakawa ni mawazo ya kijinga ya mtizamo wa
mtu, kwa vile haelewi, na mtu asiyejielewa, anajulikana kitaalamu kwa kauli
yako hiyo…ila ukweli utajuliakana na aliyemjinga atabainika, au sio...’nikasema.
‘Nina kila ushahidi wa mali zangu…ndio maana nikataka
huyu wakili awepo, ili kila jambo liwekwe sawa, najua utakuwa umshamdanganya
shemeji…sasa nataka baada ya hapa kila kitu changu kijulikane kisheria, na
uhalali wake…’akasema akimgeukia wakili wake.
‘Unasikia muheshimiwa nataka uyafanye hayo, na
uwathibitishie uhalali wa mali yangu yote kisheria, hati zipo,hati za gharama
ya ujenzi zipo…, kila kitu nilishakupatia, au sio..?’ akasema
‘Ni kweli kila kitu kipo sawa,…’akasema huyo wakili
‘Na baada ya hapo nataka ufungue mashitaka dhidi ya
huyu mtu, kwa kunisumbua, kwa kunijengea chuki na familia yangu, na zaidi
kunishuku kwa jambo ambalo mimi sijawahi kulifanya…nilipwe milioni 90 kwa
kashfa hizo,…, mengine utajua wewe , jinsi gani ya kuyaweka kisheria…’akasema
‘Sawa hilo halina shida, nitalifanyia kazi..’akasema
wakili.
‘Utakuwa umeturahisishia kazi Bwana Dalali..’nikasema
hivyo na Dalali akaniangalia kwa uso uliojaa kuuliza halafu akakunja sura na
kusema kwa dharau.
‘Tatizo hunijui vyema nilivyo..mimi ni mtu mpole
sana, mimi najua kuishi na watu wa aina mbali mbali, ndio kazi yangu ilivyo,
ila ukinigusa kubaya,…hutaweza kuamini…na wewe umeshanigusa kubaya, uliza na
hizo nyumba nilijenga kutokana na watu kama nyie..walinilipa, kwanini
unidharau, kwanini uniharibie jina langu, sasa kutoka kwako nitaenga nyingine,
wewe si utaona tu..’akasema
‘Ni kweli,… nimegusa mali yako..lakini kwanini ufikie
huko, una wasiwasi gani na mali zako,..kama ni halali yako, itabakia kuwa
hivyo, ila husika yangu kubwa ni kuhusu hilo deni ambalo linadaiwa kuwa ni la
marehemu..mengine ni yako wewe mwenyewe…’nikasema
Dalali akatulia kidogo kama anawaza jambo…alitupiana
jicho na wakili wake sijui kama walipeana ishara gani, Dalali akasema;
‘Sawa, …kama kweli upo hivyo, sawa..tutaliona hilo,
mimi sio mtu mbaya, na kiukweli niseme hivi, samahani nimekasirika bure tu, ..ngoja
tuone,ila ninachotaka mimi ni kuonyesha uhalali wa mali zangu..wakili
atalisaidia hilo, ili kuondoa hisia zenu mbaya, na hilo la kufungua mashitaka
dhidi yako siwezi kuliondoa…’akasema
Na mara mlango ukafunguliwa, sasa aliyeingia ni
mpelelezi,anayeshughulia ajali iliyosababisha kifo cha kaka yake Dalali.
*************
Wakili akamgeukia mpelelezi , naona walishaonana huko
nje kwani hawakusalimiana akasema
‘Hebu niambie mteja wangu kashikiliwa hapa kwa kosa
gani…?’ akauliza
‘Ni mteja wako sio…! Ok, hajakuambia eeh,,…yupo hapa
kuisaidia polisi, kuna maswali fulani fulani,…kuna mambo tunahitajia kumuhoji,
lakini akang’ang’ania hawezi kuhojiwa
mpaka wewe uwepo, kiujumla sisi tuliona ni maswali ya kawaida tu, sasa huenda
anahisi vinginevyo….’akasema mpelelezi na wakili akamgeukia mtu wake, na Dalali
akasema;
‘Usiwe na wasi wasi, wakili wangu, ..kama
nilivyokwisha kukuambia kinachotakiwa hapa ni wewe usikilize tu, kama utaona
ninakosea mahali unaweza kunionyesha ishara mimi nitajua tu….sasa wewe sikiliza
tu,….’akasema akitikisa kichwa kujinadi.
‘Kwahiyo…..’akataka kusema wakili wake, lakini Dalali
akamuashiria kwa mkono kuwa anyamaze, na Dalali akanigeukia mimi na kusema;
‘Wewe ndugu yangu hatujamalizana,…au sio..’akasema Dalali
.
Mimi nikaona nisikae kimia, hapo, nikasema;-
‘Kuna swala nilikushauri mapema sana, sasa naona ni
muda muafaka wa wewe kujitakasa, kabla hujachelewa, na muda ndio huu..’
nikamwambia.
‘Kwanza nikuambie ukweli, mimi sina kosa, siwezi
kukubali kosa ambalo sijawahi kulifanya, wewe ulisema mtaalamu aliongea jambo mbele ya polisi, hayo ni yake yeye kama yeye,
sio mimi…., ‘akatulia kwanza.
‘Kwangu mimi nitaongea ukweli unaonihusu mimi tu…’akatulia
hapo kidogo
‘Na kwa jinsi ninavyomfahamu mtaalamu…asingeliweza
kusema jambo ambalo halipo, hata kama aliteswa,……ni kweli mimi nilikwenda
kwake, kutokana na matatizo ya mtoto, na katika kuangalia ndio akayagundua
hayo, sioni yeye anahusika vipi na hili zaidi ya hapo…’akasema.
Hapo ndio mpelelezi
akaingilia kati na kusema;
‘Wewe mtu wa jamii, hayo maswali yako kwa mujibu wa
mpelelezi muhusika, yasubirie kwanza, hadi hapo atakapofika yeye, sasa hivi nataka kumuhoji huyu jamaa kuhusiana
na ajali ya marehemu, jana alikataa kuongea akidai anahitaji wakili wake awepo,
sasa wakili wake ndio huyu hapa ameshafika…’akasema mpelelezi na wakili akatoa
makabrasha yake kwenye mkoba.
************
‘Mhh, kwanza kabla ya kuanza haya
mazungumzo,…nilitaka tukiongea na yeye awepo, kuna umuhimu mkubwa wa yeye
kuwepo hapa… sijajua hali yake inaendeleaje…’akasema Dalali.
‘Shemeji yako hajambo…na kutokana na hali yake ,
japokuwa sio kuwa anaumwa,..ila sisi tukaona haina haja ya yeye kuwepo, kwahiyo
hili jambo linakuhusu wewe, kama atahitajika ni baadae…’akasema mpelelezi
‘Oh…mnanifanya nishindwe kukifanya nilichokidhamiria,…bila
yeye,…ok, wakili wangu unasemaje hapo..?’ akamgeukia wakili wake.
‘Kwa vile ni kuhojiwa tu, mimi sioni kwamba kuna
tatizo,…ila itakapofika kwenye makubaliano, basi ni lazima awepo…….’akasema
wakili
‘Ndio hivyo, mimi lengu langu nikumuhoji kwanza, kama
kuna tatizo, basi tutalishughulikia ipasavyo…..’akasema mpelelezi.
Mara mlango ukafunguliwa na askari mmoja akaingia,
akamnongeza kitu mpelelezi, na mpelelezi, akatikisa kichwa, halafu akasema;
‘Una bahati sana, mama mjane yupo hapo nje,
..’akasema mpelelezi
‘Oh, tayari keshapona, …ina …’Dalali alitaka kusema
jambo akakatisha, kwani kule mlangoni aliingia huyo mwanamama, kwa haraka
akatembea hadi pale alipokaa mpelelezi, akawa anamnong’oneza kitu.
Mpelelezi akasema;
‘Basi ni vyema,..ila hayo yatamsubiria
mwenzangu,…’akasema huyo mpelelezi, na mama mjane akainua uso kumuangalia
Dalali,…ile angalia yake ilionyesha jambo, sasa sijui ni kwa kumuonea huruma au
kuna kitu kingine kimejitokeza hapo, na Dalali akawa anamuangalia shemeji yake
kwa uso wa mashaka.
‘Sasa tuanze, au sio…’mpelelezi akasema
Hapo hapo Dalali akamgeukia shemeji yake na kusema;
‘Shemu usijali , mimi sina hatia, haya yatakwisha ,
leo hii hii,…nimeshukuru sana kuwa haujambo, sijui kitu gani kilikupata, na
unisamehe kwa lugha yangu pale….’akasema hivyo , na shemeji yake akabakia kimia
tu, kitendo hicho kilizidi kumtia mashaka Dalali, na kabla hajasema neno,
mpelelezi akasema;
‘Sawa wanafamilia nyie, … mjue hiki ni kikao tu cha
kuulizana maswali, haikuwa na haja ya mawakili nk…lakini hatuwezi kumnyima mtu
haki yake, ….’akasema mpelelezi.
‘Sawa mimi
nipo tayari, maana wakili wangu yupo, nimependelea hivi, baada ya kuona
nashinikizwa kwenye makosa ambayo sikuwahi kuyafanya, na sijui shemeji yangu
ana nini , naona kama bado hayupo sawa….’akasema Dalali akimuangalia shemeji yake.
‘Mimi nipo sawa,..tuendelee tu …’akasema mama mjane
‘Haya wanandugu…’akasema mpelelezi akimuangalia
Dalali
‘Ndugu Dalali, je una uhakika kweli kuwa kaka yako alifariki kwa ajali tu…?’ mpelelezi
akauliza hilo swali hivyo kwa Dalali
Ilivyojionyesha, Dalali hakutegemea swali kama
hilo..maana nilimuona Dalali uso wake ukibadilika, ni kama alipatwa na mshtuko
fulani, na aliyeokoa hiyo hali alikuwa
ni wakili wake aliyesema;
‘Kwanza kabla hajajibu hilo swali, hebu tuwekane wazi
hapo…, umesema kuwa mteja wangu
kashikiliwa hapa kwa kuisaida polisi na awali alikuwa akiyajibu maswali yanahusiana
na deni, nikajua hayo ndio mteja wangu aliyoitiwa, lakini sasa naona unakuja na
hoja nyingine mpya…’akasema wakili.
‘Mimi nilichomuitia bwana Dalali ni hicho, kumuhoji
kuhusiana na ajali iliyosababisha kifo cha kaka yake, na ni kweli…kuna ajenda
ya deni la marehemu, ajenda hiyo mimi
sihusiki nayo mimi, atakuja mwenzangu
ndiye mtaendelea naye….’akasema mpelelezi.
‘Kuna makubaliano kuwa matatizo yaliyojitokeza,
yamalizwe kinyumbani,..je na hili mnalikiuka,..au imekuwaje,..nataka niwekwe
wazi kwanza, kabla ya hayo maswali yako…’akasema wakili.
‘Sisi tunajua
wajibu wa kazi yetu, na hili jambo lilikuwa la kifamilia, ilitakia tatizo hili
limalizwe kifamilia, lakini kutokana na ukweli uliokuja kubainika baadae,
ikaonekana kuna upelelezi unahitajika kufanyika, na upelelezi unahitajia kuwahoji
watu…huyu tumemuita hapa kumuhoji, ..lakini akagoma ndio maana akakuhitajia wewe…’akasema mpelelezi.
‘Sawa, kwahiyo
kwa leo hii, utamuhoji wewe kuhusiana na ajali ya marehemu, na baadae atahojiwa
na mwingine kuhusiana na deni, je itachukua muda gani, maana kwa hli ilivyo,
mteja wangu kachoka…’ Akasema wakili.
‘Mteja wako hajalalamika hilo, kama atahitajia siku
nyingine ya maswali kutoka kwa mwenzangu ni hiari yake,, ila hawezi kuondoka
hapa kwa vile bado anaisaidia polisi…’akasema mpelelezi
‘Haiwezekani, hamuwezi kumshikilia mteja wangu zaidi,
..kama kuna kei ya kujibu, sawa, hata hivyo, yeye ana haki ya dhamana…’akasema
wakili
‘Nimeshakuambia mteja wako, hajashitakiwa bado, sasa
hivi anaisaidia polisi,..kama itafikia huko tutawaambia..’akasema mpelelezi.
Mara mama mjane akanyosha mkono kutaka kuongea,
mpelelezi akasema
‘Samahani mama mjane,…hayo yako yasubirie mwenzangu,
usijali, …’akasema mpelelezi.
‘Jamani,…mimi nimekuja kwa haraka, na huko nyuma
nimeacha vurugu, watu wamefika wakitaka mnada ufanyike, na mara wakaja wengine
wakidao, wao ndio wenye haki…sasa siwezi kuendelea kukaa hapa zaidi, kwa vile
sina uhakika wa huko nyumbani kwangu….’akasema mama mjane
‘Ni nani hao wanataka kufanya mnada bila mimi
kufahamu..?’ akauliza Dalali.
‘Mimi siwajui, wanasema wewe uliongea nao,
ukawaruhusu huo mnada uendelee, maana ni amri ya mahakama…’akasema mama mjane.
‘Shemeji hawa watu watatupotezea muda, hawana
ushahidi wowote hawa watu, na baada ya hapa hata tukifika mahakamani, tutaombwa
ushahidi, na mashahidi je kweli tunao hao mashahidi.’akasema Dalali.
‘Kwa uwezo wa mungu utapatikana tu….’akasema mama
mjane…kauli hiyo ilimfanya Dalali, ashituke na kutulia kimia, akabakia hivyo,
…wakili wake ndiye akaingilia kati, na kuuliza;
‘Je tunaanza kipi, maana huyu mama anakuja na ajenda
yake, hatuwezi kumchanganya mteja wangu, kwa mambo mawili…’akasema wakili
‘Wakili wangu,
usiwe na wasiwasi, mimi yote haya nitapambana nayo,..hamna shida, ila nimepata
jambo la kunifanya nifarijike kidogo, kusikia kauli ya shemeji kuwa huenda
kaupata ushahid ,…’akasema Dalali akimtupia shemeji yake jicho.
‘Ushahidi utapatikana tu, kwa uwezo wa mungu maana
haya yote yametokea na kutendeka ….kwa mapenzi yake,, …’akasema mama mjane
‘Shemeji, hayo maneno tu hayawezi kutusaidia,
..nilijua labda umepata kitu,..kumbe ni maneno tu,..hahaha, shemeji naye bwana,
mimi nilishafarijika ..’akasema Dalali, na shemeji yake akabakia kimia.
‘Mama mjane wewe kuwepo kwako hapa ni kuhusiana na
nini, ni Deni au ajali….’akauliza wakili, ni kama anataka kupoteza muda.
‘Ni deni….’akasema hivyo mama mjane.
‘Sawa basi hilo litasubiria kwanza…au sio afande,
kama ni lazima abakie hapa kusikiliza tu sawa, ila kama ana dharura anaweza koundoka
tu au sio …’akasema wakili
‘Ni kwa vile kuna hilo tatizo la hao watu watu wa
mnada, ndio maana , wasiwasi wangu ndio huo nisije kufika nyumbani, nikute huo
mnada umeshafanyika…?’ akauliza mama mjane.
Mpelelezi akamgeukia mama mjane…
‘Nimeshamtuma mtu huko, unajua hapo kuna amri ya
mahakama, sisi kama watu wa usalama, hatuwezi kuipinga moja kwa moja…inabidi
tufuate sheria,…tunalifuatilia hilo, usijali…’akasema mpelelezi.
‘Lakini afande, mimi sio kwamba nashabikia hilo, ila
naungana na shemeji yangu hapo,hapa tunaongea kimaneno tu…, Mahakama ndio
ilitoa amri, ndio maana mimi nimemuita mwanasheria wangu, ili kama kuna
pingamizi basi liende kisheria, sijataka maneno tu, je hilo pingamizi huko la
mnada limefanyikaje…?’ akauliza Dalali.
‘Usiwe na shaka na hilo,…kinachoendelea huko ni
vurugu tu , kuna watu wanadai pesa zao kutokana na zoezi hilo,…hilo ni jambo
jingine litafanyiwa kazi, kwanini watu watoe pesa kuzuia mnada, kama kweli
ulikuwepo kisheria,… , je ni rushwa, lakini pia kumejitokeza namna ya kutufanya
tuweke pingamizi,ndio taratibu zinafuatwa na mwenzangu…’akasema mpelelezi.
‘Lakini hakuna mtu aliyetoa pesa hapa afande…’akasema
Dalali
‘Waliahidiwa pesa, hao watu wanalalamika hivyo, sasa
kuahidiwa pesa kwa kazi gani,…kama watu wa usalama, inabidi kulichunguza na
hilo ..’akasema mpelelezi
‘Waliofanya hivyo, ni hawa watu…’akasema Dalali
akinionyeshea mimi kidole
‘Hawa watu, waliwaahidi pesa hao watu wa mnada ili
zoezi hilo lisifanyike, sasa …kwa hilo wa kumuuliza hapa ni huyu mtu wenu wa
jamii..’akasema Dalali.
‘Sasa hilo kundi jingine limetokea wapi..?’ nikauliza
‘Mimi sijui….’akasema Dalali…
‘Tuendelee…’akasema mpelelezi, akimgeukia mama mjane
‘Samahani, shemeji… nataka kuliweka hili wazi kwanza,
nauliza hivi, kutokana na uchunguzi uliofanyika, tunahitajia kujirizisha kwa
pande zote, sisi wachunguzi kwa upande wetu na nyie jamii, raia kwa upande
wenu, sasa nauliza hivi,…’akatulia kidogo hapo huyo mpelelezi
‘Je mama
mjane...japokuwa Dalali, hajaweza kunijibu hilo swali nililomuuliza, lakini
naona nikuulize wewe kwanza…’akasema mpelelezi.
‘Afande mimi nitakujibu swali lako…’akasema Dalali
‘Subiria kwanza , nataka kumweka mama mjane sawa tu,
ili aone umuhimu wa yeye kuwepo kwenye hiki kikao…, je wewe mke wa familia,
baada ya kupokea taarifa ya uchunguzi wa kifo cha mumeo, …najua ulikuja
kuupokea baadae sana, ulipopona, je ulirizika na uchunguzi huo uliofanyika, ..kuwa mume wako
alifariki kwa ajali ya kawaida tu…?’ akaulizwa
Mama mjane kwanza akatulia baadae akainua uso,…uso
wake ulionyesha wazi mama huyu leo ana jambo…
‘Awali mimi nilikubaliana na hilo, maana mtu sasa ameshafariki..utafanyaje eeh…na taarifa
ilishatolewa, na sijui zaidi ya hiyo taarifa…, baadaye nilipo-pona vyema, nikaanza
kujiuliza mimi mwenyewe kuhusiana na ajali hiyo na hiyo taarifa ilivyotolewa, ….’akatulia
Dalali alitaka kuongea jambo.
‘Endelea, Dalali,hili sio swali lako kwanza, nitakuja
kuuliza …’akasema mpelelezi.
‘Mimi nilipoanza kusikia maneno ya watu…kiukweli
iliniuma sana, lakin kwa vile muda ulishapita nikaoana haina haja,…ila nakumbuka
siku moja wakati nafuatilia haya maswala ya deni, nilikutana na askari mmoja,
simkumbuki jina laki ni nani,…alinihoji kidogo, kuhusiana na hiyo ajali,
akisema jalada lake halijafungwa…’akasema mama mjane
‘Alikuhoji kuhusu nini hasa…?’ akauliza mpelelezi.
‘Kuhusu hisia zangu kuwa je kweli, nimerizika na
uchunguzi uliofanyika, …nilimuambia kuhusu hisia zangu, kuwa kiukweli mimi sikuwa nimerizika na
uchunguzi huo..’akasema
‘Kwanini labda, elezea kwa ufupi tu…’akauliza
mpelelezi
‘Kwanza…gari la mume wangu ni jipya, halina
tatizo,..nijuavyo mimi…sasa uchunguzi unasema kuna nyaya sijui za umeme
…zilikatika, kuna vitu vilichomolewa vikawekwa sivyo ndivyo.., inaonekana hilo
gari, lilikuwa kwenye matengenezo na halikufungwa vyema, kitu ambacho mimi
sikubaliani nacho…maelezo hayo yalinifanya nishikwe na mashaka…’akasema
‘Basi inatosha..’akasema mpelelezi, na kuwageukia
Dalali na wakili wake..
‘Kwanini nimemuuliza mama mjane hilo swali,..ni ili
mfahamu kuwa sisi hatukurupuki tu, na wakati mwingine tunaifanya hii kazi yetu kutokana
na nyie, msaada wetu wa kutoa malalamiko ndio unatusukuma sisi kufuatilia
jambo,…’akasema mpelelezi
‘Ina maana shemeji…’akalalamika Dalali.
‘Subiria kwanza…’akasema mpelelezi na Dalali akawa
anamuangalia shemeji yake kwa macho yaliyojaa mashaka.
‘Ni kweli uchunguzi wa awali ulionyesha hivyo, kuwa
marehemu alifariki kwa ajali, na chanzo cha ajali ni gari lenyewe, lilipochunguza
lilionyesha udhaifu wa baadhi ya vifaa vyake kutokuwa imara,…ama vilichomolewa
na kuachwa kurejeshewa vyema, au kuna hujuma ndani yake na mimi niliachia hapo
kwenye uchunguzi wangu..’akasema mpelelezi.
Dalali akataka kuingilia lakini wakili wake akamzuia
‘Na maswali hayo yalitaka kumsubiria mtu
anayelifahamu vyema hilo gari, na zaidi ya mkewe ni wewe mwenyewe bwana Dalali…’akasema
mpelelezi.
‘Samahani kidogo hapo,…’Mimi nikaingilia kati
‘Bila samahani…’akasema afande
‘Ni nani awali alifanya huo uchunguzi …?’ nikauliza
‘Ni mimi, ila …sikuweza kuumalizia, maana nilipatwa
na dharura ya safari…’akasema mpelelezi
‘Sasa niliporejea kutoka safari, nikakuta hii kesi
bado ipo..hajafungwa, na uchunguzi zaidi haukuwahi kufanyika tena..na kuna
makubaliano kuwa kesi hii itamalizwa kinyumbani, lakini hapa kwenye ajali…sio
swala la kinyumbani, hili ni swala letu…’akasema mpelelezi.
‘Ni sawa, sasa ukweli unaanza kujitokeza…’nikasema
‘Ukweli gani huo …’akasema Dalali, na mpelelezi
akaendelea kuongea;
‘Ni wajibu wangu, kujirizisha kwa hili tukio, ndio
nikaanza kufanya kazi yangu ili ikibidi niweze kuimaliza hii kesi kabisa na
kuimaliza kwake ni kukamlisha uchunguzi wangu…, nilifanya juhudi za kuonana na
mama mjane,..lakini kwa kipindi hicho bado hakuwa na afya njema…nikaisubirisha,
na kwa bahati nzuri, ikatokea sababu ya mimi kuiendeleza hii kesi…’akatulia
‘Sababu mojawapo ni hilo deni….’nikasema
‘Hahaha….sio kweli…huo ni uhadithi wako tu bwana
mzee, unapotezea hisia zako bure, utaumbuka bila kutegemea…’akasema Dalali,
akicheka kwa dharau
‘Kwahiyo ni muhimu sana kukuhoji wewe Dalali, na
shemeji nilishamuhoji tayari….’akasema mpelelezi
‘Ina maana shemeji, uliongea na polisi, mbona
hukuniambia…’akalalamika Dalali
‘Usijali….sisi kazi zetu hazisubirii mtu, na wewe leo
ni zamu yako…’akasema mpelelezi
‘Sawa, uliza
hayo maswali yako afande…’akasema wakili akimuashiria Dalali kuwa hakuna
tatizo.
Mara mama mjane akasimama na kuenda pale alipo
mpelelezi akawa anamnong’oneza kitu, wakawa wanaongea, kwa sauti ya kunong’ona,
…baadae mpelelezi akatikisa kichwa kukubali.
Dalali alipoona hiyo hali hakuweza kusubiria akasema;
‘Shemeji…sio kwamba nalalamika, lakini kwanini kila
jambo unafanya bila kunishirikisha mimi.., ?’ akauliza
‘Usijali Dalali, mama mjane alikuwa bado na
anahangaika kivyake kutafuta ushahidi wa madai yake,…na alitaka kutoka kidogo
nimemzuia kiusalama,…mpaka anayehusika aje, ni mambo ya kawaida tu..na sasa
kakubali kuwa tayari kusubiria…’akasema mpelelezi.
‘Sasa yeye kapata ushahid gani ..nataka kulifahamu
hilo…?’ akauliza Dalali
‘Dalali…hayo mtakuja kuongea akija mwenzangu, sasa
hivi tunaulizana kuhus hiyo ajali, sawa,..nijibu swali langu nililokuuliza
awali….’akasema mpelelezi
‘Swali gani afande, ambalo mimi sijaweza kulijibu…?’
akauliza Dalali
‘Je wewe ulirizika na uchunguzi wa polisi kuwa ajali
hiyo iliyosababisha kifo cha kaka yako ni sahihi,..je unakubaliana na taarifa
iliyotolewa kuwa kifo cha kaka yako ni ajali ya kawaida tu…?’ akaulizwa Dalali.
Dalali, akabakia kimia….na wakili wake akataka
kuingilia kati, lakini ….
WAZO
LA LEO: Uwongo mwingine unakuwa mgumu sana kuutamka kwa
haraka, ukijua kuwa uwongo huo, madhara yake ni makubwa zaidi ya matamshi
yenyewe….wengine hawajali, ulimi wao ni mwepesi kutamkatu, hata kujiapiza…lakini
uthabiti wa kauli, unaweza kusubirishwa na mwenyewe aliyetuumba ili tu tuweze
kujirudi maana baada ya kauli hiyo huenda usije kupata muda wa kutubu, mengine
sio kwa kupenda kwetu tu…Tupo pamoja
hapo
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment